Dah!
Lakini na nyie Vilaza wa Primary mlikuwa na visa sana manake mlikuwa na wivu ingawaje mlikuwa vitoto vidogo!!
Ngoja nianze na huyu "Shetwani" enzi hizo tukiwa Darasa la II !! Sikuwa na mpinzani kwenye zile alama za good (tick) zikiwa zinahitimishwa na maneno VIZURI SANA/VEMA SANA zilizokuwa zinakolezwa kwa Bic Nyekundu!!
Sema na mimi nilikuwa na nyodo, wacha bhana hadi siku moja "litoto lihuni limoja" likaja school na chain stick!!! Yaani mitoto ya Uswahilini ina laana! Yaani kitoto cha miaka 10 (+/-) kinatembea na chain stick na kujifanya eti Bruce Lee... cjui alizipata wapi mtukutu yule!
Wacha atutwange nazo ingawaje tulimchangia ugomvi na sister angu, salama yetu ikawa wapita njia!!!
Basi bhana... kinyume na mazoea yangu ya kupata alama PATA mwanzo hadi mwisho, siku hiyo narudishiwa daftari nakuta limejaa mikasi kuanzia swali la kwanza hadi la mwisho!!
Dogo mmoja, kwa jina la Ismail, KILAZA namba moja darasani si akaanza kulitembeza daftari langu darasa zima kuonesha mikasi yangu!!
Ingawaje jamaa lilikuwa kubwa kwangu lakini sikuvumilia udhalilishaji ule! Yaani Mkali wa Darasa anapata Mikasi mwanzo mwisho halafu unaanza kumchoresha darasani?! Usin'tanie!
Tukazichapa, sana tu... sikumbuki matokeo ya mpambano ule lakini nadhani alinitandika tu!! Kwanza mitoto isiyo na akili darasani ilikuwa inajua kupigana kishenzi; no wonder yalikuwa vilaza!!
Kesi ilipofika kwa Mwalimu, teacher akawa upande wangu!! Unamwadhibu vp "Mtalaamu" hata kama ndie kaanza kurusha ngumi?!
Hayo yakapita, akatokea Mhujumu Mkubwa zaidi enzi nikiwa Darasa la VI au VII... sikumbuki vizuri!!
Kama kawaida chige na Very Good/Excellent... Keep It Up zangu siku moja nikawa nasubiria kwa hamu daftari langu baada ya kupewa zoezi la Hisabati!
Siku madaftari yamerudishwa nika-mind kishenzi kukuta hayajasahishwa wakati nilikuwa nasubiria EXCELLENT CHIGE, KEEP IT UP yangu!! Usicheze na mimi wewe... Jitu ambalo nilijaribishiwa mtihani wa LY wakati nipo Darasa VI na bado nikapasua?
Sijui niliharibikia wapi chige mimi, manake kufika Form IV nikawa naona shule kama Mgonjwa wa Coronavirus!!!
Basi bhana, nikiwa nime-mind madaftari kutosahishwa na hivyo kukosa EXCELLENT CHIGE, baadae kuja kuchunguza lile daftari, AHMADI!!
Kumbe kuna Mhujumu mmoja ali-edit majibu yangu karibu yote! Yaani nilipoandika 6, akaitengeneza kuwa 8, au nilipoandika 1 angeibadilisha kuwa 7 !! Yaani endapo yale madaftari yangesahishwa, ningekuwa nimekosa maswali YOTE na hatimae kuandikiwa PLEASE SEE ME!!!
Just imagine, kitoto cha primary kinafanya hujuma namna hiyo kwa kitoto chenzake... huko aliko huyo jamaa sijui kakubuhu kiasi gani kwa Uhujumu!!
Ni vile tu sina uhakika Mhujumu wangu alikuwa nani ingawaje nahisi alikuwa Mtoto wa Headteacher... headteacher ambae pia alikuwa ndie Mwalimu wa Hisabati!!
Hili toto lilikuwa linajifanya rafiki yangu lakini inaelekea lilikuwa na wivu kwa sababu ingawaje lenyewe lilikuwa toto la Mwalimu Mkuu lakini nilikuwa naliburuza kuanzia Std I hadi VII... pumbavu zake!!
So, kwavile mimi nilikuwa Kipanga, sikuwa na budi ku-share tabia za Vilaza Wenzenu... mlikuwa na wivu kishenzi!!! Tena ilikuwa tukitumwa kuandika ubaoni ndo mlikuwa mnateseka ile mbaya utadhani sie ndio tuliwafanya muwe mnaandika majongoo... shenzi taipu!!!