MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 10,223
- 22,303
Kwa dhati kabisa ninawasihi wanaCCM tusije tukafanya kosa la kuwafananisha TEC na CHADEMA. Nimeona uzi wa ndugu Sir John Roberts akidai wanaCCM tuachiwe TEC kukabiliana nao. Naheshimu mawazo yake kama mwanaCCM mwenzangu ila siungi mkono hoja yake kwa 100%. Sir John labda haijui kiundani TEC akadhani nao pia watajibiwa kirahisi kama tunavyowajibu chama cha Mbowe.
Kanisa katoliki kama ilivyo CCM nalo limeenda hadi ngazi ya shina.. na linaongoza kwa kuwa na waumini wengi zaidi hapa nchini na duniani kwa ujumla. Wanaposema waraka wao utasomwa kwenye jumuiya ina maana hadi wananchi wa vijiji vya ndani huko Buhigwe au Kalambo wataamshwa usingizini. CHADEMA wao mambo yao huishia tu mijini na Twitter kwahiyo damage yao ni ndogo kulinganisha na hiki wanachofanya TEC.
Kingine kinachoogopesha ni hii tabia ya wakatoliki kuwa wakimya. Mapadre na maaskofu ni wasomi ambao tangu shuleni walikuwa ni vipanga yaani hawabahatishi. Wao wakishasema lao huwa hawahagaiki sana kubishana kitu kinachotia hasira mno. Ingekuwa CHADEMA hadi muda huu ungekuta Lema au Heche kashajitokeza na kuropoka pumba. Sasa hao TEC toka Padre Kitime aongee sijasikia kiongozi mwingine yeyote akiongea. Ni watu hatari. Hata tukisema CCM tuishambulie TEC kwa maneno bado itakua sawa na kujishambulia wenyewe kwasababu kuna wanaCCM wengi ambao ni wakatoliki. Kutakuwa na upinzani wa ndani.
Ikumbukwe pia hawa TEC hadi kutamka tayari wana mawasiliano na kiongozi wao mkubwa yaani Papa. Kwa msiojua nguvu ya papa mkasome kisa cha Papa Gregory VI na King Henry IV ndo mtaelewa vizuri. Mfalme alikalishwa kwenye baridi siku 3 akisubiri kuonana na papa amwombe msamaha. Haikuwa poa. Katoliki pia limekuwa likihusishwa na siasa za nchi nyingi duniani. Kwenye story ya vita ya Biafra huko Nigeria hili kanisa lilitajwa kufadhili waasi.
Wito wangu ni kuwasihi wasomi na wataalamu wa diplomasia & siasa ndani ya chama na serikali kukaa chini na TEC ili kumalizana nao. Kama kuna mbinu nyingine ambazo sio za kidiplomasia lakini zinaweza kutuliza hali ya hewa nazo pia zitumike. Kinachofanywa na TEC ni kuchonganisha serikali na wananchi huku wakitumia mbinu hatari ambayo sio ya kubeza.
Kanisa katoliki kama ilivyo CCM nalo limeenda hadi ngazi ya shina.. na linaongoza kwa kuwa na waumini wengi zaidi hapa nchini na duniani kwa ujumla. Wanaposema waraka wao utasomwa kwenye jumuiya ina maana hadi wananchi wa vijiji vya ndani huko Buhigwe au Kalambo wataamshwa usingizini. CHADEMA wao mambo yao huishia tu mijini na Twitter kwahiyo damage yao ni ndogo kulinganisha na hiki wanachofanya TEC.
Kingine kinachoogopesha ni hii tabia ya wakatoliki kuwa wakimya. Mapadre na maaskofu ni wasomi ambao tangu shuleni walikuwa ni vipanga yaani hawabahatishi. Wao wakishasema lao huwa hawahagaiki sana kubishana kitu kinachotia hasira mno. Ingekuwa CHADEMA hadi muda huu ungekuta Lema au Heche kashajitokeza na kuropoka pumba. Sasa hao TEC toka Padre Kitime aongee sijasikia kiongozi mwingine yeyote akiongea. Ni watu hatari. Hata tukisema CCM tuishambulie TEC kwa maneno bado itakua sawa na kujishambulia wenyewe kwasababu kuna wanaCCM wengi ambao ni wakatoliki. Kutakuwa na upinzani wa ndani.
Ikumbukwe pia hawa TEC hadi kutamka tayari wana mawasiliano na kiongozi wao mkubwa yaani Papa. Kwa msiojua nguvu ya papa mkasome kisa cha Papa Gregory VI na King Henry IV ndo mtaelewa vizuri. Mfalme alikalishwa kwenye baridi siku 3 akisubiri kuonana na papa amwombe msamaha. Haikuwa poa. Katoliki pia limekuwa likihusishwa na siasa za nchi nyingi duniani. Kwenye story ya vita ya Biafra huko Nigeria hili kanisa lilitajwa kufadhili waasi.
Wito wangu ni kuwasihi wasomi na wataalamu wa diplomasia & siasa ndani ya chama na serikali kukaa chini na TEC ili kumalizana nao. Kama kuna mbinu nyingine ambazo sio za kidiplomasia lakini zinaweza kutuliza hali ya hewa nazo pia zitumike. Kinachofanywa na TEC ni kuchonganisha serikali na wananchi huku wakitumia mbinu hatari ambayo sio ya kubeza.