STORY: Miss Tanzania

STORY: Miss Tanzania

Yaani hukuuu....mzuka umenipoteaa......kaaaabsaaa...
...paka nimalizane na penny kwanza.....siku chache kufikia wiki 2......nasubiri...
 
Yaani hukuuu....mzuka umenipoteaa......kaaaabsaaa...
...paka nimalizane na penny kwanza.....siku chache kufikia wiki 2......nasubiri...
mkuu huwezi piga miguu yote miwili kwani??
 
LEGE bandika mkuu... Leo hata weekend iende vzur..!!
Liverpool hawatatuangusha leo..!!
 
Mapenzi ya kishule shule yamenikumbusha mbali.kijana anamwaga mistari unainama chini.vitoto vya siku hizi mambo yamebadilika
 
Mungu anakuona mkuu....unavyocheza na akili zetu...... umetuwekea.kigogo.kwenye paniela..... umetuteremshia huku.... haya bhana.....
Na mkasa wa love till I die..kama.utatekelezeka....akati washambiwa na kuchumbiana....
 
Sasa Mkuu Lege na huku tena Kuwe kama Paniela
Hebu Shusha vitu Mkuu leo Weekend walau Tupoze Machungu Ya Mbeleko wanayo bebewa Watani wetu (Wakimataifa)
 
Jamani miss Tanzania njoo usiwe kama peniela ametutoroka
 
3





MALANGALI SEKONDARI -IRINGA



Ni ijumaa iliyotawaliwa na kiubaridi cha asubuhi.Hakukuwa na dalili zozote za kuchomoza kwa jua ingawa mida hiyo ilipata saa nne za asubuhi.Anga lote lilifunikwa na mawingu.Pamoja na hali hii ya hewa lakini shughuli ziliendelea kama kawaida.Kwa watu wa eneo hili hali hii walikwisha izoea. Saa nne na dakika kumi basi linalofanya safari zake kati ya Mbeya na Iringa lilifunga breki katika kijiji cha Mbalamaziwa.Dakika kama mbili hivi tangu basi lile lisimame kijana mmoja akashuka akiwa na mabegi matatu.Ilionyesha dhahiri kuwa kijana yule alikuwa mwanafunzi.Baada ya kuhakikisha kuwa mizigo yake yote iko salama basi likaondoka na kumwacha kijana yule akiangaza angaza macho kana kwamba kuna kitu alikuwa akikitafuta.Muda ule ule jamaa mmoja akamfuata. “ dogo unaelekea Malangali? akauliza yule jamaa “Ndiyo kaka “akasema yule kijana. “ gari lile pale inakwenda Malangali muda si mrefu.Tunasubiri watu wawili watatu halafu tunaondoka.”Jamaa yule kumbe alikuwa ni dereva.Akamsaidia kubeba mizigo hadi katika gari dogo aina ya Toyota pick up.Kutoka hapo Mabalamaziwa hadi kijiji cha Malangali usafiri unaotumika ni huu wa gari ndogo.Gari lile halikuwa na abiria yeyote ndani zaidi ya mizigo. “ mbona hakuna abiria yeyote ?”Akauliza kijana yule “ watu wapo si unaona mizigo yao hiyo hapo.Wote wanasubiri muda ufike .Nikipiga honi tu watakuja wote.Wale wote unawaona ni abiria wengine wanakunywa chai kule na muda wa kuondoka ukifika basi watakuja..Unaweza kwenda kupumzika pale kwa yule dada naye ni mwanafunzi anaelekea huko huko Malangali wakati tunasubiri watu wawili watatu” Katika kibanda kimoja cha biashara kilichokuwa hakitumiki msichana mmoja alikuwa amekaa akisoma kitabu chake cha hadithi.Alikuwa amekiinamia kitabu hali iliyoonyesha kuwa alikuwa amenogewa sana na kilichoandikwa kitabuni. “Dada habari yako” Dada yule alistuliwa na sauti ya kijana yule .Kwa sekunde kadhaa alikaa kimya akimtazama yule kaka .Sijui ni kwa nini alifanya vile lakini ni wazi alionyesha mstuko Fulani. “Nzuri habari yako?akajibu kwa sauti laini na ya taratibu sana.Sauti ile ilionyesha kuwa dada yule hakuhitaji kusumbuliwa kwa wakati ule kwani baada tu ya kuitikia salamu ile akainama na kuendelea kusoma kitabu chake.Akiwa amesimama pembeni yake alimtazama yule dada kwa sekunde kadhaa na kugundua ni kwa nini alikuwa vile.Dada yule alikuwa na uzuri wa kipekee.Alikuwa mweupe ,mwenye nywele ndefu zilizorudishwa nyuma vizuri na kumfanya avutie zaidi.Alikuwa ni mwembamba na mrefu wastani.Binti huyu alijaaliwa sura nzuri yenye uzuri wa kipekee. “Mhh ! hii shule ninayoenda kusoma inaonekana si mchezo.Kama kuna watoto wazuri kama huyu.Anaonekana ana nyodo kweli lakini ngoja nimuulize maswali mawili matatu akikataa kunijibu basi nitaachana naye .”akawaza yule kijana “dada samahani nimeambiwa na yule dereva wa lile gari kuwa na wewe unaelekea malangali .Na wewe ni mwanafunzi pale? akauliza yule kijanaDada yule akainua uso wake na kumtazama yule kijana kama alivyofanya mwanzo. “Ndiyo. kwani vipi?akauliza “ nilitaka tu kufahamu kwa sababu mimi ni mgeni na ninaelekea huko huko Malangali na ni mara yangu ya kwanza nafika huku hivyo nilihitaji kuyafahamu mazingira ya shule yenyewe kabla sijafika”dada yule akamtazama tena .Macho ya binti huyu yalikuwa meupe na makali kiasi kwamba unaweza ukakwepesha macho yako asikuangalie. “Wewe unatokea wapi? akauliza yule dada “Natokea Mazwi secondary Sumbawanga” “Uko kidato cha ngapi?Akauliza tena yule binti “Kidato cha tatu”akajibu yule kijana “hata mimi niko kidato cha tatu”Akajibu yule dada. “Kumbe tuko kidato kimoja?” “Yeah .Ila pale kuna michepuo.Mimi niko mchepuo wa sanaa. wewe je ? “hata mimi ninasoma sanaa.Vipi unaionaje shule kwa ujumla ? ufundishaji wao ukoje ? Akauliza kijana yule nadhifu “wanajitahidi kufundisha.Kumetulia na ni sehemu nzuri kwa kusoma.Mi napapenda sana”akajibu yule binti “aisee kumbe nilifanya chaguo zuri” ‘hata mimi mwanzoni nilidhani kuwa nilikosea kuhamia shule hii .Mwanzoni nilipata shida sana kuzoea lakini mpaka sasa nimeshazoea na nimetokea kupapenda sana ”Akajibu yule dada “Kumbe hata wewe ulihamia?Yule kijana akauliza “Yes .Nilikuwa nasoma Mbeya secondary nikahamia huku.Sikutaka kusoma mjini nilitaka kusoma mahala tulivu mbali na nyumbani ” akasema yule dada “Umehamia mwaka huu? akauliza yule kijana “Hapana toka mwaka jana”
Taratibu walianza kuzoeana.Binti yule kumbe alikuwa mcheshi na muongeaji mzuri.Kwa upande wake naye alifurahia sana uchangamfu wa yule kijana. “lakini kwa ujumla unaniambiaje kuhusu mazingira ?kijana yule akauliza. “mazingira siyo mabaya.Mabweni ni mazuri kwa ajili ya wavulana .Sisi wasichana tunalala hosteli.Ni hosteli nzuri ya kanisa.Wale wasiopenda kulala hosteli wanapanga vyumba kijijini.Maisha ni mazuri ukisha zoea ila kwa wewe nadhani utapata shida kidogo mwanzoni.” Akasema yule dada huku akicheka. “kwa nini unahisi ninaweza kupata shida?akauliza kijana yule. “hahahaha! " akacheka yule dada
" muonekano wako unaonyesha hujazoea maisha ya shida”akasema huku akicheka.Kijana yule naye akacheka sana kisha akasema “sasa mimi na wewe nani anayeonekana hajazoea shida? “hahahaha ! hata mimi mwanzoni nilipata shida sana lakini kwa kiasi Fulani naweza kusema kwa sasa nimeshaanza kuizoea hali halisi ya mazingira”akasema yule msichana.Kimya kikapita cha kama dakika mbili hivi kila mmoja akiwaza lake.Yule kijana akauvunja ukimya. “Kwani wewe dada waitwa nani?Binti yule akatabasamu kisha kama anajishauri aseme au asiseme akajikuta akitamka “naitwa Happy Happy Kibaho ..Wewe unaitwa nani? “Mimi naitwa Patrick ”
“Happy nimefurahi sana kukufahamu.Na kama hutajali nitafurahi ikiwa utakuwa mwenyeji wangu” akasema Patrick. “Hilo tu usijali.Nitakufundisha jinsi ya kunywa uji na maandazi yanayoumuliwa kwa ulanzi” akasema Happy na wote wakacheka. “Ulanzi ! Mbona nasikia ulanzi ni pombe? akauliza patrick “Yes ni pombe tena kule iko nyingi sana.Unakunywa pombe?”
" Hapana sinywi pombe" akajibu patrick. “Kwa hiyo sasa hivi umetoka wapi happy ? Patrick akauliza. “Niliomba ruhusa ya wiki moja.Nilikwenda nyumbani mara moja nilikuwa na matatizo kidogo na leo ndio narudi shuleni.Twende pale kibandani tukapate chai unajua niliondoka asubuhi bila hata kunywa chai” Happy akasema Wakainuka pale kibandani walikokuwa wamekaa na kuelekea katika moja ya vibanda vinavyouza chai
.

* * * *

“Haya wale wanafunzi wa Malangali tumefika.”akasema utingo wa lile gari walimokuwa wamepanda akina Patrick.Yeye na Happy walikuwa wanafunzi pekee katika ile gari wakashuka..Mida hiyo ilipata saa saba za mchana.Safari ilikuwa ni ndefu kidogo hasa kutokana na barabara . " Patrick tushuke” Akasema Happy akiwa wa kwanza kushuka kisha akaanza kupokea mizigo ya Patrick. Happy akatoa pesa na kumlipa yule utingo . “kata nauli ya watu wawili” “No Happy nina nauli yangu hapa”akasema Patrick “Usijali Patrick just keep it”akasema Happy huku akitabasamu.Abiria wote waliokuwamo katika ile gari macho yao yalikuwa kwa binti huyu mrembo.Kwa muonekano wake alionyesha dhahiri kuwa alitoka katika familia yenye uwezo mkubwa kifedha.wote walistaajabia uzuri wa binti huyu. “Poa mrembo karibu tena siku nyingine” akasema utingo huku akimminyia Happy jicho moja gari ikatimua vumbi na kuondoka Patrick akageuza shingo na kutazama majengo ya shule.Idadi kubwa ya wanafunzi waliokuwa katika mapumziko ya mchana walikuwa wamesimama wakiwaangalia .Patrick alishangaa kidogo kwa namna walivyokuwa wakiangaliwa.Taratibu akaanza kujiuliza maswali juu ya kuangaliwa kule.Je ni kwa sababu alikuwa na Happy ?Au ni kawaida kwa mwanafunzi mgeni kuangaliwa namna ile? “Patrick beba begi hilo mimi ngoja nikusaidie hili hapa.”akasema Happy na kumstua Patrick " Ahsante Happy lakini utaweza kulibeba hilo ni zito sana.Beba hili dogo.”Wakabeba mabegi yale na kuanza kuelekea katika ofisi za shule.Ili kufika ofisini ni lazima upite katikati ya shule.Bado wanafunzi walikuwa wakiwaangalia na wengine wakisemezana.Kitendo hiki cha wanafunzi kuwaangalia kisha kuanza kusemezana wao kwa wao kilimzidishia Patrick ushawishi wa kutaka kufahamu kulikoni. “Happy mbona wanafunzi wanatuangalia sana ? “Just ignore them”akasema Happy kwa kifupi.Wakafika katika ofisi za shule mizigo ikawekwa chini. “Hapa ndio ofisi ya mkuu wa shule msaidizi .Ingia ndani ye ndiye atakayekusajili na kukupa maelekezo yote.Bye tutaonana baadae pengine tunaweza kuwa darasa moja’akasema Happy huku akichanua tabasamu pana na kuyaonyesha meno yake meupe na mwanya wa kupendeza katika meno ya juu. “Nashukuru sana Happy tutaonana baadae” akasema patrick na Happy akaondoka .Patrick akagonga mlango na kuruhusiwa kuingia. “Welcome gentleman.where are you from ? Ilikuwa ni sauti ya ukakamavu ya mtu ambaye Patrick aliamini moja kwa moja kuwa ndiye alikuwa mkuu wa shule msaidizi. “From Mazwi secondary school sir ”Patrick akajibu. “Ohh ! Mazwi!
Patrick akasajiliwa kisha mwalimu yule akatoka nje na kumwita mwanafunzi mmoja na kumuomba ampeleke Patrick katika bweni la Shaaban Robert.Mwanafunzi yule akamsaidia mizigo na kumpeleka katika bweni hilo lililo upande wa juu kabisa wa shule hii.Pale bwenini akapata kitanda kilichokuwa wazi akaweka mizigo yake.akajilaza kitandani huku akijaribu kuwaza jinsi atakavyoweza kuyakabili maisha mapya ya shuleni pale..Hakuwahi kusoma katika shule ya bweni na hii ilikuwa mara yake ya kwanza. “lakini Happy yupo atanisaidia kuyazoea maisha ya hapa.Kama yeye mtoto wa kike amezoea kwa nini mimi nishindwe ? Nitazoea tu.Halafu shule hii inaonekana ina wanafunzi washamba sana kwa nini walikuwa wakituangalia vile wakati tumeshuka mchana.Au mimi ninaonekana niko tofauti na wao? akawaza Patrick Mawazo yake yakastuliwa na sauti ya mwanafunzi mmoja aliyeingia bwenini humo kwa kelele.Akamsogelea Patrick na kumsalimu kisha akaelekea katika kitanda chake kupumzika.
* * * *
Saa kumi na moja jioni Patrick akaamua kuzunguka zunguka maeneo ya hapo shuleni.Ilikuwa ni mwishoni mwa wiki hivyo kulikuwa na pilika pilika nyingi.Ni wanafunzi wachache tu waliokuwamo madarasani jioni hii wakijisomea.Alipofika katika bwalo la chakula akamuuliza mwanafunzi mmoja yalipo madarasa ya kidato cha tatu .Alitaka kutembelea na kuangalia madarasa atakayo kuwa akisomea.Yalikuwa ni madarsa yaliyofuatana.Yaani kidato cha tatu A B na C.Yeye alikuwa amepangiwa kusoma kidato cha tatu C.Akayapita madarasa ya A na B akaelekea katika darasa la C .Mlango haukuwa umefungwa akaingia ndani na mara macho yake yakagongana na macho ya Happy . “Happy !! ..”akaita Patrick kwa mshangao.Hakutegemea kama angemkuta happy mle darasani. “Patrick ! Naona umeshaanza kuwa mwenyeji" akasema Happy huku akitabasamuPatrick akacheka.
" niambie unaendeleaje ? umeshaanza kuzoea?Umepangiwa bweni gani?”Happy akauliza maswali mfululizo huku akifunika vitabu vyake. “Nimepangiwa bweni la Shaabani Robert na darasa ni hili hili C”Happy akatoa tabasamu pana sana. “karibu sana hata mimi ninasoma humu humu.” “nafurahi sana kufahamu kuwa tutakuwa wote darasani.Vipi mbona uko hapa peke yako? “Nimeamua tu kuja kukaa huku kwa sababu kule hosteli ninaboreka sana.Mara nyingi hupenda kuja huku kujisomea mwenyewe.sipendi kelele.” “nimeambiwa kuwa kuna maktaba huku “Patrick akauliza. “Yes ipo lakini mimi sipendi kwenda huko.Mara nyingi huwa nakuja huku darasani.Sipendi kusoma na watu wengi.Patrick naomba tuwe tukisoma wote” akasema Happy.Patrick akatabasamu kisha akasema. “Usijali Happy tutasoma wote ”waliongea mpaka ikafika mida ya saa kumi na mbili Happy akaomba Patrick amsindikize kurudi hosteli kwao.Bila hiyana Patrick akakubali.wakatoka wote darasani wakaanza kupanda kilima kuelekea hosteli ya akina Happy .Kila mwanafunzi waliyekutana naye alikuwa akiwatazama.Patrick akaamua kumuuliza Happy “Happy mbona kila mtu tukikutana naye anatuangalia sana kwa nini?Toka tumefika mchana naona watu wakitushangaa mno !!Happy akatabasamu kisha akajibu “Achana nao Patrick ,Jali mambo yako.Kamwe usiwasikilize wanafunzi wa hapa wana mambo ya kipuuzi sana. wakiona mtu mgeni sijui wanakuwaje. ukitaka kuishi kwa amani mahala hapa jitahidi kufuata kile kilichokuleta yaani masomo”Happy akasema kwa sauti ambayo haikuwa ile yake ya kawaida.Patrick hakutaka kuuliza tena kuhusu suala hilo. “Patrick kesho jumamosi kuna mnada hapo kijiji cha mbele vipi ungependa kwenda kutembea ? “Yes ni vizuri kama nikienda ili nianze kuyazoea mazingira” “Ok nitakupitia basi mida ya saa tano ili tukashinde huko mpaka jioni .Huwa ni pazuri sana.Unajua sku za mwisho wa wiki hapa shuleni panakuwa kimya mno.Halafu kama utakuwa tayari , jumapili tutaenda sehemu moja inaitwa stone beach.Ni pazuri pia.Mi hupenda kwenda kutulia kule siku kama hizi za weekend.” akasema Happy " usijali Happy tutakwenda huko kote unakotaka twende” akajibu Patrick.Hatua chache mbele yao wakaliona geti la kuelekea hosteli ya wasichana wakaagana na Patrick akarejea bwenini.
Saa nne na nusu asubuhi siku iliyofuata alikuja mpishi katika bweni alilokuwa akilala Patrick na kuanza kumuulizia. “wewe ndiye Patrick? akauliza mzee yule wa makamo baada ya Patrick kujitokeza. “ ndiyo mimi”Patrick akajibu “Nimeagiziwa na binti mmoja anaitwa Happy kuwa anahitaji kukuona sasa hivi .Panda na barabara utamkuta pale mbele karibu na kanisa anakusubiri.” “Ok mzee nashukuru”Mzee yule akaondoka kisha Patrick akavaa viatu vyake akaondoka kuelekea mahala alipoagiziwa na Happy .siku hii alikuwa amependeza vilivyo.alikuwa amevaa kaptura ya jeans rangi nyeupe,juu akavaa fulana nzuri yenye mistari ya kijani na nyeupe halafu akavaa na mkufu wake wa dhahabu uliomfanya avutie zaidi.Chini akavaa raba nzuri nyeupe na soksi nzuri .Mwisho kabisa akajipulizia uturi wenye harufu nzuri .Kwa ujumla alikuwa amependeza sana kijana huyu.Wakati akitoka alisikia baadhi ya wanafunzi waliokuwa hapo bwenini wakifanya usafi wakinong’onezana. “alaaa kumbe ndo huyu !” akasema mmoja wao “Du bonge la brother maskini .haelewi “akadakia mwingine. Patrick hakutilia maanani sana minong’ono ile akawapuuza na kuondoka zake.Alitamani sana kuonana na Happy kwani aliamini ni yeye tu ndiye anayeweza kumfanya akazoea mazingira yale magumu.Tangu amewasili bado hajapata rafiki wa karibu kama Happy .Kwa mbali alimuona Happy amekaa chini ya mti amejiinamia.Moyo ukafurahi baada ya kumuona tena binti yule mrembo.Kwa mbali tu aliweza kutambua utofauti katika muonekano wa Happy .
" Happy mambo vipi ”akasema Patrick “Poa tu Patrick , mzima? Akasema Happy halafu akainua machoPatrick akastuka kisha akauliza “Happy kulikoni mbona macho mekundu na inaonyesha ulikuwa ukilia.Unaumwa?Happy akanyamaza na kuanza kulia kwa kwikwi.Patrick akajua lazima kuna kitu kimemsibu binti yule.akatoa kitambaa na kumpatia “Chukua hii futa machozi”Happy akachukua kitambaa kile na kufuta machozi. “Niambie Happy kitu gani kimekusibu mpaka ukawa katika hali hii? “Patrick naona nitashindwa.” “kwani kuna nini Happy ?.Niambie kama una tatizo ili tuone namna ya kulitatua.” “Patrick hapa shuleni mimi nina matatizo makubwa. wenzangu wananichukia sana sijui nimewakosea kitu gani.Mara waseme eti mimi ninaringa sana ,wanasema eti ninajidai kwa kuwa familia yangu ina pesa nyingi,eti ninajifanya mtoto wa tajiri.Hiyo ni sababu ambayo imewafanya wanitenge na hakuna mtu anayetaka hata kushirikiana nami kitu chochote.Hata kusoma huwa nasoma peke yangu.Kwa hivi sasa shule nzima wanajua eti mimi nimeathirika na virusi vya ukimwi..Habari hizo zimesambaa kila mahala na hii ndio imenifanya nikose hata rafiki.Mimi silijali hilo kwa sababu ninafahamu mimi mwenyewe kuwa mambo hayo si ya kweli.Hata baadhi ya walimu wanaamini hivyo .Kuna siku walikuja watu wa afya na kuwataka watu wapime afya zao na karibu wanafunzi wote wakapima kasoro mimi.Nilikataa kupima kwa sababu nimekwisha pima toka huko nilikotoka na zaidi ya yote ninajiamini mimi mwenyewe kuwa sina ugonjwa huo wanaosema ninao.Kwa kipindi hicho walichokuja kupima nilikuwa ninasumbuliwa na kifua basi baada ya kukataa kupima afya , ikawadhihirishia watu kuwa ni kweli nina ugonjwa huo.Mimi sioni ajabu kwa sababu hata huko nilikotokea mambo haya yalinikuta na ndiyo sababu kubwa iliyonifanya nihame.Huku nako nikakuta mambo ni kama yale yale .Nilipata taabu mwanzoni lakini ikafika mahala nikazoea.Nimejaribu kuwa wazi kuwa mimi sisumbuliwi na ugonjwa huo wanaodai ninao lakini hakuna anayeniamini na hasa ukichukulia huu mwili wangu jinsi ulivyo basi kila mtu anajua ninaumwa.Namshukuru Mungu kwa sababu kwa sasa nimekwisha pona lakini hakuna mtu anayetaka hata kuchangamana nami.Pale tulipokutana nilikuwa nimetoka tena kufanya vipimo ili kujua kama ugonjwa ule wa kifua ulionisumbua kwa muda mrefu umekwisha kabisa au vipi.na kwa bahati nzuri madaktari wakanithibitishia kuwa tayari nimepona .Wewe mwenyewe jana uliona wanafunzi walivyokuwa wakituangalia wakati nakusindikiza i.wote walikuwa wanakusikitikia wewe.”Happy akanyamaza na kufuta machozi yaliyokuwa yakitoka.Patrick akawa kimya kabisa kumsikiliza.Kijasho kilikuwa kikimtiririka.Happy akaendelea. “Kibaya zaidi ni leo asubuhi.Nilikuwa nimeenda kuoga nikasahau kufunga sanduku langu .Niliporudi nikakuta pesa zangu zote karibu laki moja na ishirini na tatu elfu hazipo.Nimejaribu kuuliza lakini hakuna mtu yeyote anayejua zimeenda wapi.Ninaelewa hizi ni njama za wazi za watu wasionipenda.” Patrick akavuta pumzi ndefu na kumwangalia Happy kwa makini .alimuonea huruma sana binti yule kwa matatizo anayoyapata.Sasa alipata jibu kwa nini wale wanafunzi walikuwa wakimwangalia sana na hata kusemezana wao kwa wao kila walipomuona yuko na Happy .Roho ikamuuma kumuona binti mrembo kama yule akitoa machozi.Ni wazi hakustahili kufanyiwa vile hata kama angekuwa ameathirika kama wanafunzi hao wanavyodai.. “Hawa watu wa namna gani ambao wanawafanya wenzao namna hii?Hivi ndio tunavyofundishwa kuhusu mapendo kwa wenzetu? kama wao waa tabia hizi mimi sijafundishwa namna hii.Wazazi wangu wamenifundisha kuwa na upendo kwa watu wote.Lazima nionyeshe mfano kwa watu hawa na nitaanzia kwa Happy ”Aliwaza Patrick akiwa na fundo la hasira moyoni. Taratibu akamuinamia Happy na kumshika mikono.akamwangalia usoni kwa sekunde kadhaa kisha akasema. “Happy usijali ,nyamaza kulia I’m here for you.I’ll be on your side.Hutalia tena.Hata kama dunia nzima itakutenga na kusimama mbali nawe I’ll be there for you.Hata kama ungekuwa na maradhi hayo wanayosema unayo nisingeweza kukutenga.” Happy akapatwa na furaha ya ghafla baada ya kuambiwa maneno yale akainuka na kumkumbatia Patrick kwa nguvu. “Thanks very much Patrick.Nadhani ni Mungu kakuleta ili uweze kunipa faraja.Baba alitaka kunihamisha na kunipeleka mbali lakini nilikataa kwa sababu nayapenda mazingira haya ya huku.Napenda sana kuwa katika sehemu tulivu kama hii.sikujua kumbe kuna mtu ana kuja ambaye atakuwa ni faraja yangu.” Akasema Happy huku machozi yakimtoka.hakuamini kwa mazingira yale kama kuna mtu angeweza kumtamkia maneno ya faraja kama yale. “Usijali Happy .Hutalia tena.Usijali kuhusu pesa zako kupotea.kama ilikuwa ni njama zao basi wameshindwa.Mimi bado nina kiasi cha kutosha cha pesa nitakugawia na kiasi kitakachobaki tutaendelea kukitumia taratibu.Usijali you are more than a friend to me.To me you are like my sister.” “Thanks Patrick.You are more than a brother to me”akasema Happy ‘Thanks. vipi kuhusu ile safari yetu ya mnadani bado ipo au ndio umeshaifuta? Patrick akauliza “Mimi nilikuwa nimeshaifuta kwa sababu hata kama ningeenda huko ningenunua vitu na nini?wamechukua pesa zote.” “Pole sana. hebu nisubiri kidogo hapa nakuja sasa hivi”Patrick akamwacha Happy pale na kutembea kwa kasi kurudi bwenini..akafungua sanduku lake kubwa na kutoa bahasha Fulani aliyokuwa ameificha .akaiweka mfukoni akafunga sanduku lake na kuondoka kurudi kule alikomwacha Happy . “Happy chukua hii ni laki moja na nusu itakusaidia ila kuwa makini sana wasije wakakuibia tena siku nyingine.”akasema Patrick wakati akihesabu pesa toka katika ile bahasha aliyokwenda kuichukua kule bwenini.Happy hakuamini macho yake.hakuamini kama katika dunia hii bado kuna watu wenye moyo wa huruma kama wa Patrick. “ jamani Patrick Naomba kidogo tu sasa ukinipa hizi zote na wewe je utabakiwa na nini? “Usijali Happy bado nina akiba ya kutosha”Patrick akajibu “No Patrick siwezi kuchukua zote.” “Happy kumbuka ulikuwa ukilia kwa kuibiwa na sasa narudisha kiasi kile kilichokuwa kimeibiwa ili ufute kabisa suala hilo moyoni mwako”Happy akapokea pesa zile. “nashindwa hata kupata neno la kukukushukuru litakalokufaa Patrick.Thanks very much “ “you are welcome" Patrick akasema kisha kikapita kimya kifupi. “Patrick thanks again unajua nilikuwa nawaza sana jinsi ya kumwambia daddy kuwa nimeibiwa kwa sababu si mara ya kwanza namwambia hivyo ananitumia pesa Ila kwa sasa sijui ningesemaje.You are my angel.”akasema Happy “usihofu kitu Happy muda wowote utakaokuwa na tatizo usisite kunitaarifu.I will help you.”Patrick akasema kwa kujiamini.alijisikia vizuri sana kumsaidia binti yule mwenye matatizo aliyekuwa ametengwa .Taratibu wakaondoka mahali pale na kuelekea mnadani.

* * * *
Maisha ya Patrick na Happy yaliendelea kama kawaida shuleni malangali.Kila mara walikuwa pamoja.Waliachana tu pale Happy alipokwenda hosteli kwao.Walisoma pamoja na maendeleo yakawa mazuri sana.Happy akawa ni mtu mwenye furaha kila siku .Ni kweli hakulia tena kama Patrick alivyomuahidi.Alizidi kupendeza na kuwa mrembo zaidi.Kwa muda mfupi urafiki wa Patrick na Happy ukawa gumzo pale shuleni.Wapo waliosema kuwa Patrick na Happy ni ndugu,wengine wakadai kuwa ni wapenzi ilimradi kila mtu akasema lake.Chuki dhidi ya Patrick na Happy ikaongezeka.Na kwa sasa ikawa wazi wazi.Maneno yalitamkwa bila kificho .Wengine wakadai eti Patrick anaringa ,wengine wakadai ana majivuno,wengine wakasema kuwa anaringia pesa za Happy wengine wakamwita mwanaume kama binti na majina ya kila aina.Hii ilimfanya Patrick akose rafiki wa karibu ambaye angeweza hata kumweleza matatizo yake .Rafiki yake mkuu alikuwa ni Happy .Si kwamba alipenda hali hii lakini ilijitokeza yenyewe na ikafika mahala akajikuta akiizoea.Alipenda sana kuwa na marafiki wengi lakini angewapata vipi?kila mtu hakuwa tayari kushirikiana naye. Kwa upande wake Happy naye alikumbana na visa kama alivyokumbana navyo Patrick.Hii haikuwasumbua hata kidogo.Maneno mengi yakasemwa lakini mwisho wa siku ukweli ukabaki pale pale kuwa Patrick na Happy hawawezi kutengana.Maneno ya watu pamoja na visa walivyotendewa vilikuwa ni changamoto kubwa kwao.Siku zote walipeana moyo na ujasiri wa kutokukata tama.Waliongeza juhudi katika masomo na kila mara walionekana kufanya vizuri na kupata alama za juu.Taratibu walimu wakaanza kuwapenda kutokana na juhudi walizozionyesha darasani.Hii ikazidisha chuki miongoni mwa wanafunzi .
4
Ilikuwa ni saa sita na robo siku ya jumatano.Darasani hapakuwa na mwalimu kilikuwa ni kipindi cha kujisomea.Happy akatoka na kwenda msalani.Wakati akirejea kwa bahati mbaya akaligonga daftari la mwanafinzi mmoja wa dawati la mbele kabisa na daftari lake likaanguka chini.Happy akaomba samahani na kuinama kuliokota daftari lile. “Wewe usiguse daftari langu usije na mimi ukaniambukiza magonjwa yako”akasema kwa sauti yule binti aliyeangushiwa daftari lake na Happy .Happy akapandwa na hasira kali kwa kauli ile.Siku zote alivumilia kashfa za kila aina lakini hii ya leo ilimuuma mno.Wanafunzi wakaanza kucheka kwa kejeli.Kitendo hiki kikamzidishia hasira akainuka na kumzaba kofi yule binti na mara ukazuka ugomvi. “Apigweeee huyo !!!… anaringa sanaaa…!!!!!!! acheni afundishwe adabu..”yalikuwa ni maneno ya wanafunzi wakishangilia .Wengine waliinuka na kumsaidia yule binti kumpiga Happy .Patrick ambaye alikuwa katikati ya darasa alikishuhudia kitendo kile wazi wazi naye kama ilivyokuwa kwa Happy akapandwa na hasira zisizomithilika.Akapanda juu ya meza na kuruka meza nyingine kama mbili hivi na kufika mahala pale ulipokuwa ukitokea ugomvi.Akaingilia kati na kuwaamua.Wanafunzi wawili wa kiume walipoona Patrick ameingilia kati ugomvi ule nao wakainuka na kuanza kupigana na Patrick.Kelele zikawa nyingi na zikamfikia mwalimu aliyekuwa darasa la karibu ambaye alifika haraka kuona kuna nini akakuta kuna ugomvi mkubwa.Wanafunzi walipomwona mwalimu wakakimbia kila mmoja katika kiti chake kasoro Patrick na Happy .Patrick alikuwa amevimba kwa hasira. “haya wote mliokuwa mnagombana pita mbele”Yule binti aliyekuwa akigombana na Happy akasimama na kupita mbele. “Si huyu peke yake nimewaona wengi tu piteni wote mliokuwa hapa mnagombana”Akasema mwalimu yule kwa ukali na kuwafanya wanafunzi waogope na kuanza kupita mbele .wakachukuliwa wote na kupelekwa kwa mwalimu wa darasa. “haya nipeni sababu za kugombana”Akasema mwalimu yule mkaliYule binti aliyekuwa akigombana na Happy akasema “Ni huyu hapa ndiye mkorofi.ameangusha daftari langu makusudi kabisa badala ya kuliokota akaanza kunitolea maneno ya kashfa.Mimi nikamwambia kama hataki kuliokota nakuja kushtaki kwa mwalimu yeye akaninasa kibao na kusema kuwa nenda kaseme kwa huyo mwalimu wako tuone atanifanya nini.Muda huo huo huyu hapa sijui ndugu yake akainuka naye akaja wakaanza kunichangia ndio hawa wenzangu wakaja kuniokoa.”Akadanganya yule binti Mwalimu yule akawaangalia Patrick na Happy kwa macho makali.Akawageukia wale wanafunzi wengine watano. “Eti nyie ni kweli haya maneno aliyoyasema mwenzenu? “kweli kabisa mwalimu” wakajibu Haya nyie wote nendeni nitabaki na hawa watukutu wanaojifanya matajiri wa shule.”Wanafunzi wale wengine wakaondoka na kuwaacha Patrick na Happy katika mikono ya mwalimu ambaye alikuwa ameshika fimbo kubwa . “ leo mtanieleza nyie watoto kwa nini mnasababisha ugomvi darasani?Kwanza wewe binti hebu nyoosha mkono wako hapa”Happy huku akilia akanyoosha mkono ili mwalimu aanze kumchapa. “No ! Happy .Usinyooshe.”Patrick akapiga kelele na kwenda kusimama mbele ya Happy . “ kumbe wewe ndiye unayemfundisha kiburi mwenzako.leo utanieleza . haya lala chini haraka.”akafoka mwalimu “Hapana mwalimu silali”Patrick akajibu kwa hasira ..Happy machozi yalikuwa yakimtoka. “Unaonekana una kiburi sana wewe."akadakia mwalimu mwingine aliyetokea ghafla.. “Wewe unajifanya tajiri na vihela vyako leo utaimba “Akasema mwingine huku akisogea akiwa na fimbo mbili mkononi “ walimu hali hii mpaka lini? Uonevu huu mpaka lini ? Kwa nini hamtaki kutupa na sisi nafasi ya kujieleza? Patrick akasema “Unajifanya kujua sheria ? nakwambia leo utaona”mwalimu yule akamsogelea na kutaka kumchapa Patrick mgongoni.Patrick akadaka Fimbo. “Unataka tupigane ? ”Mwalimu yule akatupa fimbo na kukunja ngumi.Ofisi ikageuka kituko.Mara mkuu wa shule msaidizi akapita akasikia kelele ofisini “wamefanya nini hawa? akauliza “wamepigana na wenzao darasani na hawataki kuadhibiwa.” “Siyo hivyo mwalimu.Huu ni uonevu.Huyu mwalimu kapewa maneno ya uongo naye kwa chuki zake anaamua kutuadhibu bila kosa.Chuki za wazi wazi zitakwisha lini?.Happy ananyanyaswa na shule nzima wanasema eti ana ukimwi.Hata kama angekuwa nao hivi ndivyo wanafunzi wanavyofundishwa kuishi na wenzao wagonjwa?”Patrick akaongea maneno mfululizo kwa hasira. “Kwa hiyo mmepigana au hamjapigana" akauliza mkuu wa shule msaidizi “Ukweli ni kwamba Happy alikuwa akitoka msalani na kwa bahati mbaya akaligonga daftari la mwenzake likaanguka chini.Akainama ili aliokote lakini wakati anataka kuliokota yule binti akasema aache daftari lake asije akamuambukiza maradhi yake.Happy akakasirika na kumnasa kibao lakini halikuwa kusudio lake.Hata kama ungekuwa ni wewe nafikiri usingevumilia.Ungejisikiaje kama huyu angekuwa mwanao na unasikia anaambiwa maneno kama yale ?Mwalimu yule msaidizi akakaa kimya kisha akawaamuru Happy na Patrick wamfuate ofisini kwake
“Enhee vijana hebu niambieni nini kilichotokea”akasema mwalimu baada ya Patrick na Happy kufika katika ofisi yake.Happy ndiye aliyeanza kueleza " mimi nilitoka msalani , kwa bahati mbaya nikaligonga daftari la Mwantumu likaanguka chini.Nikamuomba samahani nikainama ili niliokote.Wakati nikiliokota akasimama na kuniambia “acha daftari langu usije ukaniambukiza magonjwa yako”.Kwa kweli mwalimu kauli hii mimi iliniuma sana hasa ukizingatia kuwa hapa shuleni mimi nimekuwa nikitengwa na wanafunzi wanadai eti nimeathirika na ugonjwa wa ukimwi.Mwalimu hata kama ningekuwa na maradhi hayo wanayodai kwa nini basi wanitenge?Kwanini waninyayapae namna hii?Na kwa nini wanizushie kitu ambacho si cha kweli?Inauma sana mwalimu.Kila mwanafunzi ananichukia hapa shuleni na.Kibaya zaidi hata walimu nao wameungana na wanafunzi katika kuoyesha chuki zao za wazi kwangu.” Mwalimu akakaa kimya na kutafakari kisha akasema. “halafu kuna kitu nataka kuwauliza..Kuna tetesi nimezisikia kuwa nyie wawili ni wapenzi.Ni kweli?Wote wawili wakakaa kimya .Hili lilikuwa ni swali ambalo hawakukulitegemea kabisa..Walikaa kimya kwa sekunde kadhaa bila kujibu . “Mbona hamjibu ina maana ni kweli?”Akasema mwalimu kwa ukali.Happy alikuwa akitetemeka mwili.Ni kweli hajawahi kuwa na mpenzi mpaka hapa alipo Hii ilikuwa ni mara yake ya kwanza kuambiwa kuwa ana mpenzi.Patrick yeye alikaa kimya akitafakari ajibu nini.
“Mwalimu sisi si wapenzi kama ulivyosikia .Sisi ni marafiki na muda wote tuko pamoja Kitu kinacho fanya watu wahisi kuwa sisi ni wapenzi ni kwa vile tuko karibu karibu sana.Tunasaidiana karibu katika kila jambo.Tunaishi kama ndugu.Maendeleo yetu ni mazuri.Mwalimu hizo ni chuki tu za watu wasiotutakia mema.Naomba uniamini kuwa sisi si wapenzi kama watu wanavyodhani..”Patrick akasema.Happy machozi yalikuwa yakimtoka.Mbele ya mwalimu mkuu msaidizi . “haya nendeni nitakaa kikao na walimu ili kujadili suala lenu.”Happy na Patrick wakatoka ofisini huku Happy akilia.Patrick akatoa kitambaa mfukoni na kumfuta machozi. “Nyamaza Happy kila kitu kitakuwa sawa,Usilie.”Moja kwa moja wakaelekea darasani.Walipoingia tu darasani minong’ono ikaanza.Happy akashindwa kuvumilia akachukua vitabu vyake na kutoka darasani macho yakiwa yamefunikwa na machozi.Patrick naye akatoka na kumkimbilia . “Happy please hebu nyamaza.Unajua ni kwa kiasi gani unawapa ushindi wale wote wasiokupenda.tayari wanaona wamekwisha kushinda.Be strong Happy .Pambana na utashinda.I’m on your side.i’ll fight for you”Patrick akasema kwa msisitizo. Happy akafuta machozi akatabasamu na kusema. “Ahsante sana Patrick .Nafahamu kuwa uko pamoja na mimi.Naomba kwa sasa nikapumzike tutaonana baadae.Nasikia kichwa kinaniuma .” Patrick akamtazama Happy usoni kisha akasema. “Ok Happy nenda kapumzike tutaonana baadae.”Wakaacha na Patrick akarejea darasani.Ilikuwa ni siku ndefu na ngumu kwa Patrick.Kila mara alikuwa akitafakari juu ya tukio la leo.Ni tukio ambalo lilimuuma sana na kumfanya afikie hatua ya kupigana.Toka amezaliwa hajawahi kupigana na mtu yeyote.Hii ilikuwa ni mara yake ya kwanza kupigana .Ilimuuma sana. “lakini sikuwa na jinsi.Ni lazima nimtetee Happy .Kwa gharama yoyote ile.Kwa nini binti yule anyanyasike bila kosa?Nitahakikisha katika uwepo wangu hapa shuleni ninamsaidia kwa kila hali.Lazima siku moja heshima itapatikana..” akawaza Patrick huku ameinama chini .Mawazo yalikuwa yakija na kupita kwa kasi.Mara akakumbuka kitu.Akakumbuka swali waliloulizwa na mkuu wa shule msaidizi. “halafu kuna kitu nataka kuwauliza..Kuna tetsi nimezisikia kuwa nyie wawili ni wapenzi.Ni kweli? Patrick akatabasamu alipoyakumbuaka maneno haya ya mwalimu mkuu “Kumbe siku zote watu wanahisi kuwa sisi ni wapenzi .Nadhani hii ni mojawapo ya sababu inayopelekea watu kuwa na chuki zaidi kwetu kwani Happy ni binti mrembo kupita maelezo.Na kadiri siku zinavyozidi kusonga anazidi kupendeza na kuwa kama malaika.Sasa kama wao hawaupendi ukaribu huu wangu na Happy basi wameumia .Tutaendelea kuwa karibu zaidi ya hapa.Lakini kuna dalili zozote za mapenzi kati yetu?.Hapana. Nadhani tunapenda kama marafiki wa kawaida .Sijui ya huko mbele kwa sababu naona urafiki wetu umekuwa mkubwa sana na unazidi kukomaa kadiri siku zinavyosonga mbele.”. Kwa upande wake Happy baada ya kutoka darasani mchana ule akaenda mpaka katika hosteli yao akajitupa kitandani na kuanza kutafakari.juu ya tukio zima la leo. “sikuwahi hata siku moja kuwaza kuwa nitakuja kugombana na mtu .Nimevumilia mambo mengi lakini hii ya leo ilivuka mipaka..Kwa nini wananichukia namna hii?Mbona mimi sina tabia ya maringo kama wanavyodai?Mbona sijivuni japokuwa wazazi wangu wana uwezo?Nafikiri ni kwa sababu wengi hawaupendi ukaribu wangu na Patrick.Wasichana wenzangu wana chuki hawapendi sana jambo hili.Nadhani hii ni sababu kubwa ya kuwa na visa vya wazi wazi.Kumbe tayari wamepeleka maneno hadi kwa walimu kuwa mimi na Patrick ni wapenzi.Mhh jamani!!.Maskini Patrick anaonewa bure kaka wa watu.Wangejua jinsi alivyo wala wasingezusha tuhuma hizo.Lakini hata kama ingekuwa ni kweli kwani wao inawahusu nini?Wivu wao unawasumbua tu..Nasema Patrick simuachi na nitazidi kuwa rafiki yake wa karibu.Patrick ni mtu pekee ambaye amenifikisha hapa nilipo sasa.Nilikwisha kata tamaa kabisa hata ya kuendelea kusoma hapa lakini ni yeye aliyenipa moyo na kunisaidia katika kila kitu .Amenipa msaada mkubwa kimasomo.Ni yeye tu ambaye amekuwa nami siku zote pale ambapo jamii nzima imenikataa.Potelea mbali watakavyosema na waseme.Mimi sijali .Mbona wao wana wanaume kila kona mimi siwafuatiliii mambo yao .Kwa nini basi wao wafuatilie ya kwangu.?.Lakini hata kama ingekuwa ni kweli ,kuna ubaya wowote mimi na Patrick kuwa wapenzi?Nadhani hata kama nikiamua kuwa na mpenzi basi ni wazi ni lazima atakuwa ni Patrick .Kwani ni yeye pekee mpaka sasa hivi ambaye amekuwa ni mtu wangu wa muhimu sana.Ni yeye pekee ambaye anaweza kunikosesha usingizi kwa kutomuona.Je ni kweli kuwa hii ni dalili ya kuchipua kwa penzi kati yetu? Inaweza kuwa kweli kwa sababu sijawahi kuwa karibu na mvulana yeyote zaidi ya Patrick.Ni yeye ambaye amenifundisha nini maana ya kuwa rafiki wa dhati.nadhani hizi ni dalli njema.lakini hata kama nikiamua kumchagua Patrick kuwa mpenzi wangu nitamwambiaje?Mhh ! ngoja niachane na haya mambo huu si wakati wake." akawaza happy.

* * * *
Kengele ya dharura ikagongwa ikiashiria kuwa na jambo ambalo si la kawaida.Wanafunzi wote wakatoka darasani kwa haraka kama inavyotakiwa mara tu inaposikika kengele hii.Kwa haraka haraka mistari ikapangwa na huku kila mwanafunzi akiwa kimya akisubiri kusikia ni nini kitakachojiri.Walimu wote walikuwa wamejipanga na mara akatokea mkuu wa shule.Wanafunzi mioyo ikawaenda mbio kwani ni nadra sana kwa mkuu wa shule kuonekana katika eneo hilo la mkusanyiko.Mara zote anapoonekana eneo hilo huwa ni kwa sababu maalum tu. “Habari za asubuhi wanafunzi” Akasalimu wanafunzi. “Nzuri shikamoo mwalimu” “Wanafunzi nimesimama mbele yenu asubuhi hii ili kuzungumzia mustakabali mzima wa maendeleo ya shule yetu.kwa siku za karibuni shule yetu imekuwa na mambo ambayo katu hayafurahishi na ambayo yanaenda kinyume na maadili mazima ya mwanafunzi. Kwanza kabisa kumekuwa na vitendo vya ubaguzi.Wanafunzi mmeanza kubaguana.Mnawanyanyasa na kuwabagua wenzenu ambao ni wagonjwa.Hivi ndivyo mnavyofundishwa na wazazi wenu majumbani? Kuna binti mmoja nimepata malalamiko yake kuwa yeye ametengwa na wanafunzi wenzake eti kisa ni mgonjwa.Hii ni aibu kubwa kwa shule yetu..Sasa ninasema hivi kuanzia sasa wewe ukibainika kuwa unafanya kitendo chochote cha kibaguzi adhabu yake ni kufukuzwa shule.Sintataka kukuona tena katika shule yangu.Kuweni makini sana na hilo.Jambo la pili ninalotaka kulizungumza leo ni nidhamu .Kumekuwa na uvunjaji mkubwa sana wa sheria za shule.Imefikia mahali sasa ambapo mwanafunzi anaweza akamgomea hata mwalimu .Mwanafunzi anaweza akafanya kitu chochote anachotaka bila kuogopa.Hivi kweli wewe mwanafunzi unaweza ukabishana na kutaka kupigana na malimu wako?mwalimu wako ni sawa na mzazi wako hapa shuleni.Nasema kuwa kuanzia sasa sheria na taratibu za shule zitafuatwa kwa ukaribu sana.Endapo utakwenda nje ya taratibu basi tutakushughulikia kikamilifu.Kwa sasa naomba nitakaowataja wapiti mbele haraka: Patrick Charles,Happy kibaho.Mwantumu ramadhani.Pius augustinie,Pili Juma,Maria asey,Steven amanuli na Benson Chiteu.”
Wanafunzi wale walioitwa ,wakajipanga mbele ya alipokuwa amesimama mkuu wa shule,halafu akaendelea. “Hawa mnaowaona mbele yenu mnajua wamefanya nini? Akauliza mkuu wa shule.wanafunzi wote wakawa kimya .Hakuna mtu aliyethubutu kusema kitu ingaa walkuwa wakifahamu juu ya ugomvi uliotokea. “Wanafunzi hawa walioko mbele yenu walivunja sheria za shule kwa kugombana darasani.Baada ya kukutwa wkipigana mwalimu aliyewakamata akawapeleka kwa mwalimu wa darasa Patrick na mwenzake Happy ambao ndio kiini cha ugomvi wakagoma kuadhibiwa.Kibaya zaidi ni kwamba Patrick alikuwa tayari kupigana hata na mwalimu wake wa darasa.Sijui jeuri hii mnaitoa wapi ninyi watoto..Mwanafunzi unataka kupigana na mwalimu wako kweli? Hii tabia mbaya ambayo katu haitavumiliwa katika shule yetu.Kingine ni kwamba Patrick na Happy ambao wote ni wanafunzi wa darasa moja wamekuwa wakijihusisha na masuala ya kimapenzi wakiwa shuleni kitu ambacho ni kinyume kabisa na sheria na taratibu za shule.Bodi ya shule imekaa na imeamua yafuatayo.Moja wanafunzi Mwantumu Ramadhani,Pius Augustine,Pili Juma,Maria asey ,steve amanuli,na Benson chiteu watapata adhabu ya kung’oa kila mmoja visiki vitatu kwa muda wa siku sita kuanzia leo.Wanapata adhabu hii kwa kosa la kupigana darasani.Hili ni fundisho kwa wengine .Wanafunzi Patrick charles na Happy Kibaho wao wanasimamishwa masomo kwa muda wa mwezi mmoja.Hii ni kwa sababu wamesababisha ugomvi ,wamapigana darsani,wakagomea adhabu ya mwalimu na zaidi ya yote wanajihusisha na mahusiano ya kimapenzi wakiwa shuleni.Adhabu hii ni fundisho kwa wanafunzi wengine.Ninasema kuwa kuanzia sasa tutakuwa wakali mno kwa yeyote yule ambaye atajaribu kwa namna yoyote kuvunja sheria za shule.Nasema ole wenu ,ole wenu.” Mkuu wa shule akamaliza na kuondoka zake.mwalimu wa zamu akawatawanyisha wanafunzi warudi madarasani.Sehemu kubwa ya wanafunzi walkikuwa wakifurahia adhabu ile waliyoipata Patrick na Happy .Kwao uilikuwa ni alama ya ushindi mkubwa.Katika darasa la akina Patrick ilikuwa ni kama sherehe.Wanafuzi walikuwa wakipongezana.
Happy macho yalijaa machozi.Alikuwa akilia.Hakuamini kuwa kosa lille lingepelekea yeye na Patrick wasimamishwe masomo.Hakuwahi kuota kama iko siku atakuja kusimamishwa masomo.Mbaya zaidi aliumia moyo kwa uongo wa wazi kabisa .Ni wazi ulikuwa ni ukandamizaji mkubwa.Zilikuwa ni chuki za wazi .Patrick alikuwa katika hali ya mstuko kutokana na adhabu ile ambayo kwa kiasi kikubwa haikuwa ya haki.Ulikuwa ni uonevu mkubwa.Walikuwa wamesingiziwa uongo mkubwa .Ilimuuma Patrick kwa kiasi kikubwa lakini hakuwa na la kufanya .tayari maamuzi yamekwisha fanywa na kilichobakia ni utekelezaji.Kwa muda huu mfupi shule hii ilikuwa imeanza kumchosha.Taratibu akamsogelea Happy na kumshika mkono.Akatoa kitambaa mfukoni na kumfuta machozi . “Happy be strong.Najua inauma sana lakini hatuna jinsi.Tusiwape faida maadui zetu.Wanapotuona tuko na huzuni ni furaha kwao.Let us act kama vile hakuna chochote kilichotokea.

* * * *
“Patrick ninasikia uchungu sana ..Kusingiziwa kitu ambacho sijakifanya inauma mno .Inaniuma sana Patrick”Happy akashindwa kuvumilia akaanza kulia .Ilikuwa ni majira ya saa kumi na moja za jioni walipokutana katika hoteli moja kijijini baada ya kuachana mchana na kila mmoja akaenda kupumzika na kutuliza akili.Happy macho yalikuwa yamemvimba na mekundu kwa kulia.. “Kinachoniuma zaidi ni wewe kusimamishwa masomo.wewe hukustahili kwa namna yoyote ile kuipata adhabu hii.Mimi ndio chanzo cha haya yote.Mimi ndiye niliyekusababishia matatizo haya .Ni bora ningesimamishwa masomo peke yangu.Nasikitika sana Patrick .Naomba unisamehe kwa hilo.Haikuwa adhma yangu na wewe uingie katika matatizo haya .Najua hustahili adhabu hii………………….” Akasema Happy huku machozi yakimtoka lakiniPatrick akamzuia na kusema “Shhhhhhhhhhhhhhhhhhhh………….”Patrick akamfumba Happy mdomo kwa kidole. “Happy usiseme hivyo.Ninafurahi kupata adhabu hii .Ninastahili.Ulikuwa ni wajibu wangu mimi kukutetea.Nimetimiza wajibu wangu.Kumbuka niliahidi kuwa nawe katika kila jambo.Niliahidi kupambana na yeyote yule ambaye angekufanya ulie.Nimefanya nilivyopaswa kufanya..Usijilaumu Happy ninastahili adhabu hii .”Parick akasema kwa kujiamini.Akamuangalia happy kwa makini na kusema “Happy si hapa duniani tu hata nikiwa Mbinguni sintavumilia kuona mtu yeyote akikusumbua.Nitapambana naye.”Kwa mara ya kwanza Happy akacheka kwa kauli ile ya Patrick..Patrick akatabasamu kwa kuifanya sura ya Happy ikajaa tabasamu tena.
“ Umeanza vituko vyako.Mbinguni hakuna uonevu wa namna hii” akasema Happy huku akicheka
“nimesema hivyo kukuthibitishia kwamba sintakuwa tayari kuona mtu yeyote yule akikunyanyasa Happy..” akasema patrick na kumfanya Happy atabasamu tena
“Happy hii ni vita na sisi ni wapiganaji. kuna msemo wa kiingereza unaosema winners never quit.Na sisi ndio washindi hivyo tusikate tamaa.Kukata tamaa ni kuwapa ushindi wale wote wasiotupenda,wasiotutakia mema.Wao wanapamba na sisi lakini sisi tupambane na muda.tumeelewana?” “sawa Patrick nimekuelwa.nashukuru sana Patrick sijui hata nipate neno gani la kukushukuru kwa jinsi ulvyojitoa mhanga juu yangu.Sidhani kama kuna mwanaume ambaye anaweza kufanya haya uliyoyafanya kwangu.Kama wapo basi ni wachache mno.”Patrick akatabasamu na kusema... “Happy utaanzaje kuwaeleza wazazi wako juu ya tukio hili mpaka wakakuelewa.? Manake kwa mujibu wa barua zilivyoandikwa za kuwapelekea wazazi mhh ni hatari tupu.”Happy akakaa kimya kwa muda kisha akasema. “Patrick hilo suala linaniumiza kichwa kupita kiasi..unajua baba yangu ananiamini sana na hajawahi kusikia sifa yangu mbaya hata siku moja .Siku zote nimekuwa mfano hata kwa wenzangu , leo akisikia nimesimamishwa masomo mhhh !! sidhani kama kutakuwa na amani nyumbani.Kuna hatari akakataa hata kunipokea kwa jinsi baba yangu alivyo mkali.Nilikuwa nafikiria niende kujificha kwa shangazi yangu Morogoro mpaka adhabu itakapokwisha.Shangazi yangu ni mwelewa na nina imani nikimwelezea atanielewa.Sitaki baba yangu afahamu kuhusu suala hili.Akijua tu nimekwisha.Wewe je umepanga nini? Patrick akafikiri kidogo na kusema “mimi sina tofauti na wewe hata kidogo.Mzee wangu hatavumilia akisikia nimesimamishwa masomo.Hata mimi nilikuwa ninafikiria niende mahala nikatulie mpaka adhabu hii itakapoisha.Mwezi mmoja si mrefu.” Kimya kikapita Patrick ambaye alikuwa ameinama akiwaza akainua kichwa na kusema. “Happy kuna jambo nimelifikiria.Kwa kuwa sisi sote tuna wazo moja la kutotaka kuzifahamisha familia zetu juu ya adhabu hii tuliyopata ,kwani hata kama ukienda kwa shangazi yako anaweza akamweleza tu mzee wako na hapo ndipo itakuwa mbaya zaidi. kama ni hivyo kwa nini basi tusitafute mahala tukaenda kukaa kwa muda wa huo mwezi mzima mahala ambako hakuna mtu anayetujua,na tutakaa kwa raha mstarehe huku tukipata nafasi ya kutosha ya kusoma hadi muda wa adhabu utakapoisha? Happy akatabasamu lile tabasamu lake adimu sana. “That’s a good idea Patrick.Wewe una akili sana.Ni wazo zuri Patrick .Sasa ni wapi ambako unafikiri tunaweza kwenda kukaa kwa muda huu wote bila ya kufahamika? Akauliza Happy na Patrick akakaa kimya kidogo akafikiri kisha akasema “Umewahi kwenda Bagamoyo?”Patrick akauliza. “hapana sijafika huko” “Basi ninafikiria twende huko.Kule tutapumzika vya kutosha.Hakuna mtu yeyote anayetufahamu.Tutakaa kwa raha mustarehe.Tutapata nafasi nzuri ya kujisomea.Tutatembelea sehemu mbali mbali za kihistoria.Tutajifunza mambo mengi sana tukiwa kule.Usijali kuhusu gharama bado nina akiba ya kutosha ya pesa na wala hatutapata shida kwa muda kwa huo wote wa mwezi mmoja.Nafikiri hii itatusaidia sana kutoka nje ya ulimwengu huu wa watu wasiokuwa na upendo hata chembe”Furaha ya wazi ikajidhihirisha usoni mwa Happy .Hakuwa amewaza jambo kama lile hapo kabla.Huzuni yote aliyokuwa nayo ikayeyuka ghafla. “ Patrick nashindwa hata nisemeje.You are my Hero.Toka nimefahamiana na wewe maisha yangu ytamekuwa na furaha sana.Najihisi niko slama muda wote ukiwa pembeni yangu.Nafurahi kwa kuwa najua niko na rafiki anayeyenijali na kunithamini.Sina kitu cha kukulipa Patrick kwa wema wako huu ”akasema Happy.Patrick akatabasamu.
“ Sifanyi hivi kwa kuhitaji malipo Happy.Ninafanya hivi kwa sababu moyo wangu umenituma” akasema Patrick.Walijhadiliana mambo mengi hadi ilipotimu saa moja za jioni wakaondoka kwa ajili ya kwenda kujiandaa na safari ya kesho yake ya kuelekea Bagamoyo.

* * * *
Ulikuwa ni usiku mrefu sana ambao Happy hakuwahi kuupata hapo kabla.Alitamani asubuhi ifike haraka ili aweze kuondoka hapa shuleni.Tayari alikwisha maliza kufunga baadhi ya vitu vyake muhimu ambavyo angevihitaji katika safari yake ya kuelekea Bagamoyo.Vingine vilivyobaki akavikabidhi kwa mkuu wa hosteli.Wanafunzi wenzake walikuwa wakimshangaa sana kwa hali aliyokuwa nayo.Badala ya kuwa na huzuni kwa kusimamishwa masomo yeye alikuwa na tabasamu muda wote.“Me and Patrick together in bagamoyo” Neno hili lilijirudia rudia kichwani mwake mara nyingi.
“Nashukuru nimepata nafasi ya kuwa na Patrick peke yangu kwa mwezi mzima..Walau nitajitenga na karaha za shule hii kwa muda.Nafikiri baada ya kurudi nitakuwa na mabadiliko makubwa.Safari hii ya Bagamoyo nina imani itanisaidia sana kisaikolojia.Nitakuwa mtu mpya tena.”Aliwaza.
kwa upande wake Patrick alikuwa akifikiria jinsi atakavyomaliza mwezi mzima akiwa na Happy . “Ni vipi ikija kugundulika kuwa kwa mwezi mzima tulikuwa tumejificha Bagamoyo?Hii itadhihirisha wazi kuwa kuna kitu kinaendelea baina yetu.Lakini potelea mbali hata kama ikigundulika siogopi tena .na hata kama tukiwa wapenzi hakuna mtu anayehusika katika kuamua masuala ya maisha yetu .”Akawaza Patrick.








* * * *


Kengele ya mlangoni ikalia na kumwamsha Patrick toka katika usingizi mzito.Taratibu akainuka na kwenda kuufungua mlango.Alikuwa ni Happy akiwa ndani ya tabasamu pana.Ni siku yao ya kwanza katika mji wa Bagamoyo.Walifika jioni ya siku iilyotangulia na kupanga vyumba viwili katika nyumba ya kulala wageni yenye hadhi ya kawaida lakini yenye ulinzi wa kutosha na huduma nzuri.“Mhh ! Patrick amka basi uoge tunywe chai .Nimeenda kununua chai katika mgahawa wa mama mmoja hapo jirani.Kwa kuwa tutakuwepo hapa Bagamoyo kwa muda mrefu amenipa chupa ya chai na baadhi ya vyombo ambavyo tutakuwa tukitumia katika muda wote tutakaokuwepo hapa ”akasema Happy .“ Happy kumbe umeshaamka !Ahsante kwa kuniamsha nilikuwa nimeshajisahau kabisa.” Patrick akasema huku akijiinuataratibu pale kitandani.“Nimekwisha amka kitambo Patrick..Jiandae ninakusubiri tunywe chai ” akasema Happy.Patrick akaelekea bafuni akaoga na kisha wakapata kifungua kinywa.
Baada ya kupata chai wakatoka na kuanza kuzunguka katika mji wa kihistoria wakifurahia mandhari yake .Walizunguka sana na mchana wakaenda kupata chakula katika mgahawa uliomilikiwa na mama mmoja wa makamo.Walimuomba mama yule awe akiwatengenezea chakula kwa muda wote watakaokuwa pale Bagamoyo.Mama yule akakubali kuwahudumia bila matatizo.Kisha pata chakula wakarudi hotelini kupumzika hadi saa kumi jioni halafu wakaanza kusoma.
“Happy tunatakiwa tuutumie muda wetu mwingi hapa Bagamoyo kwa ajili ya kusoma ili kuwa sawa na wenzetu waliobaki shuleni .Tutakaporudi shuleni tutakuwa tunakaribia kipindi cha mitihani na lengo langu mimi ni sisi kufanya vizuri zaidi ili wale wote ambao wanatuonea wivu waone aibu.”
“Usijali Patrick nina imani tutasoma na tutafanya vizuri.”akajibu Happy .Saa mbili usiku wakaenda kupata chakula cha usiku kisha wakarejea tena kusoma hadi saa tano za usiku halafu kila mmoja akaenda kulala.Hii ilikuwa ndiyo ratiba yao kubwa kila siku.Jumamosi na jumapili walizitumia kutembelea sehemu mbali mbali za kihistoria hapo Bagamoyo.
Ilikuwa ni jumamosi angavu .Kijua kilikuwa kikali .Ni siku ya ishirini tangu wamewasili Bagamoyo. Saa sita mchana iliwakuta Patrick na Happy katika sehemu moja maarufu sana hapa Bagamoyo.Ni Patrick ndiye aliyeweka msisitizo mkubwa kuwa ni lazima wafike mahali hapa kabla hawajarudi shuleni.Hapa ni sehemu inayojulikana kama kaburi la wapendanao.Sehemu hii ni sehemu maarufu sana na watu wengi hupenda kwenda mahali hapa wakiwa na wapenzi wao na kuwekeana ahadi mbali mbali mbali katika safari nzima ya mapenzi hasa kutokana na historia ya watu hao waliozikwa hapo.
“Happy hii sehemu ndiyo inaitwa kaburi la wapendanao.Waliozikwa hapa inasemekana ni watu waliokuwa wamependana kwa dhati .”Happy akatabasamu ,na huku akiogopa ogopa.Patrick akamsogelea Happy akamsika mikono yote miwili kisha akamwangalia machoni
“Happy toka tumekuja Bagamoyo tumetembelea sehemu mbali mbali za kihistoria.Tumejifunza mambo mengi.Hii nilitaka iwe ni sehemu ya mwisho kwa sisi kutembelea tukiwa hapa Bagamoyo.” Akanyamaza kidogo kisha akaendelea“Nina sababu kubwa ya kuamua kuja eneo hili.Happy waliolala hapa chini ni watu ambao inasemekana upendo wao ulikuwa wa kweli.Hii ndio sababu kubwa ambayo watu wengi na hasa wapenzi hupenda kuja mahali hapa na kuwekeana ahadi mbali mbali katika safari yao nzima ya kimapenzi.Nadhani utajiuliza kwamba na sisi je nini kilichotuleta hapa? Happy nimeamua kukuleta hapa leo hii ili niweze kudhihirisha jinsi gani ninavyokupenda.Nakupenda sana Happy .Toka tulipokutana na kuwa marafiki niliona ishara na kuamini kuwa wewe ndiwe pekee uliyeumbwa kwa ajili yangu.Tafadhali Happy naomba unikubalie ombi langu .Naomba uwe mpenzi wangu.Nakuahidi mbele ya watu waliolala hapa chini kwamba siku zote nitakupenda ,nitakujali na kukuthamini hadi kifo kitakapotutenganisha.Hata siku moja sintakutoa machozi” akasema Patrick akimtazama Happy usoni huku ameishika mikono yake
Taratibu Happy akaiachia mikono ya Patrick,akiwa kama vile mtu aliyepigwa na bumbuwazi.Akamtumbulia macho Patrick kana kwamba ni kwa mara ya kwanza kumuona.Moyo ukamwenda mbio kijasho kikamtiririka.Akafumbua mdomo kutaka kusema kitu lakini akajikuta anashindwa.Patrick ambaye leo hii alikuwa na ujasiri wa aina yake akamsogelea ,akamshika mkono.,akamwangalia usoni.“Happy I’m sorry.Sikutegemea kama ningekuudhi.naomba vile vile ufahamu kuwa sina lengo baya na wewe,sina lengo la kukuharibia masomo au maisha yako.Naheshimu ndoto zako ,naheshimu maisha yako na ninakuheshimu wewe pia.Natambua kuwa una ndoto zako nyingi siku za usoni na hata mimi nina ndoto zangu pia na ambazo ni lazima nizitimize na moja kati ya ndoto zangu kubwa ni kuwa na wewe.You are my dream Happy .Lakini naona kama vile nimekukwaza na kauli yangu hivyo naomba usahau.Just pretend I didn’t say anything.Naomba kauli yangu hii ya leo isije ikavuruga urafiki wetu .I’m sorry.Happy” Patrick akasema . Happy machozi yalikuwa yakimtoka.Mashavu yake yote yalikuwa yamelowa machozi.Alitamani kusema neno lakini midomo ilikuwa ikicheza cheza na kushindwa kuongea.Akajikaza na kusema “Patrick ! siyo hivyo unavyofikiri.Patrick huwezi jua jinsi gani ulivyoustua moyo wangu.Sikutegemea kama ungeweza kunitamkia maneno haya leo… “Shhhhhhhhhhhhhh!!!!!!!!!!!.I’m sorry Happy .Nilishindwa kuvumilia .Nimeshindwa kupigana na hisia zangu kwako .Sahamani sana” Patrick akasema “No Patrick usinifikirie vibaya.Simaanishi hivyo unavyofikiria wewe.Ni kwamba sikuwa nimetegemea kama utakuja kuniambia kitu kama hiki leo.Naomba niwe wazi kuwa nimekuwa nikiumia sana moyoni kwa muda mrefu nikisubiri siku kama hii ya leo ambayo ungeniambia maneno haya.I love you Patrick.I love you so much.Th…….”Akashindwa kuendelea akaanza kulia kwa kwikwi.Patrick akatoa kitambaa na kumfuta machozi .Happy akamtazama Patrick usoni kwa sekunde kadhaa kisha wakakumbatiana kwa nguvu.. “Thank you so much Happy kwa kunipenda.I promise you that I’will never hurt you.Nakuahidi hapa mbele ya kaburi la wapendanao kuwa sintakubali kitu chochote kitutenganishe .Naomba kifo tu ndicho kiwe kitu pekee cha kuweka kutufanya tutengane.Naomba hata kama tukitenganishwa na kifo basi kama kuna uwezekano tufe sote na kuzikwa pamoja kama watu hawa hapa chini.” Patrick alitamka maneno haya kwa umakini mkubwa na ni wazi yalitoka ndani kabisa mwa moyo wake.Happy macho yalikuwa yamemjaa machozi wakati akisikiliza maneno ya Patrick. “Patrick hata mimi nashukuru sana kama hisia zako kwangu ni za kweli .Ninaichukua ahadi yako kama ilivyo na kuihifadhi moyoni mwangu.Na mimi kama ulivyofanya wewe nakuahidi kuwa sintakuwa radhi kutengana nawe.Naahidi kuwa hakuna chochote kitakachoweza kututenganisha zaidi ya kifo..Ila naomba hapa tuwekeane ahadi kuwa pamoja na kwamba tumekubaliana kuwa wapenzi lakini hatutafanya mapenzi mpaka hapo tutakapokuwa tumemaliza masomo yetu.Niahidi hivyo Patrick”akasema HappyPatrick akamwangalia Happy kwa tabasamu kubwa kisha akasema.“Nalifahamu hilo Happy .Ndio maana nikasema kuwa nitakuheshimu na kuziheshimu ndoto zako.Nafahamu hatari za mapenzi shuleni hivyo niko makini sana na suala hilo.Usitie shaka natumai tutakuwa na muda mzuri baada ya kumaliza masomo yetu.”Happy akatabasamu na kumkumbatia Patrick.Walibaki wamekumbatiana kwa takribani dakika kama tano hivi huu ulikuwa ni mwanzo wa ukurasa wao mpya
 
5




Siku mbili kabla ya adhabu yao kumalizika Patrick na Happy wakarejea shuleni.Mara tu baada ya kuwasili kwao shuleni tayari maneno ya chini chini na vijembe vikaanza.Muda huu walioutumia wakiwa Bagamoyo uliwajenga na kuwafanya wawe majasiri hivyo hali hii haikuwatia hofu.Uhusiano wao ukaendelea kama kawaida na safari hii wakawa karibu zaidi.Muda mwingi waliutumia kusoma pamoja hivyo kuwafanya wanafunzi wenzao kuongeza udadisi zaidi. Ilikuwa ni wiki ya tatu siku ya jumamosi tangu Patrick na Happy warejee toka katika adhabu.Siku hii kulikuwa na tamasha la michezo lililojumuisha shule ya Malangali na shule ya sekondari Ifunda.Lilikuwa ni tamasha kubwa na lililopendeza sana.Uongozi wa shule uliamua kufanya tamasha hili ili kuwaburudisha wanafunzi kabla ya kipindi cha mitihani ya kumaliza muhula wa pili kuanza. Tamasha lilianza saa nne asubuhi kwa michezo mbali mbali kama vile kukimbia ,kucheza ngoma ,sarakasi nk.Kisha maliza awamu ya kwanza ,wanafunzi wakaenda kupata chakula cha mchana kabla ya kuanza kwa awamu ya pili mchana huo.Saa nane mchana ikaanza awamu ya pili.wanafunzi wote wakakusanyika katika viwanja vya michezo.Michezo iliyokuwa ikifanyika mchana huu ni mpira wa kikapu,wavu,pete na mwisho kabisa mpira wa miguu. Karibu katika kila mchezo shule ya sekondari Ifunda ikachukua ushindi.Na sasa ushindani ukahamia katika mpira wa miguu.Wanafunzi wote wakahamia katika uwanja wa mpira wa miguu. Patrick na Happy walikuwa wakishuka taratibu sana wakielekea katika uwanja wa mpira ili kushuhudia mtanange huo wa kukata na shoka.Hawakuwa wamehudhuria mchezo wowote toka tamasha lilipoanza.Walikuwa wamejificha mahala akijisomea.Wote wawili hawakuwa wapenzi sana wa michezo. Kiujumla walikuwa wamependeza mno siku hii ya leo na kila aliyepisha nao hakukosa kugeuka kuwatazama.Hawakujali macho ya watu ,wakafika uwanjani na kutafuta sehemu moja iliyokuwa na msingi wa nyumba wakakaa.Waliamua kujitenga kabisa na wenzao.Mpira ukaanza kwa kasi sana.Dakika ya kumi na moja ya mchezo Ifunda wakapata bao la kuongoza.Mpira ukaendelea na dakika ya arobaini wakapata tena bao la pili.Mpaka mapumziko Ifunda walikuwa wakiongoza kwa mabao mawili.Ilikuwa ni simanzi kubwa kwa upande wa malangali kupoteza kila mchezo.Kipindi cha pili kikaanza kwa kasi.Dakika ya tisa ya kipindi cha pili Malangali wakapata bao lakini refa akakataa kwa madai kuwa mfungaji wa bao lile likuwaameotea.Wanafunzi wa Malangali wakavamia uwanja na ikazuka vurugu kubwa.Wachezaji wa Ifunda wakatoka uwanjani na kuanza kukimbia wakijaribu kujiokoa na ile vurugu.Mawe,fimbo ,chupa vikawa vikirushwa uwanjani.“Happy tuondoke mahali hapa si salama tena”Akasema Patrick huku akimshika mkono Happy lakini kabla Happy hajamaliza kuvaa viatu vyake vya kuchomeka alivyokuwa ameviweka kando ya miguu yake jiwe kubwa lililorushwa upande wao likampiga kichwani akaanguka chini huku damu nyingi ikimmwagika.“Nooo..!!!!!!!.........” Patrick akapiga ukelele mkubwa baada ya kumuona Happy akiwa amelala chini huku damu nyingi ikimvuja kichwani.Akamwinamia Happy kwa haraka huku machozi yaliyoambatana na hasira yakimtoka.Mwalimu Vicent ambaye alikuwa karibu na mahali pale aliliona tukio lile naye akakimbia haraka kuja kuangalia hali ya Happy .alistuka kwa hali aliyoikuta.haraka haraka akakimbia na kwenda kumwita dereva wa shule akaja na gari na kwa haraka wakampakia Happy wakamwahisha katika kituo cha afya cha karibu.Patrick hakuongea kitu machozi yalikuwa yakimchuruzika. Kituo cha afya Malangali hakikuwa mbali sana na shule.Kwa bahati mbaya wakati walipofika pale hakukuwa na daktari.Alikuwepo muuguzi mmoja tu.Kwa dakika kama mbili hivi hawakujua wafanye nini kwani hata muuguzi yule alionekana kuwa na hofu kutokana na hali aliyokuwa nayo Happy.
“I have to do something” Patrick akawaza.ghafla akatoka mbio kuelekea kijijini.Hakuna mtu yeyote aliyejua Patrick anakwenda wapi.Dakika kama kumi baadaye gari moja aina ya Toyota pick up ikaja kwa kasi kubwa maeneo hayo ya hospitali huku ikiwa imewasha taa.Watu waliokuwepo hapo nje wakaanza kuingiwa na wasi wasi labda kuna maafa mengine yametokea.Gari ikafunga breki kali na mara bila kutegemea Patrick akashuka. Mpaka muda huo bado Happy alikuwa ndani ya gari akiwa hana fahamu huku mwalimu na yule muuguzi wakizuai damu kuendela kuvuja huku wakijadiliana jinsi ya kumpata daktari ambaye kwa wakati huo hawakujua alikuwa wapi. “Haraka haraka,nisaidieni kumbeba.”Akasema Patrick akiwaambia watu wawili aliokuja nao katika ile gari.Huku mwalimu na muuguzi wakishangaa Happy akashushwa toka katika gari ya shule na kupakiwa katika ile gari ndogo aliyokuja nayo Patrick. “Patrick unafanya nini??.................Alipaaza sauti mwalimu akiwa haelewi nini Patrick alikusudia kufanya. “Dereva ondoa gari achana na huyo mwalimu”Patrick alisema huku akifunga mlango .gari ikaondolewa kwa kasi ya ajabu kila mtu akibaki ameduwaa.


* * * *

“ahsanteni sana ndugu zanguni nashukuru mmenisaidia”Patrick akawaambia dereva na yule msaidizi wake baada ya kufika katika hospitali ya Makambako na Happy kuanza kupatiwa matibabu.“Usjali dogo siku yoyote ukiwa na tatizo unasema.sisi sote binadamu lazima tusaidiane.”akasema dereva. Baada ya kuwalipa pesa zao wakaondoka kurudi malangali na kumwacha Patrick hapo hospitali.Giza tayari lilikwisha ingia.Happy alikuwa katika chumba cha upasuaji akishonwa jeraha lake la kichwa.Lilikuwa ni jereha kubwa lililompelekea apoteze damu nyingi .Bado alikuwa hajarejewa na fahamu.Patrick bado alikuwa nje ya chumba hicho akisubiri kujua hali ya Happy itakuwaje .Moyoni bado alikuwa na fundo kubwa lililomkaa juu ya kilichokuwa kimetokea.Alianza kuvuta picha ya jinsi tukio lile lilivyotokea .Alikumbuka wakati vurugu imeanza na mawe kuanza kurushwa.hadi jiwe lile kumpata Happy kichwani, ni wazi tukio lile lilikuwa limedhamiriwa.
“Naanza kupata picha kuwa mrushaji wa jiwe lile alikuwa amedhamiria kabisa kumjeruhi Happy au mimi.”akawaza Patrick.akiwa katika lindi la mawazo mara mlango wa chumba cha upasuaji ukafunguliwa na machela ikatoka. “Kijana hali ya mwenzio inaendelea vizuri .Tumeshona jeraha lake na sasa tunampeleka wodini .Tutamuongezea damu kwa sababu amepoteza damu nyingi sana.wewe unaweza kwenda kupumzika .Uje asubuhi”Alisema daktari mama wa makamo ambaye alionekana kuwa na roho ya huruma. “Ahsante daktari kwa kazi kubwa mliyoifanya.Lakini nitabaki hapa hapa mpaka asubuhi kwa sababu tayari imeshakuwa usiku na mimi hapa Makambako ni mgeni”
“Nyie mmetokea wapi” Akauliza yule daktari
“sisi ni wanafunzi wa shule ya sekondari malangali” patrick akajibu.Baada ya mahojoano mafupi na yule mama akamwangalia Patrick kwa sekunde kadhaa kisha akasema.
“Umefanya kitendo cha kijasiri sana ..kama ungeendelea kukaa pale shuleni hali ya mwenzio ingekuwa mbaya zaidi na hata kupoteza maisha.Nitamwambia dereva wetu akupeleke nyumbani kwangu ukapumzike hadi kesho.Umeonyesha moyo wa ujasiri sana wa kumsaidia mwenzako..Nisubiri hapo hapo” Alisema yule mama na kuingia ndani. Patrick aliendelea kumwomba Mungu kimoyo moyo hali ya Happy iwe nzuri. “Twende” akasema yule daktari wakaondoka na kisha Patrick akapanda gari la hospitalina kupelekwa nyumbani kwa yule daktari
.


* * * *



Saa kumi na mbili asubihi ilimkuta Patrick tayari amekwisha fika hospitali.Hakuweza kupata usingizi usiku huo licha ya kuhakikishiwa kuwa hali ya Happy ilikuwa nzuri.Moyo ulikuwa ukimwenda mbio.Aliingia katika wodi aliyolazwa Happy kwa wasi wasi mwingi.Lakini ghafla akakutana na sura angavu yenye matumaini ya Happy .tayari alikwisha pata fahamu toka usiku.Patrick akafumba mdomo kwa kiganja cha mkono wake akionyesha mshangao.kwa haraka akakimbia na kumkumbatia Happy pale kitandani. ”Pole sana Happy ” ‘ahsante Patrick.nashukuru sana kwa msaada wako” “Usijali Happy ulikuwa ni wajibu wangu kufanya hivyo”akajibu Patrick. “ nilikuwa na wasi wasi mwingi wakati fahamu zimenirudia nikiwaza nilifikaje fikaje hapa..Muuguzi mmoja aliyekuwapo zamu ya usiku akaniambia kuwa kuna rafiki yangu mmoja anaitwa Patrick pamoja na watu wengine wawili ndio waliokuleta hapa.Nilifurahi sana kusikia hivyo.nashukuru sana Patrick.Kwa sasa naamini kuwa upendo wako kwangu ni wa kweli.”Patrick hakujibu kitu akatabasamu. “sasa Patrick nina imani nitazidi kuwepo hapa hospitali kwa siku kadhaa hivyo nitakupa namba hizi za simu umpigie mama yangu na umweleze mkasa mzima jinsi ulivyokuwa ili aje anihudumie kwa kipindi hiki chote nitakachokuwa hapa hospitali. Kwa sababu wewe unatakiwa kwa sasa uanze kujiandaa na mitihani ambayo haiko mbali sana.” Patrick akakubaliana na ushauri ule na kuzichukua zile namba. “ Happy ungependa kula ni ni asubuhi hii”Patrick akauliza “Mimi nimeshashiba kwa kukuona wewe tu.Patrick wewe ni chakula tosha kabisa.Usisumbuke Patrick sintakula kitu .Jitahidi ukawasiliane na mama najua atanihamisha hapa na kwenda kutibiwa Mbeya.” Waliongea mambo mengi asubuhi hiyo hadi muda wa kuwaona wagonjwa ulipoisha kisha Patrick akamuaga Happy kuwa anaenda kupiga simu.



**********


Saa tano na dakika ishirini na saba gari moja ndogo yenye vioo vyeusi lilifunga breki katika hospitali ya Makambako .Mama mmoja akiongozana na binti mmoja ambaye ni wazi alionekana kuwa ni mwanae walishuka ndani ya gari lile na kuelekea mapokezi.Waliongea na wauguzi waliokuwapo pale mapokezi kisha wakapelekwa kwa mganga mkuu.Baada ya muda wakatoka wakiwa wameongozana na mganga mkuu na kuelekea maeneo ya wodi za wagonjwa. Patrick alikuwa nje ya wodi aliyokuwa amelazwa Happy .Hali ya hewa ilikuwa ya kiubaridi baridi kama ilivyo ada ya hali ya hewa ya Makambako.Kijua kilichomoza na kuzima.Hii haikumsumbua sana kwa sababu alikuwa bado amevaa suti aliyokuwa ameivaa jana yake.Mara akawaona mama mmoja na mwanae wakiwa wameongozana na daktari mkuu. “Mhhhh!!” Patrick akaguna.Akazidi kuwaangalia kwa makini watu wale wakija .
“Yule msichana mbona kafanana sana na Happy ? anaweza akawa ndiye yule ndugu yake ? hata yule mama amefanana sana na Happy” Patrick akaendelea kuwaza huku akiwatazama yule mama na yule binti wakielekea katika wodi aliyokuwa amelazwa Happy..Mama yule ,binti yake pamoja na daktari mkuu wakampita Patrick pale nje na kuelekea moja kwa moja katika wodi ile aliyokuwa amelazwa Happy wakaingia ndani. “Nahisi ni wenyewe hawa.nahisi huyu ndiye mama yake Happy .”Akawaza Patrick huku akijiweka sawa kwani alitegemea ni lazima wangeonana..Dakika kama tano hivi toka yule mama aingie mle wodini alikuja muuguzi na kumwita Patrick ndani. “mama huyu ndiye Patrick ni rafiki yangu na ndiye aliyeyaokoa maisha yangu kwa kunileta hapa hospitali haraka.”Akasema Happy baada ya Patrick kuingia
“ooh ! Ndiye huyu ! Ndiye huyu aliyenipigia simu asubuhi?” “Ndiye mimi mama.Shikamoo” Patrick akasema kwa adabu “Marahaba mwanangu.nashukuru sana kwa msaada wako.” “Ahsante mama”Patick akajibu.Mama yake Happy alikuwa ni mtu mchangamfu na mcheshi sana. “Patrick huyu ni mdogo wangu anaitwa Margareth.” Happy akasema “Nafurahi sana kukufahamu margareth.”Akasema Patrick huku akishikana mikono na Margareth.Mama yao alikuwa akitabasamu akasema “Patrick tunashukuru sana kwa msaada wako lakini itabidi Happy tumuhamishe hospitali.Tutaenda naye Mbeya akatibiwe kule.Kwa hiyo wewe unaweza ukarejea shuleni.Utapewa barua na mganga mkuu wa hapa ili uipeleke shuleni ya kuthibitisha ugonjwa wa mwenzio.” “sawa mama” akajibu Patrick
Saa saba na nusu za mchana Patrick akawasili shuleni na moja kwa moja akaelekea katika ofisi ya mkuu wa shule msaidizi. “Patrick !!.. akasema mkuu wa shule msaidizi baada ya Patrick kuingia ofisini kwake. “Naam mwalimu” “Umefanya nini tena? Hata wiki mbili hazijaisha toka utoke kwenye adhabu leo tena unarudia mambo yale yale? Akasema mwalimu kwa ukali “Sikiliza mwalim…………………..” “noo !! sitaki kusikiliza upuuzi wako.kwa nini ukamchukua mgonjwa na kukimbia naye mahala kusikojulikana?Sisi kama walimu ndio walezi wenu ninyi mkiwa hapa shuleni . tutajibu nini kwa wazazi wake pindi tatizo kubwa likimpata? Akaendelea kufoka mwalimu mkuu msaidizi‘.Mwalimu,siku ile ya mashindano baada ya kutokea vurugu Happy alijeruhiwa na jiwe kichwani akapoteza fahamu.damu nyingi ikawa ikimvuja.Mimi na mwalimu Steve pamoja na dereva wa shule tukampakia garini na kumpeleka zahanati .pale hakukuwa na daktari na muuguzi tuliyemkuta pale alikuwa akisita hata kumuhudumia Happy .Mimi sikuridhika na hali ile ikanibidi nikodi gari kwa pesa zangu na kumuwahisha Happy hospitali ya Makambako ambako alipatiwa matibabu,akashonwa jeraha lake ,akaongezewa damu pia.na hii hapa ni barua toka kwa mganga mkuu wa hospitali ya Makambako.”Mkuu wa shule msaidizi akaichukua barua ile na kuisoma kisha akamwangalia Patrick kwa sekunde kadhaa. “Ulifanya jambo jema Patrick .Uliokoa maisha ya mwenzio lakini siku nyingine unatakiwa ushauriane kwanza na sisi na siyo kuchukua maamuzi yako binafsi .Mashitaka yaliyoletwa hapa kwangu ni kwamba ulifanya vurugu na kumchukua Happy .Hivi sasa tulikuwa katika maandalizi ya kuripoti suala hili katika vyombo vya usalama vitusaidie kukutafuta na kukuchukulia hatua.Haya nenda ukapumzike ila kuwa mwangalifu sana kwa sasa unafuatiliwa kwa kila unachokifanya” akasema mwalimu “Ahsante sana mwalimu nitakuwa mwangalifu”Patrick akatoka ofisini kwa mkuu wa shule msaidizi na kuelekea bwenini.Akaoga na kujilaza kitandani.
* * * *

Mwezi wa kwanza mwaka uliofuata shule zikafunguliwa na ikawa ni awamu mpya kwa Patrick na Happy .Kwa sasa walikuwa kidato cha nne na walifahamu nini walichokuwa wakihitajika kukifanya hivyo hawakuwa na mzaha katika kusoma.Walisoma kwa bidii kubwa kwa lengo moja tu la kutimiza ndoto zao.Wawili hawa kwa ghafla waka ni mfano wa kuigwa na wengine.Tofauti na mwaka uliotangulia kwa sasa wakaanza kuwa na marafiki wengi wa madarasa ya chini yao ambao mara nyingi walipewa msaada mkubwa katika masomo.Kitendo cha kuheshimiwa na wanafunzi wa vidato vya chini kilizidi kuwapa wakati mgumu wale wanafunzi adui zao ambao walikuwa hawawatakii mema. Ilikuwa ni tarehe 14/03 siku ya jumamosi ambapo wanafunzi walikuwa wametangaziwa kuwa siku hiyo kungekuwa na burudani ya muziki.Burudani kama hizi huja mara chache sana hapa shuleni,hivyo wanafunzi walikuwa wamejiandaa vilivyo.Patrick na Happy nao walishauriana na kukubaliana kuwa wangeingia ukumbini japo kwa muda mchache tu halafu waendelee na ratiba yao za kujisomea. Baada ya mlo wa jioni milango ya ukumbi ikafunguliwa na wanafunzi wakaanza kujitoma ndani.Disko likafunguliwa rasmi na wanafunzi wakaanza kuserebuka.Patrick na Happy wakaingia ndani ya ukumbi lakini hawakukaa sana kutokana na joto ,wakatoka na kwenda kupunga upepo nje.Wakiwa nyuma ya bwalo la chakula wakipunga upepo huku mbalamwezi ikumulika mara ghafla likatokea kundi la vijana waliokuwa wamefunika nyuso zao wakiwa na mapanga matatu wakawazingira.Happy akaogopa na kumkumbatia Patrick “Mama yangu !!!!,”Happy akasema kwa mstuko “ kaa kimya na usijaribu kupiga kelele kwani tutawaua sasa hivi.”Akasema jamaa mmoja aliyekuwa na sauti nzito .Happy alikuwa akitetemeka.Patrick naye mikono ilikuwa ikimtetemeka.Kundi lile lilikuwa na vijana zaidi ya kumi na wote walikuwa wamefunika nyuso zao.Mmoja ambaye ndiye aliyeonekana kuwa kiongozi wao aliwasogelea na kumshika mkono Happy . “Tuna shida na huyu binti” Akasema yule jamaa huku akimvuta Happy kwake.Patrick akainua mkono lakini kabla hajafanya lolote akapigwa na chuma kizito shingoni akaanguka chini na kuona giza, yule jamaa akamshika Happy kisha kwa haraka wakamjaza vitambaa mdomoni ili asiweze kupiga kelele. “Haya jamani haraka haraka tumalize kazi.Leo ni leo.Keo nenda kaangalie kama kuna mtu yoyote anakuja maeneo haya .Ukiona kuna mtu anakuja tufahamishe haraka.”Akaamrisha yule jamaa ambaye alionekana kuwa ndiye kiongozi wa genge lile Happy alikuwa ameshikwa bara bara kiasi cha kutoweza kufurukuta akabebwa juu juu na kupelekwa katika kichaka cha karibu.Kwa kasi ya aina yaka yule jamaa kiongozi akaichana blauzi nyepesi aliyokuwa ameivaa Happy na kuyashuhudia matiti machanga ya kimwana huyu.Udenda ukamtoka.Happy alikuwa akilia lakini sauti yake ilikuwa haisikiki kutokana na vitambaa walivyomuweka mdomoni. Fedhuli yule akaishusha suruali yake hadi magotini na kuanza kumsogelea Happy huku uume wake ukiwa umesimama wima.Akaivuta suruali ya Happy na kuishusha chini kisha akaivuta nguo ndogo ya ndani aliyokuwa ameivaa na kuichana Akaitupa pembeni akawaamuru wale watu waliokuwa wamemshika Happy wampanue miguu. “Hii niyo dawa yake mshenzi huyu.Halafu anaonekana bado bikira.Hii ndiyo dawa ya wasichana kama wewe wenye maringo”
Akasema yule jamaa huku akiuchezea uume wake tayari kumwingilia Happy kwa nguvu
Taratibu Patrick akapata fahamu na kuhisi maumivu makali sana maeneo ya shingoni na mara kumbu kumbu zote zikarudi.Akakumbuka kuwa walikuwa wamevamiwa na yeye akapigwa na kitu kizito shingoni. “Happy yuko wapi?” Akajiuliza na mara akakumbuka kwamba wale wahuni waliowavamia walimchukua kwa lengo la kumtenda vibaya.Akajikaza na kuamka pale alipokuwa amelala huku akihisi maumivu makali mno.Happy hakuwapo na wala wale jamaa waliowavamia hawakuwapo.Hasira ikampanda . “ I must do something immediately kabla hawa jamaa hawajatekeleza mpango wao” AkawazaPatrick.Pale chini akakiona kile chuma alichopigwa nacho akainama na kukiokota kisha akaanza kunyata kuelekea mahala aliposikia minong’ono ya watu.Alinyata taratibu akiwa amefura kwa hasira. Ndani ya kichaka Happy alikuwa ameshikwa barabara kiasi kwamba hakuweza kufurukuta wala kupiga kelele kutokana na matambara yaliyojazwa mdomoni.Kiongozi wa genge lile alikuwa akijiandaa tayari kabisa kutekeleza kitendo cha kumbaka Happy .Ni machozi pekee ndiyo yaliyokuwa yakimtoka binti huyu mrembo .Roho ilimuuma sana kwa kushuhudia kitendo kile alichotaka kufanyiwa.Vile vile aliumia sana roho baada ya kumfikiria Patrick.Hakuwa na uhakika kama atakuwa salama kwani alishuhudia yeye mwenyewe kwa macho yake Patrick akipigwa na chuma kizito akaanguka chini.Ni uchungu ambao hauwezi kuelezeka aliokuwa nao binti huyu.Hakuwa na tumaini la kupata msaada wa aina yoyote kwa wakati ule.Msaada pekee alikuwa ni Patrick na ambaye aliamini kuwa kwa pigo lile lazima atakuwa katika hali mbaya ya kutokujitambua kama sio kufa kabisa Wakati jamaa yule akiuchezea uume wake mkubwa ,Happy huku machozi yakimtoka akafumba macho na kuomba“Ee Mungu najua sina ubaya wowote na mtu yeyote yule hadi kufanyiwa kitendo hiki.Ee baba kama sistahili kufanyiwa hivi basi na isiwe lakini kama …….Hakumaliza maombi yake mara ghafla yule jamaa aliyekuwa tayari kumwingilia akapiga ukelele mkubwa na kuanguka chini.Kilichofuata hapo ni kusikia vishindo vya watu wakikimbia.Ulikuwa ni muujiza ambao Happy hakuutegemea katu.Kijana mmoja ambaye hakuweza kumtambua kwa haraka kutokana na giza alikuwa amesimama mbele yake na kisha akamwinamia. “Happy are you ok?” Ilikuwa ni sauti ya Patrick ambaye aliongea akiwa katika maumivu makali sana. Happy hakusema kitu ni machozi tu ndiyo yaliyokuwa yakimtoka .Hakuamini kabisa kwa alichokuwa akikiona.Patrick akamtoa yale matambara aliyokuwa amewekewa mdomoni kisha akambusu. “Patrick you are my Hero.” Ni neno hilo tu ambalo Happy aliweza kulisema kwa wakati huu.Mwili wote ulikuwa ukimtetemeka. “Hawajakufanya kitu chochote washenzi hawa? Akauliza Patrick “Hwakuwahi, ulifika kwa wakati muafaka kabisa bado walikuwa hawajatimiza azma yao.Ahsante Patrick”Akasema Happy huku machozi yakimtoka Pale chini alikuwa amelala yule kiongozi wa genge lile la wahuni akivuja damu kichwani mahala alipopigwa na chuma .Patrick akamwangalia kwa hasira sana. “Patrick huyu jamaa ni mzima kweli? Happy akauliza “I don t know Happy .Sijui kama atakuwa mzima.Nilimpiga kwa nguvu zangu zote nilizokuwa nazo..Hiyo ni adhabu yake” akajibu Patrick Ghafla wakasikia makelele ya watu wakija kwa kasi kule mahala walikokuwa.
“Happy lets get out of here.wasije wakatukuta hapa hawa watu.tayari wamekwisha ambizana.” Akasema Patrick na kumshika Happy mkono wakaanza kukimbia kushuka katika korongo.Hawakufika mbali wakamulikwa na tochi usoni. “Hey ! simameni hapo hapo,mkikimbia ninaachia mshale huu”Ilikuwa ni sauti nzito ya mwanaume.Patrick na Happy wakasimama.Walikuwa ni watu wanne waliokuwa na mbwa .Watu hawa walikuwa ni wawindaji waliokuwa wakifuatilia mitego yao porini. “Tafadhali jamani naomba mtuache tuondoke tuna matatizo makubwa” Akasema Patrick “Hapana kwanza ninyi mnaonekana ni wanafunzi.Usiku huu mnafanya nini porini?Haya anzeni kuongoza tunawarudisha mpaka shuleni” Akaamuru jamaa mmoja ambaye alionekana kuwa ndiye kiongozi wa wale wawindaji. Jitihada za Patrick an Happy kuomba waachiwe hazikuweza kuzaa matunda,jamaa wakaanza kuwaongoza kuwarudisha shuleni.Hawakuwa na ujanja tena zaidi ya kufanya vile walivyoamriwa.




* * * *


“wameuaaaaaa !!!....wauajiiiiiiiiii!!!!!!......wauaweeeee!!!!!!!!!!” Hizo ni kelele zilizoufunika mji wa Malangali kwa muda huu wa usiku.Patrick na Happy walikuwa katika mikono ya polisi kwa ajili ya usalama wao.Yule jamaa aliyepigwa na chuma kichwani na Patrick alikuwa amekufa. Karibu kijiji chote kilikuwa kimeamka kutokana na makelele ya wanafunzi na kukusanyika shuleni.Wote walitaka washuhudie ni wanafunzi gani waliofanya mauaji.Baada ya kuingizwa katika kituo kidogo cha polisi kilicho pembezoni mwa shule ikawabidi polisi kupiga risasi za moto juu ili kuwatawanya wanafuzi ambao walikuwa wameanza kurusha mawe wakitaka watuhumiwa waachiwe ili wauawe pia.Ilikuwa ni kazi kubwa kuwatawanya lakini hatimaye walifanikiwa baada ya kupiga risasi kadhaa hewani. Happy machozi yalikuwa yakimtoka.Hakutegemea kama siku moja angeweza kuingia katika dhahama ile.Hakuwahi kuota kama siku moja angeitwa muuaji. “Nyamaza Happy ,usilie mambo yameshatokea..Jipe moyo Mungu yupo na yeye ndiye anayeufahamu ukweli.” Patrick akambembeleza Happy “Patrick nina uchungu mwingi sana .Ni bora ningekuwa mwenyewe lakini sasa nimekuingiza na wewe katika matatizo makubwa namna hii.tayari nimekwisha kuharibia mwelekeo mzima wa maisha yako……….” “Shhhhhhhh..!!!....Usiseme hivyo Happy .I did the right thing.Hata nikinyongwa nitakuwa na amani kwamba niliua kwa ajili ya kukulindia heshima yako.Hakuna mwanaume yeyote anayeweza kukubali kuona mpenzi wake akifanyiwa kitendo cha kinyama kama walichotaka kukufanyia hawa jamaa.nadhani nilifanya kitu sahihi.Sijutii kosa langu kwa sababu nimefanya kwa ajili ya mtu nimpendaye” Happy akamkumbatia Patrick kwa nguvu huku akilia .
Kwa ajili ya usalama wao usiku huo huo wakapakiwa katika gari la polisi na kupelekwa kituo kikuu cha polisi Iringa mjini




* * * *

Karibu kijiji chote kilikuwa kimeamka kutokana na makelele ya wanafunzi na kukusanyika shuleni.Wote walitaka washuhudie ni wanafunzi gani waliofanya mauaji.Baada ya kuingizwa katika kituo kidogo cha polisi kilicho pembezoni mwa shule ikawabidi polisi kupiga risasi za moto juu ili kuwatawanya wanafuzi ambao walikuwa wameanza kurusha mawe wakitaka watuhumiwa waachiwe ili wauawe pia.Ilikuwa ni kazi kubwa kuwatawanya lakini hatimaye walifanikiwa baada ya kupiga risasi kadhaa hewani. Happy machozi yalikuwa yakimtoka.Hakutegemea kama siku moja angeweza kuingia katika dhahama ile.Hakuwahi kuota kama siku moja angeitwa muuaji. “Nyamaza Happy ,usilie mambo yameshatokea..Jipe moyo Mungu yupo na yeye ndiye anayeufahamu ukweli.” Patrick akambembeleza Happy “Patrick nina uchungu mwingi sana .Ni bora ningekuwa mwenyewe lakini sasa nimekuingiza na wewe katika matatizo makubwa namna hii.tayari nimekwisha kuharibia mwelekeo mzima wa maisha yako……….” “Shhhhhhhh..!!!....Usiseme hivyo Happy .I did the right thing.Hata nikinyongwa nitakuwa na amani kwamba niliua kwa ajili ya kukulindia heshima yako.Hakuna mwanaume yeyote anayeweza kukubali kuona mpenzi wake akifanyiwa kitendo cha kinyama kama walichotaka kukufanyia hawa jamaa.nadhani nilifanya kitu sahihi.Sijutii kosa langu kwa sababu nimefanya kwa ajili ya mtu nimpendaye”Happy akamkumbatia Patrick kwa nguvu huku akilia .
Kwa ajili ya usalama wao usiku huo huo wakapakiwa katika gari la polisi na kupelekwa kituo kikuu cha polisi Iringa mjini .


* * * *



Uchunguzi wa kesi ya mauaji inayowakabili wanafunzi wawili wa kidato cha nne Patrick na Happy ulianza kwa kasi .Wazazi wa happy wakishirikiana na wale wa Patrick waliweka mawakili sita wa kuwatetea watoto wao.Pamoja na jitihada hizo zote za kuhakikisha kuwa watoto wao wanaachiwa huru na mahakama bado kesi ikaonekana kuwa ngumu kutokana na ushahidi mkubwa wa wanafunzi kuwakandamiza Patrick na happy.Wanafunzi zaidi ya kumi walikubali kusimama mbele ya mahakama na kutoa ushahidi kuwa Patrick na Happy kwa pamoja walishirikiana katika mauaji ya Angatile mmoja kati ya wanafunzi watukutu hapo shuleni.
Baada ya miezi miwili Happy akaachiwa huru na mahakama alipoonekana hakuwa na kesi ya kujibu.Patrick ambaye alionekana kuwa ana shataka la kujibu akabaki gerezani huku kesi yake ikiendelea kusikilizwa.Huo ukawa ni ukurasa mpya wa maisha yake gerezani.
Miezi ilizidi kukatika Patrick akiwa bado gerezani akiendelea kushikiliwa kwa shitaka la mauaji.Happy ambaye alikubaliwa na uongozi wa shule yao kuwa ataruhusiwa kurudi kufanya mtihani wake wa kidato cha nne aliendelea na masomo jijini Mbeya..Alidhoofu kwa mawazo na ukiwa aliokuwa nao.Furaha yote aliyoipata kwa muda mfupi ilikuwa imetoweka.Hakuwa tena na rafiki Rafiki yake mkuu alikuwa ni Patrick ambaye kwa sasa alikuwa gerezani.Kila siku alikuwa akilia na kumuomba Mungu amsaidie Patrick aweze kutoka gerezani .Moyoni alijua ni yeye ndiye aliyesababisha Patrick kuwapo gerezani .Patrick aliua wakati akijaribu kumtetea yeye asibakwe.Aliumia sana kila alipolifikiria suala hili. Kila mwishoni mwa wiki alikwenda kumtazama Patrick na kumpelekea vitu mbali mbali.Wazazi wa Happy halikadhalika walikwenda mara kwa mara kufuatilia maendeleo ya kesi ya Patrick na kumjulia hali.Happy alikwisha waeleza kwa kina juu ya kilichosababisha Patrick kuwepo gerezani.Wazazi wa Patrick walijitahidi kwa kila walivyoweza ikiwa ni pamoja na kuongeza mawakili maarufu wa kujitegemea katika jopo la mawakili wanaomtetea Patrick.Kilikuwa ni kipindi kigumu sana kwa familia zote mbili . Hatimaye kikafika kipindi cha kufanya mitihani ya Taifa ya kumaliza kidato cha nne Patrick akiwa bado gerezani.Siku tatu kabla ya mtihani huo kuanza Happy akamtembelea gerezani ambako waliongea mambo mengi.“Patrick mpenzi nasikia uchungu sana kwa hali hii.Tulikuwa na malengo mengi sana ya maisha yetu kwa siku za usoni lakini yote yameyeyuka.Sijui lini utatoka gerezani mpenzi wangu…………” Happy akashindwa kujizuia akaanza kulia ,Patrick akamkumbatia na kumbembeleza.“ Nyamaza Happy .Hutakiwi kulia.Be strong.Haya ni mambo ya kawaida.Kila kitu hutokea kwa sababu maalum Huwezi kujua kwa nini sisi yametutokea haya.Maandiko matakatifu yanatuasa tushukuru katika kila jambo linalotufika.Sijutii kuwapo hapa kwa sababu niko hapa kwa ajili ya mwanamke nimpendaye.Kitu kimoja tu ninachokuomba jiandae vyema na mitihani yako na Mungu akujalie ufanye vizuri.Mimi nipo na Mungu atanisaidia siku moja nitatoka.Nitakuwa nimepoteza muda mwingi na mwelekeo mzima wa maisha yangu lakini nitakuwa na furaha kuwa nilipigana kiume kulinda heshima ya mtu nimpendaye duniani.Ila nakuomba kitu kimoja Happy ………”Patrick akanyamaza akavuta pumzi ndefu ,akamwangalia Happy kwa sekunde kadhaa ,akamfuta machozi .“Happy naomba kabla muda wetu wa maongezi haujakwisha unihakikishie kitu kimoja kwamba pamoja na kuwa sijui lini nitatoka gerezani,pengine nitanyongwa lakini naomba kusikia kutoka kwako leo hii kuwa hautakuwa na mwanaume mwingine zaidi yangu pamoja na hali yangu hii kwa sasa.Naomba haya yote yaliyotokea yasipotee bure,naomba uendelee kuheshimu ahadi zetu tulizowekeana,naomba ue……………..”Patrick akashindwa kujizuia kutokwa na machozi. “Patrick mpenzi wangu ,nyamaza kulia.Najua inauma sana na ni ngumu kuibeba adhabu hii kubwa lakini naomba nikuhakikishie kuwa kwa namna yoyote ile sintadiriki kuwa na mwanaume yeyote zaidi yako.Nitakusubiri kwa muda wote mpaka utakapotoka ili tuweze kutimiza ndoto zetu pamoja.I promise.” Akasema Happy kisha wakakumbatiana kwa hisia kubwa huku kila mmoja machozi yakimdondoka.Muda ukaisha Happy akaombwa aondoke.




* * * *

Muda ulikwenda kwa kasi .Na hatimaye matokeo ya kidato cha nne yakatoka na Happy akachaguliwa kuendelea na kidato cha tano na sita katika shule ya Sekondari ya wasichana ya Iringa.Alifurahi sana kwa kuchaguliwa kwenda pale kwani atakuwa bado karibu na Patrick ambaye kwa sasa alikuwa ni sehemu ya maisha yake .Ingawa bado hakukuwa na matumaini yoyote ya Patrick kutoka gerezani kutokana na mwenendo wa kesi kuwa mgumu,lakini bado Happy alizidi kumpenda na kumpa moyo.Kila wiki alikuwa akienda kumtazama gerezani na kumpa faraja..“Patrick matokeo yametoka “Alisema Happy alipokwenda kumtembelea Patrick gerezani mara baada ya matokeo kutoka.
“Hizo ni habari njema sana.Unakwenda shule gani ? Patrick akauliza
“nimechaguliwa kuendelea na masomo hapa hapa Iringa.Nitasoma Iringa girls.Nilikuwa nikiomba Mungu nisipangwe shule yoyote ya mbali ili isiwe vigumu kuja kukutembelea.Patrick wewe ni sehemu ya maisha yangu na kamwe siwezi kuvumilia kuwa mbali nawe.Nashukuru Mungu amesikia kilio changu .” Happy alisema huku amemkumbatia Patrick .“Happy nimefurahi sana kusikia hivyo.Mungu bado anatupenda.Pamoja na misuko suko yote iliyotukumba lakini bado umeweza kufanya vizuri na kufaulu mtihani wako.Hongera sana Happy.Kumbuka kama imeandikwa kuwa mimi na wewe tutakuwa pamoja maishani hakuna ambaye anaweza kututenganisha.” Patrick akasemaIlikuwa ni siku ya furaha sana kwao.
Mpaka Happy anamaliza kidato cha sita bado Patrick alikuwa akisota katika mahabusu ya gereza kuu la Iringa.Kesi yake ilikuwa ikisomwa na kuahirishwa mara kwa mara.Tayari Patrick alikwishazoea maisha ya kukaa mahabusu.Afya yake ilikuwa imedhoofu kutokana na maisha magumu ya gerezani.Faraja pekee aliyokuwa nayo ni Happy aliyekuwa akienda kumtazama kila jumamosi pamoja na wazazi wake.Upendo wa Happy haukupungua hata kidogo.Kila siku upendo wake kwa Patrick ulikuwa ukiongezeka. Jumamosi moja Happy alienda kumtembelea Patrick kama ilivyo kawaida yake.Kwa sasa tayari alikwisha maliza shule na alikuwa akisubiri matokeo ya kidato cha sita.Wakati wakiongea Patrick akamtazama Happy usoni kwa makini na kusema. “Happy mpenzi naomba nikufahamishe kuwa Jumatatu ndo ile siku yangu ya Hukumu .Nashukuru Mungu kwani baada ya kusota gerezani kwa muda mrefu hatimaye nitaenda kusomewa hukumu yangu.Sijui nini kitatokea.Mwenendo mzima wa kesi yangu unaonesha kuwa nina hatia japokuwa kesi ilibadilishwa na ikawa ni kuua bila kukusudia...Siyo siri ninaogopa.Sijui kama nitafungwa maisha au nitahukumiwa miaka mingapi gerezani.Mungu anajua kuwa sikukusudia kufanya vile lakini nilifanya kwa sababu ya kumlinda mtu nimpendaye asidharirishwe na wahuni wale.Happy naomba usiwepo mahakamani siku hiyo ya hukumu.Sitaki uumie.Ni wewe tu ndiye unayeufahamu ukweli hivyo kusikia hukumu nitakayoipata najua itakuumiza mno.Ila kumbuka vyovyote vile itakavyokuwa naomba ujue kuwa nakupenda sana.I love you so much Happy .Wewe ni mtu pekee ambaye ninayatoa maisha yangu kwake.Sintapenda mtu mwingine kama ninavyokupenda wewe…………….”Patrick akasema kwa hisia kaliHuku akitokwa na machozi Happy akasema“Patrick nashindwa hata niseme nini.Siku zote tumekuwa tukiomba siku hii ifike haraka ili tujue hatma yako lakini kwa sasa naona kama vile siku hii isije.lakini siwezi kuizuia isifike.I’ll be strong.Nitajitahidi kuwa jasiri na kuwepo siku hiyo ya hukumu.I must be there Patrick.I mus………………” Happy akaangua kilio. Ilichukua muda kumbembeleza Happy .Huzuni kuu ilitanda kwa vijana hawa.Hawakuongea sana walikuwa wamekumbatiana huku kila mmoja akiwa kimya.Kila mmoja akiwaza lake.


* * * *

Ni siku ya Jumatatu mahakama ilifurika watu.Wote walikuja kushuhudia hukumu ya Patrick,kijana mwanafunzi aliyemuua mwanafunzi mwenzake. Ndugu za Patrick wote walikuwa wamewasili mapema sana hapa mahakamani.Si wao tu hata familia nzima ya akina Happy ilikuwa imewasili kusikiliza hukumu hii.Familia ya Happy na ile ya Patrick kwa sasa zilikuwa zimekwisha fahamiana na wote walikuwa kitu kimoja katika kumsaidia Patrick. Saa mbili kamili juu ya alama gari lililowabeba washtakiwa wa kesi za mauaji ambao walikuwa wakisomewa hukumu zao liliwasili eneo la mahakama.Simanzi kuu ikatanda eneo hilo baada ya watuhumiwa wale kuwasili.Happy alishindwa kujizuia kudondokwa na machozi pale aliposhuhudia Patrick akishushwa toka katika gari maalum la kubebea mahabusu maarufu kwa jina la karandinga..Margreth na mama yake walijitahidi kumbembeleza na kumtaka ajikaze.Happy akanyamaza. Hatimaye ule muda uliokuwa mgumu sana katika historia ya Patrick ukawadia.Muda wa hukumu.Patrick akapandishwa kizimbani akiwa ni mwenye majonzi makubwa .Macho yake yalikuwa hayaoni vizuri kutokana na machozi yaliyokuwa yanamtoka.Baadhi ya watu ambao hawakumuona kwa muda mrefu walikuwa wakimsikitikia kijana huyu kwa jinsi alivyodhoofu.Akiwa kizimbani mara akagonganisha macho yake na mama yake akajikaza na kutabasamu.Si mbali sana na alipokaa mama yake akakutanisha macho na Happy .Happy akatoa tabasamu la kulazimisha lenye kuonyesha kukata tamaa.Macho yake yalikuwa yamevimba kwa kulia.Akapata faraja kubwa baada ya kugundua kuwa ndugu zake wote walikuwa wamekuja kusikiliza hukumu yake. Jaji kutoka mahakama kuu akaanza kusoma historia ya kesi na baada ya masaa matatu ukafika ule wakati mgumu kupita wote ,wakati wa jaji kuisoma hukumu..Happy moyo ulikuwa ukimwenda mbio.Mwili wote ulikuwa ukimtetemeka.Jasho lilikuwa likimtiririka.mama yake Patrik midomo ilikuwa ikimcheza kwa uoga .Kila mtu alikuwa akiuogopa sana wakati huu.Patrick yeye alikuwa ameinama akisali kimoyo moyo akimwomba Mungu ampe ujasiri wa kuweza kuipokea adhabu yoyote atakayopewa.
Mahakama iliridhika na ushahidi wa pande zote yaani upande wa mashtaka na upande wa utetezi.Kutokana na ushahidi uliotolewa na pande zote mbili mahakama ikaridhia kuwa Patrick alikutwa na hatia ya kuua bila kukusudia hivyo akahukumiwa kwenda jela miaka mitano. Mara tu baada ya hukumu kusomwa Happy akazimia na kutolewa nje kwa ajili ya huduma ya kwanza.Mama yake naye alishindwa kujizuia na kuangua kilio baada ya kumwona mwanae akipakiwa katika gari tayari kwenda kuanza kukitumikia kifungo chake cha miaka mitano.Patrick akajikaza kiume asilie ingawa alikuwa amepatwa na mstuko mkubwa . Gari lililowabeba mahabusu likaondoka mahakamani hapo na kuacha vilio vikiendelea.mama yake Patrick naye alikuwa amezirai.Ni tukio ambalo lilivuta hisia za watu wengi. Hatimaye Patrick akayaanza maisha mapya ya gerezani katika gereza kuu Iringa.


6


MWAKA MMOJA GEREZANI

Tayari Patrick alikwisha kuyazoea mazingira ya gerezani humo.Hayakuwa mageni sana kwani amekwisha sota mahabusu kwa miaka kadhaa kabla ya kuanza rasmi kutumikia kifungo kwa hiyo maisha haya alikwisha yafahamu.na kuyazoea.Tayari alikwisha zoeana na wafungwa wengi ambao walimpenda kutokana na busara zake.Alikuwa ni kijana mdogo lakini mwenye busara za hali ya juu.Aliheshimika na kila mtu gerezani. Kila mwishoni mwa wiki alikuwa akitembelewa na ndugu na jamaa zake.Happy ni mtu pekee ambaye hajawahi kukosa kila mwisho mwa wiki kuja kumtembelea mpenzi wake.Kufungwa kwa patrick bado hakukuwafanya watengane.Bado waliendelea kupendana kwa kiwango cha juu .Alijitahidi kwa kila alivyoweza kumwonyesha upendo wa pekee Patrick kwani aliamini yeye ndiye sababu kubwa kwa Patrick kuwapo pale gerezani. Mwaka wa kwanza ulikatika ukaanza wa pili na hatimaye Happy akamaliza masomo yake ya kidato cha sita.Pamoja na kumaliza masomo yake lakini bado alikuwa akiendelea kumtembelea na kumjulia hali Patrick kila mwisho wa wiki..Matokeo ya kidato cha sita yalitoka na Happy akafaulu vizuri sana kwa daraja la kwanza. Ilikuwa ni furaha kwao wote baada ya matokeo haya kutoka.
Jumapili moja ,Happy alikwenda gerezani kama ilivyo kawaida yake akiwa katika sura iliyoonyesha kuwa na simanzi kubwa.Patrick akamshika mkono na kutaka kujua kitu kilichopelekea yeye Happy akawa katika hali ile.Huku akilia Happy akasema“Patrick nashindwa kuelewa ni kwa nini kila wakati mimi ninakuwa katika majaribu makubwa.Niko katika majaribu makali sana Patrick” Happy akainama na kuanza kulia.“Kwani kuna nini ? Hebu nieleze Happy ” Patrick akahojiHappy akasita kidogo kisha akasema“Baba amenitafutia Chuo nchini Marekani .natakiwa niende kuanza masomo katika chuo cha Howard university . Matokeo bado“
Kilipita kimya cha ghafla humo ndani.Wote wawili walizama katika lindi zito la mawazo.
“Patrick nisikilize.Najua ni kwa kiasi gani habari hii imekuumiza.Ulivyoumia wewe na ndivyo hivyo hivyo nilivyoumia mimi.Nimeumia sana Patrick.Na mpaka sasa kuna ugomvi mkubwa kati yangu na baba.Nimekataa kwenda Marekani.Siwezi kwenda na kukuacha hapa peke yako.I cant leave you alone Patrick.” Patrick akageuza sura yake na kumwangalia Happy ambaye naye macho yake yalikuwa yamejaa machozi.Akatumia vidole vyake kumpangusa machozi kisha kwa sauti ya taratibu na upole akasema. “Happy mpenzi wangu najua kuwa unanipenda sana .nafahamu pia kuwa unaelewa ni jinsi gani ninavyokupenda.Nafahamu haya yote yanayotokea hivi sasa ni majaribu tu ambayo iko siku yatapita na kutuacha sisi bado tunapendana.Nakuamini sana Happy na sina shaka yoyote juu yako kuhusu upendo wako kwangu.Sitaki Happpy ugombane au kushindwa kuelewana na wazazi wako kwa ajili yangu.Alichoamua mzazi ni kwa faida yako kwa siku za usoni. Nakushauri usigombane na wazazi wako kwa ajili yangu.Kubali kwenda kusoma Marekani.Mimi nipo na nitaendelea kuitumikia adhabu yangu hadi hapo nitakapomaliza.Natumai pindi ntakapomaliza adhabu yangu ,nawe utakuwa umemaliza au unakaribia kumaliza masomo yako na hivyo tutaungana tena na kuwa pamoja”
Patrick alitamka maneno haya ingawa moyoni alikuwa na uchungu mwingi.Happy ambaye alikuwa amemshikilia Patrick akamwachia na kumtazama kwa mshangao “Patrick are you out of your mind? Hivi kweli na wewe unakubali mimi niondoke na kukuacha hapa peke yako wakati uko hapa gerezani kwa sababu yangu??? Patrick akatabasamu na kumshika Happy mkono.“Happy kama nilivyokwisha kueleza kuwa nakuamaini sana na wala sina wasi wasi wowote juu ya penzi lako kwangu.Uamuzi huo wa kwenda kusoma ni wa wazazi wako hivyo ni lazima tuuheshimu.Happy mimi ninafurahi kwa sababu unaenda kutengeneza msingi bora wa maisha yako kwa siku za usoni.Mimi nipo na siku zote nitakuombea na kukutakia mafanikio mema katika masomo yako.Ila naomba tu uniahidi kitu kimoja kuwa hutakuwa na mwanaume mwingine yeyote huko Marekani au kwingineko kokote zaidi yangu mimi.Niahidi kuwa utanisubiri mpaka nimalize adhabu yangu ili tuweze kutimiza ndoto zetu pamoja.” Happy akatabasamu kisha akasema.“Patrick nimekwisha kuahidi mara nyingi tu kuwa , chini ya jua sintakuwa na mwanaume mwingine yeyote ambaye si wewe.Wewe ni wa kwanza na wa pekee.Na kuahidi hivyo .Nashukuru sana kwa kuridhia mimi nikasome Marekani .Naenda huko ingawa moyo wangu hautaki kabisa.Najua utabaki mkiwa kwa kunikosa.Pamoja na kwamba nitakuwa mbali nawe kimwili lakini moyo wangu naucha hapa kwako ubaki nao.”
* * * *
Pamoja na umbali kati yao mawasiliano kati ya Happy na Patrick yaliendelea kuwa mazuri.Happy alikuwa akiandika barua kwa Patrick kupitia kwa mkuu wa gereza na Patrick hujibu na kumkabidhi mkuu wa gereza ambaye ndiye aliyejitolea kuhakikisha mawasiliano kati ya vijana hawa yanakuwa mazuri.Mkuu huyu wa gereza alisikia historia ya wawili hawa ikamgusa na kumfanya aahidi kuwasaidia kwa kila alivyoweza..
Chuoni Howard university Happy alikuwa ni miongoni mwa wanafunzi wachache kutoka bara la Afrika .Alikuwa ni binti mpole kupita wote chuoni hapo na kwa muda mfupi aliweza kujulikana sana kwa upole wake.Muda mwingi alipenda kuwa peke yake katika sehemu tulivu.Hakupenda kujiunga na makundi ya wenzake na wala hakushiriki katika burudani yoyote ile.Mawazo yote yalikuwa Tanzania gerezani alikomwacha Patrick akitumikia kifungo chake. Hali hii ilivuta udadisi mkubwa miongoni mwa wanafunzi wenzake.Wapo waliodhani labda ni hali ya ugeni,wengine wakadhanii labda ni uoga na wengine wakadiriki kumwita mshamba. Siku moja profesa Adelin shawlight ambaye ndiye anayehusika na maendeleo na mienendo ya wanafunzi akamwita Michelle ,msichana anayeishi na Happy chumba kimoja na kumuhoji juu ya tabia za Happy “Hata mimi nimekuwa nikijiuliza sana juu ya hali ya mwenzangu huyu.Toka tumefahamiana hatujawahi kuzungumza mambo yoyote zaidi ya salamu.Tunaishi chumba kimoja lakini mpaka leo hii sijui ametokea nchi gani.Akiwa chumbani huwa mkimya sana na kama mara tatu hivi nimemkuta akiangalia picha Fulani huku akilia.Mi naona kuna jambo ambalo linamsumbua akili yake na pengine anahitaji msaada wa kisaikolojia zaidi “ akasema Michelle Profesa Adellin akakubaliana na Michele kuwa ni lazima kuna tatizo linalomsibu Happy na wakaweka nia ya kumsaidia ili aweze kuwa ni mtu mwenye furaha kama wenzake. Siku moja jumapili Michelle akatembelewa na kaka yake aitwaye Mike cambell anayefanya kazi katika wizara ya mambo ya nje ya Marekani.Mike na Michelle ni watoto pekee kwa wazazi wao waishio katika jimbo la California.Michelle alimchukua Mike na kwenda naye hadi chumbani kwao wanakoishi yeye na Happy .Baada tu ya kuingia chumbani humo Mike akapigwa na butwaa baada ya kukutanisha macho na Happy ambaye alikuwa amekaa kitandani akiwa na kompyuta yake ndogo.“Wow ! how beautiful the gal is.Looks like a black angel…….”Mike akawaza.“Hi “ Mike akamsalimu Happy .“Hi “ Happy akajibu na kuendelea na shughuli zake.
Michele akafungua vinywaji toka katika friji lililokuwapo humo chumbani akampatia Mike Happy lakini akakataa.Mike alikuwa akisumbuliwa na kitu moyoni mwake.Uzuri wa Happy ulikuwa umemstua sana.Baada ya kuongea na dada yake akaomba aondoke .“Bye baby” Mike Akamuaga Happy “Bye” Happy akajibu bila hata kugeuza shingo yake“Michelle hebu niambie yule mwenzio ametokea nchi gani?Akauliza Mike wakati wakishuka ngazi“Mimi sijui .tangu tumekutana hatujawahi ongea lolote zaidi ya salamu.Ulivyomuona ndivyo alivyo vile vile.Haongei na mtu na wala hataki urafiki na mtu yeyote.Ni mkimya mno.Lakini nahisi kuna kitu kinachomsumbua”“Michelle unakosea.” Akasema Mike“Ki vipi Mike.”“Wewe ndiye unayetakiwa kuwa karibu naye zaidi kwa sababu mnalala pamoja na hata kama tatizo likimtokea wewe ndiye utakayeweza kumsaidia.Wewe unatakiwa uwe mwenyeji wake hapa marekani.Pengine ni ugeni unaweza kuwa unamsumbua” akasema Mike“Si ugeni Mike,nahisi kuna kitu anakificha.Kuna jambo linamsumbua” akasema Michelle“sasa sikiliza Michelle,Jitahidi kwa jinsi yoyote ile kuwa naye karibu sana.Jitahidi uweze kumzoea na hapo ndipo utakapoweza kumsaidia.Nasikitika sana kumuona binti mrembo kama yule akiwa katika ukiwa wa namna ile”“Mbona unaongea kwa msisistizo Mike ?“Anavutia yule binti ,ningependa kumfahamu zaidi “ akajibu Mike.Michelle akatabasamuna kusema “kama ndio hivyo basi hakuna shida nitajitahidi sana niwe naye karibu.ili hata kama unamuhitaji basi iwe rahisi.Hata hivyo ni binti mrembo hata mimi ananivutia sana kwa urembo wake.”“Nitafurahi sana Michelle kama utafanikiwa kuwa karibu na binti yule.Utakuwa umenifanyia kitu kikubwa sana katika maisha yangu.”Mike akasisitiza.“Usihofu Mike nitajitahidi kwa kila namna niwezavyo ili kuwa karibu naye “Waliagana kisha Michelle akarudi chumbani kwao akiwa ni mwingi wa mawazo jinsi gani atakavyoanza kumzoea Happy msichana ambaye hakutaka mazoea na mtu yeyote yule.Michelle akaingia chumbani akajimiminia kinywaji katika glasi na kuanza kunywa huku akimtazama Happy kwa makini sana.“Excuse me my dear sister” Michelle akajikaza na kumsemesha Happy ambaye bado alikuwa anafanya kazi na kumpyuta yake ndogo“Yes ,what’s up “ Akasema Happy bila kumuangalia Michelle.“Sister unajua tangu tumepangwa kuishi wote katika chumba hiki hatujawahi kuongea hata siku moja,hatujawahi hata kufahamiana.Binafsi sipendezwi na staili hii ya maisha tunayoishi.Tuko katka chumba kimoja yatupasa tuishi kama ndugu,tupendane na kusaidiana.Mimi naitwa Michelle camble natokea California.” Akaanzisha mazungumzo Michelle.Happy akaacha kufanya kazi katika kompyuta yake akamuangalia Michelle kwa muda kisha akasema “Naitwa Happy ..Happy Kibaho ,natokea Tanzania”“Uuugh ! nafurahi sana kusikia unatoka Tanzania.I love Tanzanians.Nasikia ni watu wapole na wakarimu sana.Mama yangu amewahi kwenda Tanzania kupanda mlima Kilimanjaro na aliporudi akatuhadithia kuwa hajawahi kukutana na watu wakarimu kama watanzania.”
Happy akatabasamu .Ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Michelle kumuona happy akitabasamu.
“Happy you are so pretty.Unajua sikuwahi kukuangalia vizuri.You are amazing” Michelle akajibu na kumfanya Happy afurahi.
“Jina lako zuri sawa kabisa na sura yako..ukitabasamu unakuwa mzuri zaidi ya malaika..” akasema Michelle na kumfanya Happy acheke kwa nguvu. Huo ukawa ni mwanzo wa urafiki mkubwa kati ya Happy na Michelle.


* * * *
Urafiki kati ya Happy na Michelle uliendelea kuimarika siku hadi siku.Michelle alijitahidi kadiri alivyoweza kuwa karibu na Happy .Kila mwisho wa wiki walitoka na kwenda sehemu mbali mbali za starehe lengo likiwa ni kumchangamsha Happy.Pamoja na mambo hayo yote ambayo Michelle alijitahidi kufanya ili kumfanya Happy awe na furaha lakini haikuweza kumsahauliasha kuhusu Patrick hata nukta moja.Alijitahidi kila awezavyo ili asiweze kumsahahu kijana huyu mwenye upendo wa ajabu kwake. Ili tokea siku moja chuo kikafungwa kwa muda wa wiki mbili,Michelle akamuomba Happy wazitumie wiki mbili hizo kwa kuitembelea familia yao huko California.Happy akakubaliana na mwaliko huo na kesho yake wakapanda ndege na kuelekea California.Walipewa mapokezi mazuri na familia ya akina Michelle.Ilikuwa ni furaha iliyoje kwao kumpata mgeni aliyetoka Tanzania. . Siku mbili tu baada ya kuwasili kwao hapo nyumbani ,Mike naye akawasili akitokea jiji la New York anakofanya kazi.Tayari alikwisha taarifiwa na mdogo wake Michelle kuwa tayari Happy alikuwa hapo nyumbani kwao.Mike aliwasili mida ya mchana na kuwakuta familia nzima ikiwa imejipumzisha.Akasalimiana na wote kisha akaelekea chumbani kwake.Kijasho kilikuwa kikimtiririka hasa baada ya kulishuhudia kwa mara ya kwanza tabasamu pana la Happy .Alikaa kitandani na kujaribu kuwaza ni jinsi gani atakavyoweza kujiweka karibu na binti huyu mwenye urembo usioelezeka..Alishindwa kupata jibu akaamua kwenda kuoga kisha akaelekea bustanini ambako Michelle na Happy walikuwa wamepumzika kwa muda huo. Mara tu baada ya Mike kuwasili hapo bustanini ,Michelle akainuka na kwenda ndani kuongeza vinywaji,akawaacha Mike na Happy .Mike moyo ulikuwa ukimdunda .Ilihitaji ujasiri wa aina yake kuanzisha maongezi na binti huyu mwenye uzuri wa kimalaika.Baada ya kimya cha sekunde kadhaa toka amefika pale Mike akajikaza kiume na kuanzisha maongezi.“Happy unanikumbuka?”:Happy akanyamaza kidogo kana kwamba anajaribu kukumbuka kitu kisha akajibu.“hapana”“Nilikuja siku moja chuoni kwenu nikakukuta umeiinamia kompyuta yako” akasema Mike na Happy akatabasamu“Ouh ! nimekukumbuka.kumbe ni wewe ! Samahani siku ile sikuwa katika hali nzuri ndio maana sikukujibu vizuri.” Akasema Happy huku akitabasamu“.hata mimi nilijua haukuwa katika hali nzuri kwa sababu siku hazifanani.” Mike akasema huku akatabasamu baada ya kumuona Happy akitabasamu“Vipi unaionaje hali ya Marekani”Mike akauliza“ ni nzuri,Marekani kuzuri,kila kitu kizuri ,but I miss home” akajibu Happy“Tanzania? Mike akauliza‘Yes ! nani kakwambia kuwa natokea Tanzania?‘Michelle” Mike akajibu .Happy akatabasamu“Hata mimi” Mike akaendelea “naipenda sana Tanzania.Nasikia ni nchi ya amani na watu wake ni wakarimu mno.” Happy akatabasamu baada ya kauli ile ya Mike“Nafurahi kusikia hivyo.Umekwisha wahi tembelea nchi yoyote ya Afrika? Akauliza Happy“Hapana bado sijatembelea nchi yoyote ya Afrika. Ila nina mpango wa kufanya ziara Afrika na nchi ya kwanza kutembelea itakuwa Tanzania.”
“Nini kinakuvutia mpaka uifanye Tanzania kuwa nchi ya kwanza kuitembelea? Happy akauliza
“Just to see pretty women” Mike akajibu na wote wakaangua kicheko.
“ Nina hakika Tanzania imebarikiwa kwa kuwa na vivutio vingi vya kiasili lakini hata hivyo kuna wasichana warembo mno” akasema Mike na wote wakaendela kucheka.Ilikuwa ni wiki nzuri sana kwa Happy .Alifurahi kukutana na familia yenye watu wakarimu kama hii ya akina Michelle.Kwa kiasi Fulani ziara hii ya California ilisaida kumuondolea msongo wa mawazo uliokuwa ukimkabili.Mike na Michelle walijitahidi kwa kila walivyoweza kuhakikisha kuwa Happy anakuwa na furaha kwa muda wote atakaokuwa hapo kwao. Jumapili Mike akamuomba Happy watoke kwa ajili ya matembezi.Michelle alikuwa hajisikii kutoka.Jioni ya siku hiyo wote wawili wakiwa wamependeza vilivyo walipanda gari na kutoka.Safari iliishia katika klabu moja kubwa na maarufu .Ilikuwa ni sehemu tulivu na yenye mandhari ya kuvutia mno.Waliagiza vinywaji na kuanza kunywa taratibu huku wakiendelea na maongezi ya hapa na pale.Kisha Mike akabadili maongezi na kusema.“Happy leo ni siku ya furaha sana kwangu kuwa karibu nawe katika mahali tulivu kama hapa na ni siku muhimu vile vile kwa kuwa nimedhamiria kuutua mzigo mzito unaonikabili kwa muda mrefu sasa”Happy akastuka kidogo kwa kauli ile ya Mike lakini akamuacha Mike aendelee.“Happy nina furaha moyoni mwangu kukutamkia kuwa u mwanamke pekee ambaye umeweza kuuteka moyo wangu kwa kiasi ambacho siwezi elezea.Kwa ufupi Happy nakupenda sana na tafadhali ninaomba uridhie ombi langu la mimi na wewe kuwa wapenzi.Naomba unielewe Happy kuwa penzi langu kwako ni la dhati lenye lengo la kuja kuishi nawe kama mume na mke pindi utakapomaliza masomo yako.” Happy akaiweka glasi chini ,akamuangalia Mike kana kwamba ni mara ya kwanza anamuona.Mike naye akamuangalia Happy kwa makini Happy akatabasamu ,tabasamu ambalo kwa kiasi kikubwa linamchanganya Mike.“Mike you are very handsome” Happy akasema akainua glasi yake ya kinywaji akanywa funda moja
“Oh ! thank you Happy” mike akasema huku akitababasamu na kuirekebisha tai yake aliyokuwa amevaa.Happy akaendelea
“ Mike wewe ni kijana ambaye kila mwanamke angependa uwe naye.Una kila sifa za kijana bora.U mcheshi,mchangamfu na unayevutia.Nashukuru kwa kuwa wazi na hisia zako.Ila samahani kaka yangu mimi tayari nina mtu ambaye sijui hata nikuelezeje ili unielewe kwa jinsi ninavyompenda Kijana huyu ndiye aliyeushika moyo wangu,ameyashika maisha yangu.yeye ni kila kitu kwangu.Nampenda Patrick kuliko ninavyojipenda mimi.Kama nisingekuwa na Patrick nisingekukataa Mike.” Happy akasema kwa kujiamini. Mike akainama chini kwa sekunde kadhaa akiwaza.tayari alikwisha uona ugumu uliopo mbele yake.katika kumshawishi Happy akubali ombi lake la kuwa naye katika mahusiano.“Happy naheshimu mawazo yako na ninauheshimu sana uhusiano wa mtu.Si lengo langu kuvuruga uhusiano wako.Kwa kuwa tayari una mpenzi anayekupenda na wewe unampenda basi naomba kitu kimoja tu kutoka kwako.”“Kitu gani Mike?” Happy akauliza“ nataka tuwe marafiki wa kawaida”“Kwa hilo hakuna shida.Mike nashukuru sana kwa kunielewa.Nitakuombea ili uweze kumpata msichana kama mimi ambaye nina imani utampenda zaidi yangu.”“nafurahi kusikia hivyo Happy ” Mike akasema katika hali ya unyonge.Maisha yaliendelea vizuri na baada ya wiki mbili kumalizika Michelle na Happy wakarudi chuoni Mike akarejea kazini kwake New york


* * * *


Patrick aliendelea na maisha ya gerezani kama kawaida.Siku moja Patrick akaitwa na mkuu wa gereza na kuambiwa ajiandae kwa safari alikuwa akihamishwa gereza.Hii ilikuwa ni taarifa ambayo ilimvunja moyo sana kiasi cha kumfanya adondoshe machozi.Ni wafungwa watatu tu ndio waliokuwa wakihamishwa gereza.Haikuweza kufahamika mara moja sababu ya kuhamishwa kwao Wakati wakijiandaa kuondoka ,hakukuwa na mfungwa mwingine wa karibu ambaye angeweza kumwachia ujumbe wowote.Hakujua anahamishiwa gereza gani. Alizoea kila wiki kupokea barua za Happy .Hakujua angewezaje kumfahamisha juu ya uhamisho ule wa ghafla.Safari ilianza bila kuchelewa .Ilikuwa ni safari ndefu na yenye kuchosha.Gari walilopanda lilikuwa na madirisha madogo juu kwa ajili ya kuingiza hewa .hivyo kutokutambua ni wapi walikokuwa wakielekea. Wakiwa wamepitiwa na usingizi walistuliwa na sauti ya kufunguliwa kwa mlango.Walifunguliwa pingu walizokuwa wamefungwa mikononi na kuamriwa kushuka.Walikuwa wamechoka kupita kiasi.Ilikuwa ni safari ndefu na njaa ilikuwa ikiwauma kupita maelezo.Tangu wapewe chakula mchana ambacho kilikuwa ni chipsi kavu na maji ya kunywa hawakula tena chochote.Tayari giza lilikwisha tanda angani.Hawakujua ilikuwa ni saa ngapi mida hiyo.Hali ya mahala hapo ilikuwa ni ya baridi kali.Wote walikuwa wakitetemeka.Walisimamishwa hapo kwa takribani dakika ishirini kisha askari mmoja akatoka ndani akawaangalia na kuamuru wapelekwe ndani wakapumzike.Waliongozwa na askari wawili wenye silaha hadi ndani ya gereza.Kila mmoja akaonyeshwa chumba chake cha kulala.Hili lilikuwa ni gereza jipya kabisa na la kisasa lililokuwa limejengwa mjini songea kwa msaada wa watu wa Marekani.Lilikuwa ni gereza la kwanza la mfano nchini Tanzania kuwa na ubora wa hali ya juu afrika mashariki na kati.Patrick alishukuru Mungu kwa kuletwa hapa .Kutokana na uchovu wa safari aliokuwa nao akajitupa kitandani na kulala.Saa kumi na mbili asubuhi king’ora kikalia .Patrick mwili wote ulikuwa ukimuuma kwa uchovu na alihisi njaa kali.“Hey amka ndugu ” Akastuliwa na sauti ya mtu aliyekuwa akimtikisa.Akafumbua macho na kukutana na macho ya kijana mdogo mwenye sura ya upole.“Vipi husikii king’ora hicho?” Akaendelea kusema yule kijana.Kiuvivu Patrick akainuka na kukaa kitandani.baada ya kama dakika tatu hivi akaja askari akafungua geti la chumba chao na kumrushia Patrick nguo mpya kabisa za kifungwa.Hakusema kitu akazikunjua na kuvaa .“Kwa hiyo nini kinaendelea saa hizi? Utaratibu wa hapa ukoje ?” Patrick akamuuliza yule kijana waliyekuwa wakilala wote chumba kimoja.“huu ni muda wa kujiandaa,kunawa au kuoga kama unataka .Kitapigwa king’ora kingine tutaenda kupata mlo wa asubuhi halafu baada ya hapo tutapangiwa kazi.”Patrick akaonyeshwa sehemu yenye mabafu akaingia na kuoga..King’ora kingine kikalia na wote wakakusanyika katika bwalo la chakula kwa ajili ya kifungua kinywa..Walikuwa wafungwa wachache kama arobaini hivi. Baadaye kazi zikapangwa na Patrick na wenzake wakapangiwa sehemu ya kufyeka.Miongoni mwao alikuwemo yule kijana anayelala naye chumba kimoja.Walifanya usafi huku wakisimuliana mambo mengi na kupeana moyo.taratibu wakaanza kuzoeana na kujenga urafiki. Usiku wa siku hiyo Patrick na yule kijana ambaye alikuja kumfahamu kama Andrew waliutumia katika kusimuliana mikasa mbali mbali ya maisha yao.Andrew alimsimulia Patrick kisa cha yeye kuwapo pale gerezani.Kifungo chake kilikuwa cha miaka mitatu na kilitokana na kusababisha ajali wakati akiendesha gari akiwa amelewa.Patrick naye alimsimulia hadithi yake na mpaka anamaliza Andrew alishindwa kujizuia kudondokwa na mchozi.“Pole sana Patrick hayo yote ni majaribu katika maisha .Ni wazi Patrick una upendo wa dhati na wapekee sana kwa huyo Happy .Usikate tamaa Mungu atakusaidia utamaliza kifungo chako.”“Ahsante sana Andrew kwa kulitambua hilo na kunipa moyo.Lakini kitu ambacho bado kinaniumiza sana kichwa ni jinsi nitakavyoweza tena kuwasiliana na Happy .Katika gereza lile nilikotoka ,mkuu wa gereza alikuwa amejitolea kunisaidia kwa kutuma barua zangu kwenda kwa Happy na kupokea zitokazo kwa happy na kuniletea..Ningeweza kuwatumia wazazi wangu lakini bado hawajui kama nimehamishwa gereza “ akasema Patrick kwa masikitiko

* * * * .
Siku moja Patrick akapangiwa kwenda kufanya usafi katika nyumba ya mkuu wa gereza.Huko alipangiwa kufyeka na kurekebisha viunga vya maua .Katika dirisha lililoelekea upande wa mbele ya nyumba dada mmoja mrembo alikuwa amekaa mkono shavuni kwa takribani dakika kumi na tano akimuangalia Patrick bila yeye kujua kama alikuwa akiangaliwa.Alistaajabu kwa kumuona kijana kama yule ambaye kwa mbali tu alionekana ni kijana mpole,mtaratibu na mwenye kuvutia ,akiwa gerezani.“ama kweli jela haina mwenyewe.How such a handsome guy be in prison?.Alifanya nini kijana yule i? Mhh ! hebu mwangalie vizuri halafu anaonekana ana mawazo mengi.Namuonea huruma ..jamani !! ..” Akawaza mwanadada yule.
Haraka haraka dada yule akaenda jikoni na kutengeneza chai akaweka katika sinia akabeba na kuelekea mahali alipokuwa akifanya kazi Patrick. “kaka habari za kazi? Patrick akastushwa na sauti tamu,laini ya mwanadada.Akageuka na ghafla akajikuta akiangusha fyekeo.Macho yake yakakutana na binti ambaye uzuri wake wa asili ulikuwa unasisimua.Hakuamini kama angeweza kukutana na binti mrembo vile maeneo yale.
“Pole na kazi “ Akasema tena binti yule baada ya kuona Patrick akimuangalia tu bila kusema kitu.‘Nzu…r..rii tu dadangu” Akajibu.Patrick kwa sauti yenye kigugumizi.
“Kaka unaweza ukapumzika walau upate kikombe cha chai kwani toka asubuhi nakuona unachapa kazi bila hata kupumzika ”Akasema yule dada akamkaribia Patrick na kuweka lile sinia chini.“Nashukuru sana dadangu lakini naogopa mkuu akinikuta hapa patakuwa hapatoshi”“Usihofu kaka yangu ,mjomba hayupo amekwenda Dar leo asubuhi na hata mkewe naye hayupo atarudi kesho”akajibu yule dada Patrick anamkazia macho yule dada baada ya kusikia kauli ile.
”Ina maana binti huyu ni mjomba wake na mkuu wa gereza? Du ! mtoto ameumbika vilivyo.Ananikumbusha sana mpenzi wangu Happy .”Patrick hakujivunga tena akaenda katika bomba na kunawa mikono“Karibu” yule dada akamkaribisha Patrick“Ahsante lakini mbona kikombe chenyewe ni kimoja? Patrick akauliza“Usijali kaka yangu hii ni kwa ajili yako”Patrick akanywa chai ile nzuri .Kwa muda mrefu hakuwahi kuipata chai nzito kama ile.Akamaliza kikombe cha kwanza na kuongeza tena cha pili na hatimaye cha tatu.Kimoyo moyo alimshukuru sana yule dada mrembo kwa chai ile kwani alihisi njaa kali asubuhi hiyo.Wakati Patrick akinywa chai ile,yule dada aliingia ndani na kwenda kukaa katika lile dirisha akiendelea kumwangalia “Anateseka huyu kaka .Namuonea huruma kweli.Halafu mpole.Sijui alifanya kosa gani huyu kaka manake haonekani kama mhalifu “ Akawaza yule dadaPatrick akamaliza kunywa chai akakusanya vyombo na kwenda kugonga mlango.Yule dada akafungua mlango na kuvipokea.“Ahsante sana dada Mungu akubariki” Akasema Patrickkisha akaendelea na kazi yake yake ya usafi .Kila dakika taswira ya yule dada mpole mwenye roho ya huruma ilikuwa ikimjia na kumfanya atabasamu
.”Kumbe duniani bado kuna watu wenye upendo “ Akasema taratibu huku akiendelea na kazi yake ya kurekebisha bustani ya maua.
“Imezoeleka katika jamii yetu kila mfungwa ni mnyang’anyi,hali ambayo kufanya wafungwa kutokuthaminiwa,kutokuhurumiwa,na hata kutokusaidiwa lakini bado wako watu wachache wenye huruma na upendo kwa wafungwa kama huyu dada alivyofanya leo.Aliwaza Patrick.Wakati akiendelea na usafi dada yule akatoka tena na kisinia kilichokuwa na glasi mbili za juice.“Kaka karibu upumzike upate juice” akasema yule dadaPatrick aliingiwa na wasiwasi iwapo wakuu wake wangekuja na kumkuta amekaa .“ahsante sana dadangu ila naogopa iwapo hawa wakuu wetu watakuja na kunikuta nimekaa nakunywa hiyo juice itakuwa ni habari nyingine” Patrick akasema huku akiwa na wasi wasi lakini moyoni alitamani sana juice ile.Huku akitabasamu dada yule akasema“Usihofu kaka nimekwambia mjomba wangu hayupo na hata mkewe hayupo kaenda Iringa .Hapa nipo mimi tu .Kaa upumzike kaka yangu unajua upatapo nafasi ya kufanya usafi katika nyumba hizi za wakuu ni nafasi yako ya kupumzika.Kazi zenu ni ngumu sana” Akasema dada yule“Ni kweli usemayo dada yangu lakini inategemea na mahali penyewe.Unajua kwa sisi wafungwa jamii inatuchukulia kama wote ni wanyang’anyi kumbe sivyo.Nimekuwa nikifanya usafi katika baadhi ya nyumba za maafisa wakubwa na wadogo lakini hakuna hata siku moja niliyowahi kupewa hata glasi ya maji.Lakini kumbe kuna watu wana roho za utofauti sana na mmoja wao ni wewe.U mkarimu sana dada yangu.”akasema Patrick Taratibu Patrick akajikuta akikaa chini kwenye bustani huku ameikamata glasi ya juice.Juice kama hii alizowea kuipata wakati Happy hajaondoka.Siku hii ya leo inamkumbusha mbali sana.Alishindwa kuyazuia machozi kudondoka mara alipomkumbuka Happy “Vipi kaka yangu mbona unalia?“ Juice hii imenikumbusha mbali sana” akajibu Patrick“Basi usilie kaka yangu Mungu yupo na atakusaidia uweze kumaliza kifungo chako”Kilipita kimya cha sekunde kadhaa Patrick akauliza“lakini dada yangu inaonyesha wewe si mwenyeji kabisa wa maeneo haya”Huku akitabasamu dada yule akajibu“kwa nini unasema hivyo”“Inaonyesha tu.Mwonekano wako haufanani kabisa na mazingira haya”Dada yule akacheka kicheko kikubwa kisha akajibu.“Una uwezo mkubwa wa kuweza kumsoma mtu na kumwelewa kwa haraka.Ni kweli mimi si mwenyeji wa hapa .Mimi naishi Dar es salaam.Mzee Joel mkuu wenu wa gereza ni mjomba wangu na nimekuja mara moja kumletea mizigo yake iliyotumwa na dada toka Ulaya.Ingawa sintakuwa na muda mrefu hapa lakini nimetokea kupapenda sana.Pana hewa nzuri na nimazingira tulivu sana.” Akasema yule dadaYule dada akatulia kidogo akanywa mafunda mawili ya Juice kisha akasema“ Kwa jina naitwa Veronika .Veronika Rugi sijui kaka wewe unaitwa nani?Patrick akanyamaza na kutafakari iwapo amweleze jina lake au vipi.Mwishowe akaamua kumtajia jina lake“Naitwa Patrick ““ nafurahi sana kukufahamu Patrick.Unajua toka nimekuona asubuhi ukifanya usafi moyo wangu haukutulia kabisa.Nilikuwa na hamu sana ya kutaka kukufahamu.U mpole sana na haufanani na wafungwa wengine”Patrick akacheka baada ya kauli ile ya Veronika.
“Kweli kabisa patrick,haufanani na wafungwa tuliozoea kuwaona.Mtu yeyite akikuona mara moja atahisi kuwa uliingizwa gerezani kimakosa.Sura yako haionyeshi kuwa unaweza ukafanya kosa katika jamii ambalo lingepelekea wewe kufungwa gerezani”
Patrick akacheka tena na safari hii kicheko kikubwa zaidi,Vero akatabasamu.“Patrick nitafurahi sana kama utaungana nami kwa chakula cha mchana leo hii.Niko mwenyewe hapa nyumbani na kama ujuavyo chakula cha peke yako katu hakina utamu”Akasema Vero“Hamna shida Veronika “Patrick akajibu .Alikwisha anza kumzoea binti yule mrembo.Veronika akamkaribisha Patrick ndani sebuleni na kumuwashia luninga kisha yeye akaelekea jikoni kuandaa chakula.Patrick alijisikia faraja kubwa kwa kukalia tena sofa nzuri kama zile baada ya muda mrefu.“ Veronika ni binti mzuri ,mrembo mwenye kila sifa inayohitajika kwa binti mrembo .Ni mwelewa na ana huruma sana.Nafurahi kukutana na binti huyu japo kwa muda mfupi.Nina imani vile vile anaweza kunisaidia kurejesha mawasiliano kati yangu na Happy “ akawaza Patrick mara akastuliwa toka katika mawazo na sauti ya Vero“Hello Patrick ,mbona unaonekana mnyonge hivyo?Usihofu kitu .Unaonekana umezama kwenye dimbwi la mawazo.Just relax.Hakuna mtu atakaye kuja kukusumbua.Pumzika mpaka muda wa kurudi ndani utakapofika.” Akasema Verokwa sautiya upole“Ahsante Vero,nashukuru sana dada yangu”Waliongea mambo mengi na kujikuta wakifahamiana na kuzoeana zaidi.Patrick alimsimulia Vero hadithi nzima ya maisha yake iliyomfanya Veronika atokwe na machozi.Hatimaye muda ukafika kwa wafungwa kurejea gerezani wakaagana huku Vero akiahidi kufanya kila njia ili waonane kabla hajaondoka kurudi Dar.

* * * *
Ulikuwa ni usiku mgumu sana kwa Vero.Hakujua ni kwa nini Patrick alikuwa ameingia moyoni mwake kwa kasi ya ajabu namna ile.“Sielewi ni kwa nini Patrick amenigusa ghafla hivi .Ni kijana mpole ,mtaratibu na mwenye kuvutia hata akiwa katika mavazi ya kifungwa.Namuonea huruma sana .Ameugusa sana moyo wangu.Nitajitahidi niweze kumsaidia katika kipindi chote atakachokuwepo gerezani.Toka nimezaliwa sijawahi kuguswa moyo wangu na kijana yeyote kama alivyonigusa leo Patrick na hadithi ya maisha yake.Ni mapenzi mazito aliyonayo kwa Happy ndiyo yaliyopelekea mpaka kijana wa watu anasota gerezani.Namuonea wivu huyo Happy kwa kumpata kijana mwenye upendo wa dhati kama Patrick.Natamani kama angekuwa ni mpenzi wangu.Ningejitahidi kwa kadiri niwezavyo kuweza kumfanya mwenye furaha daima.I’m dreaming for a man like Patrick.Ana karibu kila kitu ninachokihitaji kwa mwanaume wa ndoto zangu.Lakini mhh!!!… Mbona naanza tena kuwaza mambo ya ajabu ajabu?Ni kwa nini siwezi kupitisha hata dakika moja sijamuwaza Patrick ? Mhh !! nahisi tayari ameanza kuingia moyoni mwangu taratibu.Ouh My God help me with these feelings.” Veronika akajikuta akiwa katika mawazo mazito “Ingekuwa ni mimi ndiye niliyepelekea Patrick akafungwa nisingekubali kabisa kwenda Ulaya na kumwacha akiteseka gerezani peke yake.Stupid girl Happy . Nitafanya kila niwezalo ili kuifanya sura ya Patrick iwe na tabasamu tena.Nitahakikisha anakuwa msafi,anakula vizuri na kupata raha zote.Mkuu wa gereza ni mjomba wangu.Nitamweleza ukweli ili aweze kunisaidia.Nitamuomba kila siku Patrick awe akipangiwa kufanya kazi kwa mkuu wa gereza ili aweze kupata nafasi ya kula vizuri na kupumzika." akawaza Veronika huku akiendelea kujigeuza geuza pale kitandani akijaribu kuutafuta usingizi.
Wakati Veronika akiwa katika wakati mgumu kwa mawazo usiku huo hali haikuwa nzuri sana kwa upande wa patrick .Mchana wa siku hiyo ulimkumbusha mbali sana.Ulimkumbusha kipindi alichokuwa katika mapenzi mazito na Happy . Alizikumbuka nyakati zile za furaha alizokuwa nazo .Alihisi kuihitaji furaha ile tena.Ghafla ikaja picha ya Veronika akiwa na sinia lenye chupa ya chai .Akakumbuka toka wakati akinywa chai ile na jinsi alivyokula chakula kitamu siku hiyo .“Mhh haya ni majaribu makubwa sana” Akawaza“Bado nampenda sana Happy lakini mbona Veronika naye anakuja kwa kasi sana katika mawazo yangu.Mhh ! hapana labda ni kwa ajili ya ule ukarimu wake.Tangu nimefungwa sijawahi kukutana na binadamu ambaye si mtu wangu wa karibu mwenye roho ya huruma na upendo kama Veronika.Veronika hatofautiani sana na Happy .Nahisi hii ni sababu inayonifanya niwe nikimuwaza sana kwa sababu kila nikimkumbuka Vero ananifanya nimkumbuke Happy " akawaza Patrick .
 
7
Urafiki kati ya Patrick na Veronika ulikua kwa kasi sana.Vero kwa kupitia mjomba wake ambaye ndiye aliyekuwa mkuu wa gereza alihakikisha kuwa patrick anapangiwa kufanya kazi mbali mbali nyumbani kwa mkuu wa gereza.Bila uoga Veronika akamueleza ukweli mjomba wake Joel armendo mkuu wa gereza hilo kuhusu urafiki wake na Patrick.Alimueleza kila kitu kuhusiana na hisia zake kwa kijana huyu.Mjomba wake alimwelewa na akaahidi kumsaidia Vero lakini Ili kujiridhisha na maelezo ya Veronika mara moja akaanza kufanya uchunguzi juu ya kijana huyu ambaye jarada lake linaonyesha kuwa alihukumiwa kifungo kutokana na kesi ya kuua bila kukusudia.Hakuridhika sana na maelezo yale.Hakutaka Veronika awe na mahusiano na kijana mwenye rekodi ya uhalifu.Siku moja akamwita Patrick ofisini kwake na kuanza kumuhoji mambo kadhaa ikiwa ni pamoja na kutaka kufahamu historia kamili ya Patrick.Hadithi ya Patrick ilimkuna sana Joel na kumfanya aridhike na kuoa kuna umuhimu wa kumsaidia Patrick katika maisha ya pale gerezani.Joel akajikuta akimpenda sana Patrick hasa kutokana na tabia yake nzuri na kujituma.Familia nzima ya Joel Armando ilitokea kumpenda Patrick na kadiri siku zilivyozidi kwenda taratibu wakaanza kumhesabu kama mmoja wa wanafamilia.Kila siku alipangiwa kufanya kazi nyumbani kwa mkuu wa gereza na kusaidia kazi mbali mbali mpaka muda wa kurudi gerezani ulipowadia.Hakuhitaji tena kusimamiwa .Alikuwa ni mfungwa ambaye alitokea kuaminiwa mno siyo tu na wakuu bali hata wafungwa wenzake na askari magereza wote. Urafiki na ukaribu baina ya Patrick na Veronika ukaongezeka maradufu.Veronika alifurahi mno kwa ukaribu ule kiasi kwamba hakuwa na hamu hata ya kurudi nyumbani kwao Dar es salaam..Mama yake akashangaa sana kwa binti yake kuchukua muda mrefu namna ile kurudi nyumbani wakati makubaliano yalikuwa atumie wiki mbili tu kwa mjomba wake lakini sasa ni wiki ya tatu hajarejea . Mama yake akaamua kumpigia simu kaka yake Joel ambaye ndiye mjomba wa Vero na kumwomba amwambie Vero arudi haraka sana Dare s salaam kwani shughuli nyingi zilikuwa zikimsubiri.Veronika alikuwa ndiye msimamizi mkuu wa miradi na shughuli zote za familia yao.Veronika alilia sana usiku huo kwa kuachana na Patrick kijana ambaye tayari alikwisha mzoea kwa kiasi kikubwa na urafiki mzito ulikwisha anza kujengeka baina yao.Alikuwa na matumaini makubwa ya kuwa urafiki ule ni lazima ungekuwa ni wa manufaa kwake..Siku iliyofuata alimweleza Patrick kuwa mama yake anamwitaji arudi Dar mara moja.Taarifa hii ilikuwa ni ya mstuko kwa Patrick pia kwa sababu tayari alikwisha mzoea sana Veronika.“Usihofu Patrick pamoja na kwamba ninaondoka lakini nitajitahidi walau kila mwisho wa mwezi niwe nakuja hapa kukutazama.Niambie kitu kimoja Patrick..”“kitu gani hicho Veronika ?” Patrick akauliza“Will u miss me ?! “Patrick akatabasamu ,akamshika mkono Vero na kusema.“ Very much.I’ll miss you very much Vero”Veronika akatoa tabasamu pana sana baada ya kusikia kauli ile.“Lakini usijali kama nilivyokwambia nitajitahidi kuja mara kwa mara kukuangalia.Isitoshe familia ya mjomba ipo nawe hivyo hutajisikia mkiwa hata kidogo na hapa kuna simu nitakuwa nakupigia kila siku tunaongea .Nadhani hutanimiss sana” akasema Veronika.“Vero usijali sana .Unajua toka siku ya kwanza tumeanza urafiki nilijua tu iko siku utaondoka.Tayari nilikuwa nimekwisha jiweka tayari kwa hilo.Usihofu chochote juu yangu,mimi nimekwisha zoea kuumia.Siyo siri Vero kuondoka kwako ni jeraha jingine kubwa katika moyo wangu.Umekuwa mtu wangu wa karibu sana na kunifanya nisahau mateso na mchungu yote ya gereza japo kwa muda mfupi...”Patrick akasema“Patrick najua una uchungu sana kwa mimi kuondoka.Hata mimi ninaumia vile vile kwa kukuacha peke yako hasa katika kipindi kama hiki ambacho ni wazi unahitaji sana mtu wa kukufariji na kukupa moyo.Lakini usijali nitarudi .”“Nimekuelewa Vero.Ila naomba unisaidie kitu kimoja”“Kitu gani hicho Patrick niambie niko tayari kukusaidia kitu chochote” akasema Vero“Kama unavyofahamu kuhusu kinachoendelea baina yangu na Happy .Nina imani Happy hajui kama nimehamishwa gereza na anaendelea kunitumia barua kwa kutumia anuani ya gereza la awali .Wazazi wangu pamoja na mkuu wa gereza nilikotoka ndio waliokuwa na kazi ya kuniunganisha na Happy lakini mpaka sasa hivi hawajaja kunitazama.Kwa hiyo sifahamu nini kinachoendelea.Ninachohitaji toka kwako ni msaada wako ili niweze tena kuwasiliana na Happy .Nitaandika barua na kumweleza Happy kila kitu na nitaomba ukanisaidie kuiposti kwa haraka.” Akasema Patrick.Akionyesha uso wa furaha Veronika akajibu“Usihofu Patrick .Nimekwisha kueleza toka awali kuwa nipo kwa ajili yako,hivyo usisite kunituma jambo lolote lile na nitakusaidia kwa uwezo wangu wote”Siku hiyo Patrick akaandika barua ndefu na kumfahamisha Happy juu ya uhamisho wake na kuzidi kumsisitiza juu ya ahadi zao walizowekeana..“Kazi kubwa bado ninayo” Aliwaza vero usiku kabla ya siku ya kuondoka kwake.“Ninampenda Patrick lakini bado inaonyesha mapenzi yake yako kwa Happy .Mapenzi yao ni ya dhati kabisa.Ni ndoto yangu ya siku nyingi ya kumpata kijana mwenye mapenzi ya kweli kama Patrick.Hata hivyo bado sikati tamaa.Happy yuko mbali na mimi niko karibu na Patrick nani alisema fimbo ya mbali inaua nyoka? Kwa kuwa ninampenda Patrick nitapambana .Kwanza ni lazima niuvuruge uhusiano huu wa Patrick na Happy baada ya hapo utazaliwa uhusiano mpya kati ya Patrick na veronica.” Akawaza Veronika na kwa hasira akaifungua barua ile aliyopewa na Patrick ili akaiposti kwenda kwa Happy akaanza kuisoma.alipomaliza akairudia tena na tena.Ilikuwa ni moja kati ya barua zenye msisimko wa hali ya juu.
“Siwezi kuituma barua hii.Maneno aliyoyaandika humu yanaweza kumfanya mgonjwa aliye mahututi kupona ghafla.Ni maneno yenye mahaba mazito.I deserve a guy like him.He must be mine.” Vero akasema mwenyewe kwa hasira huku akiichana katikati ile barua aliyopewa na patrick.
" Nitakuwa mjinga kama nitaituma barua hii iende kwa Happy na kuzidi kuliimarisha penzi la Patrick na Happy wakati hata mimi ninamtaka Patrick..Natakiwa niuvuruge kabisa uhusiano wao ili niweze kuipata nafasi ya kuwa na Patrick..Penzi lao ni zito na kuwatenganisha si kazi rahisi lakini I will have to do something.Lazima nifanye kila linalowezekana niwatenganishe Patrick na Happy..I'll do anything I mean anything to separate them..." akazidi kuwaza Veronika.
* * * *
Ni siku moja tu tangu Veronika aondoke ,Patrick akatembelewa na wazazi wake.Ilikuwa ni siku ya furaha kubwa mno kuwaona tena wazazi wake .Aliruka na kufurahi,alitamani kama Vero ngekuwepo ili awafahamu wazazi wake.Kitu kikubwa ambacho alikitarajia na kukisubiri kwa hamu ni iwapo kulikuwa na barua yoyote toka kwa Happy .Aliamini wazazi wake watakuwa wamekuja na barua kwa sababu kimepita kipindi kirefu sasa toka alipopokea barua ya happy kabla hajahamishwa gereza..Patrick hakupoteza muda akauliza iwapo wamekuja na barua yoyote toka kwa Happy .Baba yake akajibu kwa masikitiko“Patrick ninasikitika kuna mambo mengi yametokea hapa kati kati na hukuwa ukifahamu..Kwa ufupi tu ni kwamba nilipata uhamisho wa ghafla kwenda Dar es salaam na ndiko tunakoishi kwa sasa.Toka tumehama hatujapata mawasiliano yoyote toka kwa Happy .Tulitaarafiwa na mkuu wa gereza ulilokuwa awali kwamba umehamishiwahuku hivyo hatukupita tena katika gereza la Iringa.Kama atakuwa ametuma barua basi zitakuwa zimetua katika mikono ya watu wengine.Nasikitika vile vile kwa kutomfahamisha juu ya kuhama kwetu ili asiendelee kutumia anwani ile tuliyokuwa tukiitumia awali “.akasema baba yake PatrickPatrick akainama kwa sekunde kadhaa akitafakari.“Oh My God” Akajikuta akitamka kwa nguvu.Kukosa mawasiliano na Happy kulimtesa sana.
“Patrick mwanangu “Akasema mama yake baada ya kumuona mwanae amezama katika mawazo ghafla.“Nadhani ni wakati sasa wa kusahau yote yaliyopita na kuanza maisha mapya.Nakuomba jitahidi toka moyoni mwako uweze kumsahau Happy .Nakuomba umsahau na uuvunjilie mbali urafiki kati yako na huyo Happy .Bila Happy usingepatwa na matatizo haya mwanagu. ,Happy kakusababishia matatizo mpaka umefungwa gerezani lakini yuko wapi leo ? yuko Ulaya anasoma ! Wewe unasota gerezani,umepoteza masomo na mwelekeo mzima wa maisha .Angalia mateso unayoyapata mwanangu.Mimi na baba yako hatulali tunakuwaza wewe mwanetu.Kama ni kweli angekuwa anakupenda na kukuthamini basi asingekubali kwenda Ulaya na kukuacha peke yako hapa gerezani ukiteseka.Sisi wazazi wako tunasema hatutaki tena kuusikia urafiki kati yako na Happy .yaliyotokea yametokea tunashukuru. na tunamwachia Mungu lakini hatutaki tena kusikia wala kumwona Happy mtoto asiye na fadhila hata kidogo.’ Akasema mama yake Happy.Patrick akastuka sana.Akamtazama mama yake na kusema
“ Hapana mama kamwe sintathubutu kufanya kitu kama hicho maishani mwangu.Siwezi kumuacha Happy hata iweje.Nilipambana kwa ajili yake na kwa ajili ya kuulinda utu na heshima yake na yote hii ni kwa sababu nampenda.Nikumuacha leo haya yote niliyoyafanya kwa ajili ya upendo wangu kwake yatakuwa ni bureWazazi wangu siwezi hata kwa sekunde moja kumsahau au kuachana na Happy..”Akasema Patrick huku machozi yakimtoka. Baba yake akamuangalia na kusema“Patrick sisi ni wazazi wako na ndio wenye tamko la mwisho.Kauli yetu ni hii hatutaki kumsikia Happy masikioni mwetu.Narudia tena hatutaki kabisa kumsikia binti huyo wala kusikia eti una mahusiano naye..You and her its over...” Akasema baba yake kwa hasira kisha akatoka nje. Hili likawa ni jaribu lingine kwa Patrick la kutenganishwa na mtu aliyempenda kupita maelezo.Alikuwa njia panda je achague kuwa na Happy au wanavyotaka wazazi wake ? Mama yake akaendelea kumbembeleza mwanae ausikie ushauri wao ili amani iweze kudumu kwani ndugu wote walikuwa wamepitisha azimio hilo kuwa hawataki kuusikia urafiki wa Happy na Patrick.Patrick hakuwa na jibu la kutoa kuhusiana na amri ile ya wazazi wake ya kumtaka atengane na Happy.Wazazi wake wakaondoka na kumuacha Patrick akiwa katika mawazo mengi mno
* * * *


Veronika alifika nyumani kwao Dar na kulakiwa na mama yake.Ilikuwa ni furaha sana kwa mama huyu kumuona tena mwanae ampendaye.Wakiwa katika mlo wa jioni mama yake Vero akaanzisha mazungumzo.“ Vero hebu niambie kisa cha kukaa kwa mjomba wako siku zote hizi hali makubalianao yetu yalikuwa ni wiki mbili tu.Unafahamu fika kuwa hapa niko peke yangu sina mtu mwingine wa kunisaidia katika biashara Msaidizi wangu pekee ni wewe.”
Vero akatabasamu na kusema “mama samahani sana kwa kukaa siku zote hizi kwa mjomba na kukuacha peke yako.Sikuwa nimetarajia kufanya hivyo ila ilitokea dharura ikanibidi nikae.Nashukuru hata ulivyonipigia simu kwani bila hivyo nadhani ningeendelea kukaa zaidi.” Akasema Vero huku akicheka kichini chini“Dharura gani hizo we mtoto hebu niambie.” Akasema mama yake.Happy akala vijiko viwili vya chakula kisha akasema“mama wewe ni mzazi wangu lakini umekuwa ndiye mshauri wangu na zaidi ya yote umekuwa ni rafiki yangu wa karibu sana.Ni kutokana na juhudi zako wewe za kunifundisha maadili mema ndio maana leo hii nimekuwa ni binti mwenye mafanikio na kukuletea heshima kubwa.Katika mambo ambayo umekuwa ukiniusia kila siku na kunionya ni kujikita katika mahusiano ya kimapenzi.Nimekuwa nikilifuatilia hilo na ndio maana mpaka umri huu najivunia usichana wangu.Kweli mama simjui mwanaume mpaka leo hii.Lakini mama mapenzi ni kitu ambacho hakikwepeki.Mapenzi yapo na kila mtu kwa wakati wake anajikuta yu mapenzini kama nilivyojikuta mimi.”Alisita kidogo baada ya kumuona mama yake akimtazama kwa macho yenye udadisi .“Mama nikiwa kule kwa mjomba Songea nilifanikiwa kukutana na mwanaume ambaye ninaamini ndiye mwanaume wa ndoto zangu.”Akatulia tena na kuyaacha yale aliyoyasema yazame kabisa kwa mama yake.Kisha akamsimulia kisa kizima,jinsi alivyokutana na Patrick na hadithi nzima ya maisha ya Patrick .Mambo yalikuwa tofauti na jinsi Veronika alivyowaza.Yeye alitegemea labda mama yake angemgombeza na kumkanya juu ya jambo lile lakini ikawa tofauti.“Vero mwanangu nimefurahi sana kwa kuwa wazi na hisia zako.Ni wazi mapenzi hayakwepeki.Yapo na kila mtu anapenda.Mimi nafurahi kusikia kuwa kijana huyo unampenda kwa dhati.Anaonekana ni kijana mtaratibu sana na mwenye mapenzi ya kweli.Mimi nakuunga mkono na niko tayari kukusaidia kwa lolote lile ili uweze kufanikiwa kumpata kijana huyo umtakaye.Kwani lengo langu ni wewe uishi maisha ya furaha na si karaha.” Waliongea mambo mengi kisha wakaagana na kila mmoja akaenda zake kulala.Hakuweza kupata usingizi usiku huo.alikuwa na furaha kubwa sana baada ya mama yake kukubali kubariki harakati zake za kumpata Patrick.“Sasa kinachofuata ni kuharibu kabisa kila kitu baina ya Happy na Patrick.” Akasema kimoyomoyo halafu akachukua kalamu na karatasi akakaa mezani na kuanza kuandika barua ambayo alipanga aitume kwa Happy .
Kwako dada Happy Ni matumaini yangu kuwa unaendelea vizuri na masomo huko uliko.Naomba kabla yote nijitambulishe kuwa mimi ni jirani wa akina Patrick hapa Sumbawanga.Tumeishi vizuri na familia yao na baadaye nikahamia mkoani Mbeya.Kwa jina naitwa Grace.Nilisikia matatizo yaliyomkumba Patrick.Nikasikitika sana.Si lengo langu kusema haya yote lakini dhumuni kuu la barua hii ni kukufahamisha kuwa Patrick mpenzio Amefariki dunia kwa ugonjwa wa kuhara akiwa gerezani.Kaka yake ndiye aliyenipa anwani yako na kunitaka niwasiliane nawe na kukufahamisha juu ya kifo hicho.Anadai kuwa hawawezi kukufahamisha kwa sababu familia yao haitaki kukusikia kabisa hasa baada ya kumsababishia matatizo mtoto wao na kumwacha akiteseka gerezani hali wewe ukipata maisha mazuri i na kuendelea na masomo yako huko Marekani.Pole sana dada ,haya ndiyo mambo ya dunia.Ulimpenda sana Patrick lakini Mungu kampenda zaidi.Jipe moyo na utampata kijana mwingine kama PatrickPole sanaGrace
Vero Aliipitia tena na tena barua ile na kuhakikisha iko safi na siku iliyofuata akadamka na kwenda kuiposti.

* * * *

Akiwa katika mawazpo mengi akimuwaza mpenzi wake Patrick na maisha anayoyaishi gerezani mara mlango waq chumba chake ukagongwa .Kwa uvivu Happy akainuka na kwenda kuufungua .Alikuwa ni mtumishi wa chuo aliyekuwa na bahasha mkononi.Akamkabidhi Happy barua ile kisha akaondoka. Happy aliitazama barua ile kwa wasi wasi .Alitazama muhuri ulikuwa wa Tanzania.Mwandiko juu ya bahasha hakuufahamu ulikuwa ni wa nani.Kwa muda wa miezi miwili sasa amekuwa akiandika barua mfululizo kwa Patrick kupitia wazazi wake bila kupata majibu.Hii ilimpa wasiwasi mkubwa .aliumia sana kila alipofikiria Patrick atakuwa katika hali gani.aliujutia uamuzi wake wa kwenda Marekani na kumwacha Patrick peke yake.Alijiuliza maswali mengi juu ya ukimya huo uliotokea ghafla. Taratibu akakaa kitandani na kuifungua barua ile na kuanza kuisoma kwa makini.Kabla hajamaliza akapiga ukelele mkubwa sana,akaanguka chini na kupoteza fahamu.Ukelele ule ulikuwa mkubwa kiasi cha kuwastua wenzake waliokuwa katika vyumba vya jirani.Watu walifika hapo chumbani na kumkuta Happy amezimia.haraka haraka wakamchukua na kumkimbiza katika hospitali ya hapo chuoni kwa ajili ya huduma ya kwanza.Hakuna aliyeweza kufahamu mara moja sababu ya Happy kupiga ukelele ule na kupoteza fahamu.Saa saba za usiku Happy akazinduka na kujikuta akiwa hospitali.Michelle pamoja na wanafunzi wengine walikuwa pembeni ya kitanda.Alifumbua macho akatazama pande zote kisha akalala tena.Baada ya kama nusu saa akaamka tena na kukaa kitandani.Daktari akafika ,akampima na kumwomba aendelee kupumzika.Alijilaza kitandani na kuanza kukumbuka mambo yaliyotokea .Alikumbuka barua ile aliyotumiwa na kuanza kulia.Michelle ambaye kwa sasa ni rafiki mkubwa wa Happy alifanya kazi ya ziada kumbembeleza
“ Nyamaza kulia Happy..tafadhali usilie tena..” akasema Michelle“siwezi kunyamaza Michelle,kilio hiki hakiishi leo,ni kilio cha milele.Nimempoteza mtu muhimu sana maishani mwangu.”akasema Happy kisha akaendelea kulia.“ Umempoteza nani,baba,mama au ndugu? Akauliza Michelle“Michelle its Patrick.Patrick is dead”“Whaat? Michelle naye akastuka.Aliufahamu uhusiano wa Patrick na Happy kwani kila siku Happy alikuwa akimuhadithia namna anavyompenda Patrick” Yes Patrick is dead” Happy akazimia tena.Baada ya muda akazinduka.Safari hii aliweza kutazama lakini hakuweza kuongea .Alijaribu kufungua mdomo lakini maneno hayatoki.Ni machozi tu ndiyo yaliyokuwa yakitiririka..Iliubidi uongozi wa chuo kuwataarifu wazazi wake juu ya ugonjwa wa mtoto wao na kwa haraka ikawalazimu waende kumtazama.Ilikuwa ni siku ya sita tangu amelazwa hospitalini hapo wazazi wake walipowasili.Aliwaeleza kilichotokea wote wakastuka sana.Hawakuwa na taarifa kwamba Patrick amefariki kwa sababu toka Happy alipoondoka na kwenda Marekani kusoma hawakuwahi kumtembelea tena Patrick gerezani kwa hiyo hawakuwa na taarifa zozote juu yake.Wazazi wake wakajitahidi kwa kila namna walivyoweza kujaribu kumliwaza binti yao ili aweze kurejea katika maishaya kawaida kwani alionekana kukata kabisa tamaa ya maisha.


* * * *


Wiki ya kwanza ikakatika bila ya Veronika kutokea.Patrick akaanza kupatwa na wasiwasi kwani Vero alimuahidi kuwa atakuwa akimtembelea karibu kila wiki.Alikuwa na hamu sana ya kutaka kupata walau ujumbe wowote toka kwa Happy kwani Vero aliahidi kufanya kila analoweza ili kurejesha mawasiliano kati yake na .Patrick alijipa moyo na kuendelea kusubiri.Wiki ya pili ikakatika hatimaye ya tatu na ya nne Vero akarudi Songea kwenda kumjulia hali Patrick. Patrick alifurahi mno kumuona tena Vero.Vero naye alifurahi sana kumuona Patrick kijana ambaye amekuwa akimkosesha usingizi.Bila ya kupoteza muda Patrick akataka kufahamu kama kuna habari yoyote kutoka kwa Happy .Veronika akamwangalia kwa sekunde kadhaa akakohoa kidogo kisha akasema“Patrick nimekuja na habari Fulani ambazo si nzuri “Patrick akastuka na kuuliza.“habari gani hiyo Vero”Vero akatulia kidogo kisha akaendelea“Patrick nimechelewa kuja kukuona kama nilivyokuwa nimekuahidi lakini kilichonichelewesha ni suala hili hili la Happy .”“Happy ? Kafanya nini tena? Patrick akauliza kwa hamaki“Patrick you are strong I know but you need to be more stronger to hear this” Vero akasema“Vero sikuelewi .Mbona unanichanganya?Go straight to the point” akasema PatrickVero akajiweka sawa akakaza sura ili asije onekana anadanganya“Patrick ! Nilipiga simu chuoni kwa Happy kama tulivyokuwa tumekubaliana na nikaambiwa kuwa Happy alikuwa amehama chuoni hapo muda mrefu.Sikuchoka nikaomba nielekezwe alihamia chuo gani nikasaidiwa nikakipata chuo alichokuwa anasoma nikapiga simu na kweli nikampata lakini nilipojitambulisha tu kuwa nina ujumbe muhimu toka kwa Patrick akakata simu.Nilistuka sana lakini sikukata tamaa.Kwa muda wa siku mbili mfululizo nikawa napiga simu lakini haipokelewi.basi nikaamua kumtumia binamu yangu mmoja ambaye naye anasoma huko huko lakini chuo kingine tofauti na hiki cha Happy .Yeye akafanya uchunguzi wake na baada ya siku kama tano hivi akaniambia kuwa amefanikiwa kumfahamu Happy lakini kwa bahati mbaya Happy amepata bwana ambaye anaishi naye na inavyosemekana tayari ana ujauzito wa mzungu huyo.Niliumia mno nikapiga tena simu kwa hasira nikaongea naye bila aibu akanijibu hivi “ sitaki kusikia habari yoyote juu ya Patrick .Kama ni gerezani alitaka kwenda mwenyewe.mwacheni akae atatoka atatafuta maisha yake.Mimi nina mtu wangu kwa sasa na sitaki usumbufu hata kidogo na wala huko Tanzania sitegemei kurudi tena ..Halafu akakata simu.Nikaj………………..” Hakumalizia sentensi yake Patrick akaanguka chini na kupoteza fahamu.Vero akapiga kelele kuomba msaada na mara wakaja askari magereza na kumbeba Patrick na kumkimbiza katika zahanati ya hapo gerezani kwa ajili ya kumpatia huduma ya kwanza.Veronika akachanganyikiwa na kijasho kikamtoka.Alijilaumu sana moyoni kwa kutunga uongo ule mkubwa kiasi cha kuhatarisha maisha ya wawili hawa waliopendana.Hakutegemea kama hali ingekuwa vile


* * * *



Hatimaye miezi ikatika bila ya mawasiliano yoyote baina ya Patrick na Happy .Wakati Happy akiamini kuwa Patrick ni marehemu ,Patrick kwa upande wake yeye alikuwa bado ana hasira moyoni kwa kusalitiwa na Happy .Alijiona mjinga sana kwa kuyatoa maisha yake kwa mtu asiyekuwa na thamani kwake hata chembe.Alilia usiku na mchana kwa kitendo hiki cha Happy .Happy yeye alikuwa akimlilia Patrick kila siku.Kila alipoiona picha yake machozi hayakukauka. Taratibu kila mmoja kwa upande wake akaanza kukubaliana na matokeo kuwa hayakuwa mapenzi ya Mungu wao kuwa pamoja.Kila mmoja akamweka mwenzie kama kumbukumbu ya pekee maishani.Pamoja na kukubali huko kuwa Patrick alikuwa amekufa lakini Happy alikuwa na dhamira moyoni ya kuja kulitafuta kaburi la Patrick na kutoa heshima zake kwa mtu pekee aliyempenda na kumthamini.Wakati Happy akiwa na wazo la kuja kutembelea kaburi la Patrick pindi atakaporejea nyumbani Patrick yeye aliamua kumsamehe kwa maamuzi aliyoyafanya na kuamua kusonga mbele na maisha yake.Ingawa ni kitu ambacho kilimuumiza akili kila siku lakini alijitahidi aweze kumsahanu Happy na kuanza maisha yake mapya bila ya kiumbe huyu aliyempenda zaidi . Ni katika wakati huu mgumu aliokuwa nao Patrick ndipo Veronika alipozidisha ukaribu wake kwa Patrick.Patrick kwa kiasi Fulani alishukuru sana kwa kufahamiana na Vero kwani yeye ndiye mfariji mkuu wake mkuu katika kipindi hiki kigumu alichokuwa nacho.Ni vero pekee ambaye anaonyesha kumuelewa na kumjali.Ukaribu wao ukaongezeka mara dufu na tayari kukaanza kuwa na kila dalili za kuibuka kwa uhusiano mzito baina yao.“Vero ni msichana mrembo ,ambaye ni wazi anaonyesha ana mapenzi ya kweli.Vero amekuwa ndiye mtu wangu wa karibu.Ni yeye tu ambaye anaonyesha kunielewa na kunisaidia.Ni kwa sababu ya Vero leo hii maisha yangu hapa gerezani yamekuwa mazuri kwani ninaishi kama niko nyumbani.Mjomba wake Vero mkuu wa gereza ananijali mno na kunithamini.Yote hii ni kwa sababu ya Vero.Amenifanya nisijione mkiwa tena,ameniondolea lindi la mawazo mazito niliyokuwa nayo juu ya Happy .Vero amenisaidia kurudisha tena matumaini ya ndoto zangu ambazo tayari zilikuwa zimeanza kufutika,kwa haya yote aliyoyafanya Kwa nini basi nisimpe nafasi aliyokuwa nayo Happy ? Nilitambua toka awali kuwa Vero ananipenda lakini ikawa vigumu kuipata nafasi ndani ya moyo wangu kwa sababu wakati huo funguo ya moyo wangu alikuwa nayo Happy .Ninakubaliana na hisia zangu kuwa Vero ndiye msichana pekee ambaye anaweza kuliziba pengo la Happy “
.Patrick akawaza kwa kina sana juu ya suala hilo na akadhamiria kumtamkia wazi wazi Vero juu ya adhma yake ya kutaka wawe wapenzi.

* * * *
Ingawa alihuzunika sana kwa kusikia kuwa Patrick mpenzi wa Happy amefariki dunia kwa upande mwingine Mike Cambell alikuwa na furaha isiyo kifani kwani aliamini kuwa sasa ni nafasi yake ya pekee ya kuwa na Happy.Aliamini kuwa kwa sasa Happy hatakuwa tena na kisingizio cha kumkataa .Alihama toka New york city hadi Washington DC ambako Happy alikuwa akisoma.Lengo likiwa ni kujaribu kujenga ukaribu kati yake na Happy . Taratibu akaanza kujenga mazoea na kuwa karibu na Happy na kumfariji kwa kumnunulia maua n.k.Yeye na dada yake Michelle wakajitahidi kwa kadiri walivyoweza katika kumfariji na kumuondolea Happy majonzi yasiyokwisha.Walitoka kila mwisho wa wiki na kwenda sehemu mbali mbali za kuvutia na burudani lengo likiwa ni kujaribu kumsahaulisha juu ya msiba wa Patrick.Baada ya miezi minne kupita tayari Happy alikwisha anza kurudia hali yake ya kawaida.Tayari ukaribu mkubwa ulikwisha jengeka kati yake na Mike kiasi kwamba hakusikia raha kupitisha siku bila kumuona kijana huyu ambaye ametokea kuwa mfariji wake mkubwa hasa katika kipindi hiki cha msiba mkubwa uliompata. Pamoja na ukaribu huo uliojengeka baina yao bado ilikuwa ngumu kwa Happy kuitoa nafasi ya Patrick kwa mtu mwingine.Kwa mapenzi mazito aliyokuwa nayo kwa Patrick alikuwa radhi aishi peke yake kwa heshima ya kijana huyu.Suala hili liliendelea kumuumiza kichwa Mike kwa muda mrefu lakini hakukata tamaa.Alizidi kuonyesha mapenzi ya wazi na nia dhahiri ya kutaka kuwa na Happy . Siku moja wakiwa katika klabu ya usiku Mike akaamua tena kumkumbushia Happy juu ya ombi lake la kutaka wawe wapenzi.
“Happy naomba kwanza nitangulize samahani kwa jambo ninalotaka kukueleza kwa sababu najua unaweza usilipende.” Akanyamaza kidogo huku Happy akimtazama kwa macho maangavu.
“Najua bado uko katika kipindi kigumu cha kufiwa na mpenzi wako.Kusema kweli ni kipindi kigumu kwetu sote kwa sababu wewe ni rafiki yetu wa karibu na hivyo huzuni yako ni yetu pia.Pamoja na yote yaliyotokea ambayo ni kazi ya Mungu,lakini maisha hayana budi kuendelea.Ninachokusihi ni kuyasahau yote yaliyotokea na kuanza maisha mapya” Akanyamaza akamtazama Happy usoni halafu akaendelea.
“Happy nimeona nikueleze tena kile nilichokueleza muda mrefu uliopita.Happy napenda kwa mara nyingine tena kukuhakikishia kuwa wewe ni mwanamke pekee ambaye umeweza kutua katika moyo wangu na kukataa kutoka kama vile nyuki anavyong’ang’ania ua lenye asali tamu..Toka mara ya kwanza nilipokutia machoni sura yako imejichora moyoni mwangu kiasi ambacho haitaweza kufutika kamwe.Happy nakupenda kupita ninavyojipenda mwenyewe.Naomba kwa mara nyingine tena unipe nafasi ndani ya moyo wako ya kuwa nawe.Ninaomba unipatie nafasi ya Patrick .Wewe ni mwanamke mrembo ambaye unahitaji mtu mwenye mapenzi ya dhati na ya kweli kama alivyokuwa Patrick.Siwezi kuwa kama Patrick lakini ninakuhakikishia kuwa upendo wangu kwako ni wa kweli na wa dhati .Niko tayari kufanya lolote lile katika dunia hii ilimradi tu niwe na wewe.Tafadhali Happy naomba unielewe ninaposema kuwa moyo wangu unateketea kwa penzi lako.Naomba unipe nafasi ndani ya moyo wako “
Mike akasema na kumtazama Happy ambaye alikuwa amenyamaza huku machozi yakimtoka kwa mbali.Akatoa kitambaa katika pochi yake akajifuta uso halafu akakaa vizuri na kusema
“Mike kwanza napenda kuchukua nafasi hii kukushukuru wewe na Michelle kwa kuwa watu wangu wa karibu.Sio siri mmenisaidia sana na hasa katika kipindi hiki kigumu nilichokuwa nacho.Bila uwepo wenu sijui ningekuwa katika hali gani.Mmekuwa na mimi katika kila hali,kila dakika.Mmefanya kila mliloweza kunifariji na mpaka leo hii ninaendelea vizuri.Sioni kitu cha kuwalipa zaidi ya maneno haya machache Ahsanteni sana.Kuhusu suala ulilonieleza ,naomba unipe muda wa kutosha wa kutafakari na kufanya maamuzi.Nitakapokuwa tayari nitakujibu”akasema Happy na Mike akamuelewa na hakutaka tena kuendelea kulionglea suala hilo.


BAADA YA MIAKA MITANO
Hatimaye siku iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu ikawadia.Ni siku ambayo Patrick alihitimisha adhabu yake ya kutumikia miaka mitano gerezani.Tangu asubuhi ya siku hiyo Patrick alikuwa ni mtu mwenye furaha sana.Aliwaaga wafungwa wenzake wote huku akiwa mwingi wa tabasamu.Wakati Patrick akiwa mwingi wa furaha kwa upande mwingine ilikuwa ni simanzi gerezani kwa kuondokewa na kijana kama huyu ambaye alipendwa karibu na kila mtu.Alikuwa mstari wa mbele katika kuwapa moyo na kuwafariji wale wenzake waliokata tamaa,vile vile alikuwa ni kiungo kikubwa katika kuwasaidia wenzake kupata vitu kama sigara,sabuni n.k kwa sababu yeye muda mwingi alikuwa akishinda nyumbani kwa mkuu wa gereza hivyo kuvipata vitu hivyo kwake ilikuwa rahisi..Kuondoka kwake lilikuwa ni pigo kubwa kwa wale wafungwa waliokuwa wakimtegemea .
Saa tatu na nusu juu ya alama Patrick aliitwa katika ofisi ya mkuu wa gereza ambako alitaarifiwa rasmi kuwa kuanzia muda huo alikuwa huru.Aliombwa awe raia mwema huko aendako ili asije rudishwa tena gerezani.Hii ilikuwa ni kama ndoto.Hakuamini hadi pale mkuu wa gereza alipompa mkono na kumwambia kuwa yuko huru na kumtakia kila la heri katika maisha yake . Katika lango la kuingilia gerezani kundi kubwa la watu likongozwa na wazazi wa Patrick lilikuwa likimsubiria kwa hamu kubwa.Walikuwepo ndugu na baadhi ya rafiki zake akiwemo rafiki yake Andrew ambaye walikutana hapo hapo gerezani lakini yeye aliwahi kutoka.Alikuwepo pia binti mrembo ambaye urembo wake leo hii ulizidi mara dufu.Alikuwa amependeza zaidi ya maelezo.Huyu ni Veronika ambaye yeye pamoja na ndugu zake na mama yake waliungana na familia ya akina Patrick katika kusherehekea tukio hili kubwa .Tayari Patrick na Vero walikwisha kuwa wapenzi na urafiki wao ulikuwa na baraka ya pande zote mbili yaani upande wa akina Patrick hali kadhalika mama na ndugu zake Veronika hawakuwa na kipingamizi chochote juu ya urafiki huu.Taratibu lango likafunguliwa na Patrick akaruhusiwa kutoka nje akiwa huru.Alitumia sekunde kadhaa kulitazama gereza hilo ambalo amekaa takribani miaka mitatu.Huku akitiririkwa na machozi mama yake alikuwa mtu wa kwanza kumkumbatia mwanae,kisha wakafuata wengine wote waliokuwapo hapo .Zilikuwa ni dakika chache zenye furaha kubwa .Wote wakapanda katika magari yaliyoandaliwa na kuanza safari ya kuelekea Dar .Patrick alipanda katika gari maalum lililokuwa likiendeshwa na Andrew rafikiye mkuu pamoja na mfariji wake na hatimaye mpenzi wake ,Veronika.ambaye kwa sasa alikuwa ni kila kitu kwake . Ndani ya gari Patrick na Vero walikuwa wamekumbatiana wote wawili machozi yakiwatoka.Patrick alikumbuka toka alivyoonana na Vero siku ya kwanza,wakazoeana na kuwa marafiki na hatimaye kwa sasa ni wapenzi.Alimshukuru sana Mungu kwa kumrudishia furaha iliyokuwa imepotea baada ya kumpoteza Happy .Mwanzoni aliamini kuwa Happy ndiye ilikuwa furaha yake lakini baada ya Happy kuondoka akatokea Vero na kuirudisha tena furaha hiyo.Veronika alionyesha mapenzi ya kweli na uvumilivu mkubwa katika kipindi chote walichofahamiana mpaka leo.“Veronika nashukuru sana kwa yote uliyonifanyia.Nashukuru kwa upendo wa ajabu ulionionyesha”Akasema Patrick kwa kunong’ona.“ahsante pia Patrick kwa kuufungua moyo wako na kunikubali .Najiona ni mwenye bahati sana kuwa na mtu kama wewe.” Akasema Veronika.
* * * *
Hatimaye Happy naye baada ya kumaliza masomo yake akarejea nyumbani Tanzania.Toka akiwa safarini alikuwa na shauku moja tu ya kutaka kufahamu mahala alipozikwa Patrick .Tayari alikwisha kuwa na mahusiano ya kimapenzi na Mike cambell.Alikubali kumpa nafasi Mike baada ya kuamini kwamba Patrick hatarejea tena. Familia yake yote ilikuwepo uwanja wa ndege kumlaki.Tayari baba yake alikwisha staafu kazi na sasa familia yote inaishi jijini Dar es salaam.Happy alipata mapokezi makubwa sana toka kwa familia yake. Siku tatu tu baada ya kuwasili nchini Happy akafunga safari hadi mjini Sumbawanga ambako ndiko Patrick alikuwa akiishi mwanzo.Kule alitaarifiwa kuwa familia ya akina Patrick ilikwisha hama muda mrefu na walihamia jijini Dar es salaam. Hakukata tamaa akaondoka na kuelekea Iringa katika gereza ambalo Patrick alikuwa amefungwa mwanzo.Lengo lilikuwa ni kupata ukweli juu ya kifo cha Patrick.Pale gerezani alitaarifiwa kuwa Patrick alihamishwa na kupelekwa katika gereza jipya huko Songea.Pale gerezani hawakuwa na kumbukumbu naye zozote.Happy hakukata tamaa akafunga safari tena hadi Songea katika gereza jipya ambako ndiko Patrick alihamishiwa.Pale akaonana na mkuu wa gereza na kumweleza kilichompeleka.Mzee Joel ambaye ni mjomba wa Veronika akamwangalia kwa mstuko .“wewe ndiye Happy kibaho? Akauliza baada ya kuikumbuka historia ya Patrick“Ndiye mimi mzee “Happy akajibuMzee Joel akamtazama kwa makini na kuuliza “Happy nimefurahi kukuona.Niliwahi kusikia habari zako toka kwa Patrick.Nimeshangaa kwa wewe kuja kumuulizia Patrick hapa gerezani ina maana hamkuwa mkiwasiliana wakati ukiwa masomoni?“Tulikuwa tukiwasiliana lakini mawasiliano yakakata ghafla sana na siku moja nikapokea taarifa kuwa Patrick alifariki kwa ugonjwa wa kuhara akiwa gerezani.Baada ya kurejea nyumbani nimeona nitafute kwanza taarifa sahihi za kifo chake na nifahamu mahala alikozikwa.Nimeelekezwa kwamba alihamishiwa katika gereza hili”Mkuu wa gereza akstuka sana alipopata taarifa ile inayohusiana na kifo cha Patrick .Kwa kiasi fulani taarfa ile ikamchanganya kwa sababu kwa mujibu wa taarifa aliyoipata toka kwa Vero ni kwamba Happy akiwa masomoni nchini Marekani alipata bwana mwingine na kuolewa naye na kumsahau Patrick kitu kilichopelekea Patrick ampe nafasi Veronika.
Mzee Joel akakaa kimya akitafakari kisha akasema“Happy kwanza nakupa pole sana kwa yote yaliyotokea kati yako na Patrick.Ni kweli Patrick alihamishiwa katika gereza hili akitokea Iringa.Patrick alikuwa ni mmoja kati ya wafungwa bora kabisa ambaye hajawahi kutokea katika gereza hili.Alipendwa na kila mtu hapa gerezani.Alikaa hapa gerezani hadi alipomaliza kifungo chake na kuachiwa huru.Hapa gerezani alitoka salama salimini .Kama ni kufariki basi atakuwa amefariki baada ya kutoka hapa kwa sababu mimi ndiye niliyeidhinisha kuachiwa huru baada ya kumaliza kifungo chake.”Maneno yale yakamfanya Happy atetemeke mwili .Aliinama chini akashindwa kuyazuia machozi kumtoka.Hakuyaamini maneno yale ikambidi aulize tena.
‘Mzee sijakuelewa vizuri.Umesema nini?
“Nimesema kuwa Patrick alimaliza kuitumikia adhabu yake akiwa mzima wa afya na mimi kama mkuu wa gereza hili ndiye niliyemuachia huru baada ya kumaliza kifungo chake.Kama ni kufariki basi alifariki baada ya kutoka hapa gerezani.Nasikitika sana kwa kumpoteza kijana kama yule.” Akasema mkuu wa gereza.
“mzee mbona taarifa niliyoipata mimi inasema kwamba Patrick alifariki akiwa gerezani? Tena inasema kuwa alifariki kwa maradhi ya kuhara? Happy akasema huku machozi yakimdondoka
“Taarifa hiyo ulipewa na nani? Mkuu wa gereza akauliza
“Taarifa hiyo nilitumiwa na mtu nisiyemfahamu akidai kuwa yeye anamfahamu Patrick kwa sababu aliishi jirani na wazazi wake kule Sumbawanga.Dada huyo alisema kwamba familia ya Patrick haikuweza kunifahamisha juu ya msiba wa mtoto wao kwa madai kwamba nilimtelekeza mtoto wao gerezani nikaenda kusoma ulaya,wakati yalikuwa ni makubaliano yetu mimi na yeye.Sikutaka kumwacha Patrick peke yake na mimi nikaenda kusoma Marekani,lakini ni Patrick huyo huyo ndiye aliyenishawishi nikubaliane na uamuzi wa baba wa kunipeleka Marekani kusoma.”akasema Happy
“Pole sana Happy.Jipe moyo.Haya ni mambo ya kawaida Jitahidi sana uyaruhusu maisha yako yaendelee.”Mkuu wa gereza akasema“Nashukuru sana mzee kwa msaada ulionipa.Japokuwa bado kuna utata mkubwa juu ya kifo hicho lakini namuachia Mungu.Kama amekufa kweli nitamuombea kwa Mungu apumzike kwa amani lakini kama hajafa kweli huko aliko atambue kuwa maumivu anayonisababishia ni makubwa kiasi ambacho siwezi kuelezea.” Happy akaagana na mkuu wa gereza ,akapanda gari lake na kuondoka huku machozi yakiendelea kumtoka.Akashindwa kuendesha gari akaegesha pembeni akainamia usukani.
“ Nina kila sababu ya kuamini kuwa Patrick hajafa.Kutokana na maelezo ya mkuu wa gereza ni kwamba Patrick alimaliza kifungo chake na kutoka gerezani salama.Na katika ile barua niliyoandikiwa ilisema kwamba Patrick alifariki akiwa gerezani.Mbona mambo haya yananichanganya? Je Patrick alinifanyia hila nijue kuwa amekufa? Kama ni kweli hajafa kwa nini basi amenifanyia hivi??”Happy akajiuliza huku akiupiga usukani kwa hasira. .“Nilimkosea nini Patrick hadi akaamua kunidanganya na kuniacha niteseke miaka yote hii?Moyo wangu hauna furaha hata kidogo yote hii ni kwa ajili yake .Au labda kitendo cha mimi kuondoka kwenda kusoma Marekani hakikumfurahisha?Anyway nitakutafuta Patrick hata kama itanigharimu maisha yangu I promise I’ll find you because you left me at the time I needed you most “ .

* * * *

Miaka sita sasa imekwisha pita toka Patrick atoke gerezani na tayari amekwisha maliza shahada yake ya kwanza ya uandishi wa habari na tayari ni mwajiriwa katika kituo kimoja kikubwa cha Televisheni nchini kama mhariri wa vipindi.Pamoja na kwamba ni muda mrefu umepita lakini picha ya Happy bado haijafutika kabisa moyoni mwake.
Uhusiano kati yake na Vero tayari umekubaliwa na ndugu wa pande zote mbili na hatimaye ukafikia hatua ya uchumba .Aliamua kumvisha pete ya uchumba Vero baada ya kuamini kuwa Happy hakuwa na nafasi tena katika maisha yake.Aliamini Vero ndiye mwanamke pekee aliyepewa na Mungu ili awe mke wake.Vero ndiye aliyekuwa naye katika kipindi kirefu cha mahangaiko,Vero amemsaidia kufuta majeraha ya moyo na kuanza maisha mapya,Vero amekuwa ni kila kitu kwake. Kwa upande mwingine baada ya Happy kugundua kuwa Patrick hakufa gerezani na kuamini kuwa bado yu hai alikumbana na shinikizo kubwa toka kwa familia yake wakimtaka amsahau kabisa kijana huyu na kuolewa na Mike cambell ,kijana mmarekani mweusi ambaye mapenzi yake kwa Happy hayana kifani.Mike amekuwa ndiye mfariji mkubwa wa Happy toka alipopata taarifa kuwa Patrick amefariki dunia.Ni yeye na dada yake Michelle ndio walioweza kumfuta Happy machozi aliyokuwa akilia kila uchao akimlilia Patrick.Ni Mike ndiye aliyejitolea kila alivyoweza kuhakikisha binti huyu mwenye uzuri uliotukuka anarejea katika maisha ya kawaida.Pamoja na ugumu uliokuwepo wa Happy kumsahau Patrick lakini Mike alivumilia na kuamini kuwa iko siku Happy atamsahau Patrick na yeye kupewa nafasi ndani ya moyo wa binti huyu mwenye sura ya kimalaika..Hatimaye baada ya kujishauri kwa muda mrefu akaamua akakubali kuvishwa pete ya uchumba na Mike Cambell katika sherehe kubwa iliyohudhuriwa na umati wa watu.Pamoja na kuamini kuwa Patrick hakuwa ridhiki yake,kitu kilichompelekea akubali kuvishwa pete ya uchumba na Mike lakini bado Happy alikuwa na kitu moyoni juu ya Patrick.Kuna kitu ambacho hakuweza kukifuta moyoni mwake kilizidi kumtesa siku hadi siku.Penzi lake kwa patrick lilizidi kumtesa.

* * *
 
8

Veronika akamtazama Patrick kwa macho makali na tayari akagundua kuna kitu kinachomsumbua mpenzi wake.Kilichomuumiza roho zaidi ni kwa nini kama Patrick ana tatizo asimwambie?Akapanda kitandani na kukaa karibu ya Patrick akamkumbatia .“Patrick mpenzi kwa siku za karibuni nimegundua mabadiliko Fulani kwako.Hauko kawaida.Kuna jambo gani linalokusumbua hebu niambie mpenzi wangu.Unajua ninapokuona katika hali hiyo hata mimi ninapata wasiwasi mwingi.Nimezoea kuiona sura yako iliyojaa tabasamu kila wakati lakini kwa sasa unajilazimisha kutabasamu na unaonekana u mwingi wa mawazo.Au kuna kitu nimekuudhi Patrick? Veronika aliongea maneno haya taratibu machozi yakimlenga hali kichwa chake amekilaza kifuani kwa Patrick“Vero mpenzi hakuna jambo lolote linalonisumbua.Nahisi ni hizi dawa ninazotumia ndiyo zinanifanya niwe katika hali hii .Usijali si muda mrefu nitarudia hali yangu ya kawaida.”Akasema Patrick huku akimsugua Veronika mgongoni.“Patrick mimi ni mchumba wako na nimekuwa karibu nawe kwa muda mrefu sasa.Sidhani kama kuna mtu mwingine anayekufahamu kiundani zaidi yangu.Nina imani kabisa kuna kitu kinakusumbua akili yako .Nina jua kabisa ni wakati gani unakuwa na furaha na ni wakati gani unakuwa na matatizo.lakini sikulazimishi kuniambia.Kama unaona tatizo hilo halina ulazima wa mimi kulijua basi hakuna neno.Ila kumbuka muda wowote utakapohitaji msaada wangu nipo tayari kukusaidia.”Vero akambusu Patrick kisha akatoka nje.
* * * *

Saa saba za usiku Patrick akastuka toka usingizini .Vero alikuwa pembeni yake amelala .Akamwangalia mpenzi wake kwa dakika kadhaa.akapatwa na uchungu mwingi baada ya kuyaona mapenzi makubwa aliyokuwa nayo binti huyu kwake.“Ni wazi vero amekuwa ni msichana wa pekee maishani mwangu ambaye ameweza kunionyesha mapenzi ya kweli na kunisaidia kupata uelekeo mpya wa maisha yangu.Nampenda Vero na nina imani ndiye mwanamke atakayenifaa maishani.lakini huyu Happy ……………mhhh …naye kajitokeza tena katika hatua za mwisho kabisa za kukamilisha ndoa yangu na Veronika.Yes ! nilimpenda Happy kuliko kitu chochote kile lakini alinitenda kitu kibaya nikamwondoa katika moyo wangu.Lakini ni kwa nini siachi kumuwaza ?Kila dakika sura yake inanijia akilini….ooh Mungu wangu nisaidie katika mtihani huu mguu nilionao.Lakini pamoja na yote yaliyotokea baina yetu lazima nimtafute Happy .Ni lazima nionane naye .Lazima nifahamu ni kwa nini alinitenda vile? “Patrick akamtazama tena vero akamkumbatia kwa nguvu. Asubuhi na mapema Patrick aliamka akaoga kisha akamuaga Happy kuwa anakwenda kumuona Andrew.Vero hakuwa mbishi akamwacha aendeAkiwa ndani ya gari Patrick alijaribu tena kupiga ile namba ya simu ambayo aliamini kabisa itakuwa na uhusiano Fulani na Happy lakini bado ikawa haipatikani.“Yawezekana labda alipopiga simu jana mchana ikapokelewa na Vero ,walitoleana lugha chafu .Pengine walitukanana ,kitendo kilichomfanya akasirike na kuizima kabisa simu yake.”akawaza PatrickAkawasili nyumbani kwa Andrew mishale ya saa moja na dakika ishirini hivi“ooh Patrick mbona asubuhi hivi.Kuna usalama kweli? Akauliza andrew kwa shauku ya kutaka kufahamu kama kulikuwa na tatizo lolote.“Si kwema andrew” akasema Patrick huku akiketi sofani.“Enhe ! kulikoni ? Akauliza tena AndrewPatrick akatulia kidogo akavuta pumzi kisha akasema“mambo katu si mazuriAndrew.Jana mchana mimi nikiwa nimelala mtu ambaye nahisi atakuwa ni Happy alipiga simu ikapokelewa na Vero.”“Mhh usiniambie Patrick.Enhee ! ikawaje? Andrew akauliza huku akionyesha hali Fulani ya mstuko‘ sielewi waliongea nini kwa sababu kwa mujibu wa maelezo ya Vero ni kwamba mtu huyo hakuongea chochote.Nikajaribu kupiga mimi mwenyewe simu ikapokelewa na sauti niliyoisikia ni dhahiri ni ya Happy .Sidhani kama ninaweza kuipotea sauti yake japokuwa hatujaonana kwa kipindi kirefu.Baada tu ya kuitikia akakata simu na kuizima kabisa na hadi muda huu tunapoongea simu yake haipatikani.Nimechanganyikiwa Andrew sijui nifanye nini ndio maana nimekuja hapa kwako asubuhi hii ili unisaidie mawazo.” Akasema PatrickAndrew akavuta pumzi ndefu akasimama na kuzunguka zunguka humo sebuleni kisha akasema.“Patrick hata mimi naanza kuhisi kuwa kuna kitu waliongea na Vero ambacho kimemfanya awe na hasira na asitake tena hata kuiwasha simu yake.lakini bado hatuna haja ya kukata tamaa,kitu tunachotakiwa kukifanya kwa sasa ni kutafuta mahala anakoishi Happy .kazi hiyo niachie mimi nitaifanya kikamilifu.Baada ya kupafahamu anakoishi itakuwa rahisi kwetu kumpata”‘Ahsante sana Andrew kwa kunisaida.” Akasema Patrick na baada ya dakika chache za maongezi Patrick akaaga na kiondoka akimuwahi Vero nyumbani.
. * * * *
Happy alistuliwa toka katika usingizi mzito na hodi iliyogongwa mlangoni.Alijiinua kiuchovu na kuangalia saa.Ilikuwa ni saa nne asubuhi.“Mhh ! dada mbona umelala hivyo? Nimepatwa na wasiwasi pengine unaumwa.” Akasema Margreth.Happy hakujibu kitu akageuka na kukaa tena kitandani huku akiyafikicha macho yake ambayo kwa sasa yalionyesha hali ya kuvimba kutokana na kulia kwa muda mrefu.“Happy hebu niambie kitu gani tena kinakufanya uwe katika hali hiyo? Patrick ulimpigia simu? Akauliza Margreth“Ah ! acha tu Margreth.Nilimpigia simu lakini ikapokelewa na mwanamke.Nilishindwa kuongea jambo lolote nikakata simu.Nahisi Patrick tayari atakuwa ameoa”Happy akashindwa kuvumilia machozi yakamtoka.“Hebu nisikilize dada.Hupaswi kulia.Ninaimani hizo ni hisia zako tu kwamba Patrick tayari ana mke.Huwezi jua pengine ni ndugu yake ,dada yake au hata katibu muhtasi wake.Hata hivyo ni muda mrefu sasa umepita toka mlipopotezana na mlipotezana katika mazingira yenye kutatanisha sana huku kila mmoja akiwa bado anampenda mwenzake,nina imani kabisa kuwa pendo lile bado liko hai.Najua hii ni sababu unahisi kuumizwa na hisia kuwa Patrick tayari ana mke kwa sababu bado unampenda.Yawezekana atakuwa ameoa au pengine ana mchumba lakini hilo lisikupe shaka.Tutalifahamu muda si mrefu.”Maneno yale ya Margreth yakampa moyo sana Happy .“nashukuru sana mdogo wangu kwa kunifariji.Pamoja na hayo naomba tafadhali hii iwe ni siri yako na asijue mtu mwingine yeyote yule.” Akasema Happy“Usijali Happy Hakuna mtu yeyote atakayefahamu juu ya Patrick.leo nataka nimfuate Patrick ofisini kwake kama hii kadi yake ya biashara inavyoonyesha.” Happy akatabasamu baada ya kauli ile ya mdogo wake kisha Margreth akaenda kujiandaa kwa ajili ya kwenda ofisini kwa Patrick .
* * * *

Saa tano na nusu ilimkuta Margreth katika jengo lenye ofisi anakofanyia kazi Patrick .Akashuka garini na na kupanda lifti kuelekea ghorofa ya saba ziliko ofisi hizo alizokuwa akizitafuta.Aliposhuka tu katika lifti akakutana na bango kubwa linaloelekeza zilipo ofisi hizo.Taratibu na kwa mwendo wa madaha kama ilivyo kawaida yake alifika mpaka katika chumba cha mapokezi akakutana na akina dada wawili warembo,Akajitambulisha na kuomba kuonana na Patrick.“Patrick kwa sasa yuko mapumzikoni nyumbani kwake.Alipatwa na matatizo ya moyo hivi karibuni hivyo amepewa muda wa kupumzika .Labda tukuelekeze nyumbani kwake kama kuna ulazima wa kumuona yeye mwenyewe ”Margreth akaelekezwa nyumbani kwa Patrick kisha akaaga na kuondoka akaanza safari ya kuelekea nyumbani kwa Patrick. Ilimchukua masaa mawili hivi kuipata nyumba ya Patrick.Kwa mujibu wa ramani aliyopewa alitumaini nyumba ile aliyokuwa amesimama nje ni yenyewe.Taratibu akalisogelea geti kubwa la mbele na kubonyeza kitufe cha kengele.Baada ya kama dakika nne hivi dada mmoja mrembo ,aliyevalia nadhifu akafungua mlango.“Karibu dada” Yule dada akasema“ahsante sana” Margreth akajibu“sijui nikusaidie nini?“Samahani dada naomba kuuliza , hapa ndio nyumbani kwa Patrick? Akasema margreth“Yes ndio hapa.Una shida naye ?
“Yes nina shida naye ya kiofisi.Kuna mzigo wake ulipitia katika ofisi zetu.Baada ya kuona kimya kingi tukaona tumtafute.Nimekwenda ofisini kwake wakanieleza kuwa Patrick ni mgonjwa na wakanielekeza hapa nyumbani kwake.” Akadanganya Margreth.“Kweli dada ,Patrick ni mgonjwa wiki ya pili sasa anamumwa.Ana matatizo ya moyo kwa hiyo amepewa muda mwingi wa kupumzika.Hivi tunavyoongea amelala lakini ninaweza kumwamsha kama kuna ulazima wa kuonana naye sasa hivi.”“Usijali dada ni masuala madogo tu ya kiofisi hivyo sioni kama kuna haja yoyote ya kumsumbua mgonjwa.Ila atakapoamka mwambie kuwa Margreth alifika hapa.”“Sawa dada Margreth karibu sana.Mimi naitwa Veronika.karibu ndani upate walau glasi ya maji.” Akasema Veronika“Nashukuru sana dada Vero siku nyingine nitaingia ndani.Haya kwa heri”Margreth akaondoka maeneo hayo huku kichwa chake kikiwa kizito mno kwa mawazo “Je yawezekana kweli Patrick akawa na mke?Inawezekana Vero akawa ndiye mke wa Patrick?Sasa nimepata picha kamili. Happy alipopiga simu ya Patrick ikapokelewa na Vero na ndio maana akashindwa kuongea.Nitamshauri Happy tujaribu tena kumpigia Patrick leo jioni.Akawaza Margreth akirudi nyumbani.



* * * *

Saa kumi na moja jioni Margreth akarejea nyumbani kwao na mtu wa kwanza kukutana naye alikuwa ni mama yake ambaye akamwita na kumuuliza“margreth ,naomba unieleze kwa undani bila kunificha ni kitu gani kinachomsumbua dada yako? Nina imani lazima utakuwa unafahamu kinachomsumbua Happy.Kutwa nzima amejifungia ndani,hajala kitu na wala hataki kuonana na mtu yeyote.Wakuu wake wa Miss Tanzania wamekuja kuonana naye leo hii mchana lakini ameshindwa kuonana nao.na hata waandishi wa habari wamekuja kutaka kumuhoji lakini hao ndio kabisaaa hataki hata kuwasikia.Sasa hebu niambie kitu gani kinachomsumbua mwenzio? Margreth akamtazama mama yake kisha akasema
“Mama hakuna jambo lolote alilonieleza.Nimekuwa nikijaribu toka jana kumshawishi ili anieleze ni kitu gani kinachomsumbua lakini amekuwa mgumu kunieleza.Ni wazi hata mimi naona kuna kitu kinamtatiza .naomba uniachie kazi hiyo mama nitajitahidi kumdadisi.”“sawa Margreth jitahidi mwanangu.hali ya dada yako inatia shaka.”“ mama nipeni chakula nimpelekee nitamkoroga mpaka atakula .” Akasema Margreth.Haraka haraka akapewa sinia la chakula na kwenda hadi mlangoni kwa Happy .Akasimama hapo mlangoni kwa takribani dakika moja akatega sikio na kwa mbali akaisikia sauti ya Happy akilia.Aliumia sana moyoni mwake kuona jinsi dada yake anavyoteseka namna ile kwa sababu ya mapenzi.Akagonga mlango kisha taratibu mlango ukafunguliwa akaingia ndani. Happy alionyesha hali ya kukata tamaa kwa jinsi alivyosawajika.Macho yalikuwa yamemvimba kwa kulia.“Happy jaribu kuwa jasiri dada yangu.Mambo yanaweza kuwa magumu zaidi iwapo hautaonyesha ujasiri .Hebu kwanza nyamaza kulia ule chakula.Mama ana wasiwasi sana juu yako.”Happy akamtazama mdogo wake usoni kisha akasema“Najua ni rahisi kutamka hivyo kwa sababu wewe hayajakukuta.Ungekuwa katika mahala pangu , sijui ungefanya nini.Huwezi jua ni maumivu kiasi gani niliyonayo moyoni .Naumia sana Margreth.Patrick amekitonesha tena kidonda kilichokuwa kimeanza kupona.” Akasema Happy kwa uchungu“Ok Dada Happy tulia basi ule halafu nikwambie habari za leo”“Hebu nieleze kuna habari gani huko utokako? Akauliza Happy huku akifuta machozi na kumtazama mdogo wakeMargreth akavuta pumzi ndefu akajiweka sawa na kusema.“Nilipotoka hapa nikaelekea moja kwa moja zilizo ofisi za Patrick kwa mujibu wa wa hii businesscard inavyoonyesha.Nilifika katika ofisi hizo na nikaambiwa kuwa Patrick hayupo anaumwa .amepatwa na maradhi ya moyo na hivyo yuko nyumbani kwake anapumzika.Wakanielekeza nyumbani kwake nikaenda nikamkuta dada mmoja anaitwa Veronika .Akanikaribisha lakini sikuingia ndani nikamuachia ujumbe kuwa Patrick akiamka amwambie kuwa nilifika pale.Kwa ufupi ndiyo hivyo.” Akasema Margreth.Happy alibaki ameshika tama asiamini alichokisikia kutoka kwa Margreth.Kilichomfanya anyong’onyee ni kusikia kuwa Margreth alikuta msichana pale nyumbani kwa Patrick.“Najua kabisa huyu ndiye aliyepokea simu yangu .Yawezekana akawa ni mke wake? Au mchumba wake? Ni lazima nimpate Patrick ili nipate ukweli toka kwake. …….”Akawaza Happy na mara simu ya simu ya Margreth ikaita.Akaangalia mpigaji na kumgeukia Happy..“Ni mike” Akasema Margreth huku akimtazama Happy.“Mwambie sipo “ Akasema Happy huku amejishika kichwa.Alichanganyikiwa ghafla.Tayari alikwishakubali matokeo kuwa Mike ndiye mtu wa maisha yake lakini Ghafla sana ametokea Patrick na kumfanya Happy achanganyikiwe.Margreth akaweka sauti kubwa ili Happy asikie watakachoongea na Mike“hallow Mike” akasema Margreth baada ya kuipokea simu“hallow margreth mambo vipi?“safi tu Mike habari ya huko?“Huku kwema vipi huko?“Huku nako kwema tu”akasema Margreth“Hebu niambie Margreth mbona Happy simpati katika simu ? Nimejaribu sana kumpigia simu lakini haipatikani kabisa.Nilipata taarifa kuwa amefanikiwa kulitwaa taji la Miss Tanzania lakini akapatwa na mstuko akaanguka na kupoteza fahamu.Mara ya mwisho alinipigia simu kabla hawajaanza mashindano toka hapo sijapata mawasiliano yoyote toka kwake.Hebu nieleze margreth nini kimetokea? Akauliza Mike Margreth akamtazama Happy kisha akasema“Happy alipatwa na mstuko kidogo baada ya kutangazwa mshindi.Lakini kwa sasa anaendelea vizuri.Kuhusu mawasiliano ni kwamba simu yake bado hakumbuki aliiweka wapi .Mike nakushauri umsubiri kidogo ili aweze kurejea katika hali yake ya kawaida ndipo mtaweza kuongea kwa kirefu zaidi lakini kwa sasa anahitaji mapumziko Akasema Margreth
“Ok nimekuelewa margreth upo karibu naye hapo walau niongee naye kidogo niisikie japo sauti yake ? akauliza Mike“Hapana Mike niko mbali naye kwa sasa” akajibu kwa ufupi Margreth
“sawa Margreth lakini kuna jambo lingine nataka kukueleza.Kwa sababu ya matatizo ya Happy nimeomba wiki mbili za dharura ili niweze kuja Tanzania kukaa naye na kumfariji katika kipindi hiki kigumu alichonacho.Kesho nitaanza safari.Naomba usimwambie chochote .Nataka nimshangaze kidogo.Nitakujulisha kabla sijaanza safari yangu.” Akasema Mike.“Ok Mike bye”Margreth akajibu na kukata simu.Happy alijilaza kitandani mikono ikiwa kichwani.“ Nampenda Mike na kidoleni nina pete yake ya uchumba ni kwa nini Patrick ametokea na kufanya akili yangu iyumbe namna hii? Happy alijikuta tena katika mtihani mgumu.Ni wazi alimpenda Mike lakini baada ya kutokea Patrick taratibu ameanza kuonyesha dalili za kuanza kumsahau Mike..
* * * *
Saa kumi na moja jioni Patrick akaamka na kumkuta Veronika amekaa pembeni ya kitanda.“Unajisikiaje mpenzi? Vero akauliza“najisikia vizuri dear”Vero akasogeza karibu meza ndogo iliyokuwemo humo chumbani na kumuandalia Patrick kinywaji.“My dear wakati umelala kuna dada mmoja alikuja kukutafuta.Lakini nilimwambia kuwa umelala na hakutaka kukusumbua.Akasema kwamba nikikutajia jina lake utakuwa umemfahamu.” Akasema Veronika“ Alisema anaitwa nani? Patrick akauliza kwa shauku“Margreth ”Vero akajibu“Nani ? !!....”“Margreth ” Vero akarudia tenaPatrick akasimama na kujishika kiuno“Veronika una uhakika na unachokisema? Patrick akauliza“Kwani vipi Patrick mpenzi wangu kuna tatizo gani?hayo ndiyo maagizo aliyoyaacha yeye mwenyewe.” Vero akajibu kwa wasiwasi“Oh My god ! Margreth came here ? Alikuwa na nani? Patrick akauliza huku akiwa bado amepatwa na mshangao“alikuwa peke yake”Patrick akakaa tena kitandani .Vero akastushwa na hali ile aliyoipata Patrick ghafla akamsogelea na kumkumbatia.
“My dear Patrick tafadhali niambie kuna kitu gani kinachokusumbua.Huyu margreth ni nani mbona umestuka hivyo uliposikia jina lake?”akauliza Veronika“Hakuna kitu Veronika.”Patrick akajibu kisha akainuka na kumwacha Vero pale kitandani.“Vero naenda kwa Andrew.Yeyote atakayekuja kunitafuta anisubiri sintakawia sana” Akasema Patrick huku akivaa shati lake.‘Patrick ngoja basi nikusindikize kwa hali hiyo huwezi endesha mwenyewe.”Vero akasema hali machozi yakimlenga lenga“Vero hakuna matatizo ninaweza kuendesha” akasema Patrick na haraka haraka akatoka ndani akaingia garini na kuondoka kwa kasi akimwacha Veronika amesimama mlangoni akimwangalia kwa uchungu akiwa na mawazo mengi mno kuhusiana na Patrick kubadilika ghafla vile mara tu aliposikia jina la margreth.
.
* * * *
“Patrick kuna tatizo gani ndugu yangu ? Aliuliza Andrew baada ya Patrick kuingia kwa kasi ndani mwake akiwa amesawajika“Uuuuuph ……………” Patrick akapumua kwa nguvu na kujitupa sofani“Mambo yanazidi kuwa magumu Andrew”“ kumetokea nini Patrick?" akauliza Andrew“Margreth alikuja nyumbani”Patrick akasemaAndrew akamtazama Patrick kwa makini sana na kusema
“margreth amekuja nyumbani kwako? Alikuja kukueleza nini? Andrew akauliza“ Nilikuwa nimelala hivyo sikuweza kuonana naye.Alionana na Vero na kumwachia maagizo kuwa nikiamka anitaarifu kuwa alifika pale.Nahisi alikuja na ujumbe wa muhimu sana toka kwa Happy .I’m confused” akasema Patrick.Kimya kizito kikatanda hapo sebuleni kila mmoja alikuwa akiwaza lake.Ghafla wote wakastushwa na mlio wa simu ya Patrick.Akaitoa mfukoni na kuangalia namba za mpigaji.Zilikuwa ni namba ngeni kabisa katika simu ya Patrick.“ Hallooo” Akaita Patrick.“Halloo naongea na nani? Ikauliza sauti ya upande wa pili ambayo ilikuwa ni sauti tamu ya kike.“ Unaongea na Patrick hapa”“Uh ! Patrick .margreth hapa.”“margreth !! .. Patrick akauliza kwa mstuko“Yes margreth Kibaho”“I cant believe this..Margreth ni wewe kweli?? akauliza Patrick“Yeah its me , margreth” akajibu Margreth.Patrick akavuta pumzi ndefu.Margreth akasema“ Patrick ,nilikuja nyumbani kwako leo mchana ulikuwa umelala nikamkuta dada mmoja anaitwa Veronika.Pole sana kwa kuumwa” akasema Margreth“Ahsante sana Margreth.Vero aliniambia kwamba ulifika nyumbani kwangu”Patrick akasema“Kwa ufupi shida iliyonileta ni kuongea na wewe.Nahitaji sana kuonana na wewe mapema iwezekanavyo.Kwa hiyo kama upo tayari nijulishe ili nikutaarifu tuonane lini na wapi” akasema Margreth“ margreth nipo tayari,nipo tayari hata sasa hivi,se…,” hakumaliza sentensi yake Margreth akadakia“Ok Patrick nitakutumia ujumbe kukufahamisha ni wapi tutaonana” akasema Margreth“Sawa Margreth lakini hebu nipe habari za Hap……”Kabla hajamalizia sentensi yake margreth akasema“Patrick I have to go.” akakata simuZilipita dakika mbili toka margreth akate simu , Patrick bado alikuwa ameishikilia simu yake .“Hebu niambie Patrick ni nani uliyekuwa ukiongea naye?Sauti ya Andrew ndiyo iliyomfanya astuke“ni Margreth “ akasema Patrick.“Anasemaje?“Anasema kuwa anahitaji sana kuonana na mimi.hakutaka maongezi mengi amesema atanitumia ujumbe kunitaarifu tuonane lini na wapi.”Andrew akainama chini kwa sekunde kadhaa akafikiri na kisha akasema“Mambo yanazidi kupamba moto.Inavyoonyesha kuna jambo zito anataka mkaliongee hususani kizungumkuti hiki kilichopo mbele yetu”“Sawa Kabisa Andrew hata mimi nadhani hivyo.”Andrew akaiendea friji na kujimiminia mvinyo katika glasi .Mara simu ya Patrick ikalia tena.Akaichukua na kuiangalia mpigaji.Ilikuwa ni simu toka kwa shemeji yake yaani dada yake Veronika aishiye Uingereza..“Hallo shemeji” Akasema Patrick“ Shemeji habari yako ?“Habari yangu nzuri shemeji.Habari za huko kwenu?‘Huku wote tu wazima,Pole sana shemeji yangu kwa matatizo.Tulijitahidi tuje kukuangalia lakini kutokana na kutingwa sana na shughuli tukashindwa”“Nashukuru sana Shemeji .Nilipatwa na tatizo kidogo la mstuko lakini kwa sasa naendelea vizuri Hivi sasa niko katika mapumziko mafupi na hali yangu inaendelea kuimarika..”akasema Patrick." nafurahi sana shemeji kusikia unaendelea vizuri.Nimepiga simu kwa vero sasa hivi akaniambia umetoka kidogo hivyo nikaona nikupigie katika simu yako ili nikujulie hali.Pamoja na kukujulia hali nataka pia kukutaarifu kuwa zile tiketi zenu za ndege za kuja na kurudi Uingereza kwa ajili ya kufanya manunuzi ya harusi yenu tayari zimekwisha tumwa katika ofisi za british airways hapo Dare s salaam na kwa kuwa kila kitu kuhusiana na safari hii kimekwisha tayarishwa basi safari itakuwa kesho kutwa.Mkiwa huku tutakupeleka katika hospitali kubwa zaidi kwa ajili ya uchunguzi wa afya yako.Msihofu shemeji hizi zote ni gharama zetu.”Ilimchukua Patrick sekunde kadhaa kurudisha akili na kukumbuka kuwa alikuwa akiongea na simu.Alikuwa amechanganyikiwa.“hallo shemeji” Aliita shemeji yake baada ya kuona muda unapita hapati jibu“Ouh shemeji.”Patrick akajibu“Vipi mbona kimya shemeji?“ shemeji nashukuru sana kwa msaada wenu .Nimefurahi sana.Kesho tutafanya maandalizi ya mwisho na kesho kutwa tutaanza safari ya kuja hapo uingereza kwa ajili ya manunuzi ya harusi yetu.”“Ok shemeji tunawatakia safari njema”“haya shemeji bye” Akakata simuKijasho chembamba kilimtiririka Patrick .Akaitupia simu yake sofani na kujishika kichwa.“Patrick kuna nini” Akauliza Andrew“Andrew I’m confused”“Kwa nini Patrick”“Si unakumbuka niliwahi kukwambia kuwa dada yake Vero yule anayekaa Uingereza alikuwa akitushughulikia safari yetu ya kwenda uingereza kufanya manunuzi ya mavazi ya harusi sasa zile tiketi za ndege za kwenda London tayari zimetumwa na wanataka safari iwe kesho kutwa.”akasema Patrick.“Ooh My God” Andrew akasema kwa sauti ndogo “Patrick” Akaita Andrew“Yes Andrew”“hata mimi nahisi kuchanganyikiwa lakini nakushauri kitu kimoja.Amua nini kifanyike kati ya mpango wa kumtafuta Happy au kushughulikia harusi yako na Vero . Suala la ndoa yako limepiga hatua kubwa sana kwa sasa na vile vile suala la kuonana na Happy nalo liko katika hatua nzuri.Sasa chagua moja ili tushughulike nalo kwa ukamilifu”Patrick hakujibu kitu akaendelea kujiinamia pale sofani .Baada ya dakika kama mbili hivi akainua kichwa akasema“Andrew siendi London ““Patrick...!!! “ Andrew akasema kwa mshangaoPatrick akainuka akaichukua simu yake na kuuendea mlango“Tutaonana Andrew”“Patrick ..!!! Andrew akapaza sauti lakini tayari Patrick alikwisha ingia garini na kuondoka zake.
Patrick alifika nyumbani na kumkuta Vero amekaa sofani akimsubiri.Alipomuona mpenzi wake akainuka akamkumbatia na kumbusu.“Welcome back darling.” Patrick hakujibu kitu akambusu shavuni na kwenda kuketi sofani“Patrick mpenzi naomba kabla ya yote ule kwanza chakula.Nimekuandalia chakula kizuri sana ili ule na urejee katika hali yako ya kawaida.”“ahsante sana vero lakini sijisikii kula kitu chochote leo.Naomba juice baridi” akasema Patrick“Hapana Patrick lazima ule chakula “ Vero akasema kwa msisitizo.Ni kweli Patrick hakuwa na hamu ya kula lakini hakutaka kumpa Vero mawazo mengi akainuka na kuelekea mezani.Vero alijitahidi kumlisha chakula na kumwonyesha mapenzi ya hali ya juu.Baada ya kumaliza kula wakaketi sofani wakiangalia Luninga.“Patrick mpenzi ,kuna habari nzuri sana nataka nikwambie “ Akasema Vero.Patrick akamwangalia Vero usoni kwa kituo kwani alikwishagundua kitu gani Vero alitaka kumwambia.Akatabasamu na kusema“jambo gani hilo Vero”Vero akakohoa kidogo akaendelea“Dada kapiga simu jioni hii na kunitaarifu kuwa tiketi zetu za kwenda na kurudi London kwa ajili ya ile shopping ya harusi zimekwisha tumwa katika ofisi za British airways na safari ni kesho kutwa.”akasema Vero huku akitabasamu.Vero aliongea maneno haya huku akimsugua sugua Patrick kifuani.Patrick hakusema kitu alikaa kimya na ni wazi alionekana yuko katika mawazo mazito sana.“Vipi dear unawaza kitu gani?Patrick akamwangalia Vero usoni kwa muda mrefu kisha akasema“Vero dear I’m sorry .Itakubidi uende peke yako.Hali yangu kwa sasa bado si nzuri kusafiri safari ndefu kama hii.Nasikitika sana Vero”Vero akasimama wima akashika kiuno huku akimwangalia Patrick“Whaat !!!!!!!! ““I’m sorry Vero itakubidi uende tu mwenyewe mimi nitabaki niendelee kupumzika .Hali yangu bado si nzuri kusafiri safari ndefu kama hii”“No ! Patrick inatubidi tumuone daktari kwanza ili athibitishe kama kweli itakuwa ngumu kwa wewe kusafiri .Halafu isitoshe dada amesema kuwa watagharamia uchunguzi wa afya yako huko huko Uingereza sasa tatizo liko wapi mpenzi?“Veronika nimeshasema hali yangu si nzuri sasa huyo daktari wa nini tena? Ni yeye anaumwa au mimi? Tafadhali Vero hakuna mjadala katika hili” Patrick akasema kwa hali Fulani ya ukaliVero akaondoka sebuleni hapo kwa kasi huku akilia
Patrick akaogopa akamfuata.Vero alikaa kitandani huku akilia kwa kwikwi.Patrick akamsogelea na kumkumbatia.“Vero mpenzi najua ni kwa kiasi gani kauli yangu hii imekuumiza moyo.Samahani sana kwa hilo mpenzi wangu.Wewe ndiwe kila kitu kwangu na wala sina sababu yoyote ya kukuliza.Nisamehe Vero mpenzi wangu.”Patrick aliingia katika kazi nzito ya kumbembeleza Vero“Patrick why you are doing this to me?Nimekukosea nini Patrick mbona unanifanyia hivi ? Patrick umebadilika ghafla.Mbona sikuelewi ?.Hebu niambie kama kuna jambo nimekukosea ili nikuombe msamaha na nijirekebishe.”Maneno yale yakamwingia vilivyo Patrick akamfuta Veronika machozi“Veronika nyamaza mpenzi wangu.Nakupenda sana kuliko kitu chochote.Sikuwa na lengo au nia mbaya kukwambia vile bali ni kutokana tu na hali yangu kiafya kutokuwa nzuri bado .Hata mimi mwenyewe inaniuma sana .Lakini hakijaharibika kitu tunaweza tukapanga ukaondoka hata na Andrew akakusaidia katika shopping” Vero akainua uso wake na kumnasa Patrick kibao kidogo shavuni.“Shame on you Patrick.Ninafunga ndoa na wewe au na Andrew ? Andrew ndiye mpenzi wangu? Patrick kaa chini na kufikiri kwa makini dada amejitolea kugharamia uchunguzi wa afya yako katika hospitali kubwa ili kabla ya harusi yetu uwe katika hali nzuri sasa unadhani atanielewaje akisikia kwamba hutakwenda? akasema VeroPatrick hakujibu kitu..Alimwonea Huruma Vero kwa hali ile aliyokuwa nayo lakini ghafla sura ya Happy ikamjia akilini akajikuta akitamka.“Vero I love you soo much.Sioni kama kuna ubaya wowote kama ukienda peke yako.Huna haja ya kuwa na wasiwasi Vero wewe ni wangu na muda si mrefu Mungu akijaalia tutafunga ndoa sasa wasiwasi wa nini mpenzi? Wewe ni wangu Vero na popote nisipokuwepo wewe ni badala yangu kwa hiyo sioni bado tatizo lolote katika suala hili” akasema Patrick.Vero hakujibu kitu akaendelea kulia.Mara ujumbe mfupi ukaingia katika simu ya Patrick .Akaufungua na kuusoma huku moyo wake ukienda kwa kasi sana..Ujumbe ule ulitoka kwa Margreth Kibaho"Kesho saa nne asubuhi Sean snacks Mbezi.margreth”baada ya kuusoma ujumbe ule akaufuta kabisa katika simu yake.Patrick na Veronika hawakuongea tena kitu chochote .

* * * *
Saa kumi na moja alfajiri Vero ndiye aliyekuwa wa kwanza kuamka .Hakutaka kumwamsha Patrick.Taratibu akaingia bafuni akaoga kisha akavaa nguo na ndipo akaamua kumwamsha Patrick.“Patrick naondoka”Patrick akafikicha macho yaliyojaa usingizi akasema“Mbona mapema hivyo kuna nini?“Nothing.Tutaonana”Akasema Vero huku akiondoka.Ni wazi Veronika aliondoka akiwa bado na hasira na haikuhitaji akili ya ziada kung’amua kuwa dada huyu mrembo alikuwa amekasirika.Patrick hakutaka kujibizana naye ingawa aliumia sana moyoni kwa hali ile waliyoifikia katika uhusiano wao.Akiwa hapo kitandani Patrick akajaribu kurudisha kumbukumbu nyuma toka alivyoanza kufahamiana na Happy ,urafiki wao ulivyoanza hadi walivyokuja kutengana.Kumbukumbu zikamjia siku alipoiona sura ya Happy katika Luninga na akapoteza fahamu.Kumbukumbu zikamrudisha tena Diamond Jubilee ambako Happy alitwaa taji la miss Tanzania.“Ni lazima nionane na Happy .”Alitamka maneno haya kwa sauti.Taratibu akajiinua kitandani na kuingia bafuni kujimwagia maji.Akiwa chumbani kwake akijiandaa mara simu yake ikaita.Ilikuwa ni simu toka kwa mama yake.“Sikamoo mama ‘“marahaba.Hivi wewe mtoto una matatizo gani jamani?Umepatwa na nini Patrick?Hivi ni kitu gani kinakusumbua ? Mama yake alisema kwa ukali.“mama kuna nini mbona hivyo? Aliuliza Patrick makusudi .Alijua tayari Vero amekwenda kumshitaki nyumbani .“Umemfanya nini mwenzio?“nani Vero? akauliza Patrick“ kwani una wenzio wangapi?“hakuna chochote kibaya mama nilichokifanya .Ni tatizo la kupishana kauli tu”“sasa sikiliza Patrick nataka ufike hapa nyumbani haraka sana asubuhi hii.Mbona unaanza kutuumiza vichwa we mtoto?Alifoka mama yakePatrick hakujibu kitu akakaa kimya kwa sekunde kadhaa kisha akastuliwa tena“Umenisikia lakini?Nataka uje hapa nyumbani haraka iwezekanavyo.Na ukae ukijua kuwa kesho ni lazima usafiri vinginevyo umtafute mama yako.”Patrick kijasho kikamtoka.Akajikaza na kusema“ huko unakofika sasa ni mbali mama yangu.Nitakuja nyumbani tuongee ila si kwa asubuhi hii.Kuna mahala natakiwa niende Nina miadi ya muhimu sana ““Hiyo miadi ni muhimu kushinda mimi mama yako?“Nothing is important than you mother”Akajibu Patrick“ Sitaki kabisa kusikia hivyo viingereza vyako.Kama unaona mimi ni muhimu njoo nyumbani haraka sana.”“mama samahani siwezi kuja nyumbani sasa hivi .Tayari nina miadi na mtu na ananisubiri asubuhi hii .Nitakuja baada ya kutoka huko.M…..Kabla hajaendelea akasikia simu ikikatwa.Patrick akabaki njia panda.Je aende kwa mama yake au aende katika miadi yake na Margreth?
Akiwa amezama katika fikra nzito hajui nini cha kufanya mara mlango unagongwa na Andrew akaingia.“Hi Patrick” Andrew akasema“Hi” Patrick akajibu.Andrew akamtazama na kusema “Hebu niambie ndugu yangu mambo yanakwendaje kwa sababu nimepokea simu toka kwa mama asubuhi hii akilalamika sana juu yako.Anasema kuwa Vero ameenda pale alfajiri na kumweleza kuwa umebadilika mno kwa siku hizi za karibuni.Na kikubwa zaidi ni kukataa safari ya kwenda London.Hilo ndilo linawafanya wawe na hasira juu yako.Sikiliza Patrick kuna kitu kimoja ulichokosea nacho ni kuonyesha wazi wazi kuwa kuna jambo zito linakusumbua.Tayari Vero amekwisha ng’amua hilo .Na hili la kukataa kwenda safari ndio limedhihirisha wazi kuwa kuna kitu unakificha.Chonde chonde Patrick jaribu kuwa makini ili tusije haribu mambo.”Patrick akafikiri kidogo kisha akasema“ Andrew nakubali nilifanya kosa kuonyesha wazi wazi kuwa kuna suala linanisumbua.Nilishindwa kujizuia.Lakini hata iweje safari hiyo ya kwenda shopping Uingereza siwezi kwenda.Leo nina miadi na Margreth na ninafikiri baada ya hapo nitaonana na Happy sasa huoni kuwa kwenda kwangu London kutaharibu kabisa mpango wangu mzima wa kuonana na Happy .Ni wazi ninahitaji kuonana na Happy .”akasema Patrick“lakini Patrick mimi bado kuna kitu kimoja ninakifikiria ambacho kinaniumiza kichwa sana” Andrew akasema“Jambo gani hilo” Patrick akauliza huku akimkazia macho Andrew“Kuhusu wazazi wako pindi watakapo gundua kuhusu Happy.Kumbuka waliwahi kukwambia kwamba hawaki kumsikia kabisa Happy. ”
Patrick akatabasamu kidogo halafu akasema“Andrew masuala haya yote niachie mimi”“Siwezi kukuachia wewe peke yako Patrick kwa sababu mimi na wewe tu kitu kimoja.Chochote unachofanya na mimi nimeshiriki.Ukikosea wewe na mimi nimekosea pia.”“Kwa hiyo unanishauri nini Andrew? Patrick akauliza“ Nafikiria kitu kimoja”“Kitu gani hicho?“Naona ni bora angali bado mapema uachane na suala hili la Happy .Kwa sasa uko katika maandalizi ya kumuoa Vero , huoni kuwa kuendelea kulipa kipaumbele suala hili la kuonana na Happy linapelekea hata masuala mengine ya msingi kuhusu ndoa yako kuanza kuharibika?.Naona ni bora ukaelekeza nguvu zako katika suala la ndoa yako.Suala la Happy bado halina uzito sana kwa sasa Isitoshe imekwisha pita miaka mingi na pengine tayari Happy ana mchumba wake.Sioni sababu ya kutumia nguvu nyingi katika kumtafuta mtu ambaye alikutia matatizoni halafu baadae akakuacha na kwenda zake Ulaya.Vero ndiye mwanamke pekee aliyekaa nawe katika kipindi chote hiki cha matatizo na ambaye amesimama na wewe hadi sasa ambapo maisha yako tayari yamekaa sawa.Hivi unavyofanya si vizuri na ninakwambia ukweli rafiki yangu unamuumiza Vero sana.” Andrew akasema na kumtazama Patrick usoni ambaye maneno yale yanamfanya abadilike uso wake.“ Andrew unaongea mambo gani ?. Patrick akauliza kwa ukali.“Andrew nimekwisha kwambia mara nyingi kwamba kama hutaki kuwa upande wangu sikulazimishi kushiriki katika masuala yangu”“Patrick ! huo ni ushauri wangu tu na si lazima uufuate.Pamoja na ushauri huo niliokupa kama rafiki yako,lakini mwisho wa siku mwenye uamuzi juu ya masuala yako ni wewe mwenyewe..Ok ! tufanye kama unavyotaka” akasema Andrew.
 
9
Saa nne kamili juu ya alama ilimkuta Patrick maeneo ya Sean snacks.Hakutaka kupoteza hata dakika moja katika miadi hii ya muhimu.Sehemu hii ni moja kati ya sehemu tulivu sana .Ni mahali panapofaa hasa kwa maongezi ya faragha.Aliegesha gari na kushuka kisha akautumia muda wa kama dakika kumi kuzunguka maeneo hayo kwa minajili ya kuangalia kama anaweza akamuona Margreth.Mara simu yake ikalia.Zilikuwa ni namba ngeni.“Halloo “ Patrick akaita“Margreth hapa uko wapi Patrick? ikajibu sauti ya upande wa pili.‘Nimeshafika kitambo ,nilikuwa najaribu kuangaza angaza kama nitakuona”“Mimi ndiyo nafika sasa hivi.Njoo basi huku nyuma kiunga L”Akiwa bado amesimama alijikagua kwanza na kuhakikisha yuko katika muonekano nadhifu kisha akapiga hatua kuelekea mahala alikoelekezwa.“Wow Patrick ! ” Ilikuwa ni sauti ya Margreth mara tu alipomuona Patrick. Patrick hakusema kitu akamtazama Margreth kisha akamkumbatia kwa nguvu.Margreth machozi yalikuwa yakimtoka.Mtu aliyeaminika kufariki dunia leo hii wameonana.“Patrck siamini kama leo tumekutana tena.Siamini kwa kweli” Margreth akasema huku akifuta machozi.“Patrick sitaki kulia tena .Tumekwisha lia vya kutosha kwa ajili yako.Tunashukuru Mungu kwamba u mzima na ametukutanisha tena.Huu ni kama muujiza ambao hakuna aliyeutegemea.” Margreth akasema na kumfanya Patrick kumshangaa kwa maneno yale.“ Margreth hata mimi sikutegemea kabisa kama nitakuja kuonana nanyi tena hasa kutokana na mambo yaliyotokea .Na ndiyo maana nilipatwa na mstuko wa moyo baada ya kumuona tena Happy katika luninga..Hebu kabla hatujaendelea naomba unipe japo kwa muhtasari maendeleo ya hali ya Happy .”akasema Patrick“Happy anaendelea vizuri” Margreth akasema kwa ufupi huku akimtazama Patrick usoni kwa makini.“Really?“Yes .She’s fine.Tuachane na hayo.tuendelee na kilichotukutanisha hapa” Margreth akasema“Ok Margreth ,lakini naona tumejisahau hata kuagiza vinywaji.Sijui unatumia nini?“Mimi nakunywa wine.Wewe je bado unaendelea na kunywa Juice mpaka sasa?akauliza Margreth“Yes margreth.Patrick habadiliki.Umuonaye ndiye Patrick yule yule wa zamani..Ingawa mhh ! mwenzangu umebadilika sana yaani umependeza sasa hivi umekuwa msichana mrembo kama dada yako Happy .” Wote wakacheka kisha Patrick akainuka na kufuata vinywaji.“Patrick” Alianza maongezi Margreth baada ya Patrick kurejea na vinywaji.“Ni mengi sana yametokea katika kipindi hiki tulichopotezana.Ni mambo mengi kiasi kwamba tukianza kukumbushana itachukua siku nzima.Kabla sijaendelea kwa niaba ya familia yetu nakupa pole nyingi sana kwa yote yaliyotokea.Sitaki kukumbusha mateso na machungu ya adhabu ile ya kifungo lakini kwa dhati kabisa naomba niweke wazi kuwa familia yetu haikukutupa na kukuacha peke yako gerezani kama inavyosemekana.Baada ya Happy kuondoka alituachia jukumu la kukuangalia mara kwa mara gerezani lakini baadae zikaja taarifa kuwa umehamishwa gereza na ndio wakati huo huo baba akawa amestaafu kazi tukahama Mbeya na kuhamia Dar es salaam.Toka hapo ndipo utengano ulipoanzia.Tulipofika Dar mdogo wetu akaanza kuumwa hivyo tukatumia muda mwingi kumuuguza kiasi cha kukusahau kabisa.Kitendo hiki cha kukusahau tayari kimetia doa kubwa sana baina yako na sisi.”Akanyamaza akanywa funda kubwa la wine kisha akaendelea.“Patrick kitu kingine kilichotufanya tukate tamaa kabisa ni baada ya kupata taarifa kuwa umefariki ukiwa gerezani”
“Nimefariki nikiwa gerezani ? Patrick akauliza kwa mstuko huku akimuangalia Margreth kwa mshangao..
“Yes Patrick Happy alipata taarifa kwamba umefariki ukiwa gerezani.”
Patrick akavuta pumzi ndefu halafu akasema kwa sauti ndogo
“Thats just a joke I cant believe this.Nani alimtumia taarifa hizo kwamba nimefariki dunia?
“Siwezi kufahamu Patrick taarifa za kifo chako alizipata toka kwa nani.Suala hilo atakueleza yeye mwenyewe kwa kirefu pindi mkionana uso kwa uso” Margreth akasema
Patrick akazama katika mawazo mengi ya ghafla.Taarifa ile ya kwamba alikuwa amefariki dunia ilikuwa imemstua mno.
Margreth akamtazama Patrick usoni halafu akaendelea.
“ Ni vigumu mno kulezea uchungu uliotupata baada ya kupata taarifa ile.Happy alilia mno ,akawa akizimia kila siku mpaka ikabidi baba na mama wasafiri kwenda marekani kukaa naye na kumfariji.Baada ya kumaliza masomo yake Happy alirudi nyumbani na kitu cha kwanza alichokifanya ilikuwa ni kutafuta ni wapi ulizikwa.Baada ya kufanya uchunguzi ikagundulika kuwa taarifa zile za wewe kufariki hazikuwa za kweli.Tulikaa tukimuomba Mungu kwa mapenzi yake atukutanishe siku moja.Mungu amesikia maombi yetu na hatimaye leo hii tumeonana tena.”Margreth akatulia ,akachukua glasi yake ya wine na kupiga funda kadhaa.Patrick jasho lilikuwa likimtoka.Alikosa kitu cha kuongea.Kutokana na joto kali alilokuwa akilisikia akavua koti kisha akatoa kitambaa na kujifuta jasho lililokuwa likimtiririka kwa wingi.Machozi yalimlenga lenga.“Patrick” Margreth akamstua“Haikuwa dhamira yangu kuongea mambo haya ila ni katika kuweka mambo na kumbukumbu sawa. kikubwa kilichonifanya nikutafute kwa hali na mali ni suala hili lililoko mbele yetu.Patrick suala hili ni suala gumu sana.kwa taarifa yako ni kwamba Happy alipatwa na mstuko mkubwa mpaka akapoteza fahamu mara tu alipokuona.Leo hii umeniambia kuwa hata wewe ulipatwa na mstuko baada ya kumuona Happy katika luninga na ukapoteza fahamu.Happy kwa sasa yuko katika wakati mgumu sana akitafuta jinsi ya kuonana na wewe na nina imani hata wewe pamoja na yote yaliyotokea utakuwa na shauku ya kutaka kuonana na Happy .”Margreth akanyamaza na kimya kikapita.
“Patrick hali ya Happy si nzuri.Nasema si nzuri kimwili na hata kiakili.Tangu amekuona Diamond Jubilee Happy anashindwa hata kula.anashinda ndani analia.Hakuna mwingine anayetaka kuongea naye zaidi yangu.Mimi peke yangu ndiye ninayeweza kuongea naye tukaelewana.Ni kutokana na hali yake hii imenibidi nichukue jukumu la kukutafuta ili tuone ni jinsi gani tunaweza kulitatua tatizo hii lililoko mbele yetu.Pamoja na kwamba mmepotezana miaka mingi sasa lakini nina imani wakati mnapotezana kila mmoja alikuwa bado akimhitaji mwenzake na ndio maana baada ya kuonana kila mmoja amepatwa na mstuko wa ajabu.Kitu ninachohitaji kukifanya ni ninyi kukutana .”Margreth akakaa kimya na kuyaacha maneno yale yazame kabisa ndani mwa Patrick.Halafu akaendelea“Yes ni lazima mkutane tena.Kinachomuumiza Happy kwa sasa ni jinsi gani ataweza kuonana na wewe.Nina imani hata wewe utakuwa na hamu ya kuonana na Happy japokuwa miaka imeenda na kila mmoja kwa sasa ameendelea na maisha yake.Nina imani mtakapoonana mtaongea na yatakwisha.Najua kila mmoja analo la kumweleza au kumuuliza mwenzake kwa hiyo mtakapokutana utakuwa ni mwanzo mpya wenye amani.Hata kama hamtarudiana tena lakini litakuwa jambo jema kama mtamaliza tofauti na kuendelea kuishi kwa amani.”Akasema MargrethPatrick alikuwa kimya kabisa jasho likiendelea kumtiririka.Akarekebisha koo na kusema“margreth uko sahihi.Ni lazima nionane na Happy .”Margreth akatabasamu kisha akasema.‘Ok Patrick nashukuru sana kama umeridhia kuonana na Happy .Nimefurahi sana.Nina imani ni fursa hiyo ambayo hata Happy alikuwa akiingojea kwa hamu kubwa.Sasa basi kama unavyojua Happy kwa sasa ni mrembo wa Tanzania.Tayari ana jina kubwa.Kila analolifanya kwa sasa linakuwa ni habari.Vyombo vya habari na hasa haya magazeti ya udaku yanamfuatilia usiku na mchana.Kwa hiyo hatutaki kutengeneza habari na kuwafaidisha watu.Makutano haya yawe ni ya siri kubwa kiasi kwamba iwe ni siri baina ya mimi wewe na Happy .makutano yenu yafanyike nje ya dare s salaam ambako hamjulikani kabisa.Mimi napendekeza makutano yenu yawe morogoro au we unasemaje?Patrick akafikiri kisha akasema“Hapana margreth Morogoro bado ni karibu sana na Dar es salaam.Morogoro hapawazuii watu kufunga safari na kuwafuatilia hasa wakijua kuwa wanatengeneza habari ambayo itawaingizia fedha.Mimi napendekeza tukakutanie Arusha.Tena nje kabisa ya mji.Pale tunaweza kukaa tukaongea na kuweka mambo sawa bila kuingiliwa na mtu yeyote yule.Au we unaonaje margreth?“Hilo ni wazo zuri .Tena zuri sana.Nina imani hata Happy mwenyewe hawezi kulipinga kwa sababu akili yake yote kwa sasa ni kuonana na wewe tu hata kama makutano ni Ulaya.Ok hebu nipe dakika tano hivi niongee naye nisikie anasemaje.”“Ok Margreth.”Margreth akatoa simu yake na kwenda pembeni kidogo na mahali walipokuwa wamekaa akapiga simu.Baada ya kama dakika kumi hivi akarejea.“Enhee anasemaje Happy ? Patrick akauliza kwa shauku.Huku akitabasamu Margreth akajibu“Amekubali bila wasi wasi na tena amefurahi sana yaani bado haamini kama ni kweli”“wow ! nipe basi niongee naye mimi mwenyewe”Patrick akasema“No ! huwezi ongea naye kwa sasa.Mtaongea mkionana uso kwa uso.Kinachotakiwa kwa sasa tupange kabisa utaratibu wa safari ni lini na ni wapi mtakwenda kukutana,nina maana ni hoteli gani mtafikia.”Huku akichezesha mguu wake kwa furaha Patrick akasema“ Kuna hoteli moja mpya kabisa imefunguliwa nje kidogo ya Usa river.Ni sehemu ya kisasa na yenye utulivu wa pekee.Ninadhani inafaa sana kwani hakuna mtu atakayekuja kufuata umbea kule.Kuhusu usafiri gharama zote zitakuwa juu yangu.Community airlines wana ndege ya kwenda kaskazini kila siku saa saba na saa kumi na moja jioni.Mimi nitatangulia na ndege ya saa saba mchana na Happy itambidi aje na ndege ya saa kumi na moja jioni.Kwa hali ilivyo hatuwezi kusafiri na ndege moja.Ngoja nimpigie simu rafiki yangu Andrew afanye mpango wa tiketi hizo haraka sana.Usihofu huyu ni zaidi ya rafiki ninamwamini sana.”Patrick akaitoa simu yake na kumpigia Andrew.“Haloo Andrew”“Patrick vipi? Mambo yanakwendaje?“mambo safi Andrew”“ Andrew ,natakiwa niende Arusha leo na hapa niko na Margreth .Nimeongea naye na mwisho wa yote natakiwa nikutane na Happy Arusha.Naomba basi ufanye hima uende pale katika ofisi za community airlines na unifanyie mpango wa tiketi mbili .Ya kwangu mimi ni ya ndege ya saa saba mchana huu na nyingine ni ya Happy Kibaho ndege ya saa kumi na moja.Please Andrew its urgent.”“Ok Patrick tena imekuwa vizuri kwa sababu hapa nilipo sasa si mbali na ofisi zao ngoja niwahi .Nipe kama dakika ishirini hivi nitakupigia simu."“Ok Andrew”Patrick akakata simu na kupumua kwa nguvu“Everything is going to be fine.Hatimaye baada ya muda mrefu ninaenda tena kuonana na lulu ya thamani kubwa maishani .” Patrick alikuwa akiongea mwenyewe na kumfanya margreth atabasamu .Waliendelea kuongea maongezi ya hapa na pale mara simu ya Patrick ikalia.“Ni Andtrew huyu”Patrick akasema“Haloo Andrew hebu nipe habari”“Patrick kila kitu tayari.Kuna rafiki yangu yule bwana Kimaro anafanya kazi pale pale amenisaidia sana kufanikisha zoezi hili kwa haraka.Kwa hiyo unaweza kupita ofisini kwangu kuchukua tiketi zenu ”“Ok Ahsante sana Andrew nitafika hapo muda si mrefu”Patrick akakata simu halafu akamwangalia Margreth kwa tabasamu pana sana kisha akasema“margreth kila kitu tayari tunaweza kwenda sasa ofisini kwa Andrew”“You are so fast Patrick”“Kwa miadi kama hii ya kukutana na Happy kila kitu lazima kiende haraka” Patrick akasema huku akitabasamuWalitoka hapo Sean snacks na kuelekea moja kwa moja ofisini kwa Andrew.Iliwachukua kama dakika arobaini hivi kuwasili zilipo ofisi za Andrew.Haraka haraka wakafululiza hadi ofisini.“Wow ! Comrade “Akasema Andrew mara tu Patrick alipoingia ofisini kwake.Wakakumbatiana kwa furaha.“Andrew kutana na Margreth kibaho mdogo wake Happy .Margreth kutana na Andrew,rafiki yangu mkubwa na wa pekee kabisa”llikuwa ni mara ya kwanza kwa Andrew kumtia machoni Margreth.Macho yake yalijikuta yameganda yakiustaajabia uzuri wa kimwana huyu.“Mhh !! mtoto mrembo kama malaika.Ama kweli familia hii imebarikiwa kwa kuwa na watoto warembo .Hapana I have to do something.Hii ni nafasi yangu na mimi” Andrew akawaza.“Hello Margreth nashukuru sana kukufahamu.Karibu sana”Andrew akasema huku akitoa tabasamu pana sana .“ Hata mimi nimefurahi sana kukufahamu Andrew”

* * * *
“Patrick “ Akasema Andrew“Kwa kuwa muda uliopo mpaka saa saba ni mfupi sana na nina imani hautaweza kuonana na mama kama ulivyomuahidi ,unaonaje kama ukimpigia simu na kumweleza kuwa hutaweza kuonana naye leo ili asijedhani umemdharau.?” Andrew akashauriPatrick akatabasamu na kusema“Andrew una akili sana”Akasema Patrick huku akiitoa simu yake na kumpigia mama yake“Halloo mama””Enhe!! Unasemaje?Mbona hufiki ? Mwenzio yuko hapa toka asubuhi ,tunakusubiri wewe” Mama yake akasema kwa ukaliPatrick akastuka akafikiri kidogo kisha akasema
“Ina maana mpaka muda huu Vero yuko hapo nyumbani?
“Vero yuko hapa akikusubiri wewe.Mbona unamtesa mwenzio namna hii ?” mama yake akauliza kwa ukali“mama samahani sintaweza kufika tena hapo nyumbani leo hii kama nilivyokuahidi.Nimepata dharura moja ya muhimu mno.Nafikiri labda kesho kutwa tutaonana”“Unasemaje wewe???? Mama yake akahamaki.
“Mama nimepata udhuru wa ghafla hivyo sintaweza kufika leo mpaka kesho kutwa.”“ Patrick una akili zote kweli ? Hivi hayo masuala yako unayaona ya muhimu kuzidi ninalokuitia mimi mama yako?“Mama”Patrick akadakia“Nafahamu unaniitia jambo la msingi kabisa na siku zote siwezi kukudharau wewe mama yangu.Lakini kwa hili naomba unisamehe mama.Ni muhimu mno kwangu”Patrick akakata simu na kuizima kabisa.Akashusha pumzi ndefu“Oh My God help me.”Akasema Patrick huku akitoa kitambaa na kujifuta jasho usoni.Andrew na Margreth wakamuangalia usoni“mama anasemaje?” Andrew akauliza.“Hakuna muafaka .Bado ananitaka niende nyumbani kwani bado Vero yuko kule wananisubiri.Anyway ni mambo ya kawaida nimeyazoea.Ila andrew nakuomba sana rafiki yangu niko chini ya miguu yako usimweleze mtu yeyote nimekwenda wapi.Najua watakusumbua sana wakiamini kuwa ni lazima utakuwa ukifahamu nimekwenda wapi.Kuonana na Happy ndilo jambo la muhimu mno kwangu kwa sasa” Akasema Patrick.
Kabla hajaendelea mbele simu ya Andrew ikaita.alikuwa ni mama yake Patrick.“Ni mama” Andrew akasema kwa wasi wasi“Ongea naye mwambie hujaniona kabisa tangu tulivyoonana asubuhi”akasema Patrick”Haloo mama “Andrew akasema baada ya kuipokea simu ile
“Samahani Andrew , huyu mwenzio yuko wapi?Uko naye hapo?“Hapana mama siko naye hapa.Bado hajafika huko nyumbani?“hapana bado hajafika.”akajibu mama yake Patrick“ nilimfuata nyumbani kwake asubuhi na kumweleza vile ulivyonituma nikamwacha hapo akijiandaa sasa nashangaa unaposema hajaonekana mpaka sasa ” akasema Andrew"Andrew huyu mwenzio ana matatizo gani kwa sasa?.Tangu apatwe na huu mstuko amebadilika sana.Mwenzake yuko hapa akimsubiri .Kanipigia simu muda si mrefu na kunitaarifu kuwa ana dharura .Dharura gani hiyo ya kuushinda wito wangu mimi mama yake? Kibaya zaidi amekata simu na kuizima kabisa.Hivi kweli Patrick amefikia hatu ya kunizimia simu hata mimi ! ukimuona mweleze kwamba sitaki tena aje nyumbani ..” “Samahani kwa kukukatisha mama ila huko unakofika mama ni mbali sana.Kwa jinsi ninavyoelewa mimi Patrick hawezi kukata simu na kuizima kabisa.Ukweli ni kwamba leo nilivyokwenda kwake asubuhi nimemkuta akihangaika kuikausha simu yake iliyomwagikiwa maji.Hivyo basi simu yake inatatizo hilo kwa sasa la kuwaka na kuzima.Hata mimi nimekuwa nikimtafuta kwenye simu bila mafanikio.” Andrew akadanganya huku Patrick akitabasamu.“Unamtetea mwenzio ? Haya anayoyafanya unaona ni mazuri? mama yake Patrick akafoka“Hapana si hivyo mama usinielewe vibaya.Wewe ni mama yetu na kamwe hatuwezi kukudanganya.Naomba mama unipe jukumu la kumtafuta Patrick na kumleta hapo nyumbani haraka iwezekanavyo.”akasema Andrew“Sawa Andrew.Jitahidi basi umtafute umlete hapa haraka Kesho wana safari na mwenzake ya kwenda London.Atake asitake ni lazima aende na mwenzake Uingereza”“sawa mama” Andrew akajibu na kukata simu.Wote wakajikuta wakiangaliana baada ya simu kukatwa.“Good.Umemjibu vizuri kiasi ambacho hata sikutegemea.Sasa hatua hiyo imekwisha.Kifuatacho sasa naona tumruhusu margreth yeye aondoke na mimi nikajiandae.Au unasemaje? akasema Patrick“ kwa heri Patrick nawatakia kila la heri.Ila please sitaki dada yangu aendelee kulia tena." akasema Margreth akiingia katika taksi.“Happy hatalia tena ,nakuahidi ” Akasema Patrick “Mhh ! Patrick hii familia ina watoto wakali sana.Sijawahi kumuona Margreth nilikuwa namsikia tu.leo ndiyo nimemwona . Mtoto huyu anawapeleka puta watu wengi..Tuachane na hayo.Patrick unajua tuko matatizoni ndugu yangu.Jinsi mama alivyokuwa akiongea halafu agundue kuwa Happy ndiye sababu ya kuifanya safari ya London isifanikiwe sijui kama patatosha.Kwa hivi sasa hata mimi haniamini tena.anajua letu moja.” akasema Andrew.Patrick akamshika bega na kusema.“Andrew nilikutahadharisha kuwa mpango huu wa kuonana na Happy ni mgumu na ambao ni lazima utatufanya tukumbane na vikwazo vingi.Nina imani siku itakuja ndugu zangu wote watanichukia na kunitenga kabisa.Jipe moyo andrew haya ni mambo madogo tu yatakwisha”“Ok Patrick kwa sasa tuelekeze macho na akili zetu katika makutano yako na Happy huko Arusha ambako ndiko kutatoa jibu la uelekeo mzima wa suala hili.Ya hapa Dar niachie mimi nitayamaliza.Muda unakwenda sana na kwa hali ilivyo hautatakiwa uende nyumbani kwako.Itabidi tuende kwangu kila kitu kuhusu safari utakipanga pale.”‘Hapo umenena ndugu yangu.Twende haraka”Wakaingia garini moja kwa moja hadi nyumbani kwa Andrew.Baada ya kupakia nguo na vitu kadhaa vya safari wakaingia garini na safari kuelekea airport ikaanza.

* * * *

Baada tu ya kushuka ndani ya gari iliyomleta toka ofisini kwa Andrew,Margreth akakimbia kuelekea ndani.Sebuleni kulikuwa na watu mbalimbali na wote walishangaa jinsi Margreth alivyoingia kwa kasi na bila kuongea au kumsalimu mtu yeyote.Moja kwa moja alikwenda kugonga mlango wa dada yake.“Happy fungua I’m back” akasema Mlango ukafunguliwa na kitu cha kwanza ikawa ni kumkumbatiana Happy kwa nguvu.Sebuleni ndugu kadhaa walikuwa wamekaa wakijadili juu ya mwenendo mzima wa hali ya Happy .Ujio wa Margreth uliwafanya wote wastuke .Mama yao ambaye naye alikuwapo sebuleni akainuka na taratibu akaelekea chumbani kwa Happy ili kujua kumetokea nini.Akakinyonga kitasa taratibu lakini kilikuwa kimefungwa kwa ndani.Akajaribu kutega sikio ili asikie ni kitu gani walikuwa wakiongea binti zake wale wawili akashindwa kusikia lolote kutokana na sauti kubwa ya muziki waliyokuwa wameifungua.Akasimama pale mlangoni kwa sekunde kadhaa ,akatikisa kichwa na kurudi tena sebuleni.“Watoto hawa mbona siwaelewi ? najua ni lazima Margreth anajua kila kitu kinachoendelea kwa dada yake na ananificha.Lakini ngoja tuwaache kwanza wafanye mambo yao wenyewe. “Aliwaza mama yao huku akipiga hatua kuelekea sebuleni.“Happy kila kitu kiko tayari kama nilivyokueleza katika simu.”margreth akatoa tiketi ya ndege na kumwonyesha dada yake ambaye aliruka kwa nguvu na kumkumbatia mdogo wake.“Margreth thank you so much.ahsante sana mdogo wangu” Happy akasema huku machozi yakimtokaHappy akainuka na kuikumbatia picha ya Patrick ambayo walipiga wote toka kipindi wako shuleni.“Ooh Patrick nuru ya maisha yangu siamini kama nimefanikiwa kukuona tena” Akasema Happy.Margreth akatabasamu na kusema“ Happy kama nilivyokueleza nimekutana na Patrick.Imekuwa ni siku yenye msisimko mkubwa sana hasa kwa Patrick.Sikuongea naye mambo mengi kutokana na muda na vile vile sikutaka kuingia kwa undani sana katika masuala yanayowahusu wewe na yeye.Lengo kuu lilikuwa ni kuwakutanisha nyie wawili na hapo ndipo mtakapokuwa na nafasi ya kutosha kwa kila mmoja wenu kuongea na kuweka wazi hisia zenu.Patrick alilikubali wazo la kuonana na wewe kwa furaha.Nilitaka mkakutanie Morogoro lakini Patrick akakataa na kupendekeza Arusha.Nje kidogo ya mji wa Usa river kuna hoteli mpya kabisa iitwayo Kobe village.Pale ni mahala palipotulia na hakuna bugudha yoyote.Unajua kwa sasa wewe umekwisha kuwa na jina kubwa hapa nchni.Kwa hiyo wanaokufuatilia ni wengi. haya matatizo tu ya siku mbili tayari kila siku yanazipamba kurasa za magazeti.Itakuwaje iwapo utakutwa faragha na Patrick?Kwa kuliogopa hilo ndio maana tukaona ni bora mkakutane mbali na hawa wadaku.Kila kitu tayari kimekamilika na hiyo hapo ndiyo tiketi yako ya ndege.safari ni leo saa kumi na moja jioni.Patrick yeye anatangulia na ndege ya saa saba mchana huu.”Happy akamkumbatia tena mdogo wake kwa nguvu.“Sasa kazi inabaki jinsi ya kumkoroga mama mpaka akubali kuniachia. atanielewa kweli? Happy akauliza.“Fanya hivi , mwambie kwamba unaomba uende mahala ukapumzike ila usimwambie ni wapi.Mwambie unahitaji kuwa sehemu ya peke yako kwa siku kadhaa.Mama anakupenda sana na hataweza kukukatalia” akashauri Margreth“Ok ! ngoja nikamjaribu” Happy akasema huku akiinuka.“Wakati unaenda kuonana naye nenda na uso wa furaha uliojaa tabasamu ili asiwe na mashaka na wasi wasi wowote.” Margreth akasemaHappy akajiangalia katika kioo akajiweka safi akatoka chumbani na kuelekea sebuleni akiwa katika tabasamu.Mama yake akastuka baada ya kumuona mwanaye ghafla pale sebuleni tena akiwa katika hali ambayo hakuna aliyeitarajia.Happy alionekana mwingi wa furaha na uso mwangavu wenye nuru.“Ouh ! Happy mwanangu” mama yake akashindwa kujizuia akainuka na kumkumbatia mwanae kwa nguvu.Watu wote pale sebuleni wakasimama na kumwangalia Happy kwa mshangao.“Unaendeleaje mwanangu ? mama yako sili silali nakuhofia wewe” Mama yake Happy akasema.Huku akitabasamu Happy akasema“Naendelea vizuri sana mama.”“Nashukuru sana mwanangu kama unaendelea vizuri.Hapa unapotuona tuko familia nzima tukijadili juu ya hali yako na isitoshe tumekuwa katika maombi ya sala ili Mwenyezi Mungu akujalie afya njema na upone haraka.Nashukuru Mungu kwa sasa u mzima.” Akamwangalia tena usoni mwanae na kumpiga piga bega huku akisema“Mwanangu u mrembo sana”“Mrembo kama wewe mama yangu ” Happy akajibu na wote mle sebuleni wakacheka.Furaha ikatawala ndani.Chakula kikaletwa watu wakala na kufurahi.Baada ya kumaliza kula Happy akamuomba mama yake waende bustanini kwa maongezi kidogo.“mama ninashida sana na ni wewe tu ambaye unaweza kunisaidia.”Happy akasema wakiwa bustanini yeye na mama yake“Kitu gani hicho mwanangu ? Sema chochote mwanangu nitakupa” akasema mama yake.“mama nadhani unafahamu matatizo yaliyonipata.Ni wazi yameniletea athari kubwa kisaikolojia na ndiyo maana kila siku zinavyokwenda mbele ninazidi kudhoofika.Daktari wangu ameongea na Margreth na kumwambia kwamba nina tatizo la kisaikolojia.Sikuwa nimejiandaa kulitwaa taji kubwa kama hili na hivyo akashauri nipate muda mwingi wa kupumzika bila kubugudhiwa na kitu chochote.Nimekubaliana na ushauri wake ambao nina imani kwamba utanisaidia sana.Mama nahitaji kusafiri,kuwa nje na nyumbani,nje na Dar es salaam kwa siku mbili au tatu.Nahitaji kuwa peke yangu kwa siku hizo kadhaa ili niweze kuyasahau yote yaliyotokea na niweze kujiandaa vyema jinsi ya kuweza kuishi maisha mapya nikiwa kama mrembo wa Tanzania.Mama najua siwezi kuongea na baba juu ya suala hili kwani hatanielewa.Please mama naomba unisaidie sana kwa hilo.Nahitaji kuwa sawa kiakili . Taji nililonalo ni kubwa sana kwa hiyo nahitaji maandalizi ya kutosha” Akasema Happy.Maneno haya yakamfanya mama yake Happy akae kimya kwa sekunde kadhaa kisha akamwangalia mwanae usoni na kusema “Happy mwanangu,mimi mama yako kwanza nafurahi sana na kumshukuru Mungu kwa kukujalia afya njema.Huwezi kuelewa ni jinsi gani mimi mama yako nilivyokuwa naumia kila nikikuona ukiwa na hali ile ya majonzi mengi.Namshukuru sana Mungu kwa muujiza huu mkubwa alioitendea familia yetu.Siku zote yeye ndiye amekuwa ngao na kinga yetu.Happy nakubaliana na mawazo yako ya kwamba unataka kwenda mbali na hapa ukapumzike.Kwa jinsi ninavyokupenda mwanangu siwezi kukukatalia kwani ninataka siku zote uwe ni mwenye furaha na afya tele.Lakini kuna kitu kimoja kinanipa wasi wasi,mwanangu hauna tatizo lolote linalokusumbua akili ?naomba kama una tatizo nieleze mimi mama yako nitakusaidia.Usiponieleza mimi mama yako nani mwingine utakayemweleza akakusaidia?Happy akacheka kidogo kisha akasema“Mama nadhani unanielewa vizuri siku zote niwapo na tatizo mtu wa kwanza kumkimbilia ni wewe.Zaidi ya kupata ule mstuko na kupoteza fahamu sina tena tatizo lingine.Naomba uniamini mama ni tatizo hili la kisaikolojia ndilo inanibidi nipambane nalo kwa sasa.Ninaamini nitakaporejea nitakuwa mzima wa afya tele.”“Vizuri kama hayo uyasemayo ni ya kweli.Lakini Happy umenipa mtihani mgumu sana kwa baba yako.Unamfahamu baba yako alivyo mkali.Iwapo nitakupa ruhusa bila ya yeye kujua nitakuwa na wakati mgumu sana kumpa majibu yenye kueleweka.Sasa nifanye nini mwanangu? “mama usiwe na wasi wasi wowote.naomba unipe ruhusa halafu mimi mwenyewe nitaongea na baba na kumuelewesha.”
Mama yake happy akainama akafikiri kidogo kisha akasema
“Unataka kwenda wapi?
“Nje ya Dar es salaam.Sijajua bado kama niende Morogoro,Tanga .Moshi au kokote kule ili mradi iwe nje ya Dar es salaam.”“ Unakwenda na Mike?Happy anastuka kidogo kwa swali lile.
“Mike? Happy akauliza
“Ndiyo Mike” mama yake akajibu“Kwa nini umeuliza hivyo mama ? Mimi nitakuwa mwenyewe tu.Sintakuwa na mtu yeyote ” Happy akajibu.Mama yake akamuangalia usoni halafu akasema“Jana Mike alipiga simu na kuniambia kuwa leo jioni atawasili lakini alisema nisikwambie kwa sababu anataka akushangaze,ndio maana nikahisi pengine mlipanga muende wote hiyo safari”“Hapana mama mimi nitakuwa peke yangu.Yeye kama akija atanisubiri hapa hadi nitakaporudi.”
“Kwa hiyo una maana unaondoka leo hii kabla mwenzio hajafika?
“ndiyo mama.Nimekwishafanya booking ya ndege ya leo jioni inayokwenda Mwanza kupitia Morogoro na Kilimanjaro.Nitashukia Morogoro halafu toka pale nitaangalia kama nitabaki Morogoro au nitakwenda sehemu nyingine.Ninaweza kwenda Iringa au Mbeya au sehemu yoyote ile.”Happy akasema huku mama yake akimkazia macho
“Happy kwa nini umepanga safari ya ghafla namna hii? Hutaki kuonana na Mike? Unamkwepa mwenzio? Hebu niambie bila kunificha kitu kwa sababu mwenzio anakuja leo na ameacha shughuli zake huko Marekani kwa dhumuni moja tu la kuwa na wewe .Endapo hatakukuta hapa nyumbani ni wazi atahitaji maelezo ya kina na hakuna mwingine atakayempa maelezo juu yako zaidi yangu.Naomba usinifiche kitu mwanangu.Mike anakupenda na sisi tunampenda “ Happy akakaa kimya kidogo halafu akasema
“Mama naomba unielewe. Sifanyi hivi kwa ajili ya kumkimbia Mike. Ninampenda Mike kupita maelezo lakini ninafanya hivi kwa ajili yangu. After all that happened I need sometime alone.Please understand me mother” Happy akasema kwa msisitizoMama yake hakuona sababu ya kumkatalia binti yake.“Happy mwanangu mimi siwezi kukukatalia kwenda huko unakotaka kwenda.Wewe ni mtu mzima kwa sasa na nina imani kuwa kila unachokiamua hakina madhara kwako.Ila mwanangu nataka tu unihakikishie kuwa huko uendako utakuwa salama.”“mama nitakuwa salama na wala usihofu kitu chochote.Simu yangu itakuwa wazi muda wote”“Sawa mwanangu hakuna shida baba yako nitamalizana naye mimi.Kwa hiyo saa ngapi unaondoka?“Saa kumi na moja jioni.Sitaki kusafiri mapema sana kwa sababu watu hasa waandishi wa habari wananifuatilia na wanaweza wakaniharibia safari yangu..Halafu mama naomba usimwambie mtu yeyote zaidi ya baba ni wapi nimekwenda.Kwa sasa mimi ni mtu maarufu hivyo habari zangu zinauzika sana katika vyombo vya habari.Sitaki watu waniharibie mapumziko yangu.”“ Happy Nenda ukajiandae mwanangu muda unakwenda mbio“ mama yake akasema huku akitabasamu .Happy akaondoka kwa furaha kubwa.
 
10
Ni kengele ya simu ya chumbani ndiyo iliyomstua Patrick toka katika jinamizi la mawazo.Tangu amefika katika hoteli hii ya Kobe Village amekuwa ni mwingi wa mawazo .Kutokana na wasi wasi mwingi aliokuwa nao aliamua kujiliwaza kwa kunywa mvinyo laini.Aliweka chini glasi yake ya mvinyo na kuiendea simu ile ya chumbani.“Haloo” Aliita kwa kitetemeshi“Haloo mapokezi hapa.Samahani kaka mgeni wako uliyesema atawasili tayari amefika.Je utakuja kumchukua au tumlete moja kwa moja chumbani?Patrick akapumua kwa nguvu ,mapigo ya moyo yakabadilika.
“Mleteni chumbani “Patrick akasema,akaurudisha mkono wa simu kisha akapumua kwa nguvu,kijasho chembamba kilimtoka .Wakati akitafakari na kuuona huu ni kama muujiza kukutana tena na Happy mara kengele ya mlangoni inalia.Taratibu akajivuta na kwenda kuufungua.
Kwa takribani dakika kadhaa wote wawili walipigwa na butwaa kila mmoja akimshangaa mwenzake.Halafu wakakumbatiana kwa nguvu huku wote wawili machozi yakiwatoka..Muhudumu aliyekuwa ameongozana na Happy akapigwa na mshangao kwa hali ile aliyoina.Hisia za penzi zito zilijidhihirisha wazi wazi baina ya wawili hawa..Tukio hili liliamsha kumbukumbu kubwa na ya pekee maishani mwao.Hakuna aliyetaka kumwachia mwenzake.Patrick akamshika Happy taratibu na kumkalisha katika sofa lililokuwamo humo chumbani.Uso wake wote ulikuwa umejaa machozi.“I cant believe this”Patrick akanong’ona.Happy hakujibu kitu midomo yake ilikuwa ikimtetemeka.Kila alipotaka kuongea alishindwa.
“Is that you Patrick? Happy akajitahidi kusema huku akifuta machozi
“Its me Happy.Its real me” Patrick akajibu
“Ni kama ninaota.bado siamini kama nimekuona tena” happy akalalama.“Ouh Patrick..Patrick.!!..let me touch you hands and prove you are not a ghost" akasema Happy .Bado machozi yaliendelea kumtoka.”Akaushika mkono wa Patrick akautazama
" Patrick my angel..I love you so much " Aliwaza Happy huku ameushika mkono wa Patrick . Patrick alikuwa amesimama akimkodolea macho Happy asiamini alichokuwa akikiona mbele yake..Baada ya kama dakika kumi hivi za ukimya ,tafakari na hisia nzito kwa kila mmoja ,hatimaye Patrick akaufungua mdomo na kusema“Welcome back my sunshine”“Welcome back to my heart Patrick” Happy akanong’ona kwa sauti laini sana.“Huu ni muujiza mkubwa sikutegemea katika maisha yangu kama nitakuja kukuona tena.,lakini Mungu ni mkubwa na ameweza kutukutanisha tena.” Akasema patrick na kauli ile inaamsha kilio kwa Happy “Happy nyamaza usilie.Umelia vya kutosha uliponipoteza ,I’m here now.”“Patrick ninaumia sana kwa kila nikikumbuka mateso niliyoyapata kwa kukupoteza.Awali ya yote naomba unisamehe kwa yote yaliyotokea kipindi cha nyuma.Najua bado una kinyongo moyoni na hata mimi nilikuwa na fundo kubwa moyoni kwa kitendo ulichonifanyia lakini tayari nimekusamehe.Naomba na wewe utafute ndani ya moyo wako jinsi ya kunisamehe.Patrick najua ulifungwa kwa ajili yangu.Mapenzi yako makubwa kwangu ndiyo yaliyosababisha ukafungwa.Uliua kwa kuniokoa mimi nisidhalilishwe.”Happy akaangusha kilio tena.Patrick akatoa kitambaa na kumfuta machozi .“Patrick halikuwa kusudio langu mimi kwenda kusoma Ulaya na kukuacha peke yako.Nilikataa kwenda lakini ukanishauri niende kusoma kwa ajili ya kutengeneza maisha bora kwangu na kwako.Ni…….”Kabla hajaendelea simu yake ikaita.Akafuta machozi haraka haraka na kuitoa katika mkoba wake mdogo.Aliangalia namba za mpigaji na kukuta ni Mike mchumba wake.Kwa hasira akakata simu na kuizima kabisa.Patrick akakiangalia kitendo kile lakini hakukitilia maanani .“Patrick ”Happy aliita huku akimwangalia machoni.“Yes” Patrick akaitika“Ninajua itakuwia ngumu sana kwa wewe kama binadamu kunisamehe kwa kile kilichotokea,japokuwa tayari mimi nimekwisha kusamehe….”“Please Happy “Patrick akadakia.“Naomba usiseme maneno hayo tena.Yanaumiza sana.Ni kweli nilikuwa na hasira sana juu yako kwa kitendo ulichonifanyia lakini huu si muda wake kuyaongelea hayo.”Happy akamvuta Patrick karibu akamkumbatia na kumpiga mabusu mfululizo.Patrick akahisi kitu kama chaji za umeme zimepita mwilini mwake.
* * * *

Saa kumi na moja za jioni dege la shirika la ndege la British airways lilitua katika uwanja wa kimataifa wa Julius Nyerere Dare s salaam.Lango la ndege lilifunguliwa na abiria wakaanza kushuka.Miongoni mwa abiria waliokuwamo katika dege hili ni Mike cambell,kijana mtanashati mwenye kila sifa ya uzuri,ambaye kila binti amuonaye angetamani awe naye.Leo hii alivaa suruali ya jeans iliyofifia na shati zuri la mikono mifupi.Kwa ujumla alikuwa amependeza vilivyo.Mike Cambell mchumba wa Happy alikuwa akitokea Marekani .Lengo kuu la safari yake hii ya tanzania lilikuwa ni kuja kumfariji mpenzi wake Happy katika maradhi yanayomsumbua pamoja na kumpongeza kwa kufanikiwa kulitwaa taji la Miss Tanzania. Baada ya kukamilisha taratibu za uwanjani Mike akatoka na kulakiwa na dereva wake aliyetoka katika ubalozi wa Marekani.Alitegemea pengine angeweza kumuona Margreth mdogo wake Happy pale uwanjani kwa kuwa alikwisha mtaarifu juu ya ujio wake lakini mpaka anamuamuru dereva aondoe gari hakumuona mtu yeyote. Toka uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere ,safari ilikuwa ya moja kwa moja mpaka nyumbani kwa akina Happy .Anapafahamu vizuri mahala pale kwani si mara yake ya kwanza kwenda Moyoni alikuwa akiomba Mungu amsaidie aweze kukuta hali ya Happy inaendelea vizuri.Walifika nyumbani kwa akina Happy geti likafunguliwa wakaingia ndani.baada ya kushuka ndani ya gari akakutana na mama yake Happy .“wow ! Mike karibu sana” Alisema mama yake Happy akimkaribisha Mike kwa furaha..Mike akaomba maji ya kunywa ya baridi sana ili aweze kulipooza joto kubwa alilokuwa analisikia.Baada ya kunywa glasi mbili za maji akauliza aliko Happy na Margreth.Mama yake Happy akapatwa na kigugumizi cha ghafla.“Margreth amekwenda katika mizunguko yake lakini Happy yeye amesafiri kidogo”“amesafiri?? Mike akauliza kwa mshangao“Ndiyo kasafiri” mama Happy akajibu huku akijitahidi kuuficha wasi wasi aliokuwa nao “Kasafiri toka lini ?” Mike akauliza“kasafiri leo mchana”Mike akashika kichwa akapumua kwa nguvu." Mbona umestuka Mike Ina maana hamkuwasiliana akakwambia kuwa atasafiri ? mama Happy akamuuliza Mike ambaye alionyesha kuchanganyikiwa baada ya kusikia Happy amesafiri.“Hapana mama sikuwasiliana naye. Kama niivyokuwa nimekueleza katika simu sikutaka afahamu kuhusu ujio wangu.Nilitaka nimfanyie mshangazo.Lakini Margreth pia nilimtaarifu juu ya safari yangu.Happy alisema anakwenda wapi?” Mike akauliza“Hakuniambia ni wapi anakwenda .Baada ya kujisikia nafuu aliniambia kwamba amepata safari ya dharura ya kwenda nje ya Dar es salaam.Hakuniambia safarii hiyo inahusu kitu gani.Ujumbe aliouacha ni kwamba kama ukija umsubiri hadi atakaporejea nadhani mdogo wake atakuwa alimdokezea kwamba unakuja”Mike hakujibu kitu akatoa simu yake na na haraka haraka akazitafuta namba za Happy akapiga.Simu ilikuwa inaita ,akatabasamu.“Yuko hewani lakini anachelewa kupokea” alisema mikeSimu iliita bila kupokelewa.Akapiga tena mara ya pili na ya tatu na ikakatika.Akapiga tena na mara hii ikawa haipatikani kabisa .Mike akapiga tena na tena lakini jibu likawa lile lile simu haipatikani tena.“amezima simu” akasema Mike akaishiwa nguvu akakaa sofani.Baada ya dakika kadhaa za ukimya Mike akaomba aondoke akapumzike kwa sababu tayari kichwa chake kilikuwa kimevurugika.Dakika kama kumi hivi toka Mike aondoke pale nyumbani Margreth akawasili.Alimkuta mama yake akiwa amekaa sebuleni akiwa mwingi wa mawazo.“mama unaumwa? Margreth akaulizaMama yake hakujibu kitu,alimwangalia usoni kwa makini na kumuomba aketi.“Margreth hebu nieleze Happy kaenda wapi?Najua ni lazima unafahamu alikoenda dada yako”“mama mimi sijui kitu chochote.Kwani wewe alikuaga anakwenda wapi?“Hakutaka kuniambia anakwenda kupumzika wapi.Lakini wewe ni lazima utakuwa unajua kwa sababu toka ametoka hospitali ni wewe tu ambaye unaongea naye.”“Hapana mama sijui kitu chochote kile,alivyokwambia wewe ndivyo alivyoniambia mimi”“Na vipi kuhusu shemeji yako Mike? Ina maana hukujua kama anawasili leo ili uende kumpokea?“Du! mama nimesahau kabisa kama Mike anakuja leo.Vipi ameshafika?“Muda mrefu sana.Ila nyie watoto!!!Yaani mwenzenu anakuja hamtaki hata kwenda kumpokea.Halafu kitu kingine cha ajabu,amempigia simu Happy mbele yangu na Happy kakataa kupokea na mwishowe akazima simu kabisa.Hivi kuna kitu gani kinaendelea?“Mhhhh” Margreth akaguna.Akamwacha mama yake hapo sebuleni na kuingia chumbani kwake.akajifungia na kujaribu kumpigia Happy lakini simu yake ilikuwa tayari imezimwa.akajitupa kitandani.

* * * *
Saa moja na nusu jioni Andrew akiwa nyumbani kwake na mpenzi wake Vick mara simu yake ikaita.Akaichukua na kuangalia mpigaji ,alikuwa ni mama yake Patrick.Moyo ukaanza kuenda mbio.“Du! Kazi imeanza”Alisema kwa sauti ndogo ambayo Vick aliisikia.“Haloo mama” akasema Andrew“andrew mwanangu hivi huyu mwenzako ana kitu gani jamani kinachomsumbua? mpaka sasa hivi sijamuona hapa nyumbani na wala hajanipigia simu na simu yake ameizima kabisa.Nimekwenda nyumbani kwake hayupo,Veronika amekaa hapa mpaka ameamua kuondoka mtoto wa watu .Sielewi ni kwa nini Patrick anaanza kutuweka roho juu juu dakika hizi za mwisho.Maandalizi ya harusi yake yanaelekea ukingoni lakini yeye haonyeshi kujali.Hebu niambie baba ulifanikiwa kumuona?”“Mama kwa kweli nimehangaika sana na hata ofisini sijakaa kwa ajili ya kumtafuta Patrick na katu siwezi kukuficha mama Patrick sijui alipo kwa sasa.Hata mimi alinieleza kuwa ana dharura leo lakini hakunifafanulia ni dharura gani hiyo.Hata mimi nimemtafuta sana katika simu hapatikani nadhani lile tatizo la simu yake bado linaendelea” Andrew akasema“andrew na wewe usitake kuniudhi kama huyu mwenzio,usinieleze kabisa upuuzi huo wa simu.Patrick si mtu wa kushindwa kununua simu nyingine,angenieleza hata mimi ningemnunulia simu mpya.Hivi kwa nini mnataka kuzichezea akili zetu nyie watoto?“Mama naomba unipe muda zaidi mpaka kesho asubuhi nitakuwa nimepata jibu wapi alipo Patrick na nitakujulisha ikiwezekana nimlete nyumbani mimi mwenyewe”“Sawa baba jitahidi umpate kwa sababu anatuweka roho juu juu kweli huyu mwenzio.”“Ok mama nitajitahidi”“Haya Andrew usiku mwema”“Ahsante mama”Uphh.!!!!.. Andrew alipumua kwa nguvu baada ya kumaliza kuongea na mama yake Patrick“:Kuna nini andrew? Vick akauliza“Patrick haonekani”“etiii....!!! ???” Vick akauliza kwa mshangao,akainuka akashika kichwa kwa mikono yake yote miwili.“Mungu wangu ! yuko wapi sasa jamani” Vick akashangaa“hata mimi sielewi Vick .Mama yake ndiyo kanipigia simu sasa hivi anaulizia kama nimemuona”“Ina maana hujaonana naye leo?” Vick akauliza huku amemkazia macho Andrew“Nilionana naye asubuhi ya leo na toka hapo sijaonana naye tena na simu yake haipatikani.”“Hakukueleza kuwa anakwenda wapi?“alinidokeza kuwa ana dharura ila hakunifafanulia zaidi”Vick akafikiri kidogo kisha akasema“andrew ,wewe ndiye rafiki mkubwa wa Patrick.Hakuna kitu ambacho huwa mnafichana.Hainiingii akilini eti Patrick awe na dharura halafu ashindwe kukueleza .You know something..."“Tafadhali Vick nimesema sijui Patrick alipo ! Mimi kaniambia hivyo kuwa ana dharura sasa siwezi kuingilia masuala yake binafsi.Umenielewa? akasema Andrew huku akionyesha wazi kwamba hakuhitaji tena maswali toka kwa Vick.Vick akamwangalia Andrew kwa sekunde kadhaa kisha akaketi sofani.Baada ya kutafakari kwa muda Andrew akaamua kumpigia simu Veronika“Haloo shemeji” Andrew akasema baada ya Vero kupokea simu“andrew I’m confused.Ni kwa nini lakini Patrick ananifanyia hivi?Nimemkosea kitu gani hadi ananitenda hivi? Vick akasema kwa hasira “Vero,shemeji yangu hebu tuliza hasira kidogo.” Andrew akamsihi“andrew I’ll go crazy if I cant see Patrick tonight.maandalizi ya safari yamekwisha kamilika.Ni yeye tu ndiye anayesubiriwa.What am I going to do?? !!! Please Andrew help me to know where Patrick is.Hapatikani hata katika simu…”Vero akashindwa kujizuia akaangua kilio“Vero please naomba unisikilize.Mama naye kanipigia simu sasa hivi akimuulizia Patrick.Mimi nilionana naye asubuhi ya leo.mama alinipigia simu na kuniagiza niende kwake nikamueleze kuwa anahitajika nyumbani.Nilimkuta akijiandaa kutoka na akanieleza kuwa amepata dharura asubuhi hiyo hivyo angekuja nyumbani mchana.Toka hapo sijaonana naye tena.”“Ouh My God! Sasa nitafanya nini mimi ? Vero akasema“Usijali Vero bado naendelea kumtafuta na mpaka kesho nitapata jibu yuko wapi”“Jitahidi Andrew ““Ndiyo Vero najitahidi sana kuwasiliana na rafiki zetu mbali mbali ili nijue yuko wapi.Kama hatatokea hadi kesho kwa nini basi nisikusindikize badala yake ? akatania Andrew“Unasemaje????!!! Vero akauliza kwa ukali “Nasema hivi kama Patrick hajatokea mpaka kesho unaonaje kama nikakusindikiza katika safari hiyo mliyopanga kwenda wote?“Nilikuwa nakuamini sana Andrew lakini kumbe wewe na rafiki yako wote ni kitu kimoja tu”Vero akajibu kwa hasira na kukata simu.
Andrew alichanganyikiwa kwa kitendo cha Vero kukata simu.Ni wazi alikuwa amekasirika.Alijilaumu sana kwa kujiingiza katika matatizo makubwa kama haya.Kwa takribani dakika mbili nzima alibaki ameduwaa ameishikilia simu yake.“andrew kuna nini?Sauti ile ya Vick inamstua toka katika jinamizi la mawazo lililomkumba ghafla.“Hakuna kitu Vick,nilikuwa nikiongea na Vero”“Kuhusu nini?“Kuhusu safari yao ya kwenda London kufanya shopping ya harusi yao”“Yeye anasemaje ?“Hana la kufanya kwani Patrick haonekani.Mimi nilijitolea kumsindikiza”“Yeye amejibuje?“Amekasirika na kukata simu halafu ameizima kabisa”“Huna haya Andrew,eti umsindikize mchumba wa mtu London.Hivi unatumia akili kweli Andrew? Wewe ndiye mchumba wake? Hata ningekuwa mimi nisingekujibu.Tena amekuheshimu sana hakukutukana.Hebu achana na mambo ya watu tuangalie ya kwetu.”akasema VickAndrew hakujibu kitu.Akainamisha kichwa chini kwa sekunde kadhaa.“Vick I’m confused”“Kwa nini?“na hali nzima ya mambo jinsi yanavyokwenda”Vick akamsogelea Andrew akamkumbatia na kukilaza kichwa chake katika kifua kipana cha andrew .“Usijali Mpenzi Patrick atarejea tu muda si mrefu.”Vero akasema huku akiipitisha mikono yake laini mwilini mwa andrew kiuchokozi.Andrew alielewa alichokuwa akihitaji mpenzi wake.Akamuinua na kwenda naye chumbani

* * * *

Ni saa tatu za usiku katika hoteli ya Kobe Village chumba namba 68 kilikuwa na mwanga hafifu wa bluu.Sauti ya muziki laini ilisikika kwa mbali.Chumba chote kilikuwa kikinukia uturi mzuri wenye harufu ya ajabu ya kuvutia.Chumba hiki kwa sasa kilikuwa katika mkao wa mahaba mazito.Juu ya kitanda kikubwa watu wawili walikuwa wamekumbatiana wakiwa katika mahaba mazito.“Patrick” Happy akaita kwa sauti laini,nyororo ya kimahaba huku akiupitisha mkono wake kifuani kwa Patrick.
“Yes Happy “ Patrick akaitikiaHappy ambaye tayari macho yake mazuri meupe yalikuwa yamelegea kama amekula kungu akasema“Patrick najilaumu sana kwa kuamua kuondoka na kukuacha peke yako.Narudia tena kuomba msamaha kwa kitendo hiki cha kukuacha peke yako na wala sintachoka kufanya hivyo tena na tena kwa sababu ni kitendo ambacho kilisababisha mimi na wewe tukatengana.Kama nisingeondoka tungekuwa na maisha yetu ya raha mstarehe.Baada ya miaka mingi kupita hatimaye leo hii nahisi amani na raha ya ajabu.Raha ambayo nimeikosa kwa miaka mingi ile raha ya aina yake kama niliyokuwa nikiipata kipindi tukiwa shuleni.Msisimko niliokuwa nao kipindi kile pindi nikiwa karibu nawe bado haujapotea.Nikiwa nawe nahisi raha kila mahali” Patrick akatabasamu akausogeza mkono wake usoni na kurudisha nyuma nywele ndefu za binti huyu mrembo
“Happy hata mimi ninajisikia hivyo hivyo.Sikutaka kuamini moja kwa moja kuwa hauko tena maishani kwangu.Nilimuomba Mungu anisaidie ili kabla siku zangu hazijaisha hapa duniani niwe nimekuona walau kwa mara ya mwisho.Mungu amesikia sala yangu na tayari amenijibu.Leo hii niko nawe tena.” Patrick akamvuta Happy karibu zaidi na kumpiga busu zito mdomoni. " Happy nadhani ni wakati muafaka sasa wa kuongelea masuala yetu namna tulivyojikuta tukitengana" akasema Patrick.Happy akamuangalia na kusema
‘Patrick naomba niwe wa kwanza kukuuliza na tafadhali naomba uwe wazi kwangu.usinifiche kitu hata kidogo”“C’mon baby uliza chochote usihofu ,kwako hata siri za baba yangu nitakupa” akasema Patrick na Wote wawili wakacheka.“Umeshaanza utani wako nawe” akasema Happy“Usijali mama uliza”Happy akatulia kidogo kana kwamba anakumbuka kitu kisha akauliza.“Hivi Patrick ni kwa nini uliamua kunidangaya kuwa umekufa?Patrick akastuka,akainuka na kukaa kitandani jasho likaanza kumchuruzika.“What !!! .me?…Dead?…..why ? Patrick alijikuta akitamka maneno mfululizo huku akimtazama Happy..“Happy nashindwa kuelewa ,eti nilifanya nini??!!……..Happy aliuona mstuko mkubwa wa wazi katika sura ya Patrick akaanza kuogopa kwani alisikia Patrick ana matatizo ya moyo.akamsogelea akamkumbatia na kumbusu akamsugua sugua shingo na kuhakikisha ile hamaki aliyokuwa nayo Patrick imekwisha halafu akaendelea“Kama unakumbuka kipindi nimeondoka kwenda kusoma tulikuwa tunawasiliana vizuri sana.Hii ilinipa faraja na kuupunguza umbali uliokuwapo kati yetu.Lakini ilitokea siku moja ambayo kwa kweli ni vigumu sana kuisahau katika maisha yangu.Ni siku hii ndiyo iliyobadili kabisa maisha yangu,siku niliyopokea barua toka kwa dada ambaye alijifahamiha kuwa alikuwa ni jirani yenu mlipokuwa mkiishi Sumbawanga.Katika barua hiyo alisema kuwa anasikitika kunitaarifu kuwa eti umefariki dunia ukiwa gerezani kwa maradhi ya kuhara”Patrick akasimama na kushika kiuno.“Happy please tell me it’s a joke”Happy akamtazama kisha akasema.“Its not a joke Patrick.Baada ya kupata taarifa ile nilipatwa na mstuko,sikutaka kusoma tena,na wala sikuona tena faida ya kuishi.You were my everything.Kwa bahati nzuri baba na mama walisafiri haraka sana na kuja kunifariji na kunifanya niendelee kuishi kwani vinginevyo ningekwisha jiua muda mrefu.Patrick ,ilipita miaka mingi bila ya kuwa na furaha na amani moyoni mwangu.Furaha yangu ulikuwa ni wewe pekee.Nilikuwa nikiomba usiku na mchana kwamba taarifa ile isiwe ya kweli na kwamba siku moja ungejitokeza lakini siku zikaenda na hukutokea.Taratibu baada ya miaka kadhaa kupita nikakubaliana na matokeo kuwa tayari umekwisha fariki.Hatimaye baada ya kumaliza masomo nikarudi nyumbani na kitu cha kwanza kukifanya ilikuwa ni kutafuta mahala ulipozikwa.Nilienda mpaka Sumbawanga nikauliza nikaambiwa kuwa familia yako ilikwisha hama muda mrefu .Nikaenda tena kule Iringa ulikokuwa umefungwa nikaambiwa kuwa ulihamishwa gereza na kupelekwa Songea.Nikachapa mguu hadi Songea katika gereza ulilohamishiwa pale ndipo niipoufahamu ukweli.Niliwekwa wazi kuwa ulimaliza kifungo chako na ukaachiwa huru na hukufa gerezani na kwamba kuna uwezekano mkubwa ukawa mzima.Pamoja na kuufahamu ukweli huo nilikonda kwa kujiuliza swali moja nililokosa mtu wa kunipa jibu,kwa nini unifanyie vile?.Sikujua sababu ya wewe kuamua kunifanyia vile yaani kusingizia umekufa na kunifanya mimi niishi maisha ya kuteseka miaka yote hii.Nimekuwa nikimuomba Mungu anikutanishe nawe ili walau nifahamu sababu iliyopelekea unifanyie vile.Patrick you were the only man I real loved and trust.I gave myself to you .Please tell me why you did that ,I’ll understand.” Happy aliongea katika hali ya uchungu sana huku ameiweka mikono yake kifuani kuonyesha machungu aliyokuwa akiyapata Patrick jasho lilikuwa likimtiririka kama mtu aliyemaliza mbio ndefu.Ingawa chumbani mle mlikuwa na kiyoyozi lakini hakikusaidia kulipunguza joto alilokuwa akilisikia baada ya kuipata taarifa ile.Alisimama na kuzunguka zunguka humo chumbani.“Happy ! sijui hata nianzie wapi.I’m confused”Happy akamsogelea akachukua kitambaa na kumfuta jasho .
“Please tell me Patrick.Tell me everything.I’ll understand.Najua mimi ndiye sababu ya wewe kuingia gerezani na pengine hukufurahi mimi kwenda Marekani.lakini sikustahili adhabu hii uliyonipa kwa miaka hii yote ” Happy akasema kwa sauti ya upole sana“Happy sina hakika kama utaniamini na kunielewa.Ukweli ni kwamba haya yote uliyoyasema wewe kwangu mimi ni mageni kabisa.Hakuna ninachoweza kukisema au kukitolea maelezo..Niliyatoa maisha yangu kwa ajili yako ,iweje leo nikudanganye nimekufa? bado hainiingii akilini . Happy kumbuka nilikuwa radhi hata kuua japo sikukusudia kwa ajili ya upendo niliokuwa nao kwako iweje leo niamue kutunga uongo wa kututenganisha ? Nashindwa kupata jibu.Katika maisha yangu hakuna kitu ambacho sikupenda kukiona kama kukuona ukiumia na hilo unalifahamu fika.Sasa kwa nini basi niamue kuumiza moyo wako kwa kusema uongo eti nimekufa? Akasema Patrick. Akatulia akafuta jasho.Happy akalifungua sanduku lake dogo akatoa bahasha ambayo ilikwisha anza kuchakaa pengine ni kutokana na kushikwa mara nyingi sana.akatoa karatasi iliyokuwamo ndani ya ile bahasha na kumkabidhi Patrick.“Barua yenyewe yenye taarifa ya kifo chako hii hapa. hebu isome”Patrick akatumia dakika kadhaa kuisoma barua ile.Alipomaliza kuisoma akarudia tena na tena.Uso wake wote ukajaa machozi.Midomo ikawa ikimtetemeka kwa hasira,akashindwa kitu cha kuongea.“Umeona Patrick? Hivyo ndivyo ilivyokuwa.Hiyo ndiyo barua ambayo iliyabadili kabisa maisha yangu .” akasema Happy Kikapita kimya cha dakika kadhaa hapo ndani,kila mmoja akiwaza lake.Patrick akakumbuka toka siku ya kwanza alipokutana na Happy katika kituo cha basi Mbalamaziwa Iringa na hapo ndipo ulipoanzia urafiki wao.Picha za uhusiano wao wakiwa shuleni zikamjia mpaka siku ile alipomuokoa Happy toka katika mikono ya wabakaji .Akakumbuka pia siku alipohukumiwa kifungo cha miaka mitano gerezani na mpaka siku Happy aliyokuja kumuaga kuwa anakwenda Marekani kusoma.Ghafla akakumbuka siku alipopata taarifa toka kwa Veronika kuwa Happy ameolewa na hatarudi tena Tanzania.Alikumbuka jinsi alivyozimia kutokana na taarifa ile.Machozi yakamtoka.
" Vero..!! Vero.." akawaza Patrick akakohoa kidogo kisha kwa sauti yenye kitetemeshi akasema“Happy nimekusikia na nimekuelewa naomba sasa na mimi nikupe hadithi yangu.Naomba unisikilize kwa makini na unielewe”
“Baada ya wewe kwenda kusoma Marekani,huku nyuma nilihamishwa gereza na kupelekwa Songea katika gereza jipya kabisa.Siku moja nilikuwa nimepangiwa kutengeneza mazingira katika nyumba ya mkuu wa gereza.Siku hiyo mkuu wa gereza hakuwepo.Nikiwa naendelea na kazi alitokea dada mmoja ambaye alionyesha kuwa na roho ya huruma sana.Alinikaribisha chai nzuri mchana huo akanikaribisha chakula.Ni dada mcheshi,mchangamfu,na mwenye huruma.Kwa mujibu wa maelezo yake ni kuwa pale alikuwa amekuja kumsalimu mjomba wake ambaye ndiye yule mkuu wa gereza.Baadae alijitambulisha kwangu kuwa anaitwa Veronika.Taratibu mimi na Veronika tukawa marafiki.Nilimhadithia mkasa mzima wa maisha yangu kwa sababu nilitokea kumwamini.Ukiacha wazazi wangu Veronika ndiye mtu pekee aliyekuwa akinipa moyo,kunifariji na kunipa ushirikiano wa kutosha.Muda wake ulipoisha alirudi Dar es salaam kuendelea na shughuli zake aliahidi kuwa angekuwa anakuja mara kwa mara kunitazama.Kwa hiyo nikamuomba yeye awe ni kiungo baina yetu yaani mimi na wewe.Kwa kuwa yeye aliahidi kuja mara kwa mara kuniona nikaona ni bora mawasiliano yetu yaliyokuwa yameanza kufififa yawe yakipitia kwa Veronika.Nikaandika barua na kumkabidhi ili aende akaiposti afikapo Dar es salaam.Katika barua hiyo nilikutaarifu kwamba nimehamishwa gereza na kukuelekeza utumie anuani ya Veronika.Siku moja ambayo sintakuja kuisahau alikuja Vero na kuniambia kuwa alikuwa na taarifa ambazo si njema sana.Nilijikaza kiume na kumuomba anieleze.Vero aliniambia kuwa haukuwepo tena katika chuo kile ulichokuwa ukisoma.Akaendelea kusema kuwa alielekezwa mahala ulipoamia na akakupigia simu lakini ukamjibu kwa kejeli kuwa huna muda na mimi tena, na wala huna mategemeo ya kurudi tena Tanzania.Alizidi kudai kuwa alimtumia binamu yake aishiye huko huko marekani kufanya uchunguzi na akagundua kuwa tayari ulikuwa umeolewa na tayari ulikuwa ni mjamzito.Nilianguka na kuzimia Sikutaka kuamini moja kwa moja taarifa zile lakini kwa kuwa nilikuwa kifungoni sikuwa na la kufanya ili kuupata ukweli.Niliwaomba wazazi wangu wanisaidie kufanya uchunguzi juu ya jambo hili lakini wao ndio hawakutaka kabisa hata kunisikia nikilitamka jina lako .Siku zilikwenda bila ya mawasiliano yoyote baina yetu na taratibu nikaanza kuukubali ukweli kuwa haupo tena na mimi.Mpaka siku namaliza kifungo changu sikuwa nimepata barua yoyote toka kwako.Nilimaliza kifungo na nikaanza upya tena kuyatengeneza maisha yangu.Nikasoma ,nikamaliza na hatimaye nikaanza maisha yangu ya kujitegemea.Siku moja nikiwa natazama luninga ,warembo waliokuwa wakishiriki fainali za kumtafuta mrembo wa Tanzania walikuwa wakijinadi nilikuona ukipita.Sikuamini nilistuka nikaanguka na kupoteza fahamu.Na ni hapo ndipo matatizo ya moyo yalipoanza.Hakuna mtu yeyote anayefahamu nini chanzo cha maradhi yangu zaidi ya rafiki yangu wa pekee Andrew.Nilijitahidi ili niweze kukuona siku ile ya shindano lakini kwa bahati mbaya mara tu uliponiona na wewe ukapatwa na mstuko ukaanguka na kupoteza fahamu.”Patrick akanyamaza akamwangalia Happy usoni.Macho yake yalijaa machozi.Hadithi ya Patrick ilimchoma moyo sana.Donge kubwa likamkaba kooni.Hakuwa na la kufanya zaidi ya kulia.Patrick akamuonea huruma ,akamkaribia na kumfuta machozi .“nyamaza Happy .Nyamaza mrembo wangu.Usilie tena.”Ilikuwa vigumu kwa Happy kunyamaza kutokana na hasira alizokuwa nazo.“Nashindwa kunyamaza kutokana na ukatili niliofanyiwa .Kwa nini walitufanyia hivi ? Ni bora mtu aliyenifanyia hivi angeniua kabisa kuliko kuniacha nikiteseka kwa muda mrefu namna hii.”Happy akaendelea kuliaKimya kikapita .Patrick akasema“Happy tayari nimekwisha pata jibu.It is Vero who did all this.Huyu msichana anayejiita Grace ni Veronika.Nimeutambua mwandiko wake.Ni yeye ndiye aliyetutenganisha.Alifanya hivi kwa sababu anazozijua yeye mwenyewe.Nafikiri mpaka hapa hakuna wa kumlaumu mwenzake kwa yaliyotokea.Kila mmoja amekwishapata picha halisi ya nini kilichotokea.Sisiti kusema kuwa Veronika ndiye chanzo kikubwa cha sisi kutengana.Nina imani kubwa kuwa ni yeye tu ndiye aliyeuvuruga uhusiano wetu kwa kutunga uongo huu mkubwa.Hakuna mwingine anayeweza kufanya kitu kama hiki zaidi yake.Mwandiko huu katika hii barua ni wake ”Patrick akainuka na kuelekea mezani huku akiwa amefura kwa hasira.“I hate you Vero.I hate you..!!”Alitamka maneno haya kwa hasira sana .Happy aliyekuwa amekaa kitandani akaogopa.Hakuwahi kumuona Patrick akiwa katika hasira namna ile.Taratibu akamsogelea na kumshika mkono.“Calm down Patrick.Its ok.”“Happy I hate this woman so much.Ametutesa kwa kipindi kirefu sana.Kwa nini? she must pay for this.This devil must pay so dearly.Ameudhulumu moyo wangu kuishi na furaha kwa miaka hii yote.Amenisababishia mateso makubwa.Alinifanya nikakuchukia..Ouh Vero kwa nini ulifanya hivi? ” Patrick akawaza akiwa na hasira.Happy akamwacha Patrick atulie kwanza na baada ya dakika kadhaa akasema.“Patrick”Patrick akastuka na kumwangalia Happy .“Patrick” Happy akaita tena.“Yes Happy nakusikiliza”“After all that happened do you still love me?Patrick akastuka kwa swali lile,akainuka na kumsogelea zaidi Happy ,akamshika mikono yake yote miwili akamtazama usoni.“Happy ” akatulia kidogo halafu akaendelea.“World do change,weather and climate do change,people do change,everything do change but Patrick never change.I’m the same Patrick you knew,who loved you that much.Nothing has changed.Pamoja na yote yaliyotokea lakini I’ve never stoped loving you not for a second.Now that I’ve known the truth I love you even more.Do you still love me Happy?Kauli ile inamfanya Happy atoe machozi.Midomo ikamtetemeka akashindwa kuongea.Patrick akamuangalia machoni na kumuuliza tena.“Happy am I still have a place in your heart ?Happy akajikaza na kusema“Patrick you were my first man I loved.You were the fisrt man to win my heart.I gave you my heart,my body,soul and everything.You were my angel,my Hero.No body will ever win my heart than u did.I’m everything I am because you loved me Patrick. Hakungekuwa na Miss Tanzania Happy Kibaho leo kama si kwa penzi lako na kujitoa kwako kwa ajili yangu.Pamoja na yote yaliyotokea Patrick I still love you more and more.You still have chance in my heart.You are the only man that I truly love,but I’m sorry Patrick….”Happy akashindwa kujizuia kulia kwa sauti.“Sorry? Sorry for what Happy ? Patrick akauliza“Its complicated”Patrick taratibu akahisi kama nguvu zinamuisha“Complicated?How” akauliza Patrick“Patrick baada ya kuamini kuwa tayari umekwisha kufa basi nikaamua kuwa na mpenzi mwingine.Mike cambell ndiye mpenzi wangu niliyenaye kwa sasa na tayari amekwisha nivisha pete ya uchumba.I’m so sorry Patrick.Sikukusudia kufanya hivi.”Patrick alihisi kama vile kila kitu mle ndani kilikuwa kikizunguka.Hakuamini kama ni kweli anaweza kumkosa Happy kirahisi namna ile.Akaunyoosha mkono wa Happy na kuangalia kidoleni.Ni kweli Happy alikuwa na pete ya uchumba kidoleni.Patrick akaingalia huku machozi yakimlenga lenga.wakati Patrick akiwa ameduwaa akiiangalia ile pete ya uchumba kidoleni Happy akasema .“I’m right.Its complicated.Hata wewe tayari una mchumba. Kila mmoja tayari amekwisha amua kuendelea na maisha yake.Kutokana na hali ilivyokuwa hakukuwa na matumaini ya kuonana tena.Hivyo hakuna mtu wa Kulaumiwa kwa maamuzi haya kati yetu sisi wawili.Kila mmoja hakuwa na njia nyingine zaidi ya kuamua kusahau yaliyopita na kusonga mbele na maisha yake.Kwa hiyo Patrick veronica ndiye mchumba wako?Patrick akakabwa na donge kubwa kooni.akababaika ajibu nini.“Happy ” Patrick akaita
“Happy nasikitika sana.Halikuwa kusudio langu kufanya hivi lakini kwa kipindi hicho sikuwa na jinsi ya kufanya niliamini kuwa tayari ndoto yetu ya mimi na wewe kuwa pamoja imeshapotea .Niliamini moja kwa moja taarifa za vero na nikawa na hasira sana juu yako kwa kuamini kuwa ulikuwa umevunja ahadi yetu.Kweli kwa wakati huo ni Veronika pekee ndiye aliyekuwa mfariji wangu mkubwa.Ukaribu wetu ukaongezeka na taratibu tukajikuta tukihama toka katika urafiki wa kawaida na kuwa wapenzi.Kwa kiasi kikubwa alinisaidia kusahau mateso na maumivu niliyoyapata juu yako.Uhusiano wetu umedumu kwa muda mrefu sasa na tukaona ni bora tufunge ndoa kabisa.Hivi sasa tunavyoongea tayari maandalizi ya harusi yetu yako katika hatua za mwisho.Nafikiri mwezi ujao tarehe za kati kati nitafunga ndoa na vero.”Happy alishindwa kujizuia kutoa kilio kikubwa.Patrick akamkumbatia.“Patrick my first love.Patrick my angel,siwezi kuuzuia uchungu huu mkubwa ninaousikia moyoni mwangu.Ninaumia mno kwa kitendo hiki alichonifanyia mwanamke mwenzangu.Ni bora hata angeniua kabisa kuliko kunifanyia ukatili huu mkubwa.Patrick you were my life,and my breath.Veronika has taken you from me, .Sikutegemea kama mwisho wetu ungekuwa hivi..Why she did that? Why ??”Happy aliongea kwa uchungu mwingi sana huku machozi mengi yakimtiririka.“Patrick nimefurahi kuufahamu ukweli.Sikulaumu kwa yaliyotokea.Hukuwa na kosa na wala wewe hupaswi kunilaumu mimi.Kwa kuwa kila mmoja tayari amekwisha anza maisha yake mimi naona ni bora iwe hivyo.Kila mmoja atabaki ni historia kwa mwenzake.Ninachokuomba mpende zaidi Veronika.Kamwe usimfanyie jambo lolote lililo baya.Alifanya kosa,alidanganya na hii yote ni katika kulipigania penzi lako la kweli.Nakubali kushindwa.Sitaki kushindana na Vero sipendi na yeye aje aumie kama nilivyoumia mimi.Nafikiri mateso yangu ni makubwa na sidhani kama anaweza kuyavumilia kama mimi.Mimi namwachia Mungu kwani yeye………….”“Happy ”Patrick akadakia“No Patrick don’t say anything yet.I’m deeply hurt.” akasema Happy kwa uchungu mkubwa.Chumba kilichokuwa katika hali ya mahaba mazito muda mfupi uliopita ,sasa kilikuwa ni sehemu yenye majonzi makubwa.Vilio vya chini chini ndivyo vilisikika.Ilikuwa ni hali yenye kuhuzunisha sana kwa wapenzi hawa wa zamani.Happy akamvuta Patrick karibu yake akamkumbatia kwa nguvu.Akamwachia na kumtazama usoni.Kwa sauti yenye kukwama kwama huku akitokwa na machozi akamwimbia wimbo“Don’t,don’t go to your heart how feels.Don’t be afraid of dreams not real,Close ur eyes,pretend it’s just the two of us again,Make belief, this moment’s here to stay,Touch, touch me the way you used to do,I know, I could be lie right here with you,From now on ,you will be with someone else instead of me,So tonight, let’s feel these memories.So for the last, hold me now don’t cry, don’t say u were just, hold me now………Time, time will be kind once we’re apart,And ur tears, tears will no have place in ur heart.I wish I,I could say how much I’ll miss you when ur gone,All my love for yoy will go away……………Happy akashindwa kuvumilia akaangua kilio kikubwa.“No Happy !! No !……This cant be”Patrick akasema kwa hasira.
" Siwezi kukuacha kamwe.Wewe ni malaika wangu.Nakupenda sana Happy.Nakupenda zaidi ya unavyofikiri." akasema Patrick akiwa amemkumbatia Happy kwa nguvu.
" Patrick I love you too..but what are we going to do ? akazidi kulia Happy.Patrick akaendelea kumbembeleza.Happy alikuwa ameumizwa kupita kiasi.
* * * *
Ulikuwa ni usiku mrefu sana na mgumu kwa Mike cambell.Kitendo cha Happy kuondoka bila kumuaga anakwenda wapi kilimchanganya akili .Kilichompa wakati mgumu zaidi ni kitendo cha Happy kumkatia simu na kisha kuizima kabisa .Kitendo hiki kilimuumiza mno.Haijawahi kutokea katika uhusiano wao.“I real love you Happy no matter what”Alitamka Mike kwa sauti huku akijimiminia mvinyo katika glasi.Toka amefika chumbani kwake leo hii amekuwa akinywa pombe kali kwa dhumuni la kuupunguza mzigo wa mawazo aliokuwa nao.Alikaa tena sofani,akawaza,akachukua simu na kubonyeza namba za Happy lakini jibu likawa ni lile lile.Simu ya Happy haikuwa ikipatikana.“Kwa jinsi ninavyomfahamu Happy lazima kutakuwa na jambo linalomsumbua akili yake.Mara nyingi akiwa na jambo linalomsumbua huwa hapendi usumbufu.Lakini ni bora angeongea nami japo hata kidogo tu na kunitoa wasiwasi .”Mike akapiga funda kadhaa za mvinyo.“I know you need to be alone for a while Happy .I will wait here for you till you come back.I hope you will be back soon.Be safe there my angel”Mike alikuwa akiongea maneno haya kwa sauti .Ni wazi alikuwa ameanza kulemewa na kilevi.Wakati Mike akiwa katika mtihani mgumu na kuamua kupoteza mawazo kwa kunywa mvinyo mkali,mambo yalikuwa magumu zaidi kwa Veronika.Usiku huu alikuwa katika kitanda chake akijigeuza geuza, macho yakiwa makavu na mekundu kwa kulia.Akainuka na kwenda kulifungua dirisha akachungulia nje kana kwamba kuna kitu alikuwa akitegemea kukiona.Alikaa hapo dirishani kwa muda mrefu akiziangalia nyota na mwezi.Machozi hayakuwa yakitoka tena alikuwa Amelia sana mchana kutwa.Ni mlio wa simu yake ndio uliomstua toka katika mawazo mazito.Taratibu akaichukua simu yake na kutazama mpigaji.Alikuwa ni mama yake Patrick.“Hallo mama”“Veronika mwanangu unaendeleaje?“mama naendelea hivyo hivyo tu.Vipi kuna habari yoyote mpaka sasa hivi?“Hapana Veronika mpaka sasa sijapata taarifa zozote kuhusu mwenzio.Ila nina wazo moja”“Ndiyo mama nakusikiliza”“Yawezekana huyu Patrick akawa katika dharura zake kama anavyodai.Mimi naona sisi kuendelea kumsubiri ni kupoteza wakati wetu.Nionavyo mimi hataki kwenda huko Uingereza ndio maana amekuwa akikimbia kimbia.Kwa hiyo Vero mwanangu ili tusiendelee kupoteza muda zaidi wewe itakubidi tu uende peke yako ufanye shopping .Hatuna njia nyingine ya kufanya.Vumilia Vero namfahamu Patrick vizuri atatulia tu muda si mrefu.”Veronika akatulia akatafakari kwa sekunde kadhaa kisha akasema“Ok nimekuelewa mama.Nitafanya hivyo.Safari ni kesho saa tano asubuhi.Ila sintachukua muda mrefu sana nadhani baada ya siku tatu au nne nitarejea.siwezi kukaa mbali na Patrick kwa kipindi kirefu na hasa wakati huu anaoumwa umwa”“Sawa Vero nashukuru sana mwanangu kwa kukubali kufanya hivyo.Nitakuja kukusindikiza kabla hujaondoka” akasema mama yake Patrick na kukata simu.
" Patrick kwa nini unanifanyia hivi? Nimekukosea kitu gani hadi unipe adhabu hii ya kukesha macho? Nimelia machozi mengi kwa ajili yako na yote hii ni kwa sababu nakupenda sana .Nakupenda kuliko kitu chochote kile." akawaza Vero kisha akaelekea katika kabati lake kubwa la nguo na kuanza kuchagua nguo chache atakazoondoka nazo
* * * *
Hatimaye Patrick akafanikiwa kumbembeleza Happy hadi akanyamaza.Akampatia glasi ya maji na kisha akapiga magoti akaishika mikono ya Happy na kusema
“Happy ” Patrick aliita huku akimuangalia usoni binti huyu mwenye uzuri wa kimalaika.“Yes Patrick”akajibu Happy kwa sauti laini sana huku naye akimwangalia Patrick usoni.“I can’t let you go.Ulinipotea mara ya kwanza nimefanikiwa kukupata tena.Safari hii hutanipotea tena.siwezi kukuacha kamwe upotee tena mikononi mwangu .Happy I love you so much.You are the only one I truly love.The only one.Please Happy stay with me.dont leave me again.”Patrick aliongea maneno haya taratibu na kwa hisia.Ni wazi maneno haya yalitoka ndani kabisa mwa moyo wake.“Patrick hata mimi sitaki kukupoteza tena maishani mwangu.Wewe ndiye pumzi ya maisha yangu.Wewe pekee ambaye unaweza kunifanya mimi niishi kwa furaha maisha yangu yote yaliyobakia hapa duniani.Nilikupoteza mwanzo na nimekuona tena.Nisingependa hata mimi kukupoteza tena lakini…………….”“Lakini?’ Patrick akadakia“Hakuna lakini Happy .Kwa namna yoyote ile siwezi kukubali upotee tena .Wewe ndiwe mwanamke pekee niliyekupa moyo wangu.Because I love you Happy , I will make a sacrifice for you.”“Sacrifice?? Happy akauliza kwa mshangao.Patrick akamtazama usoni na kwa sauti ya upole akasema “Yes Happy .Ninaifuta ndoa yangu na Veronika.Sintamuoa Veronika tena”“Patrick!!!!!!!.......Happy akasema kwa mshangao.
“Patrick please usifanye hivyo.Nakuomba Patrick niko chini ya miguu yako usifanye hivyo.Najua unanipenda na penzi lako kweli ni la dhati na la kweli lakini Patrick tumekwisha umia vya kutosha.Naomba tuendelee kuumia sisi wenyewe na tusiwaumize tena watu wengine zaidi.Kufuta ndoa yako na Vero ni suala rahisi kwako lakini so many people will get hurt.Watu wengi wataumia sana.Suala hili linagusa watu wengi sana .Patrick Vero loves you very much and Mike loves me very much.We cant hurt the people who loves us.Patri…….”“Happy ”Patrick akadakia.“Please naomba unisikilize kwa makini sana.Najua kwamba uamuzi huu utaumiza watu wengi sana.Ndiyo ni wengi wataumia na kuhuzunika lakini sina namna nyingine ya kufanya zaidi ya hivyo nilivyokwambia.Siwezi kuendelea kujidanganya kwamba nitaishi kwa furaha na amani na Veronika wakati nikijua kuwa upo na bado unanipenda.Siwezi Happy kuendelea kuwa na Veronika mtu aliyetufanyia ukatili mkubwa sana .Niko tayari kuubeba mzigo wote wa lawama na kila kitu kwa ajili ya kuitafuta furaha ya maisha yangu.Nilifungwa kwa ajili ya kuzuia usidhalilishwe kwa hiyo sioni ajabu leo hii nikivunjilia mbali ndoa yangu na vero chui mwenye ngozi ya binadamu.Alitufanyia ukatili mkubwa sana.Hastahili kabisa kuwa na mimi ” akasema Patrick.Happy ambaye bado machozi yalikuwa yakimtoka alijikaza na kusema.“Patrick ninajua una nia nzuri na mimi na uamuzi huo ni wazi umetoka ndani kabisa mwa moyo wako.Hata mimi Patrick ninaumia sana tena zaidi hata ya siku ile nilipopata taarifa zile za kufariki kwako.Ninaumia kwa sababu sijui nifanye nini ili usiende mbali na mimi tena.Lakini Patrick tayari nimempa nafasi Mike .Nilifanya vile kwa sababu nilihitaji kuwa na mtu baada ya kuamini haupo tena duniani.Pamoja na nafasi hiyo lakini nafsi yangu imekuwa nzito katika kumpa moyo wangu wote aumiliki kama nilivyofanya kwako.Bado nafsi yangu inaugulia kwa ajili yako.lakini Patrick…………………”Happy akashindwa kuendelea kuongea akainama akiliaPatrick akamshika shingoni na kumwambia“Lakini nini Happy ?“Patrick tayari hatua kubwa sana zimeshapigwa katika mahusiano yetu mapya.Naomba Patrick tusiendelee kuwaumiza watu wengine tena wanaotupenda.Naomba usimuache Vero kwa ajili yangu.Sijui kama nitaweza kuachana na Mike kwa sababu ananipenda kupita kitu chochote”Patrick akamtazama Happy kwa sekunde kadhaa kisha akasema“Happy please look at me.Look at me and tell me that you don’t love me any more.I will understand and let you go.”Happy akainua uso wake na kumtazama Patrick .“ooh Patrick please don’t leave me.I love you so much”Happy akajikuta akijilaza kifuani kwa Patrick na kumkumbatia kwa nguvu.“patrick I love you so much.Please Patrick don’t ever leave me again.”“Its ok Happy it’s ok my angel. I won’t let you out of my hands again”Happy akamkumbatia kwa nguvu zaidi Patrick .Taratibu Patrick akaanza kuzichezea nywele nzuri na ndefu za Happy .Mkono wa kulia ukashika hadi shingoni na kuisugua taratibu kisha kwa pozi za aina yake ukashuka kuelekea mgongoni ukipita kati kati kabisa ya mgongo kana kwamba anapiga kinanda.Happy akastuka.“ouh Patrick I love you.” akasema Wakatazamana na taratibu sana kama inavutwa na sumaku midomo yao ikaanza kukaribiana na mara ikakutana na zoezi tamu la kunyonyana ndimi likaanza.‘ouh Patrick my baby don’t ever leave me again” alisema Happy kwa sauti ya kuhema Patrick hakusema kitu taratibu akaanza kufungua vifungo vya shati alilokuwa amevaa Happy akalitoa na kulitupa pembeni.Moyo ukazidi kumwenda mbio baada ya kukutana na kifua kile cha Happy chenye kusisimua.Hakutaka kuwa na papara kwani tayari alijua kila kitu ni chake kwa usiku huo.Akampiga busu zito mdomoni kisha akaifungua sidiria nyeupe aliyokuwa ameivaa Happy akakutana na chuchu nzuri za mlimbwende huyu ambazo zikazidi kumpa wazimu .Kwa ufundi wa aina yake akaanza kuzinyonya chuchu zile huku Happy akitoa miguno kwa raha alizozisikia.Wakati akinyonya chuchu zile mkono wake wa kulia ukawa ukiifungua zipu ya sketi fupi aliyokuwa ameivaa Happy akafanikiwa kuifungua na taratibu akaishusha chini.Happy alikuwa amezidiwa na utamu na hata maneno aliyokuwa akiyatamka yalikuwa hayasikiki vizuri.Taratibu Patrick akaanza kushuka chini mpaka maeneo ya kitovuni na halafu chini yake zaidi.Mambo aliyoyafanya hapo siwezi yaelezea.Happy alikuwa akitoa miguno kana kwamba anataka kufa.“Patrick I…It’s..my first…time don’t hurt me.”Happy akasema kwa sauti yenye kukwama kwama.Happy hakuwahi kukutana na mwanaume yeyote kabla.Patrick alistuka kusikia hivyo.Hakutegemea kama msichana mzuri kama Happy angeweza kuutunza usichana wake mpaka wakati ule.Kwa kuwa ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Happy ,Patrick akapunguza kasi na kwenda taratibu ili mrembo huyu asiumie.
********
Ni saa nne asubuhi siku iliyofuata wakati Mike Cambell aliposimamisha gari nyumbani kwa akina Happy .Moja kwa moja akafululiza mpaka ndani na kumkuta mama yake Happy .‘ Mike karibu baba” akasema mama yake Happy“Ahsante mama shikamoo”“Marahaba mwanangu,karibu sana”“Ahsante mama.Kuna taarifa zozote za Happy ?“Hapana baba mpaka sasa hivi hatuna taarifa zozote za Happy .Bado simu yake haipatikani.Vipi wewe una taarifa zozote ?“Hapana mama .Bado sijapata hata ujumbe wowote toka kwake”“Jamani mtoto huyu kwa nini lakini anafanya hivi?“Mama,nafikiri labda tuwe wavumilivu ,tumwache kidogo pengine ni wazi anahitaji kuwa peke yake kwa kipindi hiki.Nina imani huko aliko yuko salama salimini na ni lazima atarejea salama”Mike akasema lakini ni moyoni alikuwa akiumia sana.“Nashukuru sana baba kwa kuwa mwelewa.Mimi mara nitakapopata taarifa yake nitakutaarifu mara moja”“Sawa mama nashukuru”Mike aliaga na kuondoka.Mama yake Happy alilisindikiza gari lile la Mike kwa macho mpaka likapotea kabisa.Alipogeuka akakutana na Margreth.“ Mike anasemaje? Margreth akaulizaMama yake akamtazama kwa sekunde kadhaa“Hivi nyie watoto kwa nini mnamfanyia hivi mwenzenu?“Mwenzetu yupi mama?”Si Mike? Hivi hamuoni kuwa mnavyomfanyia si vizuri? Happy hataki kuwasiliana naye ,hata wewe unamkwepa shemeji yako.Kwa nini lakini?Margreth hakujibu kitu akatazama chini“mama mi naogopa hata kumwangalia kwa sababu atahisi ni lazima ninajua Happy yuko wapi”“Mhhh!!!! …….haya” Mama yake akaguna na kuondoka


11

SIKU NNE BAADAE - ARUSHA
“Happy malaika wangu ni siku ya nne leo tangu tumefika hapa Arusha.Najua ni lazima huko tulikoondoka watakuwa na wasi wasi mwingi kwa sababu tangu tumefika hapa simu zetu zote tumezima.Nimefikiria nimpigie simu mama yangu ili nimtoe wasi wasi." akasema Patrick.Happy aliyekuwa amejilaza katika kiti kilichokuwa pembezoni mwa bwawa la kuogelea ,alimtazama Patrick kwa sekunde kadhaa kisha akasema.“Ok Patrick ,ni wazo zuri ,ingawa mimi sikuhitaji kufanya hivyo kwa sasa lakini kwa vile umeomba basi hata mimi itanibidi nifanye hivyo.”Wakainuka na kuelekea chumbani kwao.Patrick akaishika simu yake akaitazama kisha akaiwasha.Jumbe fupi za maneno zikaingia mfululizo .Hakusumbuika nazo moja kwa moja akazitafuta namba za mama yake na kumpigia.“Haloo mama shikamoo” Akasema Patrick baada ya mama yake kupokea simu“ Patrick hujambo? Uko wapi we mtoto,mbona unatuweka roho juu namna hiyo?Hatulali tunakuwaza wewe,Vero anapiga simu usiku na mchana kukuulizia,Uko wapi na unafanya nini Pat…..” Patrick hakutaka kumpa mama yake nafasi kubwa ya kuongea,ikamlazimu kuingilia kati.“Mama us……………..”Kabla hajaendelea mama yake naye akadakia“Baba yako kawa mbogo huku ,kila siku tunakwaruzana kwamba mimi na wewe letu moja.Sasa ni lini unarudi Patrick?“Mama usijali,mimi ni mtu mzima na ninajua kitu ninachokifanya.Watoe shaka watu wote mimi niko salama salimini na muda wowote nitakuja nyumbani.Ni kama nilivyokueleza nilipatwa na dharura ndo maana nikaondoka ghafla vile.”“lakini Patrick mwanangu hivi hizo dharura zako ni muhimu kuliko suala la ndoa yako? Hivi hizo dharura zina msaada gani katika ndoa yako?Angalia mwanangu harusi ni mwezi ujaona kikao cha mwisho ni wiki ijayo kisha ndoa ikaandikishwe kanisani na kuanza kutangazwa.Sasa huoni kuwa unahitaji kuwa karibu sana kwa wakati huu?“Nalielewa hilo mama na mojawapo ya mambo yaliyonileta huku ni kuhusiana moja kwa moja na hiyo harusi yangu,hivyo usijali mama,ila tafadhali naomba kikao cha mwisho kisikae kama nitakuwa sijarudi.nataka niwepo katika kikao hicho nina jambo kubwa la muhimu sana la kuongea na kamati nzima pamoja na nyie wazazi wangu,wataarifu pia wazazi na ndugu wa karibu wa Veronika"Mama yake Patrick akanyamaza kidogo kisha akastuliwa na Patrick.“Mama naomba nikate simu .wasalimu wote hapo nyumbani ila tafadhali naomba unifikishie ujumbe wangu huo kwa kamati. Bye mama.I love you.” Patrick akakata simu kisha akapumua kwa nguvu.“Darling kuna tatizo lolote? Happy akauliza baada ya kumuona Patrick akionekana kuzama katika mawazo ghafla.“Hapana dear hakuna tatizo lolote,ngoja kwanza niongee na Andrew”Patrick akazitafuta namba za Andrew na kumpigia.“Yes Comrade” Aliita Patrick baada ya simu kupokelewa na Andrew .“wow!Patrick how are you?“I’m fine andrew”“hahaha ! mambo yanakwendaje hapo Arusha brother kwa sababu naona umekaa kimya sana.Najaribu kukutafuta lakini simu yako haipatikani kabisa ..”“ Andrew huku ni burudani kila sekunde,.Tayari tumeshamaliza matatizo yetu na kwa sasa tumeazimia tunaanza upya.”“Wow! That’s great news ”Akasema Andrew“sasa andrew sina muda muda mrefu sana wa kuongea na simu hebu nipe japo kwa muhtasari juu ya hali ya mambo yanavyokwenda hapo Dar.Nimetoka kuongea na mama sasa hivi anapiga kelele hadi nikakata simu” akasema Patrick.“Patrick huku mambo yanazidi kupamba moto.Maandalizi yanaendelea kwa kasi ya ajabu.Kadi ziko tayari na kinachosubiriwa ni kikao cha mwisho cha kamati ya maandalizi kikae ili kuangalia kama kuna kitu kilichobakia .Vero alienda Uingereza peke yake japo kwa shingo upande na kila siku ananipigia simu kama ninataarifa zako zozote.Watu wanahaha kutaka kujua uko wapi .Ninapata shida sana manake kila mmoja anajua kuwa ni lazima nitakuwa ninajua mahala ulipo.”“du ! pole sana Andrew.I’m very sorry to involve you in this..Nakuomba uwe mvumilivu rafiki yangu bado yatakuja makubwa zaidi ya hayo.Mimi nitarudi muda wowote kwa sababu nataka niwepo siku kikao cha mwisho kitakapokaa.Nina mambo ya kuongea na wazazi na wanakamati .Kwa sasa bado ninaendelea kula bata na mrembo wangu” akasema Patrick huku akicheka “Sawa Patrick mimi nitafanya kila linalowezekana kufanyika.”“Ok andrew nitakuwa nakupigia mara kwa mara ingawa muda mwingi simu yangu itakuwa imezimwa.”“Ok brother take care”Patrick akakata simu na kumwangalia Happy .“Mbona Vero humpigii simu?“ forget about her”Akasema Patrick huku akimpa simu Happy ‘Ongea na mama mtoe wasi wasi najua atakuwa na wasi wasi mwingi juu yako kwani toka umefika hapa hujawasiliana naye na kumjulisha unaendeleaje”Happy akaandika namba za simu za mama yake na kupiga“Haloo mama shikamoo” akasema Happy baada ya mama yake kupokea simu.“ Happy .Hujambo mwanangu?“Sijambo mama vipi hapo nyumbani wazima?“Huku wote wazima Happy ,roho zetu juu juu kwa sababu yako.Lini utarudi? Na mbona simu yako haipatikani?“Mama msiwe na wasi wasi mi ni mzima kabisa na muda wowote ninaweza kurudi nyumbani.Simu yangu nimeizima kuepuka usumbufu wa watu ”akasema Happy“Sawa Happy mi nafurahi kusikia uko salama.lakini ni kwa nini hutaki kumpigia simu Mike? Tayari amekuja na anaumia sana moyoni kwa kukukosa.Hivi unajua ni kwa kiasi gani unavyomtesa mwenzio?. mwenzio katoka Marekani kuja kukupa hongera kwa ushindi wako lakini wewe ndiyo kwanza hata kumuona hutaki kwa nini lakini Happy ?Happy akapatwa na kigugumizi cha ghafla akashindwa ajibu nini akanyamaza kimya kwa sekunde kadhaa.“Happy nakuuliza kwa nini unamfanyia hivyo mchumba wako? Mama yake akaendelea kuhoji“Mom please I have to go,bye”Happy akaikata simu na kumpa Patrick ambaye aliizima kabisa.Patrick alikwisha ng’amua kuwa mambo katu hayakuwa mazuri kwa Happy .“Happy my baby” Akasema Patrick huku amemshika Happy mkono“Calm down my sweet love.This is just the beginning .You have to be strong”Kikapita kimya kifupi halafu Patrick akauliza“Mama alikuwa anasemaje?“Alihitaji kufahamu nitarudi lini na ni kwa nini siwasiliani na Mike.Patrick nilikubali kumpa moyo wangu Mike kwa sababu kwa wakati huo nilijua tayari umeshafariki.Laiti ningelijua kuwa bado upo hai nisingempa moyo wangu Mike.Lakini kwa vile tumeshaonana na wewe ndie mwanaume pekee nikupendaye duniani,basi sina budi kuwa wazi kwa Mike.It hurts lakini sina jinsi ni lazima nimweleze ukweli.Patrick ulinipotea mara ya kwanza lakini safari hii hutaweza kunipotea tena.I’ll fight for you” akasema Happy akiwa amekumbatiana na Patrick.
* * * * “MISS TANZANIA ATOWEKA NYUMBAN….,MREMBO WA TANZANIA ATOROKA….HAPPY KIBAHO HAJULIKANI ALIPO…..WASI WASI WATANDA JUU YA AFYA MISS TANZANIA ,MASKINI MISS TANZANIA…Hivi ni baadhi tu ya vichwa vya habari ambayo vilikuwa vikipamba kurasa za mbele za magazeti hasa yale ya udaku yenye kuandika sana habari na vituko vya watu maarufu..Magazeti mengi yaliandika habari nyingi zinazohusiana na kutoonekana hadharani kwa mrembo mpya wa Tanzania,Happy kibaho lakini hakuna hata gazeti moja ambalo lilikuwa na taarifa za ukweli juu ya wapi alipo .
Wakiwa bado Arusha Patrick na Happy waliyasoma magazeti yote na kila kilichoandikwa ,wakacheka sana.“Umekuwa maarufu sana kwa sasa” Patrick akasema“Hiz ndizo karaha za kuwa maarufu.!!’ Akajibu Happy“Na huu ni mwanzo tu Happy bado watakufuatilia sana katika kila jambo unalolifanya.Kila utakachokifanya itakuwa ni biashara kwao.Unatakiwa uwe jasiri na hasa katika hiki kizungumkuti kilichoko mbele yetu,mengi yatasemwa na mengi yataandikwa.Ningependa sana uwe mrembo mwenye sifa nzuri kama Nancy sumari,kama Hoyce Temu.Katika vipindi vyao vya kuvaa taji la miss Tanzania hawakuwa na kashfa yoyote ile iliyoyachafua majina yao.Nitafurahi ikiwa utafuata nyendo zao.” Akasema Patrick“Nakuunga mkono Patrick ,unajua Nancy ndiye aliyenivutia mimi mpaka nikaingia katika fani hii ya urembo.Nampenda na nitafurahi sana kama nitafanikiwa kuwa kama yeye yaani kumaliza kipindi cha kulivaa taji hili bila kuwa na skendo yoyote mbaya katika jamii” akasema Happy wakakumbatiana na kucheka.“Happy darl kuwa nawe hapa najiona ni kama vile ninaishi mbingu ya saba mbali na matatizo lukuki ya dunia hii.Laiti kama maisha yetu yangeendelea namna hii,kuishi kwa raha away from all troubles lakini ninasikitika sana kwamba inatubidi turejee Dar.Nina imani kila mmoja wetu anafurahia sana kuwepo hapa lakini hatuwezi kukaa hapa kwa muda mrefu kwa sababu bado tuna majukumu mengine ya kufanya huko tulikotoka na kubwa zaidi ni hili suala letu.Kikao cha mwisho cha harusi yangu kinakaribia hivyo inanibidi niwepo kabla ya kikao hicho na kuweka kila kitu bayana na hatimaye kuuvunja rasmi uchumba wangu na Vero kisha niufungue ukurasa mpya wa maisha yangu ya furaha nikiwa na wewe malaika wangu.Halikadhalika wewe pia unatakiwa uende nyumbani kabla Mike hajaondoka na kufanya kama tulivyokubaliana yaani kuachana na wapenzi wetu wa sasa na kuyaaza maisha mapya.”akasema Patrick“ Kweli kabisa Patrick hata mimi nilikuwa na wazo hilo hilo.Hatuwezi kukaa hapa kwa muda mrefu sana wakati kuna jukumu zito linatukabili mbeleni.Ni wazi tunatakiwa kurudi dar.I’m some how scared ” akasema happy.Patrick akamtazama kisha akatabasamu na kusema
“ Usihofu kitu malaika wangu..kuwa jasiri hakuna kitakachoshindikana” akasema Patrick“Kuhusu usafiri usihofu,nitaongea na Andrew atatutumia gari la kuja kutuchukua hapo kesho..”
* * * *
Saa kumi na dakika saba za jioni gari moja yenye vioo vyeusi ilifunga breki mbele ya lango la nyumba ya akina Happy .Mlango wa kulia ukafunguliwa akashuka Patrick akazunguka na kuufungua mlango mwingine akashuka mrembo mpya wa Tanzania Happy kibaho.Tayari walikwisha wasili Dar es salaam wakitokea Arusha.Kwa takribani dakika tano hivi walizitumia kuagana kisha Patrick akaingia garini na kuondoka.Happy alibaki amesimama pale huku akiupunga mkono wake ,hadi gari lilipopotea kabisa machoni pake“I looo…..oove…uuuuuu….Pa…aaa.tri…ck…..”Alisema Happy huku machozi yakimlenga ,mara geti likafunguliwa akatoka mtumishi wa ndani.“wow! Dada Happy …..!!!”Happy akastuliwa na sauti ile kugeuka akakuta ni Christina .‘wow Tina”Wakakumbatiana kwa furaha .Tina akamshika Happy mkono na kumuongoza mpaka ndani.Huko ndani ilikuwa ni furaha isiyo na kifani ,kila mtu aliruka ruka na kushangilia kwa nguvu Happy kurudi tena akonekana ni mwenye furaha sana..“Karibu sana mwanangu”Akasema mama yake“Ahsante mama nimeshakaribia”“habari za huko utokako”“huko kwema mama,sijui nyie hapa”“Sisi huku wote wazima kabisa ila hofu yetu kubwa ilikuwa kwako.Tunashukuru Mungu umerudi salama.”“Hata mimi nashukuru sana mama kama nyote mu wazima.I missed you all so much”Kisha salimiana Happy akaenda kuoga halafu akajifungia chumbani kwake akaiwasha simu yake na kujilaza kitandani akaanza kutafakari jinsi atakavyoweza kuachana na mchumba wake Mike cambell.Kabla hajaanza kuwazua ni nini afanye simu yake ikaita.Akaichukua na kuangalia ni nani mpigaji akakuta ni Patrick,Happy akatabasamu .“Haloo my sweet love” akasema Happy“Haloo darling vipi umepumzika?“Yes Patrick nimejipumzisha kitandani” akajibu Happy huku akitabasamu“Ouh my love I’ve missed you arleady ” akasema Patrick“mhh Patrick jamani hata masaa mawili hayajapita..!! Happy akasema huku akitabasamu“Yeah I miss u a lot already.I miss you each second Happy ”“Hahahahahaa….Mwaaaaaaa.I love you Patrick” Happy akasema kwa furaha“I love you too Happy ”“Ok my baby boy ngoja mi nipumzike tutawasiliana baadae.” Akasema Happy“Ok Happy mimi ndo najiandaa niende kwa andrew kisha nitapita nyumbani nikamuone mama.Ntakupigia baadae ”“Ok love.Take care” akasema Happy.Baada ya kukata simu Happy akaendelea kuitazama simu ile huku akitabasamu.“Mhh ! kila ninapoisikia sauti ya Patrick nahisi mwili wote unanichemka.I love him so much,and I’ll do anything for him”
Wakati akimuwaza Patrick mara sura ya Mike ikamjia akilini Happy akashindwa kujizuia akaangusha machozi.“I’m sorry Mike but I have to do this.Lazima nirudiane na Patrick .yeye ndiye furaha ya maisha yangu.”Akachukua simu yake tena na kuzitafuta namba ambazo Mike huwa anazitumia pindi awapo Tanzania akapiga.“Hallow baby”ilikuwa ni sauti ya upole ya Mike cambell.“Hallow Mike how are you”“ Happy unajisikiaje sasa hivi? Akauliza Mike“Najisikia vizuri Mike,nashukuru sana kwa kuja kunitazama”“Nashukuru hata mimi kama umerudi salama.Nilipata taarifa za ushindi wako na ghafla nikapata taarifa nyingine kuwa ulipoteza fahamu baada ya kutangazwa mshindi.Pole sana haya ni mambo ya kawaida.Nililazimika kuomba dharura ya wiki mbili ili nije kukaa nawe kwa kipindi hiki ambacho najua unanihitaji sana,lakini nilipofika mama akaniambia kuwa umesafiri kidogo nje ya Dar es salaam .Sikutaka kukusumbua kwani nilijua unahitaji kuwa peke yako kwa kipindi hicho.Nafurahi umerudi salama” Mike akasema“Mike naomba unisamehe kwa kutowasiliana nawe .Mambo mengi yalinitokea hivyo nilihitaji kuwa peke yangu.Samahani sana kwa hilo”“Usijali Happy nalitambua hilo na kuyaheshimu maamuzi yako.dont worry I’ll always be there for you my sweet baby.All I want is you to be happy.My love I want to remind you that anytime you need a shoulder to cry on just count on me.I’m here for you”Maneno haya yakamchoma sana Happy na kujikuta akitokwa na machozi ,alishindwa ajibu nini ,mara akastuliwa na sauti ya Mike.“Happy niko njiani nakuja nina hamu sana ya kukuona na kukupa pongezi zangu na kama utakuwa unajisikia vizuri basi tunaweza kutoka out kwa ajili ya dinner.” Happy akastuka na kuwaza kwa sekunde chache kisha akasema “Thanx Mike,nashukuru sana lakini najisikia kichwa kinaniuma mno.Nadhani nahitaji kupumzika Unaonaje ikiwa tutaonana siku ya kesho?“Ok Happy kama umeamua hivyo basi vizuri.Jiandae kesho tutoke kwa chakula cha mchana .”Mike alisema kwa sauti ambayo ilionyesha dhahiri kuwa hakuwa ameridhika na maamuzi yale ya Happy .“sawa Mike nashukuru sana ,tuonane hiyo kesho”“Ok Happy have a nice eveing.I love you………………..”Happy akashindwa atamke nini ,midomo ikawa mizito machozi yakimtoka.Akakata simu na kujitupa kitandani.“Mike I’m sorry.” Akasema huku amekishika kichwa kwa mikono yake


* * * *

“Hello Komrade” Andrew akasema kwa furaha huku akimkumbatia rafikiye Patrick kwa furaha mara baada ya kufungua mlango na kumkuta amesimama mlangoni
Andrew akaushika mkono wa patrick akauinua kidogo na kuuminya halafu akacheka kicheko kikubwa.
“Brother naona mambo ya Arusha hayakuwa madogo.Siku hizi chache tu naona hata mwili umeongezeka. “
Wote wakacheka na kuketi sofani.Andrew ambaye ndiyo kwanza alikuwa amerejea toka katika shughuli zake,akaelekea jikoni kisha akarejea s na chupa kubwa ya mvinyo.
“Nashukuru umerudi salama.Hamkupata tatizo lolote njiani?”
Akasema Andrew huku akiweka chupa ile mezani na kuumimina mvinyo katika glasi akampatia Patrick glasi moja.
“hatukupata tatizo lolote njiani.Nashukuru yule dereva uliyemtuma ni mahiri mno.” Patrick akasema kisha akanywa funda moja.
“Kaka nipe habari za Arusha.Mambo yamekwendaje? Happy hajambo? Andrew akauliza huku akitabasamu baada ya kupiga funda la mvinyo.Patrick naye akainua glasi yake akapiga funda moja halafu akalegeza tai yake na kusema
“Andrew namshukuru Mungu kwa sababu mambo yaliyotokea Arusha sikuyategemea kabisa.Ndugu yangu sikufichi nilikuwa najihisi kama niko peponi kwa raha nilizokuwa napata .Kama isingekuwa ni masuala haya ya harusi nisingerejea mapema hivi.” Patrick akanyamaza na kunywa tena funda la mvinyo halafu akaendelea
“Happy alifika Arusha kama tulivyopanga.Mara tulipokutanisha macho nilihisi kama ninapaa kwa furaha niliyoipata.Sikuwa nimetegemea kama ningekuja kuonana tena na Happy maishani.Tulikuwa na maongezi marefu sana siku hiyo.Tulikumbushana toka siku ya kwanza tulipokutana ,mambo yote yaliyotokea hadi siku niliyoingia gerezani.Happy alilia sana.Tulikumbuka mambo mengi mno.Tulikumbuka nyakati zetu za furaha na hata nyakati zile tulizokuwa katika wakati mgumu na hasa wakati ule tuliposimamishwa shule kwa kosa la kupigana darasani halafu tukaenda kujificha Bagamoyo ambako ndiko penzi letu lilikoanzia.” Patrick akanyamaza akanywa tena funda la mvinyo halafu akaendelea na maongezi.Andrew alikuwa kimya akimsikiliza.
“Andrew mambo yaliyotokea huko ni makubwa na ya kushangaza sana”
“Patrick hebu niambie ,mambo gani hayo yaliyotokea huko? Nina hamu ya kutaka kufahamu kilichoendelea huko Arusha” Andrew akasema huku akiifungua tai yake na kuitupa pembeni.
“we real had a great time”
“Usiku wa siku ile ya kwanza happy aliniuliza kitu ambacho kilinistua na kunishangaza sana.Aliniuliza eti ni kwa nini niliamua kumdanganya kwamba nimefariki dunia wakati ningali hai? “
“Etu ulifanya nini !? Andrew akauliza kwa mshangao
“Anadai nilidanganya kwamba nimefariki dunia”
“ Umefariki dunia ! How “ andrew akahoji.
“ Subiri ntakusimulia” akasema Patrick
“ wewe ukamjibuje?
“Kwanza swali lile lilinistua sana japokuwa hata Margreth alikwisha nidokeza kuhusu kuwepo kwa jambo hilo la mimi kudai nimefariki dunia.Nilimtuliza na taratibu nikamuomba anielezee kwa undani kuhusiana na mkasa ule kwa sababu mimi ndiyo kwanza niliusikia.Alianza kunieleza kwamba akiwa chuoni alipokea barua toka kwa mtu ambaye alijitambulisha kwamba ni mtu anayenifahamu mimi na familia yangu na kwa kuwa anaufahamu uhasiano wetu aliamua kumpa taarifa ambazo hazikuwa nzuri hata kidogo.Mtu huyo aliyemuandikia barua hiyo alidai kwamba Patrick yaani mimi ,nilifariki kwa ugonjwa wa kuhara nikiwa gerezani.Nikinukuu maelezo yake anasema kwamba almanusura ajitoe uhai baada ya kuipata taarifa ile kwa sababu hakuona ni namna gani angeweza kuishi bila mimi.Ilimchukua muda mrefu sana kukubaliana na ukweli kwamba nimefariki.Baada tu ya kumaliza masomo yake alirudi nchini na kitu cha kwanza alichokifanya ni kuanza kutafuta mahala nilipokuwa nimezikwa.Alikwenda hadi Sumbawanga ,mahala tulikokuwa tukiishi kabla ya baba hajahamishwa akaambiwa kwamba familia yangu ilihama kitambo.Toka Sumbawanga akaenda hadi Iringa katika gereza nililoanza kutumikia kifungo akaambiwa kwamba nilihamishwa pale gerezani na kwenda Songea nikiwa mzima wa afya.Hakukata tamaa akaenda tena hadi Songea ambako taarifa aliyoipata ilisema kwamba nilimaliza kifungo changu na kufanikiwa kutoka gerezani salama salimini.Majibu haya yalimpa wakati mgumu sana na kumfanya azidi kuchanganyikiwa kwani aligundua sikuwa nimefariki .Kwa mujibu wa maelezo yake,siku ile aliposhinda taji la Miss tanzania alipoteza fahamu baada ya kuiona sura yangu.Hakuamini kama kweli ni mimi au ni mzuka anaouona” Patrick akanyamaza ,akamtazama rafiki yake aliyekuwa kimya akimsikiliza
“Enhee ikawaje baada ya hapo? Andrew akauliza
“baada ya hapo ikanibidi na mimi nimweleze ukweli kwamba nilipokea taarifa toka kwa Vero niliyekuwa nikimtumia kama kiungo cha mawasiliano baina yangu na Happy .Taarifa hiyo ilisema kwamba yeye Happy amepata mchumba wa kizungu na tayari ana ujauzito na kwa sasa wanaishi pamoja kama mume na mke.Nilimweleza ni jinsi gani nilivyoumizwa na taarifa ile.Happy alilia sana hadi nikamuonea huruma.Alinilaumu sana kwa kuwa mwepesi wa kuamini taarifa kama ile hali nikijua kwamba alikuwa akinipenda kwa moyo wake wote.” Patrick akatulia akanywa tena mvinyo halafu akakohoa kidogo.Andrew akainuka na kuwasha feni alianza kuhisi joto.
“Enhee ikawaje tena? Akauliza Andrew huku akiongeza mvinyo katika glasi yake.
“Kilichofuata ikatubidi tukae kwa pamoja na kutafakari ni kwa nini mambo haya yalitokea.Tuligundua kwamba taarifa zile mbili zilikuwa na lengo la kuuvunja kabisa uhusiano wetu.Swali likaja ni nani ambaye aliamua kutufanyia ukatili wa namna ile? Ni nani ambaye alihitaji mimi na Happy tutengane? Happy akanionyesha ile barua aliyotumiwa ambayo ameitunza hadi hivi sasa.Nilistuka mno baada ya kuutambua mwandiko .Ulikuwa ni mwandiko wa Vero.Nilihisi kuishiwa nguvu baada ya kuligundua hilo” Patrick akatulia kidogo na kuinama chini.Andrew akastuka na kusema kwa sauti ndogo
“Ouh My God ! ..Hii sasa ni hadithi mpya”
Pamoja na feni iliyokuwa ikipuliza mle sebuleni na kuipooza hali ya hewa iliyokuwa ya joto,Andrew alikuwa akitoka jasho jingi.
“Nahisi kuna kipindi kigumu kinakwenda kuanza muda si mrefu.” Akawaza Andrew akiwa ameliinamia kabati.
“Nimestuka sana kusikia kwamba Vero ndiye aliyewatenganisha Patrick na Happy.Kwa nini alifanya hivi? Its hard to believe..” akaendelea kuwaza Andrew.
“ Pamoja na kwamba ni muda mrefu Patrick na Happy wametengana na kwa sasa anakamilisha maandalizi ya harusi yake na Vero lakini bado siku zote moyo wake uko kwa Happy.Siku zote hajaacha kumzungumzia Happy..Kwa jinsi Patrick anavyompenda Happy ,na baada ya kugundua kwamba Vero ndiye aliyewatenganisha ,sina haja ya kuuliza kwani jibu liko wazi,hapa hakuna ndoa tena.Nahisi kuchanganyikiwa ……”
Andrew akamtazama Patrick aliyekuwa ameegemeza kichwa katika ukingo wa sofa huku mkono wake mmoja ukiwa umelishika shavu lake.
“Enhee endelea kunipa michapo ya Arusha.Ikawaje baada ya kugundua kwamba ni Veronika ndiye aliyesababisha mambo haya yote? Andrew akauliza
“kwanza Happy alilia sana.Mimi kwa upande wangu nilipandwa na hasira za ajabu .Sikuamini kama Vero anaweza akafanya kitendo cha namna ile.Niliumia sana Andrew.”
“Du ! haya mambo ni makubwa sasa” Andrew akasema
“Ilituchukua muda mrefu sana kuliongelea jambo hilo lakini kuna kitu kiliibuka ambacho kiliniuma sana”
“Kitu gani hicho?
“Happy alikuwa na pete ya uchumba kidoleni”
“Ina maana tayari Happy ana mchumba? Andrew akauliza huku akishusha pumzi
“kweli Andrew.Tayari Happy ana mchumba.Baada ya kukaa muda mrefu bila kuniona aliamua kumpa nafasi mtu mwingine.”
“Too bad.” Andrew akasikitika
“Na wewe ulimweleza kuhusu harusi yako na Vero? Andrew akauliza tena
“Ndiyo Andrew.Hatukufichana chochote.Tuliweka bayana kila kitu bila kuficha chochote” Patrick akasema
“Baada ya hapo nini kiliendelea? Andrew akauliza huku akitabasamu
“Kilichofuata baada ya hapo tuliiweka dunia yote na matatizo yake kando, tukaingia katika ulimwengu mwingine kabisa wenye raha zisizoelezeka.Andrew nilihisi raha ambayo sijawahi kuipata toka nimezaliwa.Nilijiona ni mwenye bahati kubwa kuwa na mrembo kama yule”
“wow ! maelezo yako yananifanya nijenge picha ya jinsi mambo yalivyokuwa.Tell me about that first night “ Akasema Andrew
“Andrew ,ule ulikuwa ni usiku wangu wa kwanza kuhisi kama niko peponi.Nilihisi kama siko katika dunia hii iliyojaa shida na mahangaiko.Sijawahi kuwa na usiku kama ule.Sikufichi Andrew,Happy ni msichana aliyebarikiwa mno.She’s so sexy” Patrick akasema na kumfanya Andrew acheke wakagonganisha mikono.
“You had sex with her? Andrew akauliza.Huku akicheka Patrick akasema
“C’mon brother..why not ? .and one thing that you cant agree is that.I was her first man” Patrick akasema na kumfanya Andrew asimame huku akiwa na tabasamu la mshangao.
“ wuuuh ! Its unbelievable “ Andrew akashangaa
“ Andrew.hata mimi nilishangaa sana .Kwa mujibu wa maelezo yake anasema kwamba japokuwa aliamua kuwa na mpenzi mwingine lakini bado moyo wake ulikuwa kwangu.Aliamini siku zote kwamba mimi ndiye mwanaume wake wa pekee kwa hiyo alikuwa mzito sana kumpa mwili wake huyo mpenzi wake mpya”
Andrew akamimina mvinyo katika glasi yake akaiinua juu,wakagonganisha glasi
“Patrick nakupa hongera zako” Andrew akasema huku akitabasamu halafu wote wakacheka kwa nguvu.
“Andrew kwa siku hizi chace nilizokaa na Happy kule Arusha nimeonja utamu wa maisha.Sikujua hapo awali kama kuna nyakati maisha huwa matamu namna ile.Kila nikiamka asubuhi najikuta niko na malaika wangu pembeni ilimradi raha na furaha kila wakati.”akasema Patrick huku akitabasamu.
Patrick akasema na kuchukua glasi yake ya mvinyo akapiga funda kubwa.Andrew akamtazama na kusema
“Patrick naomba nikuulize jambo moja”
“Uliza Andrew”
“Ni muda mrefu hamjaonana na happy .baada ya kukutana naye safari hii umeuonaje mtazamo wake kuhusu mahusiano yenu?
“Andrew wewe ni mtu wangu wa karibu na siwezi kukuficha kitu.Pamoja na yote yaliyotokea lakini bado mimi ni mtu wa pekee kwake.Bado nafasi yangu iko pale pale ndani ya moyo wake.”
“na vipi kuhusu wewe? Pamoja na yote yaliyotokea,bado unaamini kwamba Happy ana nafasi moyoni mwako? Andrew akauliza
Swali lile likamfanya Parick anyamaze kidogo ,akachukua glasi ya mvinyo na kupiga funda moja,akakohoa kidogo na kusema
“Andrew ,pamoja na yote yaliyotokea bado Happy ndiye namba moja wangu .Yeye ndiye furaha yangu.Samahani Andrew kama kwa kusema hivi nimekukera.”
“hapana hujanikera Patrick.Nafurahi kwa sababu siku zote umekuwa mkweli kuhusu hisia zako.Kwa hiyo baada ya
hisia za kila mmoja wenu kuwa wazi kwamba bado mnapendana nini kilifuata?
“Tulikuwa na wakati mgumu mno kwa sababu sote tayari tuko katika mahusiano mapya ambayo yamekwisha piga hatua kubwa,lakini hii haikuwa sababu ya kutufanya tusiendelee na urafiki wetu hata kama tuko katika mahusiano mengine.Tulikubaliana kuendelea na urafiki wetu wa kawaida lakini tukajiuliza tena,sisi tunapendana kwa dhati,je tutakuwa tunajitendea haki sisi wenyewe ? Je tutakuwa na furaha ? Majibu ya maswali haya yote yalikuwa ni hapana.Hatutakuwa tumejitendea haki sisi wenyewe ,vile vile huko tuliko hatutaweza kuishi kwa furaha na amani.Tukajiuliza tena tufanye nini basi? Jibu likawa kwamba tunalazimika kuifanya maamuzi magumu.”
“maamuzi magumu yapi tena? Andrew akauliza
“Kuachana na wapenzi wetu wa sasa “ Patrick akasema na kumfanya Andrew asimame
“No ! you are kidding me” Akasema Andrew huku akicheka kichini chini
“Si utani Andrew.,Happy ndiye furaha ya maisha yangu.Nilimpenda Happy muda mrefu na hata nikafungwa kwa ajili yake.Pamoja na yote yaliyotokea lakini bado Happy amekuwa ni mtu wa pekee kabisa ndani ya moyo wangu .Ninampenda na nitaendelea kumpenda hadi kufa kwangu.Kwa sababu ya upendo huo mkubwa nilionao kwa Happy ,nimeamua kuachana na Vero.Nimeona uwe mtu wa kwanza kufahamu kabla sijaliweka wazi jambo hili kwa ndugu .Ndoa kati yangu na Vero haipo tena.Its over.Kwa mambo aliyoyafanya Vero simuhitaji tena katika maisha yangu.Alitumia uongo ,akatutenganisha bila kujali mateso na maumivu tuliyoyapata kwa hiyo hana nafasi tena katika maisha yangu.Happy naye ameamua kuachana na mpenzi wake ili tuweze kuwa pamoja.Nafahamu si jambo rahisi lakini siku zote nguvu ya penzi ni kubwa na hushinda kila kikwazo“ Patrick akasema na kumfanya Andrew ainame na kuzama katika mawazo ghafla.
“Nilijua tu ,hapa hakuna ndoa tena.Masikini Vero” Andrew akawaza.Patrick akasema
“Andrew nafahamu umekuwa mtu wangu wa karibu mno na umenisaidia katika mambo mengi lakini tafadhali naomba usinishauri chochote kuhusu jambo hili.Nimekwisha fanya maamuzi na siwezi kurudi nyuma tena.Kwa ajili ya Happy nitafanya kila kitu ili niwe naye maishani..Ahsante sana Andrew kwa kunisaidia katika mambo mengi lakini nakuomba katika suala hili usijihusishe kwa sababu ninafahamu kinachokwenda kutokea si kitu kizuri.Please don’t be part of this” Patrick akasisitiza.Andrew akamtazama na kusema
“Patrick wewe ni zaidi ya rafiki yangu.Tumeshauriana na tumesaidiana katika kila jambo.Mpaka sasa hivi kati ya ndugu zako wote hakuna mtu yeyote anayefahamu kitu gani kinaendelea kuhusu wewe na Happy zaidi yangu.Kusema kwamba nisikushauri au nisijihusishe kwa namna yoyote na suala hili ni jambo lisilowezekana kwa sababu I’m too involved now.Tumetoka mbali na jambo hili kwa hiyo siwezi kuishia hapa.Kama nilikubali toka mwanzo kwamba nitakuwa nawe,siwezi kamwe kukuacha peke yako hasa katika kipindi hiki kitakachokuwa kigumu zaidi kwako.Patrick utake usitake mimi nitakuwa pamoja nawe katika suala hili hata kama umekataa nisikushauri chochote lakini nitakuwa nawe hatua kwa hatua na hata ikibidi kukushauri pale itakaponilazimu japokuwa sintakushauri ubadili mawazo yako kuhusu yupi ni msichana unayemtaka maishani.” Akasema Andrew. Patrick akamtazama na kusema
“Andrew narudia tena ,kinachokwenda kutokea si kitu kizuri.Ninaomba kila kitu nikibebe mimi mwenyewe.Umenisaidia sana lakini kwa hili naomba uniache mwenyewe.Nimekwisha jitolea kuubeba mzigo huu mkubwa ,ninajua nitaumia na wengi pia wataumia lakini sina namna nyingine ya kufanya .Lazima nifanye hivyo.Lazima niachane na Vero”
“Patrik nimekuelewa vizuri naomba ufahamu kwamba hata kama hupendi bado nitaendelea kuwa nyuma yako.Naomba tafadhali tusiongelee suala hili tena.Fahamu kwamba tuko pamoja na siku zote tutaendelea kuwa pamoja.” Andrew akasema huku akimpa Patrick mkono.
“Andrew nashukuru kama kwa moyo wako umekubali kuungana nami katika suala hili.Nitakuja kukuona kesho asubuhi na kukufahamisha kwa kina mpango mzima .Naomba nikuache na tuonane kesho.”
Wakaagana na Patrick akaondoka zake na kumuacha Andrew akiwa na mawazo mengi
“Du ! mambo yanazidi kujikoroga.Sipati picha ni kitu gani kitakachotokea baada ya Patrick kutamka kwamba amevunja mahusiano yake na Vero.Sikutegemea kama suala hili lingefika hapa lilipofika.Hatua waliyokwishaifikia ni kubwa sana na umebaki muda mchache tu wafunge ndoa.Kitendo cha kusitisha masuala ya ndoa yao kimeniumiza sana japokuwa sina uwezo wa kulizuia jambo hilo lisitokee, kwani tayari Patrick amekwisha fanya maamuzi na hakuna mtu anayeweza kuyabadili.Ninamfahamu Patrick vizuri akisha amua kitu huwa hapendi kupingwa Nimemuona machoni ,alikuwa akimaanisha kile alichokisema.Sijui Happy amempa kitu gani Patrick mpaka ameshindwa kumsahau hata baada ya miaka mingi kupita.Hadi kufikia hatua ya kusitisha mipango ya harusi yake kwa ajili tu ya Happy basi hakuna kitu ninachoweza kukifanya kwa ajili ya kuinusuru ndoa hii ya Patrick na Vero.Patrick na Happy wanapendana na hilo halina ubishi.Ukijiuliza ni kwa nini Happy ajitokeze katika kipindi hiki baada ya kupotea kwa miaka hii yote utapata jibu kwamba ilipangwa wawe pamoja.Nakubaliana na ukweli huo japokuwa ninamuhurumia sana Vero kwa jinsi anavyompenda Patrick.Kosa moja ambalo alilifanya ni kutumia uongo kuwatenganisha wawili hawa.Uongo wa Vero leo hii umekuja kujulikana na hivyo kumgharimu .Kama walivyoumia wenzake kipindi kile alipowatumia taarifa za uongo zilizowafanya wakatengana basi hata yeye atasikia uchungu kama walioupata wenzake kwa miaka hii yote.Roho inaniuma sana lakini sina namna nyingine ya kuweza kumsaidia..Kingine kinachoniumiza ni gharama kubwa tuliyoitumia katika maandalizi ya harusi hii.Nimetumia fedha zangu nyingi kama mchango kwa rafiki yangu katika kuiandaa harusi hii lakini kila kitu kimepotea bure……” Andrew akawaza huku akiketi sofani akakishika kichwa chake alikuwa na mwazo mengi.
“Ngoja nimpigie mama yake Patrick ili afahamu kama mwanae amesharudi.Kwa jinsi Patrick alivyochanganyikiwa na Happy sidhani kama amekumbuka hata kumtaarifu mama yake kama amesharudi Dar es salaam.” Akawaza Andrew huku akichukua simu na kuzitafuta namba za mama yake Patrick.
“Lakini simlaumu sana Patrick kwa sababu kwa uzuri wa Happy hata mimi ningechanganyikiwa.Mtoto ameumbika mithili ya malaika.Mtoto anastahili kabisa kutwaa taji la mrembo wa dunia” Akawaza Andrew wakati akisubiri simu yake ipokelewe na mama Patrick.
“Hallo Andrew habari yako mwanangu” Akasema mama Patrick baada ya kupokea simu
“Habari nzuri mama ,pole na mihangaiko ya kutwa nzima ” Andrew akasema
“Tumeshapoa baba yangu.Kutwa nzima tumekuwa tukizunguka hapa na pale katika kuhakikisha maandalizi yanakamilika.Japokuwa kuna kamati inayoshughulikia kila kitu lakini hata mimi kuna mambo ambayo inanilazimu kuyafuatilia na kuhakikisha yamekaa sawa.Si unajua siku zimebaki kidogo sana na jiji hili lina sherehe nyingi kwa hiyo inabidi kufanya maandalizi ya mapema.”
“ Pole sana .Mama nimekupigia kukufahamisha kwamba Patick amerejea Dar es salaam jioni ya leo .Umefanikiwa kuonana naye?
“Hapana Andrew.Habari hizi wewe ndiyo wa kwanza kuniambia.Hajanitaarifu kama amerejea japokuwa alinipigia simu jana akaniambia kwamba atarejea Dar es salaam siku yoyote.Andrew huyu mwenzio amepatwa na kitu gani ? mbona amebadilika namna hii?Nimeona kuna mabadiliko makubwa sana katika siku hizi chache toka apatwe na yale matatizo ya kupoteza fahamu.Kitu gani kinamsumbua mwenzio? Mama yake Patrick akauliza
“mama siwezi kujua kitu gani kinamsumbua ,japokuwa mimi na yeye ni marafiki wakubwa lakini kuna masuala ya ndani kabisa ambayo hatuwezi kuambiana.Mimi naona tumpe muda wa kutosha ili atulie kwa sababu ninahisi hali hii inaweza kuwa inachangiwa na mambo mengi aliyonayo na hasa hili suala la harusi yake”
“Sawa Andrew.nashukuru kwa kunifahamisha kwa sababu rafiki yako haoni hata umuhimu wa kuwataarifu wazazi wake kama amerejea salama.Tena imekuwa vizuri amerejea kwa sababu mwenzake alinipigia simu kunitaarifu kwamba atarejea leo saa nane za usiku.Kwa hiyo itakuwa vizuri kama atakuwepo uwanja wa ndege na kumpokea mwenzake kwani aliondoka akiwa hana amani kwa hiyo litakuwa jambo la faraja kama akimkuta Patrick uwanjani akimsubiri .Ngoja nimpigie simu nimfahamishe kuhusu hilo.”
“Ok Ahsante mama.Usiku mwema” Andrew akasema na kukata simu kisha akaitupa sofani.
“Damn you Patrick!! Kila siku nimekuwa nikidanganya watu wazima.Umeniweka katika matatizo makubwa sana na siku mama yako akigundua kama mambo yote niliyokuwa nikimwambia yalikuwa ya uongo atatamani hata kunitoa roho.Hatatamani anione tena katika macho yake…” Andrew akatikisa kichwa kwa masikitiko.
“masikini Vero leo usiku anarejea akiwa na matumaini kwamba ndani ya wiki chache zijazo atakuwa mwanamke mwenye furaha kwani atakuwa ameolewa na mwanaume anayempenda sana.laiti angejua ..nadhani asngekubali kurudi tena Tanzania.Namuonea huruma lakini yote haya aliyataka mwenyewe.Palipo na penzi la kweli hakuna awezaye kulitenganisha.Na tusubiri tuone kitakachotokea….” Andrew akawaza akachukua glasi yake iliyokuwa na mvinyo akapiga funda kubwa.


* * * *

Akiwa katika kona ya kuingilia nyumbani kwake simu yake ikaita.Akapunguza mwendo wa gari na kutazama mpigaji.Alikuwa ni mama yake.Akasita kuipokea simu ile.
“Ukiona hivi ujue tayari amekwisha pata taarifa kuwa nimerudi.” Akawaza Patrick
“Hallo mama shikamoo” Akasema Patrick baada ya kuipokea simu ile.
“Marahaba hujambo? “ Akaitika mama yake. Patrick akaguna kidogo kwa muitikio ule kwa sababu kuna kitu alihisi hakikuwa sawa katika sauti ya mama yake.Anamfahamu mama yake vyema.
“Sijambo mama.habari za hapo nyumbani? Patrick akauliza
“Hivi wewe mwanangu naomba nikuulize kitu.Sisi wazazi wako unatuweka katika kundi gani? Mama yake akauliza kwa sauti yenye ukali.
“Kazi imeanza” akawaza Patrick
“mama samahani naomba nikupigie baada ya muda mfupi .Nataka kupaki gari.”Akasema Patrick na mama yake akakata simu bila kusema chochote.Baada ya kuliingiza gari ndani akaelekea sebuleni kisha akaketi sofani akaishika simu yake na kumpigia mama yake.
“Samahani mama kwa kukatisha maongezi yetu mida ile.”
“hakuna hata haja ya samahani kwa sababu siku hizi sisi wazazi wako hatuna tena thamani kwako.”
“kwa nini unasema hivyo mama?
“Kwani si kitu kilicho wazi.Hutaki kutusikiliza chochote tunachokwambia.Hutaki ushauri wetu tena.”
“ Si kweli mama.” Patick akajibu
“Kama si kweli unawezaje kurudi bila kututaarifu kwamba umerudi salama?
“Mama ni kweli nimerudi jioni hii na nilikuwa na mpango wa kuja hapo nyumbani lakini nikiwa njiani nilijisikia hali kubadilika ghafla ikanibidi nirudi nyumbani mara moja.Nimetumia dawa na ninajisikia safi kwa sasa.”
“Mh ! Haya .Sasa sikiliza.Mwenzako alinipigia simu na kunitaarifu kwamba anarudi leo saa nane za usiku.”
“Mwenzangu !! Patrick akauliza
“Ndiyo mwenzako.Kwani una wenzako wangapi? Ina maana Vero si mwenzako?
“Ouh kumbe unasema Vero”
“Ndiyo anarejea leo saa nane za usiku akitokea London alikoenda kwa ajili ya kufanya manunuzi ya harusi yenu.Kwa kuwa umerudi,litakuwa jambo kama ukienda kumpokea uwanja wa ndege.Patrick mwenzako aliondoka hapa akilia machozi na alikubali kwenda London baada ya mimi kumbembeleza afanye hivyo.Tafadhali mfurahishe mwenzako.Nenda ukampokee usiku huu arudipo.Atajiskia mwenye furaha sana pindi akishuka ndegeni na kukuona pale uwanjani.Atasahau kila kitu kilichopita” mama yake akasema .
Patrick akafikiri kidogo na kusema
“Sawa mama nitajitahidi kwenda huko uwanjani.Vipi kuhusu kile kikao?
“Kikao kitafanyika kesho na kila mwanamakati ana taarifa.Katika kikao cha kesho tutafanya majumuisho ya kila kitu na kuangalia kama kuna kitu kilichobaki na kisha jumatatu ndoa ikaandikishwe na kuanza kutangazwa kanisani.Kwa ujumla kila kitu kipo tayari.”
“Sawa mama .Nitafika katika kikao hicho Kuna mambo nataka kuongea na wanakamati wote kwa ndugu wa karibu kwa ujumla.Jitahidi wewe na baba muwepo na umtaarifu pia mama yake Vero naye awepo.Ni muhimu sana..”
“Patrick unataka kutueleza kitu gani? Mama yake akauliza
“Ni masuala madogo madogo tu ya kuwekana sawa kuhusu mambo haya ya harusi” Patrick akasema kisha akaagana na mama yake akaegemeza kichwa sofani na kuvuta pumzi ndefu.
“ Hatua kubwa imeshapigwa mpaka sasa.Kila kitu kiko tayari .Fedha nyingi imeshatumika katika maandalizi ya harusi hii.Ndugu jamaa na marafiki wote wana taarifa juu ya harusi yangu na wanaisubiri kwa hamu kubwa na wengi wametoa michango yao kwa ajili ya maandalizi ya harusi hii.Mambo hayatakuwa rahisi kama nilivyotegemea.Hakuna atakayekubali uhusiano huu uvunjike.hakuna atakayekubali ndoa hii isitishwe.Hakuna atakayenielewa.Hawatanielewa kwa sababu hakuna anayefahamu wapi nimetoka na Happy zaidi ya Andrew .Wazazi wangu walimchukia Happy hasa kwa kitendo chake cha kwenda kusoma Marekani na kuniacha gerezani.Sipati picha nini kitatokea wakisikia kwamba ninaachana na Vero kwa ajili ya kuwa na Happy.Nafahamu sintaeleweka katika jamii lakini siwezi kurudi nyuma.Lazima niachane na Vero.Nafahamu Vero anavyonipenda lakini alifanya kosa kubwa sana kuamua kunitenganisha na furaha ya moyo wangu.namuonea huruma sana.Atateseka sana lakini sina namna nyingine ya kufanya .Kwa ajili ya Happy chochote kile nitafanya.Kwa upande wa Happy jambo hili linaweza kumletea picha mbaya katika jamii.Ninafahamu kwa sasa yeye ni mrembo wa Tanzania na ni mtu maarufu.Kila akifanyacho kinatengeneza kichwa cha habari.Kama waandishi wa habari wakilipata jambo hili litasababisha heshima ya Happy kuporomoka ghafla.Nitakuwa nimemsababishia matatizo makubwa mtoto mzuri kama huyu ambaye taifa linamtazama kama mrembo ambaye anaweza akaliletea sifa kubwa sana kupitia taji lake hili” Akawaza Patrick akiwa ameketi sofani.Akainuka akawasha luninga akarudi tena kuketi sofani.
“Nilimuahidi mama kwamba nitakwenda kumpokea Vero usiku huu.No ! siwezi kufanya hivyo.Sijisikii kuonana na Vero kwa sasa.Ninaweza nikaharibu mambo angali bado mapema.Nataka kila kitu kiishe kesho mbele ya ndugu na jamaa.Nataka kila mmoja afahamu nini Vero alinifanyia.Kwa sababu nilikwisha muahidi mama kwamba nitakwenda kumpokea Vero,ngoja niwasiliane na Andrew ili nimuombe akampokee Vero uwanja wa ndege.”

* * * *

Honi ya gari ikamstua Andrew akiwa jikoni akijiandalia chakula cha jioni.Akazima jiko na kutoka mle jikoni akaelekea getini .Akafungua na kukutana na gari jipya kabisa aina ya Range rover vogue jeusi.Akastuka na kujiuliza ni nani yule kwa sababu hajawahi kuliona gari lile pale kwake.Akalisogelea na mara kioo cha gari kikashushwa taratibu akakutana na sura yenye tabasamu ya mpenzi wake Vick.
“ Vicky ! ” Andrew akasema kwa mshangao huku akilifungua geti lote na gari likaingia ndani.
“Naona kama ndoto .Ni wewe kweli? Andrew akauliza akiwa haamini
“Ni mimi Andrew.Kwani kuna kitu gani cha ajabu? Vick akauliza huku akishuka garini.
“wow ! umeazima wapi gari la thamani kubwa namna hii?
“Ina maana mimi siwezi kumiliki gari la namna hii?” Vick akauliza
“Kwa maana hiyo gari hili ni lako? Andrew akasema huku akicheka
“Ndiyo ni gari langu.Kuna tatizo lolote mimi kuwa na gari kama hili?
“hakuna tatizo lakini unapokuwa na kitu cha thamani kama hiki,kuna tatizo gani mwenzio akifahamu umekipataje pataje? Andrew akauliza
“Kwa maana hiyo unahofia kwamba ninaweza kuwa nimenunuliwa na mwanaume mwingine? Vick akauliza huku akimkazia macho Andrew
“Hata kama umenunuliwa na mwanaume mwingine unaweza ukaniambia?
“Hakuna kitu nilichowahi kukuficha mpenzi wangu na kwa hili ninataka kukueleza ukweli kwamba nimenunuliwa na bosi wangu ambaye mimi ni kimada wake.” Vick akasema na ghafla Andrew akageuza macho akaanguka chini
Vick akamuinamia akambusu na wote wakaangua kicheko kikubwa.
“Usirudie tena kusema hivyo.Unajua sisi wengine hatukawii kuanguka kwa presha” Andrew akasema huku akicheka
“kama ingekuwa ni kweli ningemkata kichwa huyo bosi wako” Andrew akasema na kumfanya Vick acheke kwa nguvu.
“Kweli Andrew unaweza ukakata mtu kichwa kwa ajili yangu?
“Nakwambia ukweli Vick.Niko tayari kukata mtu kichwa kwa ajili yako” Akasema Andrew na kumfanya Vick aendelee kucheka.
“Inuka twende ndani darling.Hili ni gari la mama ametumiwa na dada Toka Ulaya kwa hiyo ameniachia nilitumie” Vick akasema wakati wakiinuka na kuelekea ndani.
Mara tu baada ya kuingia sebuleni simu yake ikaita.Akaichukua na kuangalia mpigaji.Alikuwa ni Patrick.
“halo Patrick” akasema Andrew baada ya kuipokea simu ile.Vick ambaye alikuwa karibu akastuka na kugeuka.
“Patrick ! ina maana Parick amerudi? Akauliza na Andrew akamfanyia ishara kwamba anyamaze
“Andrew kuna jambo limejitokeza ninaomba msaada wako” Akasema Patrick
“jambo gani hilo? Andrew akauliza
“Nimeongea na mama muda mfupi uliopita.Amenitaarifu kwamba Vero anarejea leo saa nane za usiku na akanitaka kwenda kumpokea uwanja wa ndege.Kwa kuwa sikutaka mabishano na mama ikanilazimu kumkubalia kwamba nitakwenda huko uwanja wa ndege kumpokea Vero.Andrew sikufichi kwamba pamoja na kumkubalia mama lakini siko tayari bado kuonana na Vero kwa sasa.Ninaogopa mambo yanaweza yakaharibika mapema.kwa hiyo ninaomba kama hutajali unisaidie kwenda kumpokea Vero.Najua hili ni suala gumu kwako lakini sina mwingine ambaye ninaweza nikamkimbilia kwa msaada.naomba unisaidie kwa hilo” Patrick akasema na kumfanya Andrew akae kimya kwa muda.
“Andrew upo? Akauliza Patrick
“Nipo Patrick nilikuwa natafakari kidogo.Anyway nitakwenda huko uwanjani.”
“nashukuru sana Andrew .Umenisaidia sana ndugu yangu.Hilo ni deni kubwa kwangu.Ngoja niwasiliane na mama anipe namba ya ndege atakayokuja nayo Vero” Patrick akasema na kukata simu.Andrew akabaki katika mawazo mengi,na mara akastuliwa na Vick
“Andrew hebu nieleze.Patrick amerudi?
“Ndiyo amerudi jioni ya leo”
“Alikuwa amekwenda wapi?
“Hakuniambia alikuwa wapi ila alichoniambia ni kwamba alikuwa nje ya mkoa kwa dharura”
“Nimesikia mkiongea kuhusu namba ya ndege.Nani anakuja na dege? Vick akauliza na kumfanya Andrew asite kujibu.
“Andrew niambie tafadhali nani anayekuja na ndege?
“Vero anarudi leo toka London kwa hiyo Patrick ameniomba niende nikampokee badala yake” Andrew akasema
“ Andrew are you out of your mind? Kwa nini yeye ambaye ndiye mpenzi wake asiende na akutume wewe? Vick akauliza
“Patrick hajisikii vizuri na ndiyo maana ameniomba nikampokee Vero badala yake.”
“No Andrew you are not going “ Vick akasema uso wake ukiwa umebadilika
“Unasemaje? Andrew akauliza
“You are not going. Andrew wakati umefika sasa wa kuyaacha mambo ya Patrick na Vero na kuangalia mambo yetu. Sisi tuna mambo mengi ya kukaa na kuongea kuhusu maisha yetu ya baadae. Leo hii nimekuja ili niwe na mpenzi wangu na mimi nifurahi lakini badala yake the whole night unakwenda kumpokea mpenzi wa rafiki yako.Is that fair? Vick akauliza. Andrew akamtazama mpenzi wake halafu akamsogelea karibu akamshika mabegani.
“Vick nimekuelewa. Hata mimi si kwamba ninapenda kuwa mstari wa mbele katika masuala ya Patrick na Vero na kusahau mambo yetu. You are always my everything. You are my breath and my life. Ninamshukuru Mungu kila siku kwa zawadi hii kubwa aliyonipa ya kuwa nawe.Nakupenda sana malaika wangu na niko tayari kufanya chochote kile kwa ajili ya kukufanya uwe ni mwenye furaha daima.Nafahamu umuhimu wako kwangu lakini Patrick he is my best friend.Mimi ni rafiki yake pekee anayeniamini kwa sasa.Sina namna ya kuweza kumkatalia kwa jambo aliloniomba kwa sababu yuko katika wakati mgumu mno kwa sasa na anahitaji msaada.Please let me do this for him and after this, I’m done.Mambo yake atayafanya yeye mwenyewe lakini kwa usiku wa leo naomba uniruhusu niende nikampokee Vero.”
Vick akamtazama Andrew kwa makini akasogea karibu akamkumbatia na kumbusu kisha akasema
“Usihofu baby nimekuelewa. Nitakusindikiza huko uwanja wa ndege siwezi kukuacha uende huko peke yako.lakini naomba uniahidi kwamba baada ya hili utaachana na mambo ya Patrick na kuelekeza nguvu katika mipango yetu”
Huku akitabasamu Andrew akasema
“I promise “
Vick akambusu tena na kusema
“Ok kabla hatujakwenda huko uwanja wa ndege twende kwanza chumbani.Nafasi yangu mimi ni ya kwanza kabla ya hao rafiki zako.” Vick akasema na taratibu wakaelekea chumbani



* * * *



Ni saa tano za usiku sasa lakini hakuhisi dalili zozote za kuonyesha kupata usingizi.Kila alipojaribu kufumba macho ni picha moja tu iliyokuwa ikimjia .Picha ya Patrick.Happy alishindwa kulala akaamka na kuketi kitandani.
“Am I going crazy? Mbona najihisi kama vile siko kawaida? Patrick amenipa nini hadi nishindwe kupata usingizi kwa ajili yake? Kwa siku hizi chache nilizokaa naye Arusha amenifanya niwe kama chizi.Siku hizi chache nilizokuwa naye Arusha ndizo zilikuwa siku pekee zenye furaha katika maisha yangu.I lived my whole life in those few days.Sidhani kama nitarudi katika hali yangu ya kawaida bila ya kuwa na Patrick.Ni yeye tu ndiye atakayeweza kuniondolea uchizi huu ulionipanda kichwani .This is too much .This is beyond love.Nitafanya kila kitu kwa ajili ya kuwa naye.I swear I’m going to do anything to get him.He’s all mine.” Akawaza Happy ,akainuka akachukua glasi ya maji akanywa,akaichukua picha ya Patrick akaitazama akaibusu .
“Siwezi kupata usingizi bila kuisikia sauti ya Patrick.Sielewi ni kitu gani kimemfanya asinipigie simu wakati aliniahidi kwamba atanipigia usiku..” akawaza Happy huku akichukua simu na kupiga
“Hallo my angel” akasema Patrick
“Patrick my love, nimeshindwa kulala bila kuisikia sauti yako. Tafadhali usichelewe tena kunipigia simu mpenzi wangu. Kwa sasa siwezi kukaa muda mrefu bila kukuona na kuisikia sauti yako tamu. .Naona aibu kusema lakini ukweli ni kwamba I’m crazy for you Patrick.” Happy akasema
“Ouh my angel,samahani sana kwa kuchelewa kukupigia simu hata hivyo nilikuwa katika maandalizi ya kukupigia simu muda si mrefu.Toka nimefika hapa nilikuwa katika shughuli za usafi kuiweka nyumba katika hali nzuri.”
“Pole sana Patrick.Kuanzia sasa fahamu kwamba siwezi kumaliza siku moja bila kukuona au kuisikia sauti yako nzuri.” Happy akasema
“nalifahamu hilo Happy na ndiyo maana nimekuahidi kufanya kila niwezalo ili kuhakikisha kwamba tunakuwa pamoja daima.Ni wewe tu ambaye unanifanya nijione kama malaika wa peponi.Ni wewe tu uliyeibeba furaha ya moyo wangu” Akasema Patrick
“ Vipi umeshaongea na Vero? Happy akauliza
“Vero alikuwa safarini ulaya na anarejea usiku wa leo.Nimeitisha kikao kesho na katika kikao hicho nitawaeleza kila kitu na kuuvunjilia mbali uchumba wangu na Vero.Nafahamu halitakuwa jambo rahisi lakini nimekwisha jiandaa kukabiliana nalolote litakalojitokeza.Usiumize kichwa kuhusu hilo.Muda si mrefu ile ndoto yetu itatimia”
“nafurahi kusikia hivyo Patick.Hata mimi kesho nitaonana na Mike na nitamueleza ukweli.Mike ananipenda kwa hilo siwezi kuficha lakini sina namna nyingine ya kufanya zaidi ya kuachana naye.Ni mtu mwelewa na ninatumai atanielewa “ Happy akasema.
“Kwa hiyo mpaka kesho jioni tutakuwa na jibu lenye uhakika zaidi kuhusiana na suala hili gumu.Happy naomba uwe jasiri kwa sababu hii ni kwa ajili ya maisha yetu,kwa ajili ya furaha yetu.Kwa lolote litakalotokea,naomba uniahidi kwamba hautarudi nyuma.Tutashikamana pamoja hadi mwisho.” Akasema Patrick
“Kwa penzi zito nililonalo kwako ambalo haliwezi kulinganishwa na kitu chochote,kwa kuwa wewe ndiye mwanaume pekee niliyekukabidhi moyo wangu uutunze hadi mwisho wa maisha yangu,ninakuahidi kwamba sintarudi nyuma.Niko tayari kukabiliana na lolote lile ambalo linaweza kuwa kikwazo cha sisi kutimiza ndoto yetu ya kuwa pamoja.”
Happy akasema huku macho yake yakilengwa na machozi
“Nimekuelewa mpenzi wangu.naomba sasa ulale tutaonana kesho.Nitakupigia simu kesho asubuhi na mapema kukupa busu la asubuhi” Patrick akasema
“nashukuru sana malaika wangu .Sasa ninaweza kulala baada ya kuisikia sauti yako. kabla sijasahu naomba uniimbie ule wimbo uliopenda kuniimbia tukiwa Arusha ” Happy akasema
“Wimbo upi? Patrick akauliza
“Ule wa Diamond Platinum..Lala salama”
Patrick akacheka na kuanza kumuimbia Happy wimbo ule mzuri uliomfanya Happy ahisi kama vile yuko na Patrick karibu yake.
 
Back
Top Bottom