Tanesco Temeke: Umeme upo wa kutosha, shida miundombinu iliyopo haiwezi kutawanya umeme kwa wakati mmoja

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Kama ulikuwa unafikiria kwamba baada ya umeme wa bwawa na Nyerere kuanza kupatikana basi matatizo ya mgawo wa umeme yatakuwa yamekwisha, basi sasa ni wakati wa kubadili mawazo yako.

Tanesco wanasema kwamba, mgawo wa umeme Tanzania kimsingi hautokani na ukosefu wa umeme wa kutosha, bali ni kwa sababu miundombinu ya kutawanya umeme iliyopo haitoshi kupeleka umeme kwa kila mtumiaji kwa wakati mmoja!

Kwa kifupi wanasema chakula kipo kingi ila vyombo vya kukupakulia chakula ndio hatuna, basi endelea kuvumilia kukaa na njaa! Kwa hiyo usiuze generator yako, bado unaihitaji.

Serikali hii inatunyoosha kwelikweli!

----
Mkoa wa Kitanesco Temeke wamesema kuwa hawana changamoto ya uchache wa umeme, bali wana umeme mwingi isipokuwa miundombinu haina uwezo wa kubeba wingi wa umeme uliopo hali inayopelekea wananchi kupata mgao

Meneja mkoa wa kitanesco Temeke Ezekiel Mashora amesema Serikali imeleta mradi wa Dharula wa ujenzi wa nyaya utakaosaidia kusafirisha umeme kutoka kituo kimoja kwenda kingine na kuondoa mgao wa umeme kwenye maeneo ya Temeke, Mbagala na Kurasini.

 
Kuna siku nilikuwa nawaza moyoni hii Greed ya Taifa ameconstruct Nyerere na mahitaji kipindi kile yalikuwa chini sana. Bwawa la mtera, kidatu, vituo kama vya mgololo, mwakibete vyote ni kazi ya mwalimu. Walio fuata wote wakaridhika wakawa wanakarabati tuu. Ona sasa tumeingia kwenye mtego mkubwa sana
 
Watakuambia mwaka ule miundombinu ilikwa bado mipya😂🤣😂🤣
Mkono wa Chuma alijua kuwanyoosha hawa mabwege ukizingua anakufuata huko HUKO anakuja kukutimua tena anakufukuza waziwazi mbele ya mkeo na camera zinakuchukua,
 
Kuna siku nilikuwa nawaza moyoni hii Greed ya Taifa ameconstruct Nyerere na mahitaji kipindi kile yalikuwa chini sana. Bwawa la mtera, kidatu, vituo kama vya mgololo, mwakibete vyote ni kazi ya mwalimu. Walio fuata wote wakaridhika wakawa wanakarabati tuu. Ona sasa tumeingia kwenye mtego mkubwa sana
Mtego gani wewe hao wajinga wanataka kupiga hela tu mtego mtego wanataka kupiga hela hakuna mtego hapo
 
Taratibu.Ni mkoa wa kitanesco wa Temeke na amezungumzia Temeke,Mbagala na Kurasini.Hajazungumzia Nchi nzima.Wacha sensational news zisizo na tija.Kama una cha kusema njoo na hard facts.
 
Maskini! Nchi si yetu tena.....tunaendeshwa watakavyo😓
Uongozi wa nchi hii ni ule wananchi mahali fulani wanasema wana shida ya usafiri toka kijijini kwenda mjini kufuata huduma muhimu. Halafu serikali inawanunulia basi, then ndio inakumbuka hakuna barabara ya kutoka pale kijijini kwenda mjini!
 
Kila siku wanakuja na sababu tofauti, hiyo ni dalili ya uongo. Labda kama TANESCO imejaa wahandisi viazi ambao hawajui tatizo ni nini.
 
Taratibu.Ni mkoa wa kitanesco wa Temeke na amezungumzia Temeke,Mbagala na Kurasini.Hajazungumzia Nchi nzima.Wacha sensational news zisizo na tija.Kama una cha kusema njoo na hard facts.
Huyo ameizungumzia TANESCO kwa ujumla ndio ametoka na utetezi huo yaan kote sababu ni hio ya kiduanzi miaka Ile waliwezawezaje ku-maintain umeme bila kukatakata ovyo?
 
Taratibu.Ni mkoa wa kitanesco wa Temeke na amezungumzia Temeke,Mbagala na Kurasini.Hajazungumzia Nchi nzima.Wacha sensational news zisizo na tija.Kama una cha kusema njoo na hard facts.
Jaribu kufikiria mbali kidogo. Unafikiri kama hili tatizo lipo Temeke, Mbagala nk, kitu gani kinafanya lisiwepo kwingineko nchini?

Licha ya hivyo, hao watu wa Temeke Mbagala nk, ni halali kwao kuendelea kuwa na mgao wa umeme wakati umeme wa kutosha upo nchini?
 
Kila siku wanakuja na sababu tofauti, hiyo ni dalili ya uongo. Labda kama TANESCO imejaa wahandisi viazi ambao hawajui tatizo ni nini.
Usiwalaumu Tanesco, hata ww ukienda utafanya hayahaya - tatizo ni SERA zilizooza za nishati na usambazaji wake zinazotungwa na hao ma CCM.
 
Huyo ameizungumzia TANESCO kwa ujumla ndio ametoka na utetezi huo yaan kote sababu ni hio ya kiduanzi miaka Ile waliwezawezaje ku-maintain umeme bila kukatakata ovyo?
Umesikiliza clip na maelezo yote kwenye Twitter au unataka kuleta ubishi tu kutimiza agenda yako?
 
Kama ulikuwa unafikiria kwamba baada ya umeme wa bwawa na Nyerere kuanza kupatikana basi matatizo ya mgawo wa umeme yatakuwa yamekwisha, basi sasa ni wakati wa kubadili mawazo yako.

Tanesco wanasema kwamba, mgawo wa umeme Tanzania kimsingi hautokani na ukosefu wa umeme wa kutosha, bali ni kwa sababu miundombinu ya kutawanya umeme iliyopo haitoshi kupeleka umeme kwa kila mtumiaji kwa wakati mmoja!

Kwa kifupi wanasema chakula kipo kingi ila vyombo vya kukupakulia chakula ndio hatuna, basi endelea kuvumilia kukaa na njaa! Kwa hiyo usiuze generator yako, bado unaihitaji.

Serikali hii inatunyoosha kwelikweli!

----
Mkoa wa Kitanesco Temeke wamesema kuwa hawana changamoto ya uchache wa umeme, bali wana umeme mwingi isipokuwa miundombinu haina uwezo wa kubeba wingi wa umeme uliopo hali inayopelekea wananchi kupata mgao

Meneja mkoa wa kitanesco Temeke Ezekiel Mashora amesema Serikali imeleta mradi wa Dharula wa ujenzi wa nyaya utakaosaidia kusafirisha umeme kutoka kituo kimoja kwenda kingine na kuondoa mgao wa umeme kwenye maeneo ya Temeke, Mbagala na Kurasini.

View attachment 2910135
Tumepigwaa asee😂
 
Back
Top Bottom