Ndoto tunazoota na tafsiri zake

Habarini wakuu,

kwa siku za karibuni nimeona thread nyingi humu watu wakiwa na kiu ya kutaka kujua maana ya ndoto mbalimbali, lakini imekuwa ngumu kwao.

Wengi wamekimbilia kutisha wakiamini kuwa ndoto zote zina uhusiano wa uchawi, mashetani na ulozi, jambo ambalo si kweli.

Leo nataka nitoe somo la bure hapa. Ila kwa kuwa ndoto ziko nyingi nami nimeona kila mwenye uhitaji aniulize nami nitamjibu ktk thread hii hii.

Asanteni na karibuni sana..
Mara nyingi kuna ndoto hizi zinajirudia sana
Kwanza huwa naota either nimewachokoza watu au nimeiba kitu wanavyonikimbiza napaa juu naenda umbali mrefu sana natua sehemu baadae naendelea kupaa naenda mbali sana
Ya pili huwa naota nipo na mtu nnaemfahamu lakini baadae anakuja kugeuka sura anakuwa mtu wa kutisha na huwa nasali mpaka hanidhuru au nakutana na kundi la watu nywele zinasisimka kabisa naanza kusali pia watu hao wanageuka kuwa wa kutisha wanashindwa kunidhuru msaada
 
Okoka kwanza. Mpe Yesu maisha yako. Nenda kanisani ukaombewe halafu mwambie Mungu akutoe kwenye hilo jeneza cz wamekuua ktk ulimwengu wa kiroho ingawa unajiona mzima. Mwisho utakuta mambo hayaendi kabisa. Damu ya Yesu ikutoe ktk hilo jeneza uwe huru sasa. Tulitolewa ktk ufalme wa giza tukahamishwa na tukaingizwa ktk ufalme wa mwana wa pendo lake( Yesu kristo) Yesu akutoe huko ulipo uwe huru sasa. Ulalapo mwambie Mungu nifunike kwa Damu Ya Yesu. Kuwa na imani utatoka huko bt usiache kuomba na uwe mwaminifu kwa Mungu siku zote.
 
Mmh mercky ngoja tu niseme neno kwamba hiyo ndoto ilikuwa na maana mbili
1. Alikuwa anawangiwa ndio maana kaamka kichwa kinamuuma
2. Ni ndoto tu ya kawaida inayomtabiria mema kwakuwa kuna baadhi ya ndoto tafsiri huwa kinyume
Hiyo ndoto haimtabirii mema hata kidogo na akiipuuza atakuja kusema hapa. Ndoto ni mlango ambao shetani anautumia sana na ni mlango ambao Mungu anautumia kusema na sisi. Hapo kaamka kichwa kinamuuma ni kwel kabisa ktk ulimwengu wa kiroho wamemuua na pindi alipo amka kaamka kafadhaika na amekosa raha. Hakuna chema hapo kaka yangu shetan kapata nafasi ya kuingia na ana uhalali bila shaka hadi kuingia huko. Yampsa amwambie Mungu aingilie kati ili shetani akose uhalali katk maisha yake. Cz ndoto inagusa nafsi na nafsi ikifungwa ni hatari.
 
mbona avatar yako ni mke au wewe jike dume?
ndio mahana unaota ndoto mbaya.

swissme

Avatar yangu haihusiani na Mimi na si lazima kila avatar inayoonekana kwa ID ya mtu imuhusu kwani ni dhambi kumuweka mtu mwingine vipi Kama ni mke wangu? Vipi huyo wa kwenye avatar yako ni wewe? Vipi kwa wale wanaoweka picha za simba ,chui au vitu Kama hivyo nao ni chui au simba?
 
Umofia kwenu wakuu,

Wapo watu ambao wanapenda kujua maana au tafsiri za ndoto kwa kuwa nyingi huwa zinakuja kwa mtindo wa mafumbo. Wapo wanaoamini kuwa ndoto zina taarifa zenye miongozo au kutoa tahadhari kwenye mwenendo wa maisha yao ya kila siku. Hivyo kuzielewa kuna maana kubwa sana kwao.

Nimeona ni jambo jema kukusanya mada ambazo zimeshawahi kujadiliwa kwa kina humu JF kuhusiana na Ndoto na Tafsiri zake, ili kuweka urahisi kwa wale ambao wanataka kujua tafsiri ya ndoto zao walizoota, pasi na kuwa na haja ya kuanzisha uzi mpya kuulizia kitu cha aina moja kila uchwao..

Zifuatazo ni mada zenye maswali na majibu kuhusu ndoto mbalimbali ambazo zimeshawahi kujadiliwa humu JF;

Hizi ni ndoto hatari sana maishani mwako..

Ndoto za kupaa na kuelea hewani zinaashiria nini?


Jinamizi ni nini? Kwanini hutokea wakati wa kulala tu?

Msaada: Nimeota nimeenda eneo nisilolijua na kukutana na vitisho


Ndoto za Mapenzi zinanitesa, nifanyeje?

Kuna mahusiano kati ya ndoto na maisha ya kawaida?

Naomba tafsiri ya hii ndoto: Nimeota nimekufa na kuwekwa ndani ya jeneza


========

NB
: Kama kuna uzi ambao ushawahi kujadiliwa kwa kina kuhusu ndoto na haupo kwenye hiyo orodha hapo juu, tafadhali tukumbushane ili niuongeze hapa.

Wasalaam..

Hii nimeiota leo hii hii,
Nimeota kuna mtu anagonga mlango huku akiita jina langu kwa sauti, tena sauti ya kike akitaka nimfungulie.ghafla nikashituka na sikusikia ile sauti,nikafungua mlango sikuona mtu lakini tangu muda ule sauti yangu imekauka haitoki vizuri,hii ina maana gani?
 
Hii nimeiota leo hii hii,
Nimeota kuna mtu anagonga mlango huku akiita jina langu kwa sauti, tena sauti ya kike akitaka nimfungulie.ghafla nikashituka na sikusikia ile sauti,nikafungua mlango sikuona mtu lakini tangu muda ule sauti yangu imekauka haitoki vizuri,hii ina maana gani?
Huyo ni mchawi....ndugu...kila kitu kinachotokea kwenye Mwili ujue chanzo chake ni Ulimwengu wa Roho....watu wanarogwa sana kupitia ndotoni....utakuta unapigiwa Simu ukiwa usingizini....Lazima ujue namna yakuikemea hiyo hali iishie huko huko...
 
Hii nimeiota leo hii hii,
Nimeota kuna mtu anagonga mlango huku akiita jina langu kwa sauti, tena sauti ya kike akitaka nimfungulie.ghafla nikashituka na sikusikia ile sauti,nikafungua mlango sikuona mtu lakini tangu muda ule sauti yangu imekauka haitoki vizuri,hii ina maana gani?
kuna watu(wachawi) walichukua sauti yako kimiujiza.
 
Mimi huwa nikitamani kitu chochote ambacho sina lakini kiko ndani ya uwezo wangu kukipata lazima hicho kitu nitakipata tu iwe ni kwa kununua mimi mwenyewe au kwa kupewa(kuzawadiwa)
Mfano labda nikaona mtu ana smartphone nzuri au kitu kizuri alafu mimi nikatamani niwe nacho alafu nikakiota hicho kitu ninachokitamani lazima nitakimiliki tu..
Sasa swali langu ni je ni kwanini au kupitia ndoto inamaanisha kwamba ninachokiota nina uwezekano wa kukipata??
yote yanayotukia ktk maisha hutanguliwa na ulimwengu wa roho, uotacho ndicho hutokea au dalili ya kinachofanyika ktk ulimwengu wa roho
 
Mimi kuna ndoto huwa naiota,sijui maana yake,yaani nikiijiwa tu na wachawi ndotoni huwa nachukuaga fimbo mfano wa bua la mtama,hilo bua nikilishika tu linaninyanyua juuu na kuanza kupambana na wachawi hao,nikizidiwa nguvu,bua linaanza kufukuzana kwa kasi kubwa mpaka wachawi wanachoka,likiwadi nguvu linawafukuza mbaya,siku moja lilinibeba na kumfukuza bibi mmoja hadi akateguka miguu akawa anatembelea magoti mpaka alipotoka eneo la ajali akapotea,nini tafsiri yake hii ndoto wadau,na inanirudia sana,na huwa napendezwa saana nikiiota hii ndoto maana ni starehe kweli ukiwa unaiota
kuna kundi la wachawi huwa wanakuja kukudhuru ila huwa wanashindwa.
 
Mie niliota ndoto nang'oka meno kuna mama flan alininunia sasa nilipotazamana nae katika ndoto ndo baada ya mda mfupi nikawa nashindwa kuongea baada ya mda kidogo ndo nikawa naskia meno yanang'oka matatu ya juu.
Mkuu ina maana gani hiyo?
 
Ktk maisha tunakutana na changamoto nyingi sana,ktk mchakato huo basi nikajikuta tumefarakana na jamaa mmoja hivi na hatimaye tukaingia kwny bifu zito.
Hali iliyopelekea mpaka kukatika kwa mawasiliano baina yetu...Sasa juzi nimeota nimekutana na jamaa kanipokea Kwa bashasha tukaenda mpk kwake Kwa ajili ya chakula, nilipofika kwake mke wake alikasirika ....hebu nitafsirie Mkuu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom