Mkandara,
mimi nimeishi marekani kwa muda sana na ninafanya kazi na wato toka India kibao ambao ni waislam na wahindu huku pia nikiwa na marafiki ambao ni wayahudi na wakristo.
Nakuhakikishia kuwa wengi hapa wanakubali kuwa waislam wanapata treatment nzuri sana hapa marekani mara nyingi zaidi ya watu wa dini zingine ambao wanajaribu kushika dini zao kwenye nchi kama Pakistani na kadhalika.
Pamoja na haya yote, mimi sioni kama ni suala langu kuanza kushikia bango waislam walio Tanzania au Marekani just because wale walio arabuni wanachukia dini zingine!
The same way sidhani kama ni suala langu kushikia bango kila mkristo kwa vile eti Bush na serikali ya marekani wanaeneza ukoloni duniani. Mimi nimeanza kudili na watanzania wenzangu ambao wanahusika na kueneza huu ukoloni wa marekani badala ya kuhangaika na label za ukristo au uislam.
Marekani inalaumiwa sana kwa kufilisi nchi za central na south Amerika. Wakati wa Reagan, marekani ilivamia sana nchi za central amerika ambazo raia zake wengi ni wakristo, je kuna sababu sasa kusema kuwa marekani au Reagan alikuwa na chuki na wakristo?
Nadhani ni vizuri kuangalia utu wa mtu kabla ya dini yake maana utu wa mtu unaanza kabla ya dini. wote tunazaliwa kama binadamu kisha tunachagua kama tuwe waislam au wakristo au wasio na imani.
Asante kwa shule yako mkuu!
Suala kama utu wa mtu kabla ya dini yao. vipi unawahukumu waislam wa Tanzania kwa kuandamana badala ya kutiza utu wa maelfu ya Wairaq wanaoteseka? ni Mungu gani unayemuabudu anayekufundisha kutokuwa na huruma na viumbe wenzio? Bwana Yesu (Issa bin Maryam) ninayemjua mimi hakuwa na roho mbaya kama zenu.