DOKEZO Nguzo za Umeme zimekatika Nyasaka (Mwanza), tumeripoti TANESCO hawatujali Wananchi

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
photo_2024-02-21_09-05-43 (2).jpg
Sisi Wananchi wa Mtaa wa Chamwenda, Kata ya Nyasaka, Wilaya ya Ilemela Mkoa wa Mwanza tunaomba hii kero yetu iwafikie TANESCO.

Hili Shirika letu la Umeme tumeshtoa taarifa kwao kuhusu changamoto ya nguzo kukatika lakini hakuna hatua zilizochukuliwa.

Tumeenda mbele na kuamua kuwapigia picha kabisa ya nguzo hizo na kuwatumia kwa njia ya WhatsApp lakini hakuna chochote kilicho fanyika zaidi ya mafundi wao kuja, wanaangalia, wanasema “Tunafuata nguzo”, baada ya hapo hawarudi tena.

Taarifa ya kwanza tulitoa tarehe 29/01/2024, wakatupa namba ya taarifa 5397392, walikuja kisha wakaondoka wakisema wanafuata nguzo lakini hawakuwahi kurudi tena.

Tukarudia kutoa taarifa tarehe 06/02/2024 napo wakatoa tena namba ya taarifa 5535978 lakini paka leo hii hawajaonekana.

Hizi nguzo ni hatari kwa watu wote wanaopita maeneo hasa majirani ambao tunaona muda wowote zinaweza kuanguka na kusababisha madhara.
photo_2024-02-21_09-05-43.jpg

photo_2024-02-21_09-05-42.jpg
 
Tukarudia kutoa taarifa tarehe 06/02/2024 napo wakatoa tena namba ya taarifa 5535978 lakini paka leo hii hawajaonekana
 
Hili Shirika letu la Umeme tumeshtoa taarifa kwao kuhusu changamoto ya nguzo kukatika lakini hakuna hatua zilizochukuliwa.
TANESCO wanataka per diem iliyonona mkiambatanisha na gharama za nguzo ndio waje kuondoa hilo linguzo libovu, sasa hapo walivyo washenzi wanasubiri mpaka lishuke liue mtu kwanza lisababishe maafa kwenye baadhi ya nyumba za watu, alafu ndio utawaona hao wamekuja na nguzo nyingine na Magari wao mbwembwe kibao
 
Back
Top Bottom