Surat Maryam ndio Sura pekee katika Qur'an iliyopewa jina la Mwanamke, zijue sababu

BAKIIF Islamic

JF-Expert Member
Jul 11, 2021
600
1,840
Hiii ndio Sura (ufunuo) pekee katika Qur'an iliyopewa jina la mwanamke maalumu anayejulikana, ingawa ndani ya sura hii kumetajwa manabii wakubwa wakubwa kama vile Nabii Yahya, Zakaria, Ibrahim, Is-haq, Yaquub, Idriss, Ismail, n.k. Wote wametajwa ndani ya sura hii.

Kisa cha Bi Maryam katika kumzaa Nabii Issa, ilikua si tukio la kawaida ni miujiza ambayo ilistahiki kubakishwa na ndipo Mwenyezi MUNGU akalitumia jina la Marym katika sura hii.

Sura hii imeitwa kwa jina la mwanamke msafi, ambaye aliishi maisha yake yote katika hali ya kiimani kuanzia utoto wake hadi katika ujana wake.

Malaika walimwambia, 'Ewe Maryam, hakika Mwenyezi MUNGU amekuchagua wewe na akakutakasa, na akakuteua kuliko wanawake wa ulimwengu wote.

Sifa za Maryam
-Aliweza kulinda uke wake, hakufanya machafu ya aina yoyote, aliudhibiti uchi wake, hakufanya uchafu wowote wa zinaa, ni mwanamke ambaye alilinda nafsi yake. Lakini Mwenyezi MUNGU alimtia roho Maryam, yaani Nabii Issa.

Sura hii imeitwa Maryam kwa lengo la kubakisha historia ya mazazi ya kimiujiza,

Suratu Mariam ni sura ya 19 katika sura 114 za Quran, pia ipo juzu la 16 katika majuzu 30 ya Qur'an. Sura hii imechukua aya 98 katika aya 6666 za Qur'ani Tukufu.

Suratu Marym imeshuka katika mji wa Makka, ispokua aya mbili tu ndio zimeshuka Madina. Aya 96 zimeteremka Maka. Aya mbili zimeshuka madina ambazo ni aya ya 58 na aya ya 71.


1715589807260.png
 
Hiii ndio Sura (ufunuo) pekee katika Qur'an iliyopewa jina la mwanamke maalumu anayejulikana, ingawa ndani ya sura hii kumetajwa manabii wakubwa wakubwa kama vile Nabii Yahya, Zakaria, Ibrahim, Is-haq, Yaquub, Idriss, Ismail, n.k. Wote wametajwa ndani ya sura hii.

Kisa cha Bi Maryam katika kumzaa Nabii Issa, ilikua si tukio la kawaida ni miujiza ambayo ilistahiki kubakishwa na ndipo Mwenyezi MUNGU akalitumia jina la Marym katika sura hii.

Sura hii imeitwa kwa jina la mwanamke msafi, ambaye aliishi maisha yake yote katika hali ya kiimani kuanzia utoto wake hadi katika ujana wake.

Malaika walimwambia, 'Ewe Maryam, hakika Mwenyezi MUNGU amekuchagua wewe na akakutakasa, na akakuteua kuliko wanawake wa ulimwengu wote.

Sifa za Maryam
-Aliweza kulinda uke wake, hakufanya machafu ya aina yoyote, aliudhibiti uchi wake, hakufanya uchafu wowote wa zinaa, ni mwanamke ambaye alilinda nafsi yake. Lakini Mwenyezi MUNGU alimtia roho Maryam, yaani Nabii Issa.

Sura hii imeitwa Maryam kwa lengo la kubakisha historia ya mazazi ya kimiujiza,

Suratu Mariam ni sura ya 19 katika sura 114 za Quran, pia ipo juzu la 16 katika majuzu 30 ya Qur'an. Sura hii imechukua aya 98 katika aya 6666 za Qur'ani Tukufu.

Suratu Marym imeshuka katika mji wa Makka, ispokua aya mbili tu ndio zimeshuka Madina. Aya 96 zimeteremka Maka. Aya mbili zimeshuka madina ambazo ni aya ya 58 na aya ya 71.


View attachment 2989196
Ila mkuu majina ya surah sio kwamba ya litoka kwa Allah, hapana haya majina ya surah imetumwa na maswahaba na khalifa Abubakar( ra) kwahoyo sioni cha ajabu chochote hapo.
 
Na Surah Al Jin kwenye Kuruani Kwa Nini hiyo Sura imepewa jina la Majini
Imeitwa Surat Al-Jin kutokana na mada yake, kwani ndani yake tukio la Majini kuisikia Quran na kuukubali uilsamu kisha kurudi kwa wenzao kwenda kuwahubiria Uislamu.

Mtume Muhammad (S.a.w) alikuwa akisafiri kutoka Makka kuelekea soko la `Ikadh huko Taif ili kuwaalika watu wengi waliokuwa wakimiminika huko ili awafikishie ujumbe wa Uislamu. Hata hivyo katika mkusanyiko huu, hakuna hata mmoja wa wale waliohudhuria aliyekubali kuwa muislamu. Watu wa mji wa Taif walimkadhibisha vikali na wakamrushia mawe Mtume kiasi kwamba damu zilikuwa zikimtoka mwili mzima.

Akiwa amechoka na kufadhaika, alisimama karibu na bustani. Mahali hapo, alikutana na mtumishi wa mwenye shamba jina lake Adas. Mtumwa huyu alikubali mafundisho ya Uislamu na baada ya hapo, Mtume aliendelea na safari yake ya kurejea nyumbani Makka.

Akiwa njiani kurudi Makka, Mtume (S.a.w) alifika sehemu iliyoitwa Bonde la Majini. Alikaa hapo kwa muda wa jioni na akazama katika usomaji wa Qur'ani Tukufu. Kundi la Majini, waliokuwepo na kumsikiliza, mara moja waliikubali imani ya Uislamu. Baada ya hapo, walirudi kwenye kundi lao ili kueneza mafundisho waliyoyakubali kutoka kwa mtume.

Wakati wa usiku, Mtume alifika karibu na msitu wa miti na akiwa anashughulika katika Swala, kundi la Majini kutoka eneo la Yemen lililotokea eneo hilo lilisikia kisomo cha Qurani ya Mtume (s.a.w.w.) katika Swala yake ya al-Fajr na wakakubali mafundisho ya Uislamu hapo hapo.
 
Imeitwa Surat Al-Jin kutokana na mada yake, kwani ndani yake tukio la Majini kuisikia Quran na kuukubali uilsamu kisha kurudi kwa wenzao kwenda kuwahubiria Uislamu.

Mtume Muhammad (S.a.w) alikuwa akisafiri kutoka Makka kuelekea soko la `Ikadh huko Taif ili kuwaalika watu wengi waliokuwa wakimiminika huko ili awafikishie ujumbe wa Uislamu. Hata hivyo katika mkusanyiko huu, hakuna hata mmoja wa wale waliohudhuria aliyekubali mwaliko wake. Watu watukufu wa Taif walimkadhibisha vikali na wakamrushia mawe Mtume kiasi kwamba damu zilikuwa zikimtoka mwili mzima

Akiwa amechoka na kufadhaika, alisimama karibu na bustani. Mahali hapo, alikutana na mtumishi wa mwenye shamba jina lake Adas. Mtumwa huyu alikubali mafundisho ya Uislamu na baada ya hayo, Mtume aliendelea na safari yake ya kurejea nyumbani Makka.

Akiwa njiani kurudi, Mtume (S.a.w) alifika sehemu iliyoitwa Bonde la Majini. Alikaa hapo kwa muda wa jioni na akazama katika usomaji wa Qur'ani Tukufu. Kundi la Majini, waliokuwepo na kumsikiliza, mara moja waliikubali imani ya Uislamu. Baada ya hapo, walirudi kwenye kundi lao ili kueneza na kueneza mafundisho waliyoyakubali kutoka kwa mtume.

Wakati wa usiku huo, alifika karibu na msitu wa miti na akiwa anashughulika katika Swala, kundi la Majini kutoka eneo la Yemen lililotokea eneo hilo lilisikia kisomo cha Qurani ya Mtume (s.a.w.w.) katika Swala yake ya al-Fajr na wakakubali mafundisho ya Uislamu hapo hapo.
Nadharia kama nadharia nyingine tu za upande wa pili ila cha umuhimu kufahamu ni MUNGU yupo na sisi
 
Ila mkuu majina ya surah sio kwamba ya litoka kwa Allah, hapana haya majina ya surah imetumwa na maswahaba na khalifa Abubakar( ra) kwahoyo sioni cha ajabu chochote hapo.
Upo sahihi,
Abu Maryam' ni swahaba na jina lake hili linatokana na suratu Maryam. Yeye mwenyewe alisema 'Nilimuendea mtume s.a.w nikamwambia ewe mtume, usiku huu ambao mimi nimekuja kwako nimeruzukiwa mtoto wa kike (yaani mkewe amezaa mtoto wakike). Baada tu ya mkewe kuzaa yeye akakimbilia kwa Mtume s.a.w.

Mtume akamjibu: akamwambia na usiku huu, kama wewe umesema mkeo amezaa mtoto wakike na mimi nakueleza kwamba usiku huu ndio usiku nimeteremshiwa suratu Maryam. Kwa hivyo nenda ukampe binti yako jina la Maryma''

Kwa hiyo utaona kabisa hapa mtume mwenyewe kaiita sura hii kwa jina la Maryam'' na swahaba huyo Abu Maryam ndio likawa jina lake.
 
Imeitwa Surat Al-Jin kutokana na mada yake, kwani ndani yake tukio la Majini kuisikia Quran na kuukubali uilsamu kisha kurudi kwa wenzao kuwahubiria

Akiwa njiani kurudi Makka, Mtume (S.a.w) alifika sehemu iliyoitwa Bonde la Majini. Alikaa hapo kwa muda wa jioni na akazama katika usomaji wa Qur'ani Tukufu. Kundi la Majini, waliokuwepo na kumsikiliza, mara moja waliikubali imani ya Uislamu. Baada ya hapo, walirudi kwenye kundi lao ili kueneza mafundisho waliyoyakubali kutoka kwa mtume.

Wakati wa usiku, Mtume alifika karibu na msitu wa miti na akiwa anashughulika katika Swala, kundi la Majini kutoka eneo la Yemen lililotokea eneo hilo lilisikia kisomo cha Qurani ya Mtume (s.a.w.w.) katika Swala yake ya al-Fajr na wakakubali mafundisho ya Uislamu hapo hapo.
Kwa hiyo Yako majini maislamu ambayo huswali na waislamu wakati wa swala misikitini?
 
Dini ni upuuzi furani hivi,mud aliibi kisa cha mariamu myahudi mamake Yesu,akakiingiza kwenye story zake za kuunga unga.

Kimsingi hakuna jipya ukitaka storia kamili lazima ukasome biblia ndio utapata historia kamili sio kurwani mana visa vya kurwani ni story za kukuungaunga kutoka kwa story za wayahudi.

Tuambie huyo mariam alikua kabila gani,na kisa kilitokea wapi..?haya majibu lazima uende kwenye biblia ndia utayapata,kurwani huwezi pata jibu lolote.
 
Kwa hiyo Yako majini maislamu ambayo huswali na waislamu wakati wa swala misikitini?
Sio msikitini tu hata makanisani majini yanaingia ila maovu na ndio maana unaona huko watu wanadondoka.

Majini ni viumbe wa MUNGU kama tulivyo sisi binaadamu ispokua sisi hatuwaoni ila wao wanatuona. Majini wanaonekana na kufahamika kimakosa na wengi kati yetu. Hii ni kutokana na kuwa wao wanatuona lakini sisi hatuwaoni.

Wanadamu hatuwaoni majini kwa macho yetu japo tuko nao, tunapishana nao lakini wao wenzetu wanatuona. Wakati sisi wanadamu hatuwaoni majini, baadhi ya wanyama kama Punda na Mbwa wanaofugwa majumbani huwaona Majini.

Kama tulivyo sisi binaadamu kuna wanadaamu wema na waovu ndio hivyo hivyo kuna majini wema na waovu. Katika uovu kuna wanadaamu wamepindukia hadi kuwekwa nguvuni na wanadaamu wenzao (gerezani), ni hivyo hivyo kwa majini kuna majini maovu haswa hadi kufungwa.

Kama ilivyo kwa wanaadamu kuna watu wema na wachamungu utawapata katika mnyumba za ibada, ni hivyo hivyo kuna majini wema na wachamungu utawapata kwa nyumba za ibada.

Majini ni kama malaika ispokua wao wameumbwa kwa moto na wana utashi wa kumuasi MUNGU au kumuabudu, lakini malaika hana utashi huo yeye kaumbwa kumuabudu MUNGU tu.

Binaadamu tumepewa utashi, tuabudu au tusiabudu utashi ni wa kwako, na mwisho hukumu itakua juu yako.
 
Dini ni upuuzi furani hivi,mud aliibi kisa cha mariamu myahudi mamake Yesu,akakiingiza kwenye story zake za kuunga unga.

Kimsingi hakuna jipya ukitaka storia kamili lazima ukasome biblia ndio utapata historia kamili sio kurwani mana visa vya kurwani ni story za kukuungaunga kutoka kwa story za wayahudi.

Tuambie huyo mariam alikua kabila gani,na kisa kilitokea wapi..?haya majibu lazima uende kwenye biblia ndia utayapata,kurwani huwezi pata jibu lolote.
Mbona kama vile Roho inakuuma sana, kuna shida gani?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom