TANESCO wanataka ninunue transformer

TANESCO wanataka ninunue transformer

Hapa yenyewe bado hawako vizuri ila ni kwa sababu ni JF,aliyepewa hii kazi anapata na muda wa kusoma nyuzi zingine za kula tunda kimasihara kwa gharama za bundle la tanesco wakati siku hizi mifumo ya CRM ipo mingi sana ambayo TANESCO wanaweza kuitumia kutoa huduma bora na mitandao ya kijamii na simu zikawa ni listening points tu.
🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Kama utakumbuka Maelekezo ya Serikali hapo awali hakuna mteja anayepaswa kununua kifaa chochote cha kumfungia umeme bali ni jukumu la TANESCO kusogeza miundombinu ya umeme kwa wateja wake, tafadhali tusaidie taarifa zifuatazo

Jina

Namba ya Simu

Wilaya

Na kiasi ulichodai kuambiwa ulipie ili tukupatie ufafanuzi kwa taarifa kamili

TANESCO HUDUMA KWA WATEJA

MAKAO MAKUU
Mimi pia niliambiwa hivyo Wilaya ya kibaha,eneo linaitwa Boko Mnemela.Niliambiwa ninunue transfoma ili waniwekee umeme
 
Kisa cha muwekezaji mzawa wa kiwanda kidogo cha kubangua korosho mtwara nae alizungushwa miaka mitatu wakimdai anunue transformer hadi JPM alipofika kwenye ziara ngoma ikabuma kwahiyo visa hivyo ni vingi sana na havipendezi, bado bado mambo hayajakaa sawa
 
Unakumbuka wakati wa kununua nguzo? Ni mambo kama hayo, ila ni wajibu wa Tanesco
 
Kwa wale tuliolipia laki 3 kuunganisha umeme wakati bei elekezi ya elf 27 ilishatamkwa na waziri, ni lini tutarudishiwa chenji zetu au walau kupewa fidia ya unit za umeme.........
 
Kusema ukweli niliambiwa kwa mdomo sio kwa barua, sikuwahi kupewa barua
Ni vigumu kusaidiwa kama huna vielelezo. Cha kufanya, anza mchakato upya; waandikie barua yakuomba kuunganishiwa umeme, ukiambatanisha na michoro ya umeme wa jengo lako
 
Kosa lilianza kwenye uchaguzi wa saiti ya ujenzi wa mradi wako. Ungepata ushauri kabla. La sivyo kama miradi wa umeme ulikukuta!
 
Kitaalamu hauwezi kujibu swali kwa ujumla wake bila kujua ukweli wa taarifa husika, kujibu hivyo ni blabla ambayo taasisi yenye wataalamu kama yetu haiwezi kukurupuka kujibu bila taarifa kamili
Mbona unajibu kimipasho wewe na hao wataalamu mnafanana tabia, changamoto ya mteja unaita blah blah aisee!?
 
Mbona unajibu kimipasho wewe na hao wataalamu mnafanana tabia, changamoto ya mteja unaita blah blah aisee!?
Tafadhali pitia tena maelezo yetu ukiyasoma vizuri utaelewa tulichomaanisha, mteja aliyelalamika tumeshawasiliana naye Dm Na tumefikia pazuri
 
tutaheshimu vip kama wenyewe hawaheshimu wateja?
Ndugu mpendwa Mteja wetu

Tunafurahia kukuhudumia kupitia kurasa zetu za mitandao ya kijamii, tafadhali onesha taarifa kamili kwa huduma bora.

Jina

Eneo

Wilaya

Namba ya simu

Tatizo

Toka lini

Namba ya taarifa

Ahsante sana

TANESCO Huduma kwa Wateja
 
Back
Top Bottom