Swali la kizushi

Swali la kizushi

Wewe ni muuzaji wa duka, mteja anakuja na shilingi elfu Kumi (10,000/-) feki anataka Mkate wa shilingi 2,000/- ...wewe bila kujua unaipokea lakini unagundua hauna change ya kumpa mteja unaamua kuomba change kwa jirani yako na hiyo hiyo 10,000 feki kisha unamrudishia mteja shilingi elfu nane (8,000/-) na mkate, baadae jirani anakuja kukuambia ile pesa uliyompa ni feki unaamua kuichukua na kumpa shilingi 10,000/- halali. Je, utakuwa umepata hasara ya shilingi ngapi?
A. 12,000

B. 18,000

C. 10,000

D. 20,000

E. 8,000

F. 2,000
Hapo itategemea aliununua mkate sh. Ngapi na alitarajia kupata faida sh. Ngapi kwa kila mkate mmoja
 
ELF 8 YA CHENJI + ELFU 2 YA MKATE+ ELFU KUMI YA JIRAN YAKO = 20,000

JIBU D
soma vizuri alimpajirani feki akapewa halali,jirani akarudisha feki akapewa halali...hadi hapo ngoma droo hakuna hasara yoyote hapo
1+0 = 0+1
unaelewa nini ukiangalia hizi namba...
 
soma vizuri alimpajirani feki akapewa halali,jirani akarudisha feki akapewa halali...hadi hapo ngoma droo hakuna hasara yoyote hapo
1+0 = 0+1
unaelewa nini ukiangalia hizi namba...

Alivyorudshiwa change halal na jiran aliweka wap ile hela?
Au umesahau aliitoa kama change kwa mtu mwengne
 
D. 20,000/=

ulimpa mteja mkate (2,000/=) + chenji (8,000/=)
wewe ukabakiwa na 10,000/= feki (ambayo ina thamani ya 0/=), yaani ni sawa na hajakulipa chochote
Jumla umeshapoteza 10,000/= bila kupata chochote

Bado ulitoa tena 10,000/= halali ukarudishiwa 10,000/=feki toka kule ulipoomba chenji.
Unapoteza 10,000/= nyingine tena

Jumla 20,000/=

Hiyo 10,000 ya ziada inatoka wapi tena mkuu wakati bado alikuwa hajatia mkono kwenye mfuko wake kutoa pesa yoyote?
 
D. 20,000 mkate uliompa sh 2000 na chenji uliompa sh 8000=10,000 na 10,uliompa jirani
Jiulize: Kwani mpaka tapeli anaondoka eneo la tukio muuza duka alishaingiza mkono mfukoni mwake au kwenye droo kuchukua pesa yoyote?
 
Jiulize: Kwani mpaka tapeli anaondoka eneo la tukio muuza duka alishaingiza mkono mfukoni mwake au kwenye droo kuchukua pesa yoyote?
Ok basi itakua jibu ni A hasara yake ni sh. 12000/= elfu 10 aliyoilipa kwa jirani baada ya krudishiwa feki na elfu 2 mkate alioondoka nao tapeli.
 
Na wewe mtafute boya umbandike hiyo feki,tahadhari...uwe na mbio za kukimbia,kwa hiyo chemsha bongo yako jibu ni D.
 
Kuna vilaza wengi humu khaa..!
Hasara ni sh. 10,000 tu.
Jamaa katoa mkate halali wenye thamani ya sh. 2,000 na chenji halali sh. 8,000 jumla sh. 10,000
Muuzaji kabakiwa na pesa feki sh. 10,000
 
E
kuomba chenji bado nikapewa elfu 10 halali
nimerudisha chenji halali elfu 8
yule karudisha feki nimempa elfu 10 halali
nimepoteza elfu 8 na mkate wa elfu 2.

apana chezea switi mangi...im very experienced.
Hahahaha! Mangi weeeeeee!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom