Tambua namna ya kujua uhalali wa mileage ya gari unalonunua Yard au kwa mtu

Msolid1990

Senior Member
Apr 2, 2012
144
50
Wakuu Habari,
Leo nimeona nielezee kidogo kwa namna gani unaweza kujua uhalali wa kilometer zinazosoma kwenye gari unalotaka kununua either mkononi kwa mtu ama yard.

Hii njia haitaweza kuapply kwa magari yote kwa sababu mbali mbali ikiwemo kwamba kipindi fulani hapa nyuma magari yalikuwa yanakaguliwa hapa Tanzania na sio nchi yanakotokea kama Japan.

TBS wametoa mamlaka ya ukaguzi wa magari yote yanayokuja Tanzania kutokea Japan kampuni inayojulikana kama EAA COMPANY LIMITED(EAA Company Ltd – EAA Company Ltd), ukishanunua gari Japan kabla ya kuwa shipped litapelekwa kwenye hii kampuni na watalikagua na likikidhi vigezo vya kuingiza gari Tanzania basi gari litapatiwa Document inaitwa Certificate of Roadworthness. Hii kampuni inafanya ukaguzi pia wa Magari yanayoenda nchi nyingine kama Bahamas, Mauritius, Uganda, Zambia, Zimbabwe n.k. Kwa wenzetu wa Kenya wao shirika lao la viwango (Kenya Bureau of Standards) wanatumia kampuni inayoitwa QISJ(Quality Inspection Services Japan) kukagua magari yanayoenda Kenya.

Kwa kampuni ya EAA tunayotumia Tanzania wakishafanya ukaguzi na gari likafanikiwa kupass inspection, basi linapatiwa certificate of roadworthness. Lakini pia wana huduma ya E-certificate which means wanakuwa na hii certificate mtandaoni ambapo kunakuwa na category mbili moja ni Exporter E-Certificate na nyingine ni General Public/Client E-certificate access.

Kwa upande wa Exporter E-certificate hapa inahitaji access kuweza kuingia na kupata hiyo certificate, kwa upande wa General Public/Client E-certificate unachohitaji hapa ni Chasis number/ VIN number ya gari tu ili uweze kuona baadhi ya taarifa muhimu za hiyo gari wakati wa ukaguzi.

Sasa mojawapo ya kipengele kinachoonekana kwenye details za gari baada ya kufanyiwa ukaguzi ni kitu wanaita INSPECTED MILEAGE ambacho kinaonyesha siku gari limekaguliwa odomoter yake ilikuwa inasoma kilometer ngapi, na hii ni baada ya kampuni ya ukaguzi ya EAA kujiridhisha kwamba odomoter haijachezewa.

UKITAKA KUVERIFY GARI UNALOTAKA KUNUNUA UFANYEJE?
  • Tafuta Chasis number ya gari unalotaka kununua
  • Ingia kwenye website ya kampuni ya EAA hapa (E-certificates)
  • Kisha ingiza chasis numbe yako mara nyingi zinakuwa kwenye mfumo wa (XXXX-XXXXX)
  • Kisha bonyeza kitufe cha Verify certificate, utaona details za gari ikiwemo inspected mileage
MFANO.
Niliona gari inauzwa Instagram na kulingana na taarifa za inspection inaonekana imeingiza Tanzania miezi michache iliyopita kwa kuwa kwenye mwezi wa 8 ndo ilifanyiwa inspection plus shipping days itakuwa imeingia tu juzi kati hapa, kwa hiyo lilikuwa linauzwa kama gari Jipya na kwenye plate number wameweka chasis number na wanaonyesha Milleage ni Km 48139, Lakini nilivyochukua chasis number ya hili na kuweka kwenye website ya EAA inaoenakana inspected mileage kule Japan ilikuwa ni Kilometer 165,731 kwa maana kwamba kilometer zimeshushwa kwa takribani 100,000+ lilivyoingia Tanzania.

Nitaweka picha mbili(Tangazo la instagram na pia details za ukaguzi) nikiwa nimeficha details nyingine kwa sababu ni biashara za watu.

Ni vizuri kujua uhalali wa mileage ya gari unalonunua kuepusha kuuziwa gari lenye milleage kubwa kwa bei ya gari lenye mileage kidogo.
 

Attachments

  • instagram.jpeg
    instagram.jpeg
    41.7 KB · Views: 91
  • EAA details.jpeg
    EAA details.jpeg
    51.2 KB · Views: 95
Wakuu Habari,
Leo nimeona nielezee kidogo kwa namna gani unaweza kujua uhalali wa kilometer zinazosoma kwenye gari unalotaka kununua either mkononi kwa mtu ama yard.
Hii njia haitaweza kuapply kwa magari yote kwa sababu mbali mbali ikiwemo kwamba kipindi fulani hapa nyuma magari yalikuwa yanakaguliwa hapa Tanzania na sio nchi yanakotokea kama Japan.
TBS wametoa mamlaka ya ukaguzi wa magari yote yanayokuja Tanzania kutokea Japan kampuni inayojulikana kama EAA COMPANY LIMITED(EAA Company Ltd – EAA Company Ltd), ukishanunua gari Japan kabla ya kuwa shipped litapelekwa kwenye hii kampuni na watalikagua na likikidhi vigezo vya kuingiza gari Tanzania basi gari litapatiwa Document inaitwa Certificate of Roadworthness. Hii kampuni inafanya ukaguzi pia wa Magari yanayoenda nchi nyingine kama Bahamas, Mauritius, Uganda, Zambia, Zimbabwe n.k. Kwa wenzetu wa Kenya wao shirika lao la viwango (Kenya Bureau of Standards) wanatumia kampuni inayoitwa QISJ(Quality Inspection Services Japan) kukagua magari yanayoenda Kenya.

Kwa kampuni ya EAA tunayotumia Tanzania wakishafanya ukaguzi na gari likafanikiwa kupass inspection, basi linapatiwa certificate of roadworthness. Lakini pia wana huduma ya E-certificate which means wanakuwa na hii certificate mtandaoni ambapo kunakuwa na category mbili moja ni Exporter E-Certificate na nyingine ni General Public/Client E-certificate access.
Kwa upande wa Exporter E-certificate hapa inahitaji access kuweza kuingia na kupata hiyo certificate, kwa upande wa General Public/Client E-certificate unachohitaji hapa ni Chasis number/ VIN number ya gari tu ili uweze kuona baadhi ya taarifa muhimu za hiyo gari wakati wa ukaguzi.
Sasa mojawapo ya kipengele kinachoonekana kwenye details za gari baada ya kufanyiwa ukaguzi ni kitu wanaita INSPECTED MILEAGE ambacho kinaonyesha siku gari limekaguliwa odomoter yake ilikuwa inasoma kilometer ngapi, na hii ni baada ya kampuni ya ukaguzi ya EAA kujiridhisha kwamba odomoter haijachezewa.

UKITAKA KUVERIFY GARI UNALOTAKA KUNUNUA UFANYEJE?
  • Tafuta Chasis number ya gari unalotaka kununua
  • Ingia kwenye website ya kampuni ya EAA hapa (E-certificates)
  • Kisha ingiza chasis numbe yako mara nyingi zinakuwa kwenye mfumo wa (XXXX-XXXXX)
  • Kisha bonyeza kitufe cha Verify certificate, utaona details za gari ikiwemo inspected mileage
MFANO.
Niliona gari inauzwa Instagram na kulingana na taarifa za inspection inaonekana imeingiza Tanzania miezi michache iliyopita kwa kuwa kwenye mwezi wa 8 ndo ilifanyiwa inspection plus shipping days itakuwa imeingia tu juzi kati hapa, kwa hiyo lilikuwa linauzwa kama gari Jipya na kwenye plate number wameweka chasis number na wanaonyesha Milleage ni Km 48139, Lakini nilivyochukua chasis number ya hili na kuweka kwenye website ya EAA inaoenakana inspected mileage kule Japan ilikuwa ni Kilometer 165,731 kwa maana kwamba kilometer zimeshushwa kwa takribani 100,000+ lilivyoingia Tanzania.

Nitaweka picha mbili(Tangazo la instagram na pia details za ukaguzi) nikiwa nimeficha details nyingine kwa sababu ni biashara za watu.

Ni vizuri kujua uhalali wa mileage ya gari unalonunua kuepusha kuuziwa gari lenye milleage kubwa kwa bei ya gari lenye mileage kidogo.

Asante sana kwa hii elimu
Itoshe kusema gari ya show room ni Bahati nasibu
Nyingi zimerudiwa rangi piaa na kushonewa leather seat

Huwa nashangaa na kujiuliza
Hivi inawezekanaje gari ya 2007 eti ina km efu40
Zaidi ya miaka 20 so ilikuwa imepaki au
Halafu unakuta rangi inang’aa hakuna ht dent
 
Asante sana kwa hii elimu
Itoshe kusema gari ya show room ni Bahati nasibu
Nyingi zimerudiwa rangi piaa na kushonewa leather seat

Huwa nashangaa na kujiuliza
Hivi inawezekanaje gari ya 2007 eti ina km efu40
Zaidi ya miaka 20 so ilikuwa imepaki au
Halafu unakuta rangi inang’aa hakuna ht dent
Mbona hata huko Japan ndicho wanachofanya? Gari unayoiona kwenye website inakuwa imerekebishwa na kutengenezwa sababu ni mtumba. Ukitaka mpya kabisa ni kiwandani.

Hii ya kurudisha km nyuma huku kwetu ndo tatizo, ni tatizo sababu tunapenda kununua kitu huku ukiwaza kukiuza hivyo tunatamani kudanganywa kuwa km ni chache ili wakati tunauza tumshikishe mwingine. Mtanzania yupo tayari kununua gari namba D yenye km 70,000 zilizorudishwa nyuma na engine imechezewa kuliko kununua namba A yenye km 200,000 yenye historia iliyo wazi ya service na iliyotunzwa. Kwann? Nani atanunua namba A siku akitaka kuuza? Bora apambane na namba D bovu atakuja kulitoa tu.

Ukitumia akili ya kawaida Haiitaji kampuni ya ukaguzi ya nje kukwambia hizi km sio halisi unaponunua ist yenye miaka zaidi ya mi5 hapa nchini na km chini ya 150,000 wauzaji wanawapa kitu wateja wanataka na wateja wanataka sifa kuwa kanunua gari jipya kwa bei rahisi na upya maana yake ni km chache na namba za juu bila kujali gari imetoka kenya, ug, zanzibar au Japan. Iwe namba D tu na km chache.
 
Ni Bora ninunue gari mikononi mwa MTU aliyeagiza gari Japan kuliko kwenda kununua gari yard ingawa sio yard zote zenye ujanja mwingi Ila ukiona watu wanatangaza Sana biashara zao kwenye social media ni hatari sana...kuna Raha kubwa Sana kuagiza gari kutoka nje alafu ukishazoe kufanya hivyo hautaweza kununua hapa bongo
 
Ni Bora ninunue gari mikononi mwa MTU aliyeagiza gari Japan kuliko kwenda kununua gari yard ingawa sio yard zote zenye ujanja mwingi Ila ukiona watu wanatangaza Sana biashara zao kwenye social media ni hatari sana...kuna Raha kubwa Sana kuagiza gari kutoka nje alafu ukishazoe kufanya hivyo hautaweza kununua hapa bongo
... na ni kwanini ukanunue gari yard badala ya kuagiza mwenye Japan? Hizi yard za kibongo magumashi? Never ever!
 
Waharibifu wanao rudiaha nyuma hizo kitu, inachengesha kona kwenye swala za kufanya services and maintenance.. Unajua gari haijambe kumbe inakaribia kukata 200000km
 
Ikiwa ukikoboa mpunga unapata mchele, na mchele huo huo ukiuwekea mafuta au tui la nazi ukapika unatokea wali... Basi hatuna budi kusema wajinga ndio waliwao
 
Hebu saidia jukwaa tuwe tunaangalia nini zaid
Kwa Japan ni ngumu ila SA tunaangalia mwaka wa gari na hasa hizi za 2010 kuja juu wakati Japan gari ya 2004 ipo sokoni tena inagombaniwa SA zipo ila chache sana wengi wanatembea na model za karibu ndio zipo sokoni..
 
Back
Top Bottom