Swali chokonozi: Lengo la vitambulisho vya wamachinga ni nini na kwanini linafanywa na Serikali kuu?

Nimewahi kujiuliza who is auditing matumizi ya hizi pesa....

Sent using Jamii Forums mobile app
Unatekeleza mauzo ya Vitambulisho kwa niaba yao, then unawatumia fedha kupitia account maalum iliyotolewa ambayo kimsingi iko chini ya "tra ya magogoni" then ndio unajiuliza hilo swali "who is auditing"?

Ask yourself je hili jambo limebainishwa kwenye bajeti kama chanzo cha mapato ya serikali kuu?

Je inatekelezwa chini ya sheria Ipi?
 
na serikari imekuwa wazi ukiwa nacho asije mtu kukutoa katika makazi yako ya biashara au mgambo kukunyang'anya mzigo wako. Fair enough na hela yenyewe ndogo tu.
Swali la Mzee Mwanakijiji umelisoma na kulielewa? Hivi inashindikana kuwaambia mgambo wasinyanyase wamachinga mpaka kuwe na vitambulisho?

Unajua wanaotakiwa kuwa navyo ni wale tu wenye mauzo kwa siku ya Shilingi 10.958? Yaani hata mama ntilie yule anayeuza chakula sahani 1,500 akiuza sahani 10 tu naye hastahili kupewa hicho kitambulisho.
 
Unatekeleza mauzo ya Vitambulisho kwa niaba yao, then unawatumia fedha kupitia account maalum iliyotolewa ambayo kimsingi iko chini ya "tra ya magogoni" then ndio unajiuliza hilo swali "who is auditing"?

Ask yourself je hili jambo limebainishwa kwenye bajeti kama chanzo cha mapato ya serikali kuu?

Je inatekelezwa chini ya sheria Ipi?

Sijaelewa hapo kidogo; wenye vitambulisho wakiuza wanaikatia hela serikali?
 
Yaani ni wizi wa wazi wazi


Sent using Jamii Forums mobile app
Unajuwa kipindi cha nyuma niliona habari kuwa serikali imekula pesa za rambi rambi sikuamini. Nikasema ni fake news tu. Lakini nikawa bado naiona tu na serikali haipingi. Kufuatilia nikakuta ni kweli kule Kagera pesa zao za rambi rambi serikali ilikamata ikazitumia kwingine.
 
hapa mwanza tunauziwa kwa biti kali tumetangaziwa kufikia tarehe 28/02/2019 ambae atakua ajanunua msako mkali unaanza!! sasa unajiuliza wameleta kumsaidia machinga au wametengeneza ili kumlazimisha kila mtu anunue ili wapate mapato? nani aliongea na wamachinga wakamwambia shida yao ni vitambulisho? utamwambiaje machinga anunue kitambulisho elfu 20.Wakati ujawai mkopesha mtaji ata wa jero
 
Ni agizo la mzee baba ili akusanye pesa...ila hutaki kuamini...ila ndio ukweli huu.

Tukisema kuwatambua walahi hakuna data base....wanachukuliwa tu particulars zao kwenye makaratasi tu..

Na ukizingatia vitambulisho vyenyewe havina chochote zaidi ya zile namba zao..

Sent using Jamii Forums mobile app
Kama hataelewa kwa lugha hiyo nyepesi na ya moja kwa moja kamwe hataelewa Tena.


Hakuna taarifa zozote za maana ambazo zinahifadhiwa kwa namna yoyote ya maana.

Lengo ni mauzo ya vitambulisho Tena kimtindo ni kwa namna ya lazima ili kila aliyegaiwa amalize vyake ili asifiwe na kujenga CV Yake.
 
View attachment 1029451
(Picha kutoka Ahmad Michuzi)

Sijafuatilia sana suala hili la vitambulisho na sijapata nafasi ya kusoma uchambuzi yakinifu ya kwanini linafanyika sasa na jinsi linavyofanyika. Kwa kufuatilia tu habari kama wengine ningependa kujua zaidi ili kuweza kutoa mchango wa mawazo ipasavyo. Inawezekana kabisa kuwa hili ni wazo zuri sana (brilliant idea) lakini uzuri wake unahitaji kuangaliwa kwa macho ya darubini kuona uwezekano wa matatizo na hata matumizi mabaya ya mpango wenyewe.

1. Lengo la kuwa na hivi vitambulisho ni nini hasa? Ni kutaka kujua nani anafanya biashara, wapi, na gani? au ni kwa ajili ya kuona ni wapi serikali inaweza kupata mapato zaidi?

2. Kwanini vitambulisho hivi vimeanzia Ikulu badala ya wizara fulani kwa mfano TAMISEMI? (naelewa TAMISEMI iko chini ya Ikulu). Kwa maana ya kwamba, Ikulu inataka kutatua tatizo gani hasa?

3. Imeonekana kuna ulazima kuwa wafanyabiashara hawa wadogo wadogo - hadi wabangua kokoto - watatakiwa kuwa na vitambulisho hivi. Ulazima huu ni kwa ajili gani hasa? Wao watapata faida gani ya kuwa na vitambulisho hivi? Je, mtu asiponunua vitambulisho hivi atapata adhabu gani na kwa kosa la kuvunja sheria gani?

4. Je, vitambulisho hivi vinaingizwa kwenye database gani ambayo inakusanya na kuchanganua taarifa za wafanyabiashara hawa? Au watu wananunua vitambulisho na kusema wanavyo?

5. Je, ni kwanini viuzwe au kutolewa kupitia ofisi ya Mkuu wa Mkoa/Wilaya badala ya Halmashauri ambapo watu wanafanya shughuli zao? Mapato haya ya vitambulisho - sijui vinauzwaje yanaenda wapi? Mkoani, Halmashauri au Hazina Kuu?

6. Ni kwa vili itakuwa vigumu watu ku counterfeit vitambulisho hivi? Yaani, kuna teknolojia gani iko (embedded) kwenye hivi vitambulisho kuzuia kuigwa?

7. Kuna ulazima kweli wa kuwa na vitambulisho hivi? Watu wana leseni za biashara, wana vitambulisho mbalimbali kwanini ulazima wa kuwa na hivi; hivi vinamuongezea mtu kitu gani ambacho angeshindwa kukipata au kuvifanya kwa kutumia vitambulisho alivyo navyo tayari?

Naomba kusaidiwa kwa taarifa sahihi (facts) kuliko kukisia au kunuia. Kama mwenzangu na wewe uko kama mimi basi tuendelee kuuliza maswali; wenye majibu watatusaidia kujibu.
Mkakati wa ccm kuelekea uchaguzi serikali za mitaaa
 
Asisumbuliwe kuhusu nini?
Mchuuzi na mama ntilie, mgambo na wengine wote wenye tabia za kuwapora bidhaa waache
Kwa wauzaji sokoni wenye vibanda TRA na halmashauri waache kuwafuata wakiwa na kibali kinachowatambulisha kama wajasiriamali

Muwe mnasikiliza speech sio kuuliza maswali ambayo yametolewa ufafanuzi siku ya uzinduzi

Anyway ni tatizo la serikari kwenye ku-comminucate policy zao, usipotoa maelezo yako, wengine watakutolea kwa niaba yako ndio kama hapa.
 
Swali la Mzee Mwanakijiji umelisoma na kulielewa? Hivi inashindikana kuwaambia mgambo wasinyanyase wamachinga mpaka kuwe na vitambulisho?

Unajua wanaotakiwa kuwa navyo ni wale tu wenye mauzo kwa siku ya Shilingi 10.958? Yaani hata mama ntilie yule anayeuza chakula sahani 1,500 akiuza sahani 10 tu naye hastahili kupewa hicho kitambulisho.
Wenye kipato chini ya 500000

Maana yake anything from 0-500000 provided wewe ni mjasiriamali ukusoma grouping katika statistics
 
Msituchoshe na maswali ya kipumbavu kujionesha mnajua kuhoji! Nyie si ndio mlikuwa mnampigia debe huyo kichaa? Kawaulize.hata ma-DED na Ma-DC kama wanajua maana ya hivyo vitambulisho!
 
Sijaelewa hapo kidogo; wenye vitambulisho wakiuza wanaikatia hela serikali?
Iko hivi Rais Wa Wanyonge kaanzisha vitambulisho na kuvigawa kupitia Wizara ya TAMISEMI as you know kwamba ipo chini ya ofisi yake.


Kisha vinagawanywa/kukabidhiwa kwa wakuu wa Mikoa Tena kwa idadi maalum ambayo kila mkabidhiwa anatakiwa kuhakikisha anamaliza mgao wake.

Mkuu wa Mkoa anakuja kugawa kwa Wilaya zake zote kupitia maDC walio chini yake, nao wakishapokea wanavigawa kwa Tarafa zoote na Kata zote zilizo chini yao (chain of command inachukua mkondo wake).

Kila mmoja anahimizwa kuhakikisha anamaliza vitambulisho alivyopewa.

Kila kitambulisho kinauzwa 20,000/= hela zote zinatakiwa kuwa deposited kwenye account maalum ambayo iko chini ya Mkolomije Mkuu.
 
Mkakati wa ccm kuelekea uchaguzi serikali za mitaaa
Hata mimi nimejiuliza, kwani fungu la uchaguzi huwa lina toka wapi? Miaka ya nyuma ndo tulisikia EPA nk. Labda ni pesa ya uchaguzi. Kwasababu wafanyabiashara sidhani kama wanahamu na hii maneno. Wafadhili wa ccm sijui ndo kina nani? Labda ndo njia ya wanyonge kuchangia na wenyewe.
 
Back
Top Bottom