Hamna lolote la maana kwenye uzi wako..
Umeshakuwa compromised siku nyingi wewe..
Tunataka maelezo ziwapi 1.5Tril.
Issue hapa ni hela kutumika bila ridhaa ya Bunge; na hili ndilo CAG alilosema...
Ushauri - Watumie TV STATIONS ZOTE KWA MASAAA YOTE YA WIKI NZIMA KUKANUSHA HILI , na wawatumie wanachama wao mahiri akiwemo huyu mleta mada , Bali wafahamu kwamba ripoti ya CAG Haiwezi kufutwa na bunduki ama watu wasiojulikana .
Ukweli ni kwamba serikali kila muda inasubiri yenyewe kuwekwa kwenye kona badala ya kufafanua vitu kwa mapana ambayo wananchi wataelewa. Ndio maana wengine wameamua kuhukumu tu kuwa zimeibiwa kinyume na hoja ya msingi ya Zitto na hata ripoti ya CAG.
Hili sakata linatoa taswira halisi ya siasa zetu lakini pia uzembe wa watendaji wa serikali kuhakikisha taarifa zao hazileti taharuki kwasababu ya ufafanuzi finyu kwenye swala zito.
Hata kama tunamchukia vipi JPM haiwezi kuingia akili kubeba Trilioni 1.5 kwa kipindi kifupi na mazingira haya ya uadui aliojijengea kwa wahujumu uchumi. Hoja ya Zitto ipo pale pale na sasa bunge lifanye kazi yake.
Mkuu mwanakijiji umejaribu kumtetea zitto na kuwalaumu wanaserikali lakini hutaki kutambua kuwa wapo wapinzani wa magufuli ambao kazi yao ni kumvuruga tu kwa maslahi yao binafsi....Serikali ikisema chochote lazima waspin ili wapate popularity na ujira wao.
Naona ungefanya vyema kwa kuwakumbusha wapinzani wa Magufuli kihoji matatizo ya kweli yanayofanywa na Serikali.
Leo hii wapinzani wakihoji kwa nguvu zote juu ya upungufu wa bajeti ya afya ...hilo litakuwa ni tatizo la kweli na lenye manufaa kwao na kwa jamii.
Hawatakiwi kuspin ukweli ili uonekana kama uongo...wanatakiwa wahoji kwa manufas ya wananchi na nchi.
Geremy Corbyn amemuhoji Theresa May kuhusu kuishambuli Syria kwa ustadi mkubwa sana wapinzani wajifunze kuhoji kwa style hii.
Mbona alijibiwa zilipo na akakataa?Mkuu Mzee Mwanakijiji , nalitazama suala la 1.5T katika mtazamo tofauti na 'kuchelewa kujibu'
Moja ya sifa za Mwl Nyerere ni uwezo kutambua wapi serikali haieleweki.
Sifa hiyo iliambatana na uwezo wa kuieleza jamii tatizo lililopo (address) katika lugha rahisi sana (effective communication)
Zitto kama Raia na kiongozi amehoji. Inawezekana hakuelewa kitu. Kwa kiongozi kama Zitto kutoelewa jambo kuna maana moja, sehemu kubwa ya jamii haikuelewa.
Ndiyo maana akauliza 1.5 imekwenda wapi au ipo wapi!
Kwa hilo ametimiza wajibu kama kiongozi na Raia na alipaswa kujibiwa kwa hoja
Jamii yetu imepoteza uwezo wa kuhoji au kujibu hoja kwa hoja.
Viongozi wanatazama wataelewekaje wakisema abcd kwa wakubwa zao badala ya 'wataelewekaje kwa hoja inayozungumziwa'
Zitto amehoji 1.5 hazionekani. Majibu anayopew 'halmashauri ya Kigoma ina hati chafu'
Amehoji 1.5 mbona haionekani, majibu anayopewa ' Kuna ubadhirifu Chadema'
Pole pole anamjibu Zitto kwa hoja ya 'ashatakiwe'. Yaani kuhoji ni kosa la jinai siku hizi
Kwakuwa hakuna anayejibu hoja za Zitto kwa hoja na lugha rahisi, hoja zake zinasimama wima na kuiweka serikali katika mazingira ya utatanishi bila sababu
Lini viongozi watajifunza kujibu hoja kwa mantiki na lugha nyepesi inayoeleweka kwa walipa kodi?
Kwa hili la 1.5 serikali ieleze kwa lugha rahisi tu, zipo wapi au zimetumika wapi na kwa utaratibu upi
Kuna uwezekano hakuna tatizo lolote, bila kueleza hilo hoja za Zitto zitabaki kuwa na mantiki
Nitashangaa kama lugha itakyotumika ni ile ya '' expenditure, account receivable, liquidity, bond, collection , overhead' na madudu mengine yatakayowachanganya wananchi zaidi.
Itumike lugha rahisi tu, 1.5 zipo wapi au kwanini hesabu hazionekani kukokotolewa kwa usahihi. Hilo tu
Tena fedha ni za kwetu.sio zakeLumumba pekee mwenye uwezo wa kujenga hoja nzito humu JF.
Ana balance mambo na mnafiki.
Anyway nikirudi kwenye point nadhani kutumia pesa nje ya mipango ni utovu wa nidhamu na JPM ana kesi ya kujibu hapa,
Haitaji kua mkali.
Nani alimjibu zitto na alimjibuje? Kwa nini jibu hilo halikutolewa wakati ukaguzi unafanyika?Mbona alijibiwa zilipo na akakataa?
Halafu, mbona TRA kwenye website yao hawakuripoti mapato ya 15.3T? Na records zipo hadi leo in excel, kila idara kila mkoa na refunds etc.. Na CAG hakusema TRA imepotosha mapato by 2.2T, na akijibiwa maswali yake anakataa majibu bila kutoa sababu za kimahesabu.
Tatizo siyo lugha nyepesi, wala si kuchelea kujibu. Tatizo ni kushikilia hoja kisiasa kwa manufaa ya kisiasa. Kujiondoa uelewa makusudi, ili unufaike kisiasa. Hilo ndiyo tatizo na lipo wazi.
kwani hapa unashindwa kujiongeza kwenye kujumlisha na kutoa!!!Nani aliyekwambia zimeanza jana? We vipi?
Angalia cash budget za BoT. Kuna tofauti yeyote ya maana kwenye mapato na matumizi?
Mbona exchequer releases ni 20T? Hizo zingine zimeenda wapi?
13.16 recurrent na 6.9 development. Makusanyo, Grants na disbursed loans 3.1T na Revenue za ndani 16.34T.
Hiyo ni cash budget, easily explainable. Na BOT anakwambia (July, MER) cumulative domestic debt due ni 5.9T, waka-rollover 4.6T. Sasa explanations za leo zina tofauti gani na MER au BER? Au unaongea kishabiki tu?
Halafu nani kasema Assad ni mweupe? Are you serious?
Assad hakuuliza 1.5 hata sehemu moja. Kwenye appendix za Central Govt expenditure audits kuna hoja ya 325billions TRA ilizokusanya kwa ajili ya other agencies kuwa entered twice kwenye consolidated accounts[3.2: 4(m)].
List of qualified opinions zipo kuanzia ukurasa wa 307 mpaka 315. Hakuna 1.5T ilipotajwa, nada!
Usilazimishe mambo.