Symbion Power acquires DOWANS Power plant

Symbion Power acquires DOWANS Power plant

At the end I think while this shows a direct avoidance of the corrupt political elite (TAKUKURU calls it the "corrupt bureaucratic elite") and i believe it should be encouraged. Wale wanaofikiria kuwa kwa kufanya hivi tunatishia uhuru wetu wanashindwa kutambua mara moja chini ya hawa corrupt ruling elite uhuru wetu tayari umeshawekwa matatani.
 
Hivi IPTL mkataba unaisha lini?....watanzania hawahitaji thermal generated power,period.Ili umeme usambae hadi vijijini,inabidi serikali ikarabati mtera na kuanza kushughulikia Stieglers gorge au at least iongeze kasi kuifufua kiwira!! haya mambo ya symbiosis,GE and other bull*** is more beneficial to them,average tanzanian can't pay for thermal generated electricity!! hii ni kwa ajili yao tu(wawekezaji).

MY VIEW
MCA should be used to improve healthcare in Tanzania,cos we are really behind in this sector.
 
Mhhh hiii MCA ni kama wizara ya ya fedha ya marekani ndani ya wizara ya fedha ya Tanzania. Kwa kuwa sisi tumeshindwa na kila kitu kwetu ni siasa bora wafanye tu. Yaani watu wanfisadi hata maendeleo ya watu wao.

Fedha za MCA sidhani hata Kitibu mkuu kama anaweza kuzifanya realocaton ya kama wanavyochezeaga hela za miradi mingine .

Maana kwa miezi kama hii ya mwisho wa mwaka wa fedha Unakuta kuna wizara na idara zinahangaika kutafuna fedha just for the sake ya kuzitafuna. kwa kuwa fungu lipo lina hela hata kama sio matumizi ya muhimu na ya tija.

BInafsi sioni Ubaya kwa GE kuja na wachote hizo pesa. yaani kwa jina lao tu ni ama google na internet.
 
Ni kweli America ina agenda ya Uchumi na Security lakini kuna ubaya gani kama inatunufaisha?. Marekani ipo Korea ya Kusini, Japan, German , na nchi nyingi za Kiaarabu. Mimi sijaona unyonyaji wowote hapa bali nimeona nchi hizi zina maendeleo na wananchi wanaendelea. Hivyo agenda ya biashara ni nzuri na ndugu zangu. Kuna watu wengine wanawachukia wamarekani kwasabu za vita na nguvu lakini kama ni rafiki yetu tuendelee na maendeleo. Marekani wameshaona hii nchi ikienda vibaya, Rwanda, Burundi, Congo, Kenya Uganda hata Sudan mambo yanaweza kuharibika. Kenya inategemea Tanzania kwenye mbuga na soko, Uganda inategemea tanzania na kenya kwenye bandari, somalia inategemea kenya, Sudan ya kusini inategemea Uganda, Rwanda na Burundi zinategemea nchi zote tatu, Congo inategemea Tanzania na Zambia inategemea Tanzania kwenye bandari hivyo Tanzania ni nchi muhimu sana kwa security na kupitisha nishati kwenda nje.
 
MY VIEW
MCA should be used to improve healthcare in Tanzania,cos we are really behind in this sector.

Kobello, my friend, tatizo liko toka mwanzo tulipokubali kuwa sehemu ya hii MCA. Wengi walifikiria kuwa MCA ina lengo la kutupa sisi uwezo na kujenga uwezo wetu wa ndani la hasha. Masharti ya MCA kama yalivyo masharti ya miradi mingine mingi tu ya Wamarekani ni kuwa fedha za walipa kodi wao ni lazima zinufaishe Marekani. Sasa mimi siwezi kuwalaumu kwa hili. Fikiria dola milioni 700 zinaweza kufanya nini Marekani? Kweli tulifikiria Wamarekani watatoa hizo milioni 700 kwa Tanzania bure tu? Kwa undugu gani?

Wamarekani ni nchi yenye kufuata mfumo wa mitaji (capitalism) na hivyo misaada kwao ni uwekezaji kwani wanategemea itakuwa na manufaa zaidi (high return). Kwa hiyo, wanaposema kuwa wanatoa milioni 700 wameweka na vipengele kabisa kuwa baadhi ya miradi ambayo itafadhiliwa na fedha hizo Wamarekani wawe ne the right of first refusal. Hivyo, sisi tunataka Wamarekani watusaidie kwenye umeme wanasema "ndio tutawasaidia" na tuko tayari kulipigia milioni 50 dola; lakini tutawasaidia kutafuta kampuni ya Kimarekani ambayo itafanya kazi hii. Hivyo, wanaenda wanampata GE anakubali kufanya kazi Tanzania - ambako anajua angekuja kwa njia ya kawaida ingekuwa kasheshe yenye rushwa kibao juu na ambako anajua labda hawezi kushinda competition ya Wachina, Wajapani na Wajerumani. Anapewa mtaji hizo milioni 50 kiasi kikubwa kinarudi Marekani na kutengeneza ajira zaidi n.k Watatumia kama dola milioni 1 hivi kutupatia mafunzo ya hapa na pale huko huko kwao!

Hatuwezi kuwalaumu. Kama tungekuwa tunataka kweli iwe ni misaada ya kutunufaisha na sisi watawala wetu wangesema mapema kwenye masharti kuwa kwa kila dola moja inayopelekwa Marekani dola nyingine moja ibakie Tanzania. Lakini hatuna sera ya misaada ya kigeni Tanzania hivyo tunakuwa katika huruma ya wale wanaotoa misaada na hatuwezi kuwalaumu. Kwa wananchi wa kawaida kwa kweli hiyo haiwajalishi maana kama serikali yao imeshindwa kutatua tatizo la nishati na Wamarekani kwa kutumia fedha zao, na makampuni yao wanakuja kusaidia why not?
 
USA kama kweli walikuwa na nia njema kwa nini wanajihusisha na Dowans? Hatudanganyiki wao sio wajomba zetu kama wangekuwa na nia nzuri wangeimarisha TANESCO sio mafisadi kwa mbinu zile zile kama za BAE, Richmond etc. Ipo siku tutawaonyesha nini tunaweza kufanya hasa kwa hawa vimburu wanaoiba kila kukicha kutoka kwa walala hoi wanaolipa kodi.
 
Ndugu zangu mimi ni lazima nieleze hata mimi nilikuwa na hasira za mikataba ya umeme lakini kuendeleza hasira hazitasaidia kujenga nchi yetu.

Kuhusu gas na jet fuel: Machine zinaweza kutumia Jet fuel au gas asilia na gas asilia ni bei rahisi kuliko jet fuel na ndiyo maana bei ni tofauti. Wametoa rate zote kwasababu kuna wakati songas wanakuwa na matatizo ya kuleta gas hivyo watatumia jet fuel-mafuta ya ndege kwa kuendesha hizo machine.

Kuhusu gharama mimi nimesema mteja kama wewe na mimi kwa hapa marekani record zinaonyesha walilipa wastani wa USD 12 Cents kwa Kwh. Mimi hapa Texas nalipa USD 10 Cents na nimesaini mkataba wa mwaka mmoja. Hivyo hiyo ni bei ya mteja na kama wananchi na sio Tanesco watalipa chini ya USD 12 Cents haitakuwa mbaya sana. Hawa jamaa wametoa rate kwasababu Tanesco wakitoa rate ya juu sana kwa watu ijulikane wazi kwamba si wenyewe waliotoa hiyo rate ya juu bali ni Tenesco. Kwa ufupi wame ji cover.
Ndugu zangu nawaomba msilewe matatizo badala yake tulewe mawazo. Tunatati mawazo ya kusaidia nchi


Mkuu umeongea kitu cha ukweli!
Lakini mazingira ya utendaji wa Tanesco, wizara na kampuni husika,
Sio vizuri sana kushabikia kabla ya kipindi ambapo hata yaliyonyuma ya pazia hayajafunuka.
Sawa pamoja na yote unayoyasema, ila inabidi ukumbuke huku bei ya umeme ilishapanda sana kwa 33%
Hivyo hata kama iweje hiyo nafuu haiji tena kwa mlaji wa kawaida ukizingatia hatuna historia ya bei kushuka!
Binafsi hili suala la hawa wamarekani bado nalipimia kwanza, naona maswali ni mengi mno
,
"usimwamini shetani aliyekuja na rozari kabla hujampa maji ya baraka"
 
At the end I think while this shows a direct avoidance of the corrupt political elite (TAKUKURU calls it the "corrupt bureaucratic elite") and i believe it should be encouraged. Wale wanaofikiria kuwa kwa kufanya hivi tunatishia uhuru wetu wanashindwa kutambua mara moja chini ya hawa corrupt ruling elite uhuru wetu tayari umeshawekwa matatani.

Thats why nafikiri hata UK court imeamua kutopeleka zile funds za BEA treasury na watanzania tuko behind na hii strategy. Tunachotakiwa sasa wote watanzania kwa ushirikiano mapambano mengine tunatakiwa tufanye kila njia ya kuwa innovative kutafuta projects na kuzipeleka kwenye hizi institutions na hasa investors mbalimbali ili tujenge economy bila kutumia treasure ya mkulo na jk. We can achieve all these, why bother na usanii.
 
Ndugu zangu mimi ni lazima nieleze hata mimi nilikuwa na hasira za mikataba ya umeme lakini kuendeleza hasira hazitasaidia kujenga nchi yetu.

Kuhusu gas na jet fuel: Machine zinaweza kutumia Jet fuel au gas asilia na gas asilia ni bei rahisi kuliko jet fuel na ndiyo maana bei ni tofauti. Wametoa rate zote kwasababu kuna wakati songas wanakuwa na matatizo ya kuleta gas hivyo watatumia jet fuel-mafuta ya ndege kwa kuendesha hizo machine.

Kuhusu gharama mimi nimesema mteja kama wewe na mimi kwa hapa marekani record zinaonyesha walilipa wastani wa USD 12 Cents kwa Kwh. Mimi hapa Texas nalipa USD 10 Cents na nimesaini mkataba wa mwaka mmoja. Hivyo hiyo ni bei ya mteja na kama wananchi na sio Tanesco watalipa chini ya USD 12 Cents haitakuwa mbaya sana. Hawa jamaa wametoa rate kwasababu Tanesco wakitoa rate ya juu sana kwa watu ijulikane wazi kwamba si wenyewe waliotoa hiyo rate ya juu bali ni Tenesco. Kwa ufupi wame ji cover.
Ndugu zangu nawaomba msilewe matatizo badala yake tulewe mawazo. Tunatati mawazo ya kusaidia nchi


Mkuu naona utusaidie kitu ambacho labda kinaweza kuonekana ni kidogo sana. Ututajie wamiliki wa Symbion na utuwekee CV zao. Na pia utueleze walianzaje mchakato wa kununua mitambo ya Dowans. Nani kawauzia na kwa bei gani!!

Mwenzio naogopa kuwa agent of the devil..Ukinisaidia hayo nitaku-join!
 
mistari ile ile wanatubadilishia bit tu
hizi sasa ni sharau jamani
 
Hatuwezi kuwalaumu. Kama tungekuwa tunataka kweli iwe ni misaada ya kutunufaisha na sisi watawala wetu wangesema mapema kwenye masharti kuwa kwa kila dola moja inayopelekwa Marekani dola nyingine moja ibakie Tanzania. Lakini hatuna sera ya misaada ya kigeni Tanzania hivyo tunakuwa katika huruma ya wale wanaotoa misaada na hatuwezi kuwalaumu. Kwa wananchi wa kawaida kwa kweli hiyo haiwajalishi maana kama serikali yao imeshindwa kutatua tatizo la nishati na Wamarekani kwa kutumia fedha zao, na makampuni yao wanakuja kusaidia why not?
Mwanakijiji,tatizo sio misaada au sera za misaada.Tatizo ni kutumia misaada kuwekeza kwenye miradi ambayo haitasaidia taifa.
Kuzalisha umeme kwa kutumia mafuta ni gharama kuliko maji au makaa ya mawe (things that are abundant in tanzania).Kama kiwira inaweza kufufuliwa kwa 400m$ na kuzalisha megawati 400,sioni sababu yoyote ya hayo makampuni kutumia MCA kuzalisha umeme wa mafuta.Siwezi kuwapangia jinsi ya kutumia pesa zao bali siwezi kuwashangilia kwa kuwekeza kwenye umeme wa mafuta ilhali wakijua majority ya watanzania hawawezi kuumudu.
Usidanganyike!,Tanzania has one of the lowest tarrifs,approximately 100shillings/Kwh na still majority of tanzanians can't afford it,let alone access it....10-15c(shs 150-200) ni bei ya hapa US,na hii ni bei ambayo imetokana na high efficiency za grid zao,high accessibility(reduces cost),low cost of production(bearing in mind nuclear energy),...etc
Tanesco itabidi iongeze bei ya umeme kama tutatumia mafuta!!!,at the end of the day the story will remain the same...Getting screwed as usual!
 
Mkuu naona utusaidie kitu ambacho labda kinaweza kuonekana ni kidogo sana. Ututajie wamiliki wa Symbion na utuwekee CV zao. Na pia utueleze walianzaje mchakato wa kununua mitambo ya Dowans. Nani kawauzia na kwa bei gani!!

Mwenzio naogopa kuwa agent of the devil..Ukinisaidia hayo nitaku-join!
Pia atusaidie na hili, kwa nini wasije na mitambo mipya wananunua mitambo chakavu ya Dowans
 
Mwanakijiji tatizo lako you are too idealistic to realise kuwa fundamental problem kwetu ni TRANSPARENCY

Leo unataka uonyeshwe na upewe commercial details za hawa jamaa lakini hujiulizi kwa nini mambo madogo madogo kama kujua nani yumo kwenye baraza la usalama la taifa wako akina nani na elimu na experience zao ni zipi ...of course hakuna

leo watu wanazungumzia mambo ya muungano lakini conspiracy theorists au whatever you wanna call them walilalamika kuwa mkataba wa MUUNGANO unafichwa kwa kusudi na serikali...sasa hii ishaingia kwenye akili za watu

maybe all we need is FREEDOM OF INFORMATION ACT ili kuweza kuyajua haya llakini kabla ya yote ni kupata katiba nyingine mpa na kuondoa haya ma dinosaurs wanaututawala sasa
 
- I beg to differ, mimi siwaamini sana hawa GE kama Watanzania tunataka umeme wa kweli, na wa bei poa upo Germany na Italy, hawa GE watatumaliza hela zetu zote za taifa na hawana lolote ndege zinazotumia engine zao zinaanguka kila leo as opposed na kampuni kama Aggreko ya Italy!

- Sio kila king'aacho ni dhahabu!


William @ NYC, USA.
 
Kitu cha msingi ni kwamba makampuni mengi ya magharibi yalikuwa haya shiriki kwenye tender sababu ya hulaka ya viongozi wetu kupenda mtu wa kati ili wapitishe 90% yao , rejea weallikis ya boeimg etc .
Sasa sirikali baada ya kubanwa na wahisani na hali halisi wamefanya kile watanzania walikitaka miaka yote, fair dealing. Sasa kuna mtu anazungumzia aggreko nk . Aggreko (wataliano) nk wanakaribishwa ili mradi watumie njia za waazi au za kiushindani, na ninge penda kusema angalau huu wa GE ni waw wazi zaidi kuliko wa Richmond/Dowans.
na MCC ni part of the package, mtu hawezi kukusaidia ili wewe uweze kujiibia zaidi lazima ajaribu kuku weka katika mstari
 
Kampuni ya Kimarekani ya Symbion iliyonunua Dowans itaanza kuuza umeme Tanesco kuanzia kesho Jumanne.

Symbion itaanza kwa kuiuzia Tanesco umeme wa majaribio wenye megawati 120 wakati majadiliano juu ya makubaliono kamili ya manunuzi ya umeme yakiendelea. Hayo yamedhibitshwa na afisa mmoja wa Tanesco aliyeongea na Fox News leo. Msemaji wa Symbion bado hajapatikana kudhibitisha haya.

Habari na Fox News.
 
Good News, Taifa linahitaji hizo 120 megawati kwa hivi sasa, Dowans waendelee na kesi yao mpaka kieleweke ila sisi tunataka umeme ili uchumi isiendelee kuyumba.
 
Kinachoudhi ni jinsi wanatoa habari Marekani badala ya kwa Watanzania. Hii ni DHARAU!!
Kwa nini wasituambie sisi kwanza?
 
Back
Top Bottom