Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 92,231
- 113,608
No cuppy Kyeruuuuuu ni alama ya mshangao kwa wachaga....
Oooh....
No cuppy Kyeruuuuuu ni alama ya mshangao kwa wachaga....
Oooh....
nyie watoto wa shaban robert mlizoea kutoka na watoto wa kihindi..Ndiyo maana mlikaa kihindi hindi sana.....mlikuwa sleki sana shaban robert na mzizima....watoto wa uswahilini mlikuwa hamuwawezi....
Mimi nilikuwa mgumu wa Tambaza. Nilikuwa nawapora hela watoto wa SRSS
Basi huo si ugumu bali ulikuwa mwizi....LOL!
It will always be in my memory,
Vurugu ya mwisho tuliingia Azania na chupa za mafuta yas petrol kama mabomu, nikiwa form two.
Tukarusha mabomu mawili laboratory ya Azania, wakawahi kuizima.Mara Azania wakatoka na makwanja , tumo ndani ya senyenge zao! Kilichotokea baada ya hapo inabaki historia.
Nilikimbia jangwani mabondeni huko nikakutana na tope linanuka vibaya sana, kuna wanafunzi wa azania walikuwa huko walikula kibano.It was war-like zone
Lakini nakiri afadhali walituhamishia mikoani, maana nisingemaliza salama, umri wa kubalehe ule na kufuata mob saikoloji ungetumaliza.
Ulikuwa ukituleta darasani moto wa kuotea mbali!! makonda walikuwa wanaheshimu Tambaza bwana
Label ya shule ilikuwa kali mpaka leo sijaona mfano wake, yangu ilikuwa kijani-group two!
SAMBUKILE-TAMBAZA!!!!!!!!!!!!!!!
Sikonge haya wabeja mayo!...naona Julius kakimbia...hivi swali langu ni hivi kwa nini shule nyingi za wanaume watupu tanzania or mchanganyiko zilikuwa na fujo sana na kujiona ni wababe kupita kiasi...shule kama Forest/kigurunyembe enzi hizo ilikuwa inaongoza kwa ufuska,tambaza kwa fujo,Ilboru handsome boys (some-to-do)...kuna shule moja moshi/arusha pia wavulana walikuwa na fujo sana nimeisahau jina....sijui kama zile tabia za zamani hadi leo bado zipo...
Lakini nakiri afadhali walituhamishia mikoani, maana nisingemaliza salama, umri wa kubalehe ule na kufuata mob saikoloji ungetumaliza.
Wabs,
Aliyepiga picha hii atakuwa amesimama karibu na kisima fulani cha zamani kilikauka kikawa kama jaa la taka.
Hiyo picha inakumbusha mbali sana, hapo mlangoni kulikuwa na kijiwe cha kutesa njuka.
Napenda tu kusema kuwa kati hao jamaa waliokwenda mkoa kuna jamaa niliwakuta pale Iyunga Tech sec. Mbeya(enzi hizo).
Jamaa kweli walikuwa distinguished character.
We ulienda wapi mazee?
Bi Maringo,
Ngoja niweke maneno ya Waberoya:
Nafikiri hii ilikuwa ikichangiwa na kukosa wanawake basi inakuwa ni bomu litakalolipuka muda wowote.
Wasichana kama wapo wanasaidia kutuliza ujinga wa wavulana. Wengine huwa wanabaki kuonyesha ubabe wao kwa Wasichana badala ya wenzao. Nakumbuka nikiwa Tech. College Arusha, vijana wa Ilboru walifunga timu zote kwa mpira na mwisho wakaja kwetu wakapata goli zao za kutosha na hawakurudi tena. Mwisho ukaja ugomvi wa Wasichana wa Machame Sec. Kuna graduation moja ya Ilboru wakaja Machame. Jamaa wachache wa TCA wakazamia na wakakipata kibano. Basi ilipofika next weekend jamaa wakaja kuangalia Video show pale TCA, wakatimuliwa. Ila kwa sababu kilikuwa ni chuo, wengine ni watu wazima na wengine na wasichana, hii kitu ilikufa wiki hiyohiyo. Wiki lililofuata jamaa hawakuwa na muda wa kukaa kuwawinda Ilboru wasizamie Video Show. Kwa hali ilivyokuwa pale ilikuwa inaonekana ni jambo la kitoto sana ingawa baadhi yetu kama tungelikuwa ni Secondary na wenzetu wamepigwa basi tungelitembeza kibano.
Nikiwa Mazengo tulishashika makwanja kwenda kuwatandika jamaa wa Mazengo Flats kwa sababu wenzetu wawili walipigwa na watu wa sehemu hiyo. Mungu bariki jamaa wakampelekea headmaster habari (Mzee Mkoba) na akaja mbio kututuliza na kuahidi atafuatilia hadi wjamaa wakamatwe na hilo lisirudie tena. Ila ilisaidia kwani baadhi ya mambo yalibadilika.
Namaliza Umbwe ile hali ya umoja wa wanafunzi ikawa imeenea kwa wote, uko nako tukalianzisha na shule ya jirani inaitwa Lyamungo, pigana sana baada ya kufungwa goli moja kwenye football!!!!, acha bwana; foolish age we iache tu!!
Iyunga Tech nayo ilikuwa familia ile ile ya shule za vurugu...
Kweli mkuu, ila tuache utani kipindi kile ukimaliza boarding au shule za jinsia moja unatoka umeiva , zilikuwa zinafundisha maisha, I mean people were bright at that time,
Shule za wavulana tupu au wasichana tupu regardless day au boarding walikuwa wanafanya vizuri sana
Nasikia serikali inataka kuua kabisa boarding, mama yangu!!
Bi Maringo,
Ngoja niweke maneno ya Waberoya:
Nafikiri hii ilikuwa ikichangiwa na kukosa wanawake basi inakuwa ni bomu litakalolipuka muda wowote.
Wasichana kama wapo wanasaidia kutuliza ujinga wa wavulana. Wengine huwa wanabaki kuonyesha ubabe wao kwa Wasichana badala ya wenzao. Nakumbuka nikiwa Tech. College Arusha, vijana wa Ilboru walifunga timu zote kwa mpira na mwisho wakaja kwetu wakapata goli zao za kutosha na hawakurudi tena. Mwisho ukaja ugomvi wa Wasichana wa Machame Sec. Kuna graduation moja ya Ilboru wakaja Machame. Jamaa wachache wa TCA wakazamia na wakakipata kibano. Basi ilipofika next weekend jamaa wakaja kuangalia Video show pale TCA, wakatimuliwa. Ila kwa sababu kilikuwa ni chuo, wengine ni watu wazima na wengine na wasichana, hii kitu ilikufa wiki hiyohiyo. Wiki lililofuata jamaa hawakuwa na muda wa kukaa kuwawinda Ilboru wasizamie Video Show. Kwa hali ilivyokuwa pale ilikuwa inaonekana ni jambo la kitoto sana ingawa baadhi yetu kama tungelikuwa ni Secondary na wenzetu wamepigwa basi tungelitembeza kibano.
Nikiwa Mazengo tulishashika makwanja kwenda kuwatandika jamaa wa Mazengo Flats kwa sababu wenzetu wawili walipigwa na watu wa sehemu hiyo. Mungu bariki jamaa wakampelekea headmaster habari (Mzee Mkoba) na akaja mbio kututuliza na kuahidi atafuatilia hadi wjamaa wakamatwe na hilo lisirudie tena. Ila ilisaidia kwani baadhi ya mambo yalibadilika.
Unakumbuka yale mambo mnatoka zenu mkoa kwa kukodi mabasi?
Si tulikuwa tukichukua gogo la TAZARA(kama unakuja dar nakumbuka wanafunzi tulikuwa tunalipa nusu sijui siku hizi), enzi hizo ilikuwa ubabe kwenda mbele,kuna siku tulikutana na watoto wa mwakaleli sec. humo kwenye gogo ilikuwa noma.
watoto wa Sangu,Meta na mbeya day wanatukumbuka vizuri(Iyunga).
Ilikuwa mkisikia mmetangazwa kwenye vyombo vya habari kuwa mmefanya vurugu basi kwenu ilikuwa raha kweli.
Dah! kweli noma.
Siku ya kwanza ya kuripoti shule 'Njuka' wa Tambaza alimpiga 'fiksi'/'magirini' Njuka wa Azania kuwa yeye ni Kidato cha 2 ikabidi dogo wa Aza Boyz akubali 'mkwala' atoe hela ya kula mihogo na zile juisi zilizokuwa zinahifadhiwa kwa barafu za mortuary ya MMC!
Kwenye medani ya malavidavi mnaikumbuka hii: Tambazana vs Azajangwa?