MISS TANZANIA
SEHEMU YA 46
MTUNZI 😛ATRICK.CK
CONTACT:0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Msiwe na wasi wasi.Happy ni mtu mzima na anafahamu kitu anachokifanya.Inawezekana amepatwa na dharura kama mnavyofahamu kwa siku za hivi karibuni amakuwa na mambo mengi .Tuendeleeni kumsubiri na nina hakika atarejea muda si mrefu” mzee Kibaho akawapa moyo familia yake lakini hata yeye alikuwa na wasi wasi mwingi moyoni kutokana na mfululizo wa matukio yaliyomuandama binti yake
ENDELEA……………….
Mlio wa kengele ukasikika katika chumba walichokuwamo akina Khumalo.
“kazi imeanza.” Akasema Khumalo na kuondoka kuelekea katika chumba alichokuwamo Happy
“Hallo Happy” akasema Khumalo
“Stop it..Please stop it” akalia Happy huku akiyafunika macho yake kwa viganja vya mikono ili asiendelee kuzitazama picha zile za kutisha
“Umeona Happy? Umeona namna sumu hii inavyowatesa watu kabla hawajafa?
“ Please Job ,dont do that to Patrick.I beg you don’t hurt Patrick” akalia Happy
“Kwa hiyo umeamua nini? Uko tayari kufanya kile tunachotaka kwa ajili ya kuokoa uhai wa Patrick? Akauliza Khumalo
“I’m ready.Please don’t hurt Patrick.I’m ready to do anything to save him”
“Vizuri sana.Watu kama wewe ni wachache sana.Hata mimi namuonea wivu Patrick kwani amempata mwanamke anayempenda kwa dhati.”
“Tafadhali sema mnataka niwafanyie nini? Akasema Happy huku akifuta machozi.Khumalo akainuka pale sofani alipokuwa amekaa akamsogelea Happy
“Stop crying Happy.Usilie tena.” Akasema Khumalo halafu akanyamaza kidogo akamtazama Happy usoni na kusema
“ Aliyenituma nikulete hapa alitoa sharti moja tu ambalo ukilitekeleza utaokoa maisha ya Patrick na wewe utakuwa huru.Anao vijana wake wawili wanaokupenda sana na anataka ufanye nao mapenzi.”
“ What !!!!????...Happy akastuka na kumtazama Khumalo kama ameona mzuka
“Hilo ndilo sharti pekee alilolitoa mtu aliyekuleta hapa.Ni juu yako kukubali au kukataa.Kama hautakuwa tayari sisi tutakuacha uende zako lakini nakuhakikishia kwamba wakati wewe ukitoka ndani ya jumba hili,mtu umpendaye kuliko wote duniani atakuwa atakuwa tayari amelala usingizi wa milele.” Akasema Khumalo na kuzidi kumtisha Happy.
“ Ni nani huyo shetani ambaye amenileta hapa? Ni nani huyo asiyekuwa na hata chembe ya ubinadamu? Nimemkosea kitu gani hadi aamue kunitenda namna hii ? akasema Happy huku akilia kwa uchungu
“Happy ni juu yako kuamua .Kilio na matusi kamwe havitakusaidia na muda wetu unazidi kwenda.Ninakupa tena dakika kumi nyingine za kuamua “ akasema Khumalo na kupiga hatua kutoka mle chumbani
“Ouh My God !!!! akalia Happy.Alihisi kuchanganyikiwa
“whats happening to me? Ni kweli nina laana? Kwa nini ninaandamwa na mikosi kama hii kila siku? Huyu mtu aliyenileta hapa ni nani na kwa nini atake kunidhalilisha namna hii? Happy akazidi kulia
“Huyu mtu aliyenileta hapa lengo lake ni moja tu ,kunidhalilisha. Nini kitatokea kama nitakataa kufanya anavyotaka? Je ni kweli Patrick yuko katika hatari ya kuuawa? Sina hakika kama suala hili ni la kweli.Huyu mtu lengo lake ni kuudhalilisha utu wangu.Ninaanza kuhisi mtu huyu atakuwa ni Savanna kwani ndiye mtu niliyelumbana naye jana na tukatoleana vitisho.Pengine ameamua kunionyesha uwezo wake kwa kuniteka na kunileta hapa ili nidhalilike.Siwezi kukubali hata kidogo kuwapa nafasi ya kuuchezea mwili wangu.Ni bora waniue kuliko kuwapa nafasi ya kunichezea.” Akawaza Happy lakini mara akastuka
“What if its true and Patrick is going to die? Inawezekana pengine watu hawa wakawa wanasema kweli ..Am I ready to let Patrick die? I’m confused..!!! Happy akahisi kuchanganyikiwa
“Patrick amejitolea mengi kwa ajili yangu na hata hivi sasa anasota gerezani kwa ajili yangu.Kwa nini na mimi nishindwe kusimama imara kuutetea uhai wake? Kwa maana hiyo itanilazimu kukubaliana na matakwa yao ya kufanya mapenzi na watu wawili? Ouh Jamani akili yangu naona haifanyi kazi tena.Sijui nifanye nini” akawaza Happy na mara mlango ukafunguliwa Khumalo akaingia.Safari hii macho yake yalionekana mekundu na yasiyo na masihara hata kidogo.Happy akaingiwa na woga.Mwili ukamtetemeka
Happy dakika kumi zimekwisha na ninadhani tayari umekwisha fanya maamuzi” Akasema Khumalo huku akimuangalia Happy kwa macho makali sana.
Happy mwili ulimtetemeka na hakujua aseme nini
“Inaoneka bado hujaamua lolote.I’m so sorry Happy.” Khumalo akasema kwa masikitiko halafu akatoa simu yake na akabonyeza namba na kupiga
“Hallow Josh,amekataa kutoa ushirikiano endelea na mpango wetu,mpe Patrick chakula” akasema Kumalo halafu akamuangalia Happy kwa masikitiko
“I’m so sorry Happy.Muda mfupi toka sasa Patrick hatakuwa nasi tena.”
“Stop it !!!!!..Please stop it !!!!...” akapiga kelele Happy
“Please stop it.Dont kill Patrick.Niko tayari kufanya mnavyotaka.” Akasema Happy.Khumalo akamtazama kwa makini machoni halafu akatoa simu yake na kupiga
“Hallow Josh,subiri kwanza.Sitisha kwanza hilo zoezi” akasema Khumalo na kukata simu
“Happy nadhani sasa umeamua kumuokoa Patrick”
“Niko tayari kufanya lolote ili msimdhuru Patrick”
“Vizuri sana” akasema Khumalo huku akitabasamu
“Please don’t hurt Patrick.Hastshili mateso yoyote.Kama ni mateso naomba mnitese mimi”
“Hatukutesi Happy.Fanya kama ulivyoamriwa na utakuwa huru na hakuna mtu atakayemgusa Patrick” akasema Khumalo
“Niko tayari kufanya mnavyotaka lakini kwa sharti moja tu.Mtu huyo ambaye mnataka afanye mapenzi na mimi lazima atumia kinga”
“Usihofu kuhusu hilo Happy.Tunazingatia sana usalama wa afya yako.Jiandae Happy,baada ya muda watakuja vijana wawili unachotakiwa ni kuonyesha ushirikiano na jitahidi kuwaridhisha vijana hao.Baada ya hapo tutakuruhusu uende zako” akasema Khumalo halafu akatoka mle chumbani akimuacha Happy ameinama akilia
“Mpango mzima umekamilika .Mtashuhudia kila kitu muda si mrefu.Ninawahakikishia kwamba hili ni pigo kubwa kwa Happy” akasema Khumalo baada ya kurejea katika chumba walichokuwamo akina Linah
Baada ya dakika zipatazo kumi hivi,Khumalo akiwa ameongozana na vijana wawili waliojazia miili yao na wenye vifua vipana,wakaingia katika chumba alichokuwamo Happy.Vijana wale walikuwa wamezificha nyuso zao ili wasitambulike. Happy alipowaona akaogopa na kuanza kulia.
“Naombeni mnihurumie jamani.Nimewakosea nini hadi mnifanyie hivyo? Akalia Happy lakini Khumalo wala vijana wake hawakumsikiliza
“Happy nyamaza kulia.Futa machozi yako na tukamilishe zoezi letu ili tukurejeshe nyumbani kwenu.Nina imani familia yako ina wasi wasi mwingi sana sasa hivi” akasema Khumalo huku akiwasha taa kubwa iliyokuwamo mle chumbani na kukifanya chumba kiwe na mwanga mkali
“Happy kumbuka makubaliano yetu kwamba unatakiwa uonyeshe ushirikiano na uwaridhishe vijana wangu .Tumeelewana Happy? akasema Khumalo
“Ndiyo “ akajibu Happy
“Vizuri sana” akasema Khumalo na kutoka mle chumbani .Jamaa mmoja kati ya wale vijana walioletwa na Khumalo akamfuata Happy akaketi karibu yake na kumfuta machozi
“Fanya kama alivyokuamuru mkuu wetu.Endapo utaenda kinyume na matakwa yake anaweza akabadilika na akibadilika huwa ni mtu mbaya sana” akasema yule jamaa huku akianza kumtomasa Happy
“Please don’t hurt me “ akasema Happy
“Hautaumia mrembo.You’ll feel like you are in heaven” akasema jamaa mwingine
“Ninafanya hivi kwa ajili ya Patrick, kwa ajili ya kumlinda yeye “akawaza Happy halafu kijana mmoja akaanza kufungua vifungo vya lile shati lake dogo alilokuwa amevaa
“Leave me alone…Nitafanya mwenyewe” akafoka Happy na kumsukuma Yule jamaa halafu akasimama na kuanza kufungua vifungo vya shati lake huku machozi yakimtoka
“Mtu anayenifanyia kitendo hiki ni nani? Nimemkosea kitugani? akawaza Happy
Khumalo,Linah na Loniki walikuwa wameyaelekeza macho yao katika runinga ile kubwa mbele yao wakiangalia namna zoezi linavyoendelea.Baada ya kama dakika tano za mabishano kati ya Happy na wale vijana hatimaye vijana wale wenye nguvu walifanikiwa kumuangusha Happy kitandani na kuanza kumuingilia kwa zamu.Happy alilia sana wakati vijana wale wakiendelea na udhalimu wao juu ya mwili wake.Zoezi liliendelea huku likiendelea kurekodiwa pamoja na kupigwa picha.
Zoezi lilichukua zaidi ya dakika ishirini .Vijana wale walimaliza kazi waliyopewa huku wakihema kwa nguvu sana.Taratibu waliondoka mle chumbani na kumuacha Happy akiwa analia.
“kazi tayari” akasema Khumalo huku akitabasamu
“Ina maana kazi ndo imeishia hapa? Akauliza Loniki kwa mshangao
“Pesa zote hizi nilizotoa ni kwa ajili ya kazi hii ?
“Ndiyo Loniki.Lengo lako ni kumuadhibu Happy,? Akasema Khumalo
“Ndiyo” akajibu Happy
“Kama lengo lilikuwa hilo basi kazi imekwisha kwa leo na subiri kwa hatua itakayofuata.Kesho asubuhi nchi nzima itatikisika kwa taarifa hii.Ni skendo ambayo haijawahi kutokea hapa nchini” akasema Khumalo
“Kwa hiyo nini kitafuata baada ya hapa? Akauliza Loniki
“Niachie mimi kila kitu.Kesho asubuhi usiache kufuatilia vyombo vya habari,magazeti ya udaku na mitandao ya kijamii.Taarifa itakayokuwa inatawala ni ya picha za ngono za Happy” akajibu Khumalo.
Baada ya maongezi kadhaa na Khumalo Linah akamshika mkono rafiki yake Loniki wakaelekea katika gari ambalo liliwarudisha hadi ofisini kwa Linah ambako Loniki alichukua gari lake na kurejea nyumbani
Baada ya Loniki na Linah kuondoka ,Khumalo akaelekea katika chumba alimo Happy,akaufungua mlango na kuingia ndani.Happy alikuwa amelala kitandani akilia.Khumalo akamtazama kwa sekunde kadhaa halafu akapuliza dawa ya usingizi na kutoka mle chumbani
Baada ya dakika kumi na tano kupita toka Khumalo aipulize dawa ile katika chumba alichokuwamo Happy,Khumalo akarejea akiwa na vijana wake na kumkuta tayari Happy amelala fofofo hajitambui.Wakamuinua na kumpakia katika gari lake na kuondoka naye
“Kazi ya kwanza imekwisha.Kazi iliyobaki ni kuzisambaza picha na video.Naamini hadi kesho asubuhi zoezi hili litakuwa limekamilika na hatutakuwa na deni tena kwa Loniki“ akawaza Khumalo akiwa na vijana wake wakimrejesha Happy nyumbani kwao.Khumalo ndiye aliyekuwa ametangulia mbele na gari lake halafu gari la Happy lililokuwa linaendeshwa na kijana mwingine likafuata nyuma.Tayari Khumalo alikuwa anafahamu mahala anakoishi Happy kwani alikwisha mfanyia uchunguzi wa kutosha.
Saa saba kasoro za usiku waliwasili nyumbani kwa akina Happy.Kwa haraka haraka vijana wale wa Khumalo wakashuka katika gari la Happy.Kabla ya kushuka walimuwekea kitu fulani puani na kumzindua toka usingizini .Akapiga chafya mfululizo.Kwa haraka vijana wale wakaingia katika gari la Khumalo na kuondoka kwa kasi maeneo yale.
Mlio wa magari nje ya nyumba yake,ulimstua mzee Kibaho ambaye alikuwa macho mpaka mida hii akimsubiri mwanae arejee.Akatoka chumbani kwake na kwenda getini.Mbwa walikuwa wanabweka.Akachungulia nje kupitia uwazi mdogo na kuliona gari la Happy.Haraka haraka akafungua geti na kuliendea gari.Akachungulia ndani ya gari na kumuona Happy akiwa amelala kitini.Akapigwa na butwaa kwa hali aliyokuwa nayo .Happy alikuwa amelegea na mwili wake haukuwa na nguvu hata kidogo.Kwa haraka akamtoa mwanae garini na kumpeleka ndani na familia nzima ikaamka .Kila mtu alistushwa na hali aliyokuwa nayo Happy.Haraka haraka akaanza kupatiwa huduma ya kwanza.Hakuna aliyefahamu nini kimemsibu hata akawa katika hali ile.Ilikuwa ni hali ya kusikitisha sana.Daktari wa familia aliitwa akafika kwa haraka kuja kumuangalia Happy,akampima na kisha akampatia dawa na kumtaka akapumzike hadi asubuhi atakapopata majibu ya vipimo alivyochukua.
*******************
Kumekucha Tanzania.Ni saa moja za asubuhi, jijini Dar es salaam barabara zimesheheni watu na magari wote walikuwa wanaelekea katika shughuli mbalimbali za kila siku za uzalishaji mali.Katika vibanda na katika sehemu mbali mbali za kuuzia magazeti,kulikuwa na makundi ya watu waliokuwa wakihitaji magazeti ili kufahamu kulichoandikwamo asubuhi hii.Katika baadhi ya vituo vya kuuzia magazeti kulitokea ugomvi wa watu wakigombea magazeti kitu ambacho ni nadra sana kushuhudiwa.
Gazeti lililozusha mjadala asubuhi hii na kuwafanya watu wajazane katika vibanda vya kuuzia magazeti na wengine kufikia hata hatua ya kurushiana makonde ni gazeti la Mitikisiko,gazeti maarufu kwa kuandika habari za udaku na hasa zile zinazowahusu watu maarufu ndani na nje ya nchi.Siku hii ya leo gazeti hili lilipambwa na kichwa cha habari kilichobeba habari iliyozua gumzo nchini.
“HAIJAWAHI KUTOKEA” hiki kilikuwa ni kichwa cha habari kilichoandikwa kwa maandishi makubwa na chini yake kulikuwa na vichwa vingine vidogo vidogo.
“NI VIGUMU KUAMINI LAKINI KWELI”
“HUU NDIO UCHAFU WA MISS TANZANIA”
Vichwa hivi vya habari vilisindikizwa na picha kubwa ya Happy Kibaho,akiwa mtupu huku sehemu ya kifuani na chini ya kiuno zikiwa zimezibwa kwa rangi nyeusi.Picha nyingine ilimuonyesha Happy akiwa amelala kitandani akiwa na wanaume wawili waliozifunika nyuso zao ambao ilionyesha wazi walikuwa katika harakati za kufanya mapenzi.
“Mlimbwende aliyenyakua taji kubwa la urembo hapa nchini la miss Tanzania ambaye siku chache zilizopita amelivua taji hilo kutokana na kashfa ya kujihusisha katika ugomvi wa kumgombania mwanaume,na kusababisha kifo cha msichana aitwaye Veronika ,ameingia katika aibu kubwa baada ya picha na video yake ya ngono kuvuja” Haya yalikuwa ni maelezo ya utangulizi ya habari hii kubwa na kulifanya gazeti la Mitikisiko kuongoza katika mauzo kwa siku hii.Taarifa ile iliendelea katika ukurusa wa tatu huku ikipambwa na picha zinazomuonyesha Happy akiwa mtupu huku akifanya mapenzi na wanaume wawili waliozifunika nyuso zao katika mitindo tofauti tofauti..Ilikuwa ni aibu nzito isiyoelezeka .
Katika tovuti mbali mbali na mitandao ya kijamii,tayari video na picha za Happy vilianza kusambaa kwa kasi kubwa na kuwa gumzo mtandaoni.Watu walikuwa wanatumiana video na picha hizo za Happy akifanya ngono na wanaume wawili hadi katika simu za mikononi.Kutokana na kukua kwa teknolojia ya upashanaji habari ndani ya masaa machache tayari habari kuhusu Happy ilikwisha sambaa karibu nchi nzima.
Mlango mdogo katika geti la kuingilia nyumbani kwa akina Happy ulikuwa wazi,hivyo kumfanya mama Joseph jirani wa akina Happy,apite kama mshale na kuingia ndani huku akihema akiwa na gazeti mkononi
“Mama Happy ..!!! akaita mama Joseph .Alikuwa anahema huku jasho likimtoka.Mama yake Happy ambaye alikuwa katika kazi za usafi wa nyumba asubuhi hii,akaja kwa kasi baada ya kusikia sauti ya mama Joseph.
“Mama Joseph kuna tatizo gani? akauliza mama Happy kwa mshangao
“Mama Happy njoo huku” akasema mama Joseph huku akimvuta mama Happy kuelekea sebuleni.
“Mama Happy umeshapata taarifa?
“Taarifa gani mama Joseph? Mama yake Happy akazidi kushangaa
“Ina maana hakuna hata mtu mmoja aliyekupigia simu kukueleza nini kimetokea leo?
“mama Joseph mbona unanichanganya? Nini kimetokea?
“Soma gazeti hili” akasema mama Joseph huku akimpa mama Happy gazeti lile alilokuwa amelishika mkononi.Mara tu mama Happy alipolitupia macho akaanguka na kupoteza fahamu
Mama joseph akapiga ukulele mkubwa uliomstua mzee Kibaho aliyekuwa chumbani na kumfanya atoke haraka na kuelekea sebuleni kuangalia kumetokea nini.Alistuka baada ya kumkuta mkewe akiwa ameanguka chini akiwa hana fahamu
“Nini kimetokea? Akauliza mzee Kibaho huku akimuinamia mkewe.Mama Joseph hakuweza kujibu chochote alikuwa anatetemeka huku machozi yakimtoka.Haraka haraka mzee KIbaho akaanza kumpatia mke wake huduma ya kwanza.
Kelele zile za mama Joseph,zilimstua pia Happy .Alizisikia kelele zile akiwa usingizini na mwanzoni alidhani labda alikuwa ndotoni lakini alipofumbua macho aliendelea kuzisikia.Akaogopa pengine kuna jambo baya limetokea pale nyumbani kwao. Kichwa kilikuwa kizito na mwili wake ulimuuma sana.Alisikia maumivu makali sana sehemu za kinenani lakini akajikaza na kuinuka na kukaa kitandani.Akafikiri kidogo halafu akavaa nguo na kutoka mle chumbani na kuelekea sebuleni ambako ndiko kelele zilikokuwa zinatokea.Alistuka baada ya kumuona mama yake akiwa amelala chini hana fahamu.Baba yake alikuwa anahangaika kumsaidia ili aweze kurejewa na fahamu.
Mama Joseph na mfanyakzi wa ndani Pendo walikuwa wanalia kwa uchungu.Mara tu mama Joseph alipomuona Happy ameingia pale sebuleni akazidi kulia.Happy akatamani ajue kilichokuwa kimetokea na kumpelekea mama yake apoteze fahamu,akamfuata mama Joseph na kumuomba anyamaze ili aweze kumueleza nini kilichotokea
“Mama mdogo kuna nini? Nini kimetokea hapa? ..akauliza Happy kwa sauti dhaifu lakini mama Joseph hakujibu kitu na badala yake akamuonyeshea ishara alichukue lile gazeti lilikokuwa limeanguka chini.Taratibu Happy akainama na kuliokota ,akalikodolea macho.Mwili wote ukamtetemeka alipokuwa analisoma.Alikuwa ni kama mtu aliyeliona jitu la kutisha.Mara gazeti lile likaanguka chini na uso wa Happy ukajaa machozi .Taratibu bila kuongea na mtu yeyote akageuka na kutembea kwa kasi kuelekea chumbani kwake.
Mama Joseph aliyekuwa anamuangalia Happy kwa makini ,akaogopa sana kutokana na mstuko alioupata Happy.Akamfuata mzee Kibaho na kumuomba amfuate Happy
“Kuna nini? Happy amefanya nini? Akauliza mzee Kibaho huku akiendelea na jitihada zake za kumpatia huduma ya kwanza mke wake ili aweze kurejewa na fahamu
Mama joseph akaliokota gazeti lililoanguka chini na kumpatia mzee Kibaho
“Hili ndilo chanzo cha haya yote” akasema mama Joseph
Mzee Kibaho akaanza kulipitia lile gazeti na mara akahisi mikono yake ikimtetemeka.
“Ouh My God !!!” akasema mzee Kibaho na kwa haraka akainuka na akaelekea chumbani kwa Happy.Mlango wa Chumba cha Happy ulikuwa umefungwa.Akagonga lakini hakukuwa na dalili zozote za kuwepo mtu ndani.Akachungulia katika tundu la funguo na kuiona funguo ikiwa ndani.
“Happy fungua mlango..Fungua mlango mwanangu …” akasema mzee Kibaho lakini hakusikia dalili zozote za kuwepo mtu mle chumbani.Kwa kasi akakimbia kuelekea chumbani kwake akachukua ufunguo wa akiba na kuja kuufungua mlango akaingia ndani
“Ouh Mungu wangu ..!!!!!..Mzee Kibaho nusura aanguke kwa alichokiona mle ndani.Happy alikuwa amelala kitandani huku mapovu yakimtoka mdomoni.
“Happy..!! Happy.!!! Happy.!!!!!...akapiga ukelele mzee Kibaho huku akimtikisa Happy lakini hakuwa na fahamu hata kidogo,alikuwa anakoroma.
“Ouh Mungu wangu !!” akasema mzee Kibaho baada ya kuiona chupa ndogo yenye dawa ya kuulia panya ikiwa mezani.Haraka haraka akamuinua Happy na kukimbia naye hadi garini.Mama Joseph na Pendo wakapiga ukeleel mkubwa baada ya kuishuhudia hali ile ya Happy.Mzee Kibaho hakuwajali akawasha gari lake na kwa kasi ya aina yake akaondoka pale nyumbani huku akipishana na majirani waliokuwa wakiingia kwa kasi mle ndani baada ya kusikia kilio cha mama Joseph na Pendo.
“Please God.dont let my daughter die, Please save her” mzee Kibaho ambaye kwa mbali macho yake yalilengwa na machozi ,alikuwa akiyarudia maneno haya mara kwa mara wakati akiendesha gari kwa kasi kuelekea hospitali.Kila sekunde zilivyozidi kusonga mbele ndivyo hali ya Happy ilivyozidi kubadilika na kupoteza matumaini.Alikuwa anakoroma na povu jingi likiendelea kumtoka
Geti la hospitali ya Brahmaputra inayomilikiwa na daktari bingwa Makhresh Patel lilikuwa wazi .Gari la mzee Kibaho lilikuwa likija kwa kwendo wa kazi huku likiwa limewasha taa zote.Watu waliokuwa wamesimama karibu na geti walikimbia baada ya kuliona gari lile namba lilivyokuwa likija.
Namna gari lile lilivyoingia hospitali na sauti za matairi yakilalama kutokana na breki kali aliyofungwa,iliwafanya madaktari na wauguzi watoke nje na kushuhudia nini kilichotokea.Mzee Kibaho akashuka na kukimbia na kuwataarifu wauguzi kwamba kulikuwa na mgonjwa mahututi ndani ya gari.Kwa kasi ya aina yake,wauguzi wakampakia Happy katika kitanda na kumkimbiza katika chumba cha wagonjwa mahututi.Mzee Kibaho akaombwa asubiri nje.Bado mwili wake ulikuwa unamtetemeka kupita kiasi.Aliogopa sana.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO....