STORY: Miss Tanzania

STORY: Miss Tanzania

MISS TANZANIA
SEHEMU YA 52
MTUNZI: PATRICK.CK
CONTACT : 0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Pole Patrick.Mambo haya yote yatakwisha japokuwa ni ngumu na itachukua muda kumsahau Vero lakini naomba ujitahidi kwa kila namna kuizoea hali hii na kuiona ya kawaida”
“Nitajitahidi Savanna.I’ll be ok” akasema Patrick halafu wakazungukia nyumba yake yote na walipomaliza wakaingia garini na kuondoka kurejea katika makazi ya Savanna

ENDELEA……………..

Siku zilizidi kusonga huku Patrick akijitahidi kujaribu kusahau mambo yote ya nyuma na kuanza maisha mapya.Bado aliendelea kuishi nyumbani kwa Savanna.Maisha ndani ya nyumba hii yalikuwa mazuri,aliishi yeye,Savanna pamoja na mtumishi wa ndani,.
Siku moja mwishoni mwa wiki Savanna alimuomba Patrick watoke kwa ajili ya matembezi.Walikwenda katika hoteli moja kubwa na tulivu iliyokuwa na ufukwe mzuri na msafi.Savanna alikuwa amejitahidi sana kwa kila namna alivyoweza ili kumsahaulisha Patrick yaliyopita na kumfanya awe na furaha lakini bado alionekana kuna jambo linamnyima raha.
“Patrick ni jambo gani hasa linalokunyima raha? Tafadhani naomba unieleze .Mimi ni rafiki yako na kama kuna jambo lolote ambalio linakufanya usie na furaha naomba unieleze mimi nitakusaidia.” Akasema Savanna wakiwa ufukweni.
“Savanna wewe ni zaidi ya rafiki yangu kwa hiyo siwezi kukuficha kitu.Kitu kinachoninyima raha ni pale ninapowaza kuhusu maisha yangu.Kama unavyojua nimepoteza kila kitu pamoja na mwelekeo mzima wa maisha yangu.Nimepoteza kazi yangu na mpaka sasa hakuna hata kampuni moja iliyoonyesha dalili za kuniajiri tena.Ninajiona kama nina laana vile lakini hata hivyo nahitaji kusahau kilichotokea na kuanza maisha mapya lakini kadiri siku zinavyozidi kwenda najikuta nikishindwa namna ya kuweza kuanza tena maisha yangu na kujitegemea mimi mwenyewe.Sijisikii vizuri ninapokutegemea wewe katika kila jambo”
Savanna akatabasamu na kusema
“Pole Patrick lakini hukupaswa kuumiza kichwa chako namna hiyo.Ulipaswa kunieleza kuhusu jambo hilo kwani tayari ninalifahamu hilo na nina mipango mizuri kwa ajili yako ila sikuweza kukueleza mapema kwa sababu nilikuwa nataka nikwambie wakati kila kitu kimekamilika.Kwa ufupi tu ni kwamba nimeanzisha kiwanda cha kusindika nyama na muda wowote kuanzia sasa kitaanza kazi.Wewe ndiye utakayekuwa meneja wa kiwanda hicho.
.majukumu yote ya uendeshaji wa kiwanda hiki yako juu yako kwa hiyo usiumize kichwa chako kuhusiana na ajira,you are a manager now.” Akasema Savanna huku akicheka.Patrick akashindwa kujizuia akasimama akamkumbatia Savanna kwa furaha.
“Savanna ni kitu gani nimekufanyia hadi ukanifanyia mambo yote haya? Nitakulipa kitu gani? Patrick akasema huku akimtazama Savanna
“Ni wajibu wangu kufanya hivi nifanyavyo Patrick na hutakiwi kunilipa chochote .Nina imani hata mimi ningekuwa katika hali kama yako ungefanya kama nifanyavyo mimi.Isnt it Patrick?
“Ndiyo Savanna .Ningefanya kama ufanyavyo.Nisingethubutu kukuona ukiwa katika hali kama yangu.Naomba nikiri kwamba ni hali ngumu sana lakini nimeweza kuvumilia na kufika hapa kutokana na jitihada za watu wachache wanaonuipenda na kunijali wakiongozwa na wewe Savanna ,watu ambao wamesimama nami toka dakika ya kwanza ya matatizo yangu na hadi leo bado wako nami.Nina deni kubwa kwako Savanna na sijui nitalilipaje.” akasema Patrick halafu akainamisha kichwa chini akazama katika mawazo ghafla.
“Patrick unawaza nini? Akauliza Savanna baada ya kumuona Patrick amebadilika ghafla
“Savanna nimekumbuka kesi yangu.Kila mara niwazapo kuhusu kesi hii ninashindwa kujizuia kuogopa.Ninafikiria itakuwaje endapo nitahukumiwa kifungo gerezani na kushindwa kutimiza malengo yangu.Sitaki kufungwa jela kwa sababu ya mtu asiyekuwa na thamani kwangu hata kidogo.”
“Patrick siku zote nimekuwa nikikwambia kwamba usiwaze chochote kuhusiana na kesi hii. Mambo yote niachie mimi na nitalishughulikia suala hili na litakwisha.I give you my word Patrick” akasema Savanna huku akitabasamu .Kikapita kimya cha dakika mbili kila mmoja akiwaza lake
“Patrick ..!! akaita Savanna.Patrick akamtazama usoni
“Kuna jambo ambalo nataka kukueleza”
“Jambo gani Savanna?
“Patrick najua ni namna gani unavyoumia kila siku moyoni kwa haya yaliyotokea.Ninayaona maumivu yako na kuyahisi na kunifanya na mimi pia niumwe kwa kukuona ukiwa katika hali hii ya mateso makubwa ya moyo.Patrick nafahamu kwamba si rahisi kuyasahau yaliyotokea na kuanza maisha mapya kwa haraka.Itachukua muda kuwasahau wapendwa wako,vero,Happy na baba yako.Hawa ni watu uliowazoea na kuwapenda lakini leo hii hawako tena nawe.Pamoja na kwamba kumbu kumbu zao bado zinakujia ,lakini ni wakati sasa wa kuwaacha waende na wewe uuruhusu moyo wako uanze maisha mapya.Its time now to let them go.Kuondoka kwao si mwisho wa maisha yako wala ndoto zako .Bado unayo maisha marefu na yenye furaha lakini pale tu utakapoufungua moyo wako na kuuruhusu uanze maisha mapya.Ufungue moyo wako sasa kwa wale wanaokupenda na kukujali na kuwa tayari kusimama nawe katika nyakati zote za shida au raha.Pamoja na yaliyotokea lakini bado unahitaji kuwa na marafiki na hata mtu ambaye unaweza tena kumwamini na kumkabidhi moyo wako.” Akasema Savanna.Patrick akamuangalia kwa makini halafu akatabasamu na kusema
“Unamaanisha nini Savanna unaposema mtu ambaye ninaweza kumwamini na kumkabidhi moyo wangu?
“Ninamaanisha kwamba you have to learn to love again.Only love can help you forget the past” Akasema Savanna na kumfanya Patrick atabasamu na kucheka kidogo
“Mbona unacheka Patrick? Ni kosa la jinai kupenda? Akauliza Savanna
“Si kosa la jinai lakini…………………………”
“ Lakini ……………? Akauliza Savanna
“Sina hakaika kama moyo wangu uko tayari kupenda tena Savanna.Kidonda nilichonacho moyoni kilichosababishwa na mapenzi kitachukua muda mrefu kupona..Nimeumizwa sana na pengine sintaweza kupenda tena.Pengine nitaishi maisha yangu yote yaliyobakia nikiwa mwenyewe.Sintavumilia tena maumivu yoyote ya kuumizwa.Kuna watu katika dunia hii hawajaumbwa ili kupenda na ninaamini mimi ni mmoja wao” akasema Patrick katika hali ya kukata tamaa kabisa
“Patrick nafahamu ni namna gani ulivyoumizwa. Sisi sote tunaumizwa na mapenzi .Lakini mimi bado nasisitiza kwamba kuuruhus moyo wako kupenda tena kutakusaidia sana katika kusahau mambo yaliyopita.Find yourself someone who truly loves you and I swear you’ll be Happy again” akasema Savanna
“Hata kama nikiamua kupenda tena ni nani nitakayempenda? Nani ambaye nitamuamini katika ulimwengu huu wa sasa na kumkabidhi moyo wangu tena? Savanna naomba niwe wazi kwako kwamba sioni sababu ya kupenda tena kwani kila mara nilipojaribu kupenda nimeishia kuumizwa moyo wangu tu.Nilimpenda mno Happy na nilikuwa tayari kufanya lolote kwa ajili yake,niliwahi hadi kuua kwa ajili yake lakini ona jeraha alilonitia moyoni..I’m hurt Savanna..’m deeply hurt.”Akasema Patrick.Savanna akamshika mikono na kumuangalia usoni.
“Patrick si wanawake wote ni wabaya na wanaweza kukuumiza kama ulivyoumizwa.Usiuamini ule msemo usemao samaki mmoja akioza na wote wameoza.Bado kuna wnawake wazuri ,wenye kukupenda ,kukujali na kukuthamini,wanawake ambao kwao una maana kubwa sana.Tafadhali usiufunge moyo wako kwa mwanamke kama huyu”
“Savanna hata wale niliokuwa nao Happy na Vero walinipenda kwa mioyo yao yote.Walinijali na kunithamini.Kwa ufupi ni kwamba sina tatizo na wanawake hata kidogo lakini sina uhakika wa kupenda tena kwa sababu niliwapenda kwa moyo wangu wote.Kuna nyakati ninahisi kama dunia inaniadhibu.The world has been so cruel to me so even if I’ll start a new relationship it wont work out and I’ll get hurt again.Sitaki kuumia tena” akaendelea kusisitiza Patrick
“Patrick,Mungu ametuleta hapa duniani tuyafurahie maisha na ndiyo maana akaumba mwanamke na mwanaume kwa hiyo si sahihi kusema au kuamini kwamba kuna watu ambao wameshushwa katika hii dunia kwa ajili ya kuishi wao wenyewe bila kuwa na mahusiano.Kama kuna watu wa namna hiyo basi Mungu angewaumba bila kuwa na jinsia” akasema Savanna halafu wote wawili wakacheka sana.Savanna akaendelea
“Ninavyoamini mimi ni kwamba kila mtu ana haki ya kuwa katika mahusiano labda upende mwenyewe kutokujihusisha na mahusiano kama vile watawa na makasisi lakini hata hao watawa wanaishi chini ya uangalizi maalum tena mkali ili kuwasaida wasiweze kuingia katika vishawishi vya kimahusiano.Tukirudi katika swala lako lingine,si kweli kwamba dunia imekuwa katili sana kwako ,dunia si mbaya hata kidogo ,dunia inatupenda wote na ndiyo maana wote tunavuta hewa sawa,inatupa mazao na kila kitu.Binadamu waishio juu ya dunia ndiyo wabaya na kwa upande wako ni kwamba you fell I love with wrong people.People whom you’re not meant to be with” akasema Savanna,Patrick akatabasamu halafu akasema
“Maneno yako yanaweza kuwa na ukweli Savanna kwa sababu kuna usemi usemao kwamba kila jambo linafanyika kwa sababu maalum.Inawezekana ni kweli nilipenda watu ambao hawakuwa sahihi kwangu.Hata hivyo nahitaji kulifikiri tena suala hili kabla ya kuamua kuingia katika mahusiano mengine na nina hakika inaweza ikanichukua muda mrefu sana.Kwa sasa nataka nielekeze nguv na akili yangu katika kazi yangu mpya” akasema Patrick
“Hilo ni jambo la msingi sana Patrick.Hutakiwi kuidhulumu nafsi yako.You need to be Happy and to be be Happy you need to love and be loved ” Akasema Savanna .Patrick hakujibu kitu
“It’s getting late Patrick.Twende tuondoke .Leo nataka tukaandae pamoja chakula cha usiku.Unakumbuka ni muda mrefu sana umepita toka tulipoandaa kwa pamoja chakula cha usiku?” Akasema Savanna
“Wow ! That’s great Idea.Ni siku nyingi sana sijaingia jikoni kupika .Nakumbuka sana nyakati zile tulizokuwa tukiandaa chakula pamoja. “ akasema Patrick huku akicheka kidogo
“Unapenda tupike nini kwa ajili ya usiku wa leo? Akauliza Savanna
“Kitu chochote utakachopenda tupike Savanna mimi niko tayari.” Akajibu Patrick na kumfanya Savanna atabasamu
“Today we’re going to have a very special dinner just for two of us.Lets make this night a wonderful and memorable one.” Akasema Savanna kisha wakaondoka.
Kabla ya kuelekea nyumbani walipita kwanza kununua vitu mbali mbali ambavyo wangependa kuvitumia kwa ajili ya usku huo.Walipofika nyumbani,waliingia jikoni na kuanza maandalizi kwa pamoja.Kitendo cha kushirikiana kuandaa chakula kile kilimpa Patrick furaha ya ajabu sana na kumkumbusha nyakati zile wakati bado alikuwa katika mahusiano ya sirina Savanna
Mpaka kufika saa mbili za usiku,chakula kilikuwa tayari.Savanna akamuomba Patrick amuachie yeye kazi zilizobakia na yeye aende akajiandae kabla ya kupata mlo huo wa usiku wazo ambalo Patrick alilikubali na kwenda kujiandaa
“Tonight is the night .I’ve been waiting for this night for so long.Leo hii Patrick lazima awe wangu tena” akawaza Savanna huku akitabasamu baada ya Patrick kuondoka mle jikoni
“Baada ya usiku wa leo nitaamka nikiwa mikononi mwa mwanaume ninayempenda sana kuliko wote.After tonight I’ll be complete and no one than death can separate us again.Patrick will be mine forever” akawaza Savanna wakati akiandaa meza
Kwa upande wake Patrick baada ya kuingia chumbani kwake,moja kwa moja aliingia bafuni akajimwagia maji
“Namshukuru sana Savanna kwani kwa sasa najisikia vizuri na nina nguvu ya kuendelea na maisha yangu mapya. Bila yeye sijui ningekuwa katika hali gani hivi sasa” akawaza Patrick halafu akaendelea kujimwagia maji .Wakati akiendelea kuoga akakumbuka kitu halafu akatabasamu
“ Katika siku zote ambazo nimekuwa na Savanna ,siku ya leo nimejikuta nikiwa na furaha sana na hasa zoezi la kupika pamoja,zoezi ambalo limenikumbusha nyakati zile nilizokuwa naye katika mahusiano ya siri .Niliwahi kuwa katika mapenzi mazito na Savanna,nakumbuka wakati ule nilikuwa na furaha sana japokuwa nilikuwa tayari katika mahusiano na Vero.Savanna alinionyesha mapenzi ya dhati na moyo wangu ulifurahi .Nilikubali kuachana naye kwa shingo upande pale alipompata George.Kama nisingekuwa katika mahusiano na Vero kwa wakati ule basi tayari ningekuwa nimekwisha funga ndoa na Savanna kwani ni mwanamke mwenye kila sifa ya kuwa mke bora .Zaidi ya yote bado ananipenda kwa dhati ya moyo wake na ndiyo maana amejitolea kwa hali na mali katika kuhakikisha kwamba suala la kesi yangu linakwisha na ninakuwa huru tena.” Akawaza Patrick na kisha akaendelea kuoga
“Hata mimi toka ndani kabisa ya moyo wangu ninakiri kwamba bado ninampenda Savanna.Ninahisi yeye anaweza kuwa ndiye mwanamke anayenifaa,lakini kutokana na msaada mkubwa alionisaidia ninasita kuziamsha tena hisia za mapenzi kati yetu” akawaza Patrick halafu akaendelea kuoga.Sura ya Savanna wakiwa jikoni wakipika pamoja ikamjia kichwani akatabasamu
“She have a pretty face,macho mazuri,shepu nzuri na sauti kama malaika.Savanna ni mwanamke bora na mzuri kupita kiasi” akawaza Patrick kisha akatoka mle bafuni
Savanna aliendelea na zoezi la kuandaa meza kwa ajili ya chakula cha usiku.Alizima taa na kuwasha mishumaa na kupafanya mahala pale pawe pa kuvutia sana.Alipohakikisha kila kitu kiko sawa akaenda chumbani kwake kujiandaa kwa ajili ya usiku huo ambao aliupanga uwe maalum kwake

* * * *

“Huu ni usiku wangu wa pekee kabisa ni usiku ambao nimekuwa nikiuota kwa muda mrefu.Ni usiku ambao nitalala nikiwa kifuani kwa Patrick.” Mawazo hayakumkauka Savanna wakati akimalizia kujipaka rangi ya mdomo halafu akajitazama katika kioo na kutabasamu.Alikuwa amependeza sana.Alivaa gauni refu jepesi la rangi jeupe ambalo lilionyesha hadi nguo ya ndani.Akageuka akajitazama na kutabasamu halafu akachukua uturi wa gharama kubwa na kujipulizia kisha akatoka mle chumbani.Patrick alikuwa bado chumbani kwake wakati Savanna alipowasili sebuleni.Savanna akampigia simu na kumtaarifu kwamba muda wa kupata chakula cha usiku umewadia.
Patrick akatoka chumbani na kuelekea sebuleni.Mara tu alipoingia ,akapigwa na mshangao kwa alichokikuta.Sebule ilikuwa imebadilika na kuwa na mandhari ya kuvutia mno.Taa zote zilikuwa zimezimwa na kilichokuwa kinawaka ni mishumaa iliyopapendezesha mahala pale na kupafanya pa pekee kabisa.
“Wow ! amazing “ akasema Patrick huku akitabasamu
“karibu Patrick” akasema Savanna kwa sauti laini huku akiinuka pale sofani alipokuwa amekaa na kwenda kumshika Patrick mkono akaumuongoza kuelekea katika meza ya chakula.Japokuwa mwanga ulikuwa hafifu lakini Patrick aliweza kulishuhudia vyema vazi la Savanna na kusisimka mwili kwani aliweza kuiona hadi nguo ya ndani aliyokuwa amevaa .Mapigo ya moyo wake yakaanza kumuenda kasi.Ni muda mrefu sasa umepita hajawahi kusisimkwa mwili.Savanna na Patrick wakaangaliana kwa sekunde kadhaa Savanna akauliza
“Mbona unaniangalia hivyo Patrick?
“You are so amazing tonight” akajibu Patrick
“Thank you” akajibu Savanna kisha wakaelekea katika meza iliyokuwa imesheheni vyakula vya aina mbali mbali walivyoviandaa
“Karibu chakula Patrick,chakula ambacho ni maalum kwetu.Just for tonight let us forget the world and enjoy the night.Let us make our own world ” Akasema Savanna.
Waliendelea kula taratibu huku wakisindikizwa na muziki laini.Kila Patrick alipomtazama Savanna alisisimka mwili wake kutokana na kuzishuhuhudia chuchu za kuvutia za Savanna ambazo zilikuwa zinaonekana kwa urahisi kutokana na vazi lile alilokuwa amevaa lililoonyesha kila kitu.Taratibu akahisi mtafaruku katika sehemu za ikulu ambazo zilikuwa zimechachamaa kupita maelezo.
“Gosh ! haya ni majaribu makubwa sana.Savanna ananiweka katika wakati mgumu mn😵uh jamani nitafanya nini mimi? Akawaza Patrick huku akiendelea kumtazama Savanna ambaye alikuwa ameinamisha kichwa.Ghafla akainua kichwa na kugundua kwamba Patrick alikuwa anamuangalia akatabasamu
Baada ya kumaliza kula Savanna akamuomba Patrick waelekee katika sofa lililokuwa na meza ndogo pembeni iliyokuwa na chupa tatu za mvinyo pamoja na glasi mbili.
“Na tunywe kwa furaha huku tukitakiana maisha marefu” akasema Savanna huku akiisogelea glasi yake iliyokuwa na mvinyo karibu na Patrick wakagonganisha glasi.Waliendelea kunywa na kadiri muda ulivyozidi kusonga ndivyo maongezi na vicheko vilivyozidi.Walikumbushana mambo mengi na hasa nyakati zile walizokuwa wapenzi,Ulikuwa ni wakati wa furaha mno kwa wote.Maongezi yalikolea na kulikuwa na kila dalili kwamba walianza kulemewa na kilevi.Savanna akainuka pale alipokuwa amekaa na kuelekea katika redio akaweka muziki laini sana halafu akamfuata Patrick
“Patrick can we dance?
Bila ubishi Patrick akainuka akakumbatiana na Savanna wakaanza kucheza.Patrick akahisi kama chaji za umeme zinapita mwilini mwake pale kifua cha Savanna kilichobeba chuchu laini kilipokigusana na kifua chake.Kadiri muziki ulivyokuwa ukienda ndivyo walivyojikuta wakikumbatiana kwa nguvu zaidi.Muziki ulimalizika lakini bado waliendelea kukumbatiana kwa nguvu .Taratibu Savanna akaupeleka mkono wake wa kulia chini kidogo ya kiuno cha Patrick na kukutana na kitu kigumu kilichotuna.Taratibu na kwa ufundi Savanna akakishika kitu kile kilichotuna na kumfanya Patrick atoe mguno na kuhema kwa nguvu kisha akampiga Savanna busu zito lililomfanya aweweseke.Taratibu Patrick akausogeza mdomo wake karibu na Savanna na kuutoa ulimi wake na zoezi la kunyonyana ndimi likaanza huku wakishikana na kutomasana sehemu mbali mbali za mwili.Wote wawili walikuwa wakihema kwa nguvu na kila mmoja akiongea maneno ambayo mwenzie hakuweza kuyaelewa.
“Ouh,Ouh,ouh Patrick take ..m.me..to ..parr….r..paradise” akasema Savanna kwa sauti yenye kukwama kwama.Alikuwa hajiwezi tena kwa raha alizozisikia.Patrick akamuinua na kwenda naye chumbani.Kilichoendelea huko ni miguno na vilio vya utamu uliopitiliza

* * * *


Mlio wa saa ya ukutani ndio uliomstua Patrick akafumbua macho na kutazama ukutani kulikokuwa na saa kubwa.Ilikuwa ni saa mbili za asubuhi.Pembeni yake alikuwa amelala Savanna akiwa katika usingizi mzito.Patrick akamtazama na kutabasamu
“Gosh ! Usiku wa jana kamwe sintausahau katika maisha yangu.Sijawahi kuwa na usiku wa kipekee kama ule.Nilijihisi kama nimetoka kabisa katika ulimwengu huu.Ouh Savanna I didn’t know how much I still love you.Umenirudishia tena furaha yangu iliyopotea.” akawaza Patrick halafu akainama na kumbusu Savanna shavuni na mara Savanna akafumbua macho.
“Ouh Patrick thank you so much.You are so sweet” akasema Savanna
“Thank you for the wonderfull night.Sijawahi kuwa na usiku mzuri kama wa jana.Nimekuwa nikiuota usiku kama ule kwa miaka mingi.Ahsante sana Patrick..Ahsante sana” akasema Savanna akamvuta tena Patrick kwake na kumpa busu zito.Patrick akatabasamu na kusema
“Savanna you are wonderfull,you are amazing.Baada ya usiku wa jana,najiona mtu mpya.Savanna naomba nitamke kwamba najiona ni kama mfalme mwenye nguvu mwenye uwezo wa kufanya chochote nikiwa nawe.Umenipa nguvu na matumaini.Siku zote nitaendelea kumshukuru Mungu kwa kunikutanisha nawe.Nina uhakika mkubwa kwamba kukutana kwetu haikuwa kwa bahati mbaya.Mungu alikuwa na makusudi yake na ndiyo maana leo hii ninathubutu kutamka kwamba pamoja na kwamba tuliachana na kila mmoja akaendelea na maisha yake ,lakini bado moyoni mwangu una nafasi ya kipekee kabisa.Bado ninakupenda Savanna na hata siku moja upendo wangu kwako haujapungua.Sitaki kubishana na moyo wangu kwamba wewe ndiye mwanamke ambaye umeumbwa kwa ajili yangu.Savanna ninaombi moja kwako” Patrick akanyamaza akamtazama Savanna ambaye machozi yalikuwa yanamtoka
“Omba chochote Patrick nitakupatia” akasema Savanna huku akifuta machozi yale ya furaha
“Savanna pengine ombi langu kwako linaweza kuwa gumu hasa kutokana na matukio ambayo yamekuwa yananitokea lakini napenda kuwa wazi kwako kwamba ninaomba nafasi nyingine katika moyo wangu.Ninakubaliana na maneno uliyoniambia jana kwamba natakiwa kuufungua moyo wangu tena.Nimeufungua moyo wangu kwako na nina imani wewe ndiye pekee ambaye utaweza kunisahaulisha mambo yote yaliyopita na kunifanya niwe na maisha yenye furaha sana hapa duniani.Naomba uwe malkia wangu Savanna.” Patrick aliyasema maneno haya taratibu na kwa hisia kubwa.Mara tu alipomaliza kusema ya moyoni mwake,Savanna aliinuka kwa kasi na kulitupa shuka pembeni kisha akamkumbatia Patrick kwa nguvu.Alikuwa akiweweseka huku akimpiga Patrick mabusu mfululizo
“Patrick unataka kunipa uchizi.Kwa muda mrefu sana nimekuwa nikiota kuusikia mdomo wako ukitamka meneo haya mazito uliyonitamkia sasa hivi.Patrick nashukuru sana na sina cha kusema zaidi ya kukuhakikishia kwamba siku zote moyo wangu ulikuwa na nafasi kwa ajili yako pekee.Niliamini siku moja mimi na wewe tutakuwa pamoja hata kama si katika maisha haya basi katika maisha mengine baada ya kufa.Nimekuwa nikimuomba sana Mungu kwa jambo hili lakini hatimaye leo hii limekuwa kweli.Huu ni kama muujiza kwangu.Patrick nakukabidhi moyo wangu na kila kilicho changu.Naomba unitawale ee mfalme wangu.Niamuru chochote nitakutii” akasema Savanna kwa hisia kali huku akitokwa na machozi ya furaha.Ilikuwa ni kama ndoto.Hakuamini kama ile ndoto yake ya siku nyingi ya kuwa na Patrick leo hii imekuwa kweli.Walikumbatiana kwa furaha huku wakiepeana mabusu mfululizo na taratibu wakajikuta wakianza kuhama katika ulimwengu huu na kwenda katika ulimwengu uliojaa mahaba mazito.Migumo na mihemo ya kimahaba ndivyo vilitawala chumba hiki.Patrick akaufungua mpya wa mapenzi na Savanna.

TUKUTANE SEHEMU IJAYO...............
 
MISS TANZANIA
SEHEMU YA 53
MTUNZI: PATRICK.CK
CONTACT : 0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Patrick nakukabidhi moyo wangu na kila kilicho changu.Naomba unitawale ee mfalme wangu.Niamuru chochote nitakutii” akasema Savanna kwa hisia kali huku akitokwa na machozi ya furaha.Ilikuwa ni kama ndoto.Hakuamini kama ile ndoto yake ya siku nyingi ya kuwa na Patrick leo hii imekuwa kweli.Walikumbatiana kwa furaha huku wakiepeana mabusu mfululizo na taratibu wakajikuta wakianza kuhama katika ulimwengu huu na kwenda katika ulimwengu uliojaa mahaba mazito.Migumo na mihemo ya kimahaba ndivyo vilitawala chumba hiki.Patrick akaufungua mpya wa mapenzi na Savanna.

ENDELEA………………

Ukurasa mpya wa maisha ya Patrick umefunguliwa na tayari ni meneja wa kiwanda cha kusindika nyama.Maisha yake yanakwenda vizuri kwa sasa.Alinawiri na kupendeza sana.Alikiongoza kiwanda hiki cha kusindika nyama kwa ufanisi mkubwa na ndani ya kipindi kifupi kiwanda hiki kilikuwa ni moja kati ya viwanda bora kabisa nchini
Mizizi ya penzi imara kati yake na Savanna ilichomoza kwa kasi na kwa sasa penzi lao halikuwa la siri tena.Lilikuwa kwa ndugu jamaa na marafiki.Alimtambulisha rasmi Savanna kama mpenzi wake na kwa pamoja walikuwa na mipango mingi na ndoto nyingi za kutimiza katika maisha yao yajayo na kubwa likiwa ni kufunga ndoa mara tu kesi ya Patrick itakapomalizika.Bado kesi ya kuua bila kukusudia inayomkabili Patrick iliendelea kuunguruma mahakamani.Tayari upande wa mashitaka ulikwisha funga funga ushahidi wao hivyo kutoa nafasi kwa upande wa utetezi nao kuwaleta mahakamni mashahidi wanaomtetea Patrick.Upande wa utetezi ukiongozwa na Savanna uliitaka Mahakama kumuachia huru mteja wao kwa sababu alisababisha kifo wakati akijaribu kunyang’anya silaha mtu aliyekuwa ameishika silaha hiyo na aliyekuwa na dhamira ya kufanya mauaji.Baada ya Patrick kutoa ushahidi wake mahakamani ilifuata nafasi ya mashahidi kuanza kutoa ushahidi wao mbele ya mahakama.
Siku moja jioni Savanna alichelewa kurudi nyumbani na kukuta tayari Patrick amekwisha rejea toka kazini.Siku hii Savanna alionekana mchovu na mwenye mawazo mengi.Patrick aliligundua hilo na kumuuliza ni jambo gani lililokuwa limemsibu.Savanna hakujbu kitu akainuka pale sofani akajimiminia mvinyo katika glasi akanywa funda kubwa halafu akamtazama Patrick
“Savanna una tatizo gani leo mpenzi wangu? Si kawaida yako kuwa katika hali hii.Tafadhali niambie kama una tatizo lolote.” Akasema Patrick.Savanna akainama akafikiri kwa sekunde kadhaa na kusema
“Patrick nina tatizo mpenzi wangu.Kuna jambo linaniumiza kichwa changu sana.Nimekuwa nikilifikiria suala hili kwa muda mrefu sasa lakini nimeshindwa kulipatia ufumbuzi”
“Jambo gani hilo linakusumbua Savanna? Tafadhali niambie.Hakuna jambo lolote linaloweza kutushinda kulipatia ufumbuzi” akasema Patrick.Savanna akainamisha kichwa akafikiri kidogo na kusema
“Kuna tatizo kidogo katika kesi”
“Katika kesi? Patrick akastuka
“Ndiyo Patrick kuna tatizo dogo”
“Tatizo gani” akauliza Patrick ambaye tayari moyo wake ulianza kumwenda mbio
“Patrick nilishindwa kukutaarifu mapema kuhusu jambo hili kwa kuwa naamini ni jambo ambalo hutapenda kulisikia lakini naomba nikutaarifu kwamba katika orodha ya watu wanaotakiwa kutoa ushahidi wao mahakamani lipo pia jina la Happy”
Patrick kijasho kikamtoka .Alistushwa sana kwa taarifa ile
“Ou my God “ akasema kwa sauti ndogo huku akimkazia macho Savanna
“Happy kibaho? Akauliza Patrick
“Ndiyo.Happy Kibaho”
“Ouh my Gosh.! How could you do that Savanna?Tulikubaliana kwamba Happy hatahusika na chochote katika kesi hii,aliniacha nikisota gerezani kwa kosa ambalo sikulifanya,hakuona umuhimu wangu,kwake yeye hata kama nikifungwa gerezani hatajali,kwa nini basi tumtumie mtu kama huyu? Savanna Happy kibaho ni jina ambalo sitaki kulisikia tena katika masikio yangu.” Patrick akasimama
“Patrick hii ndiyo sababu sikutaka kukueleza mapema.Nilijua lazima ungeshtushwa sana na taarifa hiyo”
“Savanna tafadhali niko chini ya miguu yako naomba kama kuna uwezekano liondoe jina la Happy katika orodha ya mashahidi.Tunao mashahidi wengi ambao tutawatumia katika kesi hii.” Akasema Patrick.Savanna akamshika mabegani na kusema
“Patrick mpenzi wangu ninafahamu ni namna gani Happy alivyokuumiza na jinsi gani unavyomchukia.Nafahamu pia uhusika wa Happy katika kesi hii unavyokuumiza kwani utairudisha tena taswira ya mtu ambaye hutaki tena kumuona au kumsikia katika maisha yako.Hata mimi suala hili ni gumu sana kwangu lakini naomba niwe wazi kwako kwamba Happy ni mtu muhimu sana katika hatua hii tuliyofikia.Ushahidi wake una nguvu sana”
“Savanna mashahidi hawa wote tulionao hawatoshi hadi Happy naye ashirikishwe katika kutoa ushahidi? To be honest I hate her.Sitaki kuiona tena sura yake kutokana na mambo aliyonifanyia.” Akasema Patrick
“Ushahidi mzito tuliouwasilisha mahakamani pamoja na ule unaoendelea kutolewa na mashahidi unajitosheleza sana lakini katika ushahidi wote huo Happy ametajwa sana kwani yeye ndiye aliyekoswa na risasi iliyotoka katika bastora aliyokuwa ameishika Vero.Happy anatakiwa aieleze mahakama kila kitu kilichotokea jioni ile.Ni ushahidi muhimu mno ambao ninaamini ndio utakaoisaidia mahakama kuamua hatima ya kesi hii.Patrick nakuomba mpenzi wangu tumtafute Happy na kumuomba atoe ushahidi wake .Nafahamu kwamba unamchukia na hutaki kumuona tena lakini kwa hatua hii Happy ni mtu muhimu sana kwetu.Patrick we’re almost to the end now so we need to do everything we can to win.Ninamuomba sana Mungu atusaidie ili tuweze kulimaliza suala hii haraka na tuitimize ndoto yetu ya kufunga ndoa.Naomba uniruhusu mpenzi wangu nimtafute Happy ili aweze kuja kutoa ushahidi wake “ akasema Savanna.
Patrick akashika kichwa kwa mikono yake akainama na kuzama katika mawazo.Akainuka pale alipokuwa amekaa akaenda dirishani,akasimama na kuelekeza macho yake nje kana kwamba kuna kitu alikuwa anakiangalia
“Happy Kibaho !” akasema taratibu halafu akainama tena
“Nilimpenda kiasi ambacho siwezi kuelezea.Nilimpa kila kitu na kuamini kwamba yeye ndiye mwanamke pekee ambaye nimepangiwa niwe naye katika maisha yangu.Pamoja na kumuonyesha kila aina ya upendo lakini Happy bado alidiriki kufanya kitendo kichafu ambacho sikuwahi kutegemea au hata kuota kama msichana kama Happy anaweza akafanya.Aligundua kosa alilolitenda na akapotea moja kwa moja akiniacha nikiozea gerezani kwa kosa ambalo alilisababisha yeye mwenyewe.Je mtu wa namna hii aliyenisababishia majeraha makubwa ya moyo ninastahili kuonana naye tena ana kwa ana? Moyo wangu hautaki kabisa na hauko tayari kuonana tena na Happy lakini kwa kuwa hili ni ombi la Savanna itanibidi nikaze moyo na kukubali aje atoe ushahidi wake.” Akawaza Patrick halafu akamgeukia Savanna
“Unafahamu mahala aliko Happy kwa sasa? Savanna akainuka na kumfuata Patrick pale alipokuwa amesimama.
“Patrick kuna jambo lingine ambalo naomba ulifahamu”
“Jambo gani hilo Savanna?
“Happy hayupo hapa nchini”
“Hayupo hapa nchini?.How do you know that she’s not here? Akauliza Patrick kwa wasi wasi
“Samahani Patrick kwa kutokufahamisha suala hili toka mwanzo lakini naomba nikufahamishe kwamba mimi ndiye niliyemsaidia Happy kuondoka hapa nchini” akasema Savanna.Patrick akazidi kuchanganyikiwa
“Savanna unazidi kunichanganya akili yangu.Ulimsaidia Happy kuondoka hapa nchini? Kwa nini hukuniambia muda wote huu? Do you know where she is now?
“Patrick ni hadithi ndefu sana na sikutaka kukwambia mapema kwa sababu nilijua utaumia na mimi sitaki kukuona ukiumia.”
“Ok niambie nini kilitokea? Happy yuko wapi? Akauliza Patrick.Savanna akainama akafikiri kidogo halafu akasema
“Nilipigiwa simu usiku na mzee Kibaho baba mzazi wa Happy akaniuliza kama nina taarifa zozote kuhusiana na Happy kwani hakuwa ameonekana nyumbani kwao toka alipoondoka asubuhi.Sikujua mahala alipokuwa Happy na mara ya mwisho kuonana naye ilikuwa ni gerezani asubuhi.Hii ilikuwa ni siku ile nilipokuja gerezani na mama na tukamkuta Happy pale mama akamfokea sana.” Savanna akasema halafu akamtazama Patrick kisha akaendelea
“Asubuhi ya siku iliyofuata nikiwa najiandaa kuja gerezani ,alikuja mmoja wa wafanyakazi wangu akiwa na gazeti lililokuwa na picha chafu za Happy katika ukurasa wa mbele.Nilistuka sana baada ya kuziona picha zile na kama haitoshi mtumishi yule akainionyesha pia na video iliyokuwa mtandaoni.Ilinibidi nimpigie simu Margreth naye akanifahamisha kwamba Happy alikuwa amekunywa sumu kwa lengo la kujiua.Nilikwenda hadi katika hospitali ya Brahmaputra ambako Happy alikuwa amekimbizwa na kupatiwa huduma ya kuondolewa sumu mwilini.Nilishauriana na familia yake na tukakubaliana kwamba ili kumuepusha Happy na aibu kubwa aliyoipata itabidi kumpeleka mafichoni nje ya nchi sehemu ambako hakuna mtu anayemfahamu .Kama mchango wangu kwao nilijitolea usafiri wa kwenda Kigali Rwanda ambako tayari nilikwisha fanya mawasiliano na meneja wa hoteli moja kubwa mjini Kigali ambaye ni rafiki yangu na kumuomba Happy akae katika hoteli yake hadi hapo atakapopona kabisa .Mimi baba yake,mzee Kibaho pamoja na daktari mmoja tulielekea Kigali Rwanda na nilimuacha Happy kule akiwa na baba yake pamoja na daktari “ akasema Savanna.
“So she’s in Kigali now? Akauliza Patrick
“Alikuwa Kigali lakini kwa taarifa nilizozipata toka kwa rafiki yangu Christine ni kwamba Happy alitoweka pale hotelini na hakuna anayefahamu alikwenda wapi.” Akasema Savanna
“Ouh my God.Tumekwama tena” akasema Patrick
“Tukitaka kumpata Happy hatuna budi kuwasiliana na familia yake.Nina imani lazima watakuwa wanafahamu mahala alipo”
“Hilo nalo ni tatizo lingine.Sina hakika kama familia yake inaweza kutupa ushirikiano na kutuambia mahala aliko Happy” akasema Patrick
“Mimi ndiye nitakayekwenda kuonana nao.Nina imani msaada wangu hawataweza kuusahau kwa hiyo watanisaidia”
“Hata kama familia yake itakubali kushirikiana nasi ,vipi kuhusu Happy mwenyewe atakuwa tayari kurudi tena hapa Tanzania kutoa ushahidi wake baada ya mambo ya aibu kubwa aliyoyafanya? Sina hakika kama anaweza akakanyaga tena Tanzania hasa kutokana na aibu kubwa aliyoipata kutokana na uchafu mkubwa alioufanya.Sina hakika kama suala hili litafanikiwa Savanna,Naomba tusiumize vichwa vyetu kuhusu huyu mwanamke.Tutafute njia nyingine ya kutusaidia na si kumtegemea Happy” akasema Patrick akionyeaha kukata tamaa kabisa ya kumpata Happy
“Patrick mpenzi wangu laiti kama kungekuwa na njia nyingine ya kufanya nisingethubutu kukutajia jina la Happy lakini kwa hatua tuliyofikia ni lazima tumpate Happy.We’re almost to the end.Patrick naomba uniruhusu mimi nikaonane na familia ya Happy nitawalilia na kuwaomba wanisaidie.Mzee Kibaho ni mtu mwelewa sana na nina hakika atakuwa tayari kutusaidia”
Patrick akainama akafikiri kidogo na kusema
“Do what you have to do Savanna lakini moyo wangu haujapenda kuonana na Happy kabisa”
“Ahsante sana mpenzi wangu.Umefanya jambo la maana sana kwa kukubali.Najua si maamuzi mepesi lakini its for the best of us.I promise you that we’re going to finish this once and for all” akasema Savanna,Patrick hakujibu kitu

* * * *

Saa nne za asubuhi siku iliyofuata ilimkuta Savanna nje ya geti la nyumba ya akina Happy.Ni muda mrefu umepita toka alipokuja katika nyumba hii.Akiwa ndani ya gari lake ,alilitazama geti la nyumba ile na kuvuta pumzi ndefu
“Help me God.Laiti ningekuwa na namna nyingine ya kufanya katu nisingethubutu kuja tena katika nyumba hii.Sikutaka Happy aonane tena na Patrick hasa katika wakati ambao penzi letu limekwisha weka mizizi imara,lakini kwa hali halisi ilivyo ninalazimika kurejea tena katika nyumba hii kutafuta msaada” akawaza Savanna halafu akashuka na kwenda kubonyeza kengele ya getini
Baada ya dakika moja geti likafunguliwa.Alikuwa ni mama yake Happy.Savanna akaingiwa na woga kidogo lakini akakaza moyo akasalimiana na mama yake Happy na kukaribishwa ndani
“Savanna umepotea sana mwanangu.Habari za siku nyingi?
“Kazi zimekuwa nyingi mama na ndiyo maana sijafika hapa muda mrefu sijafika kuwatembelea.Habari za hapa?
“Habari za hapa nzuri Savanna.Karibu sana” akasema mama Happy kisha mtumishi wa ndani akawahudumia vinywaji
“Mama mna mawasiliano yoyote na Happy? Nilipigiwa simu na Christine yule rafiki yangu niliyemkabidhi amuhudumie kule Kigali kwamba Happy aliondoka katika hoteli ile aliyokuwa anakaa na mpaka sasa hajui alipo.Nimepata wasi wasi sana na nikaona ni bora nije kuuliza kama mnalifahamu jambo hili” akasema Savanna na mama yake Happy akaonyesha mstuko Fulani
“Savanna suala hili tumelisikia na hata sisi limetustua sana.Mpaka hivi sasa hatujui Happy yuko wapi na hatuna mawaliano naye yoyote.Tumeamua kumuachia Mungu na kumuomba amlinde na kumpa uzima kokote kule aliko.Tunaamini siku moja lazima atarejea nyumbani” akasema mama Happy
Savanna kijasho kikamtoka.Akavuta pumzi ndefu na kusema
“Ouh my gosh !
Kimya kikatanda mle sebuleni halafu Savanna akauliza
“Margreth naye yuko wapi?
“Margreth yuko kazini “
Savanna akainama na kufikiri kwa muda kisha akasema
“Mama mimi nakwenda.Tutaonana tena siku nyingine.Endapo mtapata mawasiliano yoyote ya Happy naomba mtanitaarifu “akasema Savanna huku akiinuka.Mama yake Happy akastuka
“Savanna kulikoni? Mbona ghafla hivyo?
“Utanisamehe mama nimekumbuka kwamba nina miadi na mtu wa muhimu sana muda mfupi ujao.Nitakuja tena kukusalimu siku nyingine” Akasema Savanna na kuonyesha kwamba hakutaka tena maongezi akaingia katika gari lake na kuondoka
“Kuna kitu nimekigundua toka kwa mama yake Happy. Alikuwa na wasi wasi mwingi.Inaonekana kuna jambo analifahamu kuhusu Happy na hakutaka kunieleza.Margreth au mzee Kibaho wanaweza wakanipa ukweli halisi.Ngoja kwanza nikaonane na Margreth” akawaza Savanna halafu akaegesha gari pembeni ya barabara akachukua simu yake na kumpigia Margreth
“Hallo Savanna.Habari za siku nyingi? Akasema Margreth baada ya kupokea simu
“Habari nzuri Margreth.Hatujaonana muda mrefu sana”
“Ni kweli Savanna.Mbona umekuwa kimya hivyo?
“Ni mihangaiko tu Margreth.Uko wapi sasa hivi?
“Sasa hivi niko kazini lakini niko mbioni kutoka nataka kwenda kuhudhuria mazishi ya rafiki yangu”
“Margreth,ninahitaji sana kuonana nawe.Kuna jambo muhimu nahitaji kuongea nawe.Tunaweza kuonana kabla hujaenda msibani?
“Hakuna tatizo Savanna.Tukutane wapi?
“Tuonane pale Lemina Café.Ninaelekea huko sasa hivi.Utanikuta pale”
“Sawa Savanna.Nakuja hapa muda si mrefu” akajibu Margreth na kukata simu.

* * * *

Habari za siku nyingi Margreth? Alianzisha mazungumzo Savanna baada ya kuonana na Margreth
“Habari nzuri Savanna.Umepotea sana dada yangu”
“Ni kweli Margreth ni muda mrefu sana hatujaonana.Hii inachangiwa na majukumu mengi ya kazi”
“Ni kweli kabisa Savanna” akajibu Margreth.
“ Patrick anaendeleaje? Kesi yake imefikia wapi?
“ Patrick anaendelea vizuri na kesi yake naendelea vizuri pia.Kwa hivi sasa kinachoendelea na kusikilizwa kwa mashahidi wa utetezi.Tutalimaliza suala hili” akasema Savanna
“ namuombea Mungu Patrick suala hili liishe na aendelee na maisha yake” akasema Margreth kisha kikapita kimya kifupi.Savanna akasema
“Margreth nimekuita hapa nina tatizo ambalo nahitaji sana msaada wako” akasema Savanna
“Usijali Savanna niko tayari kukusaidia kwa lolote”
“Ahsante sana.Tatizo langu ni kutaka kufahamu mahala aliko Happy.Nahitaji kuzungumza naye”
Margreth akastuka na kumuangalia Savanna
“Happy ..?!! akauliza Margreth.
“Ndiyo.Nina shida kubwa ya kuongea na Happy.”
“Happy yuko Kigali mahala ulikomuacha” akajibu Margreth na kumfanya Savanna acheke kidogo
“Happy hayuko Kigali.Aliondoka kule muda mrefu sana .Tafadhali naomba Margreth unisaidie nizungumze na Happy.” Akasema Savanna.Margreth akaona aibu kidogo na kutabasamu
“Samahani Savanna kwa kutaka kukudanganya lakini ukweli ni kwamba taarifa hiyo uliyonayo ndiyo hata sisi tunayo.Tulitaarifiwa kwamba Happy ameondoka katika hoteli aliyokuwa akikaa na haijulikani alielekea wapi.Tumejaribu sana kumtafuta bila mafanikio.Kwani kuna tatizo gani Savanna?
“Nina tatizo kubwa sana kumuona Happy.Tatizo ninalomtafutia Happy ni kwa sababu ya Patrick.”
“Patrick !!..” Margreth akashangaa
“Patrick anamtafutia nini Happy?
“Nadhani ulisikia kwamba Patrick alipata dhamana akatoka gerezani”
“Dada Savanna kwa kweli sihitaji kusikia au kufuatilia lolote linalohusiana na Patrick.Yeye ndiye chanzo cha dada yangu kuteseka na kupoteza mwelekeo mzima wa maisha yake.Kila anapokuwa karibu na Happy basi lazima kuna jambo baya linatokea.Kabla hajaonana na Patrick maisha ya Happy yalikuwa mazuri na yenye furaha lakini mara tu alipokutana na Patrick basi maisha yake yamebadilika ghafla na kupoteza kabisa mwelekeo mzima wa maisha yake.To be honest I hate that dude” akasema Margreth
“Nakuelewa sana Margreth lakini naomba nikukumbushe kwamba mara ya kwanza Patrick aliua bila kukusudia wakati akimuokoa dada yako asidhalilishwe na kundi la wahuni waliokuwa na lengo la kumbaka.Alifungwa gerezani na yakatokea yaliyotokea hadi walipokuja kukutana tena siku chache kabla ya kufunga ndoa.Kwa mapenzi makubwa waliyokuwa nayo na kwa ridhaa yao wenyewe waliamua kuachana na wapenzi wao ili waweze kutimiza ndoto yao ya kuwa pamoja.Katika ugomvi ule uliotokea na kupelekea kifo cha Vero na ni Happy ndiye aliyemsukuma Vero akajigonga ukutani na kufariki dunia.Kwa mapenzi makubwa aliyokuwa nayo Patrick wa Happy aliamua kuubeba mzigo wote wa kesi hii.Na kwa taarifa yako ni kwamba mimi ndiye niliyepambana na kumtoa Happy katika kesi ile kwa ombi la Patrick.Kwa maana hiyo hakuna sababu ya kumlaumu Patrick” akasema Savanna.Margreth hakusema kitu na kwa mbali macho yake yalionyesha kulengwa na machozi
“Kesi ya Patrick inaendeleaje? Akauliza Margreth
“Mashahidi wanaendelea kutoa ushahidi wao na wiki hii shahidi aliyebaki atatoa ushahidi wake na baada ya hapo atabaki shahidi mmoja tu katika orodha ya mashahidi upande wa uetetezi.Ni Happy.Yeye ndiye mtu wa mwisho kutoa ushahidi wake .Ushahidi wake una nguvu sana kwa sababu yeye ndiye anayeifahamu vyema historia yake na Patrick na kila kitu kilichotokea usiku ule.Kwa hiyo namuhitaji sana Happy.Nakuomba kama unafahamu mahala alipo niambie tafadhali”akasema Savanna.
“Sifahamu aliko Happy” akajibu Margreth.Savanna akamtazama kwa macho makali na kusema
“Margreth nafahamu kuna kitu ambacho unanificha”
“I don’t know anything Savanna” akasema Margreth
“Margreth mimi ni rafiki wa familia yenu.Nilimsaidia Happy kama ndugu yangu wakati alipokutwa na matatizo.Na mimi nimepatwa na tatizo na ninaomba mnisaidie kama ndugu yenu.Sina maana ya kwamba nataka Patrick na Happy warudiane tena la hasha.Ninachotaka mimi ni ushahidi tu tena teknolojia imeimarika sana siku hizi anaweza akatoa ushahidi wake huko huko mahala aliko na si lazima aje Tanzania” akasema Savanna
“Savanna nimekwisha kwambia kwamba sifahamu mahala aliko Happy,mbona hutaki kunielewa? Akafoka Savanna
“Ok! Ok! nimekuelewa Margreth.Hakuna yeyote kati yenu anayeiona thamani ya Patrick tena.Natumai nyote mnatamani kusikia Patrick amefungwa gerezani.I cant let Patrick go to jail after all that has sacrificed.He’s my friend and I’ll do anything to set him free.Nitakwenda kumtafuta Happy mimi mwenyewe kwa gharama zangu na kwa njia ninayoijua mimi.Kama bado yuko hai nakuhakikishia kwamba nitampata tu.Kesho nitakwenda Kigali na nitaanza kumtafuta Happy tokea pale.Nina marafiki wengi pale na watanisaidia kujua Happy alipo.Ahsante kwa kuitika mwito wangu.Tutazidi kuonana” akasema Savanna halafu akainuka akachukua mkoba wake na kuanza kuondoka.
“Savanna wait…!! akasema Margreth.Savanna akageuka ,akamtazama Margreth na kurejea pale mezani
“Unasemaje Margreth? akauliza Savanna
“Naomba ukae chini Savanna” akasema Margreth
“Savanna umenipa wakati mgumu sana.Nashindwa nifanye nini lakini naomba nikufahamishe kwamba ninafahamu mahala alipo Happy” akasema Margreth.Uso wa Savanna ukaonyesha tabasamu .
“Ahsante sana Margreth kwa kuwa muwazi.Happy yuko wapi?
“Happy aliondoka Kigali na kuelekea Marekani .Kwa sasa anashi Los angeles .Yeye binafsi hataki mtu yeyote zaidi ya familia yake afahamu mahala aliko.Hivi sasa maisha yake ni mazuri na yenye amani.Nimeamua kukueleza ukweli wa mahala alipo Happy kutokana na uzito wa suala unalomtafutia japo najua kutakuwa na mtafaruku kwa sababu nimevunja makubaliano yetu ya kutomweleza mtu yeyote mahala aliko” akasema Margreth
“Usihofu Margreth.Hakuna mwingine zaidi yangu atakayejua kuhusu jambo hili.Sasa nieleze nitampata vipi? Unaweza kunipatia mawasiliano yake?
“Its not that simple Savanna.Nitakachofanya mimi ndiye nitakayeongea naye kwanza ili tuone atatoa jibu gani.Naomba niwe wazi kwako kwamba Happy hataki mawasiliano na mtu yeyote sasa na hasa hasa wewe.Sijui ulimfanya kitu gani kwani aliweka wazi kwamba katika watu anaowachukia basi wewe ni mmoja wao.Naomba uniachie mimi hiyo kazi nitaongea naye halafu nitakwambia jibu atakalonipa” akasema Margreth
“Ahsante sana Margreth.Nakuomba ujitahidi kwa kadiri utakavyoweza umshawishi akubali.Mkumbushe kwamba hatima ya Patrick iko mikononi mwake.”
“Ni kazi ngumu Savanna lakini nitajitahidi” akajibu Margreth.
“Jitahidi Margreth.Hata kama italazimika kumtumia tiketi ya ndege ya kuja na kurudi mimi niko tayari kugharamia.Kitu kingine ambacho unapaswa kumkumbusha ni kwamba hakuna mtu mwenye lengo la kumshawishi arejeshe uhusiano wake na Patrick kwani najua tayari ana maisha yake yenye furaha halikadhalika Patrick naye ana maisha yake yenye furaha pia.Tunachohitaji sisi ni ushahidi tu ambao utamuweka huru Patrick “ akasema Savanna halafu akafungua pochi lake na kutoa bunda la noti akahesabu noti kumi na tano za elfu kumi kumi na kumkabidhi Margreth.
“Hizi ni kwa ajili ya mawasiliano na Happy” akasema Savanna.Margreth akazichukua fedha zile na kumrudishia
“Nashukuru sana Savanna lakini naomba uziweke pesa hizo utazitumia kwa kitu kingine.Nitafanya mawasiliano kwa gharama zangu.” Akasema Margreth .Savanna akazichukua fedha zile na kuweka mkobani wakaagana akaondoka
Baada ya Savanna kuondoka,bado Margreth aliendelea kubaki pale mezani akiwa na mawazo mengi
“Nimefanya kosa kubwa sana kuvunja makubaliano yangu na Happy . Kwa mdomo wake mwenyewe alitamka kwamba hataki tena kurudi Tanzania.Nitaanzaje kumwelezea kuhusiana na suala hili? Ouh my gosh ! nimekoroga mambo.Happy atanilaumu sana kwa jambo hili lakini kwa upande mwingine ana haki ya kufahamu kinachoendelea huku nyumbani.Ana kila sababu ya kuja kutoa ushahidi mahakamani na kumuepusha Patrick na adhabu yoyote anayoweza kuipata kwa kosa ambalo hakulitenda.” Akawaza Margreth halafu akainuka akachukua mkoba wake na kuondoka
Margreth alifika nyumbani kwao lakini kabla hajaingia chumbani kwake mama yake akatokea
“Margreth mbona umewahi kurudi leo?
“Ninakwenda kuhudhuria mazishi ya yule rafiki yangu aliyefariki juzi” akasema Margreth
“Maggie ,Savanna alifika hapa “
“Alikuwa anataka nini? Akauliza Margreth
“Kikubwa alichoniuliza ni kama tuna mawasiliano na Happy au kama tufahamu mahala aliko hivi sasa.”
“Ulimjibu nini?
“Nilimjibu kwamba hata sisi hatufahamu mahala aliko Happy.Baada ya jibu hilo akaondoka zake.Nina wasi wasi sana kwa kuamua kumtafuta Happy hivi sasa.Sitaki kabisa wafahamu mahala Happy alipo” akasema mama yake
“Mama nimeonana na Savanna.Alinipigia simu wakati nikitoka kazini na nikaonana naye.Ni kweli ana tatizo na ndiyo maana anamtafuta Happy.” Akasema Margreth
“Ana tatizo gani? Sitaki wamuhusishe tena mwanangu katika masuala yao.”
“Mama Savanna ana matatizo makubwa na ni lazima aonane au awasiliane naye”
“Ana tatizo gani?
“Ni kuhusiana na ile kesi ya Patrick”
“Kesi ya Patrick ?!!..mama yake akashangaa
“Ndiyo mama.Happy anatakiwa atoe ushahidi wake.”
“Margreth ..!!!! akasema mama yake
“Hapana Margreth.Mwanangu Happy kamwe sintaruhusu aje tena huku na kuonana tena na Yule kijana.Mambo aliyokumbana nayo yanatosha sitaki tena mwanangu aumie.Maisha yake ni mazuri kwa sasa na tayari amekwisha msahau Patrick.Sitaki aonane tena na yule kijana aliyejaa mabalaa mwili mzima”

TUKUTANE SEHEMU IJAYO..........
 
Aisee kawawa ubalikiwe tupia mbili za kulalia mkuu
 
MISS TANZANIA
SEHEMU YA 54
MTUNZI😛ATRICK.CK
CONTACK:0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Mama Savanna ana matatizo makubwa na ni lazima aonane au awasiliane naye”
“Ana tatizo gani?
“Ni kuhusiana na ile kesi ya Patrick”
“Kesi ya Patrick ?!!..mama yake akashangaa
“Ndiyo mama.Happy anatakiwa atoe ushahidi wake.”
“Margreth ..!!!! akasema mama yake
“Hapana Margreth.Mwanangu Happy kamwe sintaruhusu aje tena huku na kuonana tena na Yule kijana.Mambo aliyokumbana nayo yanatosha sitaki tena mwanangu aumie.Maisha yake ni mazuri kwa sasa na tayari amekwisha msahau Patrick.Sitaki aonane tena na yule kijana aliyejaa mabalaa mwili mzima”

ENDELEA………………….

“mama..!!! “ akasema Margreth
“Hapana Margreth.Siruhusu mwanangu kushiriki kwa namna yoyote katika kesi hii.Tayari maisha yake yametulia hivi sasa na sitaki apate tena matatizo mengine.”
“Mama kama Happy asipofanya hivyo kuna uwezekano Patrick akafungwa gerezani.”
“Itakuwa vyema kama akifungwa.Ninamchukia sana yule kijana na kama ningekuwa na uwezo ningemuondoa kabisa katika uso wa dunia” mama yake Happy akasema kwa ukali
“mama si sahihi kusema hivyo.Kumbuka Patrick alikubali kuubeba mzigo mzito wa kesi kwa kosa ambalo hakulitenda.Happy ndiye aliyeua na ndiye anayestahili kusimama mahakamani hivi sasa lakini Patrick ameliepusha hilo na amejitolea yeye mwenyewe kuubeba mzigo huu.Mama huoni kwamba Happy analazimika kuwa mstari wa mbele kumtetea Patrick? Ninajua kwa sasa amekwisha anza maisha mapya na hana mpango tena na Patrick wala kurejea nyumbani lakini pamoja na hayo bado ana wajibu wa kuja kumtolea ushahidi mwenzake.” Margreth akajitahidi kumuelewesha mama yake ambaye bado alionekana kutokubaliana kwa namna yoyote ile na hoja ile ya kumtaka Hapy atoe ushahidi kwa Patrick
“Pamoja na hayo,bado sitaki mwanangu arejee.Sitaki aumie tena.Margreth wewe mwenyewe unafahamu fika kwamba yule kijana sijui amempa nini Happy.Kitendo cha Happy kumuona tu basi huwa anasahu kila kitu na kumkimbilia yeye.Kwa sasa Happy amekwisha rudiana tena na Mike na maisha yake yana furaha sitaki aonane tena na yule kijana.“ mama Happy bado aliendelea kuushikilia msimamo wake
“Mama natambua Happy tayari ameamua kuendelea na maisha yake na hana tena mpango wa kuendelea na Patrick kwa hiyo usiogope hata kama wataonana hakuna kitakachotokea.Anachotakiwa kufanya yeye ni kutoa tu ushahidi wake halafu aondoke zake akaendelee na maisha yake.Isitoshe hata Patrick naye amekwisha endelea na maisha yake na hana tena mpango na Happy”
“Margreth nimekwisha kueleza kwamba hata unishawishi vipi Happy hatakuja tena na kuonana na Patrick.Neno langu mimi ni la mwisho na sitaki tena mjadala huu uendelee.” Akasema mama yake Happy huku akiondoka akiwa amekasirika sana.Margreth naye akaelekea chumbani kwake na kujitupa kitandani
“Sikubaliani na mama hata kidogo.Hatutatenda haki kama Happy hatatoa ushahidi wake mahakamani kumtetea Patrick mtu aliyeubeba mzigo wa mashtaka yaliyokuwa yanamkabili yeye.Lazima niwasiliane na Happy nisikie naye ana maoni gani kuhusu suala hili.Tukifanya mchezo Patrick anaweza akafungwa” Akawaza Margreth halafu akaichukua simu yake na kuzitafuta namba za Happy akapiga huku moyo wake ukimwenda mbio.Simu iliita na kukata.Akaangalia saa ya ukutani ilionyesha ni saa sita za mchana
“Yawezekana yuko katika usingizi mzito kwani mida hii huko kwao bado ni usiku.Ngoja nimpigie tena” Margreth akapiga tena
“Hallow “ simu ikapokelewa na sauti nzito ya kiume.Margreth akastuka na kudhani labda amekosea namba
“Halow naitwa Margreth,napiga simu toka Tanz…..” kabla hajamaliza,yule mwanaume aliyepokea simu akasema
“Margreth,Mike hapa naongea.Habari za Tanzania?Umekwisha isahau sauti yangu mara hii?
Margreth akavuta pumzi ndefu na kusema
“Mike !! nafurahi kuongea nawe tena.Ni muda mrefu umepita.Samahani kwa kukusumbua na kukuamsha usingizini.Nilikuwa Nahitaji kuongea na Happy”
“Happy niko naye hapa.Subiri kidogo nimuamshe” akasema Mike na baada ya muda sauti yenye usingizi ya Happy ikasikika
“Hallow Margreth”
“Happy.!! Samahani nimekuamsha”
“Usijali Margreth hata hivyo nimelala muda si mrefu sana.Mike amekuja leo hivyo tukaenda club,Habari za huko?
“Huku kwema Happy,tunaendelea vizuri isipokuwa yule rafiki yangu Salama amefariki dunia wakati akijifungua na leo tunamzika”
“Salama yule aliyeolewa na mzungu?
“Ndiyo huyo”
“Dah ! poleni sana.Habari nyingine?
“Habari nzuri Happy.” Akasema Margreth
“Maggie nilikuahidi kukutumia ile hela ya kununua gari,sijasau nitakutumia wiki ijayo,wiki hii nilikuwa nimetingwa sana na kazi”
“Ahsante sana Happy lakini sijakupigia kwa ajili ya suala hilo.Kuna suala linguine”
“Suala gani Maggie?
“Happy kuna tatizo limejitokeza”:
“Tatizo gani? akauliza Happy.Margreth akashusha pumzi na kusema
“Its about Patrick”
“Patrick ..!!!! “ Happy akastuka
“Ndiyo Happy.Nimeoanana na Savanna muda si mrefu na amenifahamisha kwamba Patrick alifanikiwa kupata dhamana na yuko huru lakini kesi yake inaendelea kusikilizwa na kinachoendelea hivi sasa ni mashahidi wa upande wa utetezi kutoa ushahidi wao.Savanna alitaka kufahamu mahala ulipo” akasema Margreth
“Ananitafuta mimi? Kwa nini? Akauliza Happy kwa wasi wasi
“Jina lako liko katika orodha ya watu wanaotakiwa kutoa ushahidi wao mahakamani kumtetea Patrick”
“No ! No ! no !!!..Thats impossible.Margreth no body should know where I am.” Akasema Happy
“Its too late Happy.Nimelazimika kumweleza ukweli Savanna kutokana na uzito wa suala lenyewe.”
“Ouh Margreth how on earth could you do such a thing? Tulikubaliana kwamba asiambiwe mtu mwingine yeyote mahala nilipo.Kwa nini lakini umefanaya hivyo? How could you betray me? Akalalama Happy
“Naomba unisamehe sana Happy kwa kilichotokea.Najua yalikuwa ni makubalianao yetu kwamba asifahamu mtu mwingine yeyote mahala ulipo lakini nimelazimika kumweleza Savanna na hakuna mtu mwingine yeyote anayelifahamu hilo zaidi yake.”
“Margreth siwezi kukuamini tena.Umeyafanya maisha yangu yawe magumu tena.Umenifanya nirudi tena katika kile ambacho nimekuwa nikikimbia kwa muda huu wote” akasema Happy
“Happy naomba unisikilize kwa makini.Nililazimika kumweleza Savanna mahala ulipo baada ya kuniweka wazi kwamba ushahidi wako una nguvu sana ya kumsaidia Patrick asihukumiwe kifungo.Happy hata mimi inaniuma sana kukukumbusha mambo ambayo unajitahidi kuyasahau lakini naomba niwe muwazi kwako kwamba you have to save Patrick.He saved you from going to jail and its your turn now to save him” akasema Margreth.Baada ya ukimya mfupi Happy akasema
“Margerth nimekuelewa lakini sina hakika kama nitaweza kufanya hivyo.Ninapambana hivi sasa kumsahau Patrick na kuendelea na maisha yangu mapya yenye furaha na siko tayari kuonana tena na Patrick ana kwa ana.” Akasema Happy
“Happy sina maana ya kwamba ukitoa ushahidi utarudiana tena na Patrick na wala sikushauri ufanye hivyo lakini nakukumbusha tu kwamba Patrick ameubeba mzigo mkubwa sana na endapo atafungwa kwa sababu tu ya kukosekana ushahidi wenye nguvu,nakuapia Happy hautakuwa na furaha hata siku moja katika maisha yako.Patrick’s shadow will haunt you forever” Akasema Margreth
“What can I do Margreth? Let it be.Look Margreth ,there is nothing I can do now to help him.I’m trying to pick up the pieces and arrange my life again so I cant go back to square one.Nilimtenda vibaya Mike na kumsababisia maumivu makali ya moyo lakini hivi sasa ndiye amekuwa msaada wangu mkubwa na ndiye anayenisaidia kusahau mambo yote yaliyopita.Ninaishi hapa Marekani kwa sababu yake.Amenitafutia nyumba,kazi na kila kitu.He loves me and I’m learning to love him so how could I tell him that I’m going back to Tanzania? Please Margreth,this conversation is over.” Akasema Happy
“Happy kabla hujakata simu naomba nikukumbushe kitu kimoja.Ulinitamkia wewe mwenyewe kwa mdomo wako kwamba Patrick hakusababisha kifo cha Vero bali ni wewe uliyemsukuma akajigonga ukutani na kufariki.Patrick kwa mapenzi makubwa aliyokuwa nayo kwako aliamua kujitwisha yeye mzigo wote .Ameteseka gerezani kwa kipindi kirefu na bado anaendelea na kesi.Nomba leo unitamkie neno moja tu kwa mdomo wako kwamba uko tayari Patrick afungwe gerezani kwa kosa ambalo hakulitenda? Nipe jibu moja tu na nitakuelewa” akasema Margreth.Happy machozi yakamtoka
“I don’t know Margreth.’ll call you later” akasema Happy na kukata simu.Machozi yalianza kumtoka na akaanza kulia kwa kwikwi.Mike aliyekuwa chumbani akatoka haraka aliposikia Happy akilia kwa kwikwi.
“Happy kuna nini? Mbona unalia? Kuna taarifa ambayo si nzuri? Akauliza Mike
Happy akamkumbatia Mike kwa nguvu huku akiendelea kulia
“Nyamaza kulia mpenzi wangu na uniambie nini kinakuliza.Kuna tatizo gani nyumbani? Akauliza Mike.Happy hakujibu kitu aliendelea kulia kwa kwikwi.Mike akamletea glasi ya maji akanywa
“Tafadhali niambie Happy una tatizo gani?
“Mike kuna tatizo limetokea”
“Niambie Happy ni tatizo gani ? Niko hapa kukusaidia”
“Si tatizo kubwa lakini linahusiana na kesi ya Patrick” akasema Happy na kumstua Mike
“Nini kimetokea katika hiyo kesi?
“Savanna wakili anayemtetea Patrick amefika nyumbani leo hii na kuulizia taarifa zangu na kuomba apatiwe mawasiliano yangu lakini kwa bahati mbaya amekutana na Margreth na akamueleza kila kitu kuhusu mimi”
“Ouh my gosh ! Kwa nini lakini amefanya hivyo wakati mlikwishakubaliana kwamba mtu yeyote asifahamu mahala ulipo?
“Kwa madai ya Margreth ni kwamba aliamua kumweleza ukweli Savanna kutokana na uzito wa suala hilo alilokuwa ananitafutia”
“Ni suala gani alilokuwa anakutafutia?
Happy akafikiri kidogo na kusema
“Natakiwa kutoa ushahidi wangu mahakamani kumtetea Patrick.”
Kimya kikatanda mle ndani.Kila mmoja alikuwa anawaza lake.Mike alionekana kuishiwa nguvu.
“Happy my angel tell me its not true and if true you wont do it” akasema Mike
“Its true Mike.Natakiwa mahakamani nikatoe ushahidi wangu.
“That’s impossible.You cant go back there” akasema Mike.Alistushwa sana na taarifa ile ya Happy
“Happy mpenzi naomba unihakikishie kwamba hutakwenda tena Tanzania.Hutakwenda kuonana tena na Patrick.Kama ingekuwa ni kesi inayomkabili mtu mwingine nisingekuwa na wasi wasi wowote lakini kukuacha ukaonane tena na Patrick hilo ni jambo ambalo siwezi kulifanya” akasema Mike huku amemshika Happy mabegani
“Mike kuna jambo ambalo ningependa ulifahamu” akasema Happy
“Jambo gani Happy ? Mbona unanipa wasi wasi mpenzi wangu? Akauliza Mike.Happy akavuta punzi ndefu na kusema
“Patrick hakumuua Vero”
Mike akastuka na kumtumbulia Happy macho.
“Sikuelewi unamaanisha nini Happy.Patrick anatuhumiwa kwa kusababisha kifo cha Vero.Kwa nini unasema kwamba si yeye aliyesababisha kifo cha Vero? Akauliza Mike.Happy akamtazama usoni na kusema
“Mimi ndiye nilisababisha kifo cha Vero.” Akasema Happy
Mike akastuka na kumuachia Happy mikono halafu akasimama na kumuangalia Happy kana kwamba ni mara ya kwanza anamuona
“That’s not true .Its not true…” akasema Mike
“Its true Mike.I killed her.Samahani kwa kutokwambia kuhusu suala hili kwa sababu hii ni sehemu moja ya maisha yangu ambayo ninapambana ili niisahau.”akasema Happy
“Sikuelewi mpenzi wangu.Kwa nini unifiche kitu kikubwa kama hiki?
“Nisamehe mpenzi wangu.Naomba unisamehe Mike na unielewe kwamba sikufanya makusudi kutokwambia kitu kama hiki.Naamini hata wewe ungekuwa katika nafasi yangu ungefanya kama nilivyofaya mimi yaani kuliweka jambo hili kuwa ni siri ya moyoni.Ni jambo ambalo kila nikilifikiria huwa linanipa wakati mgumu sana.I’ve been trying to forget that night but I cant..” akasema Happy huku akishindwa kujizuia na kutoa machozi.Mike akamsogelea na kumkumbatia
“Nyamaza mepnzi wangu.Nyamaza Happy.Naomba unieleze ni kitu gani kilitokea usiku huo na kwa nini Patrick ndiye anayetuhuiwa kwa kusababisha mauaji hayo? Akasema Mike.Happy akafuta machozi akafikri kidogio na kusema
“Tulikuwa hotelini mimi na wewe tukipata chakula nilipopigiwa simu na Patrick kwamba kuna matatizo yametokea na baba yake amelazwa katika hospitali kuu ya magonjwa ya moyo .Kama utakumbuka nilikuomba unirudishe nyumbani ambako nilichukua gari langu na kukimbia hospitali.Nilimkuta Patrick halafu tukapanda katika ghorofa ya juu ambayo bado ujenzi wake ulikuwa unaendelea na Patrick akaanza kunisimuilia kilichotokea.Ghafla akatokea Vero akiwa na bastora mkononi.Alikuwa amekasirika na sura yake ilionyesha kwamba alikuwa amedhamiria kufanya kitu kibaya.Nadhani nilikueleza kuhusiana na kitendo alichokifanya Patrick cha kuvunja uchumba na Vero kitendo ambacho kilimuumiza sana.Alituelekezea bastora ile huku akitoa vitisho vingi sana na kutishai kututoa uhai mimi na Patricki.Patrick alimsihi aache utani na silaha za moto na ndipo alipoonyesha kwamba hakuwa akitania pale alipoachia risasi iliyonikosa na kupiga nguzo.Nilihisi kama nimekufa nikaanguka chini.Kitendo kile kilimkasirisha Patrick ambaye bila kujali hatari iliyokuwepo akamfuata Vero na kuanza kumnyang’anya Vero ile silaha.Kitendo kile kiliniogopesha sana na nikajua Vero angeweza kumdhuru Patrick hivyo nikainuka na kwenda kumsukuma Vero ambaye alijigonga ukutani na kufariki dunia.Patrick hakutaka nihusishwe katika kesi ile kwa kuamua kuubeba mzigo wote wa kesi ya mauaji .Kila mtu anajua kwamba Patrick ndiye aliyesababisah kifo cha Vero.Alikubali kuubeba mzigo huu mzito wa kesi kubwa kama hii kwa ajili yangu kwa ajili yua kunikinga na kesi hii.”akasema Happy.Mike akamtazama kwa makini na kusema
“Ahsante Happy kwa kunieleza ukweli lakini pamoja na hayo ninataka kukuuliza jambo moja ”
“Uliza Mike”
“Do you still love him? Akauliza Mike
“Mike !! ..akasema Happy
“Just answer my question Happy.Do you have any feeling for him?
“Mike I’m with you now.Its you that I love now.Nimekuwa nikijitahidi kuifuta picha ya Patrick moyoni mwangu na hiyo inamaanisha kwamba sina hisia zozote kwake”
“Are you sure? Akauliza Mike
“Yes Mike I’m sure”
“Kama ni kweli hayo unayoniambia kwa nini ulikuwa unalia baada ya kuzipata taarifa hizi?
“Mike hata kama ungekuwa ni wewe lazima ungetoa machozi.Patrick naye ni binadamu na anakabiliwa na kesi kwa kosa ambalo hakulitenda .Nilishindwa namna ya kufanya hasa katika wakati huu ninaojitahidi kumsahau ndiyo maana nikashindwa kujizuia kulia” akasema Happy
“Its ok Happy.Forget about that.Umeshaamua kuyasahau yote ya nyuma kwa hiyo songa mbele.Mimi niko hapa na niko tayari kukusaida kwa kila namna nitakavyoweza ili uweze kusahau historia na matukio yote yaliyopita.Let him go”
“Mike ! How could you say that? Ingekuwa ni wewe uko katika nafasi yangu ungefanya nini? Ungemuacha mtu kama huyu afungwe gerezani? He saved me.He saved a woman you love.So that’s how you repay him? Akauliza Happy
“So what’s your decision? Akauliza Mike
“Nitakwenda Tanzania.Nitakwenda kutoa ushahidi wangu mahakamani.Siko tayari Patrick afungwe gerezani.Tafadhali Mike naomba uniruhusu niende Tanzania nikamtolee Patrick ushahidi.Lengo langu ni ili Patrick awe huru na aendelee na maisha yake.Najua unaogopa nini kitatokea endapo nitaonana naye lakini nakuhakikishia kwamba kitakachonipeleka huko ni kutoa tu huo ushahidi wangu na jambo lingine lolote.Me and him its over.” akasema Happy.Mike akazunguka zunguka mle ndani na kusema
“Laiti nisingekuwa na marufuku ya kukanyaga ardhi ya Tanzania nisingekubali uende peke yako.Ningekupeleka ukatoe ushahidi wako halafu turudi wote marekani.Sijui ni kwa nini ninakosa imani na Patrick.” Akasema Mike kwa masikitiko
“Kwa maana hiyo unaniruhusu niende Tanzania? Akaulza Happy
“Sina haja ya kukuruhusi kwani tayari umekwisha fanya maamuzi na siwezi kukukatalia.Ni kweli Patrick anastahili kutendewa wema kama alioutenda kwako.Lakini sijui kwa nini roho yangu bado inasita sana”
“Huniamni Mike?
“Nakuamini sana mpenzi wangu lakini nashindwa kujizuia kuwa na wasi wasi kuja kwamba unakwenda kuonana na Patrick tena.Patrick alifanya kitendo cha kijasiri sana ambacho hata mimi kimenigusa ,lakini naomba nikiri kwako mpenzi wangu kwamba siwezi kushindana na Patrick katika vita ya kukugombania .Nafahamu Patrick amekuwa moyoni mwako kwa miaka mingi sana .Nenda Tanzania mpenzi lakini ujue kwamba ninakuamini na kwamba hutafanya kitendo kama ulichonifanyia kipindi kile kwani sijui kama nitaweza kuyavumilia maumivu na mateso ya moyo kama niliyoyapata wakati ule.” Akasema Mike
“Mike naomba uniamini haya nikwambiayo kwamba kilichobaki kati yangu na Patrick ni historia tu.Kinachonisukuma kutaka kwenda kutoa ushahidi wangu ni kumsaidia ili kama ikiwezekana aweze kuachiwa huru.Alionyesha ubinadamu mkubwa kwangu kwa hiyo na mimi sina budi kumsaidia.After this I’m done with him.Patrick atakuwa huru na maisha yake na mimi nawe tutakuwa huru” akasema Happy

* * * *

Margreth akiwa msibani pamoja na waombolezaji wengine mara simu yake ikaita.Alikuwa ni Happy aliyempigia
“Hallo Happy” akasema Margreth baada ya kupokea simu
“Tayari umefika msibani?
“Ndiyo Happy.Tunajiandaa kwenda kuzika”
“Sawa Magreth,nimekupigia kukutaarifu kwamba ninakuja Tanzania kutoa ushahidi wangu halafu nitarejea tena marekani. Najua nitakabiliana na matatizo mengi lakini sina namna lazima nikabiliane na kila kitu.Naomba uongee na Savanna na akwambie ni lini ninahitajika mahakamani.”
“Ouh god thank you so much.Ahsante sana Happy kwa uamuzi huu.Nitamtaarifu Savanna halafu nitakufahamisha jibu atakalonipa” akasema Margreth na kukata simu halafu akamtafuta Savanna na kumtaarifu kuhusiana na jibu la Happy” .Hizi zilikuwa ni habari njema sana kwa Savanna japokuwa alishindwa kujizuia kuwa na wasi wasi nini kitatokea pale Patrick na Happy watakapokutana tena
“Sijui ni kwa nini ninakuwa na wasi wasi mwingi kuhusu Patrick kuonana na Happy.Labda ni kutokana na historia yao kwamba kila wakutanapo hushindwa kuzizuia furaha zao basi mapenzi yao huanza upya.Lakini sipaswi kuwa na wasi wasi wowote.Patrick ni wangu na hakuna yeyote mwenye uwezo wa kumnasua toka katika mikono yangu.Ni Happy pekee ndiye mwenye kunipa wasi wasi “akawaza Savanna akiwa ofisini kwake

TUKUTANE SEHEMU IJAYO.....
 
MISS TANZANIA
SEHEMU YA 55
MTUNZI: PATRICK.CK
CONTACT:0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Sijui ni kwa nini ninakuwa na wasi wasi mwingi kuhusu Patrick kuonana na Happy.Labda ni kutokana na historia yao kwamba kila wakutanapo hushindwa kuzizuia furaha zao basi mapenzi yao huanza upya.Lakini sipaswi kuwa na wasi wasi wowote.Patrick ni wangu na hakuna yeyote mwenye uwezo wa kumnasua toka katika mikono yangu.Ni Happy pekee ndiye mwenye kunipa wasi wasi “akawaza Savanna akiwa ofisini kwake

ENDELEA………………….

Ndege ya shirika la ndege la afrika kusini iliwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam saa mbili za usiku.Miongoni mwa abiria waliokuwemo katika ndege hii ni Happy Kibaho ambaye monekano wake ulikuwa umebadilika sana na alionekana mrembo zaidi ya alivyokuwa alipoondoka Tanzania miezi zaidi ya kumi iliyopita.Kama ungekutana naye ghafla ingekuwia ugumu kidogo kumtambua.
Baada ya kukamilisha taratibu alitoka nje na kulakiwa na familia yake yote.Kilikuwa ni kipindi cha furaha kubwa kwa familia hii kukutana tena na mtoto wao ambaye hawakuwa wametegemea kama wangeonana naye tena hivi karibuni.Wote waliustaajabia uzuri wa Happy na namna alivyokuwa amebadilika.Hakukuwa na mwandishi yeyote wa habari aliyekuapo pale uwanjani kwani ujio wa Happy ulikuwa ni wa siri kubwa
“Wow Happy umebadilika sana” akasema mzee Kibaho na kumkumbatia mwanae kwa mara ya pili
“Ouh Dady ! nililazimika kufanya mabadiliko kidogo katika muonekano wangu wa zamani.Nilitaka nibadilike na kuwa Happy wa tofauti na zamani”
“You look so wonderfull and amazing as always.You look more than an angel” akasema mzee Kibaho kisha wote wakaelekea katika gari lao na kurejea nyumbani.Waliwasili nyumbani ambako kuliandaliwa tafrija ndogo ya kumkaribisha tena nyumbani Happy.Baada ya chakula na maongezi Happy akapelekwa chumbani kwake kulala.
“Margreth naomba nikalale chumbani kwako.Sitaki kulala katika chumba change cha zamani.Kuna kumbukumbu nyingi za nyuma ambazo nimekwisha anza kuzisahau.” Akasema Happy na kuelekea katika chumba cha Margreth.Kabla ya kulala,Happy akamkumbusha Margreth amtaarifu Savanna kwamba tayari amekwisha wasili na kama ana nafasi waonane kesho .Margreth akazitafuta namba za simu za Savanna akapiga.
Kwa muda wa dakika kadhaa sasa Savanna alikuwa anamkodolea macho Patrick bila kuongea lolote
“C’mon my angel ! Mbona unanitazama namna hiyo? Akauliza Patrick
“Sijui ni kwa nini nimejikuta nikiwa hivi siku ya leo.Natamani niendelee kukuangalia usiku kucha.Patrick nakupenda sana.Nakupenda zaidi ya unavyoweza kufikiri.Naomba niwe wazi kwako kwamba sintaweza kuishi maisha yangu bila ya kuwa nawe.” Akasema Savanna kwa sauti laini yenye mahaba mazito.Patrick akamvuta kwake na kumbusu kisha akasema
“Savanna wewe ni malaika wangu.Naomba ufahamu kwamba nakupenda na nitakupenda daima.Nakuahidi mara tu mambo haya yatakapokwisha basi tutafunga ndoa na tutaishi sote hadi kifo kitakapotutenganisha.” Akasema Patrck
“Patrick my love kwa nini tusifunge ndoa hata kabla ya kesi hii kumalizika? Binafsi sioni kipingamizi chochote cha kutuzuia tusifunge ndoa mapema” akasema Savanna
“Hakuna kipingamizi chochote Savanna cha kutufanya mimi nawe tushindwe kufunga ndoa.Kitu pekee kinachonisukuma na kunifanya niamni kwamba ni vyema kama tutafunga ndoa baada ya kesi kumalizika ni kuogopa kuchanganya mambo.Ninafikiria ni bora kama tukaelekeza nguvu katika jambo moja kwanza na baada ya kulimaliza basi tuelekeze nguvu katika jambo lingine ambalo ni ndoa yetu”
“Nakubaliana nawe Patrick japokuwa nilipenda sana jambo hili tulifanye mapema.Hata hivyo wazo lako zuri ni la msingi sana.Hatuna budi kuelekeza nguvu zetu zote kwa sasa katika kesi na baadae tushughulike na ndoa.” Savanna akastushwa na mlio wa simu yake.Akausogeza mkono na kuichukua
“Ni Margreth” akasema Savanna
“Anataka nini usiku huu? Akauliza Patrick
“sijui ngoja nimsikilize” akasema Savanna na kubonyeza kitufe cha kupokelea
“Hallo Margreth”
“Hallo Savanna.Samahani kwa kukusumbua usiku huu”
“Bila samahani Margreth.Jisikie huru kunipigia wakati wowote”
“Ahsante sana.Savanna nimekupigia kukutaarifu kwamba Happy amekwisha wasili.Amefika usiku huu.Ameomba kesho muonane hapa nyumbani”
“Ouh ok.Thats good news.Mwambie nashukuru sana kwa kufika kwake .Amefanya jambo kubwa na la maana sana na kesho nitakuja kuonana naye” akasema Savanna
“Kitu kingine Savanna,utakapokuja kuonana na Happy please don’t bring Patrick with you.Make sure Patrick and Happy they wont see each other.”
“Usijali Margreth.Siwezi kuambatana na Patrick. “
“Thank you Savanna.Good night”
“Good night Margreth” akajibu Savanna na kukata simu halafu akamgeukia Patrick
“Happy amekwisha wasili”
Patrick akavuta pumzi ndefu kisha akasema
“Hizo ni habari njema sana.”
“Yah.Amefanya jambo la maana ” akasema Savanna kisha akamkazia macho Patrick
“Nini Savanna? Mbona unaniangalia hivyo?
“Kuna kitu ambacho nahitaji uhakika toka kwako”
“Kitu gani Savanna?
“Are you sure there will be no problem when you see Happy again?
Patrick akamtazama Savanna akavuta pumzi ndefu na kusema
“Usihofu Savanna,nakuhakikishia kwamba hakutakuwa na tatizo lolote.Siwezi kukuficha kwamba tayari nimekwisha mtoa Happy moyoni mwangu lakini bado nina donge kubwa limenikaa kooni la kutaka kufahamu ni kwa nini alitenda vile ? Kwa nini alifanya kitendo kile cha kupiga picha na video za utupu na kuzivujisha? Zaidi ya yote kwa nini aliamua kunitelekeza gerezani wakati akifahamu fika kwamba nilikuwa nimeubeba mzigo ambao ulimuhusu yeye? Ningefurahi sana kama ningepata nafasi ya kumuuliza na kupata majibu ya maswali yangu lakini sintaweza kufanya hivyo kwani sitaki kukumbuka mambo ya nyuma.Kitu cha msingi ninachoshukuru ni kwa kukubali kwake kuja kutoa ushahidi.Baada ya kumaliza kutoa ushahidi sintahitaji kumuona tena.Nataka niendelee na maisha yangu nikiwa na wewe mpenzi wangu ambaye unanipenda,unanijali na kunithamini.” Akasema Patrick na uso wa Savanna ukajenga tabasamu pana,akainama na kumbusu halafu wakakumbatiana.

* * * *

Ni Happy ndiye aliyemuamsha mdogo wake Margreth asubuhi ili ajiandae awahi kazini.Usiku wa kuamkia siku hiyo ulikuwa mrefu sana kwa Happy na hakuweza kupata kabisa usingizi.Picha za matukio yaliyotokea miezi zaidi ya kumi iliyopita zilikuwa zkimjia kila alipojaribu kufumba macho.Alikumbuka toka kipindi alichokutana na Patrick shuleni Malangali Iringa hadi muda huu.
“Happy leo hujalala kabisa” akasema Margreth kwa sauti iliyojaa usingizi.Happy akatabasamu
“Mimi ni kawaida yangu.Huwa nina muda mchache sana wa kulala,muda mwingi ninafanya kazi.Amka ujiandae uende kazini” akasema Happy
Margreth akaamka akajindaa na kuondoa zake kuelekea kazini.Happy naye akatoka na kuanza kuizunguka nyumba yao.
Saa nne za asubuhi ilimkuta Savanna katika geti la akina Happy.Akapiga honi na Pendo mfanyakazi wa ndani akamfungulia geti na kumkaribisha ndani
Mtu wa kwanza kusalimiana naye alikuwa ni mzee Kibaho.Kwa kuwa mzee KIbaho alikuwa na haraka ya kuwahi katika shughuli zake hakuongea sana na Savanna akaondoka na kumuacha Savanna akiongea na mama yake Happy hadi pale Happy alipojitokeza.Savanna alishindwa kujizuia kutoa tabasamu pana sana baada kumuona tena Happy na namna alivyobadilika na kuwa mzuri
“My gosh ! huyu ni Happy au ni mzimu wake? Gosh ! she’s so pretty.She’s amazing.Dah ! binti huyu amejaaliwa uzuri wa aina yake” akawaza Savanna
“Hallow Savanna” akasalimu Happy
“Hallow Happy” akajibu Savanna na kuinuka kisha wakakumbatiana
“karibu tena nyumbani Happy” akasema Savanna
“Ahsante Savanna,nimefurahi sana kurejea tena nyumbani.Poleni na matatizo ya kila siku”
“Tumekwisha poa Happy.” Akasema Savanna halafu mama yake Happy akainuka na kuwaacha peke yao pale sebuleni ili kuwapa nafasi nzuri ya kuongea mambo yao kwa uhuru.
“Savanna twende bustanini ,naona hapa sebuleni hapatufai kwa maongezi yetu” akasema Happy kisha wakainuka na kuelekea bustanini
“Karibu sana Savanna.Habari za siku? Akaanzisha mazungumzo Happy baada ya kufika bustanini
“Habari nzuri Happy.Nimefurahi tena kukuona.Umebadilika sana.Ouh my gosh you are so beautiful.You are mazing” akasema Savanna na Happy akatabasamu
“Thank you Savanna” akajibu Happy
“Vipi maisha yako kwa ujumla? Akauliza Savanna
“Namshukuru Mungu .Kwa kweli Mungu anaweza.Ukimuomba kwa dhati Mungu anajibu.Nilikwisha kata tamaa kabisa na maisha yangu.Nilimuomba Mungu nikamlilia anisaidie na kweli amenisaidia na hali yangu imebadilika kama unavyoniona” akasema Happy na kucheka kidogo
“Nilipatwa na wasi wasi mkubwa Christine aliponipigia simu na kunitaarifu kwamba umetoweka pale hotelini Kigali na hawajui mahala ulipo.” Akasema Savanna na kumfanya Happy acheke kidogo
“Savanna kwanza kabisa napenda nikushukuru wewe binafsi kwani msaada wako ulikuwa mkubwa mno na ambao siwezi kuulipa.Ulinisaidia sana kujitambua na kunifanya niamue kuishi tena.Baada ya kukaa kwa muda pale Kigali nilipata wazo la kuondoka .Niliamua niende Marekani .Nilijua ile ndiyo sehemu salama kwa mimi kuishi tofauti na pale Rwanda ambako ni karibu sana na Tanzania.Vile vile tayari taarifa zangu zilikwisha fika kule na tayari nilianza kufahamika.Mtu pekee aliyenisaidia nikarejea tena Marekani ni Mike.Ninamshukuru sana kwa msaada wake mkubwa.Kwa sasa ninaishi na kufanya kazi Los Angeles na maisha yangu yanakwenda vizuri.” Akasema Happy
“So you are back together,you and Mike” akauliza Savanna
“I’m sorry to say this Savanna but yes ! we’re back together and deeply in love na tunategemea kufunga ndoa” akasema Happy huku akitabasamu kuona aibu kwa mbali
“Ouh ! Congraturations” akasema Savanna
“Thank you” akajibu Happy kisha kimya kifupi kikapita
“What a stupid woman..Yaani anadiriki kusema wazi wazi kwamba amerudiana na Mike na wanatarajia kufunga ndoa huku akisahau kwamba alimuacha Patrick akisota gerezani kwa kosa ambalo hakulitenda.” Akawaza Savanna.Happy akasema
“Savanna haikuwa rahisi kwangu kuamua kuja tena Tanzania.Niliapa kutokurudi tena Tanzania lakini kutokana na uzito wa suala lenyewe nimevunja kiapo changu ili na mimi niweze kutoa msaada wangu japo mdogo kwa Patrick ambaye alifanya jambo la kijasiri sana kuniokoa mimi nisikae gerezani kwa hiyo isingekuwa vyema kama ningekataa kuja kumtolea ushahidi .Nimekuita hapa ili unipe mwongozo wa kinachoendelea na ninachotakiwa kukisema mahakamani” akasema Happy
“Happy nimefurahi sana kusikia maendeleo yako na kukuona ukiwa ni mwenye furaha.Lakini kabla hatujaendelea na maongezi yetu aren’t you gonna ask?
“Ask what? Happy akashangaa
“How he’s doing”
“Savanna,Patrick ni mtu ambaye nilimpenda kwa moyo wangu wote.Sijawahi kupenda mtu kama nilivyompenda yeye.Amenifanyia mambo mengi ambayo hakuna mtu yeyote anaweza akanifanyia.Patrick made me a woman.Kuna mengi ambayo naweza kueleza kwa siku nzima kuhusu Patrick lakini naweza kusema kwamba maisha ni kitu cha ajabu sana.Pamoja na upendo wote na kila kitu alichonifanyia Patrick lakini hivi sasa I’m fighting to forget him.Its difficult but I thank God I’m doing fine without him.Ninaamini mimi na Patrick hatukupangwa tuwe pamoja.” Akasema Happy akanyamaza akameza mate na kuendelea
“Sijataka kumuulizia kwa sababu ninajua mimi ni mtu ambaye hataki kuniona tena katika maisha yake na ana hasira kubwa na mimi kwanza kwa kuziona picha zile na pili kwa kuondoka na kumuacha gerezani.Savanna moyo wangu unaniuma sana japokuwa hakuna anayeweza kulifahamu hilo.Bado kitendo kile cha kudhalilishwa kwa zile picha chafu hakijapona na kurudi kwangu tena Tanzania kumekitonesha kidonda change.Sina hakika kama ulimueleza Patrick ukweli halisi wa kilichotokea.Japo kwa ufupi unaweza ukanieleza anaendeleaje?
“Patrick is fine.He’s doing ok.Tuliibadili kesi na kuwa kesi ya kuua bila kukusudia na akapatiwa dhamana.Anaendelea vizuri na maisha yake mapya na kwa sasa ni meneja wa kiwanda cha kusindika nyama.” akasema Savanna
“Ouh that’s great.Is he married ? akauliza Happy huku akitabasamu.Savanna naye akatabasamu
“Not yet”
“Ouh Gosh ! what he’s waiting for? Is he still waiting for me?
“Tunasubiri mambo haya yamalizike ndipo tuanze taratibu za ndoa yetu” akasema Savanna huku akitabasamu
“We? are you two together? Akauliza Happy kwa mshangao.
“Yes ! we’re together now.We live together though not yet married” akasema Savanna
Happy akavuta pumzi ndefu na kumeza fundo la mate.Akapatwa na kigugumizi akakohoa kidogo na kusema
“Congraturations guys” akasema Happy na sura yake ilionyesha mabadiliko kidogo.
“Thank you “ akasema Savanna.Ni wazi maneno yale ya Savanna yalimchoma Happy.Savanna aliligundua hilo na hakutaka kuendeleza maongezi kuhusu mahusiano yake na Patrick na badala yake akaendelea kumweleza Happy kuhusiana na mwenendo wa kesi na namna atakavyotoa ushahidi wake.Baada ya maongezi marefu Savanna akaondoka zake.

* * * *

Ni alhamisi siku ambayo Happy alitakiwa kusimama kizimbani na kutoa ushahidi wake.Siku hii aliamka mapema sana asubuhi akaanza kujiandaa.Alikuwa mkimya na mwenye wasi wasi.Mpaka ilipotimu saa tatu za asubuhi tayari alikwisha jiandaa tayari kabisa kuelekea mahakamani .Familia nzima ilikuwa imejiandaa kuandamana naye mahakamani.
“Are you ready Happy? akauliza mzee Kibaho
“I’m ready dady though I’m a bit nervous” akajibu Happy
“Be strong .You can do it” akasema mzee Kibaho
“Yes Dady.I’ll be strong.I need to finish this”
“Tuko pamoja Happy usiogope” akasema Margreth kisha kwa pamoja wakaingia garini na safari ya kuelekea mahakamani ikaanza.
Mahakama ilifurika watu tofauti na siku za kawaida.Tetesi za Happy kuwepo mahakamani siku hii zilisambaa na kuwafanya watu wafurike mahakamani ili kumuona mrembo huyu ambaye aliviteka vyombo vya habari miezi zaidi ya kumi iliyopita kutokana na skendo zake mbali mbali na hasa ile ya mwisho ambapo picha na video zake za utupu vilisambaa katika magazeti na mitandao na kisha akatoweka ghafla bila kujulikana alielekea wapi.Wengi walikuwa na hamu ya kumuona tena.
Saa tano na dakika ishirini,Happy aliwasili mahakamani akiwa ameongozana na familia yake.Pale mahakamani alipokewa na Savanna na kuongozwa kuelekea ndani ya jengo la mahakama.Wengi hawakuweza kumtambua kwa haraka kutokana na namna alivyokuwa amebadilika.
“Nashukuru sana umekuja Happy.Naomba ondoa wasi wasi” akasema Savanna
“Usijali Savanna.I’ll do my best” akajibu Happy huku uso wake ukijilazimisha kutabasamu
Savanna aliingia ndani ya mahakama na Happy akaufungua mlango wa chumba kimoja mle mahakamani akaingia ndani na kumuomba Happy naye aingie.Mara tu alipoingia ndani ya chumba kile Happy akapatwa na mstuko mkubwa.Alitumbua macho kana kwamba ameona mzuka au kitu cha kushangaza.Alibaki amesimama huku akihisi mwili wake kuingiwa na baridi.Alikuwa anatazamana na Patrick ambaye naye alipatwa na mstuko .Chumba kikagubikwa na ukimya mzito.Savanna ambaye alisimama katikati yao akawaangalia wote na kisha akasema
“I’ll be outside.I’ll leave you guys alone so that you can great each other” akasema Savanna na kutoka mle chumbani.Patrick na Happy waliendelea kutazamana huku wote wakiwa bado wamesimama.Baada ya kama dakika mbili Patrick akakohoa kidogo na kusema
“Hallow …Ha..Happy”
“Hallo Patrick” akajibu Happy kwa sauti ndogo yenye kutetemeka.Kimya kidogo kikapita Patrick akasema
“Nimefurahi kukuona tena Happy”
“Hata mimi nimefurahi kukuona tena Patrick” akajibu Happy.Baada ya maneno hayo machache ukatanda ukimya mzito mle chumbani.Hakuna aliyemsemesha mwenzake.Patrick akaketi kitini na kuinama chini.Happy akamtazama kwa makini na kutaka kusema neno akafumbua midomo yake lakini sauti ikakwama.
“ouh my gosh ! Hiki ndicho nilichokuwa nakikwepa.Sikutaka kuonana tena na Patrick ana kwa ana.Kwa nini Savanna amenikutanisha naye wakati tulikubaliana kwamba sitaki kuonana na Patrick? Ouh gosh ! Nitafanya nini sasa? .akawaza Happy ,akaufunika uso wake kwa viganja vya mikono.Machozi yalikuwa yanamtoka
“God please help me.Niko katika wakati mgumu sana.Kumbu kumbu zote za nyuma zimerejea ghafla baada ya kumuona tena Patrick.I feel so guilty.I don’t know what to do anymore.” Akawaza Happy na mara mlango ukafunguliwa Savanna akaingia
“Are you guys ok? Akauliza Savanna
“Yes ! we’re ok” akajibu Happy.Macho yake yalionekana kujaa machozi.Savanna akamuuliza
“Are you ready Happy?
“Yes ! Yes !.I’m ready” akajibu Happy huku akifuta machozi
“Patrick ni muda sasa wa kuingia mahakamani.” Akasema Savanna Patrick akainuka na kuelekea katika chumba cha mahakama.
“Savanna kwa nini umefanya hivi? Kwa nini umenikutanisha na Patrick? Akauliza Happy
“Happy ni vigumu kukwepa kuonana na Patrick lakini hata hivyo tutaongea baadae lakini kwa sasa hebu tuelekeze mawazo yetu katika jambo lililotuleta hapa” akasema Savanna huku akikusanya mafaili yake
“Usiogope Happy.Ondoa hofu.You can do it” akasema Savanna na kisha akaongozana na Hapyy kuelekea katika chumba cha mahakama.Happy alikuwa anamulikwa na mianga ya kamera za waandishi wa habari waliofika kwa wingi mahakamani

* * * *

Saa nane za mchana Happy alimaliza kutoa ushahidi wake.Toka mashahidi wa upande wa utetezi walipoanza kutoa ushahidi wao haikuwahi kutokea siku ambayo Mahakama ilikumbwa na simanzi kama siku hii ya leo.Watu wote walikuwa kimya kabisa wakimsikiliza Happy
Happy ambaye alikuwa anaongea kwa hisia kubwa na wakati mwingine kulazimika kusimama na kufuta machozi,alianza kwa kuielezea mahakama historia fupi ya mahusiano yake na Patrick toka walipokutana shuleni,wakajenga mahusiano hadi walivyopotezana baada ya yeye kuondoka na kwenda masomoni Marekani.Aliielezea mahakama namna Veronika alivyotunga uongo na kuwatenganisha yeye na Patrick hadi walipokuja kuonana tena siku aliyoshinda taji la miss Tanzania.Aliendelea pia kuielezea mahakama juu ya maamuzi waliyoamua kuyachukua kwa pamoja yeye na Patrick ya kuachana na wapenzi wao na kuurejesha tena uhusiano wao kwani bado walikuwa wanapendana.Alikiri kumpenda Patrick zaidi ya anavyoweza kueleza na ndiyo maana alikuwa tayari kuachana na mpenzi wake Mike na kuurejesha uhusiano wa kimapenzi na Patrick.
Happy aliieleza makahama kilichotokea jioni ile na kusababisha kifo cha Vero.Sehemu hii ilikuwa ni sehemu ambayo iliwatoa machozi watu wengi akiwamo Patrick ambaye alishindwa kuyazuia machozi kumchuruzika mashavuni pale Happy alipotamka kwamba Vero aliteleza na kujigonga ukutani wakati akinyang’anyana silaha na Patrick ,silaha ambayo alitaka kuitumia kufanya mauaji
Baada ya kumaliza kutoa ushahidi wake na mahakama kuahirishwa,Happy alitoka huku ameinamisha kichwa.Bado machozi yaliendelea kumtoka.Familia yake ilikuwa pamoja naye wakiongozana kutoka nje ya jengo la mahakama.Waandishi wa habari na wapiga picha waliendelea kumfuata Happy na kumpiga picha nyingi.Ili kuwakwepa waandishi wa habari waliokuwa wakimsonga Happy,familia yake ikamuwahisha katika gari na kufunga milango kabla gari halijaondoka Happy akaomba wasubiri alitaka kuongea na Savanna.Margreth akampigia simu Savanna na kumfahamisha kwamba Happy anahitaji kuonana naye.Baada ya kama dakika tano Savanna akafika
“Thank you Happy.You did great” akasema Savanna.Happy akafuta machozi na kusema
“Nini kitaendelea baada ya hapa?
“Tayari tumefunga ushahidi kwa upande wetu.Nitakufahamisha baadae nini kitakachoendelea” akasema Savanna ,kisha wakaagana na kuondoka
Baada ya kuachana na akina Happy,Savanna naye akaingia garini na Patrick wakaondoka .Hawakutaka kupita sehemu yoyote na moja kwa moja wakaelekea nyumbani.Ndani ya gari ,Patrick alikuwa kimya sana
“Say something my love” akasema Savanna baada ya kuona kimya kimezidi mle garini
“I have nothing to say my love” akasema Patrick
“Still thinking about her?
“No ! She’s not in my thoughts anymore.Ninachowaza ni nini kinakwenda kutokea baada ya hapa”
“Usihofu Patrick.Niamini ninachokwambia kwamba mpaka hapa tumefanya vizuri sana na nina hakika tutashinda kesi hii.Ushahidi uliotolewa ni dhahiri unaendana na hoja tuliyoijenga ya kuitaka mahakama ikuache huru.” Akasema Savanna
“Nilihitaji sana kuonana na Happy ana kwa ana.Nina maswali mengi ambayo nataka anijibu lakini mara tu nilipomuona sikuweza tena kuwa na ujasiri wa kumuuliza chochote.” Akawaza Patrick
“Happy amebadilika sana.Uzuri wake umeongezeka maradufu.Inaonekana ameridhika na maisha anayoishi sasa.She’s already forgoten about me.Kweli dunia ina maajabu sana.Happy msichana ambaye nilimpenda kwa moyo wangu wote na tuliwekeana ahadi lukuki kwamba hatutaachana hadi kifo kitutenganishe lakini leo hii tumetazamana kama hatujuani,kama hatujawahi kuwa katika mahusiano.Nilipoteza kila kitu kwa ajili yake lakini pamoja na mambo yote aliyonitendea hakuthubutu hata kusema samahani kwa mambo aliyoyafanya.Inaonekana hajutii kabisa kitu alichokifanya.” Akawaza Patrick
“I was so stupid kuamua kuacha kila kitu kwa sababu yake nikiamini kwamba ndiye mwanamke ambaye ananifaa maishani.Nilikuwa na upofu wa fikra nikiamini kwamba hakuna mwanamke mwingine ambaye anafanana naye.Nilifanya kosa kubwa sana.Kwa sababu yake nimempoteza Vero mwanamke aliyenipenda kwa moyo wake wote,nimempoteza baba yangu,marafiki na nilipoteza hata dira na mwelekeo mzima wa maisha yangu na mwishowe na yeye mwenyewe akanikimbia na kuniacha nikiteseka gerezani.Anyway sitakiwi kuwaza sana kuhusu mambo haya.Yaliyopita yamepita na kinachotakiwa kwa sasa ni mimi kuelekeza nguvu na akili yangu katika kuyajenga maisha yangu na Savanna.Hata hivyo Happy amenifundisha kitu kimoja kikubwa.Amenisaida kumjua binadamu ni kiumbe wa namna gani.” akawaza Patrick halafu akageuza shingo yake na kumtazama Savanna ambaye naye aligeuza shingo yake wakatazamana na kutabasamu
“Why you are looking at me like that?
“Its nothing Savanna.” Akasema Patrick na kutabasamu halafu akaegemeza kichwa chake kitini.
“Namshukuru sana Mungu kwani pamoja na yote yaliyotokea lakini bado ameendelea kuwa upande wangu na ameniletea tena mwanamke mwingine ambaye ninaamini ndiye aliyeumbwa kwa ajili yangu.Savanna ananipenda kwa moyo wake wote .Amekuwa nami toka matatizo haya yalipotokea .Amenipigania kwa nguvu zake zote.Ananijali na kuniheshimu.Ni yeye ndiye aliyeokota vipande vya moyo wangu uliovunjwa vunjwa na Vero akaviunga na kunifanya nirejee tena katika maisha yangu ya kawaida.Yeye ni sababu ya mimi kuamua kupenda tena.Hakika huyu ndiye mwanamke ambaye nitampenda kwa moyo wangu wote na kwa siku zote za uhai wangu.Hata siku moja sintathubutu kumtoa chozi.Wanawake kama yeye ni nadra sana kuonekana zama hizi zilizojaa ulaghai.Najiona ni mtu mwenye bahati kubwa sana kuwa na Savanna na nitamuomba Mungu atujalie maisha mazuri na yenye furaha” akawaza Patrick halafu akamgeukia Savanna na kumtazama
“I love you Savanna.I love you so much.I just want you to know that you mean a lot to me” akasema Patrick na kumfanya Savanna atabasamu.akauchukua mkono wa kulia wa Patrick na kuubusu.
“I love you too Patrick more than words can say” akasema Savanna na safari ikaendelea

TUKUTANE SEHEMU IJAYO...
 
Mkuu shusha mbili za maana sina ela ya chai nazuga apa kwa ofisi naenda kunywa chai
 
Hii hadithi nmeshindwa kuelewe nilipo maliza epsod ya 10 ambapo veronica anarejea kutoka nje episode ya 11 sijaiona nakuja kukutana sehem nyingine kabisa kuwa patric amemuua veronoca sijaelewa mtunzi
 
Hii hadithi nmeshindwa kuelewe nilipo maliza epsod ya 10 ambapo veronica anarejea kutoka nje episode ya 11 sijaiona nakuja kukutana sehem nyingine kabisa kuwa patric amemuua veronoca sijaelewa mtunzi
Fatilia zipo zote
 
MISS TANZANIA
SEHEMU YA 56
MTUNZI😛ATRICK.CK
CONTACT:0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Wanawake kama yeye ni nadra sana kuonekana zama hizi zilizojaa ulaghai.Najiona ni mtu mwenye bahati kubwa sana kuwa na Savanna na nitamuomba Mungu atujalie maisha mazuri na yenye furaha” akawaza Patrick halafu akamgeukia Savanna na kumtazama
“I love you Savanna.I love you so much.I just want you to know that you mean a lot to me” akasema Patrick na kumfanya Savanna atabasamu.akauchukua mkono wa kulia wa Patrick na kuubusu.
“I love you too Patrick more than words can say” akasema Savanna na safari ikaendelea

ENDELEA…………………

“Happy jitahidi ule walau kidogo.Nyamaza kulia” Margreth alikuwa anambembeleza Happy ambaye toka wamerejea amekuwa akilia
“Margreth ninajuta ni kwa nini nimerudi Tanzania” akasema Happy huku akifuta machozi.
“Usiseme hivyo Happy.Umefanya jambo la maana sana kuja kutoa ushahidi wako kwa Patrick”
“Nilidhani nimekwisha msahau Patrick na hayupo tena moyoni mwangu lakini nilikuwa najidanganya”
“kwa nini unasema hivyo Happy?
“Margreh sikufichi mara tu nilipoonana na Patrick moyo wangu ulistuka .Nilihisi kama moyo wangu unataka kusimama.Nilikosa kitu cha kuongea,midomo ilikuwa inanitetemeka .Mwili wote ulikuwa wa baridi.Ouh gosh !!” akasema Happy
“Pale mahakamani nilikuwa natoa ushahidi wangu huku machozi yananitoka kutokana na uchungu niliokuwa nao moyoni baada ya kuonana tena na Patrick.Historia nzima ya maisha yangu ya nyuma ilirudi tena .Niliona aibu kubwa ,nilijisikua uchungu mkubwa na kuutambua ujinga nilioufanya wa kuamua kuondoka na kumuacha Patrick akiteseka gerezani” akasema Happy akainama na kukishika kichwa chake.Margreth akamtazama na kusema
“Sasa utafanya nini Happy?
“I don’t know what to do Margreth.Nahisi kuchanganyikiwa kabisa.Sijui nifanye nini” akasema Happy
“Kwa nini usifanye mpango wa kuonana na Patrick ili muongee na muyaweke sawa mambo haya? Nadhani mkikaa na kuyaongea mambo haya na mkaombana msamaha nyote mtabaki na amani.Nina hakika hata yeye mwenyewe ana hamu ya kuongea na wewe.Nadhani ni wakati muafaka sasa wa Patrick kufahamu kilichotokea.Hata wewe mwenyewe umekuwa mgumu sana kueleza kuhusu tukio lile na hata sisi ndugu zako mpaka leo hii hatufahamu nini kilitokea na ni akina nani waliokutenda kitendo kile.Naona ni wakati muafaka sasa wa kuliweka wazi jambo hili.Nina hakika hata Patrick angependa kusikia sababu iiliyokufanya ukaondoka ghafla na kumuacha peke yake gerezani.” Akasema Margreth
“Margreth kwa mara ya kwanza najilaumu sana kwa jambo nililolifanya.Nimetambua kosa langu.Nilipaswa kusimama imara na kueleza kilichotokea.Sikupaswa kuikimbia nchi.Sikupaswa kumuacha Patrick peke yake gerezani.Kwa hivi sasa nimechelewa sana na hakuna ambaye ataniamini hata nikisema ukweli.Natamani nipate walau dakika hata mbili za kuongea na Patrick na kumfahamisha juu ya kilichotokea na kumuomba anisamehe.lakini….” Happy akasita
“lakini nini Happy?
“Patrick has moved on.Tayari yuko katika mahusiano na Savanna na wana mipango ya kufunga ndoa mara tu baada ya kumalizika kwa kesi” akasema Happy
“Tell me you are jocking.!!!! Margreth akashangaa
“Si utani Maggie.Haya ni maneno toka katika kinywa cha Savanna mwenyewe”
“Gosh .! akasema Margreth
“Hiyo ndiyo hali halisi.Maisha yana maajabu sana” akasema Happy kwa huzuni
“I think there must be ana explanation to this.Hainiingii akilini kabisa.Ninachofahamu ni kwamba Parick anakupenda sana na yuko tayari hata kufanya jambo lolote kwa ajili yako.Mambo aliyoyafanya Patrick kwako ni makubwa sana na yananifanya nisiwe mwepesi kuamini kama ni kweli Patrick anaweza akahamisha penzi lake kwa Savanna katika kipindi kifupi namna hii”akasema Margreth.Happy akamtazama mdogo wake na kusema
“Margreth bado kuna mambo mengi ambayo hujayafahamu bado lakini kitu kimoja ambacho napenda ufahamu ni kwamba I’m no longer in Patrick’s heart”
“Kwa nini unasema hivyo Happy? Una hakika na unachokisema?
“Mbona umelin’ang’ania sana suala la kutaka kuonana na Patrick ? Akauliza Happy
“Naomba usinielewe vibaya Happy.Lengo langu si kutaka wewe na Patrick mrudiane kwani hilo ni jambo ambalo haliwezekani kwa sasa kwani kila mmoja tayari amekwisha anza maisha mapya.Ninachokitaka mimi ni wewe na Patrick mkutane muongee na mzimalize tofauti zenu ili muishi kwa amani.Kama hutafanikiwa kuonana na Patrick na ukamfahamisha kilichotokea ,nina hakika hautakuwa na amani kwa maisha yako yote yaliyobakia kwa sababu ni wewe ndiye uliyeondoka bila kumtaarifu chochote Patrick.Kama alifanikiwa kuziona picha zile na jinsi ulivyoondoka ghafla bila taarifa yoyote ni wazi Patrick ataelewa kwamba ulifanya kitendo kile .Suluhisho hapa ni wewe kuonana na Patrick mkaongea na ukamueleza kila kitu bila kumficha.I swear to god you’ll be free “
“Margreth sikatai ushauri wako kwani hata mimi ninahitaji sana kupata nafasi ya kuonana na Patrick lakini laiti ungeuona uso wa Patrick leo mara tu niliponana naye ungekubaliana na ninachokisema kwamba siko tena katika moyo na akili yake.He hates me.I deserve all that for what I did to him.It hurt so much” akasema Happy na kushindwa kuvumilia kutokwa na machozi
“Usilie Happy.Kama kweli una nia ya dhati ya kuonana na Patrick ili muongee na kuyaweka sawa mambo haya basi tunatakiwa tutafute njia.”
“Nahitaji sana kuonana na Patrick lakini sijui ni kwa namna gani nitafanikiwa kwa hilo” akasema Happy
“Happy I‘m your sister and a friend too so tell me the truth” akasema Margreth
“What truth?
“Do you still love Patrick?
“Baada ya kurejesha uhusiano wangu na Mike niliamini kwamba Patrick amekwisha toka moyoni mwangu lakini baada ya kuonana naye leo nimegundua kitu kimoja” Happy akasita na kutazama chini.
“Umegundua kitu gani Happy? Akauliza Margreth
“I was so wrong.Patrick ni mtu ambaye siwezi kumfuta kirahisi katika moyo wangu.To answer your question Yes I still love him.” Maneno yale yakamfanya Margerth akae kimya kwa muda akamuangalia dada yake.

* * * *

Ni saa nne za usiku,Linah rafiki mkubwa wa Loniki alikuwa amejilaza katika sofa kubwa lililokuwa sebuleni.Kama ilivyokuwa kwa watu wengine wenye ukaribu na familia ya Vero,Linah naye alikuwepo mahahakani kusikiliza ushahidi wa Happy.Baada ya kutoka mahakamani alirejea moja kwa moja nyumbani kwake.Toka amerudi alikuwa amejilaza katika sofa hili akitazama runinga huku katika meza ndogo iliyokuwa pembeni kulikuwa na chupa kubwa ya mvinyo
“Leo nilipomuona Happy mahakamani moyo wangu ulistuka sana.Niliumia mno hasa nikikumbuka kitendo tulichomfanyia.Kwa nini nilikubali kushirikiana na Loniki kumfanyia Happy mambo yale? Najilaumu sana kwa jambo lile.Happy hastahili hata kidogo kufanyiwa ukatili wa namna ile.” akawaza Linah halafu akachukua glasi yake ya mvinyo na kupiga funda kubwa
“Maelezo aliyoyatoa mahakamani yalinitoa machozi.Aliongea kwa uchungu sana na kwa hisia kubwa.Wote tuliokuwa hatufahamu historia yake na Patrick leo tumeufahamu ukweli.Sioni sababu ya kuwalaumu Patrick na Happy kwa sababu aliyeanzisha haya yote ni Vero pale alipodiriki kutunga uongo na kuwatenganisha.Uongo wake umekuja kumuumbua na badala yake akataka kufanya mauaji.Stupid girl” akawaza Linah na kuchukua glasi yake ya mvinyo akanywa
“Naungana na yule wakili anayeongoza jopo la mawakili wanaomtetea Patrick kuitaka mahakama imuachie huru Patrick.Hakuna kesi ya maana hapa.Nasikitika niliingia kichwa kichwa katika jambo hili kabla sijaufahamu ukweli halisi.Sitaki tena kushirikiana na Loniki” akawaza Linah lakini ghafla akastuka
“Mhh !! Inabidi nitumie akili nyingi ili kuanza kumkwepa Loniki na kumfanya asiendelee na mipango yake ya kulipiza kisasi.Mpaka sasa lengo lake bado halijabadilika. Bado anataka Patrick auawe.Amekuwa akinitumia fedha nyingi ili niweze kusuka mipango ya kumuua Patrick.,fedha ambazo nimekuwa nikigawana na Khumalo.Iwapo atagundua kwamba nilikuwa namdanganya na kwamba hakuna mpango wowote wa kumuua Patrick basi lazima kutazuka vita kubwa sana kati yangu naye.Ngoja kwanza nimpigie simu nimpe taarifa za kilichotokea leo mahakamani” akawaza Linah na kuinuka akachukua simu yake akampigia Loniki.
“hallow Loniki,habari za London?
“London kwenda,habari za huko nyumbani?
“Huku nako ni kwema kabisa” akasema Linah na kuvuta pumzi.Sauti ya Loniki ilionyesha ni kama mtu ambaye hakuwa na furaha kama ilivyozoeleka
“Mama kanipigia simu na kuniambia kwamba Happy alikuwepo mahakamani leo na ametoa ushahidi wake” akasema Loniki
“Ndiyo Lonny,Happy ametokea mahakamani leo na ametoa ushahidi wake “ akajibu Linah
“Vipi kuhusu mwenendo mzima wa kesi? Akauliza Loniki
“Lonny pamoja na jitihada zote tulizozifanya,naomba niwe wazi kwako kwamba kutokana na ushahidi uliotolea mahakamani na upande wa utetezi na hasa huu ambao umetolewa leo na Happy,tuna kazi ngumu ya kufanya kuhakikisha kwamba Patrick anafungwa.Niliongea na mwanasheria mmoja wa serikali na akaniweka wazi kwamba ushahidi uliotolewa mahakamani ni mzito sana na unatosha kabisa kuishawishi mahakama kumuachia huru Patrick”
“Damn it !!..That wont happen..!! akaongea Loniki kwa ukali
“Linah nilikuachia kazi hii na ukanihakikishia kwamba utafanya kila uwezalo na kuhakikisha kwamba Patrick anauawa au anafungwa gerezani .Nimekuwa nakutumia fedha nyingi kwa ajili ya kufanikisha hayo sasa iweje leo unipe kauli yenye utata namna hiyo? Unataka kunihakikishia kwamba juhudi zote tulizofanya na mamilioni yote ambayo nimekuwa nakutumia wewe na Khumalo nimetwanga maji kwenye kinu? Akauliza Loniki
“Loniki wewe ni zaidi ya rafiki kwa hiyo naomba uniamini kile ninachokwambia.Ni kweli mipango ilifanyika na kama nilivyokueleza .Nimekwisha hakikishiwa na watu wazito mahakamani kwamba Patrick lazima afungwe hata kama kutatolewa ushahidi wa aina gani.Kwa hiyo usiwe na wasi wasi Loniki” Linah akamdanganya Loniki
“Sawa Linah.Naomba iwe hivyo lakini endapo itatokea vinginevyo sijui itakuaje kwa sababu tumepoteza fedha nyingi sana mpaka sasa na hakuna matunda yoyote.Lengo langu mimi lilikuwa kuwaua Patrick na Happy lakini ni wewe Na Khumalo ndio mliopinga jambo hilo kwa hiyo basi hakikisheni kwamba kwa vyovyote itakavyokuwa kama haitawezekana kumuua basi lazima Patrick afungwe gerezani.Endapo mtashindwa kulitekeleza hilo basi nitarudi mimi mwenyewe na safari hii sintakuwa na namna nyingine zaidi ya kutafuta watu wengine na kuwaua Patrick na Happy.Inaniuma sana kuwaona washenzi hawa wakiendelea kuvuta hewa hii safi wakati mdogo wangu waliyemkatili uhai wake anaoza kaburini.” Akasema Loniki kwa ukali
“Loniki naomba unisiklize vizuri.Suala hili si jepesi kama unavyolifikiri.Tulilipinga wazo lako la kutaka Patrick na Happy wauawe kutokana na athari ambazo zingeweza kujitokeza.Lakini kwa kuwa lengo lako lilikuwa ni kulipa kisasi ndiyo maana tukapendekeza kwamba badala ya kufanya mauaji basi tuyafanye maisha yako yawe magumu na Patrick afungwe kigerezani.Hicho ndicho nimekuwa na kifanya na Khumalo muda huu wote..” akasema Linah ambaye alikuwa ameukunja uso wake kwa hasira. Na mara simu ikakatwa
“Amekata simu Sitaki tena kujihusisha na mipango ya Loniki.Sitaki kutafuta mgogoro na vyombo vya dola kwa sababu ya hivi vimilioni alivyokuwa ananitumia.Ninayamudu maisha yangu mwenyewe.Biashara zangu zinaniingizia fedha nyingi na kunifanya niishi kama binti mfalme.Patrick na Happy hawana kosa lolote la kustahili kutendewa hivyo anavyotaka..Najua atakuwa amekasirika lakini simuogopi hata kidogo.Tena ngoja nimpigie simu Khumalo nimueleze kuhusiana na ujinga wa Lonny” akawaza Linah

* * * *

Saa nne za usiku Happy bado alikuwa amekaa kitandani.Alikuwa ameegemea kitanda macho yake yamemvimba
“Happy tafadhali usiendelee kulia.Toka umerudi umekuwa unalia.Tafadhali usilie tena.Inatosha sasa” akasema Margreh aliyekuwa pembeni ya dada yake
“let me cry Margreth.Nina uchungu mwingi sana na sijui nifanya nini.I’m confused” akasema Happy.Margreth akamtazama dada yake usoni akainuka na kuiendea meza ndogo akachukua simu
“Mpigie savanna sasa hivi na umwambie kwamba unahitaji kuonana na Patrick” akasema Margreth.Happy akamtazama na kusema
“Are you sure you want me to do this? Akauliza Happy
“Happy kama kweli una nia ya dhati ya kutaka akili yako itulie na maisha yako yawe na amani tafadhali ongea na Patrick”
“Nitamwambia kitu gani? Ninaogopa Margreth”
“Ukweli.Mweleze ukweli” akajibu Margreth na kuzitafuta namba za Savanna akapiga
“Hallow” akasema Savanna baada ya kupokea simu
“Hallow Margreth…!! Akasema tena Savanna.Happy akakohoa kidogo na kusema
“Savanna its me Happy”
“Ouh Happy.How are you my dear? Akasema Savanna
“I’m ok Savanna”
“Nafurahi kusikia kwamba unaendelea vizuri”
“Yah !..” akasema Happy
“Happy napenda nikushukuru sana kwa kitendo ulichokifanya leo.You did it so well” akasema Savanna
“Yah ! akajibu Happy na kumfanya Savanna astuke kidogo
“Happy are you ok? Akauliza Savanna.Happy hakujibu kitu
“Happy is there anything wrong? Akauliza tena Savanna
“Savanna I’m sorry to disturb you at this time” akasema Happy
“Usijali Happy.Hujanisumbua chochote.Muda wowote unaruhusiwa kunipigia simu.Una tatizo lolote Happy? Akauliza Savanna.Happy akasita kidogo kisha akasema
“Savanna unaweza kuniruhusu niongee na Patrick japo kwa dakika mbili? Akasema Happy.Savanna akasita kidogo na kusema
“Hakuna tatizo Happy.Patrick huyu hapa ongea naye” akasema Savanna na kumpatia Patrick simu
“Happy anahitaji kuongea nawe” akasema Savanna.Patrick akamtazama usoni
“Ongea naye”akasisitiza Savanna.Patrick akaiweka simu sikioni
“Hallow” akasema
“Hallow Patrick “ akajibu Happy
“Are you ok ? akauliza Happy
“I’m ok” akajibu Patrick kwa ufupi
“Savanna ameniambia kwamba unataka kuongea na mimi” akasema Patrick
“Ndiyo Patrick.Kwanza samahani sana kwa kukusumbua”
“Bila samahani Happy”
“Patrick sina hakika kama utakuwa tayari lakini nahitaji kukuona.Nina maongezi nawe ya maana sana”
“Maongezi na mimi?! Patrick akashangaa
“Ndiyo Patrick.Nina maongezi nawe kidogo”
“Unataka tuongee kuhusu nini Happy?
“Patrick kuna mambo ambayo nahitaji kukueleza.Kuna mambo ya maana sana ambayo unahitaji kuyafahamu”
“mambo hayo huwezi kunieleza simuni sasa hivi?
“hapana Patrick.hatuwezi kuongea simuni.Nahitaji sana kuonana nawe ana kwa ana” akasema Happy
“Sawa Happy niko tayari kuonana nawe ili unieleze hicho unachotaka kunieleza lakini nina sharti moja tu kwamba lazima na Savanna kipenzi cha roho yangu awepo.Yeye anastahili kufahamu kila kinachoendelea katika maisha yangu.Uko tayari kwa hilo? Akauliza Patrick lakini ghafla simu ikakatika ‘
“Amekata simu” akasema Patrick
“Mpigie pengine ni tatizo la kimawasiliano” akasema Savanna
“Hakuna sababu ya kumpigia.Isitoshe sina mpango na sihitaji kuonana naye sasa na katika maisha yangu yote yaliyobaki.Biashara ya mimi na yeye ilikwisha pale alipoamua kuondoka na kunitelekeza gerezani” akasema Patrick
“Pengine ana jambo la maana anataka kukwambia” akasema Savanna
“Hana tena jambo lolote la maana ambalo anaweza akanieleza.Ninachoshukuru ni yeye kukubali kuja kunitolea ushahidi na baada ya hapo mimi naye hatuna tena mahusiano.Mahusiano yangu naye yaliisha alipoondoka na kunitelekeza gerezani” akasema Patrick. Savanna akamuangalia na kuuliza
“Why are you avoiding her?
Patrick akamvuta Savanna karibu yake akambusu .
“It’s because I have you now.Sihitaji kuiumiza akili yangu kwa mambo yaliyokwisha pita.Ninachokiangalia hivi sasa ni maisha yangu na mbele nikiwa nawe malaika wangu.Nakupenda sana Savanna zaidi ya ninavyoweza kueleza” akasema Patrick na kumbusu tena Savanna mdomoni
Suala la Patrick kuweka sharti la kuongozana na Savanna lilimuumiza sana moyo Happy na kumfanya akate simu na kuitupa kitandani
“Damn you Patrick..How could you do that to me? Happy akahamaki
“Patrick kasemaje? Akauliza Margreth
“Amesema hawezi kuonana nami hadi aongozane na mpenzi wake Savanna.Margreth I’ve lost him..I’ve lost Patrick.” akasema Happy kwa uchungu
“Usiseme hivyo Happy.Kama kweli bado unampenda kwa dhati,tafuta namna utakayoweza kumtafuta mkakaa na kuliongea jambo hili.” Margreth akajaribu kumpa moyo dada yake
“No way Margreth.Nimeshampoteza Patrick.Tayari yuko katika mahusiano mengine na amekwisha nisahau.Sitaki tena kuingilia mahusiano yake kwani nimekwisha jifunza wakati ule wa Vero.Ni kosa langu na ninastahili kuteseka kwa maisha yangu yote.Sikupaswa kukimbia na kumuacha Patrick peke yake gerezani.Kitendo kile kimemfanya Patrick anichukie sana na hata nilipomtazama machoni niliona wazi kwamba ananichukia mno” akasema Happy
“Sasa utafanya nini Happy?
“Sina cha kufanya tena.Its my mistakes and I cant blame anybody”
“will you be ok?
“No ! I’ll never be ok in my life but I’m going to try living my life without him .Margreth my life will never be the same again.Patrick ndiye alikuwa ni kila kitu kwangu”
Margreth akamtazama dada yake kwa huruma na kusema
“Laiti ningekuwa na njia yoyote ya kuweza kufanya ili kuurejesha tena uhusiano wako na Patrick ningefanya hivyo lakini nasikitika sina namna yoyote ninayoweza kufanya kwa sasa.May be the best thing is to let him go for good” akasema Margreth
“May be that’s the best way for now. Its obvious me and Patric we’re finished.Patrick atabaki kuwa sehemu ya kumbu kumbu yangu .Pamoja na hayo sintaondoka Tanzania hadi hukumu yake itakapotolewa.Nataka niwepo siku hiyo ya hukumu.” Akasema Happy

TUKUTANE SEHEMU IJAYO.....

NAWATAKIA NYOTE PASAKA NJEMA ...
 
MISS TANZANIA
SEHEMU YA 57
MTUNZI😛ATRICK.CK
CONTACT:0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Laiti ningekuwa na njia yoyote ya kuweza kufanya ili kuurejesha tena uhusiano wako na Patrick ningefanya hivyo lakini nasikitika sina namna yoyote ninayoweza kufanya kwa sasa.May be the best thing is to let him go for good” akasema Margreth
“May be that’s the best way for now. Its obvious me and Patric we’re finished.Patrick atabaki kuwa sehemu ya kumbu kumbu yangu .Pamoja na hayo sintaondoka Tanzania hadi hukumu yake itakapotolewa.Nataka niwepo siku hiyo ya hukumu.” Akasema Happy

ENDELEA…………….

Abiria waliokuwa katika ndege ya shirika la ndege la British airways walianza kutoka nje ya uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere.Miongoni mwao alikuwamo Loniki akitokea jijini London Uingereza anakoishi.Linah rafiki yake mkubwa alikuwepo uwanjani kumpokea.
“Karibu tena nyumbani Lonny” akasema Linah huku akikumbatiana na Loniki
“Ahsante sana Linah.Wow ! Unazidi kunawiri” akasema Loniki na wote wakacheka kisha wakaondoka pale uwanjani.
“Mambo yanakwendaje Linah? Akauliza Loniki wakiwa garini
“Mambo ni kama vile nilivyokwambia Lonny.Tunasubiri siku ya hukumu”
“Vizuri sana.Mambo yote umeyaweka sawa?
“Kwa mujibu wa mtu ambaye yuko ndani ya mahakama ambaye ndiye tunamtumia kurekebisha mambo ametuhakikihsia kwamba kila kitu kimewekwa sawa na kwamba Patrick lazima atafungwa.”
“Nafurahi kusikia hivyo.Khumalo ana taarifa kwamba ninakuja na tunakwenda kuonana naye usiku huu?
“Ndiyo.Nilimtaarifu mapema na amenielekeza mahala ambako tutamkuta”
“Ok thats good” akasema Lonny na safari ikaendelea
Ni siku tatu zimebaki kabla ya hukumu ya Patrick kutolewa.Hii ndiyo iliyomsukuma Loniki na kumlazimu aje mara moja ili kufanikisha mipango yake ya kuhakikisha kwamba Patrick anafungwa gerezani baada ya mipango ya kumuua kuonekana kugonga mwamba.
“Lonny ..!! akaita Linah.Loniki akageuka na kumtazama
“Itakuaje iwapo itatokea mahakama ikamuachia huru Patrick?
Loniki akatabasamu kidogo na kusema
“I will kill him myself.Hicho ndicho kitu ambacho kimenirejesha nyumbani.Kama mahakama itamuachia huru Patrick lazima afe.Sintakubali kumuona akiendelea kuishi kwa furaha wakati mdogo wangu ameoza kaburini.Lazima naye afe na ndiyo maana usiku huu nataka nikamtaarifu Khumalo ili alifahamu hilo.Kwa nini umeuliza?
“Never mind its nothing” akajibu Linah na safari ikaendelea kimya kimya hadi walipofika katika klabu moja ya usiku ambako ndiko Khumalo alikokuwa anastarehe.Waliingia pale klabuni na kuelekea moja kwa moja sehemu alipo Khumalo.Alikuwa amezungukwa na mabinti watatu wazuri waliovaa nusu utupu.Mara tu alipowaona Linah na Loniki akawaondoa wale mabinti na kuwakaribisha
“Pole na safari Lonny” akasema Khumalo
‘Nashukuru nimefika salama.Habari za huku?
“Habari za huku nzuri .maisha yanaendelea kama unavyoona” akasema Khumalo na kucheka kidogo halafu akatoa pakiti la sigara akatoa moja na kumrushia Lonny naye akatoa sigara moja akawasha na kuendela kuvuta
“Maisha ni mazuri na matamu.Sina sababu yoyote ya kulalamika” akasema Khumalo
“yah ! Hata mimi naona” akajibu Lonny huku akipuliza moshi mwingi hewani
“Linah alinitaarifu kwamba utafika jioni ya leo na kwamba ulihitaji kuonana nami.Nilistuka kidogo nikajua lazima una suala zito ambalo huwezi kulala bila kuniona”
“Ndiyo Khumalo.Nadhani unafahamu kilichonirejesha nyumbani”
“Nafahamu Loniki na hukuwa na sababu ya kuacha kupumzika na kuja kuniona.”
“Nisingeweza kupata usingizi bila kukuona.Kama unavyofahamu hukumu ni jumanne ijayo.Nataka Kujua mipango inaendaje.Mmejiandaa vipi?
“Kujiandaa kwa nini Lonny? Ninavyofahamu mimi ni kwamba tuliufuta mpango wa kumuua Patrick na tumekuwa tukifanya kila linalowezekana ili Patrick ahukumiwe kifungo kirefu gerezani.Hayo si ndiyo yalikuwa makubaliano yetu?
“Ndiyo Khumalo lakini kuna mambo mawili ambayo yanaweza yakatokea hapa.Patrick anaweza akafungwa au akachiwa huru.Endapo ikitokea akahukumiwa kifungo gerezani basi biashara na wewe itakuwa imekwisha lakini ikitokea kwamba ataachiwa huru na mahakama basi kazi bado itaendelea.Lazima Patrick auawe.Siko tayari kumuona Patrick akiendelea kutamba mtaani wakati alimuua mdogo wangu kwa makusudi kabisa” Loniki aliongea pasi na masihara
“Hilo ni suala ambalo halina tatizo.Kama ataachiwa huru na mahakama basi tutatekeleza huo mpango wako wa kumuua.Lakini naomba utambue kwamba kama ukitaka Patrick auawe itatulazimu tuongee biashara mpya”
Loniki akastuka sana baada ya kauli ile ya Khumalo
“Fedha !!...” akauliza Khumalo kwa mshangao.
“Ndiyo Lonny.Unatakiwa kuongeza fedha kwani itakuwa ni kazi nyingine.”
“You are kidding Khumalo.Nimekuwa nawatumia mamilioni ya fedha kwa ajili ya kazi hii.Mnataka tena niongeze fedha nyingine?
“Loniki pesa ulizokuwa unatuma zote tumezitumia katika kusuka mipango ili Patrick aweze kufungwa.Na kama unavyofahamu hii ni kama bahati nasibu.Mnaweza mkatumia fedha na mkashindwa vile vile kwa hiyo endapo itatokea Patrick ataachiwa huru na ukataka auawe basi itakulazimu kuongeza fedha.Kitu kingine naomba ufahamu kwamba mimi huwa sipendi kuzungumzia mambo ya biashara au kazi katika sehemu za sterehe.Nimewaheshimu sana na ndiyo maana nimekubali kuonana nanyi kati kati ya starehe zangu.Kwa hiyo sitaki tuendele kubishana.Naomba jibu moja kama utaongeza fedha au utatafuta mtu mwingine wa kukufanyia kazi yako? Akasema Khumalo.Loniki akaingiwa na woga kwa namna Khumalo alivyokuwa amebadilika
“Manataka niongeze shilingi ngapi? Akauliza Loniki huku ameukunja uso wake
“millioni arobaini” akajibu Khumalo.Lonny akasimama na kushika kiuno chake akamtazama Khumalo kwa jicho la kali.
“Milioni arobaini?
“Ndiyo.Si fedha nyingi kwa kazi kama hiyo unayoitaka ya kutoa uhai wa mtu.Kama utaona ni nyingi naomba utafute mtu mwingine.”
Loniki akainama akafikiri na kusema
“Nitaangalia namna ya kufanya.Tusubiri kwanza hukumu itolewe” akasema Loniki akiwa na hasira akamshika mkono Linah wakaondoka na kuelekea nyumbani kwa akina Loniki wakaagana na Linah akaanza safari ya kurejea kwake.
“Loniki ni mtu mwenye roho mbaya sana.Bado nia yake ya kumuua Patrick iko pale pale.Hapana siko tayari kumuacha afanikishe mipango yake hiyo.I have to do something to stop her.Ninachotakiwa kukifanya kwa sasa ni kuonana na Sarah.Kwa pamoja tunaweza kumzuia asifanye mpango wowote wa mauaji.Mimi peke yangu siwezi kumshauri aachane na mipango hiyo kwa sababu nimeshiriki kuanzia mwanzo na tayari nimekwisha tumia fedha zake nyingi nikimdanganya kwamba kuna mipango ninaisuka ili Patrick afungwe gerezani.Najua Sarah atataka kuufahamu ukweli wote lakini sina namna nyingine itabidi nimueleze kila kitu kuhusiana na uchafu wa Loniki” Akawaza Linah akapunguza mwendo wa gari na kuchukua simu yake akazitafuta namba za simu za Sarah na kumpigia.
“Hallow Sarah” akasema Linah baada ya Saraha kupokea simu
“Hallow Linah,habari yako? Nimestuka sana baada ya kuiona simu yako mida hii.Si kawaida yako kunipigia simu hasa kwa nyakati kama hizi’ akasema Sarah
“Samahani Sarah kwa kukusumbua.Ni kweli sijawahi kukupigia simu kwa muda kama huu lakini imenilazimu kufanya hivyo leo.Saraha nina shida na wewe ya muhimu sana.Nahitaji kuonana nawe usiku huu kuna jambo la muhimu mno nataka tuongee”
“Linah mbona unanipa wasi wasi? Kuna tatizo gani? akauliza Sarah kwa wasi wasi.
“Usihofu Sarah ni mambo ya kawaida tu ya kuelekezana.Uko wapi sasa hivi?
“Niko nyumbani kwangu.Wewe uko wapi?
“Niko barabarani,nimetoka kumpeleka Loniki nyumbani”
“Loniki !!!...Sarah akashangaa.
“Ndiyo .Ina maana huna taarifa kwamba Loniki anakuja leo?
“Hapana Linah.Sina taarifa yoyote ile kuhusu Lonny.Unajua mimi na dada yangu hatuna maelewano mazuri toka ulipotokea msiba wa Vero kwa hiyo mawasiliano kati yetu si mazuri”
“Yah ! nalifahamu hilo Sarah.Kwa hiyo tunaweza kuonana usiku huu?
“Unaweza ukaja nyumbani kwangu? Unajua siwezi kutoka usiku huu kwani mume wangu amerejea usiku huu kwa hiyo siwezi kuondoka na kumuacha peke yake”
“Nmekuelewa Sarah.Ninakuja hapo hapo nyumbani kwako.” Akajibu Linah na kukata simu
Ilimchukua zaidi ya dakika arobaini kufika nyumbani kwa Sarah.Akafunguliwa geti na kuingia ndani.
“Karibu sana Linah.” Akasema Sarah
“Ahsante sana Sarah.Ni muda mrefu hatujaonana”
“Kweli Linah.karibu sana”
“Nashukuru sana Sarah.Lakini nisingependa kukupotezea muda zaidi .Tunaweza tukaongea hapa nje?
“Hapana Linah.Twende tukaongelee ndani“ Sarah akamuongoza Linah hadi katika chumba cha maongezi
“Linah umenistua sana leo.Kuna tatizo gani? akauliza Sarah akiwa na shauku ya kutaka kufahamu kilichomleta Linah nyumbani kwake usiku ule
“Usiogope sarah.Nimelazimika kuja usiku huu kutokana na unyeti wa jambo lenyewe.Sarah kilichonileta hapa ni kuhusiana na Loniki”
“Loniki kafanya nini tena?! Saraha akashangaa
“Ni hadithi ndefu kidogo lakini nitajaribu kukuelezea kwa ufupi.Ni kwamba kwa muda mrefu sasa Loniki amekuwa katika mikakati ya kuhakikisha analipiza kisasi kwa wale waliosababisha kifo cha Vero,hapa anawalenga Patrick na Happy”
“Yah ! Nilijua toka mwanzo kwamba Lonny alikuwa na mpango wa kulipiza kisasi kwani aliwahi kunitamkia hata mimi kwamba ni lazima atalipiza kisasi kwa watu waliosababisha kifo cha Vero na hilo ndilo jambo ambalo limekuwa likituweka mbali mbali mimi nay eye kwani sioni mantiki ya kulipiza kisasi wakati tayari shauri hili liko katika vyombo vya maamuzi” akasema Sarah
“Kama aliwahi kukutamkia hivyo basi hakuwa anatania.Alimaanisha alichokuwa anakisema.Alinishirikisha mimi pia katika mipango yake kwa kuniomba nimsaidie kutafuta mtu au watu ambao watamsaidia kuifanya kazi hiyo.Nilimsaidia kumpata mtu mmoja ambaye alikuwa tayari kuifanya kazi hiyo.Niliwakutanisha wakaongea na kuelewana namna watakavyotekeleza mpango huo wa kulipa kisasi.Loniki alitaka Patrick na Happy wauawe.Khumalo alilipinga wazo hilo la kuwaua Patrick na Happy kwa haraka kama alivyokuwa anataka Lonny badala yake akashauri kwamba kwa kuwa wakati ule Patrick alikuwa gerezani basi nguvu ielekezwe kwa Happy lengo hapa likiwa ni kumfanyia udhalilishaji mkubwa ambao utapelekea uhusiano wake na Patrick kuvunjika.Khumalo na genge lake walifanikiwa kumteka Happy na kumpeleka mafichoni na huko alifanyiwa udhalilishaji mkubwa sana.Alifanyishwa ngono na vijana wawili huku akirekodiwa na kupigwa picha .Aliamriwa kufanya vile kwa kisingizio kwamba endapo angekataa basi Patrick angeuawa na kwa kuwa Happy anampenda sana Patrick alikubali kufanya vile ili kumuokoa Patrick” akasema Linah na kumtazama Sarah usoni ambaye alionyesha mstuko mkubwa
“My Gosh ! kumbe Lonny ndiye aliyemfanyia Happy kitendo kile?? Akauliza Sarah
“Ndiyo.Happy alifanyiwa udhalilishaji ule huku Loniki akishuhudia.Sarah kwa kweli lile lilikuwa ni tukio baya sana ambalo halitaweza kufutika moyoni mwangu.Ninalijutia sana kosa lile kwani hata mimi nilishiriki” akasema Linah kwa masikitiko halafu akaendelea
“Kilichofuata baada ya hapo ni kama tulivyoona katika magazeti na mitandao.” Linah akanyamaza,akamtazama Sarah na kuendelea
“Katika kipindi hiki ambacho amekuwa Uingereza bado ameendelea na mipango yake ya kuhakikisha kwamba Patrick anafungwa gerezani tena kifungo kirefu.Amekuja leo hii ili kufanikisha kile ambacho amekwisha kianza muda mrefu .Kikubwa zaidi kilichonifanya nikutafute usiku huu ni kwamba amedhamiria kumuua Patrick endapo mahakama itamuachia huru” akasema Linah.Sarah akasimama kwa hasira
“Why are you telling me all this now? Akauliza Sarah
“Because we have to stop her !! akasema Linah naye akasimama
“No Linah ! go away.Wewe na Happy lenu moja.Nyote mmeshiriki katika njama hizi.Linah how could you do that? How could you hurt Parick like that? .akauliza Sarah kwa uchungu
“Sarah please forgive me. Sikuwa nikiufahamu ukweli wa mambo na ndiyo maana nilikubali kushirikiana na Loniki.Kwa sasa baada ya kuufahamu ukweli ninajutia na tafadhali Sarah naomba tushirikiane sote tumuokoe Patrick “
“Go away Linah ! You and Lonny are both killers and tomorrow morning I’m going to report you ” akasema Sarah ambaye alikuwa amepandwa na hasira
“Tafadhali usifanye hivyo Sarah.Tunatakiwa tutafute namna ya kufanya ili kumzuia Lonny asitekeleze mipango yake bila kuwashirikisha polisi.Ukitoa taarifa hizi polisi Loniki anaweza akaenda gerezani.” Akasema Linah
Sarah akainama akafikiri kwa sekunde kadhaa halafu akainua kichwa akamuangalia Linah kwa macho makali.
“Bado siamini kama na wewe umekubali kuungana na Loniki.Nilikuheshimu sana kama dada yangu lakini kwa jambo hili ulilolifanya umenifanya nikutazame upya” akasema Sarah
“C’mon Sarah.Huu si wakati wa kuanzisha malumbano.Tunatakiwa kushirikiana katik…………….” Kabla hajamaliza sentensi yake Sarah akamzuia
“Hakuna njia nyingine zaidi ya kulifikisha suala hili katika vyombo vya dola.Wewe na rafiki yako mtakwenda kujieleza mbele ya vyombo vya sheria.” Akasema Sarah kwa ukali.Linah akamsogelea na kumshika bega
“Nisikilize vizuri Sarah.Najua wewe na Loniki hamna maelewano mazuri lakini yule ni dada yako,ni ndugu yako wa damu.Ukilifikisha suala hili polisi Loniki atakamatwa na anaweza akafungwa gerezani.So tell me are you sure you want to send your sister to jail?
Sarah akainama halafu akainua kichwa akamtazama Linah na kusema
“Unataka tufanye nini?
“Kwa sasa bado najaribu kuangalia namna tutakavyoweza kumzuia Lonny asitekeleze mpango wake.Leo nimeona nikufahamishe kinachoendelea.Nitakupugia simu kesho kukufahamisha mipango yake inavyoendelea na kwa pamoja tutaona namna ya kuweza kumzuia.Sitaki afahamu kama nina mawasiliano nawe kwa hiyo usinipigie simu mimi ndiye nitakayekupigia.Naomba vile vile unihakikishie kitu kimoja”
“kitu gani hicho Linah?
“Naomba haya tuliyoyaongea hapa yabaki kati yetu”
Sarah akamtazama Linah na kusema
“Sintamwambia mtu yeyote lakini naomba utafute haraka mpango wa kumzuia Loniki asiweze kutekeleza mpango huo wa kumuua Patrick” akasema Sarah
“Usihofu Sarah.Nitakufahamisha kila kitu namna tutakavyofanya” akasema Linah halafu akaagana na Sarah akaondoa zake.
“Kazi ya kwanza nimeimaliza.Japokuwa haikuwa rahisi lakini nashukuru Sarah amenielewa.Kinachofuata sasa ni kuongea na Khumalo.” Akawaza Linah akiwa garini akapunguza mwendo wa gari na kuliegesha pembeni ya bara bara akachukua simu yake na kumpigia Khumalo.
“hallo Linah´ akasema Khumalo
“Khumalo bado uko klabuni?
“Ndiyo Linah bado niko hapa klabuni na warembo wangu.Unasemaje?
“Ni kuhusu Lonny”
“Lonny kafanya nini tena? Si tumekwisha malizana naye?
“Nafahamu hilo Khumalo lakini kuna jambo ambalo nataka tulijadii.” Akasema Linah na kuliwasha gari akaliingiza barabarani.
“jambo gani hilo Linah?
“Ni kuhusu huu mpango wake wa kumuua Patrick”
“Kuna tatizo gani katika hilo?
“Are you real gonna do it? Akauliza Linah
“Do what ? khumalo naye akauliza
“Kill Patrick” akasema LInah.Khumalo akacheka kidogo na kusema
“Kwa nini unauliza hivyo Linah wakati unafahamu kabisa kwamba hakuna mpango wowote wa kumuua Patrick? Mimi na wewe tulikwishakubaliana kwamba tutakula fedha za Loniki lakini hatutakeleza mpango wake wowote.Tulichomfanyia Happy kinatosha sana.Siwezi kuendelea kuumiza tena watu wasio na hatia”
“Nimekeuelewa Khumalo lakini nina wazo moja”
“Wazo gani Linah?
“Ninaomba uondoke hapa Dar na usirudi hadi hapo nitakapokutaarifu.”
“Hata hivyo huo ndio ulikuwa mpango wangu.Kesho nilipanga niende Zanzibar kula raha na mpenzi wangu Sakina.Nasubiri milioni arobaini za mwisho toka kwa Lonny”
“Hilo ni jambo zuri sana Khumalo na nina imani endapo ikitokea mahakama ikamuachia huru Patrick Lonny atakutafuta na akikukosa basi hatakuwa na la kufanya tena zaidi ya kuahirisha mpango wake”
“usihofu Linah.Endapo kutakuwa na tatizo lolote na utahitaji msaada wangu utanitafuta na nitawatuma vijana wangu wakusaidie”
“Ahsante sana Khumalo” akasema Linah akaagana na Khumalo na kukata simu
“Sasa mambo yamekaa sawa.Nadhani huu ndio mwisho wa urafiki wangu na Loniki.Ni heri kuishi bila kuwa na rafiki kuliko kuishi na rafiki kama Lonny.” Akawaza Linah huku akielekea nyumbani kwake


* * * *

Siku mpya imeanza.Saa tatu za asubuhi ilimkuta Loniki mbele ya kaburi la Veronika. Kwa muda wa dakika kadhaa alikuwa amesimama akiliangalia kaburi hili huku michirizi ya machozi ikionekana mashavuni
“Vero mdogo wangu nilikuahidi kwamba lazima nikulipizie kisasi kwa wale wote waliokukatili na kusababisha kifo chako.Ule muda wa malipo umewadia.Kesho ni hukumu ya Patrick.Endapo mahakama itamuachia huru basi sintakuwa na njia nyingine zaidi ya kuhakikisha naye anauawa.Ni adhabu mbili tu anazostahili Patrick,kifungo gerezani au kifo.Yule mwanamke wake hali kadhalika naye anastahili adhabu ya kifo.Nitamsaka kokote aliko na kuhakikisha kwamba naye anakufa.Sintakuangusha mdogo wangu” akasema Loniki huku akitoa machozi.Akachukua maua aliyokuja nayo akayaweka juu ya kaburi na kuondoka


* * * *

Saa tatu za usiku,Patrick amejilaza kitandani.Pembeni yake alikuwepo mpenzi wake Savanna.Kutwa nzima ya leo Patrick alikuwa ni mtu mwenye mawazo mengi sana.
“Patrick mpenzi wangu,nimekwisha kuambia kwamba usiwe na mawazo wala wasiwasi.Kesi hii tumepambana nayo vya kutosha na nina uhakika mkubwa wa kushinda.I’ve done my best na ndiyo maana nina uhakika mkubwa wa kushinda kesi hii.Endapo itakuwa vnginevyo basi yatakuwa ni matakwa ya mahakama lakini hata kama ikiwa hivyo basi nitakata rufaa na kupambana tena.Kitu muhimu ni kuwa tayari kwa maamuzi yoyote yatakayotolewa na mahakama.” Akasema Savanna.Patrick ambaye alikuwa amejilalaza akainuka na kukaa halafu akamtazama Savanna kwa makini na kusema
“I’m scared.Sielewi kwa nini nina hofu kubwa.Sijawahi kuwa na hofu ya namna hii maishani mwangu.|” akasema Patrick huku akiupeleka mkono wake sehemu ya kifua unapokaa moyo
“Kitu gani kinakufanya uwe na hofu Patrick? Akauliza Savanna
“Nahofia iwapo nitahukumiwa kifungo maisha yangu ambayo kwa sasa tayari yameanza kwenda vizuri yataharibika na kila kitu kitapotea” Akasema Patrick
“Patrick,tumepambana vya kutosha na mimi kama wakili niliyeisimamia kesi hii ninauhakika mkubwa sana kwamba nimefanya kazi yangu ipasavyo kuishawishi mahakama ikuachie huru.Hoja tulizojenga na kuziwasilisha ni nzito na zina ushahidi wa kutosha.Lakini watoa hukumu nao ni binadamu na inawezekana wakaamua tofauti na tunavyotegemea sisi lakini hata kama ikitokea watakuhukumu kifungo tutakata rufaa.” Akasema Savanna na kumfanya Patrick atabasamu na kumvuta Savanna karibu akambusu
“Kila mara namshukuru sana Mungu kwa kunipa mwanamke ambaye ni jasiri na ambaye yuko tayari kufanya kila linalowezekana kwa ajili yangu.Endapo mahakama itaniachia huru basi ndani ya kipindi kifupi sana lazima tufunge ndoa.”
Uso wa Savanna ukajenga tabasamu pana
“Patrick mpenzi wangu ,Mungu aliyetukutanisha anafahamu ni namna gani ninakupenda.Ni Mungu huyu huyu ambaye atatusaidia ili tuweze kuitimiza ndoto yetu hii kubwa.Siku zote tunatakiwa tumuamini na kumtegemea yeye pekee.Kwa imani niliyonayo kwa Mungu huyu mmoja muumba wa mbingu na nchi nina imani tutashinda kesi na tutafanikiwa kuwa pamoja milele “ akasema Savanna huku amemkumbatia Patrick kwa nguvu
“Savanna endapo nitapewa adhabu ya kifungo gerezani tafadhali naomba usinitelekeze kama walivyofanya wengine.Naomba unisubiri hadi hadi hapo nitakapomaliza kifungo changu ili tuweze kuitimiza ndoto yetu ya kuwa pamoja.Will you wait for me darling?
“Patrick kwanza naomba ufahamu kwamba hutakwenda gerezani.Hata kama ikitokea kwamba utahukumiwa kifungo basi itapambana hadi nihakikishe ninakutoa.Kuhusu kukusubiri usitie shaka kuhusu hilo.Niko tayari hata kutumia muda wangu wote uliobaki hapa duniani kukusubiri wewe tu kwa hiyo usiwe na hofu hata kidogo na hilo.” Akasema Savanna kwa sauti laini
Waliongea mambo mengi sana usiku huo .Savanna alijitahidi kwa kila alivyoweza kumpa moyo Patrick kuhusu hukumu yake siku itakayofuata.Huu ulikuwa ni usiku mgumu sana kwa Patrick.Alitumia muda mwingi kusali na kumuomba Mungu amuepushe na kifungo
TUKUTANE SEHEMU IJAYO......
 
Back
Top Bottom