Stori ya kusisimua - Laiti Ningejua!

Stori ya kusisimua - Laiti Ningejua!

Laiti Ningejua! 29

Mtunzi Bishop Hiluka

“Ukweli ni kwamba, unajua mimi ni bachela na wewe tayari una mtu na siku si nyingi mtafunga ndoa na kwenda kuishi Uarabuni…” nilisema huku nikimkazia macho. Jameela alinitazama kwa makini bila kusema neno.

“Hivi umejiuliza nitaishi vipi bila wewe au unadhani mimi sina wivu? Nimekubali matokeo na sioni sababu ya kuona wivu, kwa nini wewe ufanye hivi? Kumbuka umekuja tuagane, sasa kama kuagana kwenyewe ni kwa staili hii sawa, nakuruhusu uende,” nilisema kwa uchungu huku nikimpisha aondoke.

Jameela alinitazama kwa makini nikauona uso wake ukikunjuka na zile hasira zikaanza kuyeyuka, alishusha pumzi za ndani kwa ndani na kujipweteka juu ya kochi.

Endelea...

Nilimfuata pale kwenye kochi nikambembeleza na kuanza kuzitoa tena nguo zake na kuzitupa pale sakafuni moja baada ya nyingine hadi alipobakiwa na nguo ya ndani tu, kisha nikaanza tena kumpapasa.

“Bilali, nisamehe ni kwa kuwa nakupenda sana, unajua kuna wakati nafikiria kutoroka nyumbani, tutafute sehemu yoyote ambayo watu hawatujui tukaishi,” Jameela aliongea huku akinitazama machoni. Nikagundua kuwa alikuwa analengwa na machozi.

“Hata mimi ningetamani hivyo lakini…” nilishindwa kumalizia sentensi yangu baada ya kusikia muungurumo wa gari likifunga breki nje ya nyumba. Kumbe Jameela naye aliusikia ule muungurumo, tukatazamana.

“Rehema huyo karudi,” Jameela aliongea kwa sauti ya chini huku akinikazia macho kwa makini.

“Sidhani,” nilimjibu kwa wasiwasi huku nikijiuliza kama si yeye basi angekuwa nani?

“Na kama atakuwa ni yeye utafanyaje?” Jameela aliniuliza huku akiendelea kunitazama machoni kwa makini.

“Nitamtimua bila...” nilimjibu Jameela lakini sikuweza kumalizia sentensi yangu nikakatishwa na sauti ya mtu aliyekuwa anagonga mlango wangu kwa nguvu.

Aina ya ugongaji wa mlango ilinishtua kidogo, nikajiuliza ni nani aliyekuwa akigonga ule mlango. Mimi na Jameela tukatazamana katika hali ya kuulizana lakini hakuna aliyethubutu kuuliza. Ule mlango ukagongwa tena, lakini safari hii kwa nguvu zaidi.

Nilihisi donge la hasira likinikaba kooni kwangu, hasa nilipokumbuka kuwa huenda alikuwa ni Rehema aliamua kuja kunifanyia vurugu japokuwa alikuwa hataki kufanya ngono na mimi.

Niliinuka haraka nikiwa nimechukizwa na kuusogelea ule mlango nikiwa nina boksa tu tayari kwa kumkabili Rehema, nikaapa kuwa nitamfundisha adabu ili asisahau maishani mwake, nikashika kitasa cha mlango na kuufungua ule mlango huku nikiangalia nje kwa mategemeo ya kumuona Rehema akiwa kasimama mlangoni.

Nilichokiona kikanifanya kupigwa na butwaa, nilijikuta nikiganda kama sanamu nisijue nini nifanye. Adnan alikuwa amesimama nje ya mlango wangu akinitazama huku tabasamu pana la kirafiki likichanua usoni kwake.

Nilijikuta nashindwa kufanya lolote, nikabaki nimekodoa macho yangu kama nilikuwa nimeona mzuka au kitu cha kutisha, nilitamani ardhi ipasuke ili niingie ndani yake kuepuka aibu amabayo ingenikuta muda mfupi baadaye.

Adnan alinitazama kwa makini kuanzia chini hadi juu na kuangua kicheko hafifu huku akiongea kwa sauti ya kunong’ona. “Samahani ndugu yangu kwa kuvuruga starehe yako, kumbe upo na shemeji...”

Nilitaka kusema neno lakini sauti ilikuwa haitoki, nikaishia kufumbua mdomo tu huku nikiendelea kumkodolea macho.

“Basi ngoja niende kwanza kwa shangazi nitarudi baadaye,” Adnan alinong’ona tena na kuanza kupiga hatua kutaka kuondoka.

“Baby, kwani ni nani huyo?” nilisikia sauti ya Jameela ikiniuliza na hapo hapo nikamuona Adnan akisita na moja kwa moja macho yake yakatazama kwa makini kitu kilichokuwa nyuma yangu. Nami nikageuza haraka shingo yangu kutazama nyuma.

Lahaula! Niliishiwa kabisa nguvu baada ya kumuona Jameela akija na kusimama nyuma yangu huku akilalia mgongo wangu na kuchungulia nje ya mlango kumtazama mgeni aliyekuwa akiongea kwa sauti ya chini pale mlangoni. Pasipo kujua kilichokuwa kinaendelea Jameela alikuwa amekuja kuchungulia.

Macho ya Jameela na ya Adnan yalikutana na Jameela akashtuka sana kama aliyekuwa amepigwa na shoti ya umeme, aliruka kurudi nyuma lakini tayari alikuwa amechelwa, kwani Adnan alikuwa amemuona na kumtambua.

Assalale! Mwili wangu ulizizima kwa hofu kama uliopatwa ganzi, kilichotokea pale ilikuwa ni songombingo ambalo liliniachia aibu kubwa isiyoelezeka pale mtaani, Adnan alikasirika sana huku akiwa hayaamini macho yake.

Kama mtu aliyepandwa na wazimu Adnan alirudi nyuma hatua moja na kuruka kwa nguvu zote, alinivamia na kunipiga kikumbo kilichoniangusha chini. Msukumo wa nguvu wa kikumbo hicho ulinitupa chini kwa mshindo mkubwa na kunifanya kugaragara pale sakafuni kama mtu mwenye kifafa.

Wakati huo huo na yeye alianguka kwa kishindo katikati ya sebule kutokana na ile nguvu kubwa aliyoitumia. Jameela alipoona kuwa kaka yake ameanzisha vurugu alipiga kelele ya hofu na kukimbilia chumbani, akajifungia kwa funguo.

Adnan alinirukia tena, mapigano na tifu la aina yake lililozuka pale vilisababisha watu kujaa mlangoni na madirishani na hivyo kujionea sinema ya bure.

Sikukubali, huku nikiwa na boksa tu niliamua kupambana kiume ili nisije kuadhirika, hivyo niliinuka haraka lakini Adnan alikuwa mwepesi, aliruka kama mkizi akanikumba, wote tukapiga mweleka sakafuni. Nikiwa bado nipo sakafuni Adnan aliwahi kusimama huku hasira zikiwa zimempanda kichwani kama mbogo aliyejeruhiwa.

Aliwahi akanikwida shingoni na kiunoni kisha akaninyanyua juu juu kama Joh Cena, yule mcheza mieleka na kunibwaga juu ya meza ya kioo iliyokuwa pale sebuleni. Vioo vilipasuka vipande vipande na kuniumiza mgongo, nilihisi maumivu makali yasiyoelezeka na kupiga yowe kali huku nikijitahidi kusimama.

Hata hivyo, Adnan alionekana kuwa mpiganaji wa kiwango cha juu huku akionekana kuwa makini sana akizisoma nyendo zangu. Akiwa amepandwa na hasira aliruka na kunivaa akanipiga kichwa kikavu kilichonipata katikati ya macho na pua.

Damu zikaanza kunitoka puani utadhani mrija wa maji uliopasuka! Nilisalimu amri na kushika pua yangu nikaiminya nikijaribu kuzuia damu isiendelee kunitoka, na wakati nikiizuia damu isitoke Adnan alinirukia na kunikaba kabali ya nguvu.

Nilijitahidi kukukuruka kutaka kujitoa kwenye ile kabali lakini Adnan alizidisha kabali yake na kunifanya kuanza kuishiwa nguvu. Mwisho wa siku mchezo uliisha huku Adnan akiibuka mshindi na kuondoka na Jameela huku wakiniacha naendelea kuvuja damu.

Itaendelea...

Cc the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, Mine eyes, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY
Tuko pamoja as usual mkuu Bishop, shukran sana

the Legend☆
 
Laiti Ningejua! 32

Mtunzi Bishop Hiluka

Japo alikuwa na umbo kubwa lakini kifua chake kilibeba matiti ya wastani na tumbo lake lilikuwa flati huku kiuno chake kikiwa chembamba mithili ya dondola. Miguu yake ilikuwa mizuri mno iliyotazamika.

Mwanadada yule alikuwa amevaa gauni zuri la kitenge na alikadiriwa kuwa na miaka kati ya 25 na 28. Alikuwa amesimama pale akimtazama sana Rehema kama aliyekuwa akimfananisha.

Mara Rehema akainua uso wake na kumtupia jicho yule mwanadada kisha akanitazama kwa makini.

Endelea...

Nilimtazama tena yule mwanadada kwa makini lakini sikumfahamu kabisa hivyo sikuwa na hofu kama angeweza kuwa mmoja wa wasichana niliofahamiana nao. Nikageuza tena shingo yangu kumtazama Rehema ambaye aliendelea kumtazama yule mwanadada katika namna ya kumfananisha. Wakaendelea kutazamana kwa makini zaidi kwa kitambo kirefu.

“Unamfahamu?” nilimuuliza Rehema huku nikimkazia macho.

“Namkumbuka, lakini sura yake inanijia na kutoka,” alisema rehema huku akiendelea kumtazama yule mwanadada.

Yule mwanadada akatafuta kiti akaketi huku akigeuka tena kumtazama Rehema, kisha akaachia tabasamu pana na kuinuka akitufuata pale tulipoketi.

“Rehema, umenisahau?” yule mwanadada aliuliza huku akiketi kwenye kiti karibu ya Rehema.

Rehema akaachia tabasamu. “Sura naikukumbuka lakini umen’toka kidogo. Nikumbushe basi.”

“Miye Joyce.”

Rehema akamtazama kwa makini na kuonesha kumkumbuka. “Joyce… Mgaya, siyo?”

“Ee… Joyce Mgaya. Si tulikuwa pamoja pale Forodhani Secondary au umesahau?”

“Ndiiiiyooo! Mtumeeee! Ndiyo uko hivi, babu wee! Umekuwa bonge!”

Joyce akacheka sana huku akimshika Rehema begani. “Ndiyo hivyo tena! Nimeridhika mwenziyo!” alisema Joyce na kugeuza shingo yake kunitazama kwa makini huku akiangua kicheko cha kishambenga. Rehema akatabasamu tu.

Nilimtupia jicho la wizi Joyce hukunami nikitabasamu.

“Vipi, ndiye shemegi huyu?” Joyce aliuliza kwa bashasha huku akinikazia macho.

“We nawe! Hujaacha tu, hata hungoji kutambulishwa?” Rehema alisema huku akiguna na kugeuka kunitazama kisha akaachia tabasamu.

“Aa babu, ngoja ngoja yaumiza matumbo ati!”

“Okay… ni shemeji yako mtarajiwa,” Rehema alisema huku akinishika mkono wangu na akuviminya minya vidole vyangu vya mkono.

Joyce akanyoosha mkono wake kwa bashasha kunisalimia. Na mimi nikanyoosha mkono wangu na kukutanisha na mkono wake. Tukasalimiana.

“Ooh shemegi, nimefurahi sana kukufahamu!” alisema Joyce kwa uchangamfu. Nikaachia tabasamu huku nikibetua kichwa changu bila kusema neno.

“Umeshaolewa, Joyce?” Rehema alimuuliza Joyce huku akimtazama kwa makini.

“Hee! Zamani gani! Lile balaa lilipokwisha tu nikaolewa. Si uliyasikia yaliyonikuta mwenziyo baada ya kifo cha mama yangu?”

“Niliyasikia! Pole sana mwaya! Halafu nikasikia sakata lile lilikufanya ukalazwa Muhimbili. Ni kweli?”

“Kweli! Yule mama aling’ang’ania mpaka baba akanileta bila ya miye mwenyewe kupenda. Lakini sikukaa siku nyingi nikatoroka,” alisema Joyce na kuachia kicheko cha kishambenga.

“Lo! Pole sana, na yule kaka’ko… Michael, yuko wapi siku hizi?”

“Alikwenda zake Sauzi Afrika! Yule ndiyo basi tena, nasikia ana jimama la Kisauzi linamlea!” Joyce alisema na kuachia tena kicheko cha kishambenga.

Waliendelea kuongea na kukumbushana mengi tangu walipokuwa shule, wakati huo mimi nilikuwa kimya tu nikiwasikiliza. Joyce alikuwa mcheshi na muongeaji sana, kiasi kwamba ilikuwa vigumu kumchoka.



* * * * *



Jioni ya siku ile baada ya kuachana na Rehema nilikuwa nimetulia sebuleni kwangu juu ya sofa nikiwa nawaza sana, kwani pamoja na juhudi zote za kumshawishi sana Rehema lakini aliendelea kusisitiza kuwa mbali nami.

Pale sebuleni nilikuwa nimewasha runinga na muda ule nilikuwa nimeweka chaneli iliyokuwa ikionesha kipindi cha wanyama. Japo nilikuwa nimetulia na macho yangu yalikodolea kwenye runinga lakini ukweli sikuwa nikiona chochote kwenye ile runinga.

Muda wote nilikuwa namfikiria Rehema tu na sikujua nifanye nini ili kuurudisha moyo wake kwangu.

Mbele yangu juu ya meza kulikuwa na chupa kubwa ya konyagi, chupa ya soda Sprite na bilauri moja. Tayari nilikuwa nimeshakunywa nusu na niliendelea kumimina pombe kwenye bilauri na kuchanganya na soda, kisha nikanyanyua bilauri na kuinywa pombe yote iliyomo ndani yake na kuikita ile bilauri juu ya meza huku nikisisimkwa.

Kijasho kikaanza kunitoka usoni, nikaijaza tena pombe ile bilauri na kuitazama kwa makini lakini kabla sijainywa nikasikia sauti ya mtu akigonga mlango. Nilinyanyuka na kwenda kuufungua ule mlango kisha nikachungulia nje.

Rehema alikuwa kasimama mbele yangu huku akiniangalia kwa wasiwasi jinsi ambavyo jasho lilikuwa linanitoka usoni kutokana na ile pombe niliyokunywa. Nilibaki nikimkodolea Rehema kwa macho ya kilevi. Rehema alinitazama kwa makini na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.

Nilimpisha nikikaribisha ndani, bila kujivunga Rehema aliingia ndani na kuketi kwenye kochi huku akinitazama kwa makini. “Unakunywa pombe?” aliniuliza kwa mshangao mkubwa.

Sikumjibu, niliinua tena ile bilauri nikaigida ile pombe yote na kuikita ile bilauri juu ya meza huku nikisisimkwa sana. Rehema alitingisha kichwa chake kwa huzuni huku akiinuka na kuichukua ile chupa ya konyagi akaiondoa pale mbele yangu.

“Kwa nini unakunywa pombe? Ni kipi kibaya nimekifanya hadi uchukue uamuzi huu wa kunywa pombe?” Rehema aliniuliza huku akinitazama kwa makini. Sikumjibu bali nilitulia tu kama sanamu huku nikimwangalia kwa matamanio.

Akiwa bado amezubaa akinitazama kwa mshangao nilimsogelea nikapeleka mikono yangu na kuipapasa shingo yake. Rehema aliendelea kunitazama, nikashusha mikono yangu na kuanza kumgusa matiti yake madogo yaliyosimama wima yakijitahidi kunidhihaki. Na yalifanikiwa hasa hasa kunikebehi.

Nikamgusa huku na kule akiwa ametulia tu akinitazama. Nilipotaka kumvua nguo akanizuia na alipogundua nilichokuwa nataka kufanya akagutuka na kujaribu kujitoa kwenye mikono yangu. Sikutaka kumpa nafasi, nikazidi kumng’ang’ania.

Nilikuwa nimekunywa pombe kiasi hivyo sikuwa na aibu, nikaamua kutumia nguvu, niliamua kumbaka kama angeendelea kushikilia msimamo wake na kutoniruhusu kuzitoa nguo zake kistaarabu.

Pepo mbaya wa ngono alikuwa amefanikiwa kuikamata nafsi yangu, sikutaka tena kungoja, nikazirarua nguo zake kisha nikaichana sidiria yake, na hatimaye nikaiondoa nguo yake ya ndani, sasa akabaki mtupu kabisa kama alivyozaliwa huku harufu nzuri ya manukato yake ikinishawishi kuendelea na hatua inayofuata.

Nilipouona mwili wake mtupu msisimko wa mapenzi ukanitambaa mwilini na sasa mapigo yangu ya moyo yakaanza kwenda mbio isivyo kawaida. Nilimtazama kwa uchu kama vile fisi atazamavyo mzoga. Rehema alihaha huku na kule asiamini kile kilichokuwa kinatokea mbele yake.

Please, let me go. Leave me please!” (Tafadhali, niache niende. Niache tafadhali) rehema alilia kwa uchungu huku akinibembeleza. Sikutaka kabisa kumsikiliza.

Akajitahidi kujitoa mikononi mwangu na kufanikiwa. “Have you gone crazy?” (Umechanganyikiwa?) Rehema aliniuliza huku akinitazama kwa hofu.

Akataka kukimbilia nje uchi lakini nikamdaka mkono na kumsukumia juu ya kochi ili niweze kutimiza lengo langu… Kamwe sikuwahi kumwona binti yule akiwa katika uoga namna ile! Alikuwa amekodoa macho yake… na alikuwa anatetemeka.

Niliitoa fulani niliyokuwa nimeivaa na kuitupa chini kisha nikafungua mkanda wa suruali na kuivuta suruali yangu nikiiacha idondoke chini, ikadondoka na kubakiwa na boksa.

Muda ule sikuwa na huruma hata kidogo, nilichotaka ni kitu kimoja tu, ngono. Nifanye naye ngono kisha akinichukia na achukie. Nikazidi kumtazama kwa matamanio huku nikihema kwa nguvu kutokana na ashki, nikamrukia.

Mara akatokwa na kelele kubwa zilizonishtua sana ambazo sikuwa nimezitegemea kabisa. Sikujua kama angeweza kufanya kitendo kile.

“Ananibakaaaaa! Nisaidieeni ananibaaaka!” Alipiga kelele kubwa, nilimshika nikajaribu kumziba mdomo lakini alining’ata na kunifanya niugulie kwa maumivu. Kisha akaendelea kupiga kelele ambazo ziliwafanya wasamalia wema kukimbilia pale zilipokuwa zikisikika kelele.

Mara mlango wangu ukapigwa kumbo na watu wakaingia na kunikuta nikiwa juu ya Rehema, wakaninivagaa na kuanza kunishushia kipigo. Nilijaribu kujitetea lakini walizidi kunishushia kipigo hadi nikapoteza fahamu na sikujua tena kilichoendelea baada ya hapo.

Itaendelea...

Cc the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, Mine eyes, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY
 
Laiti Ningejua! 33

Mtunzi Bishop Hiluka

Mara akatokwa na kelele kubwa zilizonishtua sana ambazo sikuwa nimezitegemea kabisa. Sikujua kama angeweza kufanya kitendo kile.

“Ananibakaaaaa! Nisaidieeni ananibaaaka!” Alipiga kelele kubwa, nilimshika nikajaribu kumziba mdomo lakini alining’ata na kunifanya niugulie kwa maumivu. Kisha akaendelea kupiga kelele ambazo ziliwafanya wasamalia wema kukimbilia pale zilipokuwa zikisikika kelele.

Mara mlango wangu ukapigwa kumbo na watu wakaingia na kunikuta nikiwa juu ya Rehema, wakaninivagaa na kuanza kunishushia kipigo. Nilijaribu kujitetea lakini walizidi kunishushia kipigo hadi nikapoteza fahamu na sikujua tena kilichoendelea baada ya hapo.

______

Nilipozinduka nilijikuta nikiwa katika hospitali ya Amana nikiwa na majeraha mwilini huku nimefungwa pingu mkononi iliyounganishwa na kitanda. Nilikuwa na maumivu makali sana mwili mzima. Nikajaribu kukumbuka kilichonitokea na mara nikakumbuka kuwa nilifumaniwa nikitaka kufanya ubakaji.

Nilipogeuka kutazama upande mwingine macho yangu yalikutana na macho ya ofisa wa polisi aliyekuwa na cheo cha Sajenti ambaye alikuwa kaketi pembeni kwenye kiti akinitazama kwa makini huku kakunja sura yake.

Niliendelea kuwepo pale hospitali kwa siku tatu na baada ya nguvu kunirejea mwilini niliondolewa pale hospitali nikapelekwa mahabusu ya kituo cha polisi cha Buguruni. Nilikaa pale mahubusu nikisubiri kufunguliwa kesi mbaya ya ubakaji.

Siku iliyofuata wakati nikiwa nimejikunyata kwenye kona ya chumba cha mahabusu nilishuhudia lango la mahabusu ile likifunguliwa na askari mmoja ambaye aliita jina langu. Kwa unyonge niliinua shingo yangu kumtazama yule askari ambaye alikuwa na cheo cha Koplo.

“We mbakaji, inuka unifuate!” alisema baada ya kuona namtazama kwa wasiwasi.

Mahabusu wote katika kile chumba walinitazama kwa makini, baadhi yao walinihurumia lakini wengine walitabasamu kwa kejeli. Niliinuka kwa unyonge nikamfuata yule askari, aliniongoza tukipita kwenye korido hadi kwenye mlango wa ofisi ya mkuu wa kituo.

Tulipoingia ndani ya ofisi ile ya mkuu wa kituo nilipigwa butwaa baada ya kumkuta mama yake mkubwa na Rehema, Bi Aisha akiwa kwenye ile ofisi na Mkuu wa Kituo kile, Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP), Shaban Mungi, ambaye alikuwa kajiegemeza kwenye kiti chake cha kuzunguka. Wote waligeuka kunitazama kwa makini nilipokuwa naingia.

Nilijikuta nagwaya baada ya kuhisi uwepo wa hali ya majonzi na ukimya mzito sana ndani ya ile ofisi. Nilipowatupia jicho la wizi niliowakuta mle ofisini niliona huzuni kwenye macho yao. Mkuu wa kituo alinionesha kiti, nikaketi nikiwa na wasiwasi mkubwa.

Mkuu wa kituo aliendelea kunitazama kwa macho yaliyokuwa yameficha kitu nyuma yake. Sikuweza kujua nini kilichokuwa kikiendelea pale, nikajiuliza, yuko wapi Rehema?

Nilianza kuingiwa wasiwasi, hata hivyo, nilibaki kimya nikiwatazama wote kwa makini ingawa nilianza kuhisi kuwa kulikuwa na jambo lisilo la kawaida lililokuwa limetokea. Niliogopa kuuliza. Bi Aisha alinitazama akashindwa kuvumilia, nilimuona akiinuka na kutoka nje huku akilia kwa uchungu mkubwa.

Mkuu wa kituo alishusha pumzi na kufungua droo moja katika meza yake, kisha akatoa bahasha ndogo iliyokuwa na barua ndani yake, akaishika vizuri ile bahasha mkononi mwake huku akinitazama kwa huzuni.

“Bilali, kuanzia sasa uko huru, shika barua yako!” aliniambia huku akinyoosha mkono wake kunipa ile bahasha.

Kauli ya yule mkuu wa kituo cha polisi ikanishangaza sana, nilidhani labda nilikuwa ndotoni na mara ningeamka ningekuta mambo hayapo hivyo, lakini yule mkuu wa kituo aliendelea kunyoosha mkono wake kunitaka nichukue ile barua.

Nilimtazama usoni kutaka kuona kama kweli hatanii kisha nikaipokea ile barua huku mikono yangu ikitetemeka, ilitetemeka kwa sababu sikujua ilitoka wapi na ilihusu nini. Niliitazama ile barua kwa wasiwasi.

“Unaweza kusoma hapa hapa ukipenda!” yule mkuu wa kituo aliniambia huku akifuta machozi yake. Nikiwa na wasiwasi niliifungua ile bahasha na ndani yake kulikuwa na barua ndefu iliyotoka kwa Rehema.

“Mpenzi Bilali, haikuwa nia yangu kukusababishia kipigo kikali na kuitwa mbakaji, bali nimefanya haya kwa sababu nakupenda kutoka moyoni na ninapenda uishi miaka mingi…

“Bilali ni wewe mwanaume pekee niliyetokea kuvutiwa nawe kihisia ukauteka moyo wangu na kujikuta nikiwa mtumwa wa mahaba yako japo ulijaribu sana kuniumiza kihisia lakini bado sikuacha kukupenda…

“Ni kweli sikutaka kulala na wewe kwa kuwa nina kasoro kubwa ambayo hainipi hadhi ya kulala kitanda kimoja na wewe, sikutaka kuwa muuaji kwa kuruhusu unibake… hivi, Bilali unadhani mpapaso wako haukunisisimua? Nilisisimka hasa na nilitamani nikutimizie kwa hiari kile ulichotaka, labda mimi nilikuwa muhitaji kuliko wewe mpenzi, lakini… lakini nisingeweza kukuua…

“Bilali, wala usisikitike kusikia hili, mimi nimefurahi sana kufa nikiupigania uhai wa mwanaume niliyempenda, ninayempenda na ninayekufa kwa ajili yake. Kifo hiki kiwe kumbukumbu yako milele kuwa nilikupenda sana…

“Nilitaka kukwambia lakini nilishindwa, nimekuwa nikiishi na virusi vya UKIMWI kwa muda mrefu baada ya kuambukizwa na wazazi wangu… nilizaliwa nikiwa na Virus vya Ukimwi, na mama kabla ya kufa alinikanya kuwa ni heri nife peke yangu kuliko kuua yeyote asiyekuwa na hatia…

“Kwa kuwa utaalamu umeongezeka nilikubali unioe kwa kuwa tungefuata ushauri wa kitaalamu ili nisikuambukize, maana wewe huna hatia na haustahili kufa… laiti kama ungenibaka basi leo hii ningekufa nikiwa muuaji…

“Ninafurahi kuwa nakufa kama shujaa. Ninayaandika haya huku chupa ya sumu ikiwa pembeni yangu, nakufa leo lakini nimewaomba wakuache uwe huru. Bahati nzuri mkuu wa kituo ni baba yangu mdogo hivyo naamini atakuacha uwe huru, huru kabisa, wakati mimi nikiungana na mama yangu nimweleze kuwa sikuwahi kuua duniani na nimeamua kuondoka ili siku moja nisije kuua yeyote. Buriani Bilali, mpenzi wa moyo wangu…”

Sikujua kilichoendelea baada ya pale kwani niliishiwa nguvu, moyo wangu ukashikwa na mfadhaiko, mikono yangu ilikuwa inatetemeka na jasho jingi likaanza kunitoka sehemu mbalimbali za mwili wangu.

Macho yangu nayo yakaanza kupoteza nguvu ya kuona na hatimaye shughuli mbalimbali za mwili wangu nazo nikazihisi kuwa zilikuwa mbioni kusitisha utendaji wake.

______

Siku mbili baadaye nilikwenda kwenye makaburi ya Kisutu ambako Rehema alikuwa amezikwa, nilisimama mbele ya kaburi jipya la Rehema na kulitazama kwa huzuni, nikafuta machozi yaliyokuwa yakinilengalenga.

Haikuwa ndoto, ni kweli ilitokea kuwa Rehema alijiua kwa sumu na kuzikwa… barua ile niliyopewa ilikuwa imetwa kando ya mwili wake chumbani… sasa macho ya watu yalikuwa yakinitazama kwa kunisuta, wapo waliokuwa na hasira juu yangu, wapo ambao walinitazama kwa dharau na baadhi walinitazama kwa huzuni. Kwa kweli sikujua nifanye nini!

Nilitamani ardhi ipasuke ili nijifiche chini ya ardhi kukwepa macho ya jamii. Nilitamani kunywa sumu ili nami niondoke hapa duniani, hasa baada ya kuujua ukweli kuhusu maisha ya Rehema, mwanamke aliyenijali na kunipenda kwa dhati!

Niliendelea kusimama nikilitazama kaburi la Rehema kwa kitambo kirefu huku machozi yakinitoka. Nilifuta machozi nikashusha pumzi ndefu za ndani kwa ndani.

“Upumzike pema peponi Rehema… kamwe sitakusahau mpenzi!” nilisema kwa huzuni kisha nikainamisha kichwa changu mbele ya kaburi la rehema kama ishara ya kutoa heshima zangu za mwisho. Sikuweza kuendelea kusimama pale nikaondoka taratibu kwa huzuni, mikono yangu ikiwa nyuma.

MWISHO
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom