Tafadhali Magufuli: Matatizo Haya Mengine Mnajitakia Bure

Tafadhali Magufuli: Matatizo Haya Mengine Mnajitakia Bure

Pamoja na li mada ako lirefuuuuuuuuuu ni ujinga kuamini kwamba huyu mtu ndiye mtu sahihi wa kutuvusha!! Aachane na u-much know, wenzake watamwumiza tayari wameshamjua kwamba ni mweupe ndiyo maana zinapigwa!! Aachane na mambo ya kujiamulia kila kitu hatatoka salama!! Aende wenye mfungo akaombe hekima labda itakuwa salama yake!!
 
Ukweli utabaki pale pale.

kumtisha cag haibadilishi lolote kwenye ukweli kwamba Trilion 1.5 haijulikani ilipo.kwa luga rahisi imepigwa na jiwe.
 
kwani hapa unashindwa kujiongeza kwenye kujumlisha na kutoa!!!

Kati ya
Shilingi
bilioni 25,307.48 zilizokusanywa,
Shilingi
bilioni
23,792.30 zilitolewa kwa ajili ya mishahara ya watumishi,
matumizi mengine, matumizi ya maendeleo na fedha kwa ajili ya
kulipa madeni yatokanayo na amana za Serikali pamoja na riba
Kobello ajibu hoja hii, cag alihojiwa na azam tv akasema kuna pesa zimetumika na anaamini zimetumika kwenye eti kwenye matumizi mengine ya serikali ambayo hayakuwa yameidhinishwa na bunge na akataka bunge lihoji zimekwenda wapi? Je cag hapa alikuwa mjinga kutoa kauli hii? Tatizo hapa ni kuwa kobello anaamini serikali iko sahihi wakati wote na ndo maana post zake zote hutetea serikali hata kama ndo imekosea! imefika hatua cag anaitwa in public na rais ili atoe kauli ya kuisafisha serikali si hatari hii! yaani auditee anamtaka auditor amsafishe kwa nguvu wakati report ipo waaaazi kabsaaaa. Ndipo nchi ilipofika kwa sasa anyway magu husema tupo pazuri sana na tutembee kifua mbele!
 
nimejifunza kitu kimoja.
katika zama hizi za mitandao au dunia kuwa familia taarifa zinasafiri haraka.
kujibu kwa wakati au kutoa ufafanuzi kwa baadhi ya mambo yanayoleta utata kutaleta tija ktika pande zote watawala na watawaliwa.
mitandao imewaweka wananchi karibu na taarifa leo kuliko miaka yote.
Na wakati huo huo Mtukufu anaona mitandao ndio ADUI namba moja, wala sio wateule wake au yeye mwenyewe wasiojua wajibu wao!! Bado tunayo safari ndeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeefu!
 
Kizazi cha usiseme hiki,usifanye hiki,usishirikiane na yule,usikae huko hakuna maendeleo.Ujinga tumeshauondoa,ila upumbavu unazidi kukomaa.
 
Umechambua vzr sana ila sehem moja tuu imefanya hii thread yko iwe taka taka na ya ovyo ovyo. Nadhan umeelewa
 
Mahaba ni hatari, ule uwezo na umakini was mwanakijiji sijui umeenda wapi!....kama vile anamatarajio Fulani Siku hizi!....time will tell..
Typical GAMBA. Utayasikia MAGAMBAs kule bungeni yakitokwa mapovu, then yanahitimisha hotuba zao kwa KUUNGA MKONO HOJA!!
 
Na wakati huo huo Mtukufu anaona mitandao ndio ADUI namba moja, wala sio wateule wake au yeye mwenyewe wasiojua wajibu wao!! Bado tunayo safari ndeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeefu!
Pia kama wako safi kwanini wanaogopa uwazi? Kwenye kuendesha shughuli za serikali, ikiwemo na bungelive,pia kwann wanatumia nguvu kubwa kuuwa upinzani hali Uko kikatiba,nini ajenda iliyopo.
 
Nani alimjibu zitto na alimjibuje? Kwa nini jibu hilo halikutolewa wakati ukaguzi unafanyika?
Humu JF alishajibiwa, Polepole alishamjibu jibu ambalo linafanana na jibu hilohilo alilolitoa Naibu FM leo bungeni.
Kwanini jibu litolewe wakati ukaguzi unafanyika? Kwani Prof. Assad aliuliza hilo mpaka ajibiwe? Hilo ni swali alilokuja nalo Zitto.
Pof. Assad hakuuliza swali kama hilo.
 
Ninaweza kusema Serikali hawakujibu mapema kwa sababu hata wao hawakuwa na majibu. Sionisababu yoyote. Ili suala limekuwepo tangu Prof alipokabidhi ripoti, Zitto aliliamplify tu. Je hawakuliona tangu wakati wa ukaguzi?

Uongozi unaotaka mapungufu yasionekane unakuwa na dalili za udhaifu. Kwa mazingira ya sasa hii haiwezekani na ukiilazimisha utapata msongo wa mawazo katika uongozi wako.
 
Nasikia kuna mwanasheria kakutwa Na hatia kwa kumnanga mataputapu kwenye WhatsApp.
Haya tuendelee Na tahadhari wajamani, wengine hizo milioni tano za kumpa kaka hakimu tuna matumizi nayo mengine
Yap ni kweli,mwanasheria Yule nilisoma naye darasa Moja,tulikuwa naye kwenye maombi ili asifungwe,bora hiyo faini ya 5M kuliko kuswekwa kule.
Nalog off
 
CAG Hakuwahi kuuliza 1.5T. Hizo zimeibuliwa ukurasa wa 34 collection vs. expenditure.
Kwa mfumo wa IPSAS, collection huhesabiwa hata kama zipo kwenye form ya hatifungani ambazo hazijaiva.
Kuelewa kirahisi, jumlisha hela za kodi na zisizo za kodi na mikopo na misaada kutoka nje. Hizo ndiyo hela cash ambazo unaweza kuzitawanya chapchap utapozipata.
Hatifungani, pamoja na kuwa ni hela halali, liquidity yake siyo sawa na hela za kodi na misaada. Securities huwa zinawachanganya watu, na nyingi zao hutumika ku-rollover madeni ya ndani.
Hata wanasiasa wa CCM,CDM,CUF,ACT wote nimeshawasikia wakizielezea vibaya hela za hatifungani. Wengi wao, pamoja na kusoma kwao bado ni weupe sana kwenye haya mambo.
Wanasiasa wengi Tanzania, hawapo enlightened na hii itakuja kutugharimu mbele tusipochukua tahadhari.


Mkuu nje ya inchi???

CAG hakuwai kuuliza 1.5tril iko wapi?? Alivyo sema bunge lihoji ulipo na ilivyo tumika manaake ni nini?


PAC kama daraja kati ya serekali na CAG wamesubiri Maelezo lakini wapi.

IPSAS ni new to the government but not new to ACCOUNTING usifikiri Abas hajui alicho kiandika. IPSAS ni mlango wa kukimbia shutuma.

Wewe ndo hujaelewa achana na kukimbilia hatifungani. Pesa ilikuwepo na imetumika ila haikuingia kwenye vitabu vya mahesabu.
 
Ukweli ni kwamba serikali kila muda inasubiri yenyewe kuwekwa kwenye kona badala ya kufafanua vitu kwa mapana ambayo wananchi wataelewa. Ndio maana wengine wameamua kuhukumu tu kuwa zimeibiwa kinyume na hoja ya msingi ya Zitto na hata ripoti ya CAG.

Hili sakata linatoa taswira halisi ya siasa zetu lakini pia uzembe wa watendaji wa serikali kuhakikisha taarifa zao hazileti taharuki kwasababu ya ufafanuzi finyu kwenye swala zito.

Hata kama tunamchukia vipi JPM haiwezi kuingia akili kubeba Trilioni 1.5 kwa kipindi kifupi na mazingira haya ya uadui aliojijengea kwa wahujumu uchumi. Hoja ya Zitto ipo pale pale na sasa bunge lifanye kazi yake.
Mhhmm ndugu bunge hili la Ndugai???
 
Back
Top Bottom