DOKEZO Tabora Mjini hali tete, mafuta hakuna! Maji hakuna

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

syndicate

JF-Expert Member
May 5, 2016
204
315
Niendee moja kwa moja kwenye mada husika!

Mkoa wa Tabora hivi sasa ninapoandika uzi huu, uko kwenye taharuki kubwa ya kukosa mafuta!

Hali ni mbaya hapa mjini, petro station moja tu mji mzima inatoa huduma ya mafuta!

Hakuna kiongozi yoyote wa chama (CCM) au serikali ambaye ametoa ufafanuzi wowote!

Mkoa huu wa kishu'shu'shu na KI'CCM hali ni tete..! Mkoa umebaki mtupu hakuna mtetezi!

Nikumbushe kuwa jumatano ijayo ya mwanzo wa mwezi kwa fununu zilizopo EWURA wanatangaza bei mpya za mafuta, kitu ambacho kinatarajiwa, ni mafuta kupaa zaidi bei.

Nikumbushe pia mwezi mmoja uliopita ilitokea taharuki kama hii ya sasa, na kuonekana baadhi ya wafanyabiashara wakificha mafuta na baada ya wiki moja na nusu mafuta yakapaa kwa bei ambayo haijawahi kushuhudiwa kwa kizazi hiki cha miaka 30 iliyopita!

SHIDA YA MAJI
Maji pia yamekuwa shida, zaidi ya wiki sasa maji hayapatikani...!
Hali ni mbaya tumefika pabaya!!

=============
e5828430-baff-416a-97cb-f794bafcb74a.jpg

3b1419e5-0296-44c0-b0ba-beaf137044b8.jpg

EWURA YAKIFUNGIA KITUO CHA GBP TABORA
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imechukua hatua hiyo kwa kutouza mafuta kwa siku 3 kama kanuni inavyoelekeza wakati kikiwa na akiba ya mafuta kwenye ghala.

Hatua hiyo imechukuliwa siku moja baada ya Mdau wa JamiiForums.com kudai baadhi ya Wafanyabiashara wanaficha Petroli na Dizeli Mkoani hapo wakati wakisubiri #EWURA itangaze bei mpya ambayo kama itakuwa kubwa itawapa faida kubwa.

Taarifa ya EWURA Tabora imeeleza baada ya kukifungia kituo hicho, hatua inayofuata ni kutakiwa kujieleza sababu za kutouza mafuta, baada ya hapo mamlaka itatoa maamuzi kama kukifungulia au kutoa adhabu.
 
Hii nchi ukipata nafasi ya kusepa hakikisha unarudi kuzikwa tu manina, kuna mahali nipo Arusha tena mjini tu maji hakuna hii wiki inaingia ya pili na watu wamekalisha kende zao tu.

Leo asubuhi napokea namba ngeni kuna mpuuzi anajitambulisha msoma mita eti anatishia kunikatia maji while kwa mwezi yanatoka sio zaidi ya siku 10 nilichomjibu kitakuwa kinamzunguka kichwani mpaka saa hii, waheeeed kabisa 🚮🚮🚮
 
Hii nchi ukipata nafasi ya kusepa hakikisha unarudi kuzikwa tu manina, kuna mahali nipo Arusha tena mjini tu maji hakuna hii wiki inaingia ya pili na watu wamekalisha kende zao tu.

Leo asubuhi napokea namba ngeni kuna mpuuzi anajitambulisha msoma mita eti anatishia kunikatia maji while kwa mwezi yanatoka sio zaidi ya siku 10 nilichomjibu kitakuwa kinamzunguka kichwani mpaka saa hii, waheeeed kabisa 🚮🚮🚮
Urudi kuzikwa ili iweje wakati hata huko pia kuna Maeneo ya kuzikia?
 
Tabora ni pa hovyo sana. Nilipata kufanya project moja kwa miezi miwili, ila niliona kama nimekaa mwaka.

Turudi kwenye mada;
Poleni sana. Hii janja janja ya Wafanyabiashara ikomeshwe.

Vumilieni, mpaka kesho jioni mafuta bwerere.
Kwa maana hiyo serikali pia ni ya hovyo hapa Tabora sio!?? Kwahiyo makazini kesho twende by foot!? How serious are we..?!

Hivi imagine watu vyombo vyao vya usafirishaji havina mafuta! Watu wana wagonjwa usiku huu wamezidiwa inamaana wawabebe mikononi kuwawaisha hospital!?

Hivi unajua hivi sasa huko KIZIMKAZI KUNA NINI KINAENDELEA!??
 
Back
Top Bottom