Jokajeusi
JF-Expert Member
- Jun 1, 2018
- 6,305
- 10,564
Wakuu kwema!
Kwa sasa tumeshakuwa watu wazima, maisha yanaendelea vizuri. Leo nimekumbuka mambo niliyokuwa nayapenda enzi hizo miaka kumi iliyopita nilipokuwa masomoni.
Mimi nilikuwa miongoni mwa vijana vipanga enzi hizo, kuanzia shule ya msingi mpaka namaliza chuo kikuu sijawahi kushuka daraja la kwanza au kupata chini ya wastani wa A. Matokeo yangu ya darasa la saba niliwafurumusha wenzangu kwa kupata maksi 239 kwenye masomo matano yenye jumla ya maksi 250, hii ni kusema nilikosa maksi kumi na moja tuu kupata 100%.
Kidato cha pili nilipata maksi 979 kwenye masomo kumi na moja kwa wastani wa 89.
Kidato cha nne nilipata divisheni one ya 9 kwenye masomo tisa, nikiwa nimepata masomo matano A na manne B
Kidato cha sita ndio ilikuwa bwerere, hapa nilinyuka one ya 4, masomo mawili nikichapa A huku somo moja nikipiga B, na GS nikinyuka A.
Chuo kikuu mambo yalikuwa matamu nilipata First Class GPA YA 4.6
Kwa sisi Vipanga kufaulu ni tabia sio kusoma au juhudi, wakati wengine wanawekeza kusoma ili wafaulu sisi vipanga tunawekeza kwenye tabia ya kufaulu na hivyo kwenye mitihani tunakula bata tuu.
Mambo ambayo sisi Vipanga tulikuwa tunayapenda tukiwa masomoni enzi hizo twasoma!
1. Tunapenda Mitihani
Vipanga wote tulikuwa tunapenda mitihani. Sifa ya kipanga ni kupenda mitihani. Ukiona ulikuwa huipendi mitihani basi jua ulikuwa kilaza. Vipanga tunapenda sana mitihani, nilikuwa naombea kila siku kuwe na mitihani ili nisifundishwe darasani. Kwa kweli nilikuwa sipendi mwalimu aingie darasani aanze kufundisha hasa akiwa na fimbo au atoe notes nyingi tuandike. Vipanga hatupendi kuandika notes. Ukiona ulikuwa na notes nyingi na ulikuwa unaandika notes basi jua wewe bado haupo kundi la vipanga.
Kipindi cha mitihani tunakifurahia sana, nilikuwa nataka kujua akili ya mwalimu wangu ikoje, na akili ya mwalimu ipo kwenye utungaji wa mitihani.
Kwetu mitihani ilikuwa kama fimbo ya kuchapia vilaza na kuwadhalilisha wajione ni wajinga wasio na tofauti na wanyama. Unakuta upo ndani ya mtihani kilaza anakukodolea macho akitaka kupiga chabo.Vipanga tuna miondoko mingi sana,kipindi cha mitihani tunakuwa tunatembea kama wanasayansi wa NASA. Mimi nilikuwa siumwi na macho lakini utaniona nimevaa miwani yenye kioo cheupe nyakati za mitihani hapo ukiongeza na mwendo wangu wa kisayansi basi vilaza walikuwa wanatukodolea macho kweli kwa hofu
2. Tunapenda matokeo
Vipanga wote tukishafanya mitihani tulikuwa tunajua matokeo kabla hayajatoka, tulikuwa tunapenda matokeo yatoke mapema ili tupewe sifa na tuzidi kuogopwa. Ucheleweshaji wa matokeo ni kutufanya vipanga tukose Kiki tuwapo mtaani au shuleni/vyuoni. Kikawaida vipanga hatuangaliaga matokeo pindi yatokapo huwa tunaletewa na vilaza wanaoenda kuangalia kwenye Ubao wa matangazo wa shule. Hiki ni kipindi chetu cha kutamba.
Kwa level ya shule za msingi na sekondari ugawaji wa karatasi za matokeo pia tulikuwa tunaupenda. Vipanga tulikuwa tunapenda mwalimu ataje jina na maksi jambo ambalo vilaza walikuwa wanaona ni adhabu kubwa ni bora wachimbe visiki. Hivi unatajaje maksi za shalobaro wa darasa kapata mbili, alafu unataja mbele ya mademu Waalimu wengine mlikuwa mnawakera vilaza mashalobaro. Au mbabe wa darasa kala zake tatu chini ya mia alafu utaje maksi Kwa nini usipigwe mayai viza.
Mimi karatasi yangu ikiitwa kwanza darasa zima wanajua hapo sio chini ya 80%, mwalimu ataita mimi nitachelewa kuinuka kwenye kiti makusudi ili arudie jina langu mara kadhaa kisha darasa zima litageuka nyuma (nilikuwa backbencher) kunitazama kwa hofu huku wengine wakinitolea macho ya hasira utadhani mimi ndio nimewapa ukilaza. Nitachukua miwani yangu na kuiweka usoni kisha nitaupinda mgongo kidogo na kuunza mwendo wa kitesla, mwendo huu nikitembea hapana shaka mpaka mwalimu anaamini mimi ni kichwa
3. Hatupendi Masahihisho
Hakuna jambo baya ambalo vipanga hatulipendi kama masahihisho ya mitihani. Vilaza hupenda masahihisho kwa vile wamekosa nusu ya mtihani, mtu kapata 20% kwa nini asipende masahihisho. Mimi nimepata 93% hizo maksi nane ndio zinifanye nihangaike na masahihisho? Thubutuu!
4. Tunapenda Mahafali
Vipanga tunapenda mahafali, na kwa bahati nzuri ukiwa kipanga OG lazima ualikwe kwenye matukio muhimu kama mahafali ya wanafunzi wengine hata kama sio darasa lako. Kipanga yoyote yule lazima awepo kwenye mahafali hata kama sio yake, hii ni kutokana na ratiba ya zawadi kwa vipanga wa shule. Ufikapo muda wa zawadi lazima jina lako litajwe kwa vyovyote vile. Kama sio zawadi ya kushika nafasi ya kwanza basi zawadi ya kuongoza somo la mathematics, Fizikia, kemia na Biolojia. kuna mwendo wa kuchukulia zawadi pia, hapa kwenye mchomekeo lazima uvae kidogo mayeno kwa mbali kama ishara ya kushindikana kwenye masomo. Wale wavaa milegezo tulikuwa tunawaona akili yao ipo chini kabisa ya matako yao.
Pia siku ya mahafali tunakuwaga na suruali zetu spesheli kwa tukio la mahafali. Ni lazima suruali iwe na marinda ili tuweze kuvaa mayeno, unajua modo haipendezi mayeno ndio maana siku ya mahafali vipanga wote duniani tunavaa duruali zenye marinda kusudi tupandishe yeno kwa mbali kama ishara akili zetu zinaenda juu sio chini kama wavaa milegezo.
5. Tunapenda Usaili/ Interview
Vipanga tunapenda kufanyiwa usaili ndipo tupate kazi au jambo lolote. Hatupendi kazi za bure bure, Mimi nilikuwa napenda usaili ili niweze kuwapima wale wanataka kuniajiri, kwenye usaili licha ya kuwa mimi ndio muombaji wa kazi lakini wanaonifanyia usaili wanajikuta kwenye wakati mgumu sana kwani wakimaliza kunipima nami nitakuwa nimemaliza kuwapima. Vipanga tunapenda usaili hasa mimi, kwa sababu pale HR anapochukua CV na vyeti vyangu na kuvipitia nikiwa namtazama lazima awe na hofu kubwa kwani HR wengi zaidi ya 99% hawajawahi kunikaribia ufaulu nilioupata. Pia hakuna swali ambalo HR angeniuliza ambalo nitashindwa kulijibu.
Nilishangaa humu wakimshambulia YEHODAYA alipokuwa akiwaponda wasomi wa masuala ya fedha alafu hawajui Noti ya elfu kumi inamnyama gani, ndio shida ya vilaza,, hilo ni swali dogo sana, huwezi shindwa swali la kitoto kama hilo.
Niliposoma post ya YEHODAYA, Pembeni yangu alikuwepo mke wangu, yeye ni Daktari Muhimbili, nikamuuliza kwenye sindano ya kumchomea mgonjwa, zipo mililita ngapi? Akabaki anashangaa wakati kila siku anashika sindano. Huo ni ukilaza, basi tulisemana tukitaniana huku naye akinitafutia maswali ili nami aniite kilaza lakini alikosa kwani yote aliyouliza nilijibu.
Hayo ndio mambo Vipanga tuliyokuwa tunayapenda enzi tukiwa masomoni.
Jokajeusi
Kwa sasa tumeshakuwa watu wazima, maisha yanaendelea vizuri. Leo nimekumbuka mambo niliyokuwa nayapenda enzi hizo miaka kumi iliyopita nilipokuwa masomoni.
Mimi nilikuwa miongoni mwa vijana vipanga enzi hizo, kuanzia shule ya msingi mpaka namaliza chuo kikuu sijawahi kushuka daraja la kwanza au kupata chini ya wastani wa A. Matokeo yangu ya darasa la saba niliwafurumusha wenzangu kwa kupata maksi 239 kwenye masomo matano yenye jumla ya maksi 250, hii ni kusema nilikosa maksi kumi na moja tuu kupata 100%.
Kidato cha pili nilipata maksi 979 kwenye masomo kumi na moja kwa wastani wa 89.
Kidato cha nne nilipata divisheni one ya 9 kwenye masomo tisa, nikiwa nimepata masomo matano A na manne B
Kidato cha sita ndio ilikuwa bwerere, hapa nilinyuka one ya 4, masomo mawili nikichapa A huku somo moja nikipiga B, na GS nikinyuka A.
Chuo kikuu mambo yalikuwa matamu nilipata First Class GPA YA 4.6
Kwa sisi Vipanga kufaulu ni tabia sio kusoma au juhudi, wakati wengine wanawekeza kusoma ili wafaulu sisi vipanga tunawekeza kwenye tabia ya kufaulu na hivyo kwenye mitihani tunakula bata tuu.
Mambo ambayo sisi Vipanga tulikuwa tunayapenda tukiwa masomoni enzi hizo twasoma!
1. Tunapenda Mitihani
Vipanga wote tulikuwa tunapenda mitihani. Sifa ya kipanga ni kupenda mitihani. Ukiona ulikuwa huipendi mitihani basi jua ulikuwa kilaza. Vipanga tunapenda sana mitihani, nilikuwa naombea kila siku kuwe na mitihani ili nisifundishwe darasani. Kwa kweli nilikuwa sipendi mwalimu aingie darasani aanze kufundisha hasa akiwa na fimbo au atoe notes nyingi tuandike. Vipanga hatupendi kuandika notes. Ukiona ulikuwa na notes nyingi na ulikuwa unaandika notes basi jua wewe bado haupo kundi la vipanga.
Kipindi cha mitihani tunakifurahia sana, nilikuwa nataka kujua akili ya mwalimu wangu ikoje, na akili ya mwalimu ipo kwenye utungaji wa mitihani.
Kwetu mitihani ilikuwa kama fimbo ya kuchapia vilaza na kuwadhalilisha wajione ni wajinga wasio na tofauti na wanyama. Unakuta upo ndani ya mtihani kilaza anakukodolea macho akitaka kupiga chabo.Vipanga tuna miondoko mingi sana,kipindi cha mitihani tunakuwa tunatembea kama wanasayansi wa NASA. Mimi nilikuwa siumwi na macho lakini utaniona nimevaa miwani yenye kioo cheupe nyakati za mitihani hapo ukiongeza na mwendo wangu wa kisayansi basi vilaza walikuwa wanatukodolea macho kweli kwa hofu
2. Tunapenda matokeo
Vipanga wote tukishafanya mitihani tulikuwa tunajua matokeo kabla hayajatoka, tulikuwa tunapenda matokeo yatoke mapema ili tupewe sifa na tuzidi kuogopwa. Ucheleweshaji wa matokeo ni kutufanya vipanga tukose Kiki tuwapo mtaani au shuleni/vyuoni. Kikawaida vipanga hatuangaliaga matokeo pindi yatokapo huwa tunaletewa na vilaza wanaoenda kuangalia kwenye Ubao wa matangazo wa shule. Hiki ni kipindi chetu cha kutamba.
Kwa level ya shule za msingi na sekondari ugawaji wa karatasi za matokeo pia tulikuwa tunaupenda. Vipanga tulikuwa tunapenda mwalimu ataje jina na maksi jambo ambalo vilaza walikuwa wanaona ni adhabu kubwa ni bora wachimbe visiki. Hivi unatajaje maksi za shalobaro wa darasa kapata mbili, alafu unataja mbele ya mademu Waalimu wengine mlikuwa mnawakera vilaza mashalobaro. Au mbabe wa darasa kala zake tatu chini ya mia alafu utaje maksi Kwa nini usipigwe mayai viza.
Mimi karatasi yangu ikiitwa kwanza darasa zima wanajua hapo sio chini ya 80%, mwalimu ataita mimi nitachelewa kuinuka kwenye kiti makusudi ili arudie jina langu mara kadhaa kisha darasa zima litageuka nyuma (nilikuwa backbencher) kunitazama kwa hofu huku wengine wakinitolea macho ya hasira utadhani mimi ndio nimewapa ukilaza. Nitachukua miwani yangu na kuiweka usoni kisha nitaupinda mgongo kidogo na kuunza mwendo wa kitesla, mwendo huu nikitembea hapana shaka mpaka mwalimu anaamini mimi ni kichwa
3. Hatupendi Masahihisho
Hakuna jambo baya ambalo vipanga hatulipendi kama masahihisho ya mitihani. Vilaza hupenda masahihisho kwa vile wamekosa nusu ya mtihani, mtu kapata 20% kwa nini asipende masahihisho. Mimi nimepata 93% hizo maksi nane ndio zinifanye nihangaike na masahihisho? Thubutuu!
4. Tunapenda Mahafali
Vipanga tunapenda mahafali, na kwa bahati nzuri ukiwa kipanga OG lazima ualikwe kwenye matukio muhimu kama mahafali ya wanafunzi wengine hata kama sio darasa lako. Kipanga yoyote yule lazima awepo kwenye mahafali hata kama sio yake, hii ni kutokana na ratiba ya zawadi kwa vipanga wa shule. Ufikapo muda wa zawadi lazima jina lako litajwe kwa vyovyote vile. Kama sio zawadi ya kushika nafasi ya kwanza basi zawadi ya kuongoza somo la mathematics, Fizikia, kemia na Biolojia. kuna mwendo wa kuchukulia zawadi pia, hapa kwenye mchomekeo lazima uvae kidogo mayeno kwa mbali kama ishara ya kushindikana kwenye masomo. Wale wavaa milegezo tulikuwa tunawaona akili yao ipo chini kabisa ya matako yao.
Pia siku ya mahafali tunakuwaga na suruali zetu spesheli kwa tukio la mahafali. Ni lazima suruali iwe na marinda ili tuweze kuvaa mayeno, unajua modo haipendezi mayeno ndio maana siku ya mahafali vipanga wote duniani tunavaa duruali zenye marinda kusudi tupandishe yeno kwa mbali kama ishara akili zetu zinaenda juu sio chini kama wavaa milegezo.
5. Tunapenda Usaili/ Interview
Vipanga tunapenda kufanyiwa usaili ndipo tupate kazi au jambo lolote. Hatupendi kazi za bure bure, Mimi nilikuwa napenda usaili ili niweze kuwapima wale wanataka kuniajiri, kwenye usaili licha ya kuwa mimi ndio muombaji wa kazi lakini wanaonifanyia usaili wanajikuta kwenye wakati mgumu sana kwani wakimaliza kunipima nami nitakuwa nimemaliza kuwapima. Vipanga tunapenda usaili hasa mimi, kwa sababu pale HR anapochukua CV na vyeti vyangu na kuvipitia nikiwa namtazama lazima awe na hofu kubwa kwani HR wengi zaidi ya 99% hawajawahi kunikaribia ufaulu nilioupata. Pia hakuna swali ambalo HR angeniuliza ambalo nitashindwa kulijibu.
Nilishangaa humu wakimshambulia YEHODAYA alipokuwa akiwaponda wasomi wa masuala ya fedha alafu hawajui Noti ya elfu kumi inamnyama gani, ndio shida ya vilaza,, hilo ni swali dogo sana, huwezi shindwa swali la kitoto kama hilo.
Niliposoma post ya YEHODAYA, Pembeni yangu alikuwepo mke wangu, yeye ni Daktari Muhimbili, nikamuuliza kwenye sindano ya kumchomea mgonjwa, zipo mililita ngapi? Akabaki anashangaa wakati kila siku anashika sindano. Huo ni ukilaza, basi tulisemana tukitaniana huku naye akinitafutia maswali ili nami aniite kilaza lakini alikosa kwani yote aliyouliza nilijibu.
Hayo ndio mambo Vipanga tuliyokuwa tunayapenda enzi tukiwa masomoni.
Jokajeusi