Viongozi wangu wa CCM inatosha sasa, TEC hawatatuelewa hadi tueleweke!

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Lazima niseme. Nguvu kubwa inafanywa na viongozi wetu wa CCM Taifa ambao pia ni viongozi serikalini kupata 'uungwaji mkono' na Maaskofu wa Kanisa Katoliki. Ni maandalizi ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2025. Kuanzia Mwenyekiti/Rais hadi viongozi wengine waandamizi wamekuwa 'busy' na kutafuta kukubalika na wakatoliki.

Pamoja na ukweli kuwa ili ushindi upatikane na utulivu wa kiuongozi utamalaki lazima ukubalike na TEC, sasa imekuwa 'too much'. Makada wabobezi na waandamizi (hasa tulio wakatoliki) tunatumwa bila kusemwa kwa Kardinali, Maaskofu, Mapadre na wengineo ili kusaka kukubalika kwa viongozi wetu.

Amini nawaambia viongozi wangu wa kichama na kiserikali, TEC hawatashawishika kirahisi.

Hawatasahaulishwa msimamo na Tamko lao juu ya mkataba tata wa DP World. Hawatalaghaiwa kwa ahadi za kifedha; kupokelewa uwanjani au kupewa kanzu. TEC bado wanalo la bandari na wamejipanga kuusimamia msimamo wao.

Ili CCM tujisafishe mbele ya TEC, Tamko lao liheshimiwe. Kupigana vikumbo kujisogeza kwao hakutasaidia chochote. TEC imesheheni waelewa wa mambo zaidi ya wanasiasa wa zamani na wa sasa. Si wepesi kuyumbishwa kwa ahadi zisizo na kadi; michngo ya michongo na zawadi maridadi.

CCM tumeshaanza kampeni, wenzetu vipi?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kilosa, Morogoro)
 
Hata Mimi naunga mkono,kwani lazima Kila kitu hao TEC waunge mkono? Ni upuuzi kutokubalia kukubaliana na itakuwa Haina maana Sasa ya kuwa na Taifa.

Maendeleo huletwa katikati ya mgongano wa fikra,TEC na RC hawaendeshi hii Nchi ni mambo ya kipuuzi kuwaza hivyo na inajenga mbegu ya chuki kw watu wa madhehebu na dini zingine.

Inakera sana.
 
Lazima niseme. Nguvu kubwa inafanywa na viongozi wetu wa CCM Taifa ambao pia ni
Wewe ndo muakilishi wa hao TEC au unesemea hisia zako? Kuna mtu ambaye anaweza kugomea CCm hapa Tz kweli, wewe utakua hujui siasa za CCM, TEC inahitaji sana CCM kiliko CCM inavo hitaji TEC, au umesahau pesa za kifisad za Escrow zilipitia Mkombozi benk ambayo ni Benki ya kanisa na Kanisa elipokea fungu, wataka uchunguzi wa hiyo kesi ufufuliwe uone kama mkombozi bank itakuepo tena............acha kushezea state hususani ukiwa Africa.
 
TEC haifanani na akina Waitara, Katambi, Mollel, Kafulila au akina Mkumbo; ambao wakiwa na njaa wanapiga sana kelele, wakirushiwa mfupa, ni kushangilia na musifia kama wehu.

TEC haiwezi kunyamazishwa au kubadilishwa katija wanachokiamini kuwa siyo sawa, kwa kurushiwa mchango au kutembelewa maofisini kwao. Kitakachobadilisha msimamo wa TEC ni Serikali na viongozi kuachana na ule mkataba wa kishenzi wa DP.
 
Lazima niseme. Nguvu kubwa inafanywa na viongozi wetu wa CCM Taifa ambao pia ni viongozi serikalini kupata 'uungwaji mkono' na Maaskofu wa Kanisa Katoliki. Ni maandalizi ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2025. Kuanzia Mwenyekiti/Rais hadi viongozi wengine waandamizi wamekuwa 'busy' na kutafuta kukubalika na wakatoliki.

Pamoja na ukweli kuwa ili ushindi upatikane na utulivu wa kiuongozi utamalaki lazima ukubalike na TEC, sasa imekuwa 'too much'. Makada wabobezi na waandamizi (hasa tulio wakatoliki) tunatumwa bila kusemwa kwa Kardinali, Maaskofu, Mapadre na wengineo ili kusaka kukubalika kwa viongozi wetu.

Amini nawaambia viongozi wangu wa kichama na kiserikali, TEC hawatashawishika kirahisi. Hawatasahaulishwa msimamo na Tamko lao juu ya mkataba tata wa DP World. Hawatalaghaiwa kwa ahadi za kifedha; kupokelewa uwanjani au kupewa kanzu. TEC bado wanalo la bandari na wamejipanga kuusimamia msimamo wao.

Ili CCM tujisafishe mbele ya TEC, Tamko lao liheshimiwe. Kupigana vikumbo kujisogeza kwao hakutasaidia chochote. TEC imesheheni waelewa wa mambo zaidi ya wanasiasa wa zamani na wa sasa. Si wepesi kuyumbishwa kwa ahadi zisizo na kadi; michngo ya michongo na zawadi maridadi.

CCM tumeshaanza kampeni, wenzetu vipi?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kilosa, Morogoro)

Wengine bado tunasubiri fukuto na wanaharakati life Kwa kudra za Mola.
 
Lazima niseme. Nguvu kubwa inafanywa na viongozi wetu wa CCM Taifa ambao pia ni viongozi serikalini kupata 'uungwaji mkono' na Maaskofu wa Kanisa Katoliki. Ni maandalizi ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2025. Kuanzia Mwenyekiti/Rais hadi viongozi wengine waandamizi wamekuwa 'busy' na kutafuta kukubalika na wakatoliki.

Pamoja na ukweli kuwa ili ushindi upatikane na utulivu wa kiuongozi utamalaki lazima ukubalike na TEC, sasa imekuwa 'too much'. Makada wabobezi na waandamizi (hasa tulio wakatoliki) tunatumwa bila kusemwa kwa Kardinali, Maaskofu, Mapadre na wengineo ili kusaka kukubalika kwa viongozi wetu.

Amini nawaambia viongozi wangu wa kichama na kiserikali, TEC hawatashawishika kirahisi.

Hawatasahaulishwa msimamo na Tamko lao juu ya mkataba tata wa DP World. Hawatalaghaiwa kwa ahadi za kifedha; kupokelewa uwanjani au kupewa kanzu. TEC bado wanalo la bandari na wamejipanga kuusimamia msimamo wao.

Ili CCM tujisafishe mbele ya TEC, Tamko lao liheshimiwe. Kupigana vikumbo kujisogeza kwao hakutasaidia chochote. TEC imesheheni waelewa wa mambo zaidi ya wanasiasa wa zamani na wa sasa. Si wepesi kuyumbishwa kwa ahadi zisizo na kadi; michngo ya michongo na zawadi maridadi.

CCM tumeshaanza kampeni, wenzetu vipi?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kilosa, Morogoro)
Asante ujumbe umefika
 
Wewe ndo muakilishi wa hao TEC au unesemea hisia zako? Kuna mtu ambaye anaweza kugomea CCm hapa Tz kweli, wewe utakua hujui siasa za CCM, TEC inahitaji sana CCM kiliko CCM inavo hitaji TEC, au umesahau pesa za kifisad za Escrow zilipitia Mzalendo benk ambayo ni Benki ya kanisa na Kanisa elipokea fungu, wataka uchunguzi wa hiyo kesi ufufuliwe uone kama mkombozi bank itakuepo tena............acha kushezea state hususani ukiwa Africa.
Mzalendo tena
 
Hata Mimi naunga mkono,kwani lazima Kila kitu hao TEC waunge mkono? Ni upuuzi kutokubalia kukubaliana na itakuwa Haina maana Sasa ya kuwa na Taifa.

Maendeleo huletwa katikati ya mgongano wa fikra,TEC na RC hawaendeshi hii Nchi ni mambo ya kipuuzi kuwaza hivyo na inajenga mbegu ya chuki kw watu wa madhehebu na dini zingine.

Inakera sana.
Utakereheka kwa sababu ya ujinga.

TEC kama taasisi ina haki kusimama katika inachokiamini. Na wewe kama mtu binafsi au taasisi yako mna haki kuendelea kusimama katika mnachokiamini. Wafanya maamuzi watapima uzito wa hoja za kila upande na athari ya kuzipuuza au kuzifuata. Lakini pia sisi wananchi tuna haki ya kupima uzito wa hoja za kila upande, ukiwemo upande wa Serikali.

Mwisho wa yote, wananchi ndio waamuzi wa mwisho. Yule ambaye hoja zake zinaungwa mkono na wengi na zipo kwaajili ya maslahi ya umma, ndiye atakuwa na turufu.

Serikali ikishupaza, TEC ina haki ya kuwaambia waumini wake na hata wasiowaumini wa RC, kuwa kwa mtazamo wetu kama viongozi wenu, ni dhahiri Serikali hii haipo kwa manufaa yenu na vizazi vijavyo kwa sababu inapora rasilimali za nchi na kuwagawia moja kwa moja wageni.

Atakayeiunga mkono atambue kuwa ameshindwa kutimiza wajibu wake wa msingi kama muumini, ambao ni kumpenda jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe. Na jirani zetu ni hawa Watanzania wanaoishi leo na wale watakaofuatia baada yetu. Waumini na wengineo watafanya maamuzi yao maana katika kuufuata ujumbe wa Mungu, hakuna anayelazimishwa.
 
Utakereheka kwa sababu ya ujinga.

TEC kama taasisi ina haki kusimama katika inachokiamini. Na wewe kama mtu binafsi au taasisi yako mna haki kuendelea kusimama katika mnachokiamini. Wafanya maamuzi watapima uzito wa hoja za kila upande na athari ya kuzipuuza au kuzifuata. Lakini pia sisi wananchi tuna haki ya kupima uzito wa hoja za kila upande, ukiwemo upande wa Serikali.

Mwisho wa yote, wananchi ndio waamuzi wa mwisho. Yule ambaye hoja zake zinaungwa mkono na wengi na zipo kwaajili ya maslahi ya umma, ndiye atakuwa na turufu.

Serikali ikishupaza, TEC ina haki ya kuwaambia waumini wake na hata wasiowaumini wa RC, kuwa kwa mtazamo wetu kama viongozi wenu, ni dhahiri Serikali hii haipo kwa manufaa yenu na vizazi vijavyo kwa sababu inapora rasilimali za nchi na kuwagawia moja kwa moja wageni. Atakayeiunga mkono atambue kuwa ameshindwa kutimiza wajibu wake wa msingi kama muumini, ambao ni kumpenda jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe. Na jirani zetu ni hawa Watanzania wanaoishi leo na wale watakaofuatia baada yetu. Waumini na wengineo watafanya maamuzi yao maana katika kuufuata ujumbe wa Mungu, hakuna anayelazimishwa.
Isimamie na Wala hakuna mtu amekataza wao kusimamia na nakereka na kujipendekeza Kwa viongozi wa Serikali.

Serikali nayo inatakiwa kusimamia na inachokiamini,hii Nchi haiongizwi na TEC
 
Lazima niseme. Nguvu kubwa inafanywa na viongozi wetu wa CCM Taifa ambao pia ni viongozi serikalini kupata 'uungwaji mkono' na Maaskofu wa Kanisa Katoliki. Ni maandalizi ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2025. Kuanzia Mwenyekiti/Rais hadi viongozi wengine waandamizi wamekuwa 'busy' na kutafuta kukubalika na wakatoliki.

Pamoja na ukweli kuwa ili ushindi upatikane na utulivu wa kiuongozi utamalaki lazima ukubalike na TEC, sasa imekuwa 'too much'. Makada wabobezi na waandamizi (hasa tulio wakatoliki) tunatumwa bila kusemwa kwa Kardinali, Maaskofu, Mapadre na wengineo ili kusaka kukubalika kwa viongozi wetu.

Amini nawaambia viongozi wangu wa kichama na kiserikali, TEC hawatashawishika kirahisi.

Hawatasahaulishwa msimamo na Tamko lao juu ya mkataba tata wa DP World. Hawatalaghaiwa kwa ahadi za kifedha; kupokelewa uwanjani au kupewa kanzu. TEC bado wanalo la bandari na wamejipanga kuusimamia msimamo wao.

Ili CCM tujisafishe mbele ya TEC, Tamko lao liheshimiwe. Kupigana vikumbo kujisogeza kwao hakutasaidia chochote. TEC imesheheni waelewa wa mambo zaidi ya wanasiasa wa zamani na wa sasa. Si wepesi kuyumbishwa kwa ahadi zisizo na kadi; michngo ya michongo na zawadi maridadi.

CCM tumeshaanza kampeni, wenzetu vipi?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kilosa, Morogoro)
Saa 100 si aliwahonga 100m juzi mbona hawakuzikataa
 
Isimamie na Wala hakuna mtu amekataza wao kusimamia na nakereka na kujipendekeza Kwa viongozi wa Serikali.

Serikali nayo inatakiwa kusimamia na inachokiamini,hii Nchi haiongizwi na TEC
Pole Sana ndg kitu ambacho hujui hao viongozi Wana madhehebu yao na wanaheshimu kauli za viongozi wao hiyo ccm ni taasisi ndg Sana linapokuja swala la kuheshimu viongozi wa dini

Sent from my RMX2189 using JamiiForums mobile app
 
Pole Sana ndg kitu ambacho hujui hao viongozi Wana madhehebu yao na wanaheshimu kauli za viongozi wao hiyo ccm ni taasisi ndg Sana linapokuja swala la kuheshimu viongozi wa dini

Sent from my RMX2189 using JamiiForums mobile app
Viongozi kuwa na madhehebu Yao ni sawa ila msimamo wa madhehebu Yao haupaswi kuwa msimamo wa Nchi.

Ukiwa na madaraka kwenye Nchi hipaswi kuleta mambo ya madhehebu yenu.

Upuuzi wa hivi ukome maana unaweza kuja kuleta shida baadae
 
Back
Top Bottom