Bishop Hiluka
R I P
- Aug 12, 2011
- 7,150
- 14,724
- Thread starter
- #61
Laiti Ningejua! 11
Mtunzi Bishop Hiluka
Niliivuta ile kabali ya mlango na kuinyonga huku nikijaribu kuusukuma ule mlango kwa nguvu, lakini ule mlango haukufunguka kwa kuwa ulikuwa umepinda kidogo na kubonyea kwa ndani kutokana na gari lile kugonga ule mti mkubwa, hivyo nikaamua kuufungua kwa teke moja la nguvu.
Ule mlango ulisalimu amri na kufunguka, lakini kabla sijashuka kutoka ndani ya lile gari nikajiwa na wazo la kumuokoa yule mrembo ambaye muda ule alionekana kama aliyekuwa amepigwa bumbuwazi na presha ilikuwa imepanda na hivyo kumfanya asijue la kufanya.
Nilikuwa nimejiwa na wazo la kumuokoa kwani sikuona sababu ya kujiokoa mwenyewe huku nikimwacha yule mrembo auawe kinyama katika mazingira ambayo nilidhani ninawajibika kufanya hivyo. Bila kuchelewa nikamshika mkono na kumsukumia nje ili ashuke, lakini alionekana kuendelea kushangaa.
Nilipotupa macho yangu kule barabarani muda ule nikawaona majambazi wawili kati ya wale watatu waliokuwa wameruka kutoka ndani ya lile gari aina ya Toyota Land Cruiser Pick-up wakikimbilia kuja kule lilikokuwa lile gari letu, huku wakiwa wameshika vyema bunduki zao mikononi.
Sikutaka kuendelea kushangaa tena, nikamnyanyua yule msichana mrembo kutoka kwenye siti yake kisha nikaruka naye nje ya lile gari na kutua chini kwa miguu yangu.
Kutokana na kiza kilichokuwa kimetanda katika eneo lile nilishindwa kuona vizzuri sehemu niliyorukia na kujikuta nikitua kwenye bonde dogo na hivyo mguu wangu wa kushoto ukashtuka na hapo nikasikia maumivu makali sana kwenye kifundo cha mguu wangu wa kushoto yaliyopanda hadi juu ya goti.
Kutokana na kiza kilichokuwa kimetanda katika eneo lile nilishindwa kuona vizzuri sehemu niliyorukia na kujikuta nikitua kwenye bonde dogo na hivyo mguu wangu wa kushoto ukashtuka na hapo nikasikia maumivu makali sana kwenye kifundo cha mguu wangu wa kushoto yaliyopanda hadi juu ya goti.
Hata hivyo, sikujali yale maumivu makali ya mguu wangu niliyoyahisi, nilimbeba juu juu yule msichana mrembo na kujitahidi kuondoka haraka kutoka eneo lile huku nikikimbilia kichakani.
Sikuweza kufika mbali kwani nilihisi mguu wangu ukipinda, kisha nikaanguka huku nikiwa bado nimembeba yule msichana mrembo, hata hivyo, kwa namna ya ajabu nilijikuta nikimuinua juu yule mrembo huku nikijipinda na kulalia mgongo huku yule mrembo akiangukia juu ya kifua changu.
Kitendo kile cha kuanguka chini na yule mrembo kunilalia juu kikamzindua kutoka kwenye lile bumbuwazi, na hapo nikamuona akitazama huku na kule kwa hofu kubwa na kutaka kupiga kelele. Niliwahi kumziba mdomo wake huku nikimsukuma haraka kumuondoa eneo lile.
“Tafadhali kimbilia kichakani kabla hawajafika,” nilimnong’oneza sikioni yule mrembo huku nikimsukuma aondoke haraka eneo lile na kwenda kwenye kichaka kikubwa ambacho hakikuwa mbali kutoka pale chini tulipokuwa tumeangukia.
Yule msichana mrembo alionekana kuganda juu yangu kama sanamu akiwa ameanza kuchanganyikiwa na hivyo kumfanya asijue lipi la kufanya na kwa wakati gani.
Muda ule walee abiria wengine walikuwa wametaharuki na kuanza kutimua mbio ovyo wakikimbilia barabarani huku wakipiga kelele ovyo kwa hofu. na hapo milio mingine kadhaa ya risasi ikavuma tena hewani, kufumba na kufumbua nikawaona watu watatu miongoni mwa wale abiria wakitupwa hewani na kupiga mayowe ya uchungu.
Wale watu walipoanguka chini walitulia kimya huku uhai ukiwa mbali na nafsi zao, kwani zile risasi zilizofyatuliwa zilikuwa zimepenya kwenye maeneo nyeti ya kichwa na kifua na kuacha matundu makubwa yaliyokuwa yanavuja damu.
Milio ile ya risasi ikamzindua tena yule msichana mrembo, nami nikazidi kumsisitiza kwa sauti yenye kusihi na kushawishi sana kuwa akimbilie kichakani kabla wale majambazi hawajafika pale na kutuona tukiwa katika hali ile. Maneno yangu yakamfanya anitazame kwa makini kama vile alikuwa amesikia habari mpya kabisa masikioni mwake.
Nikamsukuma kwa nguvu nikimtaka aondoke haraka eneo lile, safari hii aliinuka haraka pasipo upinzani wowote, nikamuona akitimua mbio huku akiwa ameinamisha mgongo wake kuelekea kwenye kichaka cha lile pori lililokuwa kando ya ile barabara.
Nikiwa bado nimelala pale kwenye majani, nilimtazama yule msichana mrembo namna alivyokuwa akipotelea kwenye kile kichaka hadi alipotoweka kabisa machoni kwangu, nami nikaubana mguu wangu wa kushoto uliokuwa na maumivu makali na kuanza kutambaa kama nyoka, haraka nikapotelea gizani huku nikielekea kwenye kile kichaka.
Muda ule abiria wengine wanne waliobaki walisambaratika kwa hofu kila mmoja na njia yake wakikimbilia porini na hivyo kusalimisha roho zao. Nilifanikiwa kufika pale kwenye kichaka japo kwa taabu nikamkuta yule mrembo akiwa kajikunyata kwa hofu kubwa huku akilia kwa uchungu kilio cha kwikwi.
Sikuwa na shaka kabisa kuwa yule mrembo pale kwenye kichaka alikuwa amechanganyikiwa kutokana na hali ile ya taharuki aliyokuwa ameishuhudia na kuna wakati alitaka kupiga yowe la hofu lakini niliwahi kumziba mdomo wake baada ya kuhisi hatari ambayo ingetukabili pindi wale wauaji wangelisikia yowe lake.
Wale wauaji wawili waliisogelea ile gari yetu kwa tahadhari wakati yule jambazi wa tatu alikuwa amesimama kwa mbali kule barabarani akionekana kulinda eneo lile pamoja na kuwalinda wale wawili endapo hatari yoyote ingetokea.
Mara nikamuona mmoja kati ya wale wauaji wawili waliokuwa wamesima kwenye lile gari akianza kusogea taratibu kuelekea pale kwenye kile kichaka tulichokuwa tumejificha mimi na yule msichana mrembo huku akielekeza mtutu wa bunduki yake pale kichakani.
Yule mrembo akaingiwa na kiwewe na kutaka kutoka ili akimbie lakini niliwahi kumdaka na kumzuia kwa mikono yangu yenye nguvu ili asikimbie, kisha nikamziba mdomo wake kwa nguvu ili asipige kelele. Ni wazi kabisa kuwa kwa muda ule alikuwa amechanganyikiwa na hakujua hatari ambayo ingempata endapo angejaribu kukimbia.
Wakati nikiwa nimemziba mdomo yule mrembo nikaamuona yule muuaji akizidi kusogea pale kwenye kichaka kwa kupitia uwazi wa matawi na majani katika kile kichaka, niliweza kumuona vizuri yule mtu wakati akitembea kwa tahadhari kusogea pale.
Kiza kilichokuwepo katika eneo lile hakikunizuia kumtambua yule muuaji kutokana na umbile lake na hata utembeaji wake, alikuwa ni yule jamaa aliyeshuka kwenye lile gari Toyota Land Cruiser Pick-up pale jirani na kituo cha kujazia mafuta cha Gapco cha Kibiti na kuja kuuliza usafiri wa kwenda Dar es Salaam kwenye gari letu.
Nilimtazama kwa mshangao akiwa ameishika vyema bunduki yake aina ya sub machine gun huku misuli ya shingo na mikono yake ikiwa imetuna kwa ukomavu. Mwonekano wake ukanitanabaisha kuwa alikuwa ni mtu hatari sana na aliyependa matata.
Yule muuaji akaendelea kutembea kwa tahadhari akikikaribia kile kichaka na wakati huo yule mwenzake alikwenda moja kwa moja hadi kwenye siti ya mbele kushoto kwa dereva alipokuwa ameketi yule mzee wa makamo mwenye suti maridadi, nikamuona akichukua kitu kutoka kwenye mikono ya yule marehemu.
Itaendelea...
Mtunzi Bishop Hiluka
Niliivuta ile kabali ya mlango na kuinyonga huku nikijaribu kuusukuma ule mlango kwa nguvu, lakini ule mlango haukufunguka kwa kuwa ulikuwa umepinda kidogo na kubonyea kwa ndani kutokana na gari lile kugonga ule mti mkubwa, hivyo nikaamua kuufungua kwa teke moja la nguvu.
Ule mlango ulisalimu amri na kufunguka, lakini kabla sijashuka kutoka ndani ya lile gari nikajiwa na wazo la kumuokoa yule mrembo ambaye muda ule alionekana kama aliyekuwa amepigwa bumbuwazi na presha ilikuwa imepanda na hivyo kumfanya asijue la kufanya.
Nilikuwa nimejiwa na wazo la kumuokoa kwani sikuona sababu ya kujiokoa mwenyewe huku nikimwacha yule mrembo auawe kinyama katika mazingira ambayo nilidhani ninawajibika kufanya hivyo. Bila kuchelewa nikamshika mkono na kumsukumia nje ili ashuke, lakini alionekana kuendelea kushangaa.
Nilipotupa macho yangu kule barabarani muda ule nikawaona majambazi wawili kati ya wale watatu waliokuwa wameruka kutoka ndani ya lile gari aina ya Toyota Land Cruiser Pick-up wakikimbilia kuja kule lilikokuwa lile gari letu, huku wakiwa wameshika vyema bunduki zao mikononi.
Sikutaka kuendelea kushangaa tena, nikamnyanyua yule msichana mrembo kutoka kwenye siti yake kisha nikaruka naye nje ya lile gari na kutua chini kwa miguu yangu.
Kutokana na kiza kilichokuwa kimetanda katika eneo lile nilishindwa kuona vizzuri sehemu niliyorukia na kujikuta nikitua kwenye bonde dogo na hivyo mguu wangu wa kushoto ukashtuka na hapo nikasikia maumivu makali sana kwenye kifundo cha mguu wangu wa kushoto yaliyopanda hadi juu ya goti.
Kutokana na kiza kilichokuwa kimetanda katika eneo lile nilishindwa kuona vizzuri sehemu niliyorukia na kujikuta nikitua kwenye bonde dogo na hivyo mguu wangu wa kushoto ukashtuka na hapo nikasikia maumivu makali sana kwenye kifundo cha mguu wangu wa kushoto yaliyopanda hadi juu ya goti.
Hata hivyo, sikujali yale maumivu makali ya mguu wangu niliyoyahisi, nilimbeba juu juu yule msichana mrembo na kujitahidi kuondoka haraka kutoka eneo lile huku nikikimbilia kichakani.
Sikuweza kufika mbali kwani nilihisi mguu wangu ukipinda, kisha nikaanguka huku nikiwa bado nimembeba yule msichana mrembo, hata hivyo, kwa namna ya ajabu nilijikuta nikimuinua juu yule mrembo huku nikijipinda na kulalia mgongo huku yule mrembo akiangukia juu ya kifua changu.
Kitendo kile cha kuanguka chini na yule mrembo kunilalia juu kikamzindua kutoka kwenye lile bumbuwazi, na hapo nikamuona akitazama huku na kule kwa hofu kubwa na kutaka kupiga kelele. Niliwahi kumziba mdomo wake huku nikimsukuma haraka kumuondoa eneo lile.
“Tafadhali kimbilia kichakani kabla hawajafika,” nilimnong’oneza sikioni yule mrembo huku nikimsukuma aondoke haraka eneo lile na kwenda kwenye kichaka kikubwa ambacho hakikuwa mbali kutoka pale chini tulipokuwa tumeangukia.
Yule msichana mrembo alionekana kuganda juu yangu kama sanamu akiwa ameanza kuchanganyikiwa na hivyo kumfanya asijue lipi la kufanya na kwa wakati gani.
Muda ule walee abiria wengine walikuwa wametaharuki na kuanza kutimua mbio ovyo wakikimbilia barabarani huku wakipiga kelele ovyo kwa hofu. na hapo milio mingine kadhaa ya risasi ikavuma tena hewani, kufumba na kufumbua nikawaona watu watatu miongoni mwa wale abiria wakitupwa hewani na kupiga mayowe ya uchungu.
Wale watu walipoanguka chini walitulia kimya huku uhai ukiwa mbali na nafsi zao, kwani zile risasi zilizofyatuliwa zilikuwa zimepenya kwenye maeneo nyeti ya kichwa na kifua na kuacha matundu makubwa yaliyokuwa yanavuja damu.
Milio ile ya risasi ikamzindua tena yule msichana mrembo, nami nikazidi kumsisitiza kwa sauti yenye kusihi na kushawishi sana kuwa akimbilie kichakani kabla wale majambazi hawajafika pale na kutuona tukiwa katika hali ile. Maneno yangu yakamfanya anitazame kwa makini kama vile alikuwa amesikia habari mpya kabisa masikioni mwake.
Nikamsukuma kwa nguvu nikimtaka aondoke haraka eneo lile, safari hii aliinuka haraka pasipo upinzani wowote, nikamuona akitimua mbio huku akiwa ameinamisha mgongo wake kuelekea kwenye kichaka cha lile pori lililokuwa kando ya ile barabara.
Nikiwa bado nimelala pale kwenye majani, nilimtazama yule msichana mrembo namna alivyokuwa akipotelea kwenye kile kichaka hadi alipotoweka kabisa machoni kwangu, nami nikaubana mguu wangu wa kushoto uliokuwa na maumivu makali na kuanza kutambaa kama nyoka, haraka nikapotelea gizani huku nikielekea kwenye kile kichaka.
Muda ule abiria wengine wanne waliobaki walisambaratika kwa hofu kila mmoja na njia yake wakikimbilia porini na hivyo kusalimisha roho zao. Nilifanikiwa kufika pale kwenye kichaka japo kwa taabu nikamkuta yule mrembo akiwa kajikunyata kwa hofu kubwa huku akilia kwa uchungu kilio cha kwikwi.
Sikuwa na shaka kabisa kuwa yule mrembo pale kwenye kichaka alikuwa amechanganyikiwa kutokana na hali ile ya taharuki aliyokuwa ameishuhudia na kuna wakati alitaka kupiga yowe la hofu lakini niliwahi kumziba mdomo wake baada ya kuhisi hatari ambayo ingetukabili pindi wale wauaji wangelisikia yowe lake.
Wale wauaji wawili waliisogelea ile gari yetu kwa tahadhari wakati yule jambazi wa tatu alikuwa amesimama kwa mbali kule barabarani akionekana kulinda eneo lile pamoja na kuwalinda wale wawili endapo hatari yoyote ingetokea.
Mara nikamuona mmoja kati ya wale wauaji wawili waliokuwa wamesima kwenye lile gari akianza kusogea taratibu kuelekea pale kwenye kile kichaka tulichokuwa tumejificha mimi na yule msichana mrembo huku akielekeza mtutu wa bunduki yake pale kichakani.
Yule mrembo akaingiwa na kiwewe na kutaka kutoka ili akimbie lakini niliwahi kumdaka na kumzuia kwa mikono yangu yenye nguvu ili asikimbie, kisha nikamziba mdomo wake kwa nguvu ili asipige kelele. Ni wazi kabisa kuwa kwa muda ule alikuwa amechanganyikiwa na hakujua hatari ambayo ingempata endapo angejaribu kukimbia.
Wakati nikiwa nimemziba mdomo yule mrembo nikaamuona yule muuaji akizidi kusogea pale kwenye kichaka kwa kupitia uwazi wa matawi na majani katika kile kichaka, niliweza kumuona vizuri yule mtu wakati akitembea kwa tahadhari kusogea pale.
Kiza kilichokuwepo katika eneo lile hakikunizuia kumtambua yule muuaji kutokana na umbile lake na hata utembeaji wake, alikuwa ni yule jamaa aliyeshuka kwenye lile gari Toyota Land Cruiser Pick-up pale jirani na kituo cha kujazia mafuta cha Gapco cha Kibiti na kuja kuuliza usafiri wa kwenda Dar es Salaam kwenye gari letu.
Nilimtazama kwa mshangao akiwa ameishika vyema bunduki yake aina ya sub machine gun huku misuli ya shingo na mikono yake ikiwa imetuna kwa ukomavu. Mwonekano wake ukanitanabaisha kuwa alikuwa ni mtu hatari sana na aliyependa matata.
Yule muuaji akaendelea kutembea kwa tahadhari akikikaribia kile kichaka na wakati huo yule mwenzake alikwenda moja kwa moja hadi kwenye siti ya mbele kushoto kwa dereva alipokuwa ameketi yule mzee wa makamo mwenye suti maridadi, nikamuona akichukua kitu kutoka kwenye mikono ya yule marehemu.
Itaendelea...