Tuache siasa katika elimu. Tahasusi mpya ni sahihi na zinapaswa kuongezwa zaidi

ubongokid

JF-Expert Member
Apr 30, 2017
2,032
3,913
Habari za wakati huu;

Nimeona watu wakitoa maoni yao mbalimbali kuhusu tahasusi mpya zilizotangazwa na TAMISEMI. Katika kufuatilia mijadala, nimekutana na maoni mengi sana ila nalazimika kusimama hapa na kuiunga mkono serikali kwa uamuzi wake huu. Uamuzi huu ni uamuzi sahihi kwa wakati sahihi na kwa sababu sahihi. Nitaelezea sababu zangu hapa kwa kutoa hoja zenye nguvu kabisa.

Kwanza kabisa nataka tutambue kwamba kwa muda mrefu sana elimu ya A-level imeonekana kuwa na elimu ya kupoteza muda. Ndio maana kuna watu wengi sana wanapata Division 1 nzuri o-level ila wakienda A-level wanafeli vibaya sana. Ndio maana tuna watu wengi sana ambao wamesoma PCB na PCM na PGM lakini kwa sasa ni wahasibu, bankers, wachumi, nk., na pia wapo wengine ambao wamesoma HGL na HKL ambao sasa wanafanya kazi za IT na aina fulani za kazi za engineering. Tafsiri yake ni kwamba kwa sasa idadi ya tahasusi na uelekeo wake hauendani na wakti huu.

Sasa hivi tunaishi katika zama za TEHAMA. Lakini zaidi kuna kitu kinaitwa AKILI BANDIA aka AI ambacho kinaleta changamoto mpya kila siku. Hii ina maana kwamba, kwa sasa hivi hakuna haja ya kumfunga mtu katika tahasusi bali ni kuacha uwanja mpana zaidi wa kujifunza na kujikita katika eneo ambalo unalimudu.

Nianze kwa kuzigusa kidogo baadhi ya tahsusi MPYA mfano tahasusi za lugha, dini pamoja na tahasusi ambazo zimechanganya biashara, sayansi na dini, n.k.

Sasa hivi dini nazo ni biashara, dunia imekuwa kijiji na watu wanaofahamu lugha nyingi wanaweza kupata fursa zaidi. Kwa sasa hivi tunafanya biashara kubwa sana na Wachina na Waarabu na sio vibaya tukafahamu lugha zao tukiwa wadogo kabisa ili tuweze kuwasiliana nao. Sasa hivi sio lazima ukiwa daktari basi usiwe na ufahamu wa kuhusu lugha au utaalamu mwingine kwani kwa sasa, daktari anapaswa pia kufahamu lugha ili aweze kuwasiliana vizuri na kuwasilisha utaalamu wake kwa dunia.

Kwa ufupi, hizi tahasusi zinaendana na mahitaji. Na bado zinahitajika nyingine. Binafsi ningeshauri kabisa kwamba sasa mwanafunzi aruhusiwe kuchagua masomo yake kabisa cha msingi yawe katika orodha hiyo na Wizara iendelee kuboresha hiyo orodha kwa kuongeza masomo mengine kadiri rasilimali zinavyopatikana.

Tuachane na hao ambao kwao kila kitu ni siasa na tuanze sasa kuhamasisha specialization katika umri mdogo ili tuhakikishe kwamba tunazalisha jamii ambayo ina hazina ya utaalamu wa kila namna na maarifa ya kila namna.

Pongezi zangu sana kwa timu nzima iliyoandaa tahasusi hizi na ni ushauri wangu kwao waweke pia option ya mtu kupanga tahasusi zake mwenyewe kwa kuchagua masomo kutoka makundi tofauti mfano mtu anataka asome physics, English literature na computer science au na Islamic knowledge anaweza kabisa kusoma.
 
mfano mtu anataka asome physics, English literature na computer science au na Islamic knowledge anaweza kabisa kusoma.
Huyu atasoma taaluma gani?

Ulianza vizuri kusema advance level ni ya kupotezeana muda..

Baadaye una changanya dhana ya tahasusi kama daraja la kukupela kusoma taaluma fulani, na Tahasusi kwa dhana kwamba ndiyo taaluma yenyewe..

ieleweke kwamba ukisha maliza Advance, na kuishia hapo, huna haki ya kujiona umesoma.. kwa sababu huna taaluma yoyote.
 
Mtoa mada wewe ni kijani. Samahan lakin Kwa Hilo. Wote uliyosema yanaendana na Dunia ya Sasa katika kutukomboa sisi kama taifa.? Nisaidie Kwa hili.

Je umaskni wetu kama taifa unachangiwa zaidi na uchache wa tahasusi zilizopo? Kwenye kuongeza hizi tahasusi ndo kutatufanya tuendelee kama taifa?

Unajua kuwa Mtoto aliyemaliza form 6 hawezi ajiriwa popote pale make Hana utalamu wowote ule? Anakuwa anazidiwa na darasa la Saba au form 4 aliyeenda veta?
 
Kidato cha tano na sita ni kupoteza muda tu, mtu amalize kidato cha nne hiyo miaka miwili aanze kusomea fani kwa level fulani sio kupoteza muda na elimu ambayo haiwezi kumsaidia yeye binafsi ukiachilia mbali taifa.
 
Habari za wakati huu;

Nimeona watu wakitoa maoni yao mbalimbali kuhusu tahasusi mpya zilizotangazwa na TAMISEMI. Katika kufuatilia mijadala, nimekutana na maoni mengi sana ila nalazimika kusimama hapa na kuiunga mkono serikali kwa uamuzi wake huu. Uamuzi huu ni uamuzi sahihi kwa wakati sahihi na kwa sababu sahihi. Nitaelezea sababu zangu hapa kwa kutoa hoja zenye nguvu kabisa.

Kwanza kabisa nataka tutambue kwamba kwa muda mrefu sana elimu ya A-level imeonekana kuwa na elimu ya kupoteza muda. Ndio maana kuna watu wengi sana wanapata Division 1 nzuri o-level ila wakienda A-level wanafeli vibaya sana. Ndio maana tuna watu wengi sana ambao wamesoma PCB na PCM na PGM lakini kwa sasa ni wahasibu, bankers, wachumi, nk., na pia wapo wengine ambao wamesoma HGL na HKL ambao sasa wanafanya kazi za IT na aina fulani za kazi za engineering. Tafsiri yake ni kwamba kwa sasa idadi ya tahasusi na uelekeo wake hauendani na wakti huu.

Sasa hivi tunaishi katika zama za TEHAMA. Lakini zaidi kuna kitu kinaitwa AKILI BANDIA aka AI ambacho kinaleta changamoto mpya kila siku. Hii ina maana kwamba, kwa sasa hivi hakuna haja ya kumfunga mtu katika tahasusi bali ni kuacha uwanja mpana zaidi wa kujifunza na kujikita katika eneo ambalo unalimudu.

Nianze kwa kuzigusa kidogo baadhi ya tahsusi MPYA mfano tahasusi za lugha, dini pamoja na tahasusi ambazo zimechanganya biashara, sayansi na dini, n.k.

Sasa hivi dini nazo ni biashara, dunia imekuwa kijiji na watu wanaofahamu lugha nyingi wanaweza kupata fursa zaidi. Kwa sasa hivi tunafanya biashara kubwa sana na Wachina na Waarabu na sio vibaya tukafahamu lugha zao tukiwa wadogo kabisa ili tuweze kuwasiliana nao. Sasa hivi sio lazima ukiwa daktari basi usiwe na ufahamu wa kuhusu lugha au utaalamu mwingine kwani kwa sasa, daktari anapaswa pia kufahamu lugha ili aweze kuwasiliana vizuri na kuwasilisha utaalamu wake kwa dunia.

Kwa ufupi, hizi tahasusi zinaendana na mahitaji. Na bado zinahitajika nyingine. Binafsi ningeshauri kabisa kwamba sasa mwanafunzi aruhusiwe kuchagua masomo yake kabisa cha msingi yawe katika orodha hiyo na Wizara iendelee kuboresha hiyo orodha kwa kuongeza masomo mengine kadiri rasilimali zinavyopatikana.

Tuachane na hao ambao kwao kila kitu ni siasa na tuanze sasa kuhamasisha specialization katika umri mdogo ili tuhakikishe kwamba tunazalisha jamii ambayo ina hazina ya utaalamu wa kila namna na maarifa ya kila namna.

Pongezi zangu sana kwa timu nzima iliyoandaa tahasusi hizi na ni ushauri wangu kwao waweke pia option ya mtu kupanga tahasusi zake mwenyewe kwa kuchagua masomo kutoka makundi tofauti mfano mtu anataka asome physics, English literature na computer science au na Islamic knowledge anaweza kabisa kusoma.
Kwa ufupi ni kwamba hatuna haja ya kupangiwa tahasusi na serikali. Serikali inatakiwa kupanga categories tu;
kwa mfano Science category na masomo yake,
Social science category na masomo yake,
Art category na masomo yake,
language category na masomo yake,
Religion category na masomo yake,
Economics & Business category na masomo yake.

Baada ya hapo wanafunzi wanajipangia wenyewe combination zao kutoka kwenye category husika + option ya somo moja au mawili ya ziada kujitanulia wigo kwenye kusomea taaluma fulani chuo kikuu.
 
Habari za wakati huu;

Nimeona watu wakitoa maoni yao mbalimbali kuhusu tahasusi mpya zilizotangazwa na TAMISEMI. Katika kufuatilia mijadala, nimekutana na maoni mengi sana ila nalazimika kusimama hapa na kuiunga mkono serikali kwa uamuzi wake huu. Uamuzi huu ni uamuzi sahihi kwa wakati sahihi na kwa sababu sahihi. Nitaelezea sababu zangu hapa kwa kutoa hoja zenye nguvu kabisa.

Kwanza kabisa nataka tutambue kwamba kwa muda mrefu sana elimu ya A-level imeonekana kuwa na elimu ya kupoteza muda. Ndio maana kuna watu wengi sana wanapata Division 1 nzuri o-level ila wakienda A-level wanafeli vibaya sana. Ndio maana tuna watu wengi sana ambao wamesoma PCB na PCM na PGM lakini kwa sasa ni wahasibu, bankers, wachumi, nk., na pia wapo wengine ambao wamesoma HGL na HKL ambao sasa wanafanya kazi za IT na aina fulani za kazi za engineering. Tafsiri yake ni kwamba kwa sasa idadi ya tahasusi na uelekeo wake hauendani na wakti huu.

Sasa hivi tunaishi katika zama za TEHAMA. Lakini zaidi kuna kitu kinaitwa AKILI BANDIA aka AI ambacho kinaleta changamoto mpya kila siku. Hii ina maana kwamba, kwa sasa hivi hakuna haja ya kumfunga mtu katika tahasusi bali ni kuacha uwanja mpana zaidi wa kujifunza na kujikita katika eneo ambalo unalimudu.

Nianze kwa kuzigusa kidogo baadhi ya tahsusi MPYA mfano tahasusi za lugha, dini pamoja na tahasusi ambazo zimechanganya biashara, sayansi na dini, n.k.

Sasa hivi dini nazo ni biashara, dunia imekuwa kijiji na watu wanaofahamu lugha nyingi wanaweza kupata fursa zaidi. Kwa sasa hivi tunafanya biashara kubwa sana na Wachina na Waarabu na sio vibaya tukafahamu lugha zao tukiwa wadogo kabisa ili tuweze kuwasiliana nao. Sasa hivi sio lazima ukiwa daktari basi usiwe na ufahamu wa kuhusu lugha au utaalamu mwingine kwani kwa sasa, daktari anapaswa pia kufahamu lugha ili aweze kuwasiliana vizuri na kuwasilisha utaalamu wake kwa dunia.

Kwa ufupi, hizi tahasusi zinaendana na mahitaji. Na bado zinahitajika nyingine. Binafsi ningeshauri kabisa kwamba sasa mwanafunzi aruhusiwe kuchagua masomo yake kabisa cha msingi yawe katika orodha hiyo na Wizara iendelee kuboresha hiyo orodha kwa kuongeza masomo mengine kadiri rasilimali zinavyopatikana.

Tuachane na hao ambao kwao kila kitu ni siasa na tuanze sasa kuhamasisha specialization katika umri mdogo ili tuhakikishe kwamba tunazalisha jamii ambayo ina hazina ya utaalamu wa kila namna na maarifa ya kila namna.

Pongezi zangu sana kwa timu nzima iliyoandaa tahasusi hizi na ni ushauri wangu kwao waweke pia option ya mtu kupanga tahasusi zake mwenyewe kwa kuchagua masomo kutoka makundi tofauti mfano mtu anataka asome physics, English literature na computer science au na Islamic knowledge anaweza kabisa kusoma.
Mkuu mnataka mu force ajira?
 
Mkuu mnataka mu force ajira?
Issue sio ajira,Issue ni Kumpa mtu uhuru wa Kupanga career yake.Nchi za wenzetu kuna dual path degree ambapo mtu anaweza soma engineering na lugha/management etc.Katika zama hizi ambapo elimu ni huria hakuna sababu ya kupangia mtu ni kuweka tu mwongozo ambao ni rahisi kusimamiwa.
 
Back
Top Bottom