TANESCO haina tena nguzo za kusambaza umeme majumbani

sikuamini hata kidogo, upo Mji gani? Nguzo zimejaa na hata mita, umeme mpaka vijijini wewe unataka nguzo za nini tena? unganisha umeme wa REA funga kinu sagisha uwele
Umeme wa Rea ni wa kisiasa. Ni wa kuwashia TV na kuchajia simu hauna nguvu ya kuwasha mashine. Umeme wenye nguvu ni three phase yenye nyaya 3 au zaidi na pawe na transformer ya 33kv na zaidi.
 
Umeme wa Rea ni wa kisiasa. Ni wa kuwashia TV na kuchajia simu hauna nguvu ya kuwasha mashine. Umeme wenye nguvu ni three phase yenye nyaya 3 au zaidi na pawe na transformer ya 33kv na zaidi.
Hakuna kitu kama hicho, mimi huku nilipo kwa sasa, umeme ni wa mradi wa REA, na kuna mashine nyingi sana, za kukoboa mpunga, zenye kutumia three phase.umeme huo wanautoa kwenye HT, Za tanesco, sema sehemu nyingi wanachobania ni transfoma kuwa chache hivyo kupelekea umeme kuwa na nguvu kidogo, kulinganisha na mahitaji!!!na hili hujitokeza baadaye watumiaji wanapokuwa wanaongezeka.
Kuhusu kuwa na nyaya tatu(three phase) sio kila mtumiaji ana kuwa na sifa hiyo, kuwekewa , bali mahitaji yako ndio yatakufanya uwekewe hiyo, na gharama zake huwa ziko juu.
 
Nenda Tanesco wakupe namba ya saveya kisha mpe rushwa saveya ili saveya aje. Amasivyo utasubiria miezi sita mpaka mwaka na nusu. Na akimaliza kazi akikupigia hesabu ya vifaa jiandae kisaikolojia kununua nguzo na gharama za line.
Wala inshu sio namba ya surveyor, kuja kufanya survey, atakuja sawa, labda kama hakuna hitaji la nguzo, lakini kama kuna hitaji la nguzo na mfumo unaotumika sasa tanesco, wa FIFO, na nguzo zenyewe ndio hizo hakuna, ataliwa pesa zake na umeme hatapata kwa muda anaotaka yeye!!siku amesahau ndio ataona wanampigia simu tunakuja kukufungia umeme.unaongea kama una mtisha vile wakati kitu kipo wazi, majukumu ya saveya akija ni kuangalia mchoro wako wa wiring basi, na kupiga hesabu ya umbali toka ilipo njia kuu ya umeme, kama ni zaidi nguzo mbili, hiyo tena kwa mtu mmoja imeshakuwa mtihani, lazima ijengwe njii yake!lakini kama ni nguzo 1, 2, utapigiwa hesabu kalipie, subilia foleni ikufikie.
 
Wala inshu sio namba ya surveyor, kuja kufanya survey, atakuja sawa, labda kama hakuna hitaji la nguzo, lakini kama kuna hitaji la nguzo na mfumo unaotumika sasa tanesco, wa FIFO, na nguzo zenyewe ndio hizo hakuna, ataliwa pesa zake na umeme hatapata kwa muda anaotaka yeye!!siku amesahau ndio ataona wanampigia simu tunakuja kukufungia umeme.unaongea kama una mtisha vile wakati kitu kipo wazi, majukumu ya saveya akija ni kuangalia mchoro wako wa wiring basi, na kupiga hesabu ya umbali toka ilipo njia kuu ya umeme, kama ni zaidi nguzo mbili, hiyo tena kwa mtu mmoja imeshakuwa mtihani, lazima ijengwe njii yake!lakini kama ni nguzo 1, 2, utapigiwa hesabu kalipie, subilia foleni ikufikie.
Basi mkuu, umeshinda.
 
Basi mkuu, umeshinda.
Sio kama nimeshinda mkuu, hawa wanasiasa ndio wameshatuona wananchi mapimbi!!ki ukweli kwa sasa tanesco hawana nguzo kabisa, juzi kuna jamaa yangu aliposikia eti kuna umeme wa 27, 00 akaenda , yeye anatakiwa nguzo moja, wamempigia hesabu ni kama 320, 000!! Akauiliza vipi inakuwaje bei hiyo, walichomjibu, achana na matamko ya wanasiasa!!na wakamwambia hata ukilipia leo, subilia labda ndani ya siku 60 -90 za kazi!!kwa sasa kuna uhaba wa nguzo.
 
Sio kama nimeshinda mkuu, hawa wanasiasa ndio wameshatuona wananchi mapimbi!!ki ukweli kwa sasa tanesco hawana nguzo kabisa, juzi kuna jamaa yangu aliposikia eti kuna umeme wa 27, 00 akaenda , yeye anatakiwa nguzo moja, wamempigia hesabu ni kama 320, 000!! Akauiliza vipi inakuwaje bei hiyo, walichomjibu, achana na matamko ya wanasiasa!!na wakamwambia hata ukilipia leo, subilia labda ndani ya siku 60 -90 za kazi!!kwa sasa kuna uhaba wa nguzo.
Duh! Kwani Iringa kwa Qwihaya nguzo zimeisha. Au kazidiwa na order?
 
Duh! Kwani Iringa kwa Qwihaya nguzo zimeisha. Au kazidiwa na order?
Kulikuwa na mgogoro baina ya wazarishaji wa nguzo na makampuni yanayozinunua na kuiuzia tanesco!!haya makampuni yanayonunua nguzo kila leo yanapunguza bei ya kununua, sasa na wazarishaji wakazikataa bei hizo!!juzi naibu waziri alikuwa huko.Lakini tatizo sio hilo tu hata fedha zenyewe za kuwalipa hao wakandarasi ni tabu tupu!!ljana namsikia amerukia kwenye bei ya gesi za kupikia majumbani, kuwa ametoa siku 14, washushe!!!
 
Kulikuwa na mgogoro baina ya wazarishaji wa nguzo na makampuni yanayozinunua na kuiuzia tanesco!!haya makampuni yanayonunua nguzo kila leo yanapunguza bei ya kununua, sasa na wazarishaji wakazikataa bei hizo!!juzi naibu waziri alikuwa huko.Lakini tatizo sio hilo tu hata fedha zenyewe za kuwalipa hao wakandarasi ni tabu tupu!!ljana namsikia amerukia kwenye bei ya gesi za kupikia majumbani, kuwa ametoa siku 14, washushe!!!
Hivi hao wazalishaji wa nguzo kama Qwihaya wanamuuzia nani? Je ni Tanesco au Wakandarasi wa Rea? Au inakuwaje? Je wanalipa kwanza halafu ndio nguzo wanachukua, au wanachukua nguzo halafu wanalipa baadae?
 
Hivi hao wazalishaji wa nguzo kama Qwihaya wanamuuzia nani? Je ni Tanesco au Wakandarasi wa Rea? Au inakuwaje? Je wanalipa kwanza halafu ndio nguzo wanachukua, au wanachukua nguzo halafu wanalipa baadae?
Kwenye miradi ya REA, baada ya mkandarasi kuwa ameshinda Tenda, yeye ni kujenga line tu, vifaa vyote analetewa na tanesco, tanesco wao ndio huwa wanatangaza zabuni kwa makampuni, yanayoshinda yanapewa hizo kazi, za nguzo, yanaenda mfano sao hills, au kwa wazalishaji wengine wa nguzo, na kuingia nao mikataba, tanesco akiwa kama mdhamini, inategemea na makubaliano, yao lakini mala nyingi huweza kulipa advance tu, nyingine badaye.
 
Kwenye miradi ya REA, baada ya mkandarasi kuwa ameshinda Tenda, yeye ni kujenga line tu, vifaa vyote analetewa na tanesco, tanesco wao ndio huwa wanatangaza zabuni kwa makampuni, yanayoshinda yanapewa hizo kazi, za nguzo, yanaenda mfano sao hills, au kwa wazalishaji wengine wa nguzo, na kuingia nao mikataba, tanesco akiwa kama mdhamini, inategemea na makubaliano, yao lakini mala nyingi huweza kulipa advance tu, nyingine badaye.
Duh! Sasa imekuwaje huko? Je oda ni nyingi? Au madeni? Maana serikali huwa inachelewa mno kulipa madeni....... Nini kimetokea?
 
Duh! Sasa imekuwaje huko? Je oda ni nyingi? Au madeni? Maana serikali huwa inachelewa mno kulipa madeni....... Nini kimetokea?
Kwa muda mwingi nch hii wakandarasi wanaofanya kazi na serikali wanakuwa hoi, kutokana na pesa zao kutolipwa kwa wakati, hasa awamu ya tano immewaacha hoi mno!!una kuta wakandarasi wengine wanakwenda kwenye taasisi za fedha kukopa pesa, ili ziwasaidie kwenye hizi tender wanazopata, mfano usafirishaji wa nguzo, hata kuzinunua, sasa balaa ni kwenye yeye kulipwa ndio utasikia tuna hakiki, .Mkuu elewa tu kwa sasa hali bado sio nzuri serikalini, hasa ni kutokana na madeni ya nyuma, miradi mikubwa mikubwa iliyoachwa!!!fikiria wizara ya mambo ya ndani tu ilikuwa inadaiwa wa wakandarasi wa ndani karibia 50 bilioni!!huko nyuma juzi ndio wameanza kuzipunguza!!unadhania huyo mzabuni alikuwa kwenye hali gani?!!kufanya kazi na serikali yataka moyo, japo kuna faida kubwa, na uhakika wa malipo, kuhusu lini hiyo ni inshu nyingine tena
 
Kwa muda mwingi nch hii wakandarasi wanaofanya kazi na serikali wanakuwa hoi, kutokana na pesa zao kutolipwa kwa wakati, hasa awamu ya tano immewaacha hoi mno!!una kuta wakandarasi wengine wanakwenda kwenye taasisi za fedha kukopa pesa, ili ziwasaidie kwenye hizi tender wanazopata, mfano usafirishaji wa nguzo, hata kuzinunua, sasa balaa ni kwenye yeye kulipwa ndio utasikia tuna hakiki, .Mkuu elewa tu kwa sasa hali bado sio nzuri serikalini, hasa ni kutokana na madeni ya nyuma, miradi mikubwa mikubwa iliyoachwa!!!
Aisee mkuu, yaani ukijumlisha na hii Tozo mtu unajisikia kuumwa Kabisa.
 
Aisee mkuu, yaani ukijumlisha na hii Tozo mtu unajisikia kuumwa Kabisa.
Ki ukweli, acha tu, lakini haya yote wameshatuona kwani hawa pimbi watafanya nini?watapiga kelele siku mbili tu, watasahau!!maisha yatendelea, sio ajabu ukaja kuona watu wameandamana kupongeza hizi tozo kuwa MAMA, anatupenda kuzileta kwani ndio muarobaini wa sisi kina mama kujifungulia njiani!!na wakapewa airtime ya kutosha!!!wanaotupigania, tunawaona wajinga.wakati mwingine unasema sawa hadi akili itukaeee
 
Ki ukweli, acha tu, lakini haya yote wameshatuona kwani hawa pimbi watafanya nini?watapiga kelele siku mbili tu, watasahau!!maisha yatendelea, sio ajabu ukaja kuona watu wameandamana kupongeza hizi tozo kuwa MAMA, anatupenda kuzileta kwani ndio muarobaini wa sisi kina mama kujifungulia njiani!!na wakapewa airtime ya kutosha!!!wanaotupigania, tunawaona wajinga.wakati mwingine unasema sawa hadi akili itukaeee
😂
 
Mimi nimeambiwa surveyor atakuja kukagua aone kama kweli nahitaji nguzo,mwezi wa pili huu sasa,kila nikiuliza naambiwa ana kazi nyingine atakuja...mapinga jirani tuu na Dar
Yaani hii ipo kila mahali, mimi huu ni mwezi wa 3
 
Katika Hali isiyo ya kawaida ,Kwa mara ya kwanza tangu awamu ya tano,imetokea Hali isiyo ya kawaida ya kukosekana Kwa nguzo za kuunganisha wateja umeme Tanzania. Hakuna wilaya hata moja nchini insyotoa huduma ya kuwapatia wateja nguzo ili wananchi waweze kupata huduma ya umeme. Kila ukiuliza unaambiwa tunaweka nguzo keenye bajeti. Ni bajeti ipi hiyo ambayo ilisomwa July na Sasa ni August.
Tafadhali tusaidie umeomba au kulipia umeme kwa jina gani? Wilaya na namba ya simu
 
Tafadhali tusaidie umeomba au kulipia umeme kwa jina gani? Wilaya na namba ya simu
Piga namba zifuatazo wakueleze Hali ilivyo mbaya kuhusu nguzo za tanesco.
1. 0784-422-884
2.0784-390-625
3. 0682-304-430
Ukipata majibu nijulishe walichokuambia. Tatizo tanesco mnaficha matatizo. Tangu bei ya kuunganishiwa umeme iwe Tsh 27,000 hamjawahi kuhufumia mteja hata mmoja kumpatia nguzo Kwa bei hiyo.
JPM tutamkumbuka sana'
 
Piga namba zifuatazo wakueleze Hali ilivyo mbaya kuhusu nguzo za tanesco.
1. 0784-422-884
2.0784-390-625
3. 0682-304-430
Ukipata majibu nijulishe walichokuambia. Tatizo tanesco mnaficha matatizo. Tangu bei ya kuunganishiwa umeme iwe Tsh 27,000 hamjawahi kuhufumia mteja hata mmoja kumpatia nguzo Kwa bei hiyo.
JPM tutamkumbuka sana'
Ahsante kwa taarifa tumezipokea
 
Back
Top Bottom