Nimelia sana nilipofika bwawa la Mwalimu Nyerere, kwaheri mgawo wa umeme

MANKA MUSA

JF-Expert Member
Jul 9, 2014
922
1,093
Kutoka angani naliona Bwawa kubwa, liliojengwa kutoka kwenye urithi wetu wa mto Rufiji, katikati ya Hifadhi yenye jina lake Nyerere mtu wa kipekee. Naliona Bwawa lile na kukumbuka kwamba wakati Mama Kizimkazi anaingia madarakani lilikuwa 33% tu, angeliweza kuamua kuachana nalo, lakini kwa mapenzi kwa nchi yake na busara tele alizojaaliwa, sasa ndoto hii inaenda kutimia. Machozi ya furaha yalinilenga.

Mama ni mwenye maono na hesabu kali, ameukwepa mtego wa Umeme wa mafuta kama ule wa Symbion na Richmond kila wakati ulileta kashfa kubwa katika nchi yetu. Mawaziri kutoka kwa Kalemani aliyeanza kutoka asilimia 0-37 hadi kwa January aliyefikisha kutoka asilimia 37 hadi 91 mnastahili pongezi.

Mama amefunga mkanda hatimaye Megawatts 235 zimeingia leo kwenye gridi ya Taifa chini ya usimamizi wa Dkt Biteko mashine moja iliyowashwa kati ya Tisa zilizopo hapa ni sawa na vinu vinne vya bwawa la Kidatu, vinu vinne vina jumla ya megawatts 204 hapa JNHPP kuna vinu 9 kila moja kinazalisha megawatts 235 jumla zitazalisha megawatts 2115.

Mungu mkubwa, yeye alitupa Rais huyu mwenye maono na sasa ndoto ile ya umeme wa uhakika inakwenda kutimia.

Hakika Rais Samia anastahili pongezi toka siku ya kwanza ulipounga mkono kuendeleza jitihada hizi amelipigania utafutaji wa fedha nyingi na kutekeleza, Ulale salama Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuasisi mradi licha ya maneno mengi kwenye mradi huu ulisimama imara. Kwa taarifa miradi ya kimkakati uliyoiacha hakuna kilichosimama. Taifa linakushukuru.

Mama ameandika Historia kubwa sana itakayofuta vilio vya Wananchi wengi nimewaza juu ya kuimarika kwa upatikanaji wa Umeme. Tutawahadithia wajukuu zetu juu ya mgao mkali wa Umeme waone kama ni ndoto au ni jambo la kihistoria nyakati ngumu hazidumu mbele ya viongozi imara kama Rais Samia.

Dear Mama Samia, Hayati Baba wa Taifa na Hayati Magufuli alipo wamefurahi sana kuwa Rais Samia amekamilisha kile kilichokwama zaidi ya miaka 60.

Hongera sana Mama umeweza sana wacha nilie na dua njema, nakuombea.

#MamaYukoKazini

IMG-20240226-WA0001.jpg
 
 
NIMELIA SANA NILIPOFIKA BWAWA LA MWALIMU NYERERE, KWAHERI MGAO.

Kutoka angani naliona Bwawa kubwa, liliojengwa kutoka kwenye urithi wetu wa mto Rufiji, katikati ya Hifadhi yenye jina lake Nyerere mtu wa kipekee...
Nimesoma kufika katikati nikataka kuacha kusoma nikajua ni Lucas mwanshambwa, nikarudi juu kuangalia tena jina nikaona ni another mwashambwa nikaamua kumalizia kusoma.
 
Hapo nilipo bold ungesema Magufuli kulikuwa na shida gani!? Mama apewe maua yake kwa kuuendeleza.

JPM mlim sabotage. Toka JKN kuna marais watatu walitishwa na wazungu wakanywea. Chuma kikakaza mradi ukaanza, mama alikuwa hana jinsi imebidi amalizie tuu asingeweza kuutelekeza.
Sawa Mkuu ila rekodi iwekwe sawa kwamba Nyerere ndio aliyekuwa na maono akaanzisha mradi kwa kufanya taratibu zote za utafiti wa mazingira na utafiti wa capacity ya umeme na watalaam hawa JPM alikuta wameshalipwa hakuna deni.

Utafiti wa mradi wa umeme kama huo huchukua sio chini ya miaka 10.
Kwa miaka aliyokaa kwenye urais haiwezekani kufanya utafiti na kujenga kwa mradi mlubwa kiasi hicho.

Nyerere hakuweza kuujenga kwa kukosa fedha. Marais waiotangulia siwezi kuwasemea labda Mungu tu hakuwajalia katika hili, ila JPM apongezwe kwa kuthubutu kuchukua file na kutangaza tenda za ujenzi. Hapo apewe maua yake, lakini watu walidhani Mama atashindwa lakini kawasha bila kupiga tarumbeta kimya kimya mawaziri wanaongea yeye anapiga kazi. Hizo sabotage kwa JPM kuhusu huo mradi ndio kwanza tunakusukia wewe mkuu. Mungu ibariki Jamhuri ya Muungano Tanzaniia.
 
Back
Top Bottom