Tajiri mpole
JF-Expert Member
- Apr 15, 2018
- 3,127
- 6,098
😳😀😀🙂...Rehema ana karoho ka uchoyo tuu, ona kafa na utamu wake.. Angemwambia Bilal atumie kondomu mambo yangekua mukide...
Ukimwi kitu gani bhana, watu wananjunjana kama kawaida...
😀😀😀 Jameela sasa hivi yupo Oman ana watoto watano, jamaa anafyatua kama hana akili nzuri... 😀😀😀wakuu mwenye namba ya jameela anipatie
by the wei asante mkuu bishop
Laiti Ningejua! 33
Mtunzi Bishop Hiluka
Mara akatokwa na kelele kubwa zilizonishtua sana ambazo sikuwa nimezitegemea kabisa. Sikujua kama angeweza kufanya kitendo kile.
“Ananibakaaaaa! Nisaidieeni ananibaaaka!” Alipiga kelele kubwa, nilimshika nikajaribu kumziba mdomo lakini alining’ata na kunifanya niugulie kwa maumivu. Kisha akaendelea kupiga kelele ambazo ziliwafanya wasamalia wema kukimbilia pale zilipokuwa zikisikika kelele.
Mara mlango wangu ukapigwa kumbo na watu wakaingia na kunikuta nikiwa juu ya Rehema, wakaninivagaa na kuanza kunishushia kipigo. Nilijaribu kujitetea lakini walizidi kunishushia kipigo hadi nikapoteza fahamu na sikujua tena kilichoendelea baada ya hapo.
______
Nilipozinduka nilijikuta nikiwa katika hospitali ya Amana nikiwa na majeraha mwilini huku nimefungwa pingu mkononi iliyounganishwa na kitanda. Nilikuwa na maumivu makali sana mwili mzima. Nikajaribu kukumbuka kilichonitokea na mara nikakumbuka kuwa nilifumaniwa nikitaka kufanya ubakaji.
Nilipogeuka kutazama upande mwingine macho yangu yalikutana na macho ya ofisa wa polisi aliyekuwa na cheo cha Sajenti ambaye alikuwa kaketi pembeni kwenye kiti akinitazama kwa makini huku kakunja sura yake.
Niliendelea kuwepo pale hospitali kwa siku tatu na baada ya nguvu kunirejea mwilini niliondolewa pale hospitali nikapelekwa mahabusu ya kituo cha polisi cha Buguruni. Nilikaa pale mahubusu nikisubiri kufunguliwa kesi mbaya ya ubakaji.
Siku iliyofuata wakati nikiwa nimejikunyata kwenye kona ya chumba cha mahabusu nilishuhudia lango la mahabusu ile likifunguliwa na askari mmoja ambaye aliita jina langu. Kwa unyonge niliinua shingo yangu kumtazama yule askari ambaye alikuwa na cheo cha Koplo.
“We mbakaji, inuka unifuate!” alisema baada ya kuona namtazama kwa wasiwasi.
Mahabusu wote katika kile chumba walinitazama kwa makini, baadhi yao walinihurumia lakini wengine walitabasamu kwa kejeli. Niliinuka kwa unyonge nikamfuata yule askari, aliniongoza tukipita kwenye korido hadi kwenye mlango wa ofisi ya mkuu wa kituo.
Tulipoingia ndani ya ofisi ile ya mkuu wa kituo nilipigwa butwaa baada ya kumkuta mama yake mkubwa na Rehema, Bi Aisha akiwa kwenye ile ofisi na Mkuu wa Kituo kile, Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP), Shaban Mungi, ambaye alikuwa kajiegemeza kwenye kiti chake cha kuzunguka. Wote waligeuka kunitazama kwa makini nilipokuwa naingia.
Nilijikuta nagwaya baada ya kuhisi uwepo wa hali ya majonzi na ukimya mzito sana ndani ya ile ofisi. Nilipowatupia jicho la wizi niliowakuta mle ofisini niliona huzuni kwenye macho yao. Mkuu wa kituo alinionesha kiti, nikaketi nikiwa na wasiwasi mkubwa.
Mkuu wa kituo aliendelea kunitazama kwa macho yaliyokuwa yameficha kitu nyuma yake. Sikuweza kujua nini kilichokuwa kikiendelea pale, nikajiuliza, yuko wapi Rehema?
Nilianza kuingiwa wasiwasi, hata hivyo, nilibaki kimya nikiwatazama wote kwa makini ingawa nilianza kuhisi kuwa kulikuwa na jambo lisilo la kawaida lililokuwa limetokea. Niliogopa kuuliza. Bi Aisha alinitazama akashindwa kuvumilia, nilimuona akiinuka na kutoka nje huku akilia kwa uchungu mkubwa.
Mkuu wa kituo alishusha pumzi na kufungua droo moja katika meza yake, kisha akatoa bahasha ndogo iliyokuwa na barua ndani yake, akaishika vizuri ile bahasha mkononi mwake huku akinitazama kwa huzuni.
“Bilali, kuanzia sasa uko huru, shika barua yako!” aliniambia huku akinyoosha mkono wake kunipa ile bahasha.
Kauli ya yule mkuu wa kituo cha polisi ikanishangaza sana, nilidhani labda nilikuwa ndotoni na mara ningeamka ningekuta mambo hayapo hivyo, lakini yule mkuu wa kituo aliendelea kunyoosha mkono wake kunitaka nichukue ile barua.
Nilimtazama usoni kutaka kuona kama kweli hatanii kisha nikaipokea ile barua huku mikono yangu ikitetemeka, ilitetemeka kwa sababu sikujua ilitoka wapi na ilihusu nini. Niliitazama ile barua kwa wasiwasi.
“Unaweza kusoma hapa hapa ukipenda!” yule mkuu wa kituo aliniambia huku akifuta machozi yake. Nikiwa na wasiwasi niliifungua ile bahasha na ndani yake kulikuwa na barua ndefu iliyotoka kwa Rehema.
“Mpenzi Bilali, haikuwa nia yangu kukusababishia kipigo kikali na kuitwa mbakaji, bali nimefanya haya kwa sababu nakupenda kutoka moyoni na ninapenda uishi miaka mingi…
“Bilali ni wewe mwanaume pekee niliyetokea kuvutiwa nawe kihisia ukauteka moyo wangu na kujikuta nikiwa mtumwa wa mahaba yako japo ulijaribu sana kuniumiza kihisia lakini bado sikuacha kukupenda…
“Ni kweli sikutaka kulala na wewe kwa kuwa nina kasoro kubwa ambayo hainipi hadhi ya kulala kitanda kimoja na wewe, sikutaka kuwa muuaji kwa kuruhusu unibake… hivi, Bilali unadhani mpapaso wako haukunisisimua? Nilisisimka hasa na nilitamani nikutimizie kwa hiari kile ulichotaka, labda mimi nilikuwa muhitaji kuliko wewe mpenzi, lakini… lakini nisingeweza kukuua…
“Bilali, wala usisikitike kusikia hili, mimi nimefurahi sana kufa nikiupigania uhai wa mwanaume niliyempenda, ninayempenda na ninayekufa kwa ajili yake. Kifo hiki kiwe kumbukumbu yako milele kuwa nilikupenda sana…
“Nilitaka kukwambia lakini nilishindwa, nimekuwa nikiishi na virusi vya UKIMWI kwa muda mrefu baada ya kuambukizwa na wazazi wangu… nilizaliwa nikiwa na Virus vya Ukimwi, na mama kabla ya kufa alinikanya kuwa ni heri nife peke yangu kuliko kuua yeyote asiyekuwa na hatia…
“Kwa kuwa utaalamu umeongezeka nilikubali unioe kwa kuwa tungefuata ushauri wa kitaalamu ili nisikuambukize, maana wewe huna hatia na haustahili kufa… laiti kama ungenibaka basi leo hii ningekufa nikiwa muuaji…
“Ninafurahi kuwa nakufa kama shujaa. Ninayaandika haya huku chupa ya sumu ikiwa pembeni yangu, nakufa leo lakini nimewaomba wakuache uwe huru. Bahati nzuri mkuu wa kituo ni baba yangu mdogo hivyo naamini atakuacha uwe huru, huru kabisa, wakati mimi nikiungana na mama yangu nimweleze kuwa sikuwahi kuua duniani na nimeamua kuondoka ili siku moja nisije kuua yeyote. Buriani Bilali, mpenzi wa moyo wangu…”
Sikujua kilichoendelea baada ya pale kwani niliishiwa nguvu, moyo wangu ukashikwa na mfadhaiko, mikono yangu ilikuwa inatetemeka na jasho jingi likaanza kunitoka sehemu mbalimbali za mwili wangu.
Macho yangu nayo yakaanza kupoteza nguvu ya kuona na hatimaye shughuli mbalimbali za mwili wangu nazo nikazihisi kuwa zilikuwa mbioni kusitisha utendaji wake.
______
Siku mbili baadaye nilikwenda kwenye makaburi ya Kisutu ambako Rehema alikuwa amezikwa, nilisimama mbele ya kaburi jipya la Rehema na kulitazama kwa huzuni, nikafuta machozi yaliyokuwa yakinilengalenga.
Haikuwa ndoto, ni kweli ilitokea kuwa Rehema alijiua kwa sumu na kuzikwa… barua ile niliyopewa ilikuwa imetwa kando ya mwili wake chumbani… sasa macho ya watu yalikuwa yakinitazama kwa kunisuta, wapo waliokuwa na hasira juu yangu, wapo ambao walinitazama kwa dharau na baadhi walinitazama kwa huzuni. Kwa kweli sikujua nifanye nini!
Nilitamani ardhi ipasuke ili nijifiche chini ya ardhi kukwepa macho ya jamii. Nilitamani kunywa sumu ili nami niondoke hapa duniani, hasa baada ya kuujua ukweli kuhusu maisha ya Rehema, mwanamke aliyenijali na kunipenda kwa dhati!
Niliendelea kusimama nikilitazama kaburi la Rehema kwa kitambo kirefu huku machozi yakinitoka. Nilifuta machozi nikashusha pumzi ndefu za ndani kwa ndani.
“Upumzike pema peponi Rehema… kamwe sitakusahau mpenzi!” nilisema kwa huzuni kisha nikainamisha kichwa changu mbele ya kaburi la rehema kama ishara ya kutoa heshima zangu za mwisho. Sikuweza kuendelea kusimama pale nikaondoka taratibu kwa huzuni, mikono yangu ikiwa nyuma.
MWISHO
Shukrani Bishop.Laiti Ningejua! 33
Mtunzi Bishop Hiluka
Mara akatokwa na kelele kubwa zilizonishtua sana ambazo sikuwa nimezitegemea kabisa. Sikujua kama angeweza kufanya kitendo kile.
“Ananibakaaaaa! Nisaidieeni ananibaaaka!” Alipiga kelele kubwa, nilimshika nikajaribu kumziba mdomo lakini alining’ata na kunifanya niugulie kwa maumivu. Kisha akaendelea kupiga kelele ambazo ziliwafanya wasamalia wema kukimbilia pale zilipokuwa zikisikika kelele.
Mara mlango wangu ukapigwa kumbo na watu wakaingia na kunikuta nikiwa juu ya Rehema, wakaninivagaa na kuanza kunishushia kipigo. Nilijaribu kujitetea lakini walizidi kunishushia kipigo hadi nikapoteza fahamu na sikujua tena kilichoendelea baada ya hapo.
______
Nilipozinduka nilijikuta nikiwa katika hospitali ya Amana nikiwa na majeraha mwilini huku nimefungwa pingu mkononi iliyounganishwa na kitanda. Nilikuwa na maumivu makali sana mwili mzima. Nikajaribu kukumbuka kilichonitokea na mara nikakumbuka kuwa nilifumaniwa nikitaka kufanya ubakaji.
Nilipogeuka kutazama upande mwingine macho yangu yalikutana na macho ya ofisa wa polisi aliyekuwa na cheo cha Sajenti ambaye alikuwa kaketi pembeni kwenye kiti akinitazama kwa makini huku kakunja sura yake.
Niliendelea kuwepo pale hospitali kwa siku tatu na baada ya nguvu kunirejea mwilini niliondolewa pale hospitali nikapelekwa mahabusu ya kituo cha polisi cha Buguruni. Nilikaa pale mahubusu nikisubiri kufunguliwa kesi mbaya ya ubakaji.
Siku iliyofuata wakati nikiwa nimejikunyata kwenye kona ya chumba cha mahabusu nilishuhudia lango la mahabusu ile likifunguliwa na askari mmoja ambaye aliita jina langu. Kwa unyonge niliinua shingo yangu kumtazama yule askari ambaye alikuwa na cheo cha Koplo.
“We mbakaji, inuka unifuate!” alisema baada ya kuona namtazama kwa wasiwasi.
Mahabusu wote katika kile chumba walinitazama kwa makini, baadhi yao walinihurumia lakini wengine walitabasamu kwa kejeli. Niliinuka kwa unyonge nikamfuata yule askari, aliniongoza tukipita kwenye korido hadi kwenye mlango wa ofisi ya mkuu wa kituo.
Tulipoingia ndani ya ofisi ile ya mkuu wa kituo nilipigwa butwaa baada ya kumkuta mama yake mkubwa na Rehema, Bi Aisha akiwa kwenye ile ofisi na Mkuu wa Kituo kile, Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP), Shaban Mungi, ambaye alikuwa kajiegemeza kwenye kiti chake cha kuzunguka. Wote waligeuka kunitazama kwa makini nilipokuwa naingia.
Nilijikuta nagwaya baada ya kuhisi uwepo wa hali ya majonzi na ukimya mzito sana ndani ya ile ofisi. Nilipowatupia jicho la wizi niliowakuta mle ofisini niliona huzuni kwenye macho yao. Mkuu wa kituo alinionesha kiti, nikaketi nikiwa na wasiwasi mkubwa.
Mkuu wa kituo aliendelea kunitazama kwa macho yaliyokuwa yameficha kitu nyuma yake. Sikuweza kujua nini kilichokuwa kikiendelea pale, nikajiuliza, yuko wapi Rehema?
Nilianza kuingiwa wasiwasi, hata hivyo, nilibaki kimya nikiwatazama wote kwa makini ingawa nilianza kuhisi kuwa kulikuwa na jambo lisilo la kawaida lililokuwa limetokea. Niliogopa kuuliza. Bi Aisha alinitazama akashindwa kuvumilia, nilimuona akiinuka na kutoka nje huku akilia kwa uchungu mkubwa.
Mkuu wa kituo alishusha pumzi na kufungua droo moja katika meza yake, kisha akatoa bahasha ndogo iliyokuwa na barua ndani yake, akaishika vizuri ile bahasha mkononi mwake huku akinitazama kwa huzuni.
“Bilali, kuanzia sasa uko huru, shika barua yako!” aliniambia huku akinyoosha mkono wake kunipa ile bahasha.
Kauli ya yule mkuu wa kituo cha polisi ikanishangaza sana, nilidhani labda nilikuwa ndotoni na mara ningeamka ningekuta mambo hayapo hivyo, lakini yule mkuu wa kituo aliendelea kunyoosha mkono wake kunitaka nichukue ile barua.
Nilimtazama usoni kutaka kuona kama kweli hatanii kisha nikaipokea ile barua huku mikono yangu ikitetemeka, ilitetemeka kwa sababu sikujua ilitoka wapi na ilihusu nini. Niliitazama ile barua kwa wasiwasi.
“Unaweza kusoma hapa hapa ukipenda!” yule mkuu wa kituo aliniambia huku akifuta machozi yake. Nikiwa na wasiwasi niliifungua ile bahasha na ndani yake kulikuwa na barua ndefu iliyotoka kwa Rehema.
“Mpenzi Bilali, haikuwa nia yangu kukusababishia kipigo kikali na kuitwa mbakaji, bali nimefanya haya kwa sababu nakupenda kutoka moyoni na ninapenda uishi miaka mingi…
“Bilali ni wewe mwanaume pekee niliyetokea kuvutiwa nawe kihisia ukauteka moyo wangu na kujikuta nikiwa mtumwa wa mahaba yako japo ulijaribu sana kuniumiza kihisia lakini bado sikuacha kukupenda…
“Ni kweli sikutaka kulala na wewe kwa kuwa nina kasoro kubwa ambayo hainipi hadhi ya kulala kitanda kimoja na wewe, sikutaka kuwa muuaji kwa kuruhusu unibake… hivi, Bilali unadhani mpapaso wako haukunisisimua? Nilisisimka hasa na nilitamani nikutimizie kwa hiari kile ulichotaka, labda mimi nilikuwa muhitaji kuliko wewe mpenzi, lakini… lakini nisingeweza kukuua…
“Bilali, wala usisikitike kusikia hili, mimi nimefurahi sana kufa nikiupigania uhai wa mwanaume niliyempenda, ninayempenda na ninayekufa kwa ajili yake. Kifo hiki kiwe kumbukumbu yako milele kuwa nilikupenda sana…
“Nilitaka kukwambia lakini nilishindwa, nimekuwa nikiishi na virusi vya UKIMWI kwa muda mrefu baada ya kuambukizwa na wazazi wangu… nilizaliwa nikiwa na Virus vya Ukimwi, na mama kabla ya kufa alinikanya kuwa ni heri nife peke yangu kuliko kuua yeyote asiyekuwa na hatia…
“Kwa kuwa utaalamu umeongezeka nilikubali unioe kwa kuwa tungefuata ushauri wa kitaalamu ili nisikuambukize, maana wewe huna hatia na haustahili kufa… laiti kama ungenibaka basi leo hii ningekufa nikiwa muuaji…
“Ninafurahi kuwa nakufa kama shujaa. Ninayaandika haya huku chupa ya sumu ikiwa pembeni yangu, nakufa leo lakini nimewaomba wakuache uwe huru. Bahati nzuri mkuu wa kituo ni baba yangu mdogo hivyo naamini atakuacha uwe huru, huru kabisa, wakati mimi nikiungana na mama yangu nimweleze kuwa sikuwahi kuua duniani na nimeamua kuondoka ili siku moja nisije kuua yeyote. Buriani Bilali, mpenzi wa moyo wangu…”
Sikujua kilichoendelea baada ya pale kwani niliishiwa nguvu, moyo wangu ukashikwa na mfadhaiko, mikono yangu ilikuwa inatetemeka na jasho jingi likaanza kunitoka sehemu mbalimbali za mwili wangu.
Macho yangu nayo yakaanza kupoteza nguvu ya kuona na hatimaye shughuli mbalimbali za mwili wangu nazo nikazihisi kuwa zilikuwa mbioni kusitisha utendaji wake.
______
Siku mbili baadaye nilikwenda kwenye makaburi ya Kisutu ambako Rehema alikuwa amezikwa, nilisimama mbele ya kaburi jipya la Rehema na kulitazama kwa huzuni, nikafuta machozi yaliyokuwa yakinilengalenga.
Haikuwa ndoto, ni kweli ilitokea kuwa Rehema alijiua kwa sumu na kuzikwa… barua ile niliyopewa ilikuwa imetwa kando ya mwili wake chumbani… sasa macho ya watu yalikuwa yakinitazama kwa kunisuta, wapo waliokuwa na hasira juu yangu, wapo ambao walinitazama kwa dharau na baadhi walinitazama kwa huzuni. Kwa kweli sikujua nifanye nini!
Nilitamani ardhi ipasuke ili nijifiche chini ya ardhi kukwepa macho ya jamii. Nilitamani kunywa sumu ili nami niondoke hapa duniani, hasa baada ya kuujua ukweli kuhusu maisha ya Rehema, mwanamke aliyenijali na kunipenda kwa dhati!
Niliendelea kusimama nikilitazama kaburi la Rehema kwa kitambo kirefu huku machozi yakinitoka. Nilifuta machozi nikashusha pumzi ndefu za ndani kwa ndani.
“Upumzike pema peponi Rehema… kamwe sitakusahau mpenzi!” nilisema kwa huzuni kisha nikainamisha kichwa changu mbele ya kaburi la rehema kama ishara ya kutoa heshima zangu za mwisho. Sikuweza kuendelea kusimama pale nikaondoka taratibu kwa huzuni, mikono yangu ikiwa nyuma.
MWISHO
Nalazimika kusema ahsante sana ndugu mwandishi kwa simulizi him matata.Nimeburudika vya kutosha,nimejifunza mambo mengi mno kutokana na simulizi hii, nimegundua kipaji chako kukubwa sana ulichonacho,hususani namna ulivyowatumia wahusika ipasavyo tena umewafafanua na kuwaelezea ki-utadi mkubwa mno.
Umewapa wahusika nguvu na umewavalisha uhusika kana kwamba nilipokuwa nasoma, nikawa kama nawaona ama kuwafahamu kabisa.Pia umewapa nguvu ya mamlaka ya kutenda,mfano wale majambazi wa pori la kibiti,Mr Bilall,Rehema na Adnan.
Visualization, nilisahau kuwa ni simulizi ya kutunga badala take nikafikiri ni simulizi ya kweli katika maisha halisi, hadi nikapatwa na uchungu Rehema alipojiua.
Makosa hayakosekani, mwandishi yani umeshindwa kabisa kutanabaisha ,baada ya hapo bwana Adnan alikwenda wapi? Jameela nae alikwenda Oman ? Je aliolewa? Na vipi uchunguzi wa majambazi kule kibiti, ulimalizikaje? Na je walikamatwa? Vipi mahusiano kati ya Adnan na Bwana Billal yaliendeleaje?.
Bwana Billal alikuwa Mkurugenzi katika kampuni yake, kwanini hakuwahi kwenda kazini hata baada ya kupona? Inamaana kampuni anaiendeshaje?, kila kukicha yeye kufuatilia mademu tu kweli?
Kuna kipindi bwana Billal alipanga aitishe semina ya kukuza kampuni yake, je hiyo nayo iliishia wapi?
Vipi lile dili la pesa alilokuwa analiwahi Dar Es Salaam bwana Billal, lilipotelea wapi?
Haya ni makosa baadhi tu, yazingatie ili kazi zijazo ziwe na weledi uliotukuka.
Ahsante.
Ahsante sana, majibu yako ni mazuri pia nimeridhika,heshima kwako mkuuNashukuru kwa maoni yako, lakini kumbuka kila mwandishi ana aina yake ya kuwakilisha na kumaliza stori yake, si lazima kila mtu amalize vile unavyodhani au kutaka.
Ulipaswa kwanza kujua ni nani aliyebeba stori, stori ilihusu nini na je, lengo lake limetimia? Hii siyo tamthilia kwamba kila aliyetajwa humu lazima tuone ameishia wapi...
Hata hivyo, kama ungefuatilia stori kwa makini kila kitu kimejibiwa, Jameela alikuja kuagana na Bilali kwani ndoa ilikuwa inanukia (ingawa si lazima kuonesha harusi yake kwa kuwa yeye siye aliyebeba stori), uhusiano kati ya Bilali na Adnan hakuna tena, au wewe ulitakaje? Habari ya polisi na wauaji haimhusu tena Bilali, alikwishatoa maelezo na polisi wakamweleza walipofikia lakini wakisisitiza kuwa hayo mengine hayamhusu.
Kumbuka: si lazima nimalize vile unavyotaka bali vile ninavyoiona hadithi yangu...
Sent using Jamii Forums mobile app
F.u.c.k you Bilal kwa kumfanyia Vibaya Rehema...Laiti Ningejua! 27
Mtunzi Bishop Hiluka
Nilimtazama nikatabasamu bila kusema neno. Mara nikaisikia sauti ya Rehema akisalimia na wapangaji pale kwenye korido kisha hatua za haraka zilikuja hadi kwenye mlango wangu, kisha zikasimama.
“Nani?” Tausi aliniuliza kwa sauti ndogo huku akifinya macho yake. Nilibetua mabega yangu na sikusema neno japo nilikwisha mjua aliyekuwa kasimama mlangoni.
Taratibu mlango wa pale sebuleni ulifunguliwa. Rehema akiwa amevaa sketi fupi nyeusi yenye miraba myeupe, blauzi ya bluu ya mikono mirefu na viatu vyenye vikanyagio virefu vya mchuchumio akaingia.
Endelea...
Mkononi alikuwa amevaa bangili nyingi za pembe na alikuwa amejimwagia mafuta mazuri yaliyosambaa chumba kizima. Alipoingia alisimama akitutazama kwa makini.
“Karibu Rehema,” niliongea huku nikiachia tabasamu. Sauti yangu ilikuwa tulivu sana. “Kutana na best wangu, Tausi…” nilimwambia Rehema kisha nikageuza shingo kumtazama Tausi, “Huyu ni dada yangu mpenzi, Rehema.”
Rehema aliachia tabasamu japo nilihisi halikuwa tabasamu halisi ila lilificha kitu ndani yake, alipiga hatua akaja kuketi kwenye kiti tupu karibu yangu huku akinitazama kwa makini kisha akayahamishia macho yake kwa Tausi.
Tausi akageuza shingo yake kunitazama kwa jicho la kuuliza lakini hakuthubutu kusema chochote. Niliachia tabasamu nikionekana kutobabaika kabisa, kikapita kimya kirefu, huku wanawake wote wawili wakinitazama kwa makini.
“Sijauelewa vizuri utambulisho wako, unaweza kunitambulisha tena huyu ni nani?” Rehema aliniuliza kwa sauti tulivu.
“Mwanamke,” lilikuwa jibu langu.
“Najua kuwa ni mwanamke, lakini nataka kujua yeye ni nani?”
“Nimeshakwambia anaitwa Tausi, hayo mengine wayatakia nini?” niliongea kwa kufoka.
Rehema alinitazama kwa makini, nikayaona machozi yakimlenga lenga kwenye macho yake, hakutaka kuendelea kukaa pale aliinuka na kuondoka haraka, akafungua mlango na kutoka kisha nikasikia muungurumo wa gari yake ilipokuwa ikiondoka na kupotelea mtaani.
Kwa kiasi fulani moyo wangu uliridhika kwa kitendo nilichomfanyia Rehema nikiamini kuwa baada ya siku ile angeniheshimu, maana nilijua kuwa alikuwa ananiona bwege. Moyoni mwangu nikaahidi kuendelea na vimbwanga vya hapa na pale hadi anyooke.
Tausi alinitazama kwa kitambo bila kusema neno, nilijua kuwa alikuwa amejisikia vibaya sana kwa kile kilichotokea kwa mwanamke mwenzake, japo sikujali, nilijitahidi kumsemesha lakini alibaki kimya akinitazama kwa makini. Kisha alishusha pumzi ndefu.
“Bilali, najua wewe ni kijana mtanashati sana na kila mwanamke angependa kuwa na wewe, lakini nimehuzunika sana kwa kuwa sipendi kugombanisha wapendanao, usingefanya uliyofanya, mimi ningeweza kuwapisha badala ya hiki kilichotokea,” Tausi alisema kwa uchungu.
Nilimtoa wasiwasi kuwa Rehema hakuwa mpenzi wangu bali tulizoeana tu kwa kuwa nilimsaidia kwenye lile tukio la kule Kibiti. Nilimsimulia kuhusu tukio zima lilivyokuwa na jinsi nilivyomuokoa Rehema hadi pale polisi walipokuja na mimi kupoteza fahamu.
Tausi aliamua kukubali yaishe lakini hakuonekana kuridhika na maelezo yangu.
Baada ya siku ile ilipita wiki nzima nikiwa sina mawasiliano na Rehema ingawa ukweli sikutaka uhusiano wetu uishie katika hali ile, niliamini kuwa Rehema alikuwa ananipenda ingawa sikujua kwa nini hakuwa tayari kushiriki tendo, bila sababu zozote za msingi.
Japo chozi la Rehema liliniumiza sana siku ile lakini sikujali. Kwa nini alikuwa ananinyima penzi? Nilijiuliza nikakosa majibu. Hatimaye nikafikia uamuzi wa kuachana naye. Lakini tatizo lilikuwa ningeachana naye vipi bila kumjua ladha yake?
Nilijiapia kuwa jambo hilo lisingewezekana hata kidogo, mimi kama mwanamume kamili angenitangaza kwa marafiki zake, kuwa sijawahi kulala naye tukafanya tendo. Ingekuwa aibu kubwa kwangu!
Ndiyo maana ilipopita wiki na Rehema hakuwa amenitafuta niliamua kujishusha, niliacha shughuli zangu na kwenda kwao kumtafuta. Nilipokuwa nakaribia nyumbani kwa kina Rehema mita chache mbele yangu nikawaona wanawake wawili waliokuwa wanatokea upande niliokuwa naelekea.
Nilishtuka kidogo nikiwa siamini macho yangu kuwa niliowaona mbele yangu ni Jameela na mwanamke mwingine wa makamo aliyekuwa na umbo kubwa lililovutia. Mwanamke yule alikuwa mrefu kama alivyokuwa Jameela na alikuwa mwarabu.
Mara moja nikagundua kuwa huyo ndiye yule shangazi yake aliyekuwa akinielezea habari zake. Mwanamke yule alikuwa na macho makubwa mazuri yaliyoambatana na kope nyingi nyeusi ambazo zilizoachia nafasi kwa nyusi ili zipate kujidai, na midomo yake ilikuwa minene yenye kingo nyepesi na mikunjo midogo midogo.
Jameela aliponiona aliongea kitu kwa yule mwanamke kwa sauti ya chini kisha akainua mikono yake kunipokea kwa uchangamfu.
“Wow Bilali,” alisema kwa bashasha huku akinipokea na kuongeza, “habari za nyumbani kwako?”
“Nzuri tu Jameela, sijui nyinyi?”
“Sisi tu wazima… kutana na shangazi yangu, Bi Aisha…” alinitambulisha kwa yule mama kisha alimgeukia, “Shangazi, kutana na Bilali Ibrahim, yulee…” alisema na kuachia kicheko hafifu, wote wakacheka.
Bi Aisha akanyoosha mkono wake na kunisalimia kwa bashasha huku akiachia tabasamu pana usoni kwake.
“Nimefurahi sana kukufahamu, maana kila siku nilikuwa najiuliza huyu Bilali yukoje maana tulikuwa hatuli wala hatulali, kila siku Bilali, Bilali!!” yule mwanamke aliongea kwa sauti ya kishambenga na kuendelea.
“Pole sana kwa mkasa uliokupata.”
“Nimekwisha poa, shikamoo,” nilimwamkia yule mama huku nikiwa na haya usoni kwangu.
“Marhaba… karibu nyumbani kwetu,” aliitikia huku akinikaribisha kwa ukarimu mno na kunionesha kwa kidole ilipo nyumba yao.
Nilishtuka sana maana nyumba aliyonionesha ilikuwa imepakana na nyumba aliyokuwa akiishi Rehema na mama yake mkubwa. Pia nilishtushwa sana kwa kuwa hata yeye pia aliitwa Bi Aisha.
“Twende ukapaone nyumbani kwetu, au kuna sehemu ulikuwa unaelekea?” aliniuliza Jameela baada ya kuona nipo kimya nikiwa nimenywea.
Nilishusha pumzi za ndani kwa ndani, nikatingisha kichwa. “Kuna mtu ninakwenda kumuona mara moja, ni muhimu sana maana muda wote ananisubiri mimi,” niliamua kuongopa ingawa ukweli nilikuwa nakwenda kwa Rehema.
Waliridhishwa na uongo wangu, lakini Jameela alisema kuwa baadaye angekuja nyumbani kuniona. Niliondoka nikiwa na maswali mengi kichwani, sikuwa nimefikiria kabisa kukutana na Jameela katika mazingira yale, nikawaza sana kuwa kumbe Jameela na Rehema walifahamiana!
Na kweli baadaye Jameela alikuja nyumbani na kuniambia kuwa alikuja kuniaga kwa kuwa harusi yake ilikuwa imekaribia, alisema kuwa alitafuta kila njia ya kuja ili tuagane na alikuja kulala kwangu na kesho yake angerudi Kibiti kwa ajili ya kukaa ndani kama ilivyokuwa desturi yao.
Nilipomuuliza kuhusu shangazi yake Jameela aliniambia kuwa anajua kila kitu na ni msiri wake, hivyo sikutakiwa kuwa na wasiwasi kabisa.
Aliichukua simu yangu na yake akazifungia ndani ya kabati. “Sihitaji simu yoyote saa hizi, leo ni mimi na wewe tu hadi lyamba,” alisema Jamila huku akitoa kila kitu na kubakiwa na nguo ya ndani tu, kisha akajibwaga juu ya kitanda.
Itaendelea...
Safi sana...Laiti Ningejua! 29
Mtunzi Bishop Hiluka
“Ukweli ni kwamba, unajua mimi ni bachela na wewe tayari una mtu na siku si nyingi mtafunga ndoa na kwenda kuishi Uarabuni…” nilisema huku nikimkazia macho. Jameela alinitazama kwa makini bila kusema neno.
“Hivi umejiuliza nitaishi vipi bila wewe au unadhani mimi sina wivu? Nimekubali matokeo na sioni sababu ya kuona wivu, kwa nini wewe ufanye hivi? Kumbuka umekuja tuagane, sasa kama kuagana kwenyewe ni kwa staili hii sawa, nakuruhusu uende,” nilisema kwa uchungu huku nikimpisha aondoke.
Jameela alinitazama kwa makini nikauona uso wake ukikunjuka na zile hasira zikaanza kuyeyuka, alishusha pumzi za ndani kwa ndani na kujipweteka juu ya kochi.
Endelea...
Nilimfuata pale kwenye kochi nikambembeleza na kuanza kuzitoa tena nguo zake na kuzitupa pale sakafuni moja baada ya nyingine hadi alipobakiwa na nguo ya ndani tu, kisha nikaanza tena kumpapasa.
“Bilali, nisamehe ni kwa kuwa nakupenda sana, unajua kuna wakati nafikiria kutoroka nyumbani, tutafute sehemu yoyote ambayo watu hawatujui tukaishi,” Jameela aliongea huku akinitazama machoni. Nikagundua kuwa alikuwa analengwa na machozi.
“Hata mimi ningetamani hivyo lakini…” nilishindwa kumalizia sentensi yangu baada ya kusikia muungurumo wa gari likifunga breki nje ya nyumba. Kumbe Jameela naye aliusikia ule muungurumo, tukatazamana.
“Rehema huyo karudi,” Jameela aliongea kwa sauti ya chini huku akinikazia macho kwa makini.
“Sidhani,” nilimjibu kwa wasiwasi huku nikijiuliza kama si yeye basi angekuwa nani?
“Na kama atakuwa ni yeye utafanyaje?” Jameela aliniuliza huku akiendelea kunitazama machoni kwa makini.
“Nitamtimua bila...” nilimjibu Jameela lakini sikuweza kumalizia sentensi yangu nikakatishwa na sauti ya mtu aliyekuwa anagonga mlango wangu kwa nguvu.
Aina ya ugongaji wa mlango ilinishtua kidogo, nikajiuliza ni nani aliyekuwa akigonga ule mlango. Mimi na Jameela tukatazamana katika hali ya kuulizana lakini hakuna aliyethubutu kuuliza. Ule mlango ukagongwa tena, lakini safari hii kwa nguvu zaidi.
Nilihisi donge la hasira likinikaba kooni kwangu, hasa nilipokumbuka kuwa huenda alikuwa ni Rehema aliamua kuja kunifanyia vurugu japokuwa alikuwa hataki kufanya ngono na mimi.
Niliinuka haraka nikiwa nimechukizwa na kuusogelea ule mlango nikiwa nina boksa tu tayari kwa kumkabili Rehema, nikaapa kuwa nitamfundisha adabu ili asisahau maishani mwake, nikashika kitasa cha mlango na kuufungua ule mlango huku nikiangalia nje kwa mategemeo ya kumuona Rehema akiwa kasimama mlangoni.
Nilichokiona kikanifanya kupigwa na butwaa, nilijikuta nikiganda kama sanamu nisijue nini nifanye. Adnan alikuwa amesimama nje ya mlango wangu akinitazama huku tabasamu pana la kirafiki likichanua usoni kwake.
Nilijikuta nashindwa kufanya lolote, nikabaki nimekodoa macho yangu kama nilikuwa nimeona mzuka au kitu cha kutisha, nilitamani ardhi ipasuke ili niingie ndani yake kuepuka aibu amabayo ingenikuta muda mfupi baadaye.
Adnan alinitazama kwa makini kuanzia chini hadi juu na kuangua kicheko hafifu huku akiongea kwa sauti ya kunong’ona. “Samahani ndugu yangu kwa kuvuruga starehe yako, kumbe upo na shemeji...”
Nilitaka kusema neno lakini sauti ilikuwa haitoki, nikaishia kufumbua mdomo tu huku nikiendelea kumkodolea macho.
“Basi ngoja niende kwanza kwa shangazi nitarudi baadaye,” Adnan alinong’ona tena na kuanza kupiga hatua kutaka kuondoka.
“Baby, kwani ni nani huyo?” nilisikia sauti ya Jameela ikiniuliza na hapo hapo nikamuona Adnan akisita na moja kwa moja macho yake yakatazama kwa makini kitu kilichokuwa nyuma yangu. Nami nikageuza haraka shingo yangu kutazama nyuma.
Lahaula! Niliishiwa kabisa nguvu baada ya kumuona Jameela akija na kusimama nyuma yangu huku akilalia mgongo wangu na kuchungulia nje ya mlango kumtazama mgeni aliyekuwa akiongea kwa sauti ya chini pale mlangoni. Pasipo kujua kilichokuwa kinaendelea Jameela alikuwa amekuja kuchungulia.
Macho ya Jameela na ya Adnan yalikutana na Jameela akashtuka sana kama aliyekuwa amepigwa na shoti ya umeme, aliruka kurudi nyuma lakini tayari alikuwa amechelwa, kwani Adnan alikuwa amemuona na kumtambua.
Assalale! Mwili wangu ulizizima kwa hofu kama uliopatwa ganzi, kilichotokea pale ilikuwa ni songombingo ambalo liliniachia aibu kubwa isiyoelezeka pale mtaani, Adnan alikasirika sana huku akiwa hayaamini macho yake.
Kama mtu aliyepandwa na wazimu Adnan alirudi nyuma hatua moja na kuruka kwa nguvu zote, alinivamia na kunipiga kikumbo kilichoniangusha chini. Msukumo wa nguvu wa kikumbo hicho ulinitupa chini kwa mshindo mkubwa na kunifanya kugaragara pale sakafuni kama mtu mwenye kifafa.
Wakati huo huo na yeye alianguka kwa kishindo katikati ya sebule kutokana na ile nguvu kubwa aliyoitumia. Jameela alipoona kuwa kaka yake ameanzisha vurugu alipiga kelele ya hofu na kukimbilia chumbani, akajifungia kwa funguo.
Adnan alinirukia tena, mapigano na tifu la aina yake lililozuka pale vilisababisha watu kujaa mlangoni na madirishani na hivyo kujionea sinema ya bure.
Sikukubali, huku nikiwa na boksa tu niliamua kupambana kiume ili nisije kuadhirika, hivyo niliinuka haraka lakini Adnan alikuwa mwepesi, aliruka kama mkizi akanikumba, wote tukapiga mweleka sakafuni. Nikiwa bado nipo sakafuni Adnan aliwahi kusimama huku hasira zikiwa zimempanda kichwani kama mbogo aliyejeruhiwa.
Aliwahi akanikwida shingoni na kiunoni kisha akaninyanyua juu juu kama Joh Cena, yule mcheza mieleka na kunibwaga juu ya meza ya kioo iliyokuwa pale sebuleni. Vioo vilipasuka vipande vipande na kuniumiza mgongo, nilihisi maumivu makali yasiyoelezeka na kupiga yowe kali huku nikijitahidi kusimama.
Hata hivyo, Adnan alionekana kuwa mpiganaji wa kiwango cha juu huku akionekana kuwa makini sana akizisoma nyendo zangu. Akiwa amepandwa na hasira aliruka na kunivaa akanipiga kichwa kikavu kilichonipata katikati ya macho na pua.
Damu zikaanza kunitoka puani utadhani mrija wa maji uliopasuka! Nilisalimu amri na kushika pua yangu nikaiminya nikijaribu kuzuia damu isiendelee kunitoka, na wakati nikiizuia damu isitoke Adnan alinirukia na kunikaba kabali ya nguvu.
Nilijitahidi kukukuruka kutaka kujitoa kwenye ile kabali lakini Adnan alizidisha kabali yake na kunifanya kuanza kuishiwa nguvu. Mwisho wa siku mchezo uliisha huku Adnan akiibuka mshindi na kuondoka na Jameela huku wakiniacha naendelea kuvuja damu.
Itaendelea...
Cc the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, Mine eyes, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY
Inahuzunisha sana...Laiti Ningejua! 33
Mtunzi Bishop Hiluka
Mara akatokwa na kelele kubwa zilizonishtua sana ambazo sikuwa nimezitegemea kabisa. Sikujua kama angeweza kufanya kitendo kile.
“Ananibakaaaaa! Nisaidieeni ananibaaaka!” Alipiga kelele kubwa, nilimshika nikajaribu kumziba mdomo lakini alining’ata na kunifanya niugulie kwa maumivu. Kisha akaendelea kupiga kelele ambazo ziliwafanya wasamalia wema kukimbilia pale zilipokuwa zikisikika kelele.
Mara mlango wangu ukapigwa kumbo na watu wakaingia na kunikuta nikiwa juu ya Rehema, wakaninivagaa na kuanza kunishushia kipigo. Nilijaribu kujitetea lakini walizidi kunishushia kipigo hadi nikapoteza fahamu na sikujua tena kilichoendelea baada ya hapo.
______
Nilipozinduka nilijikuta nikiwa katika hospitali ya Amana nikiwa na majeraha mwilini huku nimefungwa pingu mkononi iliyounganishwa na kitanda. Nilikuwa na maumivu makali sana mwili mzima. Nikajaribu kukumbuka kilichonitokea na mara nikakumbuka kuwa nilifumaniwa nikitaka kufanya ubakaji.
Nilipogeuka kutazama upande mwingine macho yangu yalikutana na macho ya ofisa wa polisi aliyekuwa na cheo cha Sajenti ambaye alikuwa kaketi pembeni kwenye kiti akinitazama kwa makini huku kakunja sura yake.
Niliendelea kuwepo pale hospitali kwa siku tatu na baada ya nguvu kunirejea mwilini niliondolewa pale hospitali nikapelekwa mahabusu ya kituo cha polisi cha Buguruni. Nilikaa pale mahubusu nikisubiri kufunguliwa kesi mbaya ya ubakaji.
Siku iliyofuata wakati nikiwa nimejikunyata kwenye kona ya chumba cha mahabusu nilishuhudia lango la mahabusu ile likifunguliwa na askari mmoja ambaye aliita jina langu. Kwa unyonge niliinua shingo yangu kumtazama yule askari ambaye alikuwa na cheo cha Koplo.
“We mbakaji, inuka unifuate!” alisema baada ya kuona namtazama kwa wasiwasi.
Mahabusu wote katika kile chumba walinitazama kwa makini, baadhi yao walinihurumia lakini wengine walitabasamu kwa kejeli. Niliinuka kwa unyonge nikamfuata yule askari, aliniongoza tukipita kwenye korido hadi kwenye mlango wa ofisi ya mkuu wa kituo.
Tulipoingia ndani ya ofisi ile ya mkuu wa kituo nilipigwa butwaa baada ya kumkuta mama yake mkubwa na Rehema, Bi Aisha akiwa kwenye ile ofisi na Mkuu wa Kituo kile, Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP), Shaban Mungi, ambaye alikuwa kajiegemeza kwenye kiti chake cha kuzunguka. Wote waligeuka kunitazama kwa makini nilipokuwa naingia.
Nilijikuta nagwaya baada ya kuhisi uwepo wa hali ya majonzi na ukimya mzito sana ndani ya ile ofisi. Nilipowatupia jicho la wizi niliowakuta mle ofisini niliona huzuni kwenye macho yao. Mkuu wa kituo alinionesha kiti, nikaketi nikiwa na wasiwasi mkubwa.
Mkuu wa kituo aliendelea kunitazama kwa macho yaliyokuwa yameficha kitu nyuma yake. Sikuweza kujua nini kilichokuwa kikiendelea pale, nikajiuliza, yuko wapi Rehema?
Nilianza kuingiwa wasiwasi, hata hivyo, nilibaki kimya nikiwatazama wote kwa makini ingawa nilianza kuhisi kuwa kulikuwa na jambo lisilo la kawaida lililokuwa limetokea. Niliogopa kuuliza. Bi Aisha alinitazama akashindwa kuvumilia, nilimuona akiinuka na kutoka nje huku akilia kwa uchungu mkubwa.
Mkuu wa kituo alishusha pumzi na kufungua droo moja katika meza yake, kisha akatoa bahasha ndogo iliyokuwa na barua ndani yake, akaishika vizuri ile bahasha mkononi mwake huku akinitazama kwa huzuni.
“Bilali, kuanzia sasa uko huru, shika barua yako!” aliniambia huku akinyoosha mkono wake kunipa ile bahasha.
Kauli ya yule mkuu wa kituo cha polisi ikanishangaza sana, nilidhani labda nilikuwa ndotoni na mara ningeamka ningekuta mambo hayapo hivyo, lakini yule mkuu wa kituo aliendelea kunyoosha mkono wake kunitaka nichukue ile barua.
Nilimtazama usoni kutaka kuona kama kweli hatanii kisha nikaipokea ile barua huku mikono yangu ikitetemeka, ilitetemeka kwa sababu sikujua ilitoka wapi na ilihusu nini. Niliitazama ile barua kwa wasiwasi.
“Unaweza kusoma hapa hapa ukipenda!” yule mkuu wa kituo aliniambia huku akifuta machozi yake. Nikiwa na wasiwasi niliifungua ile bahasha na ndani yake kulikuwa na barua ndefu iliyotoka kwa Rehema.
“Mpenzi Bilali, haikuwa nia yangu kukusababishia kipigo kikali na kuitwa mbakaji, bali nimefanya haya kwa sababu nakupenda kutoka moyoni na ninapenda uishi miaka mingi…
“Bilali ni wewe mwanaume pekee niliyetokea kuvutiwa nawe kihisia ukauteka moyo wangu na kujikuta nikiwa mtumwa wa mahaba yako japo ulijaribu sana kuniumiza kihisia lakini bado sikuacha kukupenda…
“Ni kweli sikutaka kulala na wewe kwa kuwa nina kasoro kubwa ambayo hainipi hadhi ya kulala kitanda kimoja na wewe, sikutaka kuwa muuaji kwa kuruhusu unibake… hivi, Bilali unadhani mpapaso wako haukunisisimua? Nilisisimka hasa na nilitamani nikutimizie kwa hiari kile ulichotaka, labda mimi nilikuwa muhitaji kuliko wewe mpenzi, lakini… lakini nisingeweza kukuua…
“Bilali, wala usisikitike kusikia hili, mimi nimefurahi sana kufa nikiupigania uhai wa mwanaume niliyempenda, ninayempenda na ninayekufa kwa ajili yake. Kifo hiki kiwe kumbukumbu yako milele kuwa nilikupenda sana…
“Nilitaka kukwambia lakini nilishindwa, nimekuwa nikiishi na virusi vya UKIMWI kwa muda mrefu baada ya kuambukizwa na wazazi wangu… nilizaliwa nikiwa na Virus vya Ukimwi, na mama kabla ya kufa alinikanya kuwa ni heri nife peke yangu kuliko kuua yeyote asiyekuwa na hatia…
“Kwa kuwa utaalamu umeongezeka nilikubali unioe kwa kuwa tungefuata ushauri wa kitaalamu ili nisikuambukize, maana wewe huna hatia na haustahili kufa… laiti kama ungenibaka basi leo hii ningekufa nikiwa muuaji…
“Ninafurahi kuwa nakufa kama shujaa. Ninayaandika haya huku chupa ya sumu ikiwa pembeni yangu, nakufa leo lakini nimewaomba wakuache uwe huru. Bahati nzuri mkuu wa kituo ni baba yangu mdogo hivyo naamini atakuacha uwe huru, huru kabisa, wakati mimi nikiungana na mama yangu nimweleze kuwa sikuwahi kuua duniani na nimeamua kuondoka ili siku moja nisije kuua yeyote. Buriani Bilali, mpenzi wa moyo wangu…”
Sikujua kilichoendelea baada ya pale kwani niliishiwa nguvu, moyo wangu ukashikwa na mfadhaiko, mikono yangu ilikuwa inatetemeka na jasho jingi likaanza kunitoka sehemu mbalimbali za mwili wangu.
Macho yangu nayo yakaanza kupoteza nguvu ya kuona na hatimaye shughuli mbalimbali za mwili wangu nazo nikazihisi kuwa zilikuwa mbioni kusitisha utendaji wake.
______
Siku mbili baadaye nilikwenda kwenye makaburi ya Kisutu ambako Rehema alikuwa amezikwa, nilisimama mbele ya kaburi jipya la Rehema na kulitazama kwa huzuni, nikafuta machozi yaliyokuwa yakinilengalenga.
Haikuwa ndoto, ni kweli ilitokea kuwa Rehema alijiua kwa sumu na kuzikwa… barua ile niliyopewa ilikuwa imetwa kando ya mwili wake chumbani… sasa macho ya watu yalikuwa yakinitazama kwa kunisuta, wapo waliokuwa na hasira juu yangu, wapo ambao walinitazama kwa dharau na baadhi walinitazama kwa huzuni. Kwa kweli sikujua nifanye nini!
Nilitamani ardhi ipasuke ili nijifiche chini ya ardhi kukwepa macho ya jamii. Nilitamani kunywa sumu ili nami niondoke hapa duniani, hasa baada ya kuujua ukweli kuhusu maisha ya Rehema, mwanamke aliyenijali na kunipenda kwa dhati!
Niliendelea kusimama nikilitazama kaburi la Rehema kwa kitambo kirefu huku machozi yakinitoka. Nilifuta machozi nikashusha pumzi ndefu za ndani kwa ndani.
“Upumzike pema peponi Rehema… kamwe sitakusahau mpenzi!” nilisema kwa huzuni kisha nikainamisha kichwa changu mbele ya kaburi la rehema kama ishara ya kutoa heshima zangu za mwisho. Sikuweza kuendelea kusimama pale nikaondoka taratibu kwa huzuni, mikono yangu ikiwa nyuma.
MWISHO
Ndiyo hivyo, huwa inatokea wakati mwingine anakufa asiye na hatia na kumwacha mhalifu anaendelea kupeta. Mwisho wa siku lazima tujiulize tumejifunza nini...