Tabia ya mtu haibadiliki

Tabia ya mtu haibadiliki

In the final analysis JPM atahukumiwa kwa jinsi alivyoshughulikia suala la covid 19 na si kwa ujenzi wa flyovers, SGR, bwawa la Steigler’s Gorge au ufufuaji wa ATCL na vita dhidi ya ufisadi kwa uchache.

May the fates be kind unto Tanzania and her people.
 
The end justifies the means.

Amefanikiwa kwenye mengi na huwa anayaongea sana kwenye hotuba zake.

Jaribu kurejea.
Kwamba wananchi hawawezi kuona mafanikio yake mpaka aseme yeye mwenyewe ?
 
Kiukweli binafsi sijawahi kumkubali huyu kiongozi hata kidogo. Hafuati kanuni, taratibu na sheria ya chochote.

Hajali watumishi, hajawapandisha madaraja wala mishahara Miaka mitano sasa.

Anaona fahari kutumbua watumishi hata kwa vimakosa kidogo. Hana utu hata kidogo.
Kwa hili la corona tutadharaulika na Dunia nzima.
Sio tutadharaulika tumeshadharaulika tayari sasa hivi ni aibu kujiita mtanzania ...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwamba wananchi hawawezi kuona mafanikio yake mpaka aseme yeye mwenyewe ?
Wananchi wanayaona mafanikio ila wachache hawayaoni,(cdm)huwa anayasema/kuwakumbusha wayaone sio kupiga kelele tu
 
Kila siku nawaambia, hii tabia yetu ya kutafuta Rais wetu kwa ushabiki wa kisiasa sasa tunajuta!

Rais wa nchi yetu halisi na wote tunajua alikuwa Mh. Membe.. ugomvi wake na Lowassa ndiyo tumeingia kwa shino hili.

Afu eti Mh. Membe wamemtimua.....mijitu ya madaraka bana....

Membe wana CCM tunakutakaaa!! CCM ni chama cha amani sisi si magaidi....

CCM chama chetu cha upendo... wavamizi wajiandae kusepa 2020; Membee oyeeeeee......
 
Huku kwenye ujenzi kaja na force account ambayo imefeli vibaya sana,

Kanunua ndege cash kwa mbwembwe lakini anashinndwa kuwanulia wanyonge barakoa na sanitizer
Hakuna kitu inanichosha Kama barabara ya njia sita Dar chalinze,wenzake waliweka mipango mizuri na WB kujenga barabara hiyo.alivyopata urais akadhani kila kitu ni kutumia nguvu tu na mabavu,sijui alikuwa na ugomvi na mtu pale kimara? Bwana wewe acha nyumba zibomolewa bwana,WB walivyomwambia kwa ubomoaji huo bila fidia pesa hapa hakuna.Kaja kimara mwisho kufanya igizo la kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa barabara hiyo kwa fedha za ndani Kama jibu kwa WB kuwa pesa anayo. Unajua nini kinaendelea 3 years tangu kuwekwa jiwe la msingi? Aise Kuna watu hawana aibu kabisa
 
Wananchi wanayaona mafanikio ila wachache hawayaoni,(cdm)huwa anayasema/kuwakumbusha wayaone sio kupiga kelele tu
Mafanikio yapi mkuu,ya kujenga barabara ya Kimara kibaha kilometa 17 kwa miaka mitano au?
 
Kalamu1,
Alipokuwepo Jakaya Kikwete watu wakawa wanajipigia fedha,na wengine kubeba kwenye sandarusi mkawa mnasema rais gani huyu mpole anacheka cheka tu.

Amekuja huyu mzee wa kazi mnaanza maneno mengine. Rais lazima awe mkali na lazima aogopwe ili mambo yaende. Sasa ile Petrol station kama ilikuwa kwenye hifadhi ya barabara we ulitaka iachwe? I am not a politician but i have common sense.
Jakaya ilikuwa billion .300 jiwe kaiba trillion 2.4 alafu poa tu bunge dhaifu
 
Kalamu1,
Alipokuwepo Jakaya Kikwete watu wakawa wanajipigia fedha,na wengine kubeba kwenye sandarusi mkawa mnasema rais gani huyu mpole anacheka cheka tu.

Amekuja huyu mzee wa kazi mnaanza maneno mengine. Rais lazima awe mkali na lazima aogopwe ili mambo yaende. Sasa ile Petrol station kama ilikuwa kwenye hifadhi ya barabara we ulitaka iachwe? I am not a politician but i have common sense.
Jakaya ilikuwa billion .300 jiwe kaiba trillion 2.4 alafu poa tu bunge dhaifu
 
Mimi nakumbuka na sitasahau umeme (TANESCO). Sijui kwanini walikuwa wanakatakata na kutusababishia kutumia majenereta. Mpaka Wakurugenzi wakuu (km Mrema) alimgomea asikate umeme

Leo umeme chee, friji haiozeshi tena JF siikosi kama si mvua naweza kwenda popote TZ na Vits
Hayo mabaya nawaachieni lkn angekuwa Rais mwingine sijui matajiri wangetuweka wapi?
Teh...mafisadi walishaiweka nchi mfukoni....yanapiga hela halafu umeme hauonekani...
 
Mafanikio yapi mkuu,ya kujenga barabara ya Kimara kibaha kilometa 17 kwa miaka mitano au?
Utayaonaje wakati umeshajitoa ufahamu una yakana sababu tu ya chuki yako umeziba macho na masikio
 
Sasa mtu amejenga ndani ya hifadhi ya barabara alafu unataka alipwe? Nenda kasome Road Act,2007. Section 1 mpaka mwisho.
Mkuu unajua sheria zipo kwa ajiri ya watu au?unadhani why sheria huwa zinabadirishwa? Serikali ni Mali ya watanzania na IPO kwa ajiri ya kuwahudumia,ni bahati mbaya tuna rais ambaye anadhani serikali ni chombo cha kuwakomoa watanzania na pesa za serikali hazitokani na watanzania
 
Uzembe tu unao wasumbua hasa kizazi hiki cha Chips mayai, na Magufuli hataki huo Ujinga na ndiyo maana wao wanauita ni mikwaruzano kwenye Miradi yake,

Uzembe wa miradi iliyokuwa inapaswa iishe ndani miezi mitatu inachukua miaka tatu,?

Kati ya ya kandarasi anayeshindwa kumaliza kandarasi yake na anayekuja kumuuliza Kwa nini uko nje ya mkataba, hivi ni Nani mkorofi Kati Yao kama sio mkandarasi
Amfukuze na Estim hawezi akajenga barabara ya 17 kms for 4 years na Kama shida ni pesa basi nae ajitadhimini Kama anatosha
 
Back
Top Bottom