Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 20,920
- 30,261
DARSA LA TAFSIR YA QUR'AN LA SHEIKH ABDALLAH IDDI CHAREMBO MWEZI WA RAMADHANI MSIKITI WA MTORO MIAKA YA 1970
Hukaa nikaangalia nyuma na ''nostalgia'' yaani simanzi.
Naangalia ujana wangu ulivyoondoka kama moshi na nawakumbuka masheikh wetu waliotangulia mbele ya haki.
Nawaona kama jana vile Mwezi Mtukufu wa Ramadhani baada ya sala ya L' Asr wamekaa mbele ya Sheikh Abdallah Chaurembo kusikiliza tafsiri ya Qur'an Tukufu ndani ya Msikiti wa Sheikh Mtoro Mwinyi Mangara.
Nathubutu kusema kuwa hili ndilo darsa pekee ambalo baada ya kufariki Sheikh Chaurembo sijaona tena darsa katika msikiti wowote hapa Dar es Salaam ambao masheikh wanajumuika kumsikiliza sheikh mwenzao anatafsir Qur'an.
Madaris yapo mengi hasa Mwezi wa Ramadhani lakini wasomaji na wasikilizaji ni waumini wa kawaida.
Iweje masheikh waje kumsikiliza sheikh mwenzao na katika hawa wako masheikh ambao walisomeshwa pamoja na Sheikh Chaurembo katika madrasa ya Bingwa wa Mabingwa wa Tafsir, Mufti wa Tanganyika kisha Tanzania, Sheikh Hassan bin Ameir.
Naam; na kwa nini wasije?
Sheikh Abdallah Chaurembo alikuwa ndiye mwanafunzi mkubwa kushinda wote wa Sheikh Hassan bin Ameir.
Msemaji amesema Sheikh Chaurembo hakumbakishia mwalimu wake chochote anaitafsir Qur'an kama alivyokuwa akitafsir sheikh wake kwa mtindo ule ule na kamuiga mwalimu wake mpaka sauti yake.
Hadi vitu vidogo vidogo katikati ya darsa kaiga, atawauliza wanaomsikiliza, ''Mmefahamu?''
Utulivu uliokuwapo hapo na ule ukimya watu wakimsikiliza Sheikh Chaurembo hauna mfano.
Sauti iliyokuwa ikisikika ni sauti ya mapanga boi yakizunguka...wawawawawa!
Darsa inaendelea na watu wanazidi kuingia msikitini kuja kumsikiliza sheikh waliochelewa wanaunga nyuma.
Huu ulikuwa ule msikiti wa zamani wa Mtoro Mtaa wa Mahiwa na Livingstone ulioanza kama msikiti mdogo wa udongo na leo ni msikiti wa fahari katika misikiti mikubwa nchini.
Namuona Sheikh Ramadhani Abbas, Sheikh Abdulrahman Shamte, Sheikh Kassim Juma, Sheikh Maulid Digila, kwa kuwataja wachache.
Namuona Sheikh Mohamed Khan aliyekuwa na hoteli maarufu Steak Inn mtu mwema na karimu akiwalipa mishahara watu wa dini kwa siri kubwa akitafuta radhi za Allah.
Namuona Sheikh Zubeir Chanzi akimjua baba yangu pale Mtaa wa Kipata toka udogo wao miaka ya 1930 na kila akiniona msikitini ataniadhimisha sana kwa mapenzi na kumkumbuka rafiki yake.
Sheikh Zubeir alikuwa njiwa wa msikiti hapungui hapo miaka nenda miaka rudi.
Darsa inaanza.
Qari atasoma aya chache na Mtoro Mashaallah walikuwapo wasomaji Qur'an wa sifa wenye kiraa cha kumtoa machozi msikilizaji.
Ilikuwa katika darsa hii ya Sheikh Chaurembo ndipo nilipokisikia kisa cha Banu Nadir kwa ukamilifu wake sheikh akikieleza utadhani unaangalia senema.
Sheikh Churembo akisafiri kutoka rejea moja na kuingia nyingine na katika ile nyingine akatoka kaingia nyingine tena wataalamu wanaita, ''reference and cross reference.''
Kilichokuwa kikinishangaza ni kuwa Sheikh Chaurembo alikuwa akitoa hizi rejea nyingi kichwani na mara moja moja utaona anaangalia karatasi yake ya ukurasa mmoja.
Sikuweza kustahamili siku moja nikamuuliza mwanae Iddi Abdallah Chaurembo, ''Kaka Iddi hebu niambie yale yote anayotusomesha sheikh yote yale kahifadhi kichwani?''
Sheikh Chaurembo alikuwa akitueleza pale darsani akisema, ''Sheikh Hassan bin Ameir alikuwa na ibra moja nayo ni kuwa kila anaechukua kitabu kwenda kusoma kwake akili zake si za kawaida.''
Hapa namkumbuka rafiki yangu marehemu Sheikh Manzi wa Msikiti wa Mwinyimkuu, Magomeni.
Siku kama mbili kabla hajafariki tumekutana njiani kama kawaida yetu lazima tusimame angalau dakika tatu tuzungumze.
Kumbe yeye akijua kuwa mimi nampenda Sheikh Hassan bin Ameir.
''Mimi Sheikh Hassan kanisomesha,'' Sheikh Manzi ananieleza.
Jibu langu lilimfurahisha na akacheka.
Nilimwambia kuwa sitoshangaa tena.
Sikuwa na sababu tena ya kushangazwa na ile ilm aliyokuwanayo.
Sikumuona tena Sheikh Manzi baada ya siku ile.
Turejee kwa Banu Nadir.
Hawa Banu Nadir walikuwa Wayahudi na walikula njama na maadui wa Waislam kumpiga vita Mtume SAW.
Nimebahatika mwaka wa 1997 kufika sehemu ambayo hawa Wayahudi waliishi pale Madina na nimeyaona magofu ya nyumba zao.
Sheikh wangu Sheikh Ali bin Abbas akiniliwaza kwa maneno haya, ''Mohamed usisoneneke kuwa hukupata kumsikia Sheikh Hassan bin Ameir akidarsisha, mradi unamsikiliza Sheikh Abdallah Chaurembo ni kama umemsikiliza sheikh mwenyewe.''
Mwaka mmoja Mwezi wa Ramadhani Sheikh Chaurembo akalifahamisha darsa akasema kuwa amemwalika Sheikh Issa Fatawi kutoka Zanzibar aje kufunga darsa la Tafsir ya Qur'an la Mwezi wa Ramadhani.
Sheikh Fatawi alikuwa mwanafunzi mwenzake kwa Sheikh Hassan bin Ameir.
Siku ile Sheikh Fatawi bin Issa alishika darsa akatusomesha kuhitimisha darsa yetu hadi Mfungo Mosi.
Mwisho Sheikh Kassim alisimama na kuzungumza na kusoma dua.
Nilitaka ndugu zangu leo tutabaruku na hawa wazee wetu watu wa kheri waliotangulia mbele ya haki na tuwaombee Allah awalipe Pepo ya Firdaus.
Amin
Picha ya kwanza haihitaji maelezo.
Picha ya pili Sheikh Ali bin Abbas.
Picha ya tatu Sheikh Kassim bin Juma akiwa amezungukwa na waumini wa Msikiti wa Mtoro na msikiti ni huo pembeni kulia.
Picha hii ilipigwa mwaka wa 1993.
Sheikh Hassan bin Ameir alipofariki mwaka wa 1979 nilimwandikia taazia fupi iliyochapwa katika Daily News upande wa barua za wasomaji.
Sheikh Chaurembo alimwalika Mwalimu Nyerere katika khitma yake Msikiti wa Mtoro na alihudhuria.
Mimi nilikuwapo na tulikula chakula ndani ya msikiti na Mwalimu Nyerere.
Sheikh Hassan bin Ameir ni kati ya masheikh walioipa TAA na kisha TANU nguvu na kuwa bega kwa bega na Mwalimu Nyerere katika kupigania uhuru wa Tanganyika.
Sehemu ya pili soma Kumbukumbu ya Ramadhani - Sehemu ya 2
Hukaa nikaangalia nyuma na ''nostalgia'' yaani simanzi.
Naangalia ujana wangu ulivyoondoka kama moshi na nawakumbuka masheikh wetu waliotangulia mbele ya haki.
Nawaona kama jana vile Mwezi Mtukufu wa Ramadhani baada ya sala ya L' Asr wamekaa mbele ya Sheikh Abdallah Chaurembo kusikiliza tafsiri ya Qur'an Tukufu ndani ya Msikiti wa Sheikh Mtoro Mwinyi Mangara.
Nathubutu kusema kuwa hili ndilo darsa pekee ambalo baada ya kufariki Sheikh Chaurembo sijaona tena darsa katika msikiti wowote hapa Dar es Salaam ambao masheikh wanajumuika kumsikiliza sheikh mwenzao anatafsir Qur'an.
Madaris yapo mengi hasa Mwezi wa Ramadhani lakini wasomaji na wasikilizaji ni waumini wa kawaida.
Iweje masheikh waje kumsikiliza sheikh mwenzao na katika hawa wako masheikh ambao walisomeshwa pamoja na Sheikh Chaurembo katika madrasa ya Bingwa wa Mabingwa wa Tafsir, Mufti wa Tanganyika kisha Tanzania, Sheikh Hassan bin Ameir.
Naam; na kwa nini wasije?
Sheikh Abdallah Chaurembo alikuwa ndiye mwanafunzi mkubwa kushinda wote wa Sheikh Hassan bin Ameir.
Msemaji amesema Sheikh Chaurembo hakumbakishia mwalimu wake chochote anaitafsir Qur'an kama alivyokuwa akitafsir sheikh wake kwa mtindo ule ule na kamuiga mwalimu wake mpaka sauti yake.
Hadi vitu vidogo vidogo katikati ya darsa kaiga, atawauliza wanaomsikiliza, ''Mmefahamu?''
Utulivu uliokuwapo hapo na ule ukimya watu wakimsikiliza Sheikh Chaurembo hauna mfano.
Sauti iliyokuwa ikisikika ni sauti ya mapanga boi yakizunguka...wawawawawa!
Darsa inaendelea na watu wanazidi kuingia msikitini kuja kumsikiliza sheikh waliochelewa wanaunga nyuma.
Huu ulikuwa ule msikiti wa zamani wa Mtoro Mtaa wa Mahiwa na Livingstone ulioanza kama msikiti mdogo wa udongo na leo ni msikiti wa fahari katika misikiti mikubwa nchini.
Namuona Sheikh Ramadhani Abbas, Sheikh Abdulrahman Shamte, Sheikh Kassim Juma, Sheikh Maulid Digila, kwa kuwataja wachache.
Namuona Sheikh Mohamed Khan aliyekuwa na hoteli maarufu Steak Inn mtu mwema na karimu akiwalipa mishahara watu wa dini kwa siri kubwa akitafuta radhi za Allah.
Namuona Sheikh Zubeir Chanzi akimjua baba yangu pale Mtaa wa Kipata toka udogo wao miaka ya 1930 na kila akiniona msikitini ataniadhimisha sana kwa mapenzi na kumkumbuka rafiki yake.
Sheikh Zubeir alikuwa njiwa wa msikiti hapungui hapo miaka nenda miaka rudi.
Darsa inaanza.
Qari atasoma aya chache na Mtoro Mashaallah walikuwapo wasomaji Qur'an wa sifa wenye kiraa cha kumtoa machozi msikilizaji.
Ilikuwa katika darsa hii ya Sheikh Chaurembo ndipo nilipokisikia kisa cha Banu Nadir kwa ukamilifu wake sheikh akikieleza utadhani unaangalia senema.
Sheikh Churembo akisafiri kutoka rejea moja na kuingia nyingine na katika ile nyingine akatoka kaingia nyingine tena wataalamu wanaita, ''reference and cross reference.''
Kilichokuwa kikinishangaza ni kuwa Sheikh Chaurembo alikuwa akitoa hizi rejea nyingi kichwani na mara moja moja utaona anaangalia karatasi yake ya ukurasa mmoja.
Sikuweza kustahamili siku moja nikamuuliza mwanae Iddi Abdallah Chaurembo, ''Kaka Iddi hebu niambie yale yote anayotusomesha sheikh yote yale kahifadhi kichwani?''
Sheikh Chaurembo alikuwa akitueleza pale darsani akisema, ''Sheikh Hassan bin Ameir alikuwa na ibra moja nayo ni kuwa kila anaechukua kitabu kwenda kusoma kwake akili zake si za kawaida.''
Hapa namkumbuka rafiki yangu marehemu Sheikh Manzi wa Msikiti wa Mwinyimkuu, Magomeni.
Siku kama mbili kabla hajafariki tumekutana njiani kama kawaida yetu lazima tusimame angalau dakika tatu tuzungumze.
Kumbe yeye akijua kuwa mimi nampenda Sheikh Hassan bin Ameir.
''Mimi Sheikh Hassan kanisomesha,'' Sheikh Manzi ananieleza.
Jibu langu lilimfurahisha na akacheka.
Nilimwambia kuwa sitoshangaa tena.
Sikuwa na sababu tena ya kushangazwa na ile ilm aliyokuwanayo.
Sikumuona tena Sheikh Manzi baada ya siku ile.
Turejee kwa Banu Nadir.
Hawa Banu Nadir walikuwa Wayahudi na walikula njama na maadui wa Waislam kumpiga vita Mtume SAW.
Nimebahatika mwaka wa 1997 kufika sehemu ambayo hawa Wayahudi waliishi pale Madina na nimeyaona magofu ya nyumba zao.
Sheikh wangu Sheikh Ali bin Abbas akiniliwaza kwa maneno haya, ''Mohamed usisoneneke kuwa hukupata kumsikia Sheikh Hassan bin Ameir akidarsisha, mradi unamsikiliza Sheikh Abdallah Chaurembo ni kama umemsikiliza sheikh mwenyewe.''
Mwaka mmoja Mwezi wa Ramadhani Sheikh Chaurembo akalifahamisha darsa akasema kuwa amemwalika Sheikh Issa Fatawi kutoka Zanzibar aje kufunga darsa la Tafsir ya Qur'an la Mwezi wa Ramadhani.
Sheikh Fatawi alikuwa mwanafunzi mwenzake kwa Sheikh Hassan bin Ameir.
Siku ile Sheikh Fatawi bin Issa alishika darsa akatusomesha kuhitimisha darsa yetu hadi Mfungo Mosi.
Mwisho Sheikh Kassim alisimama na kuzungumza na kusoma dua.
Nilitaka ndugu zangu leo tutabaruku na hawa wazee wetu watu wa kheri waliotangulia mbele ya haki na tuwaombee Allah awalipe Pepo ya Firdaus.
Amin
Picha ya kwanza haihitaji maelezo.
Picha ya pili Sheikh Ali bin Abbas.
Picha ya tatu Sheikh Kassim bin Juma akiwa amezungukwa na waumini wa Msikiti wa Mtoro na msikiti ni huo pembeni kulia.
Picha hii ilipigwa mwaka wa 1993.
Sheikh Hassan bin Ameir alipofariki mwaka wa 1979 nilimwandikia taazia fupi iliyochapwa katika Daily News upande wa barua za wasomaji.
Sheikh Chaurembo alimwalika Mwalimu Nyerere katika khitma yake Msikiti wa Mtoro na alihudhuria.
Mimi nilikuwapo na tulikula chakula ndani ya msikiti na Mwalimu Nyerere.
Sheikh Hassan bin Ameir ni kati ya masheikh walioipa TAA na kisha TANU nguvu na kuwa bega kwa bega na Mwalimu Nyerere katika kupigania uhuru wa Tanganyika.
Sehemu ya pili soma Kumbukumbu ya Ramadhani - Sehemu ya 2