Tabora: EWURA yakamata Malori ya mafuta yaliyofichwa kwenye Kituo cha mafuta cha GBP

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,462
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Kanda ya Magharibi imefanikiwa kukamata malori matatu ya mafuta ya Dizeli na Petrol yaliyokuwa yamefichwa kwenye Kituo kimoja cha mafuta cha GBP Mjini Tabora.

Inadaiwa kuwa yalikuwa kwenye mkakati wa kucheleweshwa wa lengo la kutengeneza mazingira ya kupandisha bei ya mafuta hayo ambayo yalikuwa yanasafirishwa kutoka Jijini Dar-es-Salaam kuelekea mikoa ya Katavi, Tabora na Shinyanga ambayo kwa sasa inatajwa kuwa na upungufu mkubwa wa mafuta.

Akifafanua kilichotokea, Kaimu Meneja wa EWURA Kanda ya Mashariki, Walter Christopher amesema:

“Tumegundua kuwa mafuta haya yalifika zaidi ya saa 24, hali hiyo inaonesha kuna mchezo mchafu unaofanywa na Wafanyabiashara, magari haya yalikuwa na Dizeli na Petroli ambapo kila moja lina uwezo wa kubeba Lita 35,000 hadi 39,000, yalikuwa yanapelekwa Katavi, Nzega na Kahama.

“Kulingana na Sheria kuna adhabu ya faini au kifungo au vyote kwa pamoja, tutaangalia ukubwa wa kosa ambalo limetendeka.


Chanzo: Azam TV
 
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Kanda ya Magharibi imefanikiwa kukamata malori matatu ya mafuta ya Dizeli na Petrol yaliyokuwa yamefichwa kwenye Kituo kimoja cha mafuta cha GBP Mjini Tabora.

Inadaiwa kuwa yalikuwa kwenye mkakati wa kucheleweshwa wa lengo la kutengeneza mazingira ya kupandisha bei ya mafuta hayo ambayo yalikuwa yanasafirishwa kutoka Jijini Dar-es-Salaam kuelekea mikoa ya Katavi, Tabora na Shinyanga ambayo kwa sasa inatajwa kuwa na upungufu mkubwa wa mafuta.

Akifafanua kilichotokea, Kaimu Meneja wa EWURA Kanda ya Mashariki, Walter Christopher amesema:

“Tumegundua kuwa mafuta haya yalifika zaidi ya saa 24, hali hiyo inaonesha kuna mchezo mchafu unaofanywa na Wafanyabiashara, magari haya yalikuwa na Dizeli na Petroli ambapo kila moja lina uwezo wa kubeba Lita 35,000 hadi 39,000, yalikuwa yanapelekwa Katavi, Nzega na Kahama.

“Kulingana na Sheria kuna adhabu ya faini au kifungo au vyote kwa pamoja, tutaangalia ukubwa wa kosa ambalo limetendeka.


Chanzo: Azam TV


Si ya kwao, yamefichwaje sasa?
 
Si ya kwao, yamefichwaje sasa?
Ukishakuwa kwenye soko maana yake umekamata market slice ya eneo husika, maana kuna limit ya idadi ya vituo mafuta ambavyo vinaruhusiwa kisheria katika kila eneo la ukubwa fulani, hivyo hata mtu mwingine mwenye uwezo akiomba kibali cha kufungua kituo cha mafuta atanyimwa maana vimeshajaa kwenye eneo husika, sasa kama kazi imekushinda ni bora ufunge biashara ili mtu mwingine apewe hiyo slot yako, na ukifanya uzembe wa makusudi hiyo inakuwa hujuma na utashtakiwa!
 
Ukishakuwa kwenye soko maana yake umekamata market slice ya eneo husika, maana kuna limit ya idadi ya vituo mafuta ambavyo vinaruhusiwa kisheria katika kila eneo la ukubwa fulani, hivyo hata mtu mwingine mwenye uwezo akiomba kibali cha kufungua kituo cha mafuta atanyimwa maana vimeshajaa kwenye eneo husika, sasa kama kazi imekushinda ni bora ufunge biashara ili mtu mwingine apewe hiyo slot yako, na ukifanya uzembe wa makusudi hiyo inakuwa hujuma na utashtakiwa!


Tanzania hii? Ina uo u perfect? Kila kona kuna kituo
 
Tanzania hii? Ina uo u perfect? Kila kona kuna kituo
Sasa watu si wanahonga.., maana hata kwenye mipango miji, kuna eneo linatengwa maalum kwa ajili ya kituo cha mafuta, sio holela holela. Kwahiyo ukishapewa nafsi maana yake umepewa dhamana ya kuhudumia wananchi, na leseni yako itaeleza wazi kwamba ukihujumu nchi nini kitakupata. Mfano ni kama uchukue mafuta ya transit ambayo hayajalipiwa kodi halafu uanze kuyauza nchi kisha usema mafuta si yangu.., hata kama yako, unapaswa kuuza nje kama ulivyoomba.

Nifafanue zaidi, ukafungua hospitali na ukapewa leseni hiyo ni dhamana kubwa mno umepewa, sasa akaja mgonjwa mwenye hali mbaya kisha ukakataa kumuhudumiankwa sababu zako tu za ajabu ajabu akapata madhara, halafu ukiulizea useme hospitali si yangu.., huo utakuwa sio utetezi. Ingekuwa night club ni sawa kusema hivyo, ila sio kwa sehemu zenye dhamana kama hizo, uneoewa dhamana uhudumie wananchi!!, maana yake umeaminika hadi kuoewa dhamana hiyo!
 
Nina uwakika Mama hajui na wala haangaiki na ishu kama hz. Ila kuteua na kutengua Yuko chap fasta fasta tu.
 
Jana vituo vingi vya kuuzia mafuta barabara ya Arusha moshi vilikuwa haviuzi petroli kwa kifupi viligoma
Ili petroli ikipandishwa wapate faida maradufu
Niwapongeze total na engine kwa kuendelea kutuhudumia
EWURA kanda ya kaskazini nyie endeleeni kulala tu si mishahara inangia.
 
Jana vituo vingi vya kuuzia mafuta barabara ya Arusha moshi vilikuwa haviuzi petroli kwa kifupi viligoma
Ili petroli ikipandishwa wapate faida maradufu
Niwapongeze total na engine kwa kuendelea kutuhudumia
EWURA kanda ya kaskazini nyie endeleeni kulala tu si mishahara inangia.
Si wameshajua dollar imepanda
 
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Kanda ya Magharibi imefanikiwa kukamata malori matatu ya mafuta ya Dizeli na Petrol yaliyokuwa yamefichwa kwenye Kituo kimoja cha mafuta cha GBP Mjini Tabora.

Inadaiwa kuwa yalikuwa kwenye mkakati wa kucheleweshwa wa lengo la kutengeneza mazingira ya kupandisha bei ya mafuta hayo ambayo yalikuwa yanasafirishwa kutoka Jijini Dar-es-Salaam kuelekea mikoa ya Katavi, Tabora na Shinyanga ambayo kwa sasa inatajwa kuwa na upungufu mkubwa wa mafuta.

Akifafanua kilichotokea, Kaimu Meneja wa EWURA Kanda ya Mashariki, Walter Christopher amesema:

“Tumegundua kuwa mafuta haya yalifika zaidi ya saa 24, hali hiyo inaonesha kuna mchezo mchafu unaofanywa na Wafanyabiashara, magari haya yalikuwa na Dizeli na Petroli ambapo kila moja lina uwezo wa kubeba Lita 35,000 hadi 39,000, yalikuwa yanapelekwa Katavi, Nzega na Kahama.

“Kulingana na Sheria kuna adhabu ya faini au kifungo au vyote kwa pamoja, tutaangalia ukubwa wa kosa ambalo limetendeka.


Chanzo: Azam TV
Nilitegemea hili wafanyabiashara siyo wa kuwachekea ni walafi sana wasioridhika na wanyonyaji wakubwa. Jana niliona malori ya mafuta pale Dar Es Salaam madereva wamejificha wametelekeza malori ili wasipakie mafuta, lengo wanasubiri bei mpya itangazwe kesho, inaonekana wamepewa taarifa na wafanyakazi wa EWURA wasio waaminifu kuwa bei ya mafuta itaongezeka. Na kumbuka bei ikongezeka tu saa 6 usiku wanaanza na bei mpya mara moja hasa km imeongezeka.

Hili ndio linawafanya wananchi wengi wanawachukia wafanyabisahara wakubwa kwa jina lingine matajiri kwasababu hawana utu, ni wauuaji, watu wasiojali binadamu wenzao. na hii inawafanya watu wa hali ya chini mpaka leo wanamlilia Magufuli maana Magu naye alikuwa anawachukia akijua tabia zao na kipindi chake walinyooka kweli walijua asingecheka nao, washenzi kabisa. Wafungiwe leseni ya biashara na hayo mafuta yataifishwe na serikali. Hata wale wa jana waliokataa kupakia mafuta na kutelekeza magari wao wakijificha wasipewe tena fursa ya kupakia hayo mafuta badala yake wafukuzwe kabisa pale kituo cha kupakia mafuta na wapigwe na faini.

Mtu mwenye hela hajawahi kumwonea huruma mtu maskini, ni wabinafsi sana. Mtu maskini atalindwa na serikali yake tu na si mwingine. Na kwa hali hii watu maskini wataendelea kuwachukia matajiri, na ndio maana biblia imeandika kuwa " Kwa tajiri kuuona ufalme wa Mungu ni rahisi zaidi kwa ngamia kupenya tundu la sindano" Kwa maana fulani ukiangalia utajiri ni laana zaidi ya umaskini. Nachukia sana tabia ya binadamu kumnyanyasa binadamu mwenzie kwasababu yoyote ile, fikiria dereva boda boda unamnyima mafuta mtu ambaye ili mkono uende kinywani yeye pamoja na wategemezi wake ni anategemea pato la siku, we unamnyima mafuta kusubiri faida kubwa na wakati ulipo huna shida yoyote unamiliki mabilioni. Serikali hii isicheke na matajiri iwe kali sana ibaki kuwa mtetezi wa wanyonge wa nchi hii.
 
Huku Urambo kwa kama wiki mbili hivi sasa kumekuwa na uhaba mkubwa sana wa mafuta, bei ilifika 5000-6000 kwa lita.
 
Waachane wafiche CCM ipo bize kutete mkataba badala ya kuhangaika na wananchi, lita ifike hata 5000 sawa tu
 
Back
Top Bottom