Stori ya kusisimua - Laiti Ningejua!

Stori ya kusisimua - Laiti Ningejua!

Laiti Ningejua! 9

Mtunzi Bishop Hiluka

Muda ule ule nikamuona mwanamume mmoja wa makamo aliyekuwa amevaa suti maridadi akija haraka eneo lile akitokea kwenye ule mgahawa wa Victoria huku akiwa amebeba brifukesi yake nzuri ya gharama katika mkono wake wa kulia na mkono wake wa kushoto alikuwa ameshika chupa kubwa ya lita moja na nusu ya maji safi.

Alipofika kwenye lile gari alishika kitasa cha mlango ule wa mbele wa ile gari, akavuta na kufungua kisha aliingia na kuketi kwenye ile siti ya abiria upande wa kushoto wa dereva. Muda ule ule nikaliona gari moja aina ya Toyota Land Cruiser Pick-up likipita pale na kusimama kwenye kile kituo cha kujazia mafuta.

Ndani ya lile gari kulikuwa na wanaume watatu, dereva na mtu mmoja walikuwa wameketi mbele na mtu mwingine alikuwa amesimama kule nyuma ya lile gari. Wote walikuwa warefu na wenye miili imara iliyojengeka. Nilijikuta nikivutiwa sana kuwaangalia wale watu ingawa sikujua kwa nini nilijikuta nikivutiwa sana kuwaangalia.

Endelea...

Mara nikamuona yule mtu aliyekuwa amesimama kule nyuma ya lile gari akishuka kisha akatazama huku na kule na kuharakisha kuvuka barabara na kuja moja kwa moja upande tuliokuwepo.

Wakati akivuka kuja upande tuliokuwepo nikawaona wanaume wawili wakitoka ndani ya ule mgahawa wa Victoria na kupanda kwenye lile Toyota Land Cruiser Pick-up lililomshusha yule mtu, na hapo lile gari likaanza kuondoka na kuingia barabara iliyoelekea Dar es Salaam.

Muda ule ule yule kijana aliyekuwa ametuleta pale kwenye lile gari akazunguka kwenda kwenye mlango wa dereva, nikamuona yule dereva akijipapasa mifukoni, na kama aliyegutuka akatugeukia, lakini kabla hajasema chochote yule jamaa aliyeshuka kwenye lile gari Toyota Land Cruiser Pick-up akasogea mlangoni kwa dereva.

Alipokuwa pale nikashtushwa sana na macho yake makubwa yaliyoonesha uchovu lakini yalikuwa ni aina fulani ya yale macho yaliyoashiria shari. Alikuwa na uso mrefu uliokuwa umetulia na ijapokuwa alikuwa amevaa kofia aina ya kapelo na miwani midogo myeusi ya jua aliyokuwa ameipandisha juu ya uso wake.

Aliposimama pale mlangoni kwa dereva akawa anachungulia mle ndani kiaina akionekana kama aliyekuwa anamtafuta mtu fulani ndani ya lile gari tulilopanda, kwani alipochungulia alikuwa akitutazama usoni kiaina. Dereva akamtazama kwa makini.

“Vipi kuna mtu unamtafuta?” dereva wa lile gari alimuuliza yule jamaa.

“Hapana, nilitaka kujua kama mnaelekea Dar,” yule mtu alimwambia yule dereva huku akiendelea kututupia jicho la wizi.

“Ndiyo, tunaelekea Dar lakini tayari gari limeshapendeza, si unaona mwenyewe,” yule dereva alimwambia yule mtu huku akiendelea kumtazama kwa macho ya udadisi.

Yule jamaa alishusha pumzi na kulizunguka akiendelea kutuangalia kwa makini, kisha akaondoka zake. Muda wote nilikuwa namtazama kwa makini na sura yake ikanitia mashaka.

Sikujua kwa nini nilikumbwa na hisia mbaya juu yake, hata hivyo, niliamua kuzipuuza hisia zangu na kuanza kuifikiria safari yangu ya kurudi Dar es Salaam.

Mara yule dereva wa lile gari tulilopanda akageuka tena nyuma na kuanza kudai nauli, alitutazama kwa utulivu huku akitengeneza tabasamu jepesi usoni mwake.

Bila kupoteza muda kila mmoja alitoa fedha na kumpa, nami bila kuchelewa nikachukua pochi yangu kutoka mfukoni na nilipoifungua nikahesabu noti zenye thamani ya nauli iliyohitajika na kumpa yule dereva kama malipo ya nauli yangu.

Yule dereva alizipokea zile fedha na kuanza kuzihesabu taratibu huku ukimya ndani ya lile gari ukitawala. Kisha alichukua noti kadhaa kutoka kwenye zile fedha na kumpa yule kijana aliyetuleta. Kisha akawasha gari tayari kwa safari ya kuelekea jijini Dar es Salaam, niliitazama saa yangu nikagundua kuwa ilikuwa imeshatimu saa kumi na mbili jioni.

Yule dereva aliliondoa lile gari kwa mbwembwe huku akiwa makini kutazama barabarani na kuingia kwenye barabara ya Dar es Salaam na mbele kidogo tukalipita lile gari aina ya Toyota Land Cruiser Pick-up likiwa limeegeshwa kando ya barabara huku nyuma yake kukiwa na alama ya pembe tatu (triangle) kama ishara ya kutambulisha kuwa gari lile lilikuwa limepata hitilafu.

Nje ya lile gari kulikuwa na wale wanaume wawili, dereva wa lile gari na mtu mmoja aliyekuwa amekaa mbele walioonekana wameinamia kwenye boneti la gari lililokuwa limefunguliwa wakiwa wanalitengeneza. Nikaangalia huku na kule lakini sikuweza kuwaona wale wanaume wengine wawili waliopandia pale kwenye kituo cha kujazia mafuta cha Gapco.

Tulipowapita nikawaona wakiinua sura zao na kugeuka kulitazama gari letu kwa makini sana kana kwamba kuna kitu kilikuwa kinawashangaza.

Tuliendelea na safari yetu huku dereva akiwa makini zaidi kutazama barabarani. Miale hafifu ya jua la machweo ilikuwa mbioni kutoweka angani na kiza kilikuwa mbioni kuchukua nafasi yake. Dereva aliendesha kwa kasi akiifuata barabara ile iliyoelekea Dar es Salaam huku taratibu tukianza kuuacha mji wa Kibiti nyuma yetu.

Nilikuwa nimezama katikati ya tafakuri nzito nikifikiria jinsi nilivyoweza kukosa dili la pesa kizembe, lakini sikukata tamaa, niliamua kutoa simu yangu na kumpigia tena simu Yeriko, nilitafuta namba ya Yeriko kisha nikapiga. Mara ikaanza kuita na haukuchukua muda ile simu ikapokelewa.

“Hello!” niliisikia sauti ya Yeriko upande wa pili wa simu iliyonipa nguvu.

Haraka sana niliumjulisha kilichokuwa kimenisibu mara baada ya kusalimiana. Yeriko alinifahamisha kuwa nisiwe na wasiwasi kwani hata yeye alikuwa amepata udhuru, hivyo dili letu lilikuwa bado lipo pale pale na tungeweza kukutana kesho yake, ila alinitaka niwasiliane naye mara tu nikifika jijini Dar es Salaam.

Muda mfupi baadaye tukawa tumeuacha kabisa mji wa Kibiti nyuma yetu na muda ule sauti pekee iliyokuwa ikisikika mle ndani ya gari ilikuwa ni sauti ya muungurumo wa injini ya lile gari.

Lile gari lilikuwa likienda mwendo wa kasi ingawa yule dereva alionekana kuwa makini sana huku akionekana pia kuizoea vizuri ile barabara, na wakati safari ikiwa inaendelea nikaanza kumchunguza yule msichana mrembo nikitafuta namna ya kumzoea.

Nilimuona akiwa ameelemewa sana na usingizi, nadhani kwa sababu ya uchovu, na muda huo giza lilikuwa limeanza kutanda angani, hata hivyo, dereva wa lile gari aliwasha taa kubwa za mbele na mwanga mkali wa taa zile ulijitahidi kulifukuza giza lile lililokuwa limetanda mbele yetu huku tukizidi kutokomea mbele zaidi.

Hakuna aliyekuwa akiongea muda huo na hivyo mle ndani ya gari kulitawaliwa na kiasi kikubwa cha ukimya wa namna yake. Nilimtazama yule msichana mrembo, sikuona tashwishwi yoyote katika sura yake kama ilivyokuwa kwa abiria wengine ndani ya lile gari, na kila mmoja alionekana kuchoka sana.

Uso wa yule mrembo ulikuwa umepoteza kabisa nuru na utulivu, kwa namna nyingine nilimuona akiitupia jicho saa yake ya mkononi mara kwa mara na kusonya na mara akaonekana kuzama kwenye fikra fulani.

Mwendo wetu ulikuwa siyo wa kubabaisha tukikatiza katikati ya pori na baada ya mwendo mfupi wa safari yetu mbele kidogo tukawaona watu kadhaa waliokuwa wakilisimamisha gari letu, hata hivyo dereva hakusimama na muda mfupi baadaye tukayavuka majengo ya Shule ya Sekondari ya Kibiti yaliyokuwa upande wetu wa kushoto.

Tuliendelea kukatisha katikati ya msitu mnene wenye giza zito huku manyunyu ya mvua yakianza kudondoka hali iliyofanya barabara ile izidi kutisha wakati ule wa usiku.

Tulipishana na magari mawili matatu wakati tukiipita barabara ya kuelekea Nyamisati, muda wote dereva alikuwa yuko makini sana huku akiendesha kwa mwendo kasi lakini wenye tahadhari za aina zote.

Kisha tukaanza kukatisha katikati ya makazi ya watu tukiuvuka mji mdogo wa Bungu ambao kwa wakati ule wa usiku nyumba za makazi ya watu zilionekana kama vichaka kwani wakazi wake wengi walikuwa wamekwisha ingia majumbani.

Safari iliendelea na ilionekana kuwa ndefu lakini yule dereva wetu alikuwa makini mno akiendelea kuendesha kwa mwendo kasi na hakuna aliyekuwa akimsemesha mwenzake muda wote wa safari yetu.

Itaendelea...
 
Wakuu, tusameheane kidogo, laptop yangu imeleta shida kidogo hivyo kulazimika kurekebisha mambo yasije yakakwaza safari yetu. Natumaini leo nitakamilisha na kuweka mambo sawa ili safari yetu iendelee. Hata hivyo sijawaacha bure...

CC Tater, moneytalk, marybaby, nipo2, ram, kisukari, the_legend, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, Mine eyes, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly SUPER EMILY, nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa SUPER EMILY iron2012
 
Wakuu, tusameheane kidogo, laptop yangu imeleta shida kidogo hivyo kulazimika kurekebisha mambo yasije yakawaza safari yetu. Natumaini leo nitakamilisha na kuweka mambo sawa ili safari yetu iendelee. Hata hivyo sijawaacha bure...

CC Tater, moneytalk, marybaby, nipo2, ram, kisukari, the_legend, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, Mine eyes, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly SUPER EMILY, nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa SUPER EMILY iron2012
Pole sana mkuu,
Na shukran pia usjali tupo na subra kama wana nchi wa STANZA[emoji4]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakuu, tusameheane kidogo, laptop yangu imeleta shida kidogo hivyo kulazimika kurekebisha mambo yasije yakakwaza safari yetu. Natumaini leo nitakamilisha na kuweka mambo sawa ili safari yetu iendelee. Hata hivyo sijawaacha bure...

CC Tater, moneytalk, marybaby, nipo2, ram, kisukari, the_legend, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, Mine eyes, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly SUPER EMILY, nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa SUPER EMILY iron2012
Pole sana Bishop kwa kuharibikiwa na PC, hata hivyo umejitahidi sana kutuburudisha
 
Usijali mkuu tupo pamoja
Wakuu, tusameheane kidogo, laptop yangu imeleta shida kidogo hivyo kulazimika kurekebisha mambo yasije yakakwaza safari yetu. Natumaini leo nitakamilisha na kuweka mambo sawa ili safari yetu iendelee. Hata hivyo sijawaacha bure...

CC Tater, moneytalk, marybaby, nipo2, ram, kisukari, the_legend, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, Mine eyes, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly SUPER EMILY, nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa SUPER EMILY iron2012

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakuu, tusameheane kidogo, laptop yangu imeleta shida kidogo hivyo kulazimika kurekebisha mambo yasije yakakwaza safari yetu. Natumaini leo nitakamilisha na kuweka mambo sawa ili safari yetu iendelee. Hata hivyo sijawaacha bure...

CC Tater, moneytalk, marybaby, nipo2, ram, kisukari, the_legend, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, Mine eyes, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly SUPER EMILY, nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa SUPER EMILY iron2012
Tuko pamoja Bishop

the Legend☆
 
Laiti Ningejua! 1

Mtunzi Bishop Hiluka

HII haikuwa mara yangu ya kwanza kufika wilaya ya Rufiji hususan katika mji wa Ikwiriri, mji mdogo uliopo kusini kwa Dar es Salaam katika Mkoa wa Pwani. Nilikuwa nimefika hapo Ikwiriri mara moja na hii ilikuwa ni mara yangu ya pili.

Kwa kiasi fulani sikuwa mgeni kabisa wa mazingira ya Ikwiriri ingawa mara ya kwanza nilipokwenda katika mji ule sikukaa kwa zaidi ya siku tatu. Kama ilivyokuwa mara ya kwanza, safari hii tena nilipokwenda katika mji wa Ikwiriri nilikuwa pale kibiashara na nilifikia nyumbani kwa rafiki yangu, Amir Ngwali, aliyekuwa anaishi Barabara ya Mtunda nje kidogo ya mji wa Ikwiriri.

Kama kawaida yangu, siku ile pia nilikuwa katika mwonekano wa kileo zaidi nikiwa nimevaa suruali ya jeans ya rangi nyeusi, buti ngumu za ngozi miguuni, shati maridadi la rangi ya samawati aina ya Levi’s nililokuwa nimelichomekea vizuri kiunoni, saa ya mkononi aina ya Seiko na kofia nyeusi ya kapelo.

Kwa ujumla nilikuwa mtanashati niliyejipenda mno kuanzia ndani ya chumba changu hadi mwili wangu, ilikuwa ni nadra sana kunifumania nikiwa nimerudia kuvaa nguo niliyoivaa jana yake.

Nikiwa katika umri wa miaka therathini nilikuwa mrefu na maji ya kunde mwenye umbo la kimichezo, nilikuwa mcheshi sana na mtu wa kujichanganya na watu wengine.

Sikuwa mbumbumbu, nilikuwa nina elimu nzuri tu ya biashara, kwani nilihitimu shahada ya kwanza ya Biashara katika Masoko (B.Com. in Marketing) kutoka katika Shule ya Biashara ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDBS), miaka mitano iliyokuwa imepita.

Baada tu ya kumaliza masomo yangu ya biashara pale Chuo Kikuu cha Dar es Salaam nilizunguka kutafuta ajira lakini baadaye nikaamua kujiajiri mwenyewe baada ya kuona mshahara niliokuwa nikitajiwa ulikuwa hauendani na matarajio yangu.

Kimsingi niliamua kuwa mtu wa dili au ukipenda unaweza kuniita ‘mishen tauni’, na ili kufanikiwa zaidi katika dili zangu niliamua kuwa mtu wa kujichanganya sana.

Tabia yangu ya kujichanganya na watu wa aina mbalimbali kwenye dili ambazo zingine wala hazikuhitaji kisomo na bila kujali elimu yangu, kwa kiasi fulani zilinifanya nianze kupata mafanikio makubwa kimaisha na kufanya watu walionifahamu kunipachika jina la utani la ‘the Jackal of all trades’, yaani dalali wa biashara zote.

Nilifanikiwa kufungua ofisi yangu ya udalali na ushauri wa biashara iliyokuwa katika eneo la Buguruni Rozana, na nilikuwa nimeajiri watu sita, mimi nikiwa ndiye mkurugenzi mtendaji wa kampuni.

Pia nilikuwa nimejenga nyumba kubwa ya kisasa iliyokuwa nje ya jiji la Dar es Salaam, katika eneo la Zingiziwa, Chanika na pia nilimiliki viwanja viwili vitatu katika maeneo tofauti jijini Dar es Salaam.

Katika maisha yangu ua utafutaji, sikupenda kabisa kujihusisha na wasichana ndiyo maana ilikuwa vigumu sana kunikuta na msichana. Lakini kwa vile binadamu hawana dogo wakaanza kusema eti huenda nilikuwa na matatizo mwilini mwangu, ndiyo maana nilikuwa naishi peke yangu licha ya kuwa na uwezo na pia kushobokewa na warembo.

Wakati najiandaa kuondoka pale nyumbani kwa Amir nikiwa mbioni kurudi jijini Dar es Salaam yalipo makazi yangu, ilikuwa yapata saa nne asubuhi, Amir na mke wake, Mwanamvua Mbonde walinisindikiza huku wakilalamika kuwa nimekuwa nikifika Ikwiriri na kukaa siku moja au mbili tu kisha naondoka, walitamani siku nyingine nikae pale kwa zaidi ya wiki.

Pia Mwanamvua alikuwa haachi kulalamika akitaka amuone mke mwenzake, kwa maana nyingine ni kwamba alikuwa akinisisitiza nioe ili washerehekee harusi yangu kabla ujana haujaisha maana sasa nilianza kuelekea kwenye utu uzima.

Tulipotoka nje ya nyumba ya Amir nikawaona watu wawili-watatu wa bodaboda waliokuwa wameegesha pikipiki zao chini ya mti mkubwa kando ya ile barabara iliyokuwa ikielekea Mtunda, na walikuwa umbali wa kama mita hamsini hivi kutoka katika ile nyumba ya Amir.

Katika umbali ule dereva mmoja wa bodaboda mjanja akaniwahi haraka kabla ya wenzake hawajashtuka baada ya kuhisi hitaji langu. Aliponiona tu alipiga honi huku akiniashiria nipande ile bodaboda, na kama vile haitoshi aliiwasha bodaboda yake haraka na kunifuata pale pale nje ya nyumba ya Amir tulipokuwa tumesimama.

Kwa mwonekano tu yule dereva wa bodaboda alikuwa ni mtu mzima aliyekadiriwa kuwa na umri usiopungua miaka arobaini na tano. Alikuwa mrefu na mwembamba mwenye sura ya ucheshi na alikuwa amevaa shati la bluu na jaketi jeusi, suruali ya kijivu na raba miguuni.

Alitusalimia kwa bashasha huku akionekana kutaniana na Amir, kisha nikapanda kwenye ile bodaboda pasipo hata kusubiri. Mara tu nilipopanda kwenye ile bodaboda yule dereva wa bodaboda akanisemesha kwa lugha ya Kindengereko na alipoona kuwa sielekei kumuelewa aliamua kubadili lugha na kunisemesha kwa Kiswahili.

“Kwani wewe si mtu wa hapa Ikwiriri?” yule dereva wa bodaboda akaniuliza kwa mshangao.

“Mimi siyo Mndengereko, mimi ni mtu wa Kigoma,” niliongea kwa utulivu huku nikimtazama kwa makini.

“Oh! Kumbe wewe ni Muha wa Kigoma? Karibu sana Ikwiriri. Mimi ni Mndengereko al-watan hapa Ikwiriri. Hakuna asiyenifahamu hata ukimuuliza mtoto mdogo tu atakwambia anamjua Kindeka mzee wa mabodaboda ni nani, au siyo Amir?” alisema yule dereva wa bodaboda kwa tambo nyingi huku akigeuza shingo yake kumtazama Amir na kuachia kicheko hafifu.

Amir na mke wake pia walicheka kicheko hafifu bila kusema neno. Mimi nilibaki kumtazama tu yule yule dereva wa bodaboda kwa makini huku nikiachia tabasamu laini ambalo baadaye likageuka kicheko hafifu.

“Lakini si kila mtu anayetoka Kigoma ni Muha, yapo pia makabila mengine kama Wabembe, Watongwe, Wamanyema…” nilimwambia yule dereva wa bodaboda, ambaye sasa nililifahamu jina lake kuwa aliitwa Kindeka.

“Kumbe!” akadakia yule dereva wa bodaboda kabla hata sijamaliza maelezo yangu huku akionekana kushangaa sana.

“Ndiyo, si hao tu, pia utawakuta Wanyamwezi, Wasukuma, Wafipa na watu wenye asili ya Congo, Rwanda na Burundi,” nikazidi kumweleza yule dereva wa bodaboda na kuzidi kumshangaza.

“Ooh, kwa hiyo wewe ni kabila gani?” aliniuliza yule dereva bodaboda huku akigeuza shingo yake kunitazama usoni kwa shauku kubwa ya kutaka kujua.

“Mimi ni Mmanyema ingawa siwezi kuzungumza lugha ya Kimanyema kwa sababu nimekulia jijini Dar es Salaam.”

Maelezo yangu yakamfanya yule dereva wa bodaboda ageuke kabisa na kunitazama usoni kwa makini kisha akaangua kicheko hafifu kabla kuniambia.

“Sishangai kwa nini vijana wengi wa zama hizi hawajui kuzungumza lugha zao za asili, wengi wanadhani labda ni ushamba au labda ni kutokwenda shule,” alisema yule dereva wa bodaboda huku akiangua tena kicheko.

Maelezo yale yakatufanya watu wote kwa pamoja tuangue kicheko cha katikati ya maongezi na kabla kicheko kile hakijafika ukomo wake, yule dereva wa bodaboda akageuka tena na kuniuliza, “Lakini bado hujaniambia tunaelekea wapi, Bosi?”

“Nipeleke stendi ya mabasi ya kuelekea jijini Dar es Salaam,” nilimjibu yule dereva wa bodaboda kwa utulivu huku nikiwa nimekwisha kaa vizuri na begi langu nikiwa nimelivaa mgongoni.

“Ooh, kumbe unaelekea Bongo? Nilisahau kama umeniambia unakaa Dar es Salaam!” akasema yule dereva wa bodaboda na kuangua tena kicheko hafifu na kuongeza, “Au kwa sasa unaishi hapa kwetu Ikwiriri?”

“Hapana, bado naishi Dar es Salaam, Ikwiriri nakuja kutembea tu mara moja moja,” nilimjibu yule dereva wa bodaboda kisha nikawaaga wenyeji wangu, Amir na mkewe kwa bashasha zote.

Kitambo kifupi cha ukimya kikafuatia wakati yule dereva wa bodaboda akiiondoa ile bodaboda kutoka pale kwenye nyumba ya Amir. Hakuwa na mbwembwe kama ilivyokuwa kwa vijana wengi waliokuwa wakiendesha bodaboda kupenda kupiga lesi.

Itaendelea...
Uhondo
 
Wakuu, tusameheane kidogo, laptop yangu imeleta shida kidogo hivyo kulazimika kurekebisha mambo yasije yakakwaza safari yetu. Natumaini leo nitakamilisha na kuweka mambo sawa ili safari yetu iendelee. Hata hivyo sijawaacha bure...

CC Tater, moneytalk, marybaby, nipo2, ram, kisukari, the_legend, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, Mine eyes, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly SUPER EMILY, nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa SUPER EMILY iron2012

Tupo pamoja Bishop...
 
Wakuu, tusameheane kidogo, laptop yangu imeleta shida kidogo hivyo kulazimika kurekebisha mambo yasije yakakwaza safari yetu. Natumaini leo nitakamilisha na kuweka mambo sawa ili safari yetu iendelee. Hata hivyo sijawaacha bure...

CC Tater, moneytalk, marybaby, nipo2, ram, kisukari, the_legend, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, Mine eyes, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly SUPER EMILY, nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa SUPER EMILY iron2012
Usijali Bishop
 
Wakuu, tusameheane kidogo, laptop yangu imeleta shida kidogo hivyo kulazimika kurekebisha mambo yasije yakakwaza safari yetu. Natumaini leo nitakamilisha na kuweka mambo sawa ili safari yetu iendelee. Hata hivyo sijawaacha bure...

CC Tater, moneytalk, marybaby, nipo2, ram, kisukari, the_legend, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, Mine eyes, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly SUPER EMILY, nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa SUPER EMILY iron2012
Pole sana.

Usijari bishop, bado tupo pamoja...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakuu, tusameheane kidogo, laptop yangu imeleta shida kidogo hivyo kulazimika kurekebisha mambo yasije yakakwaza safari yetu. Natumaini leo nitakamilisha na kuweka mambo sawa ili safari yetu iendelee. Hata hivyo sijawaacha bure...

CC Tater, moneytalk, marybaby, nipo2, ram, kisukari, the_legend, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, Mine eyes, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly SUPER EMILY, nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa SUPER EMILY iron2012
tupo pamoja mkuu bishop
 
Laiti Ningejua! 10

Mtunzi Bishop Hiluka

Tuliendelea kukatisha katikati ya msitu mnene wenye giza zito huku manyunyu ya mvua yakianza kudondoka hali iliyofanya barabara ile izidi kutisha wakati ule wa usiku.

Tulipishana na magari mawili matatu wakati tukiipita barabara ya kuelekea Nyamisati, muda wote dereva alikuwa yuko makini sana huku akiendesha kwa mwendo kasi lakini wenye tahadhari za aina zote.

Kisha tukaanza kukatisha katikati ya makazi ya watu tukiuvuka mji mdogo wa Bungu ambao kwa wakati ule wa usiku nyumba za makazi ya watu zilionekana kama vichaka kwani wakazi wake wengi walikuwa wamekwisha ingia majumbani.

Safari iliendelea na ilionekana kuwa ndefu lakini yule dereva wetu alikuwa makini mno akiendelea kuendesha kwa mwendo kasi na hakuna aliyekuwa akimsemesha mwenzake muda wote wa safari yetu.

Endelea...

Huku tukizidi kuvuka msitu mnene, vichaka na kona mbalimbali za ile barabara ya Dar es Salaam, niliwatazama tena wale abiria wenzangu ndani ya gari na kuwaona wote wakiwa hoi kwa usingizi kutokana na uchovu wa kutwa nzima.

Ni mimi na dereva tu wa lile gari ambao hatukuwa tumesinzia, na katika ukimya ule, nilijikuta nikianza kuwaza namna ambavyo ningeweza kupanua ofisi yangu ya Buguruni au hata kufungua kampuni nyingine kubwa ya ushauri wa masuala ya kibiashara na masoko na kuwaajiri vijana mbalimbali wenye utaalamu wa biashara na masoko kama wangu.

Kwa takriban mwaka sasa nilikuwa nakwenda kutoa mada katika ofisi mbalimbali jijini Dar es Salaam na maeneo ya jirani, nikiwa kama mtaalamu wa masuala ya kibiashara na masoko kwa watu waliopenda kuwezeshwa mawazo kazini kwao, zikiwemo kampuni mbalimbali zilizohitaji kuwapa wafanyakazi wao semina ya biashara lakini walikuwa na tatizo la muda.

Ni Yeriko ndiye aliyenishauri kufikiria namna nyingine ambayo ingeweza kuniingizia fedha nyingi kutokana na taaluma yangu ya biashara na masoko, kwani nimewahi kushuhudia baadhi ya wajasiriamali wakubwa walioendelea na kuingiza fedha nyingi kwa kuzungumza tu, tena kwa hesabu za dakika.

Mwanzoni nilipoanza kutoa mada nilikuwa nikitoza fedha kidogo, lakini namna nilivyotoa huduma yangu, ilinitangaza kwa kiwango kikubwa na kuniwezesha kupata watu wengi zaidi. Taratibu nilianza kufanikiwa na niliamini kuwa hatimaye ningekuwa mmoja wa watoa mada maarufu nchini na Afrika Mashariki.

Wakati nikiendelea kuwaza, nilianza kuzidiwa kwa mawazo na uchovu wa kutwa nzima, niliinamisha kichwa changu, na hapo nikaanza kusinzia lakini nilishtuka baada ya hisia mbaya kunijia akilini na hapo haraka nikainua kichwa changu na kuyapeleka macho yangu kuangalia nyuma tulikokuwa tunatoka.

Mara nikaiona miale mirefu ya mwanga mkali wa taa za gari moja lililokuwa linakuja nyuma yetu kwa mwendo wa kasi zaidi. Macho yangu yalivutiwa kulitazama lile gari namna lilivyokuwa likija kwa kasi na kutukaribia nyuma yetu, huku akili yangu ikianza kutafakari juu ya gari lile kwa jinsi lilivyokuwa likizidi kutusogelea.

Baada ya muda mfupi hatimaye lile gari likawa limetufikia na sasa lilikuwa nyuma yetu, takriban mita ishirini hivi kutoka lilipokuwa gari letu. Mara likaanza kutupita kwa kasi ya ajabu.

Tukio lile likamfanya dereva wetu apunguze mwendo wa gari na kuliruhusu lile gari lipite kwa uhuru na kuendelea na safari yake. Wakati likitupita nikapata wasaa mzuri wa kulichunguza na hapo nikagundua kuwa lilikuwa ni lile gari Toyota Land Cruiser Pick-up tulilolipita kando ya barabara pale Kibiti likiwa limeharibika.

Hisia mbaya zaidi zikanijia na kunifanya nianze kuswali kimoyomoyo nikimuomba mola atuepushe na balaa lolote, japo sikuwa mtu wa kwenda msikitini. Mara tu baada ya lile gari Toyota Land Cruiser Pick-up kutupita, nikaliona likipunguza mwendo ghafla na kwenda kutuzuia kwa mbele.

Kitendo kile cha lile gari Toyota Land Cruiser Pick-up lililotupita kupunguza mwendo ghafla mbele yetu huku likituzuia kikamfanya dereva wa gari letu kukanyaga breki za ghafla huku akijitahidi kwa kila namna kulikwepa lile gari huku ufundi wake katika udereva ukionekana kugonga mwamba.

Kutokana na mwendo wake alionekana kushindwa kuhimili na hivyo gari letu liliyumba na kuserereka huku magurudumu yakilalamika kwenye ile barabara ya lami.

Hata hivyo, alikuwa amekwisha chelewa, akaligonga lile gari kwa nyuma na kusababisha taa za mbele za gari letu kuvunjwa vibaya na ngao ngumu ya nyuma ya lile Toyota Land Cruiser Pick-up lililokuwa limesimama mbele yetu.

Muda ule ule nikawaona watu watatu waliokuwa nyuma ya lile gari Toyota Land Cruiser Pick-up wakiruka kutoka kwenye gari huku wakiwa wameshika vyema bunduki zao aina ya Sub Machine Gun na kuzielekeza upande ule tuliokuwepo.

Sasa nilikuwa na uhakika kabisa kuwa zile hisia mbaya zilizokuwa zikinijia kabla zilikuwa sahihi, na tukio lile likanidhihirishia kuwa hatukuwa salama, kwani tulikuwa tukielekea kukabiliana na utekaji kutoka kwa wale watu, na wakati nikitafakari kuhusu jambo hilo nilijikuta nikishikwa na hofu kubwa na taharuki isiyoelezeka.

Sikuwa na shaka na wala sikuhitaji mtu yeyote kunieleza kuwa mambo hayakuwa shwari tena, hivyo nilipaswa kufanya maamuzi ya haraka kabla sijashuhudia jambo baya likitokea mbele ya macho yangu, ambalo lingeacha taswira isiyoelezeka ndani ya akili yangu.

Kabla sijajua nifanye nini nikamuona dereva wa gari letu aliyekuwa amepagawa baada ya kuhisi jambo baya lilikuwa mbioni kutokea, akifanya jambo lisilotarajiwa, kwani aliingiza gia ya kurudi nyuma na hapo hapo kukanyaga pedeli ya mafuta na kulifanya gari letu lianze kurudi nyuma kwa mwendo wa kasi ya ajabu.

Sasa gari letu lilikuwa linarudi nyuma kwa kasi ya ajabu, hata hivyo, hatukuweza kwenda umbali mrefu zaidi kwani muda ule ule sote tulishtushwa na mlio mkali wa risasi zilizopasua kioo cha mbele cha gari letu na kulifanya lile gari liende likiyumbayumba barabara nzima.

Katika taharuki ile gari lile likaanza kuserereka likielekea kando ya barabara na kuanza kuingia vichakani kwa mwendo ule ule wa kasi huku likiyumba na kisha kwenda kugota kwenye mti mkubwa uliokuwa takriban mita hamsini nje kabisa ya ile barabara. Kitendo cha lile gari letu kugota pale kwenye ule mti mkubwa kikanifanya nigonge kichwa changu na kusikia maumivu makali yaliyosambaa hadi mgongoni.

Kabla sijajua nifanye nini mara nikasikia milio mingine kadhaa ya risasi ikirindima kama radi kuelekea kule tulikokuwa na hapo nikashuhudia kile kioo cha mbele cha gari letu kikitawanywa na kusambaa huku vipande vidogo vidogo mfano wa chenga chenga vikitumwagikia mwilini na kuendelea kuzua hali ya taharuki.

Kwa nukta chache nilihisi kama vile moyo wangu ulisahau mapigo yake, nilichoweza kusikia kusikia muda ule ilikuwa ni yowe dogo la hofu kutoka kwa yule dereva wa gari letu kisha nikamuona akiangukia kwa mbele kwenye usukani wa lile gari na kutulia kimya huku kifo kikiwa tayari kimemchukua. Waswahili wangeweza kusema kuwa; ‘hakuomba maji’.

Muda ule ule abiria wenzangu ndani ya lile gari walianza kupiga mayowe ya hofu, hata hivyo ule haukuwa muda wa kushauriana kwani nilijua fika ni nini ambacho kingefuatia baada ya pale. Niliweza kushuhudia zile risasi zilizorindima zikiwa zimekifumua vibaya kichwa cha yule dereva a gari letu na kutoboa bodi la lile gari.

Risasi nyingine zilikuwa zimeacha matundu mawili yakivuja damu katika sehemu ya kifua cha abiria mtu wa makamo aliyekuwa ameketi siti ya mbele upande wa kushoto kwa dereva na nyingine kupita hadi kwa abiria mwingine aliyekuwa ameketi nyuma ya yule abiria wa mbele katika ile siti ya katikati.

Kwa kweli sikuwahi kuingia na hofu kubwa maishani mwangu kama hofu iliyonipata siku ile, hata hivyo, katikati ya hofu ile sikuona namna nyingine yoyote ya kujiokoa haraka katika mkasa ule, hivyo nilichokifanya ilikuwa ni kuvuta haraka kabali ya ule mlango wa nyuma ambako tulikuwa tumeketi.

Itaendelea...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom