10
Ni kengele ya simu ya chumbani ndiyo iliyomstua Patrick toka katika jinamizi la mawazo.Tangu amefika katika hoteli hii ya Kobe Village amekuwa ni mwingi wa mawazo .Kutokana na wasi wasi mwingi aliokuwa nao aliamua kujiliwaza kwa kunywa mvinyo laini.Aliweka chini glasi yake ya mvinyo na kuiendea simu ile ya chumbani.“Haloo” Aliita kwa kitetemeshi“Haloo mapokezi hapa.Samahani kaka mgeni wako uliyesema atawasili tayari amefika.Je utakuja kumchukua au tumlete moja kwa moja chumbani?Patrick akapumua kwa nguvu ,mapigo ya moyo yakabadilika.
“Mleteni chumbani “Patrick akasema,akaurudisha mkono wa simu kisha akapumua kwa nguvu,kijasho chembamba kilimtoka .Wakati akitafakari na kuuona huu ni kama muujiza kukutana tena na Happy mara kengele ya mlangoni inalia.Taratibu akajivuta na kwenda kuufungua.
Kwa takribani dakika kadhaa wote wawili walipigwa na butwaa kila mmoja akimshangaa mwenzake.Halafu wakakumbatiana kwa nguvu huku wote wawili machozi yakiwatoka..Muhudumu aliyekuwa ameongozana na Happy akapigwa na mshangao kwa hali ile aliyoina.Hisia za penzi zito zilijidhihirisha wazi wazi baina ya wawili hawa..Tukio hili liliamsha kumbukumbu kubwa na ya pekee maishani mwao.Hakuna aliyetaka kumwachia mwenzake.Patrick akamshika Happy taratibu na kumkalisha katika sofa lililokuwamo humo chumbani.Uso wake wote ulikuwa umejaa machozi.“I cant believe this”Patrick akanong’ona.Happy hakujibu kitu midomo yake ilikuwa ikimtetemeka.Kila alipotaka kuongea alishindwa.
“Is that you Patrick? Happy akajitahidi kusema huku akifuta machozi
“Its me Happy.Its real me” Patrick akajibu
“Ni kama ninaota.bado siamini kama nimekuona tena” happy akalalama.“Ouh Patrick..Patrick.!!..let me touch you hands and prove you are not a ghost" akasema Happy .Bado machozi yaliendelea kumtoka.”Akaushika mkono wa Patrick akautazama
" Patrick my angel..I love you so much " Aliwaza Happy huku ameushika mkono wa Patrick . Patrick alikuwa amesimama akimkodolea macho Happy asiamini alichokuwa akikiona mbele yake..Baada ya kama dakika kumi hivi za ukimya ,tafakari na hisia nzito kwa kila mmoja ,hatimaye Patrick akaufungua mdomo na kusema“Welcome back my sunshine”“Welcome back to my heart Patrick” Happy akanong’ona kwa sauti laini sana.“Huu ni muujiza mkubwa sikutegemea katika maisha yangu kama nitakuja kukuona tena.,lakini Mungu ni mkubwa na ameweza kutukutanisha tena.” Akasema patrick na kauli ile inaamsha kilio kwa Happy “Happy nyamaza usilie.Umelia vya kutosha uliponipoteza ,I’m here now.”“Patrick ninaumia sana kwa kila nikikumbuka mateso niliyoyapata kwa kukupoteza.Awali ya yote naomba unisamehe kwa yote yaliyotokea kipindi cha nyuma.Najua bado una kinyongo moyoni na hata mimi nilikuwa na fundo kubwa moyoni kwa kitendo ulichonifanyia lakini tayari nimekusamehe.Naomba na wewe utafute ndani ya moyo wako jinsi ya kunisamehe.Patrick najua ulifungwa kwa ajili yangu.Mapenzi yako makubwa kwangu ndiyo yaliyosababisha ukafungwa.Uliua kwa kuniokoa mimi nisidhalilishwe.”Happy akaangusha kilio tena.Patrick akatoa kitambaa na kumfuta machozi .“Patrick halikuwa kusudio langu mimi kwenda kusoma Ulaya na kukuacha peke yako.Nilikataa kwenda lakini ukanishauri niende kusoma kwa ajili ya kutengeneza maisha bora kwangu na kwako.Ni…….”Kabla hajaendelea simu yake ikaita.Akafuta machozi haraka haraka na kuitoa katika mkoba wake mdogo.Aliangalia namba za mpigaji na kukuta ni Mike mchumba wake.Kwa hasira akakata simu na kuizima kabisa.Patrick akakiangalia kitendo kile lakini hakukitilia maanani .“Patrick ”Happy aliita huku akimwangalia machoni.“Yes” Patrick akaitika“Ninajua itakuwia ngumu sana kwa wewe kama binadamu kunisamehe kwa kile kilichotokea,japokuwa tayari mimi nimekwisha kusamehe….”“Please Happy “Patrick akadakia.“Naomba usiseme maneno hayo tena.Yanaumiza sana.Ni kweli nilikuwa na hasira sana juu yako kwa kitendo ulichonifanyia lakini huu si muda wake kuyaongelea hayo.”Happy akamvuta Patrick karibu akamkumbatia na kumpiga mabusu mfululizo.Patrick akahisi kitu kama chaji za umeme zimepita mwilini mwake.
* * * *
Saa kumi na moja za jioni dege la shirika la ndege la British airways lilitua katika uwanja wa kimataifa wa Julius Nyerere Dare s salaam.Lango la ndege lilifunguliwa na abiria wakaanza kushuka.Miongoni mwa abiria waliokuwamo katika dege hili ni Mike cambell,kijana mtanashati mwenye kila sifa ya uzuri,ambaye kila binti amuonaye angetamani awe naye.Leo hii alivaa suruali ya jeans iliyofifia na shati zuri la mikono mifupi.Kwa ujumla alikuwa amependeza vilivyo.Mike Cambell mchumba wa Happy alikuwa akitokea Marekani .Lengo kuu la safari yake hii ya tanzania lilikuwa ni kuja kumfariji mpenzi wake Happy katika maradhi yanayomsumbua pamoja na kumpongeza kwa kufanikiwa kulitwaa taji la Miss Tanzania. Baada ya kukamilisha taratibu za uwanjani Mike akatoka na kulakiwa na dereva wake aliyetoka katika ubalozi wa Marekani.Alitegemea pengine angeweza kumuona Margreth mdogo wake Happy pale uwanjani kwa kuwa alikwisha mtaarifu juu ya ujio wake lakini mpaka anamuamuru dereva aondoe gari hakumuona mtu yeyote. Toka uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere ,safari ilikuwa ya moja kwa moja mpaka nyumbani kwa akina Happy .Anapafahamu vizuri mahala pale kwani si mara yake ya kwanza kwenda Moyoni alikuwa akiomba Mungu amsaidie aweze kukuta hali ya Happy inaendelea vizuri.Walifika nyumbani kwa akina Happy geti likafunguliwa wakaingia ndani.baada ya kushuka ndani ya gari akakutana na mama yake Happy .“wow ! Mike karibu sana” Alisema mama yake Happy akimkaribisha Mike kwa furaha..Mike akaomba maji ya kunywa ya baridi sana ili aweze kulipooza joto kubwa alilokuwa analisikia.Baada ya kunywa glasi mbili za maji akauliza aliko Happy na Margreth.Mama yake Happy akapatwa na kigugumizi cha ghafla.“Margreth amekwenda katika mizunguko yake lakini Happy yeye amesafiri kidogo”“amesafiri?? Mike akauliza kwa mshangao“Ndiyo kasafiri” mama Happy akajibu huku akijitahidi kuuficha wasi wasi aliokuwa nao “Kasafiri toka lini ?” Mike akauliza“kasafiri leo mchana”Mike akashika kichwa akapumua kwa nguvu." Mbona umestuka Mike Ina maana hamkuwasiliana akakwambia kuwa atasafiri ? mama Happy akamuuliza Mike ambaye alionyesha kuchanganyikiwa baada ya kusikia Happy amesafiri.“Hapana mama sikuwasiliana naye. Kama niivyokuwa nimekueleza katika simu sikutaka afahamu kuhusu ujio wangu.Nilitaka nimfanyie mshangazo.Lakini Margreth pia nilimtaarifu juu ya safari yangu.Happy alisema anakwenda wapi?” Mike akauliza“Hakuniambia ni wapi anakwenda .Baada ya kujisikia nafuu aliniambia kwamba amepata safari ya dharura ya kwenda nje ya Dar es salaam.Hakuniambia safarii hiyo inahusu kitu gani.Ujumbe aliouacha ni kwamba kama ukija umsubiri hadi atakaporejea nadhani mdogo wake atakuwa alimdokezea kwamba unakuja”Mike hakujibu kitu akatoa simu yake na na haraka haraka akazitafuta namba za Happy akapiga.Simu ilikuwa inaita ,akatabasamu.“Yuko hewani lakini anachelewa kupokea” alisema mikeSimu iliita bila kupokelewa.Akapiga tena mara ya pili na ya tatu na ikakatika.Akapiga tena na mara hii ikawa haipatikani kabisa .Mike akapiga tena na tena lakini jibu likawa lile lile simu haipatikani tena.“amezima simu” akasema Mike akaishiwa nguvu akakaa sofani.Baada ya dakika kadhaa za ukimya Mike akaomba aondoke akapumzike kwa sababu tayari kichwa chake kilikuwa kimevurugika.Dakika kama kumi hivi toka Mike aondoke pale nyumbani Margreth akawasili.Alimkuta mama yake akiwa amekaa sebuleni akiwa mwingi wa mawazo.“mama unaumwa? Margreth akaulizaMama yake hakujibu kitu,alimwangalia usoni kwa makini na kumuomba aketi.“Margreth hebu nieleze Happy kaenda wapi?Najua ni lazima unafahamu alikoenda dada yako”“mama mimi sijui kitu chochote.Kwani wewe alikuaga anakwenda wapi?“Hakutaka kuniambia anakwenda kupumzika wapi.Lakini wewe ni lazima utakuwa unajua kwa sababu toka ametoka hospitali ni wewe tu ambaye unaongea naye.”“Hapana mama sijui kitu chochote kile,alivyokwambia wewe ndivyo alivyoniambia mimi”“Na vipi kuhusu shemeji yako Mike? Ina maana hukujua kama anawasili leo ili uende kumpokea?“Du! mama nimesahau kabisa kama Mike anakuja leo.Vipi ameshafika?“Muda mrefu sana.Ila nyie watoto!!!Yaani mwenzenu anakuja hamtaki hata kwenda kumpokea.Halafu kitu kingine cha ajabu,amempigia simu Happy mbele yangu na Happy kakataa kupokea na mwishowe akazima simu kabisa.Hivi kuna kitu gani kinaendelea?“Mhhhh” Margreth akaguna.Akamwacha mama yake hapo sebuleni na kuingia chumbani kwake.akajifungia na kujaribu kumpigia Happy lakini simu yake ilikuwa tayari imezimwa.akajitupa kitandani.
* * * *
Saa moja na nusu jioni Andrew akiwa nyumbani kwake na mpenzi wake Vick mara simu yake ikaita.Akaichukua na kuangalia mpigaji ,alikuwa ni mama yake Patrick.Moyo ukaanza kuenda mbio.“Du! Kazi imeanza”Alisema kwa sauti ndogo ambayo Vick aliisikia.“Haloo mama” akasema Andrew“andrew mwanangu hivi huyu mwenzako ana kitu gani jamani kinachomsumbua? mpaka sasa hivi sijamuona hapa nyumbani na wala hajanipigia simu na simu yake ameizima kabisa.Nimekwenda nyumbani kwake hayupo,Veronika amekaa hapa mpaka ameamua kuondoka mtoto wa watu .Sielewi ni kwa nini Patrick anaanza kutuweka roho juu juu dakika hizi za mwisho.Maandalizi ya harusi yake yanaelekea ukingoni lakini yeye haonyeshi kujali.Hebu niambie baba ulifanikiwa kumuona?”“Mama kwa kweli nimehangaika sana na hata ofisini sijakaa kwa ajili ya kumtafuta Patrick na katu siwezi kukuficha mama Patrick sijui alipo kwa sasa.Hata mimi alinieleza kuwa ana dharura leo lakini hakunifafanulia ni dharura gani hiyo.Hata mimi nimemtafuta sana katika simu hapatikani nadhani lile tatizo la simu yake bado linaendelea” Andrew akasema“andrew na wewe usitake kuniudhi kama huyu mwenzio,usinieleze kabisa upuuzi huo wa simu.Patrick si mtu wa kushindwa kununua simu nyingine,angenieleza hata mimi ningemnunulia simu mpya.Hivi kwa nini mnataka kuzichezea akili zetu nyie watoto?“Mama naomba unipe muda zaidi mpaka kesho asubuhi nitakuwa nimepata jibu wapi alipo Patrick na nitakujulisha ikiwezekana nimlete nyumbani mimi mwenyewe”“Sawa baba jitahidi umpate kwa sababu anatuweka roho juu juu kweli huyu mwenzio.”“Ok mama nitajitahidi”“Haya Andrew usiku mwema”“Ahsante mama”Uphh.!!!!.. Andrew alipumua kwa nguvu baada ya kumaliza kuongea na mama yake Patrick“:Kuna nini andrew? Vick akauliza“Patrick haonekani”“etiii....!!! ???” Vick akauliza kwa mshangao,akainuka akashika kichwa kwa mikono yake yote miwili.“Mungu wangu ! yuko wapi sasa jamani” Vick akashangaa“hata mimi sielewi Vick .Mama yake ndiyo kanipigia simu sasa hivi anaulizia kama nimemuona”“Ina maana hujaonana naye leo?” Vick akauliza huku amemkazia macho Andrew“Nilionana naye asubuhi ya leo na toka hapo sijaonana naye tena na simu yake haipatikani.”“Hakukueleza kuwa anakwenda wapi?“alinidokeza kuwa ana dharura ila hakunifafanulia zaidi”Vick akafikiri kidogo kisha akasema“andrew ,wewe ndiye rafiki mkubwa wa Patrick.Hakuna kitu ambacho huwa mnafichana.Hainiingii akilini eti Patrick awe na dharura halafu ashindwe kukueleza .You know something..."“Tafadhali Vick nimesema sijui Patrick alipo ! Mimi kaniambia hivyo kuwa ana dharura sasa siwezi kuingilia masuala yake binafsi.Umenielewa? akasema Andrew huku akionyesha wazi kwamba hakuhitaji tena maswali toka kwa Vick.Vick akamwangalia Andrew kwa sekunde kadhaa kisha akaketi sofani.Baada ya kutafakari kwa muda Andrew akaamua kumpigia simu Veronika“Haloo shemeji” Andrew akasema baada ya Vero kupokea simu“andrew I’m confused.Ni kwa nini lakini Patrick ananifanyia hivi?Nimemkosea kitu gani hadi ananitenda hivi? Vick akasema kwa hasira “Vero,shemeji yangu hebu tuliza hasira kidogo.” Andrew akamsihi“andrew I’ll go crazy if I cant see Patrick tonight.maandalizi ya safari yamekwisha kamilika.Ni yeye tu ndiye anayesubiriwa.What am I going to do?? !!! Please Andrew help me to know where Patrick is.Hapatikani hata katika simu…”Vero akashindwa kujizuia akaangua kilio“Vero please naomba unisikilize.Mama naye kanipigia simu sasa hivi akimuulizia Patrick.Mimi nilionana naye asubuhi ya leo.mama alinipigia simu na kuniagiza niende kwake nikamueleze kuwa anahitajika nyumbani.Nilimkuta akijiandaa kutoka na akanieleza kuwa amepata dharura asubuhi hiyo hivyo angekuja nyumbani mchana.Toka hapo sijaonana naye tena.”“Ouh My God! Sasa nitafanya nini mimi ? Vero akasema“Usijali Vero bado naendelea kumtafuta na mpaka kesho nitapata jibu yuko wapi”“Jitahidi Andrew ““Ndiyo Vero najitahidi sana kuwasiliana na rafiki zetu mbali mbali ili nijue yuko wapi.Kama hatatokea hadi kesho kwa nini basi nisikusindikize badala yake ? akatania Andrew“Unasemaje????!!! Vero akauliza kwa ukali “Nasema hivi kama Patrick hajatokea mpaka kesho unaonaje kama nikakusindikiza katika safari hiyo mliyopanga kwenda wote?“Nilikuwa nakuamini sana Andrew lakini kumbe wewe na rafiki yako wote ni kitu kimoja tu”Vero akajibu kwa hasira na kukata simu.
Andrew alichanganyikiwa kwa kitendo cha Vero kukata simu.Ni wazi alikuwa amekasirika.Alijilaumu sana kwa kujiingiza katika matatizo makubwa kama haya.Kwa takribani dakika mbili nzima alibaki ameduwaa ameishikilia simu yake.“andrew kuna nini?Sauti ile ya Vick inamstua toka katika jinamizi la mawazo lililomkumba ghafla.“Hakuna kitu Vick,nilikuwa nikiongea na Vero”“Kuhusu nini?“Kuhusu safari yao ya kwenda London kufanya shopping ya harusi yao”“Yeye anasemaje ?“Hana la kufanya kwani Patrick haonekani.Mimi nilijitolea kumsindikiza”“Yeye amejibuje?“Amekasirika na kukata simu halafu ameizima kabisa”“Huna haya Andrew,eti umsindikize mchumba wa mtu London.Hivi unatumia akili kweli Andrew? Wewe ndiye mchumba wake? Hata ningekuwa mimi nisingekujibu.Tena amekuheshimu sana hakukutukana.Hebu achana na mambo ya watu tuangalie ya kwetu.”akasema VickAndrew hakujibu kitu.Akainamisha kichwa chini kwa sekunde kadhaa.“Vick I’m confused”“Kwa nini?“na hali nzima ya mambo jinsi yanavyokwenda”Vick akamsogelea Andrew akamkumbatia na kukilaza kichwa chake katika kifua kipana cha andrew .“Usijali Mpenzi Patrick atarejea tu muda si mrefu.”Vero akasema huku akiipitisha mikono yake laini mwilini mwa andrew kiuchokozi.Andrew alielewa alichokuwa akihitaji mpenzi wake.Akamuinua na kwenda naye chumbani
* * * *
Ni saa tatu za usiku katika hoteli ya Kobe Village chumba namba 68 kilikuwa na mwanga hafifu wa bluu.Sauti ya muziki laini ilisikika kwa mbali.Chumba chote kilikuwa kikinukia uturi mzuri wenye harufu ya ajabu ya kuvutia.Chumba hiki kwa sasa kilikuwa katika mkao wa mahaba mazito.Juu ya kitanda kikubwa watu wawili walikuwa wamekumbatiana wakiwa katika mahaba mazito.“Patrick” Happy akaita kwa sauti laini,nyororo ya kimahaba huku akiupitisha mkono wake kifuani kwa Patrick.
“Yes Happy “ Patrick akaitikiaHappy ambaye tayari macho yake mazuri meupe yalikuwa yamelegea kama amekula kungu akasema“Patrick najilaumu sana kwa kuamua kuondoka na kukuacha peke yako.Narudia tena kuomba msamaha kwa kitendo hiki cha kukuacha peke yako na wala sintachoka kufanya hivyo tena na tena kwa sababu ni kitendo ambacho kilisababisha mimi na wewe tukatengana.Kama nisingeondoka tungekuwa na maisha yetu ya raha mstarehe.Baada ya miaka mingi kupita hatimaye leo hii nahisi amani na raha ya ajabu.Raha ambayo nimeikosa kwa miaka mingi ile raha ya aina yake kama niliyokuwa nikiipata kipindi tukiwa shuleni.Msisimko niliokuwa nao kipindi kile pindi nikiwa karibu nawe bado haujapotea.Nikiwa nawe nahisi raha kila mahali” Patrick akatabasamu akausogeza mkono wake usoni na kurudisha nyuma nywele ndefu za binti huyu mrembo
“Happy hata mimi ninajisikia hivyo hivyo.Sikutaka kuamini moja kwa moja kuwa hauko tena maishani kwangu.Nilimuomba Mungu anisaidie ili kabla siku zangu hazijaisha hapa duniani niwe nimekuona walau kwa mara ya mwisho.Mungu amesikia sala yangu na tayari amenijibu.Leo hii niko nawe tena.” Patrick akamvuta Happy karibu zaidi na kumpiga busu zito mdomoni. " Happy nadhani ni wakati muafaka sasa wa kuongelea masuala yetu namna tulivyojikuta tukitengana" akasema Patrick.Happy akamuangalia na kusema
‘Patrick naomba niwe wa kwanza kukuuliza na tafadhali naomba uwe wazi kwangu.usinifiche kitu hata kidogo”“C’mon baby uliza chochote usihofu ,kwako hata siri za baba yangu nitakupa” akasema Patrick na Wote wawili wakacheka.“Umeshaanza utani wako nawe” akasema Happy“Usijali mama uliza”Happy akatulia kidogo kana kwamba anakumbuka kitu kisha akauliza.“Hivi Patrick ni kwa nini uliamua kunidangaya kuwa umekufa?Patrick akastuka,akainuka na kukaa kitandani jasho likaanza kumchuruzika.“What !!! .me?…Dead?…..why ? Patrick alijikuta akitamka maneno mfululizo huku akimtazama Happy..“Happy nashindwa kuelewa ,eti nilifanya nini??!!……..Happy aliuona mstuko mkubwa wa wazi katika sura ya Patrick akaanza kuogopa kwani alisikia Patrick ana matatizo ya moyo.akamsogelea akamkumbatia na kumbusu akamsugua sugua shingo na kuhakikisha ile hamaki aliyokuwa nayo Patrick imekwisha halafu akaendelea“Kama unakumbuka kipindi nimeondoka kwenda kusoma tulikuwa tunawasiliana vizuri sana.Hii ilinipa faraja na kuupunguza umbali uliokuwapo kati yetu.Lakini ilitokea siku moja ambayo kwa kweli ni vigumu sana kuisahau katika maisha yangu.Ni siku hii ndiyo iliyobadili kabisa maisha yangu,siku niliyopokea barua toka kwa dada ambaye alijifahamiha kuwa alikuwa ni jirani yenu mlipokuwa mkiishi Sumbawanga.Katika barua hiyo alisema kuwa anasikitika kunitaarifu kuwa eti umefariki dunia ukiwa gerezani kwa maradhi ya kuhara”Patrick akasimama na kushika kiuno.“Happy please tell me it’s a joke”Happy akamtazama kisha akasema.“Its not a joke Patrick.Baada ya kupata taarifa ile nilipatwa na mstuko,sikutaka kusoma tena,na wala sikuona tena faida ya kuishi.You were my everything.Kwa bahati nzuri baba na mama walisafiri haraka sana na kuja kunifariji na kunifanya niendelee kuishi kwani vinginevyo ningekwisha jiua muda mrefu.Patrick ,ilipita miaka mingi bila ya kuwa na furaha na amani moyoni mwangu.Furaha yangu ulikuwa ni wewe pekee.Nilikuwa nikiomba usiku na mchana kwamba taarifa ile isiwe ya kweli na kwamba siku moja ungejitokeza lakini siku zikaenda na hukutokea.Taratibu baada ya miaka kadhaa kupita nikakubaliana na matokeo kuwa tayari umekwisha fariki.Hatimaye baada ya kumaliza masomo nikarudi nyumbani na kitu cha kwanza kukifanya ilikuwa ni kutafuta mahala ulipozikwa.Nilienda mpaka Sumbawanga nikauliza nikaambiwa kuwa familia yako ilikwisha hama muda mrefu .Nikaenda tena kule Iringa ulikokuwa umefungwa nikaambiwa kuwa ulihamishwa gereza na kupelekwa Songea.Nikachapa mguu hadi Songea katika gereza ulilohamishiwa pale ndipo niipoufahamu ukweli.Niliwekwa wazi kuwa ulimaliza kifungo chako na ukaachiwa huru na hukufa gerezani na kwamba kuna uwezekano mkubwa ukawa mzima.Pamoja na kuufahamu ukweli huo nilikonda kwa kujiuliza swali moja nililokosa mtu wa kunipa jibu,kwa nini unifanyie vile?.Sikujua sababu ya wewe kuamua kunifanyia vile yaani kusingizia umekufa na kunifanya mimi niishi maisha ya kuteseka miaka yote hii.Nimekuwa nikimuomba Mungu anikutanishe nawe ili walau nifahamu sababu iliyopelekea unifanyie vile.Patrick you were the only man I real loved and trust.I gave myself to you .Please tell me why you did that ,I’ll understand.” Happy aliongea katika hali ya uchungu sana huku ameiweka mikono yake kifuani kuonyesha machungu aliyokuwa akiyapata Patrick jasho lilikuwa likimtiririka kama mtu aliyemaliza mbio ndefu.Ingawa chumbani mle mlikuwa na kiyoyozi lakini hakikusaidia kulipunguza joto alilokuwa akilisikia baada ya kuipata taarifa ile.Alisimama na kuzunguka zunguka humo chumbani.“Happy ! sijui hata nianzie wapi.I’m confused”Happy akamsogelea akachukua kitambaa na kumfuta jasho .
“Please tell me Patrick.Tell me everything.I’ll understand.Najua mimi ndiye sababu ya wewe kuingia gerezani na pengine hukufurahi mimi kwenda Marekani.lakini sikustahili adhabu hii uliyonipa kwa miaka hii yote ” Happy akasema kwa sauti ya upole sana“Happy sina hakika kama utaniamini na kunielewa.Ukweli ni kwamba haya yote uliyoyasema wewe kwangu mimi ni mageni kabisa.Hakuna ninachoweza kukisema au kukitolea maelezo..Niliyatoa maisha yangu kwa ajili yako ,iweje leo nikudanganye nimekufa? bado hainiingii akilini . Happy kumbuka nilikuwa radhi hata kuua japo sikukusudia kwa ajili ya upendo niliokuwa nao kwako iweje leo niamue kutunga uongo wa kututenganisha ? Nashindwa kupata jibu.Katika maisha yangu hakuna kitu ambacho sikupenda kukiona kama kukuona ukiumia na hilo unalifahamu fika.Sasa kwa nini basi niamue kuumiza moyo wako kwa kusema uongo eti nimekufa? Akasema Patrick. Akatulia akafuta jasho.Happy akalifungua sanduku lake dogo akatoa bahasha ambayo ilikwisha anza kuchakaa pengine ni kutokana na kushikwa mara nyingi sana.akatoa karatasi iliyokuwamo ndani ya ile bahasha na kumkabidhi Patrick.“Barua yenyewe yenye taarifa ya kifo chako hii hapa. hebu isome”Patrick akatumia dakika kadhaa kuisoma barua ile.Alipomaliza kuisoma akarudia tena na tena.Uso wake wote ukajaa machozi.Midomo ikawa ikimtetemeka kwa hasira,akashindwa kitu cha kuongea.“Umeona Patrick? Hivyo ndivyo ilivyokuwa.Hiyo ndiyo barua ambayo iliyabadili kabisa maisha yangu .” akasema Happy Kikapita kimya cha dakika kadhaa hapo ndani,kila mmoja akiwaza lake.Patrick akakumbuka toka siku ya kwanza alipokutana na Happy katika kituo cha basi Mbalamaziwa Iringa na hapo ndipo ulipoanzia urafiki wao.Picha za uhusiano wao wakiwa shuleni zikamjia mpaka siku ile alipomuokoa Happy toka katika mikono ya wabakaji .Akakumbuka pia siku alipohukumiwa kifungo cha miaka mitano gerezani na mpaka siku Happy aliyokuja kumuaga kuwa anakwenda Marekani kusoma.Ghafla akakumbuka siku alipopata taarifa toka kwa Veronika kuwa Happy ameolewa na hatarudi tena Tanzania.Alikumbuka jinsi alivyozimia kutokana na taarifa ile.Machozi yakamtoka.
" Vero..!! Vero.." akawaza Patrick akakohoa kidogo kisha kwa sauti yenye kitetemeshi akasema“Happy nimekusikia na nimekuelewa naomba sasa na mimi nikupe hadithi yangu.Naomba unisikilize kwa makini na unielewe”
“Baada ya wewe kwenda kusoma Marekani,huku nyuma nilihamishwa gereza na kupelekwa Songea katika gereza jipya kabisa.Siku moja nilikuwa nimepangiwa kutengeneza mazingira katika nyumba ya mkuu wa gereza.Siku hiyo mkuu wa gereza hakuwepo.Nikiwa naendelea na kazi alitokea dada mmoja ambaye alionyesha kuwa na roho ya huruma sana.Alinikaribisha chai nzuri mchana huo akanikaribisha chakula.Ni dada mcheshi,mchangamfu,na mwenye huruma.Kwa mujibu wa maelezo yake ni kuwa pale alikuwa amekuja kumsalimu mjomba wake ambaye ndiye yule mkuu wa gereza.Baadae alijitambulisha kwangu kuwa anaitwa Veronika.Taratibu mimi na Veronika tukawa marafiki.Nilimhadithia mkasa mzima wa maisha yangu kwa sababu nilitokea kumwamini.Ukiacha wazazi wangu Veronika ndiye mtu pekee aliyekuwa akinipa moyo,kunifariji na kunipa ushirikiano wa kutosha.Muda wake ulipoisha alirudi Dar es salaam kuendelea na shughuli zake aliahidi kuwa angekuwa anakuja mara kwa mara kunitazama.Kwa hiyo nikamuomba yeye awe ni kiungo baina yetu yaani mimi na wewe.Kwa kuwa yeye aliahidi kuja mara kwa mara kuniona nikaona ni bora mawasiliano yetu yaliyokuwa yameanza kufififa yawe yakipitia kwa Veronika.Nikaandika barua na kumkabidhi ili aende akaiposti afikapo Dar es salaam.Katika barua hiyo nilikutaarifu kwamba nimehamishwa gereza na kukuelekeza utumie anuani ya Veronika.Siku moja ambayo sintakuja kuisahau alikuja Vero na kuniambia kuwa alikuwa na taarifa ambazo si njema sana.Nilijikaza kiume na kumuomba anieleze.Vero aliniambia kuwa haukuwepo tena katika chuo kile ulichokuwa ukisoma.Akaendelea kusema kuwa alielekezwa mahala ulipoamia na akakupigia simu lakini ukamjibu kwa kejeli kuwa huna muda na mimi tena, na wala huna mategemeo ya kurudi tena Tanzania.Alizidi kudai kuwa alimtumia binamu yake aishiye huko huko marekani kufanya uchunguzi na akagundua kuwa tayari ulikuwa umeolewa na tayari ulikuwa ni mjamzito.Nilianguka na kuzimia Sikutaka kuamini moja kwa moja taarifa zile lakini kwa kuwa nilikuwa kifungoni sikuwa na la kufanya ili kuupata ukweli.Niliwaomba wazazi wangu wanisaidie kufanya uchunguzi juu ya jambo hili lakini wao ndio hawakutaka kabisa hata kunisikia nikilitamka jina lako .Siku zilikwenda bila ya mawasiliano yoyote baina yetu na taratibu nikaanza kuukubali ukweli kuwa haupo tena na mimi.Mpaka siku namaliza kifungo changu sikuwa nimepata barua yoyote toka kwako.Nilimaliza kifungo na nikaanza upya tena kuyatengeneza maisha yangu.Nikasoma ,nikamaliza na hatimaye nikaanza maisha yangu ya kujitegemea.Siku moja nikiwa natazama luninga ,warembo waliokuwa wakishiriki fainali za kumtafuta mrembo wa Tanzania walikuwa wakijinadi nilikuona ukipita.Sikuamini nilistuka nikaanguka na kupoteza fahamu.Na ni hapo ndipo matatizo ya moyo yalipoanza.Hakuna mtu yeyote anayefahamu nini chanzo cha maradhi yangu zaidi ya rafiki yangu wa pekee Andrew.Nilijitahidi ili niweze kukuona siku ile ya shindano lakini kwa bahati mbaya mara tu uliponiona na wewe ukapatwa na mstuko ukaanguka na kupoteza fahamu.”Patrick akanyamaza akamwangalia Happy usoni.Macho yake yalijaa machozi.Hadithi ya Patrick ilimchoma moyo sana.Donge kubwa likamkaba kooni.Hakuwa na la kufanya zaidi ya kulia.Patrick akamuonea huruma ,akamkaribia na kumfuta machozi .“nyamaza Happy .Nyamaza mrembo wangu.Usilie tena.”Ilikuwa vigumu kwa Happy kunyamaza kutokana na hasira alizokuwa nazo.“Nashindwa kunyamaza kutokana na ukatili niliofanyiwa .Kwa nini walitufanyia hivi ? Ni bora mtu aliyenifanyia hivi angeniua kabisa kuliko kuniacha nikiteseka kwa muda mrefu namna hii.”Happy akaendelea kuliaKimya kikapita .Patrick akasema“Happy tayari nimekwisha pata jibu.It is Vero who did all this.Huyu msichana anayejiita Grace ni Veronika.Nimeutambua mwandiko wake.Ni yeye ndiye aliyetutenganisha.Alifanya hivi kwa sababu anazozijua yeye mwenyewe.Nafikiri mpaka hapa hakuna wa kumlaumu mwenzake kwa yaliyotokea.Kila mmoja amekwishapata picha halisi ya nini kilichotokea.Sisiti kusema kuwa Veronika ndiye chanzo kikubwa cha sisi kutengana.Nina imani kubwa kuwa ni yeye tu ndiye aliyeuvuruga uhusiano wetu kwa kutunga uongo huu mkubwa.Hakuna mwingine anayeweza kufanya kitu kama hiki zaidi yake.Mwandiko huu katika hii barua ni wake ”Patrick akainuka na kuelekea mezani huku akiwa amefura kwa hasira.“I hate you Vero.I hate you..!!”Alitamka maneno haya kwa hasira sana .Happy aliyekuwa amekaa kitandani akaogopa.Hakuwahi kumuona Patrick akiwa katika hasira namna ile.Taratibu akamsogelea na kumshika mkono.“Calm down Patrick.Its ok.”“Happy I hate this woman so much.Ametutesa kwa kipindi kirefu sana.Kwa nini? she must pay for this.This devil must pay so dearly.Ameudhulumu moyo wangu kuishi na furaha kwa miaka hii yote.Amenisababishia mateso makubwa.Alinifanya nikakuchukia..Ouh Vero kwa nini ulifanya hivi? ” Patrick akawaza akiwa na hasira.Happy akamwacha Patrick atulie kwanza na baada ya dakika kadhaa akasema.“Patrick”Patrick akastuka na kumwangalia Happy .“Patrick” Happy akaita tena.“Yes Happy nakusikiliza”“After all that happened do you still love me?Patrick akastuka kwa swali lile,akainuka na kumsogelea zaidi Happy ,akamshika mikono yake yote miwili akamtazama usoni.“Happy ” akatulia kidogo halafu akaendelea.“World do change,weather and climate do change,people do change,everything do change but Patrick never change.I’m the same Patrick you knew,who loved you that much.Nothing has changed.Pamoja na yote yaliyotokea lakini I’ve never stoped loving you not for a second.Now that I’ve known the truth I love you even more.Do you still love me Happy?Kauli ile inamfanya Happy atoe machozi.Midomo ikamtetemeka akashindwa kuongea.Patrick akamuangalia machoni na kumuuliza tena.“Happy am I still have a place in your heart ?Happy akajikaza na kusema“Patrick you were my first man I loved.You were the fisrt man to win my heart.I gave you my heart,my body,soul and everything.You were my angel,my Hero.No body will ever win my heart than u did.I’m everything I am because you loved me Patrick. Hakungekuwa na Miss Tanzania Happy Kibaho leo kama si kwa penzi lako na kujitoa kwako kwa ajili yangu.Pamoja na yote yaliyotokea Patrick I still love you more and more.You still have chance in my heart.You are the only man that I truly love,but I’m sorry Patrick….”Happy akashindwa kujizuia kulia kwa sauti.“Sorry? Sorry for what Happy ? Patrick akauliza“Its complicated”Patrick taratibu akahisi kama nguvu zinamuisha“Complicated?How” akauliza Patrick“Patrick baada ya kuamini kuwa tayari umekwisha kufa basi nikaamua kuwa na mpenzi mwingine.Mike cambell ndiye mpenzi wangu niliyenaye kwa sasa na tayari amekwisha nivisha pete ya uchumba.I’m so sorry Patrick.Sikukusudia kufanya hivi.”Patrick alihisi kama vile kila kitu mle ndani kilikuwa kikizunguka.Hakuamini kama ni kweli anaweza kumkosa Happy kirahisi namna ile.Akaunyoosha mkono wa Happy na kuangalia kidoleni.Ni kweli Happy alikuwa na pete ya uchumba kidoleni.Patrick akaingalia huku machozi yakimlenga lenga.wakati Patrick akiwa ameduwaa akiiangalia ile pete ya uchumba kidoleni Happy akasema .“I’m right.Its complicated.Hata wewe tayari una mchumba. Kila mmoja tayari amekwisha amua kuendelea na maisha yake.Kutokana na hali ilivyokuwa hakukuwa na matumaini ya kuonana tena.Hivyo hakuna mtu wa Kulaumiwa kwa maamuzi haya kati yetu sisi wawili.Kila mmoja hakuwa na njia nyingine zaidi ya kuamua kusahau yaliyopita na kusonga mbele na maisha yake.Kwa hiyo Patrick veronica ndiye mchumba wako?Patrick akakabwa na donge kubwa kooni.akababaika ajibu nini.“Happy ” Patrick akaita
“Happy nasikitika sana.Halikuwa kusudio langu kufanya hivi lakini kwa kipindi hicho sikuwa na jinsi ya kufanya niliamini kuwa tayari ndoto yetu ya mimi na wewe kuwa pamoja imeshapotea .Niliamini moja kwa moja taarifa za vero na nikawa na hasira sana juu yako kwa kuamini kuwa ulikuwa umevunja ahadi yetu.Kweli kwa wakati huo ni Veronika pekee ndiye aliyekuwa mfariji wangu mkubwa.Ukaribu wetu ukaongezeka na taratibu tukajikuta tukihama toka katika urafiki wa kawaida na kuwa wapenzi.Kwa kiasi kikubwa alinisaidia kusahau mateso na maumivu niliyoyapata juu yako.Uhusiano wetu umedumu kwa muda mrefu sasa na tukaona ni bora tufunge ndoa kabisa.Hivi sasa tunavyoongea tayari maandalizi ya harusi yetu yako katika hatua za mwisho.Nafikiri mwezi ujao tarehe za kati kati nitafunga ndoa na vero.”Happy alishindwa kujizuia kutoa kilio kikubwa.Patrick akamkumbatia.“Patrick my first love.Patrick my angel,siwezi kuuzuia uchungu huu mkubwa ninaousikia moyoni mwangu.Ninaumia mno kwa kitendo hiki alichonifanyia mwanamke mwenzangu.Ni bora hata angeniua kabisa kuliko kunifanyia ukatili huu mkubwa.Patrick you were my life,and my breath.Veronika has taken you from me, .Sikutegemea kama mwisho wetu ungekuwa hivi..Why she did that? Why ??”Happy aliongea kwa uchungu mwingi sana huku machozi mengi yakimtiririka.“Patrick nimefurahi kuufahamu ukweli.Sikulaumu kwa yaliyotokea.Hukuwa na kosa na wala wewe hupaswi kunilaumu mimi.Kwa kuwa kila mmoja tayari amekwisha anza maisha yake mimi naona ni bora iwe hivyo.Kila mmoja atabaki ni historia kwa mwenzake.Ninachokuomba mpende zaidi Veronika.Kamwe usimfanyie jambo lolote lililo baya.Alifanya kosa,alidanganya na hii yote ni katika kulipigania penzi lako la kweli.Nakubali kushindwa.Sitaki kushindana na Vero sipendi na yeye aje aumie kama nilivyoumia mimi.Nafikiri mateso yangu ni makubwa na sidhani kama anaweza kuyavumilia kama mimi.Mimi namwachia Mungu kwani yeye………….”“Happy ”Patrick akadakia“No Patrick don’t say anything yet.I’m deeply hurt.” akasema Happy kwa uchungu mkubwa.Chumba kilichokuwa katika hali ya mahaba mazito muda mfupi uliopita ,sasa kilikuwa ni sehemu yenye majonzi makubwa.Vilio vya chini chini ndivyo vilisikika.Ilikuwa ni hali yenye kuhuzunisha sana kwa wapenzi hawa wa zamani.Happy akamvuta Patrick karibu yake akamkumbatia kwa nguvu.Akamwachia na kumtazama usoni.Kwa sauti yenye kukwama kwama huku akitokwa na machozi akamwimbia wimbo“Don’t,don’t go to your heart how feels.Don’t be afraid of dreams not real,Close ur eyes,pretend it’s just the two of us again,Make belief, this moment’s here to stay,Touch, touch me the way you used to do,I know, I could be lie right here with you,From now on ,you will be with someone else instead of me,So tonight, let’s feel these memories.So for the last, hold me now don’t cry, don’t say u were just, hold me now………Time, time will be kind once we’re apart,And ur tears, tears will no have place in ur heart.I wish I,I could say how much I’ll miss you when ur gone,All my love for yoy will go away……………Happy akashindwa kuvumilia akaangua kilio kikubwa.“No Happy !! No !……This cant be”Patrick akasema kwa hasira.
" Siwezi kukuacha kamwe.Wewe ni malaika wangu.Nakupenda sana Happy.Nakupenda zaidi ya unavyofikiri." akasema Patrick akiwa amemkumbatia Happy kwa nguvu.
" Patrick I love you too..but what are we going to do ? akazidi kulia Happy.Patrick akaendelea kumbembeleza.Happy alikuwa ameumizwa kupita kiasi.
* * * *
Ulikuwa ni usiku mrefu sana na mgumu kwa Mike cambell.Kitendo cha Happy kuondoka bila kumuaga anakwenda wapi kilimchanganya akili .Kilichompa wakati mgumu zaidi ni kitendo cha Happy kumkatia simu na kisha kuizima kabisa .Kitendo hiki kilimuumiza mno.Haijawahi kutokea katika uhusiano wao.“I real love you Happy no matter what”Alitamka Mike kwa sauti huku akijimiminia mvinyo katika glasi.Toka amefika chumbani kwake leo hii amekuwa akinywa pombe kali kwa dhumuni la kuupunguza mzigo wa mawazo aliokuwa nao.Alikaa tena sofani,akawaza,akachukua simu na kubonyeza namba za Happy lakini jibu likawa ni lile lile.Simu ya Happy haikuwa ikipatikana.“Kwa jinsi ninavyomfahamu Happy lazima kutakuwa na jambo linalomsumbua akili yake.Mara nyingi akiwa na jambo linalomsumbua huwa hapendi usumbufu.Lakini ni bora angeongea nami japo hata kidogo tu na kunitoa wasiwasi .”Mike akapiga funda kadhaa za mvinyo.“I know you need to be alone for a while Happy .I will wait here for you till you come back.I hope you will be back soon.Be safe there my angel”Mike alikuwa akiongea maneno haya kwa sauti .Ni wazi alikuwa ameanza kulemewa na kilevi.Wakati Mike akiwa katika mtihani mgumu na kuamua kupoteza mawazo kwa kunywa mvinyo mkali,mambo yalikuwa magumu zaidi kwa Veronika.Usiku huu alikuwa katika kitanda chake akijigeuza geuza, macho yakiwa makavu na mekundu kwa kulia.Akainuka na kwenda kulifungua dirisha akachungulia nje kana kwamba kuna kitu alikuwa akitegemea kukiona.Alikaa hapo dirishani kwa muda mrefu akiziangalia nyota na mwezi.Machozi hayakuwa yakitoka tena alikuwa Amelia sana mchana kutwa.Ni mlio wa simu yake ndio uliomstua toka katika mawazo mazito.Taratibu akaichukua simu yake na kutazama mpigaji.Alikuwa ni mama yake Patrick.“Hallo mama”“Veronika mwanangu unaendeleaje?“mama naendelea hivyo hivyo tu.Vipi kuna habari yoyote mpaka sasa hivi?“Hapana Veronika mpaka sasa sijapata taarifa zozote kuhusu mwenzio.Ila nina wazo moja”“Ndiyo mama nakusikiliza”“Yawezekana huyu Patrick akawa katika dharura zake kama anavyodai.Mimi naona sisi kuendelea kumsubiri ni kupoteza wakati wetu.Nionavyo mimi hataki kwenda huko Uingereza ndio maana amekuwa akikimbia kimbia.Kwa hiyo Vero mwanangu ili tusiendelee kupoteza muda zaidi wewe itakubidi tu uende peke yako ufanye shopping .Hatuna njia nyingine ya kufanya.Vumilia Vero namfahamu Patrick vizuri atatulia tu muda si mrefu.”Veronika akatulia akatafakari kwa sekunde kadhaa kisha akasema“Ok nimekuelewa mama.Nitafanya hivyo.Safari ni kesho saa tano asubuhi.Ila sintachukua muda mrefu sana nadhani baada ya siku tatu au nne nitarejea.siwezi kukaa mbali na Patrick kwa kipindi kirefu na hasa wakati huu anaoumwa umwa”“Sawa Vero nashukuru sana mwanangu kwa kukubali kufanya hivyo.Nitakuja kukusindikiza kabla hujaondoka” akasema mama yake Patrick na kukata simu.
" Patrick kwa nini unanifanyia hivi? Nimekukosea kitu gani hadi unipe adhabu hii ya kukesha macho? Nimelia machozi mengi kwa ajili yako na yote hii ni kwa sababu nakupenda sana .Nakupenda kuliko kitu chochote kile." akawaza Vero kisha akaelekea katika kabati lake kubwa la nguo na kuanza kuchagua nguo chache atakazoondoka nazo
* * * *
Hatimaye Patrick akafanikiwa kumbembeleza Happy hadi akanyamaza.Akampatia glasi ya maji na kisha akapiga magoti akaishika mikono ya Happy na kusema
“Happy ” Patrick aliita huku akimuangalia usoni binti huyu mwenye uzuri wa kimalaika.“Yes Patrick”akajibu Happy kwa sauti laini sana huku naye akimwangalia Patrick usoni.“I can’t let you go.Ulinipotea mara ya kwanza nimefanikiwa kukupata tena.Safari hii hutanipotea tena.siwezi kukuacha kamwe upotee tena mikononi mwangu .Happy I love you so much.You are the only one I truly love.The only one.Please Happy stay with me.dont leave me again.”Patrick aliongea maneno haya taratibu na kwa hisia.Ni wazi maneno haya yalitoka ndani kabisa mwa moyo wake.“Patrick hata mimi sitaki kukupoteza tena maishani mwangu.Wewe ndiye pumzi ya maisha yangu.Wewe pekee ambaye unaweza kunifanya mimi niishi kwa furaha maisha yangu yote yaliyobakia hapa duniani.Nilikupoteza mwanzo na nimekuona tena.Nisingependa hata mimi kukupoteza tena lakini…………….”“Lakini?’ Patrick akadakia“Hakuna lakini Happy .Kwa namna yoyote ile siwezi kukubali upotee tena .Wewe ndiwe mwanamke pekee niliyekupa moyo wangu.Because I love you Happy , I will make a sacrifice for you.”“Sacrifice?? Happy akauliza kwa mshangao.Patrick akamtazama usoni na kwa sauti ya upole akasema “Yes Happy .Ninaifuta ndoa yangu na Veronika.Sintamuoa Veronika tena”“Patrick!!!!!!!.......Happy akasema kwa mshangao.
“Patrick please usifanye hivyo.Nakuomba Patrick niko chini ya miguu yako usifanye hivyo.Najua unanipenda na penzi lako kweli ni la dhati na la kweli lakini Patrick tumekwisha umia vya kutosha.Naomba tuendelee kuumia sisi wenyewe na tusiwaumize tena watu wengine zaidi.Kufuta ndoa yako na Vero ni suala rahisi kwako lakini so many people will get hurt.Watu wengi wataumia sana.Suala hili linagusa watu wengi sana .Patrick Vero loves you very much and Mike loves me very much.We cant hurt the people who loves us.Patri…….”“Happy ”Patrick akadakia.“Please naomba unisikilize kwa makini sana.Najua kwamba uamuzi huu utaumiza watu wengi sana.Ndiyo ni wengi wataumia na kuhuzunika lakini sina namna nyingine ya kufanya zaidi ya hivyo nilivyokwambia.Siwezi kuendelea kujidanganya kwamba nitaishi kwa furaha na amani na Veronika wakati nikijua kuwa upo na bado unanipenda.Siwezi Happy kuendelea kuwa na Veronika mtu aliyetufanyia ukatili mkubwa sana .Niko tayari kuubeba mzigo wote wa lawama na kila kitu kwa ajili ya kuitafuta furaha ya maisha yangu.Nilifungwa kwa ajili ya kuzuia usidhalilishwe kwa hiyo sioni ajabu leo hii nikivunjilia mbali ndoa yangu na vero chui mwenye ngozi ya binadamu.Alitufanyia ukatili mkubwa sana.Hastahili kabisa kuwa na mimi ” akasema Patrick.Happy ambaye bado machozi yalikuwa yakimtoka alijikaza na kusema.“Patrick ninajua una nia nzuri na mimi na uamuzi huo ni wazi umetoka ndani kabisa mwa moyo wako.Hata mimi Patrick ninaumia sana tena zaidi hata ya siku ile nilipopata taarifa zile za kufariki kwako.Ninaumia kwa sababu sijui nifanye nini ili usiende mbali na mimi tena.Lakini Patrick tayari nimempa nafasi Mike .Nilifanya vile kwa sababu nilihitaji kuwa na mtu baada ya kuamini haupo tena duniani.Pamoja na nafasi hiyo lakini nafsi yangu imekuwa nzito katika kumpa moyo wangu wote aumiliki kama nilivyofanya kwako.Bado nafsi yangu inaugulia kwa ajili yako.lakini Patrick…………………”Happy akashindwa kuendelea kuongea akainama akiliaPatrick akamshika shingoni na kumwambia“Lakini nini Happy ?“Patrick tayari hatua kubwa sana zimeshapigwa katika mahusiano yetu mapya.Naomba Patrick tusiendelee kuwaumiza watu wengine tena wanaotupenda.Naomba usimuache Vero kwa ajili yangu.Sijui kama nitaweza kuachana na Mike kwa sababu ananipenda kupita kitu chochote”Patrick akamtazama Happy kwa sekunde kadhaa kisha akasema“Happy please look at me.Look at me and tell me that you don’t love me any more.I will understand and let you go.”Happy akainua uso wake na kumtazama Patrick .“ooh Patrick please don’t leave me.I love you so much”Happy akajikuta akijilaza kifuani kwa Patrick na kumkumbatia kwa nguvu.“patrick I love you so much.Please Patrick don’t ever leave me again.”“Its ok Happy it’s ok my angel. I won’t let you out of my hands again”Happy akamkumbatia kwa nguvu zaidi Patrick .Taratibu Patrick akaanza kuzichezea nywele nzuri na ndefu za Happy .Mkono wa kulia ukashika hadi shingoni na kuisugua taratibu kisha kwa pozi za aina yake ukashuka kuelekea mgongoni ukipita kati kati kabisa ya mgongo kana kwamba anapiga kinanda.Happy akastuka.“ouh Patrick I love you.” akasema Wakatazamana na taratibu sana kama inavutwa na sumaku midomo yao ikaanza kukaribiana na mara ikakutana na zoezi tamu la kunyonyana ndimi likaanza.‘ouh Patrick my baby don’t ever leave me again” alisema Happy kwa sauti ya kuhema Patrick hakusema kitu taratibu akaanza kufungua vifungo vya shati alilokuwa amevaa Happy akalitoa na kulitupa pembeni.Moyo ukazidi kumwenda mbio baada ya kukutana na kifua kile cha Happy chenye kusisimua.Hakutaka kuwa na papara kwani tayari alijua kila kitu ni chake kwa usiku huo.Akampiga busu zito mdomoni kisha akaifungua sidiria nyeupe aliyokuwa ameivaa Happy akakutana na chuchu nzuri za mlimbwende huyu ambazo zikazidi kumpa wazimu .Kwa ufundi wa aina yake akaanza kuzinyonya chuchu zile huku Happy akitoa miguno kwa raha alizozisikia.Wakati akinyonya chuchu zile mkono wake wa kulia ukawa ukiifungua zipu ya sketi fupi aliyokuwa ameivaa Happy akafanikiwa kuifungua na taratibu akaishusha chini.Happy alikuwa amezidiwa na utamu na hata maneno aliyokuwa akiyatamka yalikuwa hayasikiki vizuri.Taratibu Patrick akaanza kushuka chini mpaka maeneo ya kitovuni na halafu chini yake zaidi.Mambo aliyoyafanya hapo siwezi yaelezea.Happy alikuwa akitoa miguno kana kwamba anataka kufa.“Patrick I…It’s..my first…time don’t hurt me.”Happy akasema kwa sauti yenye kukwama kwama.Happy hakuwahi kukutana na mwanaume yeyote kabla.Patrick alistuka kusikia hivyo.Hakutegemea kama msichana mzuri kama Happy angeweza kuutunza usichana wake mpaka wakati ule.Kwa kuwa ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Happy ,Patrick akapunguza kasi na kwenda taratibu ili mrembo huyu asiumie.
********
Ni saa nne asubuhi siku iliyofuata wakati Mike Cambell aliposimamisha gari nyumbani kwa akina Happy .Moja kwa moja akafululiza mpaka ndani na kumkuta mama yake Happy .‘ Mike karibu baba” akasema mama yake Happy“Ahsante mama shikamoo”“Marahaba mwanangu,karibu sana”“Ahsante mama.Kuna taarifa zozote za Happy ?“Hapana baba mpaka sasa hivi hatuna taarifa zozote za Happy .Bado simu yake haipatikani.Vipi wewe una taarifa zozote ?“Hapana mama .Bado sijapata hata ujumbe wowote toka kwake”“Jamani mtoto huyu kwa nini lakini anafanya hivi?“Mama,nafikiri labda tuwe wavumilivu ,tumwache kidogo pengine ni wazi anahitaji kuwa peke yake kwa kipindi hiki.Nina imani huko aliko yuko salama salimini na ni lazima atarejea salama”Mike akasema lakini ni moyoni alikuwa akiumia sana.“Nashukuru sana baba kwa kuwa mwelewa.Mimi mara nitakapopata taarifa yake nitakutaarifu mara moja”“Sawa mama nashukuru”Mike aliaga na kuondoka.Mama yake Happy alilisindikiza gari lile la Mike kwa macho mpaka likapotea kabisa.Alipogeuka akakutana na Margreth.“ Mike anasemaje? Margreth akaulizaMama yake akamtazama kwa sekunde kadhaa“Hivi nyie watoto kwa nini mnamfanyia hivi mwenzenu?“Mwenzetu yupi mama?”Si Mike? Hivi hamuoni kuwa mnavyomfanyia si vizuri? Happy hataki kuwasiliana naye ,hata wewe unamkwepa shemeji yako.Kwa nini lakini?Margreth hakujibu kitu akatazama chini“mama mi naogopa hata kumwangalia kwa sababu atahisi ni lazima ninajua Happy yuko wapi”“Mhhh!!!! …….haya” Mama yake akaguna na kuondoka
11
SIKU NNE BAADAE - ARUSHA
“Happy malaika wangu ni siku ya nne leo tangu tumefika hapa Arusha.Najua ni lazima huko tulikoondoka watakuwa na wasi wasi mwingi kwa sababu tangu tumefika hapa simu zetu zote tumezima.Nimefikiria nimpigie simu mama yangu ili nimtoe wasi wasi." akasema Patrick.Happy aliyekuwa amejilaza katika kiti kilichokuwa pembezoni mwa bwawa la kuogelea ,alimtazama Patrick kwa sekunde kadhaa kisha akasema.“Ok Patrick ,ni wazo zuri ,ingawa mimi sikuhitaji kufanya hivyo kwa sasa lakini kwa vile umeomba basi hata mimi itanibidi nifanye hivyo.”Wakainuka na kuelekea chumbani kwao.Patrick akaishika simu yake akaitazama kisha akaiwasha.Jumbe fupi za maneno zikaingia mfululizo .Hakusumbuika nazo moja kwa moja akazitafuta namba za mama yake na kumpigia.“Haloo mama shikamoo” Akasema Patrick baada ya mama yake kupokea simu“ Patrick hujambo? Uko wapi we mtoto,mbona unatuweka roho juu namna hiyo?Hatulali tunakuwaza wewe,Vero anapiga simu usiku na mchana kukuulizia,Uko wapi na unafanya nini Pat…..” Patrick hakutaka kumpa mama yake nafasi kubwa ya kuongea,ikamlazimu kuingilia kati.“Mama us……………..”Kabla hajaendelea mama yake naye akadakia“Baba yako kawa mbogo huku ,kila siku tunakwaruzana kwamba mimi na wewe letu moja.Sasa ni lini unarudi Patrick?“Mama usijali,mimi ni mtu mzima na ninajua kitu ninachokifanya.Watoe shaka watu wote mimi niko salama salimini na muda wowote nitakuja nyumbani.Ni kama nilivyokueleza nilipatwa na dharura ndo maana nikaondoka ghafla vile.”“lakini Patrick mwanangu hivi hizo dharura zako ni muhimu kuliko suala la ndoa yako? Hivi hizo dharura zina msaada gani katika ndoa yako?Angalia mwanangu harusi ni mwezi ujaona kikao cha mwisho ni wiki ijayo kisha ndoa ikaandikishwe kanisani na kuanza kutangazwa.Sasa huoni kuwa unahitaji kuwa karibu sana kwa wakati huu?“Nalielewa hilo mama na mojawapo ya mambo yaliyonileta huku ni kuhusiana moja kwa moja na hiyo harusi yangu,hivyo usijali mama,ila tafadhali naomba kikao cha mwisho kisikae kama nitakuwa sijarudi.nataka niwepo katika kikao hicho nina jambo kubwa la muhimu sana la kuongea na kamati nzima pamoja na nyie wazazi wangu,wataarifu pia wazazi na ndugu wa karibu wa Veronika"Mama yake Patrick akanyamaza kidogo kisha akastuliwa na Patrick.“Mama naomba nikate simu .wasalimu wote hapo nyumbani ila tafadhali naomba unifikishie ujumbe wangu huo kwa kamati. Bye mama.I love you.” Patrick akakata simu kisha akapumua kwa nguvu.“Darling kuna tatizo lolote? Happy akauliza baada ya kumuona Patrick akionekana kuzama katika mawazo ghafla.“Hapana dear hakuna tatizo lolote,ngoja kwanza niongee na Andrew”Patrick akazitafuta namba za Andrew na kumpigia.“Yes Comrade” Aliita Patrick baada ya simu kupokelewa na Andrew .“wow!Patrick how are you?“I’m fine andrew”“hahaha ! mambo yanakwendaje hapo Arusha brother kwa sababu naona umekaa kimya sana.Najaribu kukutafuta lakini simu yako haipatikani kabisa ..”“ Andrew huku ni burudani kila sekunde,.Tayari tumeshamaliza matatizo yetu na kwa sasa tumeazimia tunaanza upya.”“Wow! That’s great news ”Akasema Andrew“sasa andrew sina muda muda mrefu sana wa kuongea na simu hebu nipe japo kwa muhtasari juu ya hali ya mambo yanavyokwenda hapo Dar.Nimetoka kuongea na mama sasa hivi anapiga kelele hadi nikakata simu” akasema Patrick.“Patrick huku mambo yanazidi kupamba moto.Maandalizi yanaendelea kwa kasi ya ajabu.Kadi ziko tayari na kinachosubiriwa ni kikao cha mwisho cha kamati ya maandalizi kikae ili kuangalia kama kuna kitu kilichobakia .Vero alienda Uingereza peke yake japo kwa shingo upande na kila siku ananipigia simu kama ninataarifa zako zozote.Watu wanahaha kutaka kujua uko wapi .Ninapata shida sana manake kila mmoja anajua kuwa ni lazima nitakuwa ninajua mahala ulipo.”“du ! pole sana Andrew.I’m very sorry to involve you in this..Nakuomba uwe mvumilivu rafiki yangu bado yatakuja makubwa zaidi ya hayo.Mimi nitarudi muda wowote kwa sababu nataka niwepo siku kikao cha mwisho kitakapokaa.Nina mambo ya kuongea na wazazi na wanakamati .Kwa sasa bado ninaendelea kula bata na mrembo wangu” akasema Patrick huku akicheka “Sawa Patrick mimi nitafanya kila linalowezekana kufanyika.”“Ok andrew nitakuwa nakupigia mara kwa mara ingawa muda mwingi simu yangu itakuwa imezimwa.”“Ok brother take care”Patrick akakata simu na kumwangalia Happy .“Mbona Vero humpigii simu?“ forget about her”Akasema Patrick huku akimpa simu Happy ‘Ongea na mama mtoe wasi wasi najua atakuwa na wasi wasi mwingi juu yako kwani toka umefika hapa hujawasiliana naye na kumjulisha unaendeleaje”Happy akaandika namba za simu za mama yake na kupiga“Haloo mama shikamoo” akasema Happy baada ya mama yake kupokea simu.“ Happy .Hujambo mwanangu?“Sijambo mama vipi hapo nyumbani wazima?“Huku wote wazima Happy ,roho zetu juu juu kwa sababu yako.Lini utarudi? Na mbona simu yako haipatikani?“Mama msiwe na wasi wasi mi ni mzima kabisa na muda wowote ninaweza kurudi nyumbani.Simu yangu nimeizima kuepuka usumbufu wa watu ”akasema Happy“Sawa Happy mi nafurahi kusikia uko salama.lakini ni kwa nini hutaki kumpigia simu Mike? Tayari amekuja na anaumia sana moyoni kwa kukukosa.Hivi unajua ni kwa kiasi gani unavyomtesa mwenzio?. mwenzio katoka Marekani kuja kukupa hongera kwa ushindi wako lakini wewe ndiyo kwanza hata kumuona hutaki kwa nini lakini Happy ?Happy akapatwa na kigugumizi cha ghafla akashindwa ajibu nini akanyamaza kimya kwa sekunde kadhaa.“Happy nakuuliza kwa nini unamfanyia hivyo mchumba wako? Mama yake akaendelea kuhoji“Mom please I have to go,bye”Happy akaikata simu na kumpa Patrick ambaye aliizima kabisa.Patrick alikwisha ng’amua kuwa mambo katu hayakuwa mazuri kwa Happy .“Happy my baby” Akasema Patrick huku amemshika Happy mkono“Calm down my sweet love.This is just the beginning .You have to be strong”Kikapita kimya kifupi halafu Patrick akauliza“Mama alikuwa anasemaje?“Alihitaji kufahamu nitarudi lini na ni kwa nini siwasiliani na Mike.Patrick nilikubali kumpa moyo wangu Mike kwa sababu kwa wakati huo nilijua tayari umeshafariki.Laiti ningelijua kuwa bado upo hai nisingempa moyo wangu Mike.Lakini kwa vile tumeshaonana na wewe ndie mwanaume pekee nikupendaye duniani,basi sina budi kuwa wazi kwa Mike.It hurts lakini sina jinsi ni lazima nimweleze ukweli.Patrick ulinipotea mara ya kwanza lakini safari hii hutaweza kunipotea tena.I’ll fight for you” akasema Happy akiwa amekumbatiana na Patrick.
* * * * “MISS TANZANIA ATOWEKA NYUMBAN….,MREMBO WA TANZANIA ATOROKA….HAPPY KIBAHO HAJULIKANI ALIPO…..WASI WASI WATANDA JUU YA AFYA MISS TANZANIA ,MASKINI MISS TANZANIA…Hivi ni baadhi tu ya vichwa vya habari ambayo vilikuwa vikipamba kurasa za mbele za magazeti hasa yale ya udaku yenye kuandika sana habari na vituko vya watu maarufu..Magazeti mengi yaliandika habari nyingi zinazohusiana na kutoonekana hadharani kwa mrembo mpya wa Tanzania,Happy kibaho lakini hakuna hata gazeti moja ambalo lilikuwa na taarifa za ukweli juu ya wapi alipo .
Wakiwa bado Arusha Patrick na Happy waliyasoma magazeti yote na kila kilichoandikwa ,wakacheka sana.“Umekuwa maarufu sana kwa sasa” Patrick akasema“Hiz ndizo karaha za kuwa maarufu.!!’ Akajibu Happy“Na huu ni mwanzo tu Happy bado watakufuatilia sana katika kila jambo unalolifanya.Kila utakachokifanya itakuwa ni biashara kwao.Unatakiwa uwe jasiri na hasa katika hiki kizungumkuti kilichoko mbele yetu,mengi yatasemwa na mengi yataandikwa.Ningependa sana uwe mrembo mwenye sifa nzuri kama Nancy sumari,kama Hoyce Temu.Katika vipindi vyao vya kuvaa taji la miss Tanzania hawakuwa na kashfa yoyote ile iliyoyachafua majina yao.Nitafurahi ikiwa utafuata nyendo zao.” Akasema Patrick“Nakuunga mkono Patrick ,unajua Nancy ndiye aliyenivutia mimi mpaka nikaingia katika fani hii ya urembo.Nampenda na nitafurahi sana kama nitafanikiwa kuwa kama yeye yaani kumaliza kipindi cha kulivaa taji hili bila kuwa na skendo yoyote mbaya katika jamii” akasema Happy wakakumbatiana na kucheka.“Happy darl kuwa nawe hapa najiona ni kama vile ninaishi mbingu ya saba mbali na matatizo lukuki ya dunia hii.Laiti kama maisha yetu yangeendelea namna hii,kuishi kwa raha away from all troubles lakini ninasikitika sana kwamba inatubidi turejee Dar.Nina imani kila mmoja wetu anafurahia sana kuwepo hapa lakini hatuwezi kukaa hapa kwa muda mrefu kwa sababu bado tuna majukumu mengine ya kufanya huko tulikotoka na kubwa zaidi ni hili suala letu.Kikao cha mwisho cha harusi yangu kinakaribia hivyo inanibidi niwepo kabla ya kikao hicho na kuweka kila kitu bayana na hatimaye kuuvunja rasmi uchumba wangu na Vero kisha niufungue ukurasa mpya wa maisha yangu ya furaha nikiwa na wewe malaika wangu.Halikadhalika wewe pia unatakiwa uende nyumbani kabla Mike hajaondoka na kufanya kama tulivyokubaliana yaani kuachana na wapenzi wetu wa sasa na kuyaaza maisha mapya.”akasema Patrick“ Kweli kabisa Patrick hata mimi nilikuwa na wazo hilo hilo.Hatuwezi kukaa hapa kwa muda mrefu sana wakati kuna jukumu zito linatukabili mbeleni.Ni wazi tunatakiwa kurudi dar.I’m some how scared ” akasema happy.Patrick akamtazama kisha akatabasamu na kusema
“ Usihofu kitu malaika wangu..kuwa jasiri hakuna kitakachoshindikana” akasema Patrick“Kuhusu usafiri usihofu,nitaongea na Andrew atatutumia gari la kuja kutuchukua hapo kesho..”
* * * *
Saa kumi na dakika saba za jioni gari moja yenye vioo vyeusi ilifunga breki mbele ya lango la nyumba ya akina Happy .Mlango wa kulia ukafunguliwa akashuka Patrick akazunguka na kuufungua mlango mwingine akashuka mrembo mpya wa Tanzania Happy kibaho.Tayari walikwisha wasili Dar es salaam wakitokea Arusha.Kwa takribani dakika tano hivi walizitumia kuagana kisha Patrick akaingia garini na kuondoka.Happy alibaki amesimama pale huku akiupunga mkono wake ,hadi gari lilipopotea kabisa machoni pake“I looo…..oove…uuuuuu….Pa…aaa.tri…ck…..”Alisema Happy huku machozi yakimlenga ,mara geti likafunguliwa akatoka mtumishi wa ndani.“wow! Dada Happy …..!!!”Happy akastuliwa na sauti ile kugeuka akakuta ni Christina .‘wow Tina”Wakakumbatiana kwa furaha .Tina akamshika Happy mkono na kumuongoza mpaka ndani.Huko ndani ilikuwa ni furaha isiyo na kifani ,kila mtu aliruka ruka na kushangilia kwa nguvu Happy kurudi tena akonekana ni mwenye furaha sana..“Karibu sana mwanangu”Akasema mama yake“Ahsante mama nimeshakaribia”“habari za huko utokako”“huko kwema mama,sijui nyie hapa”“Sisi huku wote wazima kabisa ila hofu yetu kubwa ilikuwa kwako.Tunashukuru Mungu umerudi salama.”“Hata mimi nashukuru sana mama kama nyote mu wazima.I missed you all so much”Kisha salimiana Happy akaenda kuoga halafu akajifungia chumbani kwake akaiwasha simu yake na kujilaza kitandani akaanza kutafakari jinsi atakavyoweza kuachana na mchumba wake Mike cambell.Kabla hajaanza kuwazua ni nini afanye simu yake ikaita.Akaichukua na kuangalia ni nani mpigaji akakuta ni Patrick,Happy akatabasamu .“Haloo my sweet love” akasema Happy“Haloo darling vipi umepumzika?“Yes Patrick nimejipumzisha kitandani” akajibu Happy huku akitabasamu“Ouh my love I’ve missed you arleady ” akasema Patrick“mhh Patrick jamani hata masaa mawili hayajapita..!! Happy akasema huku akitabasamu“Yeah I miss u a lot already.I miss you each second Happy ”“Hahahahahaa….Mwaaaaaaa.I love you Patrick” Happy akasema kwa furaha“I love you too Happy ”“Ok my baby boy ngoja mi nipumzike tutawasiliana baadae.” Akasema Happy“Ok Happy mimi ndo najiandaa niende kwa andrew kisha nitapita nyumbani nikamuone mama.Ntakupigia baadae ”“Ok love.Take care” akasema Happy.Baada ya kukata simu Happy akaendelea kuitazama simu ile huku akitabasamu.“Mhh ! kila ninapoisikia sauti ya Patrick nahisi mwili wote unanichemka.I love him so much,and I’ll do anything for him”
Wakati akimuwaza Patrick mara sura ya Mike ikamjia akilini Happy akashindwa kujizuia akaangusha machozi.“I’m sorry Mike but I have to do this.Lazima nirudiane na Patrick .yeye ndiye furaha ya maisha yangu.”Akachukua simu yake tena na kuzitafuta namba ambazo Mike huwa anazitumia pindi awapo Tanzania akapiga.“Hallow baby”ilikuwa ni sauti ya upole ya Mike cambell.“Hallow Mike how are you”“ Happy unajisikiaje sasa hivi? Akauliza Mike“Najisikia vizuri Mike,nashukuru sana kwa kuja kunitazama”“Nashukuru hata mimi kama umerudi salama.Nilipata taarifa za ushindi wako na ghafla nikapata taarifa nyingine kuwa ulipoteza fahamu baada ya kutangazwa mshindi.Pole sana haya ni mambo ya kawaida.Nililazimika kuomba dharura ya wiki mbili ili nije kukaa nawe kwa kipindi hiki ambacho najua unanihitaji sana,lakini nilipofika mama akaniambia kuwa umesafiri kidogo nje ya Dar es salaam .Sikutaka kukusumbua kwani nilijua unahitaji kuwa peke yako kwa kipindi hicho.Nafurahi umerudi salama” Mike akasema“Mike naomba unisamehe kwa kutowasiliana nawe .Mambo mengi yalinitokea hivyo nilihitaji kuwa peke yangu.Samahani sana kwa hilo”“Usijali Happy nalitambua hilo na kuyaheshimu maamuzi yako.dont worry I’ll always be there for you my sweet baby.All I want is you to be happy.My love I want to remind you that anytime you need a shoulder to cry on just count on me.I’m here for you”Maneno haya yakamchoma sana Happy na kujikuta akitokwa na machozi ,alishindwa ajibu nini ,mara akastuliwa na sauti ya Mike.“Happy niko njiani nakuja nina hamu sana ya kukuona na kukupa pongezi zangu na kama utakuwa unajisikia vizuri basi tunaweza kutoka out kwa ajili ya dinner.” Happy akastuka na kuwaza kwa sekunde chache kisha akasema “Thanx Mike,nashukuru sana lakini najisikia kichwa kinaniuma mno.Nadhani nahitaji kupumzika Unaonaje ikiwa tutaonana siku ya kesho?“Ok Happy kama umeamua hivyo basi vizuri.Jiandae kesho tutoke kwa chakula cha mchana .”Mike alisema kwa sauti ambayo ilionyesha dhahiri kuwa hakuwa ameridhika na maamuzi yale ya Happy .“sawa Mike nashukuru sana ,tuonane hiyo kesho”“Ok Happy have a nice eveing.I love you………………..”Happy akashindwa atamke nini ,midomo ikawa mizito machozi yakimtoka.Akakata simu na kujitupa kitandani.“Mike I’m sorry.” Akasema huku amekishika kichwa kwa mikono yake
* * * *
“Hello Komrade” Andrew akasema kwa furaha huku akimkumbatia rafikiye Patrick kwa furaha mara baada ya kufungua mlango na kumkuta amesimama mlangoni
Andrew akaushika mkono wa patrick akauinua kidogo na kuuminya halafu akacheka kicheko kikubwa.
“Brother naona mambo ya Arusha hayakuwa madogo.Siku hizi chache tu naona hata mwili umeongezeka. “
Wote wakacheka na kuketi sofani.Andrew ambaye ndiyo kwanza alikuwa amerejea toka katika shughuli zake,akaelekea jikoni kisha akarejea s na chupa kubwa ya mvinyo.
“Nashukuru umerudi salama.Hamkupata tatizo lolote njiani?”
Akasema Andrew huku akiweka chupa ile mezani na kuumimina mvinyo katika glasi akampatia Patrick glasi moja.
“hatukupata tatizo lolote njiani.Nashukuru yule dereva uliyemtuma ni mahiri mno.” Patrick akasema kisha akanywa funda moja.
“Kaka nipe habari za Arusha.Mambo yamekwendaje? Happy hajambo? Andrew akauliza huku akitabasamu baada ya kupiga funda la mvinyo.Patrick naye akainua glasi yake akapiga funda moja halafu akalegeza tai yake na kusema
“Andrew namshukuru Mungu kwa sababu mambo yaliyotokea Arusha sikuyategemea kabisa.Ndugu yangu sikufichi nilikuwa najihisi kama niko peponi kwa raha nilizokuwa napata .Kama isingekuwa ni masuala haya ya harusi nisingerejea mapema hivi.” Patrick akanyamaza na kunywa tena funda la mvinyo halafu akaendelea
“Happy alifika Arusha kama tulivyopanga.Mara tulipokutanisha macho nilihisi kama ninapaa kwa furaha niliyoipata.Sikuwa nimetegemea kama ningekuja kuonana tena na Happy maishani.Tulikuwa na maongezi marefu sana siku hiyo.Tulikumbushana toka siku ya kwanza tulipokutana ,mambo yote yaliyotokea hadi siku niliyoingia gerezani.Happy alilia sana.Tulikumbuka mambo mengi mno.Tulikumbuka nyakati zetu za furaha na hata nyakati zile tulizokuwa katika wakati mgumu na hasa wakati ule tuliposimamishwa shule kwa kosa la kupigana darasani halafu tukaenda kujificha Bagamoyo ambako ndiko penzi letu lilikoanzia.” Patrick akanyamaza akanywa tena funda la mvinyo halafu akaendelea na maongezi.Andrew alikuwa kimya akimsikiliza.
“Andrew mambo yaliyotokea huko ni makubwa na ya kushangaza sana”
“Patrick hebu niambie ,mambo gani hayo yaliyotokea huko? Nina hamu ya kutaka kufahamu kilichoendelea huko Arusha” Andrew akasema huku akiifungua tai yake na kuitupa pembeni.
“we real had a great time”
“Usiku wa siku ile ya kwanza happy aliniuliza kitu ambacho kilinistua na kunishangaza sana.Aliniuliza eti ni kwa nini niliamua kumdanganya kwamba nimefariki dunia wakati ningali hai? “
“Etu ulifanya nini !? Andrew akauliza kwa mshangao
“Anadai nilidanganya kwamba nimefariki dunia”
“ Umefariki dunia ! How “ andrew akahoji.
“ Subiri ntakusimulia” akasema Patrick
“ wewe ukamjibuje?
“Kwanza swali lile lilinistua sana japokuwa hata Margreth alikwisha nidokeza kuhusu kuwepo kwa jambo hilo la mimi kudai nimefariki dunia.Nilimtuliza na taratibu nikamuomba anielezee kwa undani kuhusiana na mkasa ule kwa sababu mimi ndiyo kwanza niliusikia.Alianza kunieleza kwamba akiwa chuoni alipokea barua toka kwa mtu ambaye alijitambulisha kwamba ni mtu anayenifahamu mimi na familia yangu na kwa kuwa anaufahamu uhasiano wetu aliamua kumpa taarifa ambazo hazikuwa nzuri hata kidogo.Mtu huyo aliyemuandikia barua hiyo alidai kwamba Patrick yaani mimi ,nilifariki kwa ugonjwa wa kuhara nikiwa gerezani.Nikinukuu maelezo yake anasema kwamba almanusura ajitoe uhai baada ya kuipata taarifa ile kwa sababu hakuona ni namna gani angeweza kuishi bila mimi.Ilimchukua muda mrefu sana kukubaliana na ukweli kwamba nimefariki.Baada tu ya kumaliza masomo yake alirudi nchini na kitu cha kwanza alichokifanya ni kuanza kutafuta mahala nilipokuwa nimezikwa.Alikwenda hadi Sumbawanga ,mahala tulikokuwa tukiishi kabla ya baba hajahamishwa akaambiwa kwamba familia yangu ilihama kitambo.Toka Sumbawanga akaenda hadi Iringa katika gereza nililoanza kutumikia kifungo akaambiwa kwamba nilihamishwa pale gerezani na kwenda Songea nikiwa mzima wa afya.Hakukata tamaa akaenda tena hadi Songea ambako taarifa aliyoipata ilisema kwamba nilimaliza kifungo changu na kufanikiwa kutoka gerezani salama salimini.Majibu haya yalimpa wakati mgumu sana na kumfanya azidi kuchanganyikiwa kwani aligundua sikuwa nimefariki .Kwa mujibu wa maelezo yake,siku ile aliposhinda taji la Miss tanzania alipoteza fahamu baada ya kuiona sura yangu.Hakuamini kama kweli ni mimi au ni mzuka anaouona” Patrick akanyamaza ,akamtazama rafiki yake aliyekuwa kimya akimsikiliza
“Enhee ikawaje baada ya hapo? Andrew akauliza
“baada ya hapo ikanibidi na mimi nimweleze ukweli kwamba nilipokea taarifa toka kwa Vero niliyekuwa nikimtumia kama kiungo cha mawasiliano baina yangu na Happy .Taarifa hiyo ilisema kwamba yeye Happy amepata mchumba wa kizungu na tayari ana ujauzito na kwa sasa wanaishi pamoja kama mume na mke.Nilimweleza ni jinsi gani nilivyoumizwa na taarifa ile.Happy alilia sana hadi nikamuonea huruma.Alinilaumu sana kwa kuwa mwepesi wa kuamini taarifa kama ile hali nikijua kwamba alikuwa akinipenda kwa moyo wake wote.” Patrick akatulia akanywa tena mvinyo halafu akakohoa kidogo.Andrew akainuka na kuwasha feni alianza kuhisi joto.
“Enhee ikawaje tena? Akauliza Andrew huku akiongeza mvinyo katika glasi yake.
“Kilichofuata ikatubidi tukae kwa pamoja na kutafakari ni kwa nini mambo haya yalitokea.Tuligundua kwamba taarifa zile mbili zilikuwa na lengo la kuuvunja kabisa uhusiano wetu.Swali likaja ni nani ambaye aliamua kutufanyia ukatili wa namna ile? Ni nani ambaye alihitaji mimi na Happy tutengane? Happy akanionyesha ile barua aliyotumiwa ambayo ameitunza hadi hivi sasa.Nilistuka mno baada ya kuutambua mwandiko .Ulikuwa ni mwandiko wa Vero.Nilihisi kuishiwa nguvu baada ya kuligundua hilo” Patrick akatulia kidogo na kuinama chini.Andrew akastuka na kusema kwa sauti ndogo
“Ouh My God ! ..Hii sasa ni hadithi mpya”
Pamoja na feni iliyokuwa ikipuliza mle sebuleni na kuipooza hali ya hewa iliyokuwa ya joto,Andrew alikuwa akitoka jasho jingi.
“Nahisi kuna kipindi kigumu kinakwenda kuanza muda si mrefu.” Akawaza Andrew akiwa ameliinamia kabati.
“Nimestuka sana kusikia kwamba Vero ndiye aliyewatenganisha Patrick na Happy.Kwa nini alifanya hivi? Its hard to believe..” akaendelea kuwaza Andrew.
“ Pamoja na kwamba ni muda mrefu Patrick na Happy wametengana na kwa sasa anakamilisha maandalizi ya harusi yake na Vero lakini bado siku zote moyo wake uko kwa Happy.Siku zote hajaacha kumzungumzia Happy..Kwa jinsi Patrick anavyompenda Happy ,na baada ya kugundua kwamba Vero ndiye aliyewatenganisha ,sina haja ya kuuliza kwani jibu liko wazi,hapa hakuna ndoa tena.Nahisi kuchanganyikiwa ……”
Andrew akamtazama Patrick aliyekuwa ameegemeza kichwa katika ukingo wa sofa huku mkono wake mmoja ukiwa umelishika shavu lake.
“Enhee endelea kunipa michapo ya Arusha.Ikawaje baada ya kugundua kwamba ni Veronika ndiye aliyesababisha mambo haya yote? Andrew akauliza
“kwanza Happy alilia sana.Mimi kwa upande wangu nilipandwa na hasira za ajabu .Sikuamini kama Vero anaweza akafanya kitendo cha namna ile.Niliumia sana Andrew.”
“Du ! haya mambo ni makubwa sasa” Andrew akasema
“Ilituchukua muda mrefu sana kuliongelea jambo hilo lakini kuna kitu kiliibuka ambacho kiliniuma sana”
“Kitu gani hicho?
“Happy alikuwa na pete ya uchumba kidoleni”
“Ina maana tayari Happy ana mchumba? Andrew akauliza huku akishusha pumzi
“kweli Andrew.Tayari Happy ana mchumba.Baada ya kukaa muda mrefu bila kuniona aliamua kumpa nafasi mtu mwingine.”
“Too bad.” Andrew akasikitika
“Na wewe ulimweleza kuhusu harusi yako na Vero? Andrew akauliza tena
“Ndiyo Andrew.Hatukufichana chochote.Tuliweka bayana kila kitu bila kuficha chochote” Patrick akasema
“Baada ya hapo nini kiliendelea? Andrew akauliza huku akitabasamu
“Kilichofuata baada ya hapo tuliiweka dunia yote na matatizo yake kando, tukaingia katika ulimwengu mwingine kabisa wenye raha zisizoelezeka.Andrew nilihisi raha ambayo sijawahi kuipata toka nimezaliwa.Nilijiona ni mwenye bahati kubwa kuwa na mrembo kama yule”
“wow ! maelezo yako yananifanya nijenge picha ya jinsi mambo yalivyokuwa.Tell me about that first night “ Akasema Andrew
“Andrew ,ule ulikuwa ni usiku wangu wa kwanza kuhisi kama niko peponi.Nilihisi kama siko katika dunia hii iliyojaa shida na mahangaiko.Sijawahi kuwa na usiku kama ule.Sikufichi Andrew,Happy ni msichana aliyebarikiwa mno.She’s so sexy” Patrick akasema na kumfanya Andrew acheke wakagonganisha mikono.
“You had sex with her? Andrew akauliza.Huku akicheka Patrick akasema
“C’mon brother..why not ? .and one thing that you cant agree is that.I was her first man” Patrick akasema na kumfanya Andrew asimame huku akiwa na tabasamu la mshangao.
“ wuuuh ! Its unbelievable “ Andrew akashangaa
“ Andrew.hata mimi nilishangaa sana .Kwa mujibu wa maelezo yake anasema kwamba japokuwa aliamua kuwa na mpenzi mwingine lakini bado moyo wake ulikuwa kwangu.Aliamini siku zote kwamba mimi ndiye mwanaume wake wa pekee kwa hiyo alikuwa mzito sana kumpa mwili wake huyo mpenzi wake mpya”
Andrew akamimina mvinyo katika glasi yake akaiinua juu,wakagonganisha glasi
“Patrick nakupa hongera zako” Andrew akasema huku akitabasamu halafu wote wakacheka kwa nguvu.
“Andrew kwa siku hizi chace nilizokaa na Happy kule Arusha nimeonja utamu wa maisha.Sikujua hapo awali kama kuna nyakati maisha huwa matamu namna ile.Kila nikiamka asubuhi najikuta niko na malaika wangu pembeni ilimradi raha na furaha kila wakati.”akasema Patrick huku akitabasamu.
Patrick akasema na kuchukua glasi yake ya mvinyo akapiga funda kubwa.Andrew akamtazama na kusema
“Patrick naomba nikuulize jambo moja”
“Uliza Andrew”
“Ni muda mrefu hamjaonana na happy .baada ya kukutana naye safari hii umeuonaje mtazamo wake kuhusu mahusiano yenu?
“Andrew wewe ni mtu wangu wa karibu na siwezi kukuficha kitu.Pamoja na yote yaliyotokea lakini bado mimi ni mtu wa pekee kwake.Bado nafasi yangu iko pale pale ndani ya moyo wake.”
“na vipi kuhusu wewe? Pamoja na yote yaliyotokea,bado unaamini kwamba Happy ana nafasi moyoni mwako? Andrew akauliza
Swali lile likamfanya Parick anyamaze kidogo ,akachukua glasi ya mvinyo na kupiga funda moja,akakohoa kidogo na kusema
“Andrew ,pamoja na yote yaliyotokea bado Happy ndiye namba moja wangu .Yeye ndiye furaha yangu.Samahani Andrew kama kwa kusema hivi nimekukera.”
“hapana hujanikera Patrick.Nafurahi kwa sababu siku zote umekuwa mkweli kuhusu hisia zako.Kwa hiyo baada ya
hisia za kila mmoja wenu kuwa wazi kwamba bado mnapendana nini kilifuata?
“Tulikuwa na wakati mgumu mno kwa sababu sote tayari tuko katika mahusiano mapya ambayo yamekwisha piga hatua kubwa,lakini hii haikuwa sababu ya kutufanya tusiendelee na urafiki wetu hata kama tuko katika mahusiano mengine.Tulikubaliana kuendelea na urafiki wetu wa kawaida lakini tukajiuliza tena,sisi tunapendana kwa dhati,je tutakuwa tunajitendea haki sisi wenyewe ? Je tutakuwa na furaha ? Majibu ya maswali haya yote yalikuwa ni hapana.Hatutakuwa tumejitendea haki sisi wenyewe ,vile vile huko tuliko hatutaweza kuishi kwa furaha na amani.Tukajiuliza tena tufanye nini basi? Jibu likawa kwamba tunalazimika kuifanya maamuzi magumu.”
“maamuzi magumu yapi tena? Andrew akauliza
“Kuachana na wapenzi wetu wa sasa “ Patrick akasema na kumfanya Andrew asimame
“No ! you are kidding me” Akasema Andrew huku akicheka kichini chini
“Si utani Andrew.,Happy ndiye furaha ya maisha yangu.Nilimpenda Happy muda mrefu na hata nikafungwa kwa ajili yake.Pamoja na yote yaliyotokea lakini bado Happy amekuwa ni mtu wa pekee kabisa ndani ya moyo wangu .Ninampenda na nitaendelea kumpenda hadi kufa kwangu.Kwa sababu ya upendo huo mkubwa nilionao kwa Happy ,nimeamua kuachana na Vero.Nimeona uwe mtu wa kwanza kufahamu kabla sijaliweka wazi jambo hili kwa ndugu .Ndoa kati yangu na Vero haipo tena.Its over.Kwa mambo aliyoyafanya Vero simuhitaji tena katika maisha yangu.Alitumia uongo ,akatutenganisha bila kujali mateso na maumivu tuliyoyapata kwa hiyo hana nafasi tena katika maisha yangu.Happy naye ameamua kuachana na mpenzi wake ili tuweze kuwa pamoja.Nafahamu si jambo rahisi lakini siku zote nguvu ya penzi ni kubwa na hushinda kila kikwazo“ Patrick akasema na kumfanya Andrew ainame na kuzama katika mawazo ghafla.
“Nilijua tu ,hapa hakuna ndoa tena.Masikini Vero” Andrew akawaza.Patrick akasema
“Andrew nafahamu umekuwa mtu wangu wa karibu mno na umenisaidia katika mambo mengi lakini tafadhali naomba usinishauri chochote kuhusu jambo hili.Nimekwisha fanya maamuzi na siwezi kurudi nyuma tena.Kwa ajili ya Happy nitafanya kila kitu ili niwe naye maishani..Ahsante sana Andrew kwa kunisaidia katika mambo mengi lakini nakuomba katika suala hili usijihusishe kwa sababu ninafahamu kinachokwenda kutokea si kitu kizuri.Please don’t be part of this” Patrick akasisitiza.Andrew akamtazama na kusema
“Patrick wewe ni zaidi ya rafiki yangu.Tumeshauriana na tumesaidiana katika kila jambo.Mpaka sasa hivi kati ya ndugu zako wote hakuna mtu yeyote anayefahamu kitu gani kinaendelea kuhusu wewe na Happy zaidi yangu.Kusema kwamba nisikushauri au nisijihusishe kwa namna yoyote na suala hili ni jambo lisilowezekana kwa sababu I’m too involved now.Tumetoka mbali na jambo hili kwa hiyo siwezi kuishia hapa.Kama nilikubali toka mwanzo kwamba nitakuwa nawe,siwezi kamwe kukuacha peke yako hasa katika kipindi hiki kitakachokuwa kigumu zaidi kwako.Patrick utake usitake mimi nitakuwa pamoja nawe katika suala hili hata kama umekataa nisikushauri chochote lakini nitakuwa nawe hatua kwa hatua na hata ikibidi kukushauri pale itakaponilazimu japokuwa sintakushauri ubadili mawazo yako kuhusu yupi ni msichana unayemtaka maishani.” Akasema Andrew. Patrick akamtazama na kusema
“Andrew narudia tena ,kinachokwenda kutokea si kitu kizuri.Ninaomba kila kitu nikibebe mimi mwenyewe.Umenisaidia sana lakini kwa hili naomba uniache mwenyewe.Nimekwisha jitolea kuubeba mzigo huu mkubwa ,ninajua nitaumia na wengi pia wataumia lakini sina namna nyingine ya kufanya .Lazima nifanye hivyo.Lazima niachane na Vero”
“Patrik nimekuelewa vizuri naomba ufahamu kwamba hata kama hupendi bado nitaendelea kuwa nyuma yako.Naomba tafadhali tusiongelee suala hili tena.Fahamu kwamba tuko pamoja na siku zote tutaendelea kuwa pamoja.” Andrew akasema huku akimpa Patrick mkono.
“Andrew nashukuru kama kwa moyo wako umekubali kuungana nami katika suala hili.Nitakuja kukuona kesho asubuhi na kukufahamisha kwa kina mpango mzima .Naomba nikuache na tuonane kesho.”
Wakaagana na Patrick akaondoka zake na kumuacha Andrew akiwa na mawazo mengi
“Du ! mambo yanazidi kujikoroga.Sipati picha ni kitu gani kitakachotokea baada ya Patrick kutamka kwamba amevunja mahusiano yake na Vero.Sikutegemea kama suala hili lingefika hapa lilipofika.Hatua waliyokwishaifikia ni kubwa sana na umebaki muda mchache tu wafunge ndoa.Kitendo cha kusitisha masuala ya ndoa yao kimeniumiza sana japokuwa sina uwezo wa kulizuia jambo hilo lisitokee, kwani tayari Patrick amekwisha fanya maamuzi na hakuna mtu anayeweza kuyabadili.Ninamfahamu Patrick vizuri akisha amua kitu huwa hapendi kupingwa Nimemuona machoni ,alikuwa akimaanisha kile alichokisema.Sijui Happy amempa kitu gani Patrick mpaka ameshindwa kumsahau hata baada ya miaka mingi kupita.Hadi kufikia hatua ya kusitisha mipango ya harusi yake kwa ajili tu ya Happy basi hakuna kitu ninachoweza kukifanya kwa ajili ya kuinusuru ndoa hii ya Patrick na Vero.Patrick na Happy wanapendana na hilo halina ubishi.Ukijiuliza ni kwa nini Happy ajitokeze katika kipindi hiki baada ya kupotea kwa miaka hii yote utapata jibu kwamba ilipangwa wawe pamoja.Nakubaliana na ukweli huo japokuwa ninamuhurumia sana Vero kwa jinsi anavyompenda Patrick.Kosa moja ambalo alilifanya ni kutumia uongo kuwatenganisha wawili hawa.Uongo wa Vero leo hii umekuja kujulikana na hivyo kumgharimu .Kama walivyoumia wenzake kipindi kile alipowatumia taarifa za uongo zilizowafanya wakatengana basi hata yeye atasikia uchungu kama walioupata wenzake kwa miaka hii yote.Roho inaniuma sana lakini sina namna nyingine ya kuweza kumsaidia..Kingine kinachoniumiza ni gharama kubwa tuliyoitumia katika maandalizi ya harusi hii.Nimetumia fedha zangu nyingi kama mchango kwa rafiki yangu katika kuiandaa harusi hii lakini kila kitu kimepotea bure……” Andrew akawaza huku akiketi sofani akakishika kichwa chake alikuwa na mwazo mengi.
“Ngoja nimpigie mama yake Patrick ili afahamu kama mwanae amesharudi.Kwa jinsi Patrick alivyochanganyikiwa na Happy sidhani kama amekumbuka hata kumtaarifu mama yake kama amesharudi Dar es salaam.” Akawaza Andrew huku akichukua simu na kuzitafuta namba za mama yake Patrick.
“Lakini simlaumu sana Patrick kwa sababu kwa uzuri wa Happy hata mimi ningechanganyikiwa.Mtoto ameumbika mithili ya malaika.Mtoto anastahili kabisa kutwaa taji la mrembo wa dunia” Akawaza Andrew wakati akisubiri simu yake ipokelewe na mama Patrick.
“Hallo Andrew habari yako mwanangu” Akasema mama Patrick baada ya kupokea simu
“Habari nzuri mama ,pole na mihangaiko ya kutwa nzima ” Andrew akasema
“Tumeshapoa baba yangu.Kutwa nzima tumekuwa tukizunguka hapa na pale katika kuhakikisha maandalizi yanakamilika.Japokuwa kuna kamati inayoshughulikia kila kitu lakini hata mimi kuna mambo ambayo inanilazimu kuyafuatilia na kuhakikisha yamekaa sawa.Si unajua siku zimebaki kidogo sana na jiji hili lina sherehe nyingi kwa hiyo inabidi kufanya maandalizi ya mapema.”
“ Pole sana .Mama nimekupigia kukufahamisha kwamba Patick amerejea Dar es salaam jioni ya leo .Umefanikiwa kuonana naye?
“Hapana Andrew.Habari hizi wewe ndiyo wa kwanza kuniambia.Hajanitaarifu kama amerejea japokuwa alinipigia simu jana akaniambia kwamba atarejea Dar es salaam siku yoyote.Andrew huyu mwenzio amepatwa na kitu gani ? mbona amebadilika namna hii?Nimeona kuna mabadiliko makubwa sana katika siku hizi chache toka apatwe na yale matatizo ya kupoteza fahamu.Kitu gani kinamsumbua mwenzio? Mama yake Patrick akauliza
“mama siwezi kujua kitu gani kinamsumbua ,japokuwa mimi na yeye ni marafiki wakubwa lakini kuna masuala ya ndani kabisa ambayo hatuwezi kuambiana.Mimi naona tumpe muda wa kutosha ili atulie kwa sababu ninahisi hali hii inaweza kuwa inachangiwa na mambo mengi aliyonayo na hasa hili suala la harusi yake”
“Sawa Andrew.nashukuru kwa kunifahamisha kwa sababu rafiki yako haoni hata umuhimu wa kuwataarifu wazazi wake kama amerejea salama.Tena imekuwa vizuri amerejea kwa sababu mwenzake alinipigia simu kunitaarifu kwamba atarejea leo saa nane za usiku.Kwa hiyo itakuwa vizuri kama atakuwepo uwanja wa ndege na kumpokea mwenzake kwani aliondoka akiwa hana amani kwa hiyo litakuwa jambo la faraja kama akimkuta Patrick uwanjani akimsubiri .Ngoja nimpigie simu nimfahamishe kuhusu hilo.”
“Ok Ahsante mama.Usiku mwema” Andrew akasema na kukata simu kisha akaitupa sofani.
“Damn you Patrick!! Kila siku nimekuwa nikidanganya watu wazima.Umeniweka katika matatizo makubwa sana na siku mama yako akigundua kama mambo yote niliyokuwa nikimwambia yalikuwa ya uongo atatamani hata kunitoa roho.Hatatamani anione tena katika macho yake…” Andrew akatikisa kichwa kwa masikitiko.
“masikini Vero leo usiku anarejea akiwa na matumaini kwamba ndani ya wiki chache zijazo atakuwa mwanamke mwenye furaha kwani atakuwa ameolewa na mwanaume anayempenda sana.laiti angejua ..nadhani asngekubali kurudi tena Tanzania.Namuonea huruma lakini yote haya aliyataka mwenyewe.Palipo na penzi la kweli hakuna awezaye kulitenganisha.Na tusubiri tuone kitakachotokea….” Andrew akawaza akachukua glasi yake iliyokuwa na mvinyo akapiga funda kubwa.
* * * *
Akiwa katika kona ya kuingilia nyumbani kwake simu yake ikaita.Akapunguza mwendo wa gari na kutazama mpigaji.Alikuwa ni mama yake.Akasita kuipokea simu ile.
“Ukiona hivi ujue tayari amekwisha pata taarifa kuwa nimerudi.” Akawaza Patrick
“Hallo mama shikamoo” Akasema Patrick baada ya kuipokea simu ile.
“Marahaba hujambo? “ Akaitika mama yake. Patrick akaguna kidogo kwa muitikio ule kwa sababu kuna kitu alihisi hakikuwa sawa katika sauti ya mama yake.Anamfahamu mama yake vyema.
“Sijambo mama.habari za hapo nyumbani? Patrick akauliza
“Hivi wewe mwanangu naomba nikuulize kitu.Sisi wazazi wako unatuweka katika kundi gani? Mama yake akauliza kwa sauti yenye ukali.
“Kazi imeanza” akawaza Patrick
“mama samahani naomba nikupigie baada ya muda mfupi .Nataka kupaki gari.”Akasema Patrick na mama yake akakata simu bila kusema chochote.Baada ya kuliingiza gari ndani akaelekea sebuleni kisha akaketi sofani akaishika simu yake na kumpigia mama yake.
“Samahani mama kwa kukatisha maongezi yetu mida ile.”
“hakuna hata haja ya samahani kwa sababu siku hizi sisi wazazi wako hatuna tena thamani kwako.”
“kwa nini unasema hivyo mama?
“Kwani si kitu kilicho wazi.Hutaki kutusikiliza chochote tunachokwambia.Hutaki ushauri wetu tena.”
“ Si kweli mama.” Patick akajibu
“Kama si kweli unawezaje kurudi bila kututaarifu kwamba umerudi salama?
“Mama ni kweli nimerudi jioni hii na nilikuwa na mpango wa kuja hapo nyumbani lakini nikiwa njiani nilijisikia hali kubadilika ghafla ikanibidi nirudi nyumbani mara moja.Nimetumia dawa na ninajisikia safi kwa sasa.”
“Mh ! Haya .Sasa sikiliza.Mwenzako alinipigia simu na kunitaarifu kwamba anarudi leo saa nane za usiku.”
“Mwenzangu !! Patrick akauliza
“Ndiyo mwenzako.Kwani una wenzako wangapi? Ina maana Vero si mwenzako?
“Ouh kumbe unasema Vero”
“Ndiyo anarejea leo saa nane za usiku akitokea London alikoenda kwa ajili ya kufanya manunuzi ya harusi yenu.Kwa kuwa umerudi,litakuwa jambo kama ukienda kumpokea uwanja wa ndege.Patrick mwenzako aliondoka hapa akilia machozi na alikubali kwenda London baada ya mimi kumbembeleza afanye hivyo.Tafadhali mfurahishe mwenzako.Nenda ukampokee usiku huu arudipo.Atajiskia mwenye furaha sana pindi akishuka ndegeni na kukuona pale uwanjani.Atasahau kila kitu kilichopita” mama yake akasema .
Patrick akafikiri kidogo na kusema
“Sawa mama nitajitahidi kwenda huko uwanjani.Vipi kuhusu kile kikao?
“Kikao kitafanyika kesho na kila mwanamakati ana taarifa.Katika kikao cha kesho tutafanya majumuisho ya kila kitu na kuangalia kama kuna kitu kilichobaki na kisha jumatatu ndoa ikaandikishwe na kuanza kutangazwa kanisani.Kwa ujumla kila kitu kipo tayari.”
“Sawa mama .Nitafika katika kikao hicho Kuna mambo nataka kuongea na wanakamati wote kwa ndugu wa karibu kwa ujumla.Jitahidi wewe na baba muwepo na umtaarifu pia mama yake Vero naye awepo.Ni muhimu sana..”
“Patrick unataka kutueleza kitu gani? Mama yake akauliza
“Ni masuala madogo madogo tu ya kuwekana sawa kuhusu mambo haya ya harusi” Patrick akasema kisha akaagana na mama yake akaegemeza kichwa sofani na kuvuta pumzi ndefu.
“ Hatua kubwa imeshapigwa mpaka sasa.Kila kitu kiko tayari .Fedha nyingi imeshatumika katika maandalizi ya harusi hii.Ndugu jamaa na marafiki wote wana taarifa juu ya harusi yangu na wanaisubiri kwa hamu kubwa na wengi wametoa michango yao kwa ajili ya maandalizi ya harusi hii.Mambo hayatakuwa rahisi kama nilivyotegemea.Hakuna atakayekubali uhusiano huu uvunjike.hakuna atakayekubali ndoa hii isitishwe.Hakuna atakayenielewa.Hawatanielewa kwa sababu hakuna anayefahamu wapi nimetoka na Happy zaidi ya Andrew .Wazazi wangu walimchukia Happy hasa kwa kitendo chake cha kwenda kusoma Marekani na kuniacha gerezani.Sipati picha nini kitatokea wakisikia kwamba ninaachana na Vero kwa ajili ya kuwa na Happy.Nafahamu sintaeleweka katika jamii lakini siwezi kurudi nyuma.Lazima niachane na Vero.Nafahamu Vero anavyonipenda lakini alifanya kosa kubwa sana kuamua kunitenganisha na furaha ya moyo wangu.namuonea huruma sana.Atateseka sana lakini sina namna nyingine ya kufanya .Kwa ajili ya Happy chochote kile nitafanya.Kwa upande wa Happy jambo hili linaweza kumletea picha mbaya katika jamii.Ninafahamu kwa sasa yeye ni mrembo wa Tanzania na ni mtu maarufu.Kila akifanyacho kinatengeneza kichwa cha habari.Kama waandishi wa habari wakilipata jambo hili litasababisha heshima ya Happy kuporomoka ghafla.Nitakuwa nimemsababishia matatizo makubwa mtoto mzuri kama huyu ambaye taifa linamtazama kama mrembo ambaye anaweza akaliletea sifa kubwa sana kupitia taji lake hili” Akawaza Patrick akiwa ameketi sofani.Akainuka akawasha luninga akarudi tena kuketi sofani.
“Nilimuahidi mama kwamba nitakwenda kumpokea Vero usiku huu.No ! siwezi kufanya hivyo.Sijisikii kuonana na Vero kwa sasa.Ninaweza nikaharibu mambo angali bado mapema.Nataka kila kitu kiishe kesho mbele ya ndugu na jamaa.Nataka kila mmoja afahamu nini Vero alinifanyia.Kwa sababu nilikwisha muahidi mama kwamba nitakwenda kumpokea Vero,ngoja niwasiliane na Andrew ili nimuombe akampokee Vero uwanja wa ndege.”
* * * *
Honi ya gari ikamstua Andrew akiwa jikoni akijiandalia chakula cha jioni.Akazima jiko na kutoka mle jikoni akaelekea getini .Akafungua na kukutana na gari jipya kabisa aina ya Range rover vogue jeusi.Akastuka na kujiuliza ni nani yule kwa sababu hajawahi kuliona gari lile pale kwake.Akalisogelea na mara kioo cha gari kikashushwa taratibu akakutana na sura yenye tabasamu ya mpenzi wake Vick.
“ Vicky ! ” Andrew akasema kwa mshangao huku akilifungua geti lote na gari likaingia ndani.
“Naona kama ndoto .Ni wewe kweli? Andrew akauliza akiwa haamini
“Ni mimi Andrew.Kwani kuna kitu gani cha ajabu? Vick akauliza huku akishuka garini.
“wow ! umeazima wapi gari la thamani kubwa namna hii?
“Ina maana mimi siwezi kumiliki gari la namna hii?” Vick akauliza
“Kwa maana hiyo gari hili ni lako? Andrew akasema huku akicheka
“Ndiyo ni gari langu.Kuna tatizo lolote mimi kuwa na gari kama hili?
“hakuna tatizo lakini unapokuwa na kitu cha thamani kama hiki,kuna tatizo gani mwenzio akifahamu umekipataje pataje? Andrew akauliza
“Kwa maana hiyo unahofia kwamba ninaweza kuwa nimenunuliwa na mwanaume mwingine? Vick akauliza huku akimkazia macho Andrew
“Hata kama umenunuliwa na mwanaume mwingine unaweza ukaniambia?
“Hakuna kitu nilichowahi kukuficha mpenzi wangu na kwa hili ninataka kukueleza ukweli kwamba nimenunuliwa na bosi wangu ambaye mimi ni kimada wake.” Vick akasema na ghafla Andrew akageuza macho akaanguka chini
Vick akamuinamia akambusu na wote wakaangua kicheko kikubwa.
“Usirudie tena kusema hivyo.Unajua sisi wengine hatukawii kuanguka kwa presha” Andrew akasema huku akicheka
“kama ingekuwa ni kweli ningemkata kichwa huyo bosi wako” Andrew akasema na kumfanya Vick acheke kwa nguvu.
“Kweli Andrew unaweza ukakata mtu kichwa kwa ajili yangu?
“Nakwambia ukweli Vick.Niko tayari kukata mtu kichwa kwa ajili yako” Akasema Andrew na kumfanya Vick aendelee kucheka.
“Inuka twende ndani darling.Hili ni gari la mama ametumiwa na dada Toka Ulaya kwa hiyo ameniachia nilitumie” Vick akasema wakati wakiinuka na kuelekea ndani.
Mara tu baada ya kuingia sebuleni simu yake ikaita.Akaichukua na kuangalia mpigaji.Alikuwa ni Patrick.
“halo Patrick” akasema Andrew baada ya kuipokea simu ile.Vick ambaye alikuwa karibu akastuka na kugeuka.
“Patrick ! ina maana Parick amerudi? Akauliza na Andrew akamfanyia ishara kwamba anyamaze
“Andrew kuna jambo limejitokeza ninaomba msaada wako” Akasema Patrick
“jambo gani hilo? Andrew akauliza
“Nimeongea na mama muda mfupi uliopita.Amenitaarifu kwamba Vero anarejea leo saa nane za usiku na akanitaka kwenda kumpokea uwanja wa ndege.Kwa kuwa sikutaka mabishano na mama ikanilazimu kumkubalia kwamba nitakwenda huko uwanja wa ndege kumpokea Vero.Andrew sikufichi kwamba pamoja na kumkubalia mama lakini siko tayari bado kuonana na Vero kwa sasa.Ninaogopa mambo yanaweza yakaharibika mapema.kwa hiyo ninaomba kama hutajali unisaidie kwenda kumpokea Vero.Najua hili ni suala gumu kwako lakini sina mwingine ambaye ninaweza nikamkimbilia kwa msaada.naomba unisaidie kwa hilo” Patrick akasema na kumfanya Andrew akae kimya kwa muda.
“Andrew upo? Akauliza Patrick
“Nipo Patrick nilikuwa natafakari kidogo.Anyway nitakwenda huko uwanjani.”
“nashukuru sana Andrew .Umenisaidia sana ndugu yangu.Hilo ni deni kubwa kwangu.Ngoja niwasiliane na mama anipe namba ya ndege atakayokuja nayo Vero” Patrick akasema na kukata simu.Andrew akabaki katika mawazo mengi,na mara akastuliwa na Vick
“Andrew hebu nieleze.Patrick amerudi?
“Ndiyo amerudi jioni ya leo”
“Alikuwa amekwenda wapi?
“Hakuniambia alikuwa wapi ila alichoniambia ni kwamba alikuwa nje ya mkoa kwa dharura”
“Nimesikia mkiongea kuhusu namba ya ndege.Nani anakuja na dege? Vick akauliza na kumfanya Andrew asite kujibu.
“Andrew niambie tafadhali nani anayekuja na ndege?
“Vero anarudi leo toka London kwa hiyo Patrick ameniomba niende nikampokee badala yake” Andrew akasema
“ Andrew are you out of your mind? Kwa nini yeye ambaye ndiye mpenzi wake asiende na akutume wewe? Vick akauliza
“Patrick hajisikii vizuri na ndiyo maana ameniomba nikampokee Vero badala yake.”
“No Andrew you are not going “ Vick akasema uso wake ukiwa umebadilika
“Unasemaje? Andrew akauliza
“You are not going. Andrew wakati umefika sasa wa kuyaacha mambo ya Patrick na Vero na kuangalia mambo yetu. Sisi tuna mambo mengi ya kukaa na kuongea kuhusu maisha yetu ya baadae. Leo hii nimekuja ili niwe na mpenzi wangu na mimi nifurahi lakini badala yake the whole night unakwenda kumpokea mpenzi wa rafiki yako.Is that fair? Vick akauliza. Andrew akamtazama mpenzi wake halafu akamsogelea karibu akamshika mabegani.
“Vick nimekuelewa. Hata mimi si kwamba ninapenda kuwa mstari wa mbele katika masuala ya Patrick na Vero na kusahau mambo yetu. You are always my everything. You are my breath and my life. Ninamshukuru Mungu kila siku kwa zawadi hii kubwa aliyonipa ya kuwa nawe.Nakupenda sana malaika wangu na niko tayari kufanya chochote kile kwa ajili ya kukufanya uwe ni mwenye furaha daima.Nafahamu umuhimu wako kwangu lakini Patrick he is my best friend.Mimi ni rafiki yake pekee anayeniamini kwa sasa.Sina namna ya kuweza kumkatalia kwa jambo aliloniomba kwa sababu yuko katika wakati mgumu mno kwa sasa na anahitaji msaada.Please let me do this for him and after this, I’m done.Mambo yake atayafanya yeye mwenyewe lakini kwa usiku wa leo naomba uniruhusu niende nikampokee Vero.”
Vick akamtazama Andrew kwa makini akasogea karibu akamkumbatia na kumbusu kisha akasema
“Usihofu baby nimekuelewa. Nitakusindikiza huko uwanja wa ndege siwezi kukuacha uende huko peke yako.lakini naomba uniahidi kwamba baada ya hili utaachana na mambo ya Patrick na kuelekeza nguvu katika mipango yetu”
Huku akitabasamu Andrew akasema
“I promise “
Vick akambusu tena na kusema
“Ok kabla hatujakwenda huko uwanja wa ndege twende kwanza chumbani.Nafasi yangu mimi ni ya kwanza kabla ya hao rafiki zako.” Vick akasema na taratibu wakaelekea chumbani
* * * *
Ni saa tano za usiku sasa lakini hakuhisi dalili zozote za kuonyesha kupata usingizi.Kila alipojaribu kufumba macho ni picha moja tu iliyokuwa ikimjia .Picha ya Patrick.Happy alishindwa kulala akaamka na kuketi kitandani.
“Am I going crazy? Mbona najihisi kama vile siko kawaida? Patrick amenipa nini hadi nishindwe kupata usingizi kwa ajili yake? Kwa siku hizi chache nilizokaa naye Arusha amenifanya niwe kama chizi.Siku hizi chache nilizokuwa naye Arusha ndizo zilikuwa siku pekee zenye furaha katika maisha yangu.I lived my whole life in those few days.Sidhani kama nitarudi katika hali yangu ya kawaida bila ya kuwa na Patrick.Ni yeye tu ndiye atakayeweza kuniondolea uchizi huu ulionipanda kichwani .This is too much .This is beyond love.Nitafanya kila kitu kwa ajili ya kuwa naye.I swear I’m going to do anything to get him.He’s all mine.” Akawaza Happy ,akainuka akachukua glasi ya maji akanywa,akaichukua picha ya Patrick akaitazama akaibusu .
“Siwezi kupata usingizi bila kuisikia sauti ya Patrick.Sielewi ni kitu gani kimemfanya asinipigie simu wakati aliniahidi kwamba atanipigia usiku..” akawaza Happy huku akichukua simu na kupiga
“Hallo my angel” akasema Patrick
“Patrick my love, nimeshindwa kulala bila kuisikia sauti yako. Tafadhali usichelewe tena kunipigia simu mpenzi wangu. Kwa sasa siwezi kukaa muda mrefu bila kukuona na kuisikia sauti yako tamu. .Naona aibu kusema lakini ukweli ni kwamba I’m crazy for you Patrick.” Happy akasema
“Ouh my angel,samahani sana kwa kuchelewa kukupigia simu hata hivyo nilikuwa katika maandalizi ya kukupigia simu muda si mrefu.Toka nimefika hapa nilikuwa katika shughuli za usafi kuiweka nyumba katika hali nzuri.”
“Pole sana Patrick.Kuanzia sasa fahamu kwamba siwezi kumaliza siku moja bila kukuona au kuisikia sauti yako nzuri.” Happy akasema
“nalifahamu hilo Happy na ndiyo maana nimekuahidi kufanya kila niwezalo ili kuhakikisha kwamba tunakuwa pamoja daima.Ni wewe tu ambaye unanifanya nijione kama malaika wa peponi.Ni wewe tu uliyeibeba furaha ya moyo wangu” Akasema Patrick
“ Vipi umeshaongea na Vero? Happy akauliza
“Vero alikuwa safarini ulaya na anarejea usiku wa leo.Nimeitisha kikao kesho na katika kikao hicho nitawaeleza kila kitu na kuuvunjilia mbali uchumba wangu na Vero.Nafahamu halitakuwa jambo rahisi lakini nimekwisha jiandaa kukabiliana nalolote litakalojitokeza.Usiumize kichwa kuhusu hilo.Muda si mrefu ile ndoto yetu itatimia”
“nafurahi kusikia hivyo Patick.Hata mimi kesho nitaonana na Mike na nitamueleza ukweli.Mike ananipenda kwa hilo siwezi kuficha lakini sina namna nyingine ya kufanya zaidi ya kuachana naye.Ni mtu mwelewa na ninatumai atanielewa “ Happy akasema.
“Kwa hiyo mpaka kesho jioni tutakuwa na jibu lenye uhakika zaidi kuhusiana na suala hili gumu.Happy naomba uwe jasiri kwa sababu hii ni kwa ajili ya maisha yetu,kwa ajili ya furaha yetu.Kwa lolote litakalotokea,naomba uniahidi kwamba hautarudi nyuma.Tutashikamana pamoja hadi mwisho.” Akasema Patrick
“Kwa penzi zito nililonalo kwako ambalo haliwezi kulinganishwa na kitu chochote,kwa kuwa wewe ndiye mwanaume pekee niliyekukabidhi moyo wangu uutunze hadi mwisho wa maisha yangu,ninakuahidi kwamba sintarudi nyuma.Niko tayari kukabiliana na lolote lile ambalo linaweza kuwa kikwazo cha sisi kutimiza ndoto yetu ya kuwa pamoja.”
Happy akasema huku macho yake yakilengwa na machozi
“Nimekuelewa mpenzi wangu.naomba sasa ulale tutaonana kesho.Nitakupigia simu kesho asubuhi na mapema kukupa busu la asubuhi” Patrick akasema
“nashukuru sana malaika wangu .Sasa ninaweza kulala baada ya kuisikia sauti yako. kabla sijasahu naomba uniimbie ule wimbo uliopenda kuniimbia tukiwa Arusha ” Happy akasema
“Wimbo upi? Patrick akauliza
“Ule wa Diamond Platinum..Lala salama”
Patrick akacheka na kuanza kumuimbia Happy wimbo ule mzuri uliomfanya Happy ahisi kama vile yuko na Patrick karibu yake.