VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Lazima niseme. Nguvu kubwa inafanywa na viongozi wetu wa CCM Taifa ambao pia ni viongozi serikalini kupata 'uungwaji mkono' na Maaskofu wa Kanisa Katoliki. Ni maandalizi ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2025. Kuanzia Mwenyekiti/Rais hadi viongozi wengine waandamizi wamekuwa 'busy' na kutafuta kukubalika na wakatoliki.
Pamoja na ukweli kuwa ili ushindi upatikane na utulivu wa kiuongozi utamalaki lazima ukubalike na TEC, sasa imekuwa 'too much'. Makada wabobezi na waandamizi (hasa tulio wakatoliki) tunatumwa bila kusemwa kwa Kardinali, Maaskofu, Mapadre na wengineo ili kusaka kukubalika kwa viongozi wetu.
Amini nawaambia viongozi wangu wa kichama na kiserikali, TEC hawatashawishika kirahisi.
Hawatasahaulishwa msimamo na Tamko lao juu ya mkataba tata wa DP World. Hawatalaghaiwa kwa ahadi za kifedha; kupokelewa uwanjani au kupewa kanzu. TEC bado wanalo la bandari na wamejipanga kuusimamia msimamo wao.
Ili CCM tujisafishe mbele ya TEC, Tamko lao liheshimiwe. Kupigana vikumbo kujisogeza kwao hakutasaidia chochote. TEC imesheheni waelewa wa mambo zaidi ya wanasiasa wa zamani na wa sasa. Si wepesi kuyumbishwa kwa ahadi zisizo na kadi; michngo ya michongo na zawadi maridadi.
CCM tumeshaanza kampeni, wenzetu vipi?
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kilosa, Morogoro)
Pamoja na ukweli kuwa ili ushindi upatikane na utulivu wa kiuongozi utamalaki lazima ukubalike na TEC, sasa imekuwa 'too much'. Makada wabobezi na waandamizi (hasa tulio wakatoliki) tunatumwa bila kusemwa kwa Kardinali, Maaskofu, Mapadre na wengineo ili kusaka kukubalika kwa viongozi wetu.
Amini nawaambia viongozi wangu wa kichama na kiserikali, TEC hawatashawishika kirahisi.
Hawatasahaulishwa msimamo na Tamko lao juu ya mkataba tata wa DP World. Hawatalaghaiwa kwa ahadi za kifedha; kupokelewa uwanjani au kupewa kanzu. TEC bado wanalo la bandari na wamejipanga kuusimamia msimamo wao.
Ili CCM tujisafishe mbele ya TEC, Tamko lao liheshimiwe. Kupigana vikumbo kujisogeza kwao hakutasaidia chochote. TEC imesheheni waelewa wa mambo zaidi ya wanasiasa wa zamani na wa sasa. Si wepesi kuyumbishwa kwa ahadi zisizo na kadi; michngo ya michongo na zawadi maridadi.
CCM tumeshaanza kampeni, wenzetu vipi?
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kilosa, Morogoro)