TANESCO inaweza ikatengeneza faida kubwa sana endapo wataanza kukopesha units za LUKU. Hii ni ngumu kwa mteja kukwepa marejesho

ina tofauti gani na wanachofanya kampuni za simu tayari kama Vodacom wana songesha ambapo wanaweza kukukopesha ukanunua salio? Wangefanya hii idea miaka kumi iliyopita ingekuwa sawa, kwa sasa washachelewa labda waweke viwango vya riba vya chini sana
 
ina tofauti gani na wanachofanya kampuni za simu tayari kama Vodacom wana songesha ambapo wanaweza kukukopesha ukanunua salio?
Salio la songesha unaweza ukalifanyia miamala mingi tofauti na Songesha - LUKU ambayo utanunua LUKU pekee na huwezi kufanya muamala mwingine.

Songesha ya Vodacom mtu anaweza kuacha kutumia Voda akahamia Tigo na kukopa tena kwa Tigo pesa lakini ukikopa LUKU hauwezi kubadili number ya LUKU. Ukinunua kwa mtandao mwingine wowote lazima wakukamate...
 
Mkuu serikali yenyewe hailipi madeni ya Tanesco sembuse Raia,wewe unataka hili shirika lishindwe kujiendesha. Tena nawashauri na watu wa mamlaka za maji waje la mita za luku kabisa ili kuboresha makusanyo
 
Infantry hebu jaribu kuliangalia hilo kwa mukitadha wa Wapangaji, Ni kweli Tanesco kwa mantiki hiyo atapata faida, lkn hasara itakuja kwa wenye nyumba, mpangaji nitakopa umeme nitatumia then nahama kambi, vipi apo ?
 
Usiwarudishe nyumba. Walianza na mita za kawaida (unalipa baada ya matumizi), but watu walikuwa hawalipi kwa wakati au hawalipi kabisa.

LUKU ndio mpango mzima. Tena wangeanza kwenye taasisi za serikali kabla ya watu binafsi.
 
Usiwarudishe nyumba. Walianza na mita za kawaida (unalipa baada ya matumizi), but watu walikuwa hawalipi kwa wakati au hawalipi kabisa.
TANESCO waliweka limit ya kiwango cha matumizi na malipo? Unamruhusu mtu atumie umeme mpaka wa 400,000/= unategemea nini?

Kukopa umeme wa 10,000/= haiwezi kuiua TANESCO hata siku moja mkuu...
 
Unawezaje kukwepa deni la 20,000/= la LUKU?
Mimi ni mpangaji,nakaa nyumba Luku yangu kila kitu sishei na mtu

hii system ikikubalika ikaanza si wapangaji kama sisi tunakua tunakopa

umeme wa LAKI naingia nakaa miezi 6 nahama deni linabaki kwenye nyumba ya watu

huoni hapo kuna kushikana mashati? wengine sisi tukihamia nyumba hatuonekani tumehamia saa ngapi

na tukihama hatujulikani tumehama saa ngapi yani tupo kama ma zombie huoni tuta taftia watu majanga yasio ya lazima bwana mjeshi?
 
Habari za wakati huu kaka na dada zangu wa humu JamiiForums.

Kwanini TANESCO haikopeshi units za umeme wa LUKU kwa wateja wake? Mimi ninaona kama mchakato huu utawawezesha kupata faida kubwa sana kama riba kwa maana ni ngumu sana kwa mteja kukwepa marejesho.

Tofauti ya mteja wa TANESCO na mteja wa mtandao wa simu za mikononi kama Vodacom na Tigo ni kwamba, mteja wa mitandao hii ana nafasi kubwa sana ya kutokulipa deni kwa maana anaweza kubadili simcard au anaweza kufa kisha deni likawa limepotea tofauti na mteja wa TANESCO ambaye deni linakuwa limebebwa na nyumba kiasi kwamba hata akifa, deni litakatwa wakati wa ku-transfer property ownership.

Mteja wa mitandao ya simu za mikononi anaweza akakopa Vodacom kisha akahama mtandao akaanza kutumia Tigo, lakini mteja wa TANESCO hawezi kubadili number yake ya mita ya LUKU. Kama alikopa umeme wa 20,000/= kwa kutumia M-PESA inakuwa ngumu sana kukopa tena kwa kutumia mtandao mwingine kama vile TIGO PESA kwa maana atatumia number ile ile ya mita hivyo computer system itakataa kufanya muamala wa kumpa units.

TANESCO wanaweza kufanya special arrangement na kampuni husika ya mtandao wa simu kama Vodacom au Tigo kutoka mkopo wa pesa mahususi kwa kununua units za umeme tu na sio muamala mwingine wowote. Ukitumia pesa hiyo kwa muamala mwingine inakataa.

Mathalana TANESCO wanaweza kukukopesha umeme wa 15,000. Halafu utakatwa labda 25% kila utakaponunua tena mpaka deni liishe. Au ukiamua unalipa 100%.

Wataalam wa masuala ya uchumi pamoja na ICT mnaweza kulifafanua hili zaidi kwa maana hiyo sio taaluma yangu lakini ninapendekeza number itakayoruhusiwa kukopa iwe moja tu (Mmiliki wa nyumba) hususan kwa nyumba zenye wakazi (wapangaji) wengi

NB: Ndugu zangu waislam, Mungu awatangulie na kuwasimamia katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani. Siku zote 30 za mfungo zikawe za kheri na baraka kwenu. Wishing you courage and strength so that you win every challenge of this life.

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Naunga mkono hoja kwa 100%
 
Kwann mnapenda sana mkopo? Hii system ya TANESCO kutokopesha ni nzuri. Kuna nyumba za kupanga au fremu za biashara.
Mtu anakopa umeme wa laki moja ukiisha anahama. Mzigo unamwangukia mwingine
Naona waweke tu mfumo,ukinunua umeme kwa mfano wa 5000 unajijaza wenyewe. Hakuna kwenda kujaza kwenye mita
hili ndio hata mimi nalitaka litokeee iwe kama tunavyolipia vifurushi vya ving'amuzi tu
 
Ni wapi nimezungumzia mkopo wa laki moja? Vodacom wanatoa mkopo wa laki moja kwa mara moja? Ndio maana nimesema anayeweze kuruhisiwa kukopa ni mtu mmoja tu.
Sio kila nyumba ya kupanga ina watu wengi, kuna nyumba mpangaji anamiliki luku yake peke ake

si kwamba kajiwekea ile luku ila n mwenye nyumba kaiweka,sasa kigezo kikiwa n mtu mmoja tu

nadhani mpangaji kama mimi nina sifa zote za kukopa maana nipo peke angu na baada ya mkopo kodi ikiisha 🏃‍♂️🏃‍♂️
 
Tumepokea ushauri tunashukuru sana mpendwa mteja wetu

TANESCO , Makao Makuu
Mnazingua kinoma hadi nahisi hii Account yenu huku JF pamoja na kuwa Verified nahisi kuna mtu binafsi kakaa geto anatuzingua,sioni kbisa msaada wenu nyie viumbe zaidi yakujibu kama ulivyojibu hapo juu.

Ngojea namimi niji verifaishe halafu naweka Profile pic la Tanesco najibadilishia na jina tukutane kwenye thread yetu pendwa ya Tanesco maswali na majibu,ngojeeeni muone.
 
Back
Top Bottom