TANESCO wanataka ninunue transformer

TANESCO wanataka ninunue transformer

Kama utakumbuka Maelekezo ya Serikali hapo awali hakuna mteja anayepaswa kununua kifaa chochote cha kumfungia umeme bali ni jukumu la TANESCO kusogeza miundombinu ya umeme kwa wateja wake, tafadhali tusaidie taarifa zifauatazo

Jina

Namba ya Simu

Wilaya

Na kiasi ulichodai kuambiwa ulipie ili tukujipatie ufafanuzi kwa taarifa kamili

TANESCO HUDUMA KWA WATEJA

MAKAO MAKUU
Tanesco hili jibu lenu la kukimbia majukumu. Sijui lini mtajifunza namna bora ya kuhudumia wateja.
 
Kitaalamu hauwezi kujibu swali kwa ujumla wake bila kujua ukweli wa taarifa husika, kujibu hivyo ni blabla ambayo taasisi yenye wataalamu kama yetu haiwezi kukurupuka kujibu bila taarifa kamili
Hapo hujauliza taarifa kamili ndugu yangu wa TANESCO. Hii ni kwa sababu hii issue sio ya kwanza na inaonekana ni loophole ya tanesoco kudhulumu wateja. Rejea huu uzi hapa.

Hili limenitokea na roho inaniuma sana: TANESCO wanataka kufungia watu umeme kwenye transformer yangu kwa nguvu!

Vile vile tambua amekutajia wilaya aliyopo na changamoto zake. Kwa kumbukumbu zangu Tanesco hata mkipewa taarifa hamchukui hatua hata mara moja.

Anyway endeleeni kuwakamua watanzania kama kawaida gani.
 
Pole Sana mkuu, ila Kama Barua unayo iscan au piga picha tupia hapa jukwaani ili TANESCO walishughulikie suala lako!

Yawezekana ni wapiga dili wachache wanaharibu brand ya TANESCO
Tanesco hawana BRAND. Tanesco ni Kibanda cha wapiga dili. Tangu nchi hii ipate uhuru hakuna mahali pengine serikalini palipotumika kupiga dili kama TANESCO. Kuanzia KWA mbeba Nguzo mpaka Bodi ya wakurugenzi nafikiri akili zao zinawaza mitindo tofauti ya kupiga dili.
 
Tanesco hawana BRAND.Tanesco ni Kibanda cha wapiga dili.Tangu nchi hii ipate uhuru hakuna mahali pengine serikalini palipotumika kupiga dili kama TANESCO.Kuanzia KWA mbeba Nguzo mpaka Bodi ya wakulugenzi nafikiri akili zao zinawaza mitindo tofauti ya kupiga dili.
Tafadhali tupatie taarifa kamili za huduma gani tukuhudumie, eneo wilaya na namba ya simu

Tupo kukusikiliza
 
Tunaamini kabla ya kutuhumu tungepata taarifa kamili.kwanza nasisi tutoe ufafanizi sahihi hakuna mteja anayepaswa kuteseka nasisi TANESCO tupo
Hebu twende taratibu...

Let's say ninapoishi ni 5km kutoka eneo ambalo lina miundombinu ya TANESCO...

Je, nikitaka huduma yenu mtaniletea umbali wa 5 KM kwa gharama zenu?
 
Tafadhali tupatie taarifa kamili za huduma gani tukuhudumie, eneo wilaya na namba ya simu

Tupo kukusikiliza
Ndugu zangu Tanesco. Mimi niliripoti kesi zaidi ya 3 za TANESCO hapo kwenu makao makuu. Unajua mliniambiaje? Niende kwenye ofisi yenu kwa sababu ninyi hamfanyi kazi kwa coordination bali kila ofisi inafanya kazi kivyake so mkanipa namba za matawi yenu ambazo tayari nilikuwa nazo so sioni kama kuna jipya kutoka kwenu
 
Hebu twendeni taratibu...

Let's say ninapoishi ni 5km kutoka eneo ambalo lina miundombinu ya TANESCO...

Je, nikitaka huduma yenu mtaniletea umbali wa 5 KM kwa gharama zenu?
Utaletewa kama eneo lako lipo kwenye budget ya mwala husika, kama halipo unashauriwa kusubiri tukufikie kwa kuwa usambazaji wa umeme unaenda kwa awamu mbalimbali
 
Tumeshawaliana na mteja tunasubiri taarifa kamili hakuna hela inayopaswa kutolewa kwa mtu bali kwa taratibu zilizowekwa
Na taratibu zenu ni zipi kama sio hizo hizo za kupiga PESA za wanyonge
 
Ndugu zangu Tanesco.Mimi niliripoti kesi zaidi ya 3 za TANESCO hapo kwenu makao makuu.Unajua mliniambiaje?Niende kwenye ofisi yenu kwa sababu ninyi hamfanyi kazi kwa coordination bali kila ofisi inafanya kazi kivyake so mkanipa namba za matawi yenu ambazo tayari nilikuwa nazo so sioni kama kuna jipya kutoka kwenu
Je ulijibiwa ofisi ya wapi? Kama ni kweli samahani sana, tupatie taarifa zako kwa kuonesha

Jina

Eneo

Simu

Tatizo

Toka lini
 
Utaletewa kama eneo lako lipo kwenye budget ya mwala husika, kama halipo unashauriwa kusubiri tukufikie kwa kuwa usambazaji wa umeme unaenda kwa awamu mbalimbali
Tanesco,Acheni ubabaishaji.Mimi nafahamu kwamba issue sio bajeti.Issue ni ukiritimba wa kuhakikisha kuwa mnajenga mazingira ya upigaji.
 
Tanesco,Acheni ubabaishaji.Mimi nafahamu kwamba issue sio bajeti.Issue ni ukiritimba wa kuhakikisha kuwa mnajenga mazingira ya upigaji.
Twenda kwenye swala la msingi tafadhali kwani unapata changamoto gani?

Eneo

Wilaya

Simu

Mteja anatusaidia sisi kumuhudumia kwa kutoa ushirikiano
 
Back
Top Bottom