Tahasusi mpya zakosolewa na Maprofesa wa lugha na Fasihi

bagamoyo

JF-Expert Member
Jan 14, 2010
21,305
24,200
Wabobezi ktk fani ya lugha Profesa Aldin Mutembei UDSM, Prof. Mabala na Prof. Raymond Mosha wa chuo nchini U.S.A wajitosa katika mjadala mzito wa TAHASUSI / COMBINATION mpya zinazotegemea kuaza kutumika



Yalitakiwa wajadiliwe kwa upana ili umma mpana waweze kuelewa kwa undani hizi tahasusi mpya zilizoongezwa na kujua fursa zake

Kwa mfano inatarajiwa kuongeza umahiri ktk lugha ikiwemo ya Kiswahili ambayo kwa sasa watu wengi wanaboronga anasema Prof. Aldin Mutembei.

Tahasusi / combination ya KLF KISWAHILI LANGUAGE FRENCH inaifanya lugha yetu ya kiSwahili kuonekana haina fasihi / literature. KLF ilitakiwa iwe - Fasihi ya KiSwahili, Fasihi ya Kiingereza, Fasihi ya Kifaransa ili masomo yote wawe katika mzani unaolingana Prof. Mutembei anasisitiza.

Prof. Raymond Mosha wa chuo kikuu kimoja cha Chicago Marekani amesema amestushwa Tahasuhi zetu hakuna elimu asili ya kwetu inayobeba falsafa ya kiafrika na kuendeleza ukoloni kujifunza mambo ya Wachina, Waarabu, Wazungu lakini yetu wamatumbi yaani waafrika hakuna ....

Upande wa umahiri wa waalimu katika lugha na fasihi za Kiswahili, Kiingereza, Kiarabu, Kifaransa ukweli ni kuwa kuna waalimu wachache na ndiyo maana tunaona jinsi lugha ya Kiswahili inavyoharibiwa ktk matamshi na kuandika pia lugha ya kigeni kama Kiingereza ndiyo mtihani mkubwa kwa watanzania na uhakika kwa lugha ya kiarabu, kiChina na kifaransa itakuwa hivyo hivyo kutokana na kutokuwepo matayarisho na mikakati ...

Tukija katika mafunzo ya kiasili ya kiafrika kuhusu Maarifa ya Kiafrika, dawa za kiasili, teknolojia ya kiafrika hakuna tahasusi iliyopo ....

Tahasusi zenye masomo ya dini ya Kikristo na Kiislamu zipo je za Dini Maadili Asili za Kiafrika na zingine za KiHindu, Taoism, Buddha zipo wapi maana nia na madhumuni ni kupanua ufahamu sasa kujifungia ktk Ukristo na Uislamu hatuoni tunapoteza nafasi kujiongezea ufahamu mwingine mkubwa ambao ni fursa katika ulimwengu huu mpana .....
 
Back
Top Bottom