Taarifa zako binafsi zikitumiwa vibaya au kinyume na makubaliano peleka malalamiko kwa Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi

Rare Sapphire

JF-Expert Member
Jul 24, 2021
576
1,626
Wakuu,

Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi imeanza kufanya kazi toka Mei 1, mwaka huu 2023 na Tume ipo kuhakikisha huumizwi na watu au taasisi wanaotaka kutumia vibaya taarifa zako kwa maslahi yao.

Ikiwa una malalamiko ya taarifa zako kutumiwa vibaya mfano mtu katumia picha zako kwenye matangazo wakati hilo halikuwa lengo, mtu kavujisha picha au jumbe ili akukomoe unatakiwa kupeleka malalamiko yako katika Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi.

Kazi ya Tume hii ni kupokea, kuchunguza na kushungulikia malalamiko kuhusu Madai ya Ukiukwaji wa Ulinzi wa Taarifa binafsi na Faragha za watu.

Pia ili mtu au kampuni iwe na ruhusa ya kukusanya au kuchakata taarifa binafsi inatakiwa kupata usajili kutoka katika tume hii, ambayo inaongozwa na Mkurugenzi anayeteuliwa na Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania. Usajili huo ni wa miaka mitano, baada ya kipindi hicho kuisha Muhusika anatakiwa kuhuisha Usajili wake kama Kanuni zinavyoelekeza.

Swali ni je, tume hii ipo wapi mpaka sasa wakati sheria imeshanza kutumika?
 
Kuna TUME nyingi naziona hazina faida.

Hawa Jamaa wamekaa kimya wakati TCRA wakiachilia tangazo la Kuzuia VPN zisitumike mpka wao wazifahamu na kunyakua IP adress za wahusika.

Hii TUME imekaa kimya.
 
Je, wale walioiba vyeti vya watu na wanatumia majina hayo hadi leo wakati sio yao, maana wanatumia majina ya watu sbb waliwaibia vyeti na wako watu wanajulikana wengi tu nao inafaa waripotiwe.
 
Kuna TUME nyingi naziona hazina faida.

Hawa Jamaa wamekaa kimya wakati TCRA wakiachilia tangazo la Kuzuia VPN zisitumike mpka wao wazifahamu na kunyakua IP adress za wahusika.

Hii TUME imekaa kimya.
Tume hii ndio ina oversee mambo yote kuhusu ulinzi wa taarifa binafsi, ila kwenye bodi watu wanaongeza maokoto tu mfukoni
 
Kuna watu wanajihami mapema hapa!! Wanajua walishayatapua, kwa hiyo wamnawatishia watu wanaojua mambo yao wasije wakayaweka hadharani!!
 
Kuna watu wanajihami mapema hapa!! Wanajua walishayatapua, kwa hiyo wamnawatishia watu wanaojua mambo yao wasije wakayaweka hadharani!!
Kwanini uweke mambo binafsi ya watu hadharani? Kama hayana athari yoyote kwa taifa au kikundi cha watu unayatoa hadharani kwa madhumuni gani?
 
Kwa takwimu kama hizi ambazo zimekutwa gengeni zikifungiwa bidhaa nani anatakiwa kuchukuliwa hatua?
 
Back
Top Bottom