STORY: Miss Tanzania

MISS TANZANIA
SEHEMU YA 58
MTUNZI:pATRICK.CK
CONTACT:0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Patrick kwanza naomba ufahamu kwamba hutakwenda gerezani.Hata kama ikitokea kwamba utahukumiwa kifungo basi itapambana hadi nihakikishe ninakutoa.Kuhusu kukusubiri usitie shaka kuhusu hilo.Niko tayari hata kutumia muda wangu wote uliobaki hapa duniani kukusubiri wewe tu kwa hiyo usiwe na hofu hata kidogo na hilo.” Akasema Savanna kwa sauti laini
Waliongea mambo mengi sana usiku huo .Savanna alijitahidi kwa kila alivyoweza kumpa moyo Patrick kuhusu hukumu yake siku itakayofuata.Huu ulikuwa ni usiku mgumu sana kwa Patrick.Alitumia muda mwingi kusali na kumuomba Mungu amuepushe na kifungo

ENDELEA……………..

Familia nzima ya mzee Kibaho ilikuwa imekusanyika kwa ajili ya kusali sala ya jioni kama ilivyo kawaida yao kukutana na kusali pamoja kabla ya kwenda kulala.Siku hii ya leo kulikuwa na maombi maalum ya kumuombea Patrick ambaye hukumu yake ilitegemewa kutolewa siku inayofuata.Pamoja na maombi haya ya familia lakini Happy yeye alikuwa na maombi yake binafsi ya kufunga na kusali kwa muda wa siku tatu akimuomba Mungu amsaidie Patrick achiwe huru.
Baada ya kumaliza maombi yale ya jioni Happy na mdogo wake Margreth wakaenda chumbani kwao.
“Margreth I’m so nervous.Nahisi kama mwili wangu unatetemeka kila nikifkiria whats going to happen tomorrow.” Akasema Happy Margreth aliyekuwa anapanga nguo katika kabati lake akaacha kazi ile na kumfuata Happy
“Do you believe in God? Akauliza Margreth
“Ofcourse I do “ akajibu Happy
“Vizuri.Kama unamuamini Mungu muache atende kazi yake.Hana sababu ya kuogopa hata kidogo.Mtumaini yeye siku zote” akasema Margreth
“Margreth I believe in God lakini nashidwa kujizuia kuwa na wasiwasi.Sifahamu kitakachotokea kesho_Ouh Gosh! Akasema Happy
“Ilitakiwa mimi ndiye niwe nimesimama kizimbani siku ya kesho nikihukumiwa na si Patrick.Lakini Patrick ndiye anayehukumiwa badala yangu.Sijawahi kuona mtu mwenye upendo mkubwa na wa ajabu kama huyu.I’m so sorry I’ve lost him and I don’t know what to do to get him back.” Akasema Happy
“Happy tafadhali usiwaze sana kuhusu mambo hayo.Tusubiri kwanza hadi siku ya kesho tuone nini kitatokea na baada ya hapo tutajua nini cha kufanya” akasema Margreth
“Margret sina ujanja tena.Tayari nimekwisha mpoteza Patrick.” Akasema Happy na mara wote wakastushwa na mlio wa simu ya Margreth.Akaichukua na kutazama mpigani halafu akavuta pumzi ndefu
“Its mike” akasema
“Tell him I’m not around” akasema Happy
“Happy siku ya leo hii ni mara ya tatu anapiga simu na hutaki kuongea naye.Happy I dont want to lie anymore.Please talk to him” akasema Margreth
“Ouh My God I don’t know what to tell him” akasema Happy
“Tell him anything.Ana hamu sana ya kuongea nawe.Mike ni mchumba wako.Ukikataa kuongea naye unamuumiza sana na utamfanya ahisi kwamba huku mambo si shwari.Tafadhali ongea naye.” Akasema Margreth.Happy akachukua simu ile ambao bado iliendelea kuita akabonyeza kitufe cha kupokelea simu
“Hallow Mike” akasema Happy.Mara moja Mike akaitambua sauti ya Happy
“Hallo malaika wangu .” akasema Mike kwa furaha
“Unaendeleaje Mike? Akasema Happy
“Ninaendelea vizuri Happy.Nimefurahi sana kuisikia sauti yako.Unaendeleaje? akauliza Mike
“Naendelea vizuri Mike.”
“Nafurahi kusikia hivyo.I miss you a lot my angel” akasema Mike
“I miss you too” akajibu Hapy
”How’s Patrick? Akauliza Mike na kumfanya Happy asite kujibu
“Happy how’s Patrick? Uliniambia kwamba hukumu yake ni kesho?
“Ndiyo Mike hukumu yake ni kesho” akajibu Happy
“Utahudhuria mahakamani? Akauliza Mike
“Ndiyo Mike nitahudhuria kwani ndicho kitu pekee ambacho kimeniweka hapa hadi muda huu kwa hiyo siwezi kukosa mahakamani.” Akajibu Happy
“Are you guys talk often? Akauliza Mike
“Mike mbona una wasi wasi hivyo? Akauliza Happy
“Lazima niwe na wasi wasi mpenzi wangu kwa sababu nafahamu kwamba Patrick ana sehemu kubwa sana moyoni mwako kwa hiyo nashindwa kujizuia kuwa na wivu kila nikifikiria kwamba uko karibu naye na mnaweza mkaonana” akasema Mike
“Usihofu Mike.Mimi na Patrick kilichobaki ni historia tu kati yetu na hakuna chochote kinachoendelea.Tayari kila mmoja ameendelea na maisha yake.Tayari naye ana mchumba na wanategemea kufunga ndoa muda wowote.Kwa hiyo huna sababu ya kuhofu”
“Hizo ni habari njema sana.Kwa hiyo utarejea mara tu baada ya hukumu kutolewa?
“Ndiyo Mike.Ni hicho tu kilichokuwa kinaniweka hapa na baada ya siku ya kesho I’ll say goodbye to Tanzania and leave this blessed country for good.Mike kuna jambo nataka kukueleza” akajibu Happy
“Jambo gani Happy?
“Unakumbuka uliwahi kuniomba nifunge nawe ndoa na nikakwambia kwamba unisubiri hadi hapo nitakapokuwa tayari?
“Ndiyo Happy nakumbuka sana na sijawahi kukuuliza tena kuhusu suala lile kwa sababu nilitaka utafakari na kama ukiwa tayari basi unijibu”
“Mike naomba nikufahamishe kwamba tayari nimekwisha fanya maamuzi yangu na jibu langu ni ndiyo.Nitafunga ndoa nawe Mike” akasema Happy na Mike akaruka kwa furaha asiyaamini masikio yake.
“Ouh Happy kwa muda mrefu sana nimekuwa nikisubiri unitamkie maneno kama haya.Nimefurahi sana mpenzi wangu.Nitaanza maandalizi mara moja na kuwataarifu ndugu na jamaa kuhusu jambo hili jema.”
“Hapana Mike usimwambie mtu yeyote kwanza.Tutawaambia tutakapokuwa pamoja nitakaporudi”
“sawa malaika wangu.Chochote utakacho niamuru nitatii.Ninakupenda sana Happy.Ahsante sana”
“Hata mimi nakupenda sana Mike na ndiyo maana nahitaji kuwa nawe katika maisha yangu yote yaliyobaki hapa duniani” akasema Happy.Wakaagana na kukata simu
“Happy !! akaita Margreth
“Una hakika na hicho ulichokisema?
“Kitu gani Margreth?
“kwamba unataka kuolewa na Mike? Happy akainama na kusema
I don’t know Margreth but I think that’s the best way to do for now.”
“Happy kwa nini umemwambia Mike jambo ambalo huna uhakika nalo?
“Margreth I have to do this.I’ll learn to love Mike.” Akasema Happy.Margreth akainamisha kichwa akaonekana kusikitika
“Unasikitika nini Margreth?
“Ninasikitika kwa sababu you cant swallow back what you’ve promised Mike.Kwa maana hiyo basi unatakiwa usimame katika maneno yako.Lazima uolewe na Mike.Jitahidi usimuumize kama wakati ule.”
Happy akazama katika mawazo mengi na baada ya muda akasema
“Margrteh I’ve made my decision.I’ll marry Mike.Hakuna uwezekano tena wa kuwa na Patrick.I’ve lost him”

**********************

Ni dakika ya pili sasa toka alipoweka shingoni tai yake akitaka kuifunga.Alikuwa amesimama mbele ya kioo kikubwa cha kujtazamia .Sauti ndogo ya muziki ilikuwa inasikika.Patrick alikuwa anabubujikwa na machozi kutokana wimbo uliokuwa uitwao see you again wimbo ulioimbwa na Carrie underwood
I will see you again,woah
This is not where it ends
I will carry you with me oh
Till I see you again
Patrick akaimba kibwagizo cha wimbo ule na mara Savanna akaingia mle chumbani na kuuzima mziki ule
“Patrick mbona unajipa wakati mgumu namna hiyo? Kwa nini ujiumize moyo wako? Just relax.Everything will be fine.Stop torturing yourself.” Akasema Savanna huku akimfuta machozi
“Savanna malaika wangu I’m so scared .Nashindwa kujiuia kuwaza nini kitatokea endapo nitahukumiwa kifungo.Hii ni siku ngumu sana katika maisha yangu”
“Patrick usiwaze sana kuhusu nini kitatokea.Tujiandae kwa maamuzi yoyote yale yatakayotolewa na mahakama.I’ve done my level best as a lawyer lakini mahakama ndiyo yenye kutoa maamuzi.Endapo watatoa adhabu ya kifungo gerezani,tutakata rufaa kama nilivyokuahidi.I’m right here beside you ,you are not alone” akasema Savanna na kumbusu Patrick halafu akamfungia tai
“Now you look perfect.you are so handsome Patrick.I love you” akasema Savanna na kumbusu tena Patrick shavuni
Wakati Savanna akijiandaa Patrick alitoka mle chumbani na kwenda nje ya nyumba
“Ni katika nyumba hii furaha yangu ya maisha iliporejea tena.Endapo nitafungwa gerezani nitaikosa nyumba hii iliyojaa furaha amani na upendo.” Akawaza Patrick halafu akarejea ndani.Savanna alimaliza kujiandaa akajumuika na mpenzi wake mezani wakapata stafstahi
“Are you ready to go Patrick? Akauliza Savanna
“I’m ready” akajibu Patrick na kisha wakatoka wakaingia garini na kuondoka kuelekea mahakamani


* * * *

Saa tatu za asubuhi ilimkuta Sarah tayari amekwisha wasili mahakamani.Aliwahi sana kufika pale ili apate nafasi ya kuonana na Linah ambaye alimwahidi kumpigia simu na kumfahamisha kuhusiana na mpango wa namna watakavyoweza kumdhibiti Loniki asiweze kuutekeleza mpango wake wa kumdhuru Patrick endapo mahakama itamuachia huru,lakini toka walipoonana usiku ule Linah hakumpigia tena simu jambo lililoanza kumpa wasi wasi.Kilichompa wasiwasi zaidi simu ya Linah haikuwa ikipatikana na hakupafahamu mahala alipokuwa amehamia.Mtu pekee ambaye angeweza kumpa jibu la wapi alipo Linah ni Loniki lakini aliogopa kumuuliza chochote kutokana na mahusiano yao kutokuwa mazuri.Pale mahakamani alijaribu kuangaza huku na huko lakini hakumuona mtu yeyote wa familia yake.Akachukua simu na kumpigia mama yake.
“mama shikamoo’
“Marahaba Sarah.Hujambo?
“Sijambo mama”
“Uko wapi Sarah? Si unajua leo ni siku ya hukumu?
“Nafahamu mama.Tayari niko hapa mahakamani.”
“Mbona umewahi namna hiyo?
“Ndiyo mama nimeamua tu kuwahi.Unakuja mahakamani?
“Ndiyo ninakuja niko njiani”
“Uko na Loniki?
“Hapana.Loniki amekuja kuchukuliwa na rafiki yake asubuhi ya leo.Aliniaga kwamba kuna sehemu wanakwenda lakini hatachelewa kufika mahakamani”
“rafiki yake yupi unayemzungumzia? Akauliza Sarah
“Kwani Loniki ana rafiki mwingine zaidi ya Linah? Huyo ndiye aliyefika asubuhi na wakaondoka wote”
“Sawa mama.Mimi utanikuta hapa” akasema Sarah na kukata simu
“Kwa nini Linah hajawasiliana nami kama alivyoniahidi na simu yake haipatikani tena? Amekwenda wapi na Loniki asubuhi hii? Kuna kitu gani kinachoendelea? Inawezekana Linah akawa ameshindwa kupata njia ya kumdhibiti Loniki? Edapo sintakuwa nimeonana naye hadi hukumu itakapotolewa na mahakama ikamuachia huru Patrick basi sintakuwa na njia nyingine zaidi ya kulifikisha suala hili katika vyombo vya usalama.” Akawaza Sarah huku akijaribu kupiga tena namba za simu za Linah bila mafanikio

* * * *

“C’mon Khumalo what happened to you? “ akasema Loniki akiwa na simu mkononi akijaribu kupiga tena na tena namba za khumalo lakini kila alipopiga jibu lilikuwa moja tu
“Namba ya simu ya mteja unayempigia haipatikani kwa sasa.tafadhali jaribu tena baadae.”
“Damn it !!! “ akasema Loniki kwa hasira na kugonganisha mikono yake.Linah aliyekuwa katika usukani akamtazama bila kusema chochote akaendelea na kukanyaga mafuta
Loniki na Linah walikuwa wanaelekea nyumbani kwa Khumalo.Asubuhi na mapema Linah alimfuata Loniki nyumbani kwao na kumfahamisha kwamba Khumalo hakuwa anapatikana simuni,taarifa ambayo ilimstua sana Loniki na akaamuru wamfuate Khumalo nyumbani.Katika siku hii Loniki alimuhitaji sana Khumalo ili aweze kutekeleza mpango waliokuwa wameongea wa kumuua Patrick endapo mahakama ingemuachia huru.Linah alifuata kila alichokisema Loniki lakini moyoni alikuwa akifahamu wazi kwamba Khumalo hakuwepo na walipanga Khumalo atoweke baada ya kupokea fedha toka kwa Loniki.
“Huyu Khumalo mbona anaanza kunipa wasi wasi? Kwa nini hapatikani simuni wakati anajua fika kwamba leo ni siku ambayo Patrick anahukumiwa kwa hiyo lolote linaweza kutokea? Loniki akajiuliza maswali mfululizo.Linah ambaye siku hii ya leo alionekana kuwa mkimya na mwenye wasi wasi mwingi hakujibu chochote
“Say something Linah” akafoka Loniki
“Niseme nini Lonny? Khumalo hapatikani simuni .Tunachotakiwa ni kufika nyumbani kwake na kuangalia kama ana tatizo.Pengine labda simu yake ikawa na matatizo” akasema Linah
“What a stupid woman.Sihitaji tena urafiki na mjinga kama huyu.After today its over.Hanisaidii kitu chochote katika maisha yangu zaidi ya kuniingiza katika mambo ambayo yanaweza kuniletea matatizo.Amenishirikisha katika mipango yake ya visasi na kunisababishia dhambi kubwa .Kitendo cha kumdhalilisha Happy namna ile kinaniumiza sana hadi leo hii.Sitaki tena urafiki na huyu mjinga” akawaza Linah wakati wamekaribia kufika nyumbani kwa Khumalo
Walifika katika jumba la Khumalo.Linah akapiga honi ili wafunguliwe geti.Loniki baada ya kuona mlinzi anachelewa kutoka akafungua mlango wa gari na kushuka garini akaenda kubonyeza kengele ya getini.Baada ya muda kidogo mlango mdogo wa geti ukafunguliwa
“Habari yako? Akasema jamaa mnene aliyefungua geti
“Habari nzuri” akajibu Loniki
“Nikusaidie nini? Akauliza yule jamaa
“Nina shida na Khumalo.Ninaitwa Loniki na mwenzangu pale garini anaitwa Linah.Sisi ni marafiki zake na tuna biashara naye ya muhimu sana”
Una biashara gani na Khumalo?
“Kuna kazi nilikuwa nimeelewana naye aifanye ambayo anatakiwa aifanye leo lakini kitu cha kushangaza ni kwamba hapatikani katika simu hivyo tumeamua kuja hapa nyumbani kwake kuonana naye” akasema Loniki
“Samahani dada yangu.Khumalo hayupo amesafiri” akasema yule jamaa na kumfanya Loniki ahamaki
“Acha utani ndugu yangu.Khumalo amesafiri lini na bila kututaarifu?
“Khumalo hayupo dada amepatwa na safari ya ghafla na kuondoka usiku wa kuamkia leo.” Akasema yule kijana .
“Ouh gosh ! amesema atarudi lini? Akauliza Loniki ambaye alionekana kustushwa sana na jibu lile
“hakusema atarudi lini lakini mara nyingi huwa akisafiri humchukua hata zaidi ya miezi sita kurejea.” Akasema yule kijana na kuzidi kummaliza nguvu Loniki
“Hakuna namna ambayo tunaweza kumpata au kuwasiliana naye ili kama yeye hauypo basi vijana wake waifanye kazi tuliyokubaliana kwani tayari nimekwisha mlipa fedha zote alizozihitaji” akasema Loniki
“Khumalo akisafiri kumpata huwa ni kazi ngumu sana kwa sababu huwa hatulii katika sehemu moja”
Jibu lile likamnyong’onyeza kabisa Loniki akaegemea ukuta.Baada ya kutafakari akaagana na Yule kijana na kurejea tena garini
“ Damn it !!...akafoka Loniki baada ya kurejea garini.Alikuwa amekasirika sana na kijasho kilianza kumchuruzika
“amesemaje yule kijana? Khumalo yuko wapi? Akauliza Linah ambaye alikuwa amebaki garini
“Khumalo amesafiri usiku wa kuamkia leo na haijulikani kama atarejea hivi karibuni” akasema Loniki
“ How could he do that? Kwa nini aondoke kimya kimya bila kututaarifu wakati alijua kabisa tuna mkataba naye na tayari fedha zote alizozihitaji nimeshampatia?Kwa nini ametufanyia hivi?.” Akalalamika Loniki
“kwa hiyo tutafanya nini? Akauliza Linah
“Sina hakika kama ni kweli Khumalo amesafiri .Najua atakuwa amejificha mle ndani.” Akasema Loniki
“Hapana Loniki.Kama umeambiwa kwamba Khumalo hayupo ni kweli atakuwa amesafiri.”
Loniki akageuka akamtazama Linah kwa muda kisha akasema
“How could you believe him so easily?
“Kwa sababu ninamfahamu vizuri Khumalo.Ni mtu ambaye huwa muwazi siku zote na kama imetokea amesafiri ghafla namna hii basi lazima kuna sababu ya msingi sana iliyomuondoa hapa nchini usiku .Inawezekana labda alikuwa anakimbia vyombo vya usalama kutokana na shughulio anazozifanya” Akasema Linah
“you failed me Linah.Wewe ndiye uliyeniambia nimuamini Khumalo.Unaona sasa kitu ambacho ametufanyia? Nini kitafuata iwapo mahakama itamuachia Patrick huru? Linah siwezi kukubali kumuona Patrick akiachiwa huru na akendelea kula raha na Malaya wake huku mdogo wangu akiwa ameoza kaburini.Endesha gari tuondoke” akasema Loniki kwa ukali
“Tunaelekea wapi?
“Turudi nyumbani”
“Lonny huoni kama tutachelewa mahakamani? Nyumbani tunaenda kufanya nini? Akauliza Linah
“Nimesema endesha gari tunarudi nyumbani? Akafoka Lonny.Linah akageuza gari na safari ya kurejea nyumbani ikaanza.
Waliwasili nyumbani kwa akina Loniki na kwa haraka akashuka garini akaelekea moja kwa moja chumbani kwa mama yake.Kabati kubwa la nguo halikuwa limefungwa na funguo,akalifungua na kifungua droo ndogo ndani ya lile kabati halafu akatabasamu
“Nilijua tu lazima itakuwepo,Baba alikuwa na bastora mbili kabla hajafariki.Moja ni ile aliyoitumia Vero kutaka kumtoa uhai yule shetani na nyingine ni hii hapa.Kama Vero alimkosa siku ile,mimi sintamkosa leo.Nimehitimu mafunzo ya kulenga shabaha kwa hiyo nina uhakika mkubwa wa kuufumua ubongo wake leo endapo mahakama itamuachia huru” akawaza Lonny halafu akaibusu bastora ile
“Don’t fail me my baby.Do as I tell you to do” akasema Lonny kisha akaiweka bastora ile katika mkoba wake akachukua funguo za gari lililokuwa la Vero akatoka
“Shuka katika gari hilo .Tutatumia hili hapa” Loniki akamuamuru Linah ambaye alishuka na kuingia katika gari lile alilolitaka Lonny
“Drive” akasema Lonny
“Tunakwenda wapi Lonny? Mahakamani? Akauliza Linah
“Stop asking questions Linah.Endesha gari.Ndiyo tunakwenda mahakamani” akasema Lonny kwa ukali.
“Loniki tafadhali naomba usiwe na hasira na mimi.Nilimuamini Khumalo kwa kuwa ni mtu niliyewahi kufanya naye kazi mara kadhaa” akasema Linah Loniki akamtazama kwa jicho kali na kusema
“Save your breath Linah.Nitamalizana nawe baadae.Kwa sasa niache nifikirie kuhusu plan B” akasema Lonny
“Plan B? akauliza Linah
“Yes Plan B.Wewe na shetani mwenzio Khumalo mmenifanyia jambo baya sana kwa hiyo nitawaonyesha kwamba hata mimi nina uwezo wa kufanya hizi kazi.” Akasema Loniki
“Loniki tafadhali naomba tuheshimiane na usirudie tena kuniita mimi shetani.Kama mimi nitakuwa shetani wewe utakuwa nani? Akasema Linah kwa ukali huku akitaka kulisimamisha gari.
“Shut up you bastard.Usinipandishe hasira zangu muda huu.Kuanzia sasa utafanya kile nitakachokuamuru” akafoka Loniki huku akimuelekezea Linah bastora.Linah akatetemeka
“Ouh gosh ! Kumbe ana bastora..mshenzi huyu amedhamiria kweli kumuua Patrick endapo ataachiwa huru na mahakama.Lazima nifanye jambo kumzuia asifanye anavyotaka kufanya.Nitatafuta namna ya kuwasiliana na Sarah.Najua hadi hivi sasa atakuwa anajiuliza sana ni kwa nini sijampigia simu kumtaarifu chochote kama nilivyokuwa nimemuahidi.Kutwa nzima ya jana nililazimika kutoitumia ile laini yangu ya kawaida kwa sababu nilikuwa na huyu shetani muda wote kwa hiyo niliogopa asije gundua kwamba nilikuwa nawasiliana na Sarah.”akawaza Linah

TUKUTANE SEHEMU IJAYO.....
 
MISS TANZANIA
SEHEMU YA 59
MTUNZI:pATRICK.CK
CONTACT:0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Ouh gosh ! Kumbe ana bastora..mshenzi huyu amedhamiria kweli kumuua Patrick endapo ataachiwa huru na mahakama.Lazima nifanye jambo kumzuia asifanye anavyotaka kufanya.Nitatafuta namna ya kuwasiliana na Sarah.Najua hadi hivi sasa atakuwa anajiuliza sana ni kwa nini sijampigia simu kumtaarifu chochote kama nilivyokuwa nimemuahidi.Kutwa nzima ya jana nililazimika kutoitumia ile laini yangu ya kawaida kwa sababu nilikuwa na huyu shetani muda wote kwa hiyo niliogopa asije gundua kwamba nilikuwa nawasiliana na Sarah.”akawaza Linah

ENDELEA……………..

Kadiri muda ulivyokuwa unasonga ndivyo idadi ya watu ilivyokuwa inaongezeka mahakamani.Mpaka kufikia saa nne za asubuhi idadi ya watu ilikuwa kubwa.Sarah ambaye aliwahi sana kufika mahakamani macho yake hayakubanduka katika geti la kungilia akijaribu kuangaza kama atamuona Loniki na Linah
Akiwa bado ameyaelekeza macho yake katika geti la kuingilia mahakamani,aliziona gari tatu zikiingia.Alizifuatilia kwa macho hadi katika maegesho.Toka katika gari zile ikashuka familia ya Patrick ikiongozwa na mama yake,pamoja na ndugu wengine.Bila kupoteza muda Sarah apiga hatua na kuwafuata mahala walipo akawasabahi.Wakati akiongea na familia ya Patrick gari la mama yake likawasili pale mahakamni.Baada ya kuegeshwa mama yake Sarah akashuka garini akiongozana na akina mama wanne.Mahali alikoegesha gari si mbali sana na pale alipokuwa amesimama Sarah akiongea na familia ya Patrick.Mama yake Sarah akamuona mwanae na kumtazama kwa jicho kali bila kusema chochote .Tayari alikuwa katika uadui mkubwa na familia ya Patrick.Sarah akawaaga familia ya Patrick na kwenda kuungana na mama yake.
“Sarah unachokifanya si kitu kizuri hata kidogo” akasema mama yake kwa ukali
“Kwa nini mama?
“Kwa nini unadiriki kuungana na wale watu ambao unafahamu fika kwamba ni maadui zetu? Mtoto wao amemuua mdogo wako.Hupaswi kuandamana nao hata kidogo na hii ndiyo sababu inayokufanya wewe na dada yako Loniki msielewane”
“Mama mimi sipendezwi hata kidogo na tabia yenu hii ya kuichukia familia ya Patrick.Mambo yamekwisha tokea na tusubiri hukumu ya Mahakama muda mfupi ujao.Binafsi sina chuki yoyote na familia ile na ndiyo maana nashirikiana nao kwa moyo mkunjufu.” Akasema Sarah na mama yake akamtazama kwa jicho kali na kusonya halafu akapiga hatua kuondoa zake na wale akina mama aliokuwa ameambatana nao na kumuacha Sarah akiwa amesimama peke yake
Gari moja jeusi likaingia pale mahakamani na kuelekea sehemu ya maegesho.Ndani ya gari lile alikuwemo Happy Kibaho na familia yake.Wote wakaendelea kubaki ndani ya gari wakisubiri muda wa kusomwa hukumu ufike .Happy aliogopa kushuka garini kuwakwepa waandishi wa habari waliokuwa wakimtafuta usiku na mchana ili kumuhoji bila mafanikio.
Happy na familia yake wakiwa bado ndani ya gari,katika geti la kuingilia pale mahakamani likaingia gari moja la kifahari aina ya Mercedece benz s 320 CDI 4 MATIC ya rangi nyeusi na kwenda kuegesha si mbali sana na mahala walipokuwa wameegesha gari akina Happy.Baada ya sekunde kadhaa. Milango ya gari lile la kifahari sana ikafunguliwa akashuka Patrick na Savanna.Patrick alikuwa mevaa suti nyeusi iliyomkaa vyema na miwani myeusi kuyaziba macho yake.Savanna naye halikadhalika alivaa suti ya rangi nyeusi.Mara tu waliposhuka waandishi wa habari waliwazingira na kuanza kuwapiga picha.Hawakuwajali wakashikana mikono na kuelekea moja kwa moja ndani ya jengo la mahakama.
Akiwa ndani ya gari na familia yake Happy akawashuhudia Patrick na Savanna wakiingia mahakamani.Ni wazi alikuwa anaumia sana moyoni.Familia yote ilikuwa kimya kabisa.Hawakutaka kusema kwa kuogopa Happy asije umia zaidi
“Mimi ndiye niliyepaswa kumsindikiza Patrick mahakamani leo.Nasikitika sana kumpoteza Patrick” akawaza Happy
Nusu saa baadae watu wakaanza kuingia mahakamani kwani hukumu ilitarajiwa kuanza kusomwa muda wowote.Happy na familia yake wakashuka garini na kuungana na watu wengine waliokuwa wanaingia ndani ya mahakama.Wapiga picha bila kuchelewa wakaanza kumpiga picha Happy wakati akitembea kuingia ndani ya mahakama akiwa na familia yake.Ukumbi wa mahakama ulifurika watu
Saa tano na dakika kumi jopo la majaji watatu wa mahakama kuu wakiongozwa na Jaji Gregory Mkaga wakaingia mahakamani.Watu wote walikuwa kimya kabisa wakisilikiza.
Saa sita na dakika ishirini na saba Loniki na Linah wakawasili mahakamani.Walikuwa wamechelewa sana na tayari mahakama ilikuwa inaendelea.Loniki akaitoa bastora yake katika mkoba akaitazama kisha akairudisha mkobani.
“Twende tuingie mahakamani.” Akaamuru Loniki ,wakashuka na kuingia mahakamani huku mkoba uliokuwa na bastora ukibaki ndani ya gari
Hatimaye muda wa kusomwa hukumu ukawadia.Hiki kilikuwa ni kipindi kigumu sana kwa watu wote.Patrick alikuwa anatetemeka mwili huku akiomba kimoyo moyo Mungu amsaidie na amuepushe na kifungo.Happy alikuwa ameweka mkono wake wa kulia katika sehemu ya kifua mahala ulipo moyo.Alihisi mwili mzima kumtetemeka.Kila mtu pale mahakamani kiroho kilimdunda
“God please help Patrick and help me too.I don’t know what’s going to happen if Patrick will go to jail.” Happy akaomba kimya kimya.
Loniki ambaye alikuwa amesimama nyuma kabisa ya chumba cha mahakama kwa kukosa nafasi ya kukaa mikono yake ilikuwa inamtoka jasho
“Hiki ndicho kipindi cha kubaini nini kitatokea.I’m not scared to kill him if the court will set him free.I swear I’ll kill him today” akawaza Loniki huku moyo wake ukimwenda mbio sana.Linah ambaye naye aliokuwa amesimama pembeni ya Loniki miguu yake ilikuwa inamtetemeka.Alikua akitafuta njia ambayo angeitumia ili kumdhibiti Loniki asiweze kutimiza lengo lake la kumuua Patrick endapo angeachiwa huru na mahakama.Alifikiria kuwataarifu polisi kuhusu suala lile lakini akaogopa kwamba huenda hata naye lingemletea matatizo kwani alihusika kwa kiasi kikubwa katika mipango yote ya loniki
“Njia pekee hapa ni kuwasiliana na Sarah lakini nitawasiliana naye vipi wakati Loniki tayari amenibana? I Must find a way,ngoja kwanza hukumu itolewe” akawaza Linah
Savanna aliyekuwa amekaa mbele kabisa alikuwa kimya.Japokuwa anajiamini kwa kazi kubwa aliyoifanya akishirikiana na jopo la mawakili kutoka kampuni yake ya uwakili,alishindwa kujizuia kuogopa kwani hakujua nini kinakwenda kutokea muda mfupi unaokuja.
“Ee Mungu ,nakuachia wewe kila kitu.Nimeifanya kazi yangu ya kumtetea Parick kwa uwezo wangu wote ulionijalia lakini wewe ndiye mwamuzi wa yote.Kama ni kwa mapenzi yako Patrick aende gerezani sina tatizo lakini kama ikikupendeza naomba Patrick aachiwe huru.Hakutenda kosa hili na zaidi ya yote ninamuhitaji sana katika maisha yangu” Savanna naye alikuwa amefunga mikono yake kifuani akifanya maombi ya kimya kimya akisubiri hukumu..Huu ulikuwa ni wakati wa kila mtu kuomba kile alichokuwa anakitaka kitokee
Kwa mujibu wa kifungu cha 326(1) b cha sheria ya mwenendo wa mashtaka sura ya 20 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002 mahakama kuu kanda ya Dar es salaam ilimuachia huru Patrick baada ya kuridhishwa na ushahidi uliotolewa mahakamani na upande wa utetezi kwamba kifo cha Vero kilitokea kwa bahati mbaya kati kati ya purukushani za kunyang’anyana silaha ambayo Vero alitaka kuitumia katika kufanya mauaji.
“Yametimia.Twende tuondoke” Loniki akamuamuru Linah wakatoka nje na moja kwa moja wakaelekea katika gari lao.Baada ya kuingia garini Loniki akainama na kulia sana
“He killed my sister..!!! why they let him go??? Why???!!!!!!!...Loniki alilia kwa uchungu
“Vero nitakulipizia kisasi.Siwezi kukubali mtu aliyekukatili uhai wako aendelee kuwa hai.” Akasema Loniki kwa uchungu
“Pamoja na kutoa mamilioni ya fedha ili huyu shetani afungwe gerezani lakini bado imeshindikana.You failed me Linah..You failed me.I knew this would happen…!! Thank you” akasema Loniki.
“Lonny mimi si wa kulaumiwa hata kidogo haya ni maamuzi ya mahakama.Kazi yangu ilikuwa ni kusuka mipango ya kumfunga Patrick lakini kama majaji wameamua hivi na tayari wamekwisha kula hela yetu basi kuna kila ulazima wa kuwauliza kulikoni mambo yawe hivi? Akasema Linah
“Shut up Linah..! Hakuna haja ya kuwatafuta tena hao majaji.Tayari nimekwisha poteza mamilioni ya fedha ambazo hazitaweza kurudi na hakuna chochote kilichofanyika.” Akasema Loniki kwa ukali
Watu sasa walianza kutoka mahakamani.Mama yake Loniki naye alitoka mahakamani akiongozana na akina mama wanne waliokuwa wamemshikilia.Alikuwa analia,aliumizwa sana na maamuzi yale ya mahakama.Lonny akamtazama mama yake kwa uchungu akainama na kufuta machozi
“Nilijua toka mwanzo jambo kama hili linaweza kutokea na ndiyo maana sikutaka kusubiri hukumu ya mahakama.Hakuna hukumu ya haki itakayotendeka na ndiyo maana nikaamua kutafuta hukumu yangu mwenyewe lakini wewe Linah na Khumalo mkanizuia nisifanye nilivyokuwa natka kufanya..Umeona sasa kilichotokea? Muuaji wa mdogo wangu ameachiwa huru..” akasema Loniki kwa uchungu.
Watu sasa walikuwa wengi nje ya mahakama.Wengi hususani ndugu jamaa na rafiki wa Patrick walikuwa na furaha na walionekana wakipongezana.Waliifurahia hukumu ile na kuipongeza mahakama kwa kutenda haki.Happy naye alitoka mahakani akiongozana na familia yake. Uso wake ulikuwa umepambwa na tabasamu pana sana licha ya machozi kuendelea kumtiririka.Alikuwa analia kwa furaha ya Patrick kuachiwa huru.Ili kumuepusha Happy na maswali ya waandishi wa habari wakaelekea moja kwa moja katika gari lao lakini Happy akagoma kuingia
“Happy mambo yamekwisha hapa mahakamani.Ingia garini tuondoke” akasema mzee Kibaho
“No dady.!I have to talk to Patrick before I leave.May be its going to be my last talk to him” akasema Happy
Wakiwa ndani ya gari wakiangalia kilichokuwa kinaendela,Loniki na LInah wakamshuhudia Sarah akimpa mkono mama yake Patrick.Kiendo kile kikazidi kumuumiza Loniki
“ After Patrick,that bastard will be next.I must teach her a lesson.Simtambui tena Saraha kama ndugu yangu.I don’t know her anymore” akasema Loniki kwa hasira.Vicheko na kupongezana viliendelea nje ya mahakama na hatimaye baada ya muda Patrick naye akatoka akiwa ameongozana na Savanna.Watu walimpongeza na kumsifu Savanna kwa umahiri wake .Kwa mara nyingine tena alidhihirisha umahiri wake katika masuala ya sheria.
Wakati mambo haya yote yakiendelea,Happy alikuwa nyuma ya gari lao akiandika kitu katika kijitabu chake kidogo.alipomaliza akaichana ile karatasi na kuishika mkononi na kuanza kupiga hatua kuelekea katika umati ule wa watu alikokuwa Patrick bila kujali waandishio wa habair na wapiga picha waliokuwa wakimpiga picha katika kila hatua aliyopiga..Savanna ndiye aliyekuwa wa kwanza kumuona Happy karibu na mahala walipokuwa wamesimama
“Happy!” akasema Savanna na kumfuata Happy akamshika mkono akamkumbatia na kupiga piga mgongoni.
“Hongera sana Savanna.Nimeikubali kazi yako.Wewe ni mmoja kati ya wanasheria mahiri kabisa hapa nchini”
“Thank you” akajibu Savanna
“Namshukuru sana Mungu kwa kushinda kesi hii” Akasema Savanna na mara Patrick akatokea
“Happy ! akasema Patrick
“Patrick ! …akasema Happy halafu wakakumbatiana kwa furaha.Savanna ambaye alikuwa amesimama pembeni yao akatabasamu .Happy akasogeza mdomo wake hadi karibu na sikio la Parick akamnong’oneza jambo.
“Hongera sana Patrick.Thank you that you saved me,you saved my life.I’ll always be thankfull to you” akasema Happy halafu akatumbukiza kitu katika mfuko wa koti la Patrick.Taratibu huku machozi yakimtoka Happy akamuachia Patrick na kuanza kuondoka huku Savanna na Patrick wakimtazama
“dady its over now.Tunaweza kuondoka” akasema Happy baada ya kuingia garini
“Ahsante Mungu kwa kusikia kilio chetu na hatimaye Patrick yuko huru.Nina furaha na uchungu kwa wakati mmoja.Ninafuraha kwa kuwa Patrick ameachiwa huru kwa sababu hakutenda kosa lolote .Aliubeba mzigo wangu mimi.Ninalia kwa uchungu kwa sababu hivi sasa ningekuwa pembeni yake tunaufurahia ushindi huu kwa pamoja na pengine ungekuwa ni mwanzo wa kuelekea kutimiza ndoto zetu nyingi tulizokuwa nazo_Ouh gosh ! there will be no dreams anymore.There is no us.I’ve lost Patrick”akawaza Happy.
.Zaidi ya nusu saa bado zoezi la kupongzana liliendelea pale nje ya mahakama.
“Patrick tumekaa sana hapa.Sherehe hizi zinatakiwa zikaendelee nyumbani.Tunatakiwa tuandae sherehe ya kukupongeza.Leo nina furaha sana” akasema Alois kaka yake Patrick.Patrick akatabasamu halafu akamvuta Savanna karibu yake na kusema
“Nadhani yatubidi tuelekee nyumbani kwanza .Nataka nikapunzishe kichwa changu na kumshukuru malaika wangu huyu ambaye ameniwezesha leo niwe huru tena.Nina deni kubwa kwa Savanna.Amepambana kufa na kupona hadi nimeshinda kesi.Nadhani muda huu ni maalum kwa ajili yetu na jioni ya leo tutakuja nyumbani kwa ajili ya kuwashukuru familia nzima” akasema Patrick
“kama ni hivyo basi tutaandaa sherehe ndogo jioni ya leo.Tafadhali hakikisha hukosi kufika nyumbani jioni ya leo” akasema Alois
Patrick akamfuata mama yake aliyekuwa amezungukwa na akina mama wengine ,akamvuta pembeni
“mama mimi naondoka.Nimeongea na Alois nitakuja nyumbani jioni ya leo kwa ajili ya kutoa shukrani zangu kwenu kwa msaada wenu mkubwa katika kipindi chote hiki cha matatizo yangu.”
“Nilidhani tunaondoka wote na kwenda nyumbani? Tunahitaji sana kukaa kama familia leo ni siku yetu kubwa sana” akasema mama yake Patrick
“Ninafahamu hilo mama lakini kwa sasa nahitaji kupumzika kidogo na kumshukuru Mungu.Nitakuja jioni na tutajumuika pamoja” akasema Patrick halafu akaagana na mama yake akamshika mkono Savanna na kuingia katika gari lao na kuondoka
“washa gari.We follow them” akaamuru Loniki ambaye alikuwa garini na Linah .Bila ubishi Linah akawasha gari na kuanza kuwafuata akina Patrick
Sarah bado aliendelea kuangaza macho pale mahakami akitegemea kumuona Linah.Muda wote alikuwa roho juu kila alipokumbuka maneno ya Linah kwamba Loniki amedhamiria kufanya jambo baya endapo mahakama itamuachia huru Patrick.
“Inawezekana Linah alikuwa ananidanganya? Hapana ,Linah hakuwa ananidananya na katu hawezi kufanya hivyo.Ninaheshimiana naye sana na katu hawezi kuthubutu kucheza na akili yangu namna hii.Ninashawishika kuyaamini maneno yake.Lakini mbona hakunipigia simu kama alivyokuwa ameniahidi? Na simu yake kwa nini haipatikani tena?” akawaza Sarah huku akiangaza angaza na mara akawaona Patrick na Savanna wakiingia katika gari lao la kifahari wakaondoka pale mahakamani..Sarah akahisi kama nywele zinamsisimka.Alitamani awakimbilie na kumuonya Patrick kuhusu taarifa za kuwepo kwa mpango wa kumuua lakini akaogopa kwa kuwa hakuwa bado na ushahidi wa kutosha wa jambo hilo.Mtu pekee ambaye angeweza kulithibitisha hilo alikuwa ni Linah .
“Natamani nimweleze Patrick kuhusiana na mambo aliyonieleza Linah lakini naogopa.Linah yuko wapi ? akawaza Sarah na mara simu yake ikaita.Alikuwa ni shangazi yake.Sarah akaguna kidogo halafu akaipokea
“Hallow shangazi”
“Sarah uko wapi?
“Niko bado hapa mahakamani”
“Sarah njoo nyumbani mara moja.Hali ya mama yako si nzuri hata kidgo.Mtaarifu na Loniki kama utamuona kwa sababu ninajaribu kumpigia simu lakini simu yake haipatikani.Ulimuona mahakamani leo?
“Hapana sikumuona mahakamani na sina hakika kama alikuja”
“Hata mimi sikumuona sijui yuko wapi.Fanya haraka uje nyumbani” akasema shangazi yake Sarah.
“Sawa shangazi ninakuja sasa hivi” akasema Sarah na kwa haraka akaelekea katika gari lake.

* * * *

Savanna alikuwa anaendesha gari huku machozi yakimtoka
“Unalia nini malaika wangu? Akauliza Patrick
“Patrick machozi haya ya furaha yanatoka yenyewe na hasa nikikumbuka kazi kubwa iliyofanyika.To be honest haikuwa kesi rahisi.Ni moja kati ya kesi ambazo zimewahi kuniumiza kichwa change mno.Thanx God its over” akasema Savanna
“Savanna nina deni kubwa sana kwako na wale wote ambao mmepigana kufa na kupona kuhakikisha kwamba ninakuwa huru tena.Savanna umepambana vilivyo.Sioni kitu cha kukulipa mpenzi wangu.” Akasema Patrick
“Patrick ninaombi moja tu kwako”
“Omba chochote Savanna.”
“Katika watu ambao utawashukuru,usisaha kumshukuru pia Happy.Alifanya jambo kubwa sana..Ushahidi wake ulichangia sana kuipa nguvu hoja ya yetu na kuishawishi mahakama kukuacha huru”
Mara tu Savanna alipolitaja jina la Happy mara moja Patrick akakumbuka kitu.wakati akiwa wamekumbatiana Happy aliweka kitu fulani katika mfuko wake wa koti.Akaingiza mkono mfukoni na kutoa kikaratasi kidogo
“Whats that? Akauliza Savanna
“Ni karatasi Happy aliiweka mfukoni “akasema Patrick halafu akaikunjua karatasi ile na kuisoma.
Kwako Patrick
Nina kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa siku ya leo.Ninafuraha kubwa nisiyoweza kuielezea.Nashukuru mahakama kwa maamuzi yake.Namshukuru sana Savanna kwa kupambana hadi umeachiwa huru.
Patrick nimeamua kukuandikia maneno haya machache kwa sababu sintapata tena nafasi ya kuongea nawe ana kwa ana.This might be our last contact.Maneno machache ninayotaka kukueleza ni kwamba Patrick you are a great man.I’m proud of you.Ninafuraha kukutana na mtu kama wewe katika maisha yangu.
Patrick you saved me.You saved my life.Ninashukuru sana kwa upendo wako usioelezeka wala kupimika.Sina kitu cha kukulipa kwa wema ulionitendea na upendo ulionionyesha toka tulipoonana na kufahamiana.Ninaapa kwamba hatatokea mwanaume ambaye atanionyesha upendo kama ulinionyesha wewe .Nitakuombea siku zote kwa Mungu ili uwe na furaha katika maisha yako.I know Savanna will take a good care of you.You deserve someone better than me,you deserve her.
Patrick we had lots of dreams togeth.I want you to fullfil all the dreams we had.Get married to Savanna and you live a good and Happy life.
Mwisho kabisa ninaomba toka ndani ya moyo wako unisamehe kwa makosa yote niliyokukosea.
I will always miss you
Kiss and goodbye
Happy

Alimaliza kuisoma barua ile na kuirudia tena kwa mara ya pili halafu akaikunja na kuiweka mfukoni
“Anasemaje Happy? Akauliza Savanna.Patrick hakujibu kitu akaitoa barua ile na kumpatia
“utasoma mwenyewe alichokiandika”
Savanna hakuisoma barua ile kwa kuwa alikuwa anaendesha gari akaiweka pembeni kwa lengo la kuisoma baadae

TUKUTANE SEHEMU IJAYO........
 
Jamani mbona mwanzo story haileweki ilivyo wekwa inaeleweka kuanzia 41 hizo za nyuma yake zipo wapi sasa
 
Kawawa hii kitu noma aisee duh cjui ushalala mkuu utupie moja maana hii bastora ya Lony inanipa shida kwelikweli
 
MISS TANZANIA
SEHEMU YA 60
MTUNZI: PATRICK.CK
CONTACT:0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Alimaliza kuisoma barua ile na kuirudia tena kwa mara ya pili halafu akaikunja na kuiweka mfukoni
“Anasemaje Happy? Akauliza Savanna.Patrick hakujibu kitu akaitoa barua ile na kumpatia
“utasoma mwenyewe alichokiandika”
Savanna hakuisoma barua ile kwa kuwa alikuwa anaendesha gari akaiweka pembeni kwa lengo la kuisoma baadae

ENDELEA……………..

Toka mahakamani Patrick na Loniki wakaelekea moja kwa moja makaburini ambako Patrick alitaka kuweka maua katika kaburi la Vero .Waliegesha gari na kushuka wakaelekea lilipo kaburi la Vero.Akiwa na maua mkononi,Patrick akasimama mbele ya kaburi la Vero.Akalitazama kaburi lile kwa makini halafu akapiga magoti na kuyaweka maua aliyokuja nayo.
Savanna alijisogeza pembeni na kumuacha Patrick peke yake pale kaburini
“He needs to be alone” akawaza Savanna na kusogea pembeni
Wakati Patrick akiwa amepiga magoti katika kaburi la Veronika,gari walilokuwamo Linah na Loniki nalo likawasili.Walikuwa wakiwafuata kwa nyuma akina Patrick.Loniki akaitoa bastora yake akaishika mkononi
“Stay in the car” akasema Loniki na kuufungua mlango lakini kabla hajashusha mguu chini akasikia sauti za watu wakiimba wakielekea kule makaburini
“Whats that ? You hear something? Akauliza Loniki
“Nasikia kama sauti za nyimbo” akajibu Linah mara ukatokea msafara wa watu waliokuwa wanakuja kuzika
“ouh gosh !! akasema Loniki kwa ghadhabu
“Mpango wote umeharibika”
“Damn ..!!!..akazidi kulalama Loniki.Msafara ule wa magari ukazidi kukaribia ,Loniki akafunga mlango wa gari.
Sauti zile za watu wakiimba zikamstua pia Patrick,akasitisha maombi yake na kuinuka
“Twende tuondoke Savanna” akasema Patrick wakaingia katika gari laona kuondoka pale makaburini.Loniki na Linah wakaendela kuwafuatilia kwa nyuma
“ Kama si watu hawa kunivuruga ningemtundika risasi Patick juu ya kaburi la mdogo wangu.Ana bahati sana lakini kabla jua halijazama jioni ya leo lazima niitoe roho yake” akasema Lonki.Linah hakujibu kitu alikuwa anatetemeka kwa ndani.Hakujua angewezaje kumuokoa Patrick kwani Loniki alikwisha dhamiria kufanya mauaji
Toka makaburini Patrick na Savanna wakaelekea moja kwa moja nyumbani .Patrick alikuwa na kazi kubwa ya kupokea simu nyingi nyingi za pongezi toka kwa watu mbalimbali kwa kesi ile kumalizika
“Itanichukua siku nzima ya leo kupokea salamu mbali mbali toka kwa watu.Nimefarijika sana kwa pongezi na pole nyingi toka kwa watu mbalimbali” akasema Patrick kwa furaha
“Bado pongezi zangu mimi” akasema Savanna na wote wakacheka .Waliendelea na safari yao bila kufahamu kwamba walikuwa wanafuatiliwa na akina Loniki
Walifika nyumbani kwao na kusimamisha gari nje ya geti wakisubiri geti lifunguliwe.
“Nahisi wamekuja nyumbani kwao.This is the time” akasema Loniki
Linah akasimamisha gari nyuma ya gari la akina Patrick waliokuwa wanasubiri kufunguliwa geti.
“Wait for me here.Dont do anything stupid to ruin my plan.” akasema Loniki halafu akaichukua bastora yake akaificha kiunoni na kuchomoa funguo ya gari akashuka.Akapiga hatua chache na kulifikia gari la akina Patrick.Akagonga kioo cha mbele upande aliokaa Patrick ambaye aligeuza kichwa na kupatwa na mstuko mkubwa.Aliitambua sura ya mtu aliyekuwa amesimama nje ya gari.
“Loniki ..!!! akasema Patrick kwa mshangao.Hakuwa ametegemea kumuona Loniki sehemu ile na kwa wakati ule.Ni muda mrefu hajawahi kuonana na Loniki.Savanna naye akageuka na kumtazama Loniki.Mara moja akaikumbuka sura ile.Alikumbuka kuiona sura ile katika msiba wa Vero.
“What is she doing here ? akajiuliza Loniki.
Patrick akafungua mlango wa gari na kushuka huku sura yake ikionyesha wasi wasi
“Hallow Patrick.How are you? Ite been a while “ akasema Loniki huku akilazimisha kutabasamu
“Kweli ni muda mrefu sana hatujaonana Loniki.Karibu sana” akasema Patrick.
Geti lilifunguliwa na Savanna akaliingiza gari ndani.Alipatwa na wasi wasi mwingi kuhusiana na ujio ule wa ghafla wa Loniki
“Karibu ndani Loniki” akasema Patrick na kumuongoza Loniki kuelekea ndani
“Ahsante sana” akajibu Loniki na kumfuata Patrick kuelekea ndani
“wow ! Patrick una nyumba nzuri sana.Hongera” akasema Loniki
“ahsante sana “ akajibu Patrick.Bado aliendelea kuwa na wasi wasi kuhusiana na ujio ule wa ghafla wa Loniki
“Hallow I’m Savanna” Savanna akamsalimu Loniki
“Ouh I’m glad to meet you Savanna.You are Patrick’s lawyer right?
“Yes ! “ akajibu Savanna
“Naitwa Loniki.Ni dada wa Veronika.Nimepita hapa mara moja kuwasalimu na kutoa pongezi zangu kwa Patrick na kuongea naye machache ili tuyamalize yaliyopita na tuanze maisha mapya.” Akasema Loniki na kumfanya Patrick atabasamu
Mara tu alipohakikisha kwamba Loniki ameingia ndani na akina Patrick,Linah akachukua simu yake akaiwasha na kuzitafuta namba za simu za Sarah
“ouh my God naomba nimpate Sarah.” Akawaza Linah huku akibonyeza kitufe cha kupigia simu na simu ikaanza kuita.Iliita mara ya kwanza na kukatika bila kupokelewa. Akapiga tena
“Ouh C’mon Sarah pick up the phone” akasema Linah na mara simu ikapokelewa.
“Hallow Linah.Umepotelea wapi?Nimekutafuta mahakamani sijakuona.Nini kinaendelea ? Mbona hatujawasiliana tena?
Huku akihema kwa nguvu Linah akasema
“Sikiliza Sarah hatuna muda wa kupoteza tena.Loniki yuko hapa nyumbani anakoishi Patrick na Savanna.Ana bastora ameificha na akina Patrick hawajui chochote.She’s going to kill Patrick.Tafadhali fanya kila unaloweza ufike hapa mara moja ila nakuomba tafadhali usipite polisi.Ukija na polisi mambo yanaweza kuwa mabaya zaidi.Tafadhali Sarah fanya haraka” akasema Lnah
“Ouh Mungu wangu ! hebu nielekeze mahala nyumba hiyo ilipo” akasema Sarah huku mwili ukimtetemeka.Linah akamuelekeza mahala nyumba ya Savanna ilipo
“Ahsante Linah nakuja sasa hivi.Na wewe unafanya nini hapo? Kwanini usikimbie kuyanusuru maisha yako?
“Natamani sana nikimbie lakini funguo ya gari anayo yeye na amenifungia ndani ya gari”
“C’mon Linah fanya unavyoweza na uondoke humo ndani ya gari.Lazima Loniki atakuua tu.”
“Siwezi kuondoka Sarah.Nataka nijue kila kinachoendelea hapa.” Akasema Linah
“Sawa Linah ninakuja hapo sasa hivi” akajibu Saraha na kukata simu.Akageuza gari na kuanza safari ya kuelekea mahala alikoelekezwa
Akiwa njiani kuelekea nyumbani kwa Savanna akachukua simu na kumpigia shangazi yake
“Shangazi naomba unisikilize vizuri.Muda huu Loniki yuko nyumbani kwa Patrick .Amekwenda kwa lengo la kumuua na sekunde yoyote kuanzia sasa anaweza akafanya hivyo.Ana bastora ameificha .Shangazi tunatakiwa tumzuie asifanye unyama huo anaotaka kuufanya”
“Hebu nielekeze mahala huko aliko Loniki,mbona anataka kutuletea matatizo mengine makubwa? Akasema shangazi yake kwa mstuko
Sarah akamuelekeza shangazi yake mahala nyumba ya Savanna ilipo.Mara tu alipomaliza kuongea na Sarah simuni mama yake Loniki ambaye alikuwa pembeni yake akamkazia macho na kumuuliza
“Nini kimetokea? Kuna tatizo gani?
“Loniki amekwenda nyumbani kwa Patrick .Anataka kumuua ana bastora”
Mama yake akastuka na kupata nguvu za ghafla akainuka na kuelekea chumbani kwake akafungua kabati lake kubwa la nguo na mara moyo wake ukaanza kwenda mbio
“Ouh Mungu wangu ! Loniki amechukua bastora iliyokuwa humu”
Baada ya kuongea na shangazi yake,Sarah akazitafuta namba za simu za Alois na kumpigia akamfahamisha juu ya tukio hilo
“Please Alois we have to save Patrick.Loniki ana silaha na muda wowote anaweza akamuua ” akasisitiza Sarah
“Sarah nakuja huko sasa hivi” akajibu Alois

* * * *

“Habari za siku nyingi Loniki? Akasema Patrick
“habari nzuri Patrick.Ni muda mrefu sana hatujaonana.Nimerudi juzi na kilichonirudisha ni kuhudhuria siku ya leo”.akasema Loniki halafu kimya kifupi kikatanda
“Patrick mimi si mkaaji sana.Nimeona kabla sijarudi London nipite hapa nikusalimu na kukupa pole kwa matatizo yaliyokupata.Pamoja na hayo….” Lonik akainuka na kuwatazama Patrick na Savanna
“Pamoja na hayo nimekuja pia kukuaga Patrick”
“Are you leaving so soon? Akauliza Patrick
“Yah ! soon I’ll be going but today its you who is going.Patrick I’vecome to kill you” akasema Loniki na kwa kasi ya aina yake akatoa bastora yake na kuwalenga Patrick na Savanna
“Loniki ..!! Unafanya nini? Akauliza Patrick kwa mstuko
“shut up !! akafoka Loniki kwa ukali
Patrick na Savanna wakaangaliana kwa woga.Wote walikuwa wanatetemeka .Macho ya Loniki hayakuonyesha masihara hata kidogo.
“Ouh Mungu wangu mambo gani haya yananitokea? Please help me God.Ee Mungu umekuwa unaniokoa katika kila ovu,naomba usiniache katika hili pia.” Patrick akaomba kimoyo moyo huku mwili ukitetemeka
Mara mtumishi wa ndani akaingia pale sebuleni kwa kasi na sinia la vinywaji bila kujua kilichokuwa kinaendelea,ghafla akastuka baada ya kumuona Loniki amewaelekezea Patrick na Savanna bastora ,sinia la vinywaji likamponyoka na kuanguka chini.Loniki akamgeukia
“Ukijaribu kukimbia nakupiga risasi.Kaa pale na ufanye vile nitakavyokuamuru” Loniki akamwambia kwa ukali yule mtumishi wa ndani ambaye alikuwa anatetemeka.
“Pigeni magoti wote” akaamuru Loniki.
“Loniki please don’t kill us.Nitakupa kiasi chochote cha pesa unachohitaji ….!! “ akasema Savanna huku akitetemeka .Machozi mengi yalikuwa yanamtoka
“Shut up !!..akafoka Loniki na kumtazama Yule mfanyakazi wa ndani
“wewe ! Kata ule waya wa umeme na uwafunge hawa mikono kwa nyuma.!! Loniki akamuamuru yule mfanyakazi ambaye kwa woga aliokuwa nao aliitekeleza amri ile kwa haraka.Akawafunga Patrick na Savanna mikono kwa nyuma kwa kutumia waya
“Loniki tafadali naomba usitudhuru.Tumekukosea kitu gani hadi utufanye hivi?” akaomba Patrick.Kauli ile ikaonyesha uzidi kumpandisha hasira Loniki
“Huna haya mshenzi wewe.Ulimuua mdogo wangu bila kosa.Niliapa kulipa kisasi kwa wale wote walioukatili uhai wa mdogo wangu.I loved her so much.Ni kwa sababu ya mapenzi yangu kwake ndiyo maana niliweka ahadi ya kulipa kisasi.Kifo chake kiliniuma sana.How could you kill her like that? Don’t you have a soul you bastard? She loved you with all her heart and in return you killed her.I cant let you walk again.Ndani ya sekunde kadhaa zijazo utaungana naye mbele za haki mshenzi wewe” akasema Loniki na kumtemea Patrick mate usoni.
“Loniki Patrick hakufanya lolote.Hakumua Veronika.Ngoja nkwambie ukw……” akasema Savanna lakini kabla hajamaliza sentensi yake ukasikika mlio wa risasi.Wote wakaanguka na kulala chini.Taratibu Patrick akafumbua macho ,pembeni yake alikuwa amelala Savanna na damu nyingi zikimtoka
“Savanna !! Savanna !! Savannaaaaa..!!!!! “ akaita Patrick huku akilia
“Hiyo ndiyo adhabu yako kuku wewe.Wewe ndiye uliyeishawishi Mahakama imuachie huru huyu mshenzi.Hii ndiyo hukumu yako” akasema Loniki huku akiusogelea mwili wa Savanna pale chini na kuupiga teke.Patrick alikuwa amelala sakafuni mikono yake imefungwa kwa nyuma hivyo hakuweza kufanya lolote.Pembeni yake mwanamke aliyempenda sana alikuwa amelalia dimbwi la damu.
“shetani wewe !! how could you do this? I’m going to kill you !! “ Patrick akasema ghadhabu.
“Usihofu Patrick.In few minutes you’ll join her” akasema Loniki
Mlio ule wa risasi ulimstua sana Linah aliyekuwa amefungiwa garini
“Ouh Mungu wangu tayari Lonny amemuua Patrick” akasema Linah na kuchukua simu yake akampigia Sarah
“Saraha umefika wapi?
“Tayari nimefika maeneo haya.Ndani ya dakika moja nitakuwa nimewasili hapo nyumbani”
“Hurry up ! Tayari risasi moja imelia ndani”
“Ouh my God ! ..akasema Sarah na kuongeza mwendo wa gari.Mikono yake ilikuwa inamtetemeka.
“Nilisikia uchungu sana kwa kifo cha Vero.Hakuna mtu niliyempenda kama yeye.Nataka ukamjibu ni kwa nini ulimsaliti? Kabla hujamuua aliumia sana moyo wake kwa usaliti uliomfanyia. Mateso na maumivu ya moyo aliyoyapata siku ile nataka uyapate nawe leo hii. You’ll die in agony ..! akasema Loniki
“Lonny ..!! Unafanya nini? Akasema kwa sauti Sarah.Loniki akastuka mno baada ya kumuona Sarah pale.Hasira zikampanda mara dufu
“Lonny please ! naomba tafadhali usimuue Patrick..Dont……!!!! akasema Sarah lakini Loniki akamkatisha
“imekuwa vizuri umekuja mwenyewe ushuhudie namna ninavyo mlipia Vero kisasi.Nataka ushuhudie namna Patrick anavyokufa kwa maumivu” akasema Loniki kwa hasira huku mkono wake ukimtetemeka.
“Loniki tafadhali usimuue Patrick.Please I beg you my sister don’t do that..!!! akaomba Sarah huku akipiga magoti
“Sarah sikutambui tena kama ndugu yangu.I don’t know you anymore.Kwa kitendo chako cha kushirikiana na huyu nguruwe wewe si ndugu yangu.Nakukana duniani na ahera.Nina kuchukia sana na baada ya Patrick itakuwa ni zamu yako wewe na Linah…She betrayed me…!!!!
Bila kusita Loniki akaachia risasi kumuelekea Patrick akaanguka chini pembeni ya Savanna.Mlio ule wa risasi ukawastua Linah na Sarah ambao walianguka chini.Baada ya sekunde kadhaa Sarah aliyekuwa anatetemeka mwili akainua kichwa.Hakuamini alichokiona.Patrick alikuwa ameanguka pembeni ya Savanna akiwa katika dimbwi la damu
“Ouh Mungu wangu ..Lonny umemuua Patrick.Umemuua Patrick.Lonny !!! “ akapiga ukelele Sarah na kuinuka akaanza kupiga hatua kumfuata Loniki.
“Sarah simama hapo hapo,usipige hata hatua moja.” Akasema Loniki kwa ukali
“Are you going to shoot me? Akasema Sarah huku akitembea kumuendea Loniki
“Sarah tafadhali naomba usipige hatua hata moja.I’ll shoot you..!!!!! akasema Loniki kwa ukali
“Sarah usijaribu kumsogelea atakupiga risasi ,anamaanisha anachokisema“ Linah aliyekuwa amejibanza pembeni ya mlango akamuonya Sarah
“Shoot me Lonny.Kama mimi si ndugu yako nipige risasi” akasema Sarah huku akipiga hatua kumuendea Patrick aliyekuwa amelala pale sakafuni
“Sarah don’t force me to kill you.Stay where you are” akasema tena Loniki kwa ukali
“Shoot me ..!!! akasema Sarah huku akiunyanyua mguu wake lakini kabla hajaushusha chini ukasikia tena mlio wa risasi.Sarah akaanguka chini.Alikuwa anavuja damu nyingi.Loniki akaushusha chini mkono wake uliokuwa na bastora.Alikuwa anatetemeka
“gosh !! nimemuua ndugu yangu..!! akasema Loniki na kuitupa chini bastora yake akamkimbilia Sarah aliyekuwa amelala chini damu nyingi ikimtoka
“Sarah..! Sarah..!!! Saraaaahhhh….!! Akaita Loniki kwa sauti kubwa huku akilia.Alimuinua mdogo wake na kumuweka magotini pake huku akilia kwa nguvu.
“Sarah !’m sorry ..!!!..I’m sorry sarah ..!! …Please forgive me ..!! ..Loniki aliendelea kulia kwa nguvu.Pembeni ya mlango Linah alikuwa ameanguka na kuzirai
Mara katika mlango mkubwa wa sebuleni akaingia Aloisi akiwa ameongozana na askari waliokuwa wamevalia fulana za kujikinga na risasi.Sebule yote ilikuwa imetapakaa damu.Watu watatu walikuwa wamelalia damu.Loniki bado aliendelea kulia kwa nguvu.Askari polisi wakaiokota bastora ile ya Loniki aliyokuwa ameitupa pembeni.
Magari mawili ya wagonjwa yakafika haraka sana .Patrick,Savanna,Sarah,Linah na msichana wa kazi wakapakiwa katika magari na kukimbizwa hospitali.Eneo lote lilitawaliwa na vilio wakati miili inatolewa ndani.Loniki alionekana kama mtu aliyechanganyikiwa.Alikuwa anaongea maneno mfululizo yasiyoeleweka.Polisi walifanya uchunguzi wao wa kina ndani ya ile nyumba na wakiwa katika harakati za uchunguzi mara akawasili mama yake Loniki lakini mara tu alipokutana na umati mkubwa wa watu pale nje akaanguka na kupoteza fahamu.
Baada ya kukamlisha uchunghuzi wao askari polisi wakaondoak na Loniki ambaye bado alionean kama my aliyechanganyikiwa.

* * * *

St Patrick hospital moja ya hospitali kubwa na mpya jijini Dar ambayo hivi karibuni serikali imeitangaza kuwa hospitali ya rufaa iligeuka uwanja wa heka heka baada ya majeruhi wa shambulio la risasi kufikishwa pale hospitalini.Haraka haraka walikimbiza katika chumba cha wagonjwa mahututi kwa ajili ya kuokoa maisha yao.Madaktari wote mabingwa wa upasuaji wakaitwa mara moja ili kuongeza nguvu katika kuokoa maisha ya majeruhi wale.
Vipimo vya awali vilibaini kwamba Savanna tayari amekwisha fariki dunia kabla ya kufikishwa pale hospitali.Patrick na Sarah ambao walionekana kuwa hai wakakimbizwa katika chumba cha upasuaji kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji wa dharura.Katika chumba kingine cha wagonjwa wa dharura ,Linah na mfanyakazi wa ndani wa Savanna walikuwa wanaendelea vizuri baada ya kuzimia kutokana na mstuko walioupata.Tayari walikuwa chini ya uangalizi wa polisi kwani ni watu pekee ambao walilishuhudia tukio zima lilivyotokea.
Taarifa za kutokea shambulio la risasi nyumbani kwa wakili maarufu Savanna Francis Kito zilisambaa kwa kasi na kusababisha idadi kubwa ya watu kumiminika St Patrick hospital ili kuhakikisha kuhusu taarifa hizo.Walinzi waliokuwepo getini walizuia watu kuingia hospitalini hapo isipokuwa wale wagonjwa wa dharura
Alois akiwa njiani kuelekea hospitali alipatwa na wazo la kuwapigia nyumbani kwao na kuwafahamisha kilichotokea.Akapunguza mwendo wa gari na kumpigia simu mama yake.
“Hallo Alois mbona umeondoka ghafla na hujaniaga unaelekea wapi?Tunahitaji chupa tatu za shampeni pamoja na bia za kopo.Naomba wakati unarudi ununue vitu hivyo uje navyo.” Akasema mama yale.Alois akavuta pumzi ndefu na kufikiri kwa muda
“Alois umesikia “ akauliza tena mama yake
“mama .!! akaita Alois
“Nini Alois? Kama hutaweza niambie ili nimtume mtu mwingne”
“Si hivyo ,mama ila kuna tatizo limetokea”
“Tatizo gani tena?
“mama hakutakuwa na sherehe yoyote tena” akasema Alois
“Alois mbona unanistua? Kwa nini kusiwe na sherehe?
“Patrick amepatwa na matatizo”
“matatizo ?? mama yake akashangaa
“Ndiyo mama”
“Matatizo gani? Akauliza mama yake kwa wasi wasi.Alois akavuta pumzi ndefu na kusema
“Patrick amepigwa risasi….”
“Ouh Mun………..” kabla hajamliza sentensi yake akaanguka ghafla na kupoteza fahamu
“mama .!! mama..!! mama..!!!!’ akaita Alois lakini hakujibiwa.Akaogopa na kukata simu akampigia mke wake akamuomba amuangalie mama yake.
“mama ameanguka ghafla na amepoteza fahamu.Hatujui tatizo ni nini lakini alionekana alikuwa anaongea na simu kwani simu yake imeanguka pembeni na imesambaratika.Uko wapi Alois? Akasema Sesilia mke wa Alois
“Sikiliza mke wangu” akasema alois
“Kuanzia sasa hivi sitisheni shughuli zote kuhusiana na sherehe mliyokuwa mnaiandaa.Hakutakuwa na sherehe tena.Kitu kingine nakuomba uendeshe gari na mumpeleke mama haraka katika hospitali ya karibu kwa Dr Khan ili apatiwe matibabu ya haraka”
“Alois wewe uko wapi? Akauliza Sesi kwa wasi wasi
“Siwezi kuja huko nyumbani sasa hivi.Kuna jambo limetokea nitakutaarifu baadae.Ukishafika hospitali tafadhali nipigie simu” akasema Alois na kukata simu.Mwili bado uliendelea kumtetemeka
“Mambo gani haya yanatupata katika familia yetu? Hata kabla machungu ya kuondokewa na baba hayajapoa ,tunapatwa na tatizo lingine.Ouh Mungu naomba umponye Patrick.Tafadhali usimchukue kwa wakati huu” akaomba Alois.
Mara tu alipofika hospitali alijitambulisha mapokezi na kuomba kuonana na daktari ili aweze kupatiwa taarifa za maendeleo ya mgonjwa wake lakini alitaarifiwa kwamba kwa muda ule asingeweza kumuona daktari kwa kuwa walikuwa katika chumba cha upasuaji wakijaribu kuokoa maisha ya Patrick na Sarah.Alois akapelekwa katika sehemu ya mapumziko katika ofisi ya mganga mkuu akimsubiri amalize upasuaji .Akiwa amepumzika katika sofa jeusi lililokuwa nje ya ofisi ya mganga mkuu simu yake ikaita.Alikuwa ni mke wake.
“Hallow Secy .Tayari mmefika hospitali?
“Ndiyo Alois tumefika lakini kuna tatizo lingine limejitokeza.Dr Khan amempima akagundua kwamba tatizo la mama ni zaidi ya kupoteza fahamu kwa hiyo ametuandikia tumpeleke katika hospitali ya rufaa ya jeshi pale wana wataalamu wazuri na vifaa na wanaweza wakabaini kwa haraka tatizo la mama.Hivi sasa tuko njiani tunaelekea huko hospitali”
“Ouh Mungu wangu ! kwa hiyo Dr Khan hajasema lolote kwamba linaweza kuwa ni tatizo gani?
“Hapana hajasema lolote isipokuwa ametuandikia makaratasi ya kwenda nayo huko na sijui kaandika nini”
“Unaionaje hali ya mama?
“hali yake haina mabadiliko yoyote”
“Uko na nani hapo karibu?
“Niko na ndugu wengine hapa .Wewe uko wapi? Njoo Alois hali hii mimi inaniogopesha sana” akasema Secilia
“Sesilia naomba uwe na ujasiri hasa kwa wakati huu .Mimi nitakuja lakini kwa sasa niko sehemu fulani.Ukifika hospitali nitaarifu kuna jambo nitakuelezea lakini nataka wakati uko peke yako”
“Alois nini kinaendelea?”
“Nitakwambia baadae.Ukifika hospitali nijulishe” akasema Alois na kukata simu.Jasho lilikuwa linamtiririka

TUKUTANE SEHEMU IJAYO.......
 
Kawawa ubalikiwe ila shusha mbili maana nipo kwenye foleni apa mbezi magari hayasogei
 
Kawawa na lege wanaendana kiukweli washkaji hawa tabia za kiswahili wanashusha vitu on time inawezekana kawawa hajafika hom
 
Back
Top Bottom