Yes,hili ndio nilitaka kulisikia kutoka kwako,..kuna tofauti ya kuomba/kukopa hela na vizinga,..mm mumu frankly mwanaume wangu nimuone kabisaa ana uhitaji wa msaada fulani na mm uwezo wa kumuwezesha ninao haki nampa tena wala sikukopeshi wala sikusimangi tena moyoni nitajawa na amani na furaha kwasababu nime play nafasi yangu kwa mpenzi/mchumba/mume
Lakini kuna hawa vijana kwanza anakuwa na wanawake wengiii kwa ajili ya kubom hela yaani hana mapenzi ya kweli,mnafiki muongo muongo yaani unamuona tuu huyu tapeli,.hivi kweli mmekutana leo kesho kutwa anakuambia muazime laki 2 ya kodi ya nyumba,lazima ujiulize hivi tusingekutana ina maana kodi asingelipaa au?....mwanaume kukosa sio ajabu maana nayy ni binadamu na anahaki ya kusaidiwa inapobidi, lakini kuna wanaume basi tuu yaani kama wanawashwa tena asikuone uko busy na shughuli zako utaombwa mpaka vocha ya jelo hii haipendezi ukizingatia tupo wanawake ambao hatujui kuomba hata hela ya soda kwahiyo ukikutana na hizi sampuli lazima roho ikuume.