jambo Tanzania
JF-Expert Member
- May 29, 2017
- 377
- 281
kwakweli bongo bado sana yaani 1.5T hazijulikani zilipo alafu wabunge wanapiga makofi na kushangilia ???.hasira kabisa
Unaona sasa.. watu wanazungumzia trilioni 1.5... mimi nafikiri hii haikuja kwa bahati mbaya..Mimi nasubiri kuona watu wanahojiwa kuhusu upotevu wa takribani Sh Billion 40 kama kodi
Ripoti inaonesha mafuta yenye msamaha wa kodi wa takribani Sh. 12 Billion hayakutumika kwa wanufaika wa msamaha!
That said, kuna uwezekano mkubwa mafuta husika yameingizwa kwenye mzunguko pasipo kulipa kodi!!
Si hivyo tu, transit goods ambazo kodi yake ni takribani 27 Billion; hakuna ushahidi kwamba zilivuka border na kwa maana hiyo kuna uwezekano mkubwa bidhaa husika zimetumika Tanzania bila kulipa kodi!
CAG kabla ya kukamilisha ripoti Yake alitoa siku 21 kwa serekali itoe Maelezo/hesabu namna 1.5tril ilivyotumika wameshindwa.
Hapana usipite tu.. japo salimia..Mi napita tu
Mbona yeye CAG mwenyewe hakupewa maelezo mkuu ina maana hili hakulihoji kabla ya ripoti kwenda hewani?Hii ndio hoja muhimu sana. Nashangazwa na watu kukasirika kwamba wananchi wana hoji. Sasa wananchi wangefanyaje kama hakuna mtu anawapa taarifa kwa uhakika? Prof. Assad alitakiwa kusimama mara moja kabla ya kupigiwa simu na Rais kuulizwa... kwanini hakutoa maelezo kumsahihisha Zitto na badala yake kazi hiyo inafanya na Polepole? ambaye anawahi kutoa maelezo yanayofanana na yanayotolewa na Naibu Waziri leo?
Hivi hili mmelitoa wapi? jamani.. tufuatiliage mambo basi kama watu wenye dalili kuwa tuliingia kwenye majengo ya shule..
Yaani 1.5 trillion wewe unaona ni kijitakwimu kidogo? Kwa taarifa yako swala la mitandao halizuiliki siyo kwa miaka hii ya technolojia ya sasa! Hii siyo 70's huu ni mwaka 2018 the modern world. Serikali iwajibike kwa wananchi kujibu hoja na tuhuma siyo kuwafunga midomo. Hizi kukurukakara za kutumia vyombo vya dola na kuwakamata watu ovyo na kuwafungulia kesi zisizo na tija hazitowasaidia. Sana sana zinajenga chuki kwa wananchi tu.Hakuna haja ya kuwa na mitandao km inatumiwa kupotosha, kutukana na kudhalilisha watu..nchi haiwezi kuwa jalala na taifa la wahalifu, ufinyu wa akili wa watz wengi ndiyo tatizo kubwa elimu yetu haifuti ujinga tena..hata Phd holders ni wajinga, nchi hii ilikuwepo, ipo na itakuwepo kwa anayejua nadharia za maendeleo hafikirii kufa kwake ndiyo mwisho wa Tanzania, unapokuwa kiongozi una wajibu waa kulinda maslahi hata ya kizazi cha tano mbele! tunajenga taifa gani la kudhihakiana, wadogo kutukana wakubwa, lugha za matusi mitandaoni ndio ushujaa...ukiachia hali hiyo taifa halina future!! inashangaza wakati huu ambao serikali inadhibiti uhalifu na aina zote za uovu watu hawatambui, lakini hitilafu ndogo ya kitakwimu ndiyo imekuwa ajenda..siku za nyuma ambapo uovu ulitamalaki, mishahara hewa, safari hewa, Escrow..nk kelele hizi hazikusikika..nini maana yake, kelele nyingi mitandaoni ni za waathirika wa maamuzi na uendeshaji wa serikali awamu ya tano, wengi ni wahanga wa uhalifu uliozoeleka zama zilizopita ambao sasa umekomeshwa!
Na Zanzibar wakisema wana mapato ya bilioni 200 utabisha?
ripoti ikishaandikwa serikali inapewa siku 21 kujibu mapungufu. mbona hawakujib, manake walishindwa. ww unatetea nn, kwnn watu wasiamini ziliibwa!Kwanini kuwe na machafuko? wananchi nao ni lazima wawe na akili ya kutafakari vitu.. sasa mtu kasema Trilioni 1.5 haijulikani ilipo, watu wanaanza kusema imeibwa, imeliwa, amechukua kaweka Chato.. n.k sasa haya yote yanatoka wapi?
Wewe ndio unaona hilo na ndio ukweli kwa mwananchi wa kawaida unae enda na wakati .swali, je hawa viongozi wa serikali wanao ona Vinginevyo kabisa tuwaeleweje wa shamba au wako nyuma ya wakati !?nimejifunza kitu kimoja.
katika zama hizi za mitandao au dunia kuwa familia taarifa zinasafiri haraka.
kujibu kwa wakati au kutoa ufafanuzi kwa baadhi ya mambo yanayoleta utata kutaleta tija ktika pande zote watawala na watawaliwa.
mitandao imewaweka wananchi karibu na taarifa leo kuliko miaka yote.
ukiwauliza wao watakupa jibu bora kabisaa kuliko mimi mkuu.Wewe ndio unaona hilo na ndio ukweli kwa mwananchi wa kawaida unae enda na wakati .swali, je hawa viongozi wa serikali wanao ona Vinginevyo kabisa tuwaeleweje wa shamba au wako nyuma ya wakati !?
Sio anatumbukiza. Tayari tumesha vurugwa mpaka hatuna hamu nae .yaani sasa hivi dua tumegeuzia siku ziende salama na haraka tushuke kwenye hili LorryAta endelea hivi mpka lini miaka 7 mbele kwa staili hii huoni anatumbukiza inchi kwenye machafuko?