babu na mjukuu
JF-Expert Member
- Jun 23, 2016
- 3,949
- 6,752
Kawawa please sema japo neno moja.
Unashusha?
Unashusha?
Salute mkuu..big up..MISS TANZANIA
SEHEMU YA 64
MTUNZI😛ATRICK.CK
CONTACT0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Alois wakaondoka kuelekea kwa akina Happy
“Alois nitahakikisha wale wote waliomfanyia Happy kitendo hiki cha udhalilishaji wanafungwa gerezani” akasema Patrick
“Usijali kuhusu hilo Patrick.Kuna taarifa nimezipata leo kwamba Khumalo amekamatwa na polisi wa kimataifa akijaribu kuingia nchini Afrika kusini.Anarudishwa nchini kujibu tuhuma zinazomkabili.Haki itatendeka na jina la Happy litasafishwa na hesima yake itarudi” akasema Alois
ENDELEA……………..
Kila aliyekuwepo ndani alistushwa na hali aliyorudi nayo Happy.Japokuwa alikuwa amevaa miwani myeusi lakini michirizi ya machozi ilionekana katika mashavu yake.Mama yake ambaye alikuwa wa kwanza kumuona wakati akishuka garini akastuka na kudhani labda kuna taarifa mbaya.
“Happy kuna nini? Akauliza
Happy hakujibu kitu akatembea kwa kasi kuelekea chumbani kwake,mama yake akamfuata
“Happy mbona umetustua namna hiyo? Kuna jambo gani huko utokako? Patrick mzima?
“Patrick mzima mama” akajibu Happy huku akifuta machozi
Mama yake akavuta pumzi ndefu baada ya kusikia kwamba Patrick ni mzima
“Ouh ahsante Mungu nilifikiri kuna tatizo limetokea.Sasa kinachokuliza kitu gani?
“Mama tutaongea baadae.I need to be alone “ akasema Happy,Mama yake akamtazama na kutoka mle chumbani.
Baada ya mama yake kutoka mle chumbani Happy akafunga mlango halafu akalifungua sanduku lake akatoa bahasha iliyokuwa na picha ya Patrick.Akaitazama picha ile kwa muda huku machozi yakimtoka.
“Patrick kwa nini kila mara ninateseka kwa ajili yako? Nimejitahidi kukusahau lakini nimeshindwa.Nimeendelea kuwa mtumwa wa penzi lako.Nimejaribu kuendelea na maisha yangu bila ya wewe lakini nimeshindwa kwa sababu kila ninapojaribu kupiga hatua ,wewe hutokea mbele yangu na kunirudisha nyuma.Hii ina maanisha kwamba nitaendelea kuteseka hadi mwisho wa maisha yangu.Patrick kama ungefahamu ni namna gani ninakupenda usingethubutu kunitamkia maneno yale makali.” Akasema Happy kwa sauti ndogo huku akiitazama ile picha.Akaiweka picha ile pembeni,na kufuta machozi
“You don’t deserve a second chance.!! Tafadhali ondoka mbele ya macho yangu Malaya mkubwa wewe.!!!
Maneno haya aliyotamka Parick yakajirudia tena kichwani kwake.Akafuta machozi
“Patrick midomo yako mizuri ambayo siku zote imekuwa ikinitamkia maneno matamu na kunifanya nijione malkia katika himaya ya mfalme lakini leo hii siamini kama imetamka maneno hayo mazito. Hata kama nilikosea,hukupaswa kunitamkia maneno kama yale” akasema Happy kwa uchungu
“I saw your eyes.May be you are right that I’ve to stay away from your life.” Akaendelea kusema Happy akaishika tena picha ile ya Patrick
“Pengine hii inaweza kuwa njia bora zaidi kwa mimi kuendelea na maisha yangu nikiwa na amani bila ya wewe.You are right I don’t deserve you.Kila mara unapokuwa nami lazima ukutane na matatizo.Ni wakati sasa wa kuachana nawe Patrick.Ni wakati wa kufungua ukurasa mpya wa maisha yangu.Bado wako watu wanaonipenda na kunijali.Nilimuahidi Mike kwamba nitakaporejea Marekani tutafunga ndoa.Nadhani hili ndilo jambo la msingi kwa sasa.Nitajifunza kumpenda Mike kwa moyo wangu wote kwa sababu naye ananijali na kunithamini na zaidi ya yote ananipenda sana.I have to let you go Patrick.It hurt but I have to do it and leave you alone.” Akasema Happy huku akiichana katikati picha ile ya Patrick
Wakati Happy akiwa chumbani kwake,nje ya nyumba yao ikasikika honi ya gari.Mama yake akaenda kufungua mlango na kustuka kwa kuiona sura ya Patrick .Mara moja akajua kuna jambo limetokea.
“Patrick !!..akasema kwa mshangao
“mama shikamoo” akasema Patrick
“Marahaba Patrick.Karibuni ndani” akasema mama yake Happy na kuwakaribisha Patrick na Alois ndani
“Habari za hapa ? akauliza Patrick
“Habari za hapa nzuri.Vipi unaendeleaje?Nimestuka sana nilipokuona” akasema mama Happy ambaye bado aliendela kuwa na mstuko kwa ujio ule wa Patrick
“Namshukuru Mungu ninaendelea vizuri.” Akajibu Patrick halafu kikapita kimya kifupi
“Mama Happy tumemkuta? Akauliza Patrick
“Happy yupo.Ngoja nikamute”
Mama Happy akainuka nakuelekea chumbani kwa Happy.Aligonga mlango na Happy akaufungua.Alistuka kwa hali aliyomkuta nayo.
“Happy una tatizo gani?
“Sina tatizo lolote mama.Tatizo langu limekwisha” akajibu Happy huku akifuta machozi
“Patrick amekuja,anahitaji kukuona”
Happy akastuka na kumuangalia mama yake
“Umemwambia kwamba nipo?
“Ndiyo Happy.Nimemweleza kwamba upo ndani”
“Mama naomba mwambie kwamba sitaki kuonana naye.Sina muda wa kuonana naye na aondoke zake“
“Happy ! ! mama yake akasangaa
“Nini kimetokea? Kwa nini hutaki kuonana na Patrick leo? Mmekorofishana ?
“Mama sitaki kuonana na Patrick.Mimi na yeye basi.Nashukuru yuko mzima na anaendelea vizuri sasa.Sitaki kusikia lolote kuhusiana na Patrick.It’s over between us.” akasema Happy.Mama yake akamsogelea na kumshika mkono
“Niambie Happy nini kimetokea? Kila siku unaondoka hapa na kwenda kwa Patrick lakini leo umerudi unalia.nini kimetokea huko ?
“Usihofu mama hakuna kitu chochote kibaya kilichotokea .Nimeamua tu sitaki kuonana na Patrick tena.Mwambie aondoke haraka hapa nyumbani” akasema Happy.mama yake akarejea tena sebuleni
“Patrick nini kimetokea ? Happy aliniaga kwamba anakuja kwako leo asubuhi lakini nikashangaa anarudi akiwa analia.Kila nikimuuliza hataki kunijibu.Nini kimetokea kati yenu? Mmegombana? Nimemweleza kwamba uko hapa na unahitaji kuonana naye lakini amekataa kata kata na amesema uondoke haraka sana wewe na yeye basi.Nini kimetokea? Tafadhalio naomba uniweke wazi”
“Mama ni kweli kuna jambo limetokea kati yangu na yeye na ndiyo maana nimekuja hapa ili tuweze kuliongea na kulimaliza.Naomba unisaidie mama niweze kuonana naye”
“Nashindwa nikusaidiaje mwanangu kwa sababu Happy amekataa kabisa kuonana nawe.”
Patrick akainama na kufikiri kisha akasema
“Mama naomba unipeleke chumbani kwa Happy nikaongee naye huko huko”
“Tafadhali baba naomba usiende huko.Naogopa kusijetokea matatizo”
“Hakuna tatizo lolote linaloweza kutokea.Naomba unipeleke mama” akasisitiza Patrick.Mama yake Happy akamuongoza Patrick hadi chumbani kwa Happy na kumkuta Happy akiwa amejiinamia kitandani akilia
“Mama kwa nini umemleta huyu chumbani kwangu ??Akauliza Happy ka ukali
“Happy naomba muongee na kumaliza tofauti zenu.Patrick amekuja hapa ili muongee na msawazishe kilichotokea.Tafadhali nawaombeni msigombane.Ongeeni mambo yenu na muelewane”
“Mama naomba mtoe huyu mtu nje.Sitaki kumuona tena katika maisha yangu” akasema Happy kwa ukali
“Mama naomba utuache wenyewe” akasema Patrick na mama yake Happy akatoka mle chumbani.Patrick akafunga mlango
“Patrick go out.Get out of my room” akasema Happy kwa ukali
“Happy naomba unisikilize .Nimekuja hapa kuongea na wewe.Nimekuja kuomba samahani kwa maneno niliyoyasema.Happy naomba unisamehe kwa maneno yote niliyoyasema.” Akasema Patrick
“ Patrick sihitaji kuongea nawe kitu chochote tena.tafadhali ondoka”
“Happy naomba unielewe.Sintaondoka humu chumbani mpaka pale utakaponisikiliza ninachotaka kukwambia.Tafadhali Happy usilifanye jambo hili kuwa gumu kwangu. Tafadhali naomba unisikilize malaika wangu.” Akasema Patrick huku akipiga magoti kumsihi Happy atulize hasira na wakae waongee
Happy akastuka ghafla na kumtazama Patrick usoni.
“what you’ve just said? Am I your angel ? No you are mistaken.Mimi ni mwanamke Malaya na siwezi kuwa malaika wako.Please Patrick stand up and go and don’t dare look for me again in your life.It’s over between us.It’s been all lies.You said yourself ” akasema Happy
“Happy tafadhali naomba unisikilize.Nilitamka maneno yale machafu kutokana hasira nilizokuwa nazo.Sikuwa naufahamu ukweli halisi.Nisamehe sana Happy”
“Now do you know the truth?
“Yes ! I know the truth.Alois told me everything”
“Do you believe what he told you?
“You tell me! Is all that true? Akauliza Patrick .Happy akainama chini akafuta machozi
“Yes..thats the truth”
“Ouh Happy ! Kwa nini hukunieleza mapema? Kwa nini ukaniacha nikiteseka muda huu wote na kujenga chuki juu yako? Nilitamani hata kujitoa uhai wangu kwa kitendo kile nikiamini ulikifanya kwa makusudi.Endapo ungekimbia na kunieleza ukweli mapema wala tusingefika hapa tulipofika sasa hivi.” akasema kwa uchungu Patrick
“Nilijua Savanna atakueleza ukweli wote kwa sababu yeye alifahamu kila kitu kilichotokea na yeye ndiye aliyeratibu safari ya mimi kuondoka hapa nchini kwenda Kigali Rwanda.” Akasema Happy
“Baada ya tukio lile nilipatwa na uchungu mkubwa sana nilikata tamaa hata ya kuendelea kuishi.Nilifanya jaribio la kujitoa uhai kwa kunywa sumu lakini niliwahishwa hospitali na wakayanusuru maisha yangu.Patrick naomba uelewe kwamba haikuwa dhamira yangu kuondoka na kukuacha peke yako ukiteseka kwa kosa ambalo nililitenda mimi lakini kutokana na tukio lile nililazimika kuondoka kuikwepa aibu kubwa niliyoipata.Nilikata tama kabisa ya kuendelea na mahusino yetu na niliamua kukukabidhi kwa Savanna .Niliamini anakupenda na wewe unampenda na kwake utakuwa katika mikono salama.Siku zote nilizokaa mbali nawe niliteseka sana na sikuwa na amani hata kidogo hadi nilipokuja kukuona tena .Patrick naomba unisamehe kwa matatizo yote niliyokusabishia.Nimekuwa chanzo cha matatizo mengi katika maisha yako.Nina imani pamoja na mateso na maumivu yote niliyokuletea utatafuta ndani ya moyo wako nafasi ya kunisamehe ili niweze kuishi kwa amani.Najua siwezi kuulipa wema wako wote ulionitendea na sijui nifaye nini ili niweze kuifuta taswira hii mbaya ambayo tayari imejengeka kichwani kwako. Nilichokifanya ni kitua mbacho hakisameheki japo sikuwa na namna nyingine ya kufanya.Niliamini ninafanya vile kuokoa maisha ya mwanaume nimpendaye.Nimekuumiza sana Patrick.” Happy akashindwa kuendelea akaanza kulia.Patrick akamfuata na kumkumbatia
“Please Happy forgive me for everything.Sikuwa naufahamu ukweli.” akasema Patrick
“Patrick ni mimi ndiye unayetakiwa kunisamehe kwa kuwa nimekukosea sana na kukusababishia mateso makubwa.Patrick I deserve any punishment from you and the best punishment is to stay away from you…” akasema Happy
“Shhhhhhhhhhh..!!!! Please Happy don’t say anything.Kamwe hustahili mateso au adhabu ya aina yoyote ile ila waliokutenda kitendo kile na kukusababishia mateso makubwa namna hii lazima wapate adhabu kali sana.” Akasema Patrick huku akiendelea kumkumbatia Happy kwa nguvu
“so have you forgiven me? Akauliza Happy
“Yes ! Yes ! I’ve forgiven you.Have you forgiven me? Akauliza Patrick
“Niliumia sana kwa maneno uliyonitamkia leo.Nimelia sana lakini mwisho wa siku pamoja na machungu yote bado nimejikuta nikiendelea kuwa mtumwa kwako.Nitaendelea kuwa mtumwa kwako kwa maisha yangu yote .Patrick kamwe siwezi kuwa na hasira au kinyongo kwako.You are forgiven” akasema Happy.Wakakumbatiana kwa nguvu zaidi
“Happy pamoja na yote yaliyotokea kati yetu lakini moyo wangu unashindwa kabisa kukusahau.Hata pale nilipoamini kwamba tayari umeamua kunikimbia na nikaamua kuwa na Savanna bado niliendelea kukukumbuka.Happy tumepitia matatizo mengi na kila pale tulipotenganishwa na nguvu za dunia lakini tunajikuta tumekutanishwa tena katika mazingira ya ajabu ajabu.Happy we’re meant to be together.Nothing than death can separate us in this world.” Akasema Patrick
“Patrick do I still have a place in your heart? Akauliza Happy
“Happy bado nafasi yako ni kubwa sana katika moyo wangu.Siku zote utaendelea kuwa na nafasi ya pekee kabisa ndani ya moyo wangu.Happy nakupenda sana na nitakupenda daima” akasema Patrick
“Ouh Patrick I love you so so so much” akasema Happy na kumbusu Patrick kisha wakakumbatiana kwa nguvu.
“After today nothing will separate us again” akasema Patrck.Happy machozi yakiwatoka wote wawili
“Nini kinakuliza Happy? Akauliza Patrick
“Huwezi kujua ni jinsi gani nilivyoteseka kwa ajili yako Patrick.Siamini kama leo hii niko nawe tena. Niliamini tayari nimekwisha kupoteza na sintakuona tena maishani mwangu lakini kwa nguvu za Mungu niko nawe tena .Nakubaliana nawe kwamba hakuna kitu kinachoweza kututenganisha zaidi ya kifo katika hii dunia.Tumeumbwa ili tuwe wawili” akasema Happy.Patrick akamuangalia usoni na kusema
“Niliambiwa na Savanna kwamba ulikuwa umerudiana na Mike.Ni kweli? Akauliza Patrick.Swali lile likamstua Happy akamuachia Patrick na kutazama chini.
“Ni kweli.Nilirudiana na Mike kwa sababu alinisaidia kuingia tena Marekani Alinishawishi nirudiane naye tena na kwa kuwa sikuwa na mategemeo ya kurejea tena Tanzania nilikubali kurudiana naye.Naomba unielewe Patrick kwamba nilirudiana na Mike si kwa ajili ya mapenzi bali kwa ajili ya kutafuta msaada .I lied to him.I’ll have to say sorry.Najua ataumia sana lakini sina namna nyingine.Siwezi tena kurejea Marekani na siwezi kuendelea kuwa naye tena.Nitaongea naye na atanielewa.Hawezi kunifuata Tanzania kwa sababu amepigwa marufuku asikanyage ardhi ya Tanzania” Akasema Happy.Patrick akaonyesha wasi wasi
“Patrick naomba unielewe kwamba katika dunia hii mwanaume nimpendaye ni wewe pekee na ambaye umejaa moyoni mwangu.Tafadhali naomba unipokee tena katika moyo wako.Naomba nafasi nyingine tena” akasema Happy
Patric akamvuta Happy karibu yake akamkumbatia
“Huna haja ya kuomba nafasi ndani ya moyo wangu.Siku zote nafasi yako ipo hapa ndani ya moyo wangu.Karibu tena ndani ya moyo wangu Happy” akasema Patrick na kumpa Happy busu zito kisha wakakumbatiana kwa nguvu.Ukurasa mpya ukafunguliwa tena kati ya Patrick na Happy
* * * *
“Mimi Patrick ,katika imani,uaminifu na upendo,nakuchukua wewe Happy Kibaho kuwa mke wangu wa ndoa,kushirikiana nawe mipango ya Mungu katika maisha yetu ya pamoja tukiunganishwa katika kristu,Kwa msaada wa Mungu naomba anipe nguvu niwe kiongozi imara wa kiroho katika maisha yetu,katika raha na shida,ugonjwa na afya,furaha na huzuni,mpaka kifo kitutenganishe.Ninakupa kila nilichonacho na mapenzi yangu yote katika jina la yesu kristu.Kwa pete hii ninafunga kiapo changu cha kukupenda wewe Happy Kibaho,Mungu anisaidie kukilinda kiapo hiki,kwa jina la baba na la mwana na la roho mtakatifu Amen.”
Kanisa zima lililokuwa limefurika watu likalipuka kwa kelele za shangwe na vigele gele vingi baada ya Patrick kula kiapo chake mbele ya kanisa huku akimvisha Happy pete ya ndoa.Hii ilikuwa ni siku yao kubwa sana ambayo waliiota kwa muda mrefu.Ni siku waliyofunga pingu za maisha.Miezi mitano imekwiwha pita toka walipokutana tena.Hakukuwa tena na kikwazo chochote cha kuwazuia kufunga ndoa hivyo taratibu zikafanyika ili kuwawezesha kufunga ndoa.
Baada ya kutoka kanisani,ilifuata sherehe iliyohudhuriwa na watu wachache akiwemo Sarah dada yake Veronika pamoja na wazazi wa Savanna.Sherehe hii ilihusisha baadhi ya ndugu wa karibu na marafiki wachache tu.Baada sherehe kumalizika walipanda ndege kuelekea kisiwani Zanzibar kwa ajili ya fungate.
MIEZI 12 BAADAE
Ni saa tatu za usiku katika hospitali ya St Theresa,watoto mapacha wa kike wanazaliwa.Furaha ya Happy ilikuwa haielezeki kwa kuwapata watoto hawa mapacha.Mumewe Patrick ambaye alikuwepo pale hospitali alikuwa pia na furaha iliyopitiliza.
“Wataitwa Babrah na Brenda” akasema Patrick akitaja majina ya watoto wake
Maisha yaliendea kuwa ya furaha kubwa kwa familia hii.Mwezi wa pili baada ya kujifungua ,Mahakama ilitoa hukumu kwa wale wote waliohusika na tukio lililosabisha kifo cha Savanna.Mahakama ilimtia hatiani Loniki kwa kosa la kuua kwa kukusudia na kumhukumu adhabu ya kifungo cha maisha jela.Khumalo ambaye naye alishiriki katika mipango ya Loniki ya kumteka na kumdhallisha Happy,pamoja na kujihusisha na biashara za madawa ya kulevya,ujambazi na kutengeneza filamu za ngono alihukumiwa kifungo cha miaka hamsini gerezani na kazi ngumu.Vijana sita ambao walikuwa wakishirikiana naye walifungwa miaka thelathini kila mmoja kwa kujihusisha na biashara ya madawa ya kulevya.Mahakama pia ilimtia hatiani Linah kwa kujihusiha na njama za kuteka na kudhalilisha na kumhukumu miaka mitano jela.
Baada ya adhabu ile kutolewa,vilifuata vilio toka kwa ndugu na jamaa wa washtakiwa.Mzee Francis Kito na familia yake ambao walikuwepo mahakamni walipeana mikono ya pongezi na Patrick
“haki imetendeka” akasema mzee Kito huku akimkumbatia mke wake
“mahakama imetenda haki” akajibu Patrick
“Siwezi kusema kwamba nimefurahi kwa adhabu hii kwa sababu bado haiwezi kunirejeshea mwanangu Savanna.Lakini hata hivyo hizi ni sheria za nchi na lazima zifuatwe.Kwa upande wangu mimi nimekwisha wasamehe wale wote waliomuua mwanangu na sina kinyongo nao tena” akasema mzee Francis Kito.
Wakati wakiendelea kupeana pongezi kwa hukumu ile ,mara akatokea Sarah ambaye macho yake yalikuwa mekundu.Alikuwa Amelia sana.
“Pole sana Sarah.Hata mimi namuonea huruma sana Loniki lakini hakuna namna nyingine ya kufanya ili kugeuza maamuzi haya ya mahakama.” Akasema Patrick
“Hakuna lolote tunaloweza kulifanya Patrick.Mahakama imefanya kazi yake.Loniki alitenda kitendo cha kikatili sana.Nikikumbuka siku ile ninasikia uchungu mkubwa sana alitaka kutuua sote wawili.Ninaumia moyoni kumuona ndugu yangu wa damu akienda kutumikia adhabu ya kifungo cha maisha gerezani lakini kwa upande wa pili anastahili adhabu ile kutokana na mambo aliyoyafanya.Siku zote nilikuwa nikimmuonya na kumkanya kuhusu mambo ya kulipiza kisasi lakini hakunisikia.” Akasema Sarah
“Binafsi nimekwisha msamehe kwa kosa alilolitenda.Sina kinyongo naye tena cha aina yoyote” akasema Patrick
“hata mimi nimekwisha msamehe muda mrefu” akasema Sarah huku akijifuta machozi
“Patrick nimekuja kukuaga.Ninaondoka nchini”
“Unaondoka nchini? Unakwenda wapi?
“Mume wanu amehamishiwa nchini Holland kikazi kwa hiyo na mimi sina budi kumfuata.Kilichoniweka hapa hadi muda huu ni kusubiri hukumu hii .Kwa sasa baada ya hukumu kutolewa sina tena kitu cha kuendelea kusubuiri.Yanibidi niondoke nikaungane na familia yangu.Nadhani itanisaidia pia kulisahau tukio lile lililotokea.Nilinusurika kuuawa na ndugu yangu wa damu.Tukio lile limeniathiri sana kisaikolojia.Nadhani nahitaji mapumziko na kutuliza akili yangu mbali na hapa nyumbani.Tutakuwa tukiwasiliana mara kwa mara” akasema Sarah
“Nakubaliana nawe Sarah.Tukio lile ni moja ya tukio baya kabisa na unahitaji mapumziko.Nakutakia kila la heri huko uendako.Tuzidi kuombeana na kuwasiliana.Nitakuwa nikimtembelea mama mara kwa mara.Bado ni mama yangu na kwa sasa ambapo Loniki na wewe nyote hampo anahitaji mtu wa kumfariji kwa hiyo nitachukua nafasi yenu.Kwa heri Sarah” akasema Patrick akakumbatiana na Sarah wakaagana akaondoka
Hakukuwa tena na kitu chochote cha kusubiri pale mahakamani Patric na mkewe Happy wakaingia garini na kuondoka.
MWISHO…..
MWISHO WA SIMULIZI YA MISS TANZANIA,NATUMAI MMEBURUDIKA NA SIMULIZI HII.NAWASHUKURU SANA WASOMAJI WOTE KWA KUTENGA MUDA WENU NA KUTEMBELEA PAGE HII KUSOMA HADITHI,AHSANTENI SANA POLENI MLIOTOA MACHOZI KATIKA BAADHI YA SEHEMU ZA HADITHI HII,AHSANTENI TEAM PATRICK NA TEAM HAPPY PIA WOTE MLIOSHARE HADITHI HII
Episode ya 11 siioni na 12
Shukran za kipekee!