Tahadhari: Mazoezi ya Al-shaabab ndani ya Dar es Salaam

Tahadhari: Mazoezi ya Al-shaabab ndani ya Dar es Salaam

tpaul

Platinum Member
Joined
Feb 3, 2008
Posts
27,197
Reaction score
27,817
Leo asubuhi nimepita mahali fulani hapa Dar nikawashuhudia watu wamevaa kininja na vilemba vya kigaidi wakifanya mazoezi ya kungfu na kareti bila wasiwasi wowote.

Mwalimu wao mwenye asili ya kisomali alisikika akiwapa maelekezo kwa lugha ya kiarabu huku akiwa mkali kwa wale walioonekana kukosea maelekezo yake. Kikundi hiki ni cha watu wasiopungua 15.

Hatuwezi kujua vikundi hivi viko vingapi hapa jijini na kama mafunzo haya ya kigaidi wanayopata wataenda kuyatekeleza wapi. Hivyo ni jukumu la kila mmoja wetu kuwa makini na kuchukua tahadhari pindi atakapoona vikundi kama hivi.

Ulinzi na amani ya Taifa letu ni jukumu la kila raia. Juzi kati tumeshuhudia mtanzania mwenzetu akikamatwa kwa sababu za kigaidi. Huenda ugaidi huu amejifunzia hapahapa Tanzania. Chukua tahadhari kabla ya hatari!

UPDATE
tukio limeisharipotiwa kituo cha polisi na wanausalama hao wameahidi kulichunguza kwa umakini na kunipa mrejesho. tuendelee kuwa watulivu wakati polisi wakifanya uchunguzi wao. wote mnaonitukana nimewapuuza.
 
Mkuu tpaul hiyo ni Tanzania nzima.
 
Last edited by a moderator:
Hii tarifa yako mbona haina msaada ungesema ni wapi,maeneo gani,mtaa gani,ikiwezekana ukumbi au uwanja gani ili wahusika wapate kufuatilia sasa unaadika kama unatunga wimbo bana.

Mkuu Simiyu Yetu hii ni taarifa ya kiintelejensia. nl

Nahofia kutamka mahali walipo moja kwa moja wasije wakatoroka kabla ya kushughulikiwa.

Hivi sasa naelekea kibaruani. Nikirudi jioni itabidi nitoe taarifa kwenye vyombo vya usalama wafanye uchunguzi. Huwezi kujua kama wahusika nao wanapita humu JF, nikitaja mahali walipo naweza kujikuta nimewakurupua kabla hawajachunguzwa.

Cha muhimu ni kila mmoja wetu kuwa makini mahali anapokaa pindi akiona vikundi vya ajabuajabu kama hivi.
 
Last edited by a moderator:
Taarifa yako yaweza chukuliwa kwa kebehi na mizaha kwa jinsi ulivyowasilisha, THE HOME OF GREAT THINKERS iwe kweli basi. Toa taarifa sahihi, wasipochukuliwa hatua (kama kweli ni wahalifu) then tuwashutumu wahusika
 
Mkuu tpaul hiyo ni Tanzania nzima.

lakini ni muhimu kuwa makini mkuu Molembe. nataka kwanza nijiridhishe kama mafunzo haya ni halali na kama kikundi hiki kimesajiriwa kufanya shughuli hapa nchini.
 
Last edited by a moderator:
Hizo zinaitwa DOJO zimejaa kila mtaa hapa Dar! Nenda kawaripoti Wajapan wote maana ndio source ya hii kitu!
 
mkuu Simiyu Yetu hii ni taarifa ya kiintelejensia. nahofia kutamka mahali walipo moja kwa moja wasije wakatoroka kabla ya kushughulikiwa. hv sasa naelekea kibaruani. nikirudi jioni itabidi nitoe taarifa kwenye vyombo vya usalama wafanye uchunguzi. huwezi kujua kama wahusika nao wanapita humu jf. nikitaja mahali walipo naweza kujikuta nimewakurupua kabla hawajachunguzwa. cha muhimu ni kila mmoja wetu kuwa makini mahali anapokaa pindi akiona vikundi vya ajabuajabu kama hivi.

we toa taatifa ili hata wana usalama wanaopita hapa waweze kuchukua hatua. ukitoa taarifa halfu wakahama, tayari umelinda maana watajua kuwa watu wanafuatilia shughuli zao
 
Last edited by a moderator:
Taarifa yako yaweza chukuliwa kwa kebehi na mizaha kwa jinsi ulivyowasilisha, THE HOME OF GREAT THINKERS iwe kweli basi. Toa taarifa sahihi, wasipochukuliwa hatua (kama kweli ni wahalifu) then tuwashutumu wahusika

natarajia baadaye kupeleka taarifa polisi. lakini kama ujuavyo polisi wetu wasivyokuwa weledi hawakawii kwenda kunitaja kwa mkuu wa kikundi hiki na kuniweka hatarini.
 
we toa taatifa ili hata wana usalama wanaopita hapa waweze kuchukua hatua. ukitoa taarifa halfu wakahama, tayari umelinda maana watajua kuwa watu wanafuatilia shughuli zao

nitoe taarifa humu hadharani usalama wangu utalindwaje? nitapeleka taarifa polisi physically na wasipochukua hatua, nawalipua kwa kova.
 
mkuu Simiyu Yetu hii ni taarifa ya kiintelejensia. nahofia kutamka mahali walipo moja kwa moja wasije wakatoroka kabla ya kushughulikiwa. hv sasa naelekea kibaruani. nikirudi jioni itabidi nitoe taarifa kwenye vyombo vya usalama wafanye uchunguzi. huwezi kujua kama wahusika nao wanapita humu jf. nikitaja mahali walipo naweza kujikuta nimewakurupua kabla hawajachunguzwa. cha muhimu ni kila mmoja wetu kuwa makini mahali anapokaa pindi akiona vikundi vya ajabuajabu kama hivi.

Hujui kitu ww unawahi kibarua waulize wenzako kenya lilipowakuta kama kuna mtu alikumbuka kibarua na kama hofu yako ni kwamba labda na wao wanapita hum ucngepost kabsa ukatunza na kwenda polis hii habari inanitia shaka na inawezekana na ww ni mmoja wao
 
Last edited by a moderator:
kwa hiyo unataka tuwaache waendelee na mazoezi yao bila kuchunguzwa kwa kisingizio cha uchochezi? anachochewa nani hapa?
perception yako ndo kipimo chako cha akili?
 
kwa hiyo unataka tuwaache waendelee na mazoezi yao bila kuchunguzwa kwa kisingizio cha uchochezi? anachochewa nani hapa?

Haya yote kwa sababu hujarnda kulipoti polis ungeenda wala ucngeambiwa mchochezi ila ungeonekana mzalendo zaidi ya mjinga zzk anayejipachika uzalendo kwa kuficha madhara makubwa ya taifa
 
Mkuu Simiyu Yetu hii ni taarifa ya kiintelejensia. nl

Nahofia kutamka mahali walipo moja kwa moja wasije wakatoroka kabla ya kushughulikiwa.

Hivi sasa naelekea kibaruani. Nikirudi jioni itabidi nitoe taarifa kwenye vyombo vya usalama wafanye uchunguzi. Huwezi kujua kama wahusika nao wanapita humu JF, nikitaja mahali walipo naweza kujikuta nimewakurupua kabla hawajachunguzwa.

Cha muhimu ni kila mmoja wetu kuwa makini mahali anapokaa pindi akiona vikundi vya ajabuajabu kama hivi.

Kama taarifa unayoisema ni kweli basi wewe mwenyewe ndio umekosa umakini unaohimiza wengine wawe nao. Mtu makini hawezi kuona ulichoona akaacha kwenda kutoa taarifa kwa vyombo vya usalama Mara moja ili vichukue hatua, badala yake anatumia muda kupost habari isiyokamilika kwenye forum ambayo anajua hakuna hatua yoyote itachukuliwa? . Kusema kwamba utaenda ukitoka kibaruani, una uhakika gani kikundi hicho kipo pale permanently? Ukuenda jioni ukakuta wameshaondoka utakuwa umesaidia nini? Kumbuka usemi "UMAKINI BEGINS WITH YOU" la sivyo uache kupost habari za uzushi na kuwatia hofu watu bila sababu.
 
huyu tpaul ni muongo na ni mueneza unafiki, una maana gani ya kuandika haya kwenye mtandaoni, na usipeleke ripoti kwenye kituo cha usalama. Au wewe nae ni mmoja wao hao majangili na muongo katika kuharibika kujua namna idara zetu za usalama zilivyo kuwa alert. La pili kama hao jamaa waliwao ki ninja ulijuaje Mwalimu wao alikuwa na sura za ki somali, watu kama tpaul ni hatari zaidi ya magaidi wachukuliwe hatua
 
Sijui niite kick au nisemeje, taarifa ya kiintelijensia inawezaje kuanzia Jf alafu ndo Polis?
Taarifa sensitive kama hao, au unafikiri jamaa hawazijui source mbalimbali za taarifa?
Au.unafkr mtandao wao ni wakawaida?
 
Back
Top Bottom