Tahasusi za masomo ya A-Level: Kutoka 16 HADI 65, tumpongeze waziri au tumuhoji?

kiumbempole

JF-Expert Member
Jan 15, 2016
551
905
Wadau,

Kama mlivyosikia Wizara ya Tamisemi imetangaza ongezeko la tahsusi za kidato cha tano na sita katika michepuo mbalimbali ikiwemo sayansi, lugha, michezo, sanaa, biashara na dini.

Kwa tafakari ya haraka naona haya ni maendeleo katika kuruhusu wigo mpana zaidi wa kujifunza mambo ambayo zamani tulizoea kuona yakiishia O-level pekee au yakianzia vyuoni huko kwa wanaojikita kwenye michepuo husika., mfano elimu ya dini (Kikristo na kiislamu) na masuala ya sanaa (fineart). Lakini pia naona Lugha za kujifunza zimeongezeka, awali pamoja na kiswahi, lugha za kifaransa na kiingereza zilifundishwa. Kwa sasa kiarabu na kichina zimeongeka.

Kitu kimoja nilichokiona pia ni ongezeko kubwa la ghafla la idadi ya michepuo/ tahasusi hizo ambayo tuombee taasisi zinazosimamia ubora wa elimu ziwe zimejipanga kwa ngazi zote kuanzia ufundishaji hadi utungaji wa mitihani. Pia tuanze kujipanga kozi watakazozisoma kwa vyuo vya kati na vya juu kwa wahitimu hao.

Bado kuna maswali kama, je, serikali imefikia vipi uamuzi wa kuongeza lugha mbili pekee na sio kwa mfano kihindi, kidachi au kizulu?

Je, mfumo wa zamani ulikuwa na mapungufu yapi ambayo mfumo mpya umekuja kuyarekebisha? Mfano elimu za dini kufundishwa/kutolewa zaidi seminarini, masuala ya arts kufundishwa kwenye vyuo mahsusi kama pale Bagamoyo kwa ngazi ya cheti, diploma hadi digrii n.k.
 
Nasikia kuna kombi ya CCM yaani COMMERCE, CHEMISTRY na MATHEMATICS, kama kweli ipo hii inatosha kusema aliyeandaa hii kitu akili zake hazina akili, yaani collabo la COMMERCE na CHEMISTRY wapi na wapi?
 
A: Tahasusi za Sayansi ya Jamii

History, Geography, and Kiswahili (11GK)
History, Geography, and English Language (HGL)
History, Geography, and French (HGF)
History, Kiswahili, and English Language (HKL)
History, Geography, and Arabic (HGAr)
History, Geography, and Chinese (HGCh)
History, Geography, and Economics (HGE)
History, Geography, and Fasihi ya Kiswahili (HGFa)
History, Geography, and Literature in English (HGLi)

B: Tahasusi za Lugha

Kiswahili, English Language, and French (KLF)
Kiswahili, English Language, and Arabic (KLAr)
Kiswahili, English Language, and Chinese (KLCh)
Kiswahili, Arabic, and Chinese (KArCh)
Kiswahili, Arabic, and French (KArF)
English Language, French, and Arabic (LFAr)
English Language, French, and Chinese (LFCh)
French, Arabic, and Chinese (FArCh)
History, English Language, and French (HLF)
History, English Language, and Arabic (HLAr)
History, English Language, and Chinese (HLC’h)
C: Tahasusi za Masomo ya Biashara

Economics, Business Studies, and Accountancy (EBuAc)
Economics, Geography, and Mathematics (EGM)
Economics, Commerce, and Accountancy (ECAc)
Economics, Computer Science, and Mathematics (ECsM)
Business Studies, Accountancy, and Computer Science (BuAcCs)
Business Studies, Accountancy, and Mathematics (BuAcNl)
Economics, Business Studies, and Islamic Knowledge (EBuI)
D: Tahasusi za Sayansi

Physics, Chemistry, and Mathematics (PCM)
Physics, Chemistry, and Biology (PCB)
Physics, Geography, and Mathematics (PGM)
Chemistry, Biology, and Geography (C’BG)
Physics, Mathematics, and Computer Science (PMCs)
Chemistry, Biology, and Agriculture (CBA)
Chemistry, Biology, and Food and Human Nutrition (CBN)
E: Tahasusi za Michezo

Biology, Food and Human Nutrition, and Sports (BNS)
English Language, Music, and Sports (LMS)
Kiswahili, Music, and Sports (KMS)
Fasihi ya Kiswahili, Music, and Sports (FaMS)
Literature in English, Music, and Sports (LiMS)
French, Music, and Sports (FMS)
Arabic, Music, and Sports (ArMS)

F: Tahasusi za Sanaa

Kiswahili, English Language, and Theatre Arts (KLT)
Kiswahili, French, and Theatre Arts (KFT)
Fasihi ya Kiswahili, English Language, and Theatre Arts (FaLT)
Kiswahili, Literature in English, and Theatre Arts (KLiT)
Kiswahili, English Language, and Music (KLM)
Kiswahili, French, and Music (KFM)
Fasihi ya Kiswahili, English Language, and Music (FaLM)
Kiswahili, Literature in English, and Music (KLiM)
Kiswahili, English Language, and Fine Art (KLFi)
Kiswahili, French, and Fine Art (KFFi)
Fasihi ya Kiswahili, English Language, and Fine Art (FaLFi)
Kiswahili, Literature in English, and Fine Art (KLiFi)
Kiswahili, Textile and Garment Construction, and Fine Art (KTeFi)
English Language, Textile and Garment Construction, and Fine Art (LTeFi)
Arabic, Textile and Garment Construction, and Fine Art (ArTeFi)
Chinese, Textile and Garment Construction, and Fine Art (ChiTeFi)
G: Tahasusi za Elimu ya Dini

Islamic Knowledge, History, and Geography (IMG)
Divinity, History, and Geography (DHG)
Islamic Knowledge, History, and Arabic (IHAr)
Divinity, History, and English Language (DHL)
Islamic Knowledge, History, and English Language (IHL)
Divinity, History, and Kiswahili (DHK)
Islamic Knowledge, History, and Kiswahili (IHK)
Divinity, Kiswahili, and English Language (DKL)
 
Je, mfumo wa zamani ulikuwa na mapungufu yapi ambayo mfumo mpya umekuja kuyarekebisha? Mfano elimu za dini kufundishwa/kutolewa zaidi seminarini, masuala ya arts kufundishwa kwenye vyuo mahsusi kama pale Bagamoyo kwa ngazi ya cheti, diploma hadi digrii n.k. utaratibu huo ulikuwa na mapungufu gani?
 
Serikali imeanza kuwa na dini?
Sera ya sasa ni kuwa na mafunzo ya ufundi katika ngazi ya O level. Mbona haionekani elimu hiyo itakavyoweza kumpeleka mtoto level ya juu zaidi? Wanaojua nipeni ufafanuzi
 
Serikali imeanza kuwa na dini?
Sera ya sasa ni kuwa na mafunzo ya ufundi katika ngazi ya O level. Mbona haionekani elimu hiyo itakavyoweza kumpeleka mtoto level ya juu zaidi? Wanaojua nipeni ufafanuzi
Inashangaza Kwa kweli.
Kwa mujibi wa kauli ya Rais J.K. Nyerere, ni kwamba Serekali Haina Dini.

Na kitu kingine hapo kwenye Taasusi ya Biashara C: No. 27 Kwa nini waingize Dini ya kiislam pekee kwenye combi ya Biashara?Au ni njia ya kupenya masoko ya Uarabuni?

Wakati Masomo yote ya Taasusi ya Elimu ya Dini zote yapo kwenye Category G:
 
tulizoea mambo ya kukalili, hizo arabic, french sijui fasihi nini, sijui computer science watajua wenyewe...maswali ya unasoma comb gani yatapungua sasa?...akitajiwa wala hataelewa yaani :cool:
 
Wadau,

Kama mlivyosikia Wizara ya Tamisemi imetangaza ongezeko la tahsusi za kidato cha tano na sita katika michepuo mbalimbali ikiwemo sayansi, lugha, michezo, sanaa, biashara na dini.

Kwa tafakari ya haraka naona haya ni maendeleo katika kuruhusu wigo mpana zaidi wa kujifunza mambo ambayo zamani tulizoea kuona yakiishia O-level pekee au yakianzia vyuoni huko kwa wanaojikita kwenye michepuo husika., mfano elimu ya dini (Kikristo na kiislamu) na masuala ya sanaa (fineart). Lakini pia naona Lugha za kujifunza zimeongezeka, awali pamoja na kiswahi, lugha za kifaransa na kiingereza zilifundishwa. Kwa sasa kiarabu na kichina zimeongeka.

Kitu kimoja nilichokiona pia ni ongezeko kubwa la ghafla la idadi ya michepuo/ tahasusi hizo ambayo tuombee taasisi zinazosimamia ubora wa elimu ziwe zimejipanga kwa ngazi zote kuanzia ufundishaji hadi utungaji wa mitihani. Pia tuanze kujipanga kozi watakazozisoma kwa vyuo vya kati na vya juu kwa wahitimu hao.

Bado kuna maswali kama, je, serikali imefikia vipi uamuzi wa kuongeza lugha mbili pekee na sio kwa mfano kihindi, kidachi au kizulu?

Je, mfumo wa zamani ulikuwa na mapungufu yapi ambayo mfumo mpya umekuja kuyarekebisha? Mfano elimu za dini kufundishwa/kutolewa zaidi seminarini, masuala ya arts kufundishwa kwenye vyuo mahsusi kama pale Bagamoyo kwa ngazi ya cheti, diploma hadi digrii n.k.
Tumhoji mapema tusijejilaumu ama kulaumiana baadae kwani wazaramu tinasema aliye amka haaamshwi na aliye lala akiamshwa aliyeamsha atalala yeye😀😃😁😅🤣😂
 
Back
Top Bottom