Stori ya kusisimua - Laiti Ningejua!

Stori ya kusisimua - Laiti Ningejua!

Laiti Ningejua! 25

Mtunzi Bishop Hiluka

“Unataka kuniambia hujaoa hadi sasa?” Rehema aliniuliza huku akinitazama kwa udadisi.

“Sijabahatika,” nilimjibu kwa sauti tulivu.

“Kwa nini?”

“Kwa sababu Mungu bado hajanijaalia”

“Na wala huna girlfriend?”

“Ninaye!” nilijibu huku nikimkazia macho Rehema, nikamuona kashtuka kidogo ingawa hakutaka kuuonesha mshtuko wake.

“Sasa… kama una girlfriend nini tatizo hadi uanze kutanga tanga?”

“Wala sijatanga tanga kwani leo ndiyo mara ya kwanza naongea naye na hajui ni kiasi gani nampenda. Girlfriend wangu ni wewe Rehema!”

Endelea...

Rehema akataka kusema neno lakini nikamuona akisita. Aliyakwepa macho yangu yaliyokuwa yakimtazama kwa makini na kuangalia kando, kisha akashusha pumzi za ndani kwa ndani.

“Jambo unalohitaji kwangu ni jambo linalohusu maisha… yangu na yako vilevile, kwa hiyo halihitaji uamuzi wa papara,” alisema Rehema na alionekana kumaanisha kile alichokisema na kuendelea.

“Nahitaji muda wa kutafakari zaidi, nahitaji kukufahamu zaidi na kuufahamu ukoo wako kabla sijakubali au kukataa proposal yako. Najua hata wewe hunifahamu vya kutosha…”

“Ni kweli,” nilikubaliana na maneno yake ingawa moyoni sikuona sababu ya kuanza kuchunguzana wakati nilijua kabisa sitaweza kumuoa bali nilitaka kushiriki tendo tu na kumwacha kama wengine.

“Samahani, hivi wewe mwenzangu ni mzaliwa wa wapi?” nilijikuta nikimtupia swali.

“Kigoma.”

“Kigoma?” Nilimaka kwa mshangao huku nikiachia kinywa changu wazi.

“Ndiyo Kigoma… mbona umeshtuka?”

“Wewe ni kabila gani?” Nilimuuliza tena huku nikimkazia macho.

“Mmanyema, kwani vipi?”

“Ni mshtuko wa furaha kwa kuwa imeniongezea sifa nyingine nisiyoitegemea kwako wewe!”

“Sifa gani hiyo?”

“Wewe ni msichana wa kwetu, mimi pia kwetu ni Kigoma, mimi pia ni Mmanyema. Huwezi kujua, nimefurahi mno, Rehema!” nilisema huku nikihisi msisimko na ubaridi ukinitambaa mwilini mwangu.

Rehema alitabasamu tu bila kusema neno. Nikataka kusema neno lakini nikasita baada ya kumuona Bi Aisha akiingia pale sebuleni na kuketi kwenye sofa, kisha kisha mazungumzo ya kawaida ya kufahamiana zaidi yakatawala maongezi yetu.

Niliaga ili niondoke lakini Bi Aisha hakuniruhusu, aliniomba nisubiri chakula nile ndipo niondoke. Kwa kweli yule mama alikuwa mcheshi na mzungumzaji mzuri. Nilipoondoka pale ilikuwa yapata saa kumi za alasiri na moja kwa moja nilirudi nyumbani nikiwa nimefarijika sana.

Zilipita siku tatu tangu siku nilipokwenda nyumbani kwa kina Rehema na kukutana na mama yake, Bi Aisha, katika siku hizo tatu nilikuwa nashughulikia kongamano maalumu la kibiashara ambalo niliamini kuwa niliamini lingetengeneza fedha nyingi ambazo hatimaye zingenipa heshima zaidi mbele ya Rehema.

Siku ya nne nilikutana na Rehema na aliomba anitembelee nyumbani ninapoishi ili apafahamu. Sikupinga, nilimchukua hadi nyumbani na kumkaribisha ndani.

”Hapa ndipo ninapoishi, Rehema,” nilisema mara tu Rehema alipoingia ndani kwangu. “Ni padogo sana, lakini uwezo wangu ndipo ulipoishia.”

“Una maana gani?” Rehema aliniuliza huku kanikazia macho yake. Japokuwa nilishikwa na haya, lakini nilimudu kuunda tabasamu.

“Nyumba hii ni ndogo tofauti na ile ya kwenu, japo ninatamani sana kuishi maisha ya juu lakini siwezi kuishi kama mkurugenzi, ndiyo maana yangu,” nilisema na kushusha pumzi.

“Pia hii ni nyumba ya familia ambayo tumeachiwa mimi na brother wangu ambaye kwa sasa yupo South Africa. Nina hiki chumba kimoja na sebule, vyumba vingine tumepangisha,” nilizidi kujitetea mbele ya Rehema.

“Kupanga ni kuchagua, na sidhani kama huwezi kuishi kama hao wengine wakati wewe pia umesoma na huna kasoro yoyote!” alisema Rehema huku akiniangalia kwa makini.

“Ni kweli,” niliafiki. “Ila itabidi uvumilie tu maana pana joto kidogo, ila kwa huu mji wetu hilo si jambo la kushangaza.”

“Usijali…” alisema huku akiketi juu ya kochi dogo la sofa pale sebuleni kwangu. Kikakipita kimya cha kitambo kifupi.

“Kwani wazazi wako wapo wapi?” Rehema alinishtua kwa swali lake.

“Wapo Kigoma, wanaishi Mwanga mtaa wa Lumumba,” nilimwambia.

Tuliongea mengi sana siku ile na Rehema aliamua kushinda pale kwangu. Aliniuliza maswali mengi kuhusu maisha yangu binafsi na maisha ya familia yangu, nami bila ajizi nilimjibu kila swali alilouliza kwani nilijua alichokuwa akikitafuta.

Pamoja na kuwa na wakati mzuri wa kuongea na kufurahi nilijaribu sana kumuonesha kuwa nilimhitaji kwa ajili ya kushiriki tendo lakini Rehema alionesha msimamo wa kutokuwa tayari, nami niliheshimu msimamo wake kwa kuogopa kuonekana nilikuwa na papara.

Siku ile ukawa ndiyo mwanzo wa kuwa karibu zaidi na Rehema. Baadaye tukawa tukiwasiliana sana kwa simu, lakini siku moja Rehema alikuja tena nyumbani kwangu ingawa safari ile alinishtukiza maana alikuja bila kunitaarifu kama angekuja.

Ilikuwa ni siku ya Jumamosi na alinikuta nikiwa nafanya usafi ndani kwangu. Aliniambia kuwa alikuwa anapita tu akaona si vibaya akishuka kunisalimia, nikamkaribisha ndani kwa bashasha.

Hakuonesha kukaa sana lakini nami sikutaka kuipoteza nafasi ile hivyo tukiwa katikati ya maongezi nikaanzisha tena mazungumzo yaliyohusu uhusiano.

“Unajua Rehema, sifurahii aina ya maisha ninayoishi, ni ajabu kwamba katika maisha ni vitu vichache kati ya unavyovitaka ambavyo unavipata, vingi huvipati!”

“Hebu niambie Bilali, ni vitu gani katika maisha yako ambavyo hujavipata?”

Niliinamisha uso wangu kidogo nikijifanya kutafakari ingawa kimsingi sikuwa natafakari chochote, kisha nikanyanyua uso kumtazama.

“Nashukuru Mungu nimesoma kiasi cha haja, nimehitimu digrii ya Biashara katika Masoko, nimefungua kampuni na kufanikiwa kuajiari watu kadhaa na ninapata mahitaji yangu yote muhimu, lakini bado zipo haja nyingine zilizomo ndani ya nafsi yangu ninashindwa kuzipata!”

Rehema akacheka kidogo. “Kama zipi hizo?”

“Upendo…” nilijibu huku nikimtazama kwa makini.

“Unataka kuniambia kuwa familia yako hawakupendi?” Rehema aliniuliza huku akinitazama kwa mshangao.

“Familia inanipenda, lakini pendo ninalozungumzia hapa, ni lile ambalo ni tofauti na la baba, mama, dada au kaka!” nilisema huku nikiachia kicheko hafifu.

Rehema aliguna na kuangalia kando akijaribu kuyakwepa macho yangu, hata nilipojaribu kumchunguza sikuiona tashwishwi usoni kwake. Kisha nikamuona akiinuka kisha akaaga na kuanza kuondoka.

“Keti kwanza,” nilimwambia Rehema huku nikimzuia asiondoke.

Rehema alinitazama kwa makini kwa kitambo kisha alitii na kurudi kuketi kwenye kochi. Akabaki akinitumbulia macho.

Nilivuta pumzi ndefu na kuzishusha taratibu huku nikiuma midomo yangu, nikajifanya nafikiria kidogo kisha nikamkabili Rehema kwa sauti tulivu.

Itaendelea...

Cc the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk, marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, Mine eyes, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY
haya baba to... ****m*****ba sasa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ahsante sana Bishop...

Bilal kazingua sana kwa Rehema, kakosa uvumilivu.. Angeenda nae taratibu mwisho wa siku angetunukiwa papuchi..

Nilishawahi kuifuatilia papuchi miaka mitatu, nikiwa nae najidai nauhitaji wa papuchi... Kumbe namchora tuu, pembeni nakula hivo visimi hatari...
khaaaa wee nae hawavumi lakini wamo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Laiti Ningejua! 29

Mtunzi Bishop Hiluka

“Ukweli ni kwamba, unajua mimi ni bachela na wewe tayari una mtu na siku si nyingi mtafunga ndoa na kwenda kuishi Uarabuni…” nilisema huku nikimkazia macho. Jameela alinitazama kwa makini bila kusema neno.

“Hivi umejiuliza nitaishi vipi bila wewe au unadhani mimi sina wivu? Nimekubali matokeo na sioni sababu ya kuona wivu, kwa nini wewe ufanye hivi? Kumbuka umekuja tuagane, sasa kama kuagana kwenyewe ni kwa staili hii sawa, nakuruhusu uende,” nilisema kwa uchungu huku nikimpisha aondoke.

Jameela alinitazama kwa makini nikauona uso wake ukikunjuka na zile hasira zikaanza kuyeyuka, alishusha pumzi za ndani kwa ndani na kujipweteka juu ya kochi.

Endelea...

Nilimfuata pale kwenye kochi nikambembeleza na kuanza kuzitoa tena nguo zake na kuzitupa pale sakafuni moja baada ya nyingine hadi alipobakiwa na nguo ya ndani tu, kisha nikaanza tena kumpapasa.

“Bilali, nisamehe ni kwa kuwa nakupenda sana, unajua kuna wakati nafikiria kutoroka nyumbani, tutafute sehemu yoyote ambayo watu hawatujui tukaishi,” Jameela aliongea huku akinitazama machoni. Nikagundua kuwa alikuwa analengwa na machozi.

“Hata mimi ningetamani hivyo lakini…” nilishindwa kumalizia sentensi yangu baada ya kusikia muungurumo wa gari likifunga breki nje ya nyumba. Kumbe Jameela naye aliusikia ule muungurumo, tukatazamana.

“Rehema huyo karudi,” Jameela aliongea kwa sauti ya chini huku akinikazia macho kwa makini.

“Sidhani,” nilimjibu kwa wasiwasi huku nikijiuliza kama si yeye basi angekuwa nani?

“Na kama atakuwa ni yeye utafanyaje?” Jameela aliniuliza huku akiendelea kunitazama machoni kwa makini.

“Nitamtimua bila...” nilimjibu Jameela lakini sikuweza kumalizia sentensi yangu nikakatishwa na sauti ya mtu aliyekuwa anagonga mlango wangu kwa nguvu.

Aina ya ugongaji wa mlango ilinishtua kidogo, nikajiuliza ni nani aliyekuwa akigonga ule mlango. Mimi na Jameela tukatazamana katika hali ya kuulizana lakini hakuna aliyethubutu kuuliza. Ule mlango ukagongwa tena, lakini safari hii kwa nguvu zaidi.

Nilihisi donge la hasira likinikaba kooni kwangu, hasa nilipokumbuka kuwa huenda alikuwa ni Rehema aliamua kuja kunifanyia vurugu japokuwa alikuwa hataki kufanya ngono na mimi.

Niliinuka haraka nikiwa nimechukizwa na kuusogelea ule mlango nikiwa nina boksa tu tayari kwa kumkabili Rehema, nikaapa kuwa nitamfundisha adabu ili asisahau maishani mwake, nikashika kitasa cha mlango na kuufungua ule mlango huku nikiangalia nje kwa mategemeo ya kumuona Rehema akiwa kasimama mlangoni.

Nilichokiona kikanifanya kupigwa na butwaa, nilijikuta nikiganda kama sanamu nisijue nini nifanye. Adnan alikuwa amesimama nje ya mlango wangu akinitazama huku tabasamu pana la kirafiki likichanua usoni kwake.

Nilijikuta nashindwa kufanya lolote, nikabaki nimekodoa macho yangu kama nilikuwa nimeona mzuka au kitu cha kutisha, nilitamani ardhi ipasuke ili niingie ndani yake kuepuka aibu amabayo ingenikuta muda mfupi baadaye.

Adnan alinitazama kwa makini kuanzia chini hadi juu na kuangua kicheko hafifu huku akiongea kwa sauti ya kunong’ona. “Samahani ndugu yangu kwa kuvuruga starehe yako, kumbe upo na shemeji...”

Nilitaka kusema neno lakini sauti ilikuwa haitoki, nikaishia kufumbua mdomo tu huku nikiendelea kumkodolea macho.

“Basi ngoja niende kwanza kwa shangazi nitarudi baadaye,” Adnan alinong’ona tena na kuanza kupiga hatua kutaka kuondoka.

“Baby, kwani ni nani huyo?” nilisikia sauti ya Jameela ikiniuliza na hapo hapo nikamuona Adnan akisita na moja kwa moja macho yake yakatazama kwa makini kitu kilichokuwa nyuma yangu. Nami nikageuza haraka shingo yangu kutazama nyuma.

Lahaula! Niliishiwa kabisa nguvu baada ya kumuona Jameela akija na kusimama nyuma yangu huku akilalia mgongo wangu na kuchungulia nje ya mlango kumtazama mgeni aliyekuwa akiongea kwa sauti ya chini pale mlangoni. Pasipo kujua kilichokuwa kinaendelea Jameela alikuwa amekuja kuchungulia.

Macho ya Jameela na ya Adnan yalikutana na Jameela akashtuka sana kama aliyekuwa amepigwa na shoti ya umeme, aliruka kurudi nyuma lakini tayari alikuwa amechelwa, kwani Adnan alikuwa amemuona na kumtambua.

Assalale! Mwili wangu ulizizima kwa hofu kama uliopatwa ganzi, kilichotokea pale ilikuwa ni songombingo ambalo liliniachia aibu kubwa isiyoelezeka pale mtaani, Adnan alikasirika sana huku akiwa hayaamini macho yake.

Kama mtu aliyepandwa na wazimu Adnan alirudi nyuma hatua moja na kuruka kwa nguvu zote, alinivamia na kunipiga kikumbo kilichoniangusha chini. Msukumo wa nguvu wa kikumbo hicho ulinitupa chini kwa mshindo mkubwa na kunifanya kugaragara pale sakafuni kama mtu mwenye kifafa.

Wakati huo huo na yeye alianguka kwa kishindo katikati ya sebule kutokana na ile nguvu kubwa aliyoitumia. Jameela alipoona kuwa kaka yake ameanzisha vurugu alipiga kelele ya hofu na kukimbilia chumbani, akajifungia kwa funguo.

Adnan alinirukia tena, mapigano na tifu la aina yake lililozuka pale vilisababisha watu kujaa mlangoni na madirishani na hivyo kujionea sinema ya bure.

Sikukubali, huku nikiwa na boksa tu niliamua kupambana kiume ili nisije kuadhirika, hivyo niliinuka haraka lakini Adnan alikuwa mwepesi, aliruka kama mkizi akanikumba, wote tukapiga mweleka sakafuni. Nikiwa bado nipo sakafuni Adnan aliwahi kusimama huku hasira zikiwa zimempanda kichwani kama mbogo aliyejeruhiwa.

Aliwahi akanikwida shingoni na kiunoni kisha akaninyanyua juu juu kama Joh Cena, yule mcheza mieleka na kunibwaga juu ya meza ya kioo iliyokuwa pale sebuleni. Vioo vilipasuka vipande vipande na kuniumiza mgongo, nilihisi maumivu makali yasiyoelezeka na kupiga yowe kali huku nikijitahidi kusimama.

Hata hivyo, Adnan alionekana kuwa mpiganaji wa kiwango cha juu huku akionekana kuwa makini sana akizisoma nyendo zangu. Akiwa amepandwa na hasira aliruka na kunivaa akanipiga kichwa kikavu kilichonipata katikati ya macho na pua.

Damu zikaanza kunitoka puani utadhani mrija wa maji uliopasuka! Nilisalimu amri na kushika pua yangu nikaiminya nikijaribu kuzuia damu isiendelee kunitoka, na wakati nikiizuia damu isitoke Adnan alinirukia na kunikaba kabali ya nguvu.

Nilijitahidi kukukuruka kutaka kujitoa kwenye ile kabali lakini Adnan alizidisha kabali yake na kunifanya kuanza kuishiwa nguvu. Mwisho wa siku mchezo uliisha huku Adnan akiibuka mshindi na kuondoka na Jameela huku wakiniacha naendelea kuvuja damu.

Itaendelea...

Cc the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, Mine eyes, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY
 
Laiti Ningejua! 30

Mtunzi Bishop Hiluka

Damu zikaanza kunitoka puani utadhani mrija wa maji uliopasuka! Nilisalimu amri na kushika pua yangu nikaiminya nikijaribu kuzuia damu isiendelee kunitoka, na wakati nikiizuia damu isitoke Adnan alinirukia na kunikaba kabali ya nguvu.

Nilijitahidi kukukuruka kutaka kujitoa kwenye ile kabali lakini Adnan alizidisha kabali yake na kunifanya kuanza kuishiwa nguvu. Mwisho wa siku mchezo uliisha huku Adnan akiibuka mshindi na kuondoka na Jameela huku wakiniacha naendelea kuvuja damu.

Endelea...

Usiku wa siku ile sikupata kabisa usingizi, niliwaza mengi kuhusu lile tukio la kufumaniwa na Adnan nikiwa na dada yake. Niliwaza kuhusu lile gari nililoahidiwa na Adnan ambalo aliamua kuondoka nalo baada ya sakata lile. Dah! Nilijilaumu sana kwa tama zangu na kutokuwa mwangalifu.

Nilimkumbuka Rehema, nikatamani nimtafute ili nimuombe msamaha maana niliamini kuwa machozi yake yalikuwa yamebeba laana fulani iliyosababisha nifumaniwe na kupata aibu ya karne pale mtaani. Usiku mzima nikawa namuwaza Rehema tu.

Ilipofika saa nane za usiku uvumilivu ulinishinda, nilichukua simu yangu na kupiga namba ya Rehema, simu iliita kwa muda mrefu na kukata bila majibu, nikapiga tena, baada ya muda mrefu wa kuita nikasikia simu ikipokelewa upande wa pili.

“Hello… Rehema!” nilisema mara baada ya simu kupokewa upande wa pili.

“Unasemaje?” Rehema aliniuliza kwa sauti tulivu.

“Rehema, samahani sana kwa yote yaliyotokea… naomba…” simu ikakatwa kabla sijamaliza kuongea! Nilipiga mara ya pili lakini simu ilikuwa haipatikani, nikasonya na kuitupa ile simu kando.

Kwa kweli sikuweza kupata usingizi, niliinuka nikaelekea sebuleni na kuwasha runinga, hata hivyo, pamoja na kukodoa macho yangu kwenye runinga lakini sikuwa naelewa chochote. Kulipoanza kupambazuka niliamka na kuelekea bafuni nikaoga na baada ya jua kutoka nilikwenda Ilala Sharif Shamba kumtafuta Rehema.

Nilifika nyumbani kwa Bi Aisha na kusimama nje ya fensi karibu ya lango la mbele la kuingilia nikiwa na wasiwasi, nikaangalia huku na huko kwa wasiwasi na kushusha pumzi za ndani kwa ndani kisha nikabonyeza kitufe cha kengele kilichokuwa kando ya lile geti.

Nilipoona kimya nikabonyeza tena kile kitufe cha kengele na muda ule ule nikaisikia sauti ya Bi Aisha kutoka ndani ikinikaribisha.

Mara geti dogo lililokuwa kando ya lile geti kubwa likafunguliwa na Bi Aisha akachungulia nje na kuniona, nikamuona akiachia tabasamu.

“Karibu, baba,” alinikaribisha huku akisogea kando kunipisha niingie. Nilishusha pumzi huku nikibabaika kidogo.

“Sh’kamoo!” nilimsalimia nikiwa bado nimetahayari.

“Marhaba. Karibu ndani, Bilali!” alijibu huku akinitazama kwa udadisi.

Nilionekana kusita sana kuingia nikatupa macho yangu kuangalia ndani ya ule uzio kupitia upenyo wa geti lililokuwa wazi nikijaribu kuangalia kama Rehema alikuwepo mazingira yale. Bi Aisha alizidi kunitazama kwa udadisi zaidi.

“Vipi, kuna tatizo, Bilali?” aliniuliza huku akinikazia macho.

Nilitingisha kichwa changu kukataa huku nikiendelea kuchungulia ndani ya fensi. Bi Aisha aliguna huku akinitazama kwa udadisi zaidi kisha akageuza shingo yake kutazama ndani ambako macho yangu yalikuwa yameelekea.

“Rehema yupo?” hatimaye nilimuuliza Bi Aisha.

“Hayupo, amekwenda hospitali ya Amana,” alinijibu huku akinikazia macho. Jibu lake likanishtua sana.

“Hospitali… kuna nini?” niliuliza kwa wasiwasi.

“Tangu jana aliporudi alikuwa analalamika kuwa hajisikii vizuri,” alinijibu huku macho yake yakionekana kuficha kitu, sikujua kama ilikuwa ni hasira, chuki au huruma.

Sikutaka kuendelea kusimama pale, niliondoka haraka nikashika njia ya kuelekea Amana bila hata kuaga, nilimsikia Bi Aisha akiguna lakini sikujali wala kugeuka, niliendelea na safari yangu nikimwacha akinisindikiza kwa macho yenye mshangao.

Nilitembea haraka hadi Amana, na nilipokuwa naingia kwenye geti la kuingilia katika hospitali ya Amana nikamuona Rehema akiwa anafungua mlango wa gari lake ili aingie, kabla hajaingia aliniona na kushtuka sana. Nilimsogelea na kusimama mbele yake.

“Umefuata nini hapa?” aliniuliza huku kakunja uso wake.

“Nimekufuata wewe! Ni nani anayeweza kuendelea na kazi zake wakati ampendaye yuko hospitali?” biliongea kwa utulivu huku nikijitahidi sana kutabasamu.

Rehema hakujibu kitu, alinitazama kwa dharau kuanzia chini hadi juu, akinishusha na kunipandisha kisha akaangalia kando kwa muda akionekana kuwaza mbali.

“Rehema, najua nimekuudhi sana, nimekukosea sana na nimekuumiza sana… lakini sasa nimetambua kuwa kweli unanipenda kwa dhati, hivyo naomba unisikilize, usinihukumu kabla hujanipa nafasi nikuelezee…”

Rehema alionesha ishara ya kunitaka nisiendelee kuongea. “Huna unachoweza kunieleza, bwana… au unadhani sijui kilichotokea huko nyuma baada ya mimi kuondoka nyumbani kwako? Please leave me alone!

Nilishtuka sana kusikia yale maneno kutoka kwa Rehema lakini sikutaka kuonesha mshtuko wangu, nikamkazia macho. “Kilitokea nini?”

“Hata ukijidai kuficha lakini najua, na kila mtu anajua hata mama yangu mkubwa pia anajua. Kwa kuwa umefumaniwa na kupata aibu ya mwaka kwa hiyo umeona ukimbilie kwangu ili kuficha aibu yako, siyo?” alisema Rehema huku kanikazia macho. Nikaduwaa.

“Wewe siyo wa kutembea na dada wa rafiki yako, tena unajua kabisa kuwa siku si nyingi anaolewa,” aliongeza Rehema na kuingia ndani ya gari yake.

Nilishtuka sana lakini nikaamua kujikaza kisabuni huku nikimzuia asiondoe gari lake. Rehema akanitazama kwa makini huku akionekana kuzuia hasira zake kisha akashusha pumzi za ndani kwa ndani.

“Naomba nikuulize jambo, Bilali,” alisema huku akitoka ndani ya gari na kusimama mbele yangu huku akinitazama moja kwa moja usoni kwa macho makali yaliyokuwa yakiwaka kwa hasira.

“Ruksa, niulize!” nilijibu huku na mimi nikimtazama moja kwa moja usoni kwa makini. Kwa kitambo kifupi tukabaki tumetazamama kama majogoo yaliyotaka kupigana.

“Hivi, wewe unaamini kama kupenda kupo?” aliniuliza akiwa anaendelea kunitazama moja kwa moja machoni pasipo kupepesa macho.

Nilitulia kwa sekunde kadhaa nikimtumbulia macho huku nikijaribu kufikiria kidogo, kisha nikashusha pumzi ndefu.

“Mapenzi yapo, wapo wanaopenda na wapo wanaopendwa… yule anayependa huwa yumo mashakani, kwani anao uwezo wa kuyafanya mambo yasiyowezekana yakawa ya kweli kwa sababu ya kupenda, na yule anayependwa… yeye nadhani, mara nyingi… apendwaye huwa hajali!”

Rehema aliminya midomo yake na kushusha pumzi.

“Ni kweli, mara nyingi anayependwa huwa hajali! Lakini unajua kama kuna tofauti kati ya mtu anayependa na anayetamani?” aliniuliza tena akiwa bado ananitazama moja kwa moja machoni pasipo kupepesa macho.

“Mimi namzungumzia mtu anayependa, siyo anayetamani,” nilisema na kumfanya Rehema aangue kicheko cha dharau kisha akaingia ndani ya gari lake na kufunga mlango.

“Sidhani kama mimi na wewe tunasafiri kwenye boti moja. Ingawa nakupenda sana lakini sioni namna nyingine ya kufanya, kama ni uvumilivu nimefika mwisho, kwa heri Bilali na ninaomba usinitafute tena!” alisema na kuwasha injini ya gari lake kisha akaanza kuliondoa taratibu.

Itaendelea...
 
Laiti Ningejua! 29

Mtunzi Bishop Hiluka

“Ukweli ni kwamba, unajua mimi ni bachela na wewe tayari una mtu na siku si nyingi mtafunga ndoa na kwenda kuishi Uarabuni…” nilisema huku nikimkazia macho. Jameela alinitazama kwa makini bila kusema neno.

“Hivi umejiuliza nitaishi vipi bila wewe au unadhani mimi sina wivu? Nimekubali matokeo na sioni sababu ya kuona wivu, kwa nini wewe ufanye hivi? Kumbuka umekuja tuagane, sasa kama kuagana kwenyewe ni kwa staili hii sawa, nakuruhusu uende,” nilisema kwa uchungu huku nikimpisha aondoke.

Jameela alinitazama kwa makini nikauona uso wake ukikunjuka na zile hasira zikaanza kuyeyuka, alishusha pumzi za ndani kwa ndani na kujipweteka juu ya kochi.

Endelea...

Nilimfuata pale kwenye kochi nikambembeleza na kuanza kuzitoa tena nguo zake na kuzitupa pale sakafuni moja baada ya nyingine hadi alipobakiwa na nguo ya ndani tu, kisha nikaanza tena kumpapasa.

“Bilali, nisamehe ni kwa kuwa nakupenda sana, unajua kuna wakati nafikiria kutoroka nyumbani, tutafute sehemu yoyote ambayo watu hawatujui tukaishi,” Jameela aliongea huku akinitazama machoni. Nikagundua kuwa alikuwa analengwa na machozi.

“Hata mimi ningetamani hivyo lakini…” nilishindwa kumalizia sentensi yangu baada ya kusikia muungurumo wa gari likifunga breki nje ya nyumba. Kumbe Jameela naye aliusikia ule muungurumo, tukatazamana.

“Rehema huyo karudi,” Jameela aliongea kwa sauti ya chini huku akinikazia macho kwa makini.

“Sidhani,” nilimjibu kwa wasiwasi huku nikijiuliza kama si yeye basi angekuwa nani?

“Na kama atakuwa ni yeye utafanyaje?” Jameela aliniuliza huku akiendelea kunitazama machoni kwa makini.

“Nitamtimua bila...” nilimjibu Jameela lakini sikuweza kumalizia sentensi yangu nikakatishwa na sauti ya mtu aliyekuwa anagonga mlango wangu kwa nguvu.

Aina ya ugongaji wa mlango ilinishtua kidogo, nikajiuliza ni nani aliyekuwa akigonga ule mlango. Mimi na Jameela tukatazamana katika hali ya kuulizana lakini hakuna aliyethubutu kuuliza. Ule mlango ukagongwa tena, lakini safari hii kwa nguvu zaidi.

Nilihisi donge la hasira likinikaba kooni kwangu, hasa nilipokumbuka kuwa huenda alikuwa ni Rehema aliamua kuja kunifanyia vurugu japokuwa alikuwa hataki kufanya ngono na mimi.

Niliinuka haraka nikiwa nimechukizwa na kuusogelea ule mlango nikiwa nina boksa tu tayari kwa kumkabili Rehema, nikaapa kuwa nitamfundisha adabu ili asisahau maishani mwake, nikashika kitasa cha mlango na kuufungua ule mlango huku nikiangalia nje kwa mategemeo ya kumuona Rehema akiwa kasimama mlangoni.

Nilichokiona kikanifanya kupigwa na butwaa, nilijikuta nikiganda kama sanamu nisijue nini nifanye. Adnan alikuwa amesimama nje ya mlango wangu akinitazama huku tabasamu pana la kirafiki likichanua usoni kwake.

Nilijikuta nashindwa kufanya lolote, nikabaki nimekodoa macho yangu kama nilikuwa nimeona mzuka au kitu cha kutisha, nilitamani ardhi ipasuke ili niingie ndani yake kuepuka aibu amabayo ingenikuta muda mfupi baadaye.

Adnan alinitazama kwa makini kuanzia chini hadi juu na kuangua kicheko hafifu huku akiongea kwa sauti ya kunong’ona. “Samahani ndugu yangu kwa kuvuruga starehe yako, kumbe upo na shemeji...”

Nilitaka kusema neno lakini sauti ilikuwa haitoki, nikaishia kufumbua mdomo tu huku nikiendelea kumkodolea macho.

“Basi ngoja niende kwanza kwa shangazi nitarudi baadaye,” Adnan alinong’ona tena na kuanza kupiga hatua kutaka kuondoka.

“Baby, kwani ni nani huyo?” nilisikia sauti ya Jameela ikiniuliza na hapo hapo nikamuona Adnan akisita na moja kwa moja macho yake yakatazama kwa makini kitu kilichokuwa nyuma yangu. Nami nikageuza haraka shingo yangu kutazama nyuma.

Lahaula! Niliishiwa kabisa nguvu baada ya kumuona Jameela akija na kusimama nyuma yangu huku akilalia mgongo wangu na kuchungulia nje ya mlango kumtazama mgeni aliyekuwa akiongea kwa sauti ya chini pale mlangoni. Pasipo kujua kilichokuwa kinaendelea Jameela alikuwa amekuja kuchungulia.

Macho ya Jameela na ya Adnan yalikutana na Jameela akashtuka sana kama aliyekuwa amepigwa na shoti ya umeme, aliruka kurudi nyuma lakini tayari alikuwa amechelwa, kwani Adnan alikuwa amemuona na kumtambua.

Assalale! Mwili wangu ulizizima kwa hofu kama uliopatwa ganzi, kilichotokea pale ilikuwa ni songombingo ambalo liliniachia aibu kubwa isiyoelezeka pale mtaani, Adnan alikasirika sana huku akiwa hayaamini macho yake.

Kama mtu aliyepandwa na wazimu Adnan alirudi nyuma hatua moja na kuruka kwa nguvu zote, alinivamia na kunipiga kikumbo kilichoniangusha chini. Msukumo wa nguvu wa kikumbo hicho ulinitupa chini kwa mshindo mkubwa na kunifanya kugaragara pale sakafuni kama mtu mwenye kifafa.

Wakati huo huo na yeye alianguka kwa kishindo katikati ya sebule kutokana na ile nguvu kubwa aliyoitumia. Jameela alipoona kuwa kaka yake ameanzisha vurugu alipiga kelele ya hofu na kukimbilia chumbani, akajifungia kwa funguo.

Adnan alinirukia tena, mapigano na tifu la aina yake lililozuka pale vilisababisha watu kujaa mlangoni na madirishani na hivyo kujionea sinema ya bure.

Sikukubali, huku nikiwa na boksa tu niliamua kupambana kiume ili nisije kuadhirika, hivyo niliinuka haraka lakini Adnan alikuwa mwepesi, aliruka kama mkizi akanikumba, wote tukapiga mweleka sakafuni. Nikiwa bado nipo sakafuni Adnan aliwahi kusimama huku hasira zikiwa zimempanda kichwani kama mbogo aliyejeruhiwa.

Aliwahi akanikwida shingoni na kiunoni kisha akaninyanyua juu juu kama Joh Cena, yule mcheza mieleka na kunibwaga juu ya meza ya kioo iliyokuwa pale sebuleni. Vioo vilipasuka vipande vipande na kuniumiza mgongo, nilihisi maumivu makali yasiyoelezeka na kupiga yowe kali huku nikijitahidi kusimama.

Hata hivyo, Adnan alionekana kuwa mpiganaji wa kiwango cha juu huku akionekana kuwa makini sana akizisoma nyendo zangu. Akiwa amepandwa na hasira aliruka na kunivaa akanipiga kichwa kikavu kilichonipata katikati ya macho na pua.

Damu zikaanza kunitoka puani utadhani mrija wa maji uliopasuka! Nilisalimu amri na kushika pua yangu nikaiminya nikijaribu kuzuia damu isiendelee kunitoka, na wakati nikiizuia damu isitoke Adnan alinirukia na kunikaba kabali ya nguvu.

Nilijitahidi kukukuruka kutaka kujitoa kwenye ile kabali lakini Adnan alizidisha kabali yake na kunifanya kuanza kuishiwa nguvu. Mwisho wa siku mchezo uliisha huku Adnan akiibuka mshindi na kuondoka na Jameela huku wakiniacha naendelea kuvuja damu.

Itaendelea...

Cc the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, Mine eyes, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY
Ahsante Bishop nimeishafika
 
Laiti Ningejua! 31

Mtunzi Bishop Hiluka

“Ni kweli, mara nyingi anayependwa huwa hajali! Lakini unajua kama kuna tofauti kati ya mtu anayependa na anayetamani?” aliniuliza tena akiwa bado ananitazama moja kwa moja machoni pasipo kupepesa macho.

“Mimi namzungumzia mtu anayependa, siyo anayetamani,” nilisema na kumfanya Rehema aangue kicheko cha dharau kisha akaingia ndani ya gari lake na kufunga mlango.

“Sidhani kama mimi na wewe tunasafiri kwenye boti moja. Ingawa nakupenda sana lakini sioni namna nyingine ya kufanya, kama ni uvumilivu nimefika mwisho, kwa heri Bilali na ninaomba usinitafute tena!” alisema na kuwasha injini ya gari lake kisha akaanza kuliondoa taratibu.

Endelea...

Nilibaki nikiwa nimesimama nikilisindikiza gari la Rehema kwa huzuni huku nikiwa nimekata tamaa. Nilihisi donge la uchungu likinikaba kooni na kunifanya nishindwe kupumua vizuri, machozi yakaanza kunitoka machoni na kuwafanya watu waliokuwa wakipita jirani na eneo lile wanitazame kwa mshangao.

Niliangusha kilio kilichomfanya Rehema ageuke kunitazama kwa mshangao ingawa bado macho yake yalionesha chuki dhidi yangu, kisha nikamuona akisita na kukanyaga breki, gari likasimama.

Alishusha kioo cha gari na kutoa kichwa chake nje kisha akaniashiria kwa mkono nimfuate, nilimfuata kwa unyonge huku nikipangusa machozi, akaniambia niingie ndani ya gari, nami sikujivunga niliufungua mlango wa mbele wa gari kushoto kwa dereva na kuingia.

Rehema alinitupia jicho na kuliondoa gari lake bila kusema chochote, gari likatoka kwenye geti la kuingilia la hospitali ya Amana na kukata kushoto kisha tukaifuata barabara iliyokwenda kuungana na barabara ya Uhuru katika ukumbi wa Amana Vijana, akakunja tena kuingia upande wa kushoto akiifuata barabara ya Uhuru.

Aliendesha gari lake na kuvukaa vibanda vya wasusi wa Kimasai kisha akakunja kuingia mtaa wa Mafao akiyapita maghorofa ya Ilala na kwenda moja kwa moja hadi akatokea katika barabara ya Kawawa, hapo akakata kuingia upande wa kushoto akiifuata barabara ya Kawawa kama anaelekea Magomeni.

Hadi wakati huo sikujua tulikuwa tunaelekea wapi, nilibaki kimya tu nikimtazama kwa kuibia bila kusema lolote.

Rehema aliongeza mwendo wa gari na mbele kidogo akalivuka jengo la hoteli ya Lamada na alipofika mwisho wa lile jengo nikamuona akipunguza mwendo na kukunja akaingia upande wa kushoto, kisha akaliingiza gari lake kwenye geti la kuingilia katika ile hoteli ya Lamada.

Tulipoingia ndani ya ile hoteli Rehema akazima injini ya gari na kunitazama kisha akashuka, nami nikashuka kumfuata. Nilimfuata kimya kimya na tukatafuta sehemu nzuri ya kukaa kwenye mgahawa uliokuwa ndani ya hoteli ile ya Lamada.

Kwenye mgahawa ule tulikuta wateja wachache wakiwa wameketi, Rehema akaagiza mchemsho wa kuku wa kienyeji na chapatti moja. Mimi niliagiza maziwa ya moto, sambusa mbili na soseji moja.

Mhudumu alipoondoka kwenda kuleta oda zetu takabaki tukiwa kimya kila mmoja akiwaza lake, na baada ya kitambo tulipoletewa chakula, tukaanza kula taratibu huku kila mmoja akiwa kimya.

Wakati tunakula Rehema alikuwa akinitupia jicho mara kwa mara akionekana kuwa makini zaidi na mimi.

“Rehema… najua nimekukosea sana, lakini ni vizuri kama tutazungumza kuhusu matatizo yetu kuliko ukimya huu! Ni pepo mbaya tu alinipitia lakini naahidi sitorudia tena…”

“Kwani ulikuwa unatakaje?” Rehema alinikata kauli.

“Tafadhali naaomba uniahidi kuwa umenisamehe,” nilisema huku nikimkazia macho.

“Nimekwisha kusamehe hata kabla hujaniomba msamaha, ingawa siwezi kusahau yote uliyonifanyia,” aliniambia huku akiendelea kula chakula taratibu.

“Nashukuru kama umenisamehe, na ninashukuru kwa kuwa unanipenda lakini naomba ubadilike kidogo ili na mimi nibadilike, kama kweli unanipenda kwa nini uendelee kukataa kunanihii?” nilimuuliza tena huku nikiwa siyatoi macho yangu kwenye uso wake.

“Je, ni lazima swali lako nilijibu sasa hivi?” Rehema aliniuliza huku na yeye akinikazia macho.

“Ikikupendeza unaweza kunijibu sasa hivi, vinginevyo naweza kukupa muda!” nilisema kwa sauti tulivu nikiendelea kumtazama.

“Basi nipe muda, kwani ni swali gumu lililoulizwa katika wakati mbaya na mahali pagumu!” alisema huku akitafuna nyama ya kuku.

“Hebu tuwe wakweli, Rehema, msichana mrembo kama wewe unaweza kuishi bila kufanya mapenzi? Hii hainiingii akilini… Wanaume wangapi, tena wenye mali zao wanakutongoza, kwani wewe ni nani hadi usiingie majaribuni?” nilimuuliza kwa wasiwasi huku nikimkazia macho kujaribu kuyasoma mawazo yake.

Rehema alinitazama kwa makini kwa kitambo kirefu na kuonekana kukerwa sana na kauli yangu.

“Kwa kweli unanikosea sana heshima, Bilali, kwa nini uongeee vitu usivyovijua? Naomba uelewe, mimi siko kama unavyodhani!” Rehema aliongea kwa huzuni.

“Kumbuka ni wewe pekee niliyeamua kukuweka kwenye moyo wangu wa nyama. Najua huwezi kuamini ila siku nikipotea jumla ndiyo utajua kuwa nilikuwa nakupenda kiasi gani,” Rehema alisema na kuinamisha uso wake chini akionekana kuwaza mbali sana. Machozi yalikuwa yakimlenga.

Nilishtuka sana kwa maneno yale. Nilitaka kusema neno lakini nikasita baada ya kuhisi kulikuwa na mtu aliyeingia na kusimama nyuma yangu. Nikageuza shingo yangu na kumuona mwanadada mmoja aliyekuwa na umbile kubwa lakini lililovutia.

Kwa yeyote awaye mwanaume rijali hapana shaka kama angemuona angekiri kuwa alikuwa na umbo zuri sana la kibantu na alikuwa ni moto wa kuotea mbali.

Kwa mlingano wa macho tu, alitoa tafsiri ya kuwa na ule uzuri usiomithilika, uzuri kama wa mdoli.

Nywele zake zilikuwa nyeusi tii zilizotumwa vema sambamba na sura yake ya kitoto yenye mvuto wa asilimia mia moja. Nyusi na kope zake zilikuwa ndefu zilizong’ara na kuyafanya macho yake yawe wazi nusu.

Pua yake ilikuwa ndefu kiasi, nyoofu ya wastani na midomo yake ilikuwa minene. Alikuwa na rangi angavu yenye ung’avu wa kuteleza.

Japo alikuwa na umbo kubwa lakini kifua chake kilibeba matiti ya wastani na tumbo lake lilikuwa flati huku kiuno chake kikiwa chembamba mithili ya dondola. Miguu yake ilikuwa mizuri mno iliyotazamika.

Mwanadada yule alikuwa amevaa gauni zuri la kitenge na alikadiriwa kuwa na miaka kati ya 25 na 28. Alikuwa amesimama pale akimtazama sana Rehema kama aliyekuwa akimfananisha.

Mara Rehema akainua uso wake na kumtupia jicho yule mwanadada kisha akanitazama kwa makini.

Mambo yanazidi kunonga, fuatana nami hadi mwisho wa safari hii...
 
Ahsante sana Bishop...

Bilal kazingua sana kwa Rehema, kakosa uvumilivu.. Angeenda nae taratibu mwisho wa siku angetunukiwa papuchi..

Nilishawahi kuifuatilia papuchi miaka mitatu, nikiwa nae najidai nauhitaji wa papuchi... Kumbe namchora tuu, pembeni nakula hivo visimi hatari...
Hahahaa jinga sn ww!

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom