MWINDAJI HARAMU
JF-Expert Member
- Dec 21, 2013
- 211
- 295
Bilaliiiii, shukran Chief
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] nyonga mkalia ini wangu,unajua nakupenda eehKwanini unanitesa hivi.!? Unapata furaha gani kuona mapigo yangu ya moyo yakiwa hovyo hovyo..!?
Nimeshawakuta kitamboo,sasa tunaenda sawa sawaUsijali, natumaini utatukuta wala hatujafika...
haya baba to... ****m*****ba sasaLaiti Ningejua! 25
Mtunzi Bishop Hiluka
“Unataka kuniambia hujaoa hadi sasa?” Rehema aliniuliza huku akinitazama kwa udadisi.
“Sijabahatika,” nilimjibu kwa sauti tulivu.
“Kwa nini?”
“Kwa sababu Mungu bado hajanijaalia”
“Na wala huna girlfriend?”
“Ninaye!” nilijibu huku nikimkazia macho Rehema, nikamuona kashtuka kidogo ingawa hakutaka kuuonesha mshtuko wake.
“Sasa… kama una girlfriend nini tatizo hadi uanze kutanga tanga?”
“Wala sijatanga tanga kwani leo ndiyo mara ya kwanza naongea naye na hajui ni kiasi gani nampenda. Girlfriend wangu ni wewe Rehema!”
Endelea...
Rehema akataka kusema neno lakini nikamuona akisita. Aliyakwepa macho yangu yaliyokuwa yakimtazama kwa makini na kuangalia kando, kisha akashusha pumzi za ndani kwa ndani.
“Jambo unalohitaji kwangu ni jambo linalohusu maisha… yangu na yako vilevile, kwa hiyo halihitaji uamuzi wa papara,” alisema Rehema na alionekana kumaanisha kile alichokisema na kuendelea.
“Nahitaji muda wa kutafakari zaidi, nahitaji kukufahamu zaidi na kuufahamu ukoo wako kabla sijakubali au kukataa proposal yako. Najua hata wewe hunifahamu vya kutosha…”
“Ni kweli,” nilikubaliana na maneno yake ingawa moyoni sikuona sababu ya kuanza kuchunguzana wakati nilijua kabisa sitaweza kumuoa bali nilitaka kushiriki tendo tu na kumwacha kama wengine.
“Samahani, hivi wewe mwenzangu ni mzaliwa wa wapi?” nilijikuta nikimtupia swali.
“Kigoma.”
“Kigoma?” Nilimaka kwa mshangao huku nikiachia kinywa changu wazi.
“Ndiyo Kigoma… mbona umeshtuka?”
“Wewe ni kabila gani?” Nilimuuliza tena huku nikimkazia macho.
“Mmanyema, kwani vipi?”
“Ni mshtuko wa furaha kwa kuwa imeniongezea sifa nyingine nisiyoitegemea kwako wewe!”
“Sifa gani hiyo?”
“Wewe ni msichana wa kwetu, mimi pia kwetu ni Kigoma, mimi pia ni Mmanyema. Huwezi kujua, nimefurahi mno, Rehema!” nilisema huku nikihisi msisimko na ubaridi ukinitambaa mwilini mwangu.
Rehema alitabasamu tu bila kusema neno. Nikataka kusema neno lakini nikasita baada ya kumuona Bi Aisha akiingia pale sebuleni na kuketi kwenye sofa, kisha kisha mazungumzo ya kawaida ya kufahamiana zaidi yakatawala maongezi yetu.
Niliaga ili niondoke lakini Bi Aisha hakuniruhusu, aliniomba nisubiri chakula nile ndipo niondoke. Kwa kweli yule mama alikuwa mcheshi na mzungumzaji mzuri. Nilipoondoka pale ilikuwa yapata saa kumi za alasiri na moja kwa moja nilirudi nyumbani nikiwa nimefarijika sana.
Zilipita siku tatu tangu siku nilipokwenda nyumbani kwa kina Rehema na kukutana na mama yake, Bi Aisha, katika siku hizo tatu nilikuwa nashughulikia kongamano maalumu la kibiashara ambalo niliamini kuwa niliamini lingetengeneza fedha nyingi ambazo hatimaye zingenipa heshima zaidi mbele ya Rehema.
Siku ya nne nilikutana na Rehema na aliomba anitembelee nyumbani ninapoishi ili apafahamu. Sikupinga, nilimchukua hadi nyumbani na kumkaribisha ndani.
”Hapa ndipo ninapoishi, Rehema,” nilisema mara tu Rehema alipoingia ndani kwangu. “Ni padogo sana, lakini uwezo wangu ndipo ulipoishia.”
“Una maana gani?” Rehema aliniuliza huku kanikazia macho yake. Japokuwa nilishikwa na haya, lakini nilimudu kuunda tabasamu.
“Nyumba hii ni ndogo tofauti na ile ya kwenu, japo ninatamani sana kuishi maisha ya juu lakini siwezi kuishi kama mkurugenzi, ndiyo maana yangu,” nilisema na kushusha pumzi.
“Pia hii ni nyumba ya familia ambayo tumeachiwa mimi na brother wangu ambaye kwa sasa yupo South Africa. Nina hiki chumba kimoja na sebule, vyumba vingine tumepangisha,” nilizidi kujitetea mbele ya Rehema.
“Kupanga ni kuchagua, na sidhani kama huwezi kuishi kama hao wengine wakati wewe pia umesoma na huna kasoro yoyote!” alisema Rehema huku akiniangalia kwa makini.
“Ni kweli,” niliafiki. “Ila itabidi uvumilie tu maana pana joto kidogo, ila kwa huu mji wetu hilo si jambo la kushangaza.”
“Usijali…” alisema huku akiketi juu ya kochi dogo la sofa pale sebuleni kwangu. Kikakipita kimya cha kitambo kifupi.
“Kwani wazazi wako wapo wapi?” Rehema alinishtua kwa swali lake.
“Wapo Kigoma, wanaishi Mwanga mtaa wa Lumumba,” nilimwambia.
Tuliongea mengi sana siku ile na Rehema aliamua kushinda pale kwangu. Aliniuliza maswali mengi kuhusu maisha yangu binafsi na maisha ya familia yangu, nami bila ajizi nilimjibu kila swali alilouliza kwani nilijua alichokuwa akikitafuta.
Pamoja na kuwa na wakati mzuri wa kuongea na kufurahi nilijaribu sana kumuonesha kuwa nilimhitaji kwa ajili ya kushiriki tendo lakini Rehema alionesha msimamo wa kutokuwa tayari, nami niliheshimu msimamo wake kwa kuogopa kuonekana nilikuwa na papara.
Siku ile ukawa ndiyo mwanzo wa kuwa karibu zaidi na Rehema. Baadaye tukawa tukiwasiliana sana kwa simu, lakini siku moja Rehema alikuja tena nyumbani kwangu ingawa safari ile alinishtukiza maana alikuja bila kunitaarifu kama angekuja.
Ilikuwa ni siku ya Jumamosi na alinikuta nikiwa nafanya usafi ndani kwangu. Aliniambia kuwa alikuwa anapita tu akaona si vibaya akishuka kunisalimia, nikamkaribisha ndani kwa bashasha.
Hakuonesha kukaa sana lakini nami sikutaka kuipoteza nafasi ile hivyo tukiwa katikati ya maongezi nikaanzisha tena mazungumzo yaliyohusu uhusiano.
“Unajua Rehema, sifurahii aina ya maisha ninayoishi, ni ajabu kwamba katika maisha ni vitu vichache kati ya unavyovitaka ambavyo unavipata, vingi huvipati!”
“Hebu niambie Bilali, ni vitu gani katika maisha yako ambavyo hujavipata?”
Niliinamisha uso wangu kidogo nikijifanya kutafakari ingawa kimsingi sikuwa natafakari chochote, kisha nikanyanyua uso kumtazama.
“Nashukuru Mungu nimesoma kiasi cha haja, nimehitimu digrii ya Biashara katika Masoko, nimefungua kampuni na kufanikiwa kuajiari watu kadhaa na ninapata mahitaji yangu yote muhimu, lakini bado zipo haja nyingine zilizomo ndani ya nafsi yangu ninashindwa kuzipata!”
Rehema akacheka kidogo. “Kama zipi hizo?”
“Upendo…” nilijibu huku nikimtazama kwa makini.
“Unataka kuniambia kuwa familia yako hawakupendi?” Rehema aliniuliza huku akinitazama kwa mshangao.
“Familia inanipenda, lakini pendo ninalozungumzia hapa, ni lile ambalo ni tofauti na la baba, mama, dada au kaka!” nilisema huku nikiachia kicheko hafifu.
Rehema aliguna na kuangalia kando akijaribu kuyakwepa macho yangu, hata nilipojaribu kumchunguza sikuiona tashwishwi usoni kwake. Kisha nikamuona akiinuka kisha akaaga na kuanza kuondoka.
“Keti kwanza,” nilimwambia Rehema huku nikimzuia asiondoke.
Rehema alinitazama kwa makini kwa kitambo kisha alitii na kurudi kuketi kwenye kochi. Akabaki akinitumbulia macho.
Nilivuta pumzi ndefu na kuzishusha taratibu huku nikiuma midomo yangu, nikajifanya nafikiria kidogo kisha nikamkabili Rehema kwa sauti tulivu.
Itaendelea...
Cc the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk, marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, Mine eyes, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY
khaaaa wee nae hawavumi lakini wamoAhsante sana Bishop...
Bilal kazingua sana kwa Rehema, kakosa uvumilivu.. Angeenda nae taratibu mwisho wa siku angetunukiwa papuchi..
Nilishawahi kuifuatilia papuchi miaka mitatu, nikiwa nae najidai nauhitaji wa papuchi... Kumbe namchora tuu, pembeni nakula hivo visimi hatari...
Ahsante Bishop nimeishafikaLaiti Ningejua! 29
Mtunzi Bishop Hiluka
“Ukweli ni kwamba, unajua mimi ni bachela na wewe tayari una mtu na siku si nyingi mtafunga ndoa na kwenda kuishi Uarabuni…” nilisema huku nikimkazia macho. Jameela alinitazama kwa makini bila kusema neno.
“Hivi umejiuliza nitaishi vipi bila wewe au unadhani mimi sina wivu? Nimekubali matokeo na sioni sababu ya kuona wivu, kwa nini wewe ufanye hivi? Kumbuka umekuja tuagane, sasa kama kuagana kwenyewe ni kwa staili hii sawa, nakuruhusu uende,” nilisema kwa uchungu huku nikimpisha aondoke.
Jameela alinitazama kwa makini nikauona uso wake ukikunjuka na zile hasira zikaanza kuyeyuka, alishusha pumzi za ndani kwa ndani na kujipweteka juu ya kochi.
Endelea...
Nilimfuata pale kwenye kochi nikambembeleza na kuanza kuzitoa tena nguo zake na kuzitupa pale sakafuni moja baada ya nyingine hadi alipobakiwa na nguo ya ndani tu, kisha nikaanza tena kumpapasa.
“Bilali, nisamehe ni kwa kuwa nakupenda sana, unajua kuna wakati nafikiria kutoroka nyumbani, tutafute sehemu yoyote ambayo watu hawatujui tukaishi,” Jameela aliongea huku akinitazama machoni. Nikagundua kuwa alikuwa analengwa na machozi.
“Hata mimi ningetamani hivyo lakini…” nilishindwa kumalizia sentensi yangu baada ya kusikia muungurumo wa gari likifunga breki nje ya nyumba. Kumbe Jameela naye aliusikia ule muungurumo, tukatazamana.
“Rehema huyo karudi,” Jameela aliongea kwa sauti ya chini huku akinikazia macho kwa makini.
“Sidhani,” nilimjibu kwa wasiwasi huku nikijiuliza kama si yeye basi angekuwa nani?
“Na kama atakuwa ni yeye utafanyaje?” Jameela aliniuliza huku akiendelea kunitazama machoni kwa makini.
“Nitamtimua bila...” nilimjibu Jameela lakini sikuweza kumalizia sentensi yangu nikakatishwa na sauti ya mtu aliyekuwa anagonga mlango wangu kwa nguvu.
Aina ya ugongaji wa mlango ilinishtua kidogo, nikajiuliza ni nani aliyekuwa akigonga ule mlango. Mimi na Jameela tukatazamana katika hali ya kuulizana lakini hakuna aliyethubutu kuuliza. Ule mlango ukagongwa tena, lakini safari hii kwa nguvu zaidi.
Nilihisi donge la hasira likinikaba kooni kwangu, hasa nilipokumbuka kuwa huenda alikuwa ni Rehema aliamua kuja kunifanyia vurugu japokuwa alikuwa hataki kufanya ngono na mimi.
Niliinuka haraka nikiwa nimechukizwa na kuusogelea ule mlango nikiwa nina boksa tu tayari kwa kumkabili Rehema, nikaapa kuwa nitamfundisha adabu ili asisahau maishani mwake, nikashika kitasa cha mlango na kuufungua ule mlango huku nikiangalia nje kwa mategemeo ya kumuona Rehema akiwa kasimama mlangoni.
Nilichokiona kikanifanya kupigwa na butwaa, nilijikuta nikiganda kama sanamu nisijue nini nifanye. Adnan alikuwa amesimama nje ya mlango wangu akinitazama huku tabasamu pana la kirafiki likichanua usoni kwake.
Nilijikuta nashindwa kufanya lolote, nikabaki nimekodoa macho yangu kama nilikuwa nimeona mzuka au kitu cha kutisha, nilitamani ardhi ipasuke ili niingie ndani yake kuepuka aibu amabayo ingenikuta muda mfupi baadaye.
Adnan alinitazama kwa makini kuanzia chini hadi juu na kuangua kicheko hafifu huku akiongea kwa sauti ya kunong’ona. “Samahani ndugu yangu kwa kuvuruga starehe yako, kumbe upo na shemeji...”
Nilitaka kusema neno lakini sauti ilikuwa haitoki, nikaishia kufumbua mdomo tu huku nikiendelea kumkodolea macho.
“Basi ngoja niende kwanza kwa shangazi nitarudi baadaye,” Adnan alinong’ona tena na kuanza kupiga hatua kutaka kuondoka.
“Baby, kwani ni nani huyo?” nilisikia sauti ya Jameela ikiniuliza na hapo hapo nikamuona Adnan akisita na moja kwa moja macho yake yakatazama kwa makini kitu kilichokuwa nyuma yangu. Nami nikageuza haraka shingo yangu kutazama nyuma.
Lahaula! Niliishiwa kabisa nguvu baada ya kumuona Jameela akija na kusimama nyuma yangu huku akilalia mgongo wangu na kuchungulia nje ya mlango kumtazama mgeni aliyekuwa akiongea kwa sauti ya chini pale mlangoni. Pasipo kujua kilichokuwa kinaendelea Jameela alikuwa amekuja kuchungulia.
Macho ya Jameela na ya Adnan yalikutana na Jameela akashtuka sana kama aliyekuwa amepigwa na shoti ya umeme, aliruka kurudi nyuma lakini tayari alikuwa amechelwa, kwani Adnan alikuwa amemuona na kumtambua.
Assalale! Mwili wangu ulizizima kwa hofu kama uliopatwa ganzi, kilichotokea pale ilikuwa ni songombingo ambalo liliniachia aibu kubwa isiyoelezeka pale mtaani, Adnan alikasirika sana huku akiwa hayaamini macho yake.
Kama mtu aliyepandwa na wazimu Adnan alirudi nyuma hatua moja na kuruka kwa nguvu zote, alinivamia na kunipiga kikumbo kilichoniangusha chini. Msukumo wa nguvu wa kikumbo hicho ulinitupa chini kwa mshindo mkubwa na kunifanya kugaragara pale sakafuni kama mtu mwenye kifafa.
Wakati huo huo na yeye alianguka kwa kishindo katikati ya sebule kutokana na ile nguvu kubwa aliyoitumia. Jameela alipoona kuwa kaka yake ameanzisha vurugu alipiga kelele ya hofu na kukimbilia chumbani, akajifungia kwa funguo.
Adnan alinirukia tena, mapigano na tifu la aina yake lililozuka pale vilisababisha watu kujaa mlangoni na madirishani na hivyo kujionea sinema ya bure.
Sikukubali, huku nikiwa na boksa tu niliamua kupambana kiume ili nisije kuadhirika, hivyo niliinuka haraka lakini Adnan alikuwa mwepesi, aliruka kama mkizi akanikumba, wote tukapiga mweleka sakafuni. Nikiwa bado nipo sakafuni Adnan aliwahi kusimama huku hasira zikiwa zimempanda kichwani kama mbogo aliyejeruhiwa.
Aliwahi akanikwida shingoni na kiunoni kisha akaninyanyua juu juu kama Joh Cena, yule mcheza mieleka na kunibwaga juu ya meza ya kioo iliyokuwa pale sebuleni. Vioo vilipasuka vipande vipande na kuniumiza mgongo, nilihisi maumivu makali yasiyoelezeka na kupiga yowe kali huku nikijitahidi kusimama.
Hata hivyo, Adnan alionekana kuwa mpiganaji wa kiwango cha juu huku akionekana kuwa makini sana akizisoma nyendo zangu. Akiwa amepandwa na hasira aliruka na kunivaa akanipiga kichwa kikavu kilichonipata katikati ya macho na pua.
Damu zikaanza kunitoka puani utadhani mrija wa maji uliopasuka! Nilisalimu amri na kushika pua yangu nikaiminya nikijaribu kuzuia damu isiendelee kunitoka, na wakati nikiizuia damu isitoke Adnan alinirukia na kunikaba kabali ya nguvu.
Nilijitahidi kukukuruka kutaka kujitoa kwenye ile kabali lakini Adnan alizidisha kabali yake na kunifanya kuanza kuishiwa nguvu. Mwisho wa siku mchezo uliisha huku Adnan akiibuka mshindi na kuondoka na Jameela huku wakiniacha naendelea kuvuja damu.
Itaendelea...
Cc the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, Mine eyes, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY
Nioneshe nwanaume mwenye mwanamke mmoja nami nikuoneshe mbuzi inayotaga mayai!
Hahahaa jinga sn ww!Ahsante sana Bishop...
Bilal kazingua sana kwa Rehema, kakosa uvumilivu.. Angeenda nae taratibu mwisho wa siku angetunukiwa papuchi..
Nilishawahi kuifuatilia papuchi miaka mitatu, nikiwa nae najidai nauhitaji wa papuchi... Kumbe namchora tuu, pembeni nakula hivo visimi hatari...
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] nyonga mkalia ini wangu,unajua nakupenda eeh
Sent using Jamii Forums mobile app
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]Usipotee sana mama k.. Uwepo wako mi muhimu kuliko hata mods...
Tulikua tunaenda polisi na Shunie kutoa taarifa za kupotea kwa mpendwa wetu....