Stori ya kusisimua - Kizungumkuti!

Stori ya kusisimua - Kizungumkuti!

Kizungumkuti! - 56

Na Bishop Hiluka

ILIPOISHIA

“Sijui unatumia kinywaji gani?” Jacob alimwuliza Jacky huku akimtazama kwa makini.

“Mvinyo mwepesi tafadhali,” Jacky alisema, na hapo Jacob akainuka na kuelekea kwenye jokofu kubwa la vinywaji.na kurudi na chupa ya mvinyo, akamimina katika bilauri mbili, moja akampatia Jacky na nyingine akabaki nayo mwenyewe, kisha waligongesha zile bilauri kutakiana afya njema huku Jacob akiachia tabasamu pana.

Endelea...

Alikunywa kidogo na kuiweka bilauri yake juu ya meza huku akimtazama Jacky katika namna ya kuuajabia uzuri wake. Jacky alikuwa amevaa gauni jepesi jeusi la kata mikono lililokuwa limelichora vyema umbo lake na kuishia juu ya magoti yake na hivyo kuifichua hazina nzuri ya miguu yake. Miguuni alikuwa amevaa viatu vyekundu vyenye visigino virefu.

Kope zake zilikuwa zimekolea wanja mwembamba mfano wa mwezi mwandamo na kuyafanya macho yake makubwa, meupe na legevu yaifanye akili ya Jacob isikinai kumtazama muda wote. Kila wakati tabasamu lake lilizisogeza kingo pana za mdomo wake wa juu na wa chini na hivyo kufanya meno yake meupe yaliyopangika vizuri kuonekana bila kificho.

Alikuwa amevaa hereni nzuri za madini ya tanzanite kwenye masikio yake huku mkufu mwembamba wa dhahabu safi ukiizunguka vyema shingo yake nyembamba na kisha kidani chake kupotelea katikati ya matiti yake.

When you called me you really confused me a lot, and so far I don’t know what’s exactly the problem can be that makes you want to see me so quickly!” (Uliponipigia simu kwa kweli ulinichanganya sana, na hadi sasa sijajua una tatizo gani kiasi cha kutaka kuniona haraka kiasi hiki!) Jacob alisema huku akipiga funda jingine la mvinyo na kuketi karibu ya Jacky huku akimtazama kwa makini.

First I must thank you for giving me such great honor to welcome me to your home. A great person like you to invite someone like me is not a small thing,” (Kwanza nakushukuru sana kwa kunipa heshima kubwa kama hii kunikaribisha nyumbani kwako. Mtu mkubwa kama wewe kukubali kunikaribisha mtu kama mimi si jambo dogo) Jacky alisema kwa mzaha huku akilazimisha tabasamu.

Stop flattering me, here is your home and you don't need to ask to come here, you’re welcome anytime, by the way, I’d not want to miss an angel like you. You don’t know the joy I had after receiving your phone call. After many years of escaping me today I am lucky to be with you, just the two of us, alone, my heart is full of joy,” (Acha kunizingua, hapa ni nyumbani kwako na huna haja ya kuomba kuja, muda wowote unakaribishwa, hata hivyo, nisingeweza kukosa kuonana na malaika kama wewe. Huwezi kujua furaha niliyokuwa nayo baada ya kupokea simu yako. Baada ya miaka mingi ya kunikimbia hatimaye leo hii nimepata bahati ya kuwa na wewe, tukiwa wiwili tu, faragha, moyo wangu umejaa furaha sana) Jacob alisema huku akiupitisha mkono wake mmoja nyuma ya Jacky na kuanza kumpapasa nyama za mgongo.

Jacky alijitahidi kutabasamu lakini uso wake haukuonesha furaha na wala haukuwa na tashwishwi yoyote, alionesha kuwa alikuwa jambo zito lililokuwa likimtatiza sana moyoni, alikuwa na huzuni moyoni iliyojionesha wazi wazi kwenye macho yake ingawa alijitahidi sana kuificha hali ile lakini hakufanikiwa.

Jacob alimtazama Jacky kwa makini na kuhisi uwepo wa jambo lisilo la kawaida, moyo wake ukaingiwa na ganzi huku akijaribu kujiuliza nini kilichokuwa kikimtatiza Jacky?

Jacob alijikuta akiiona siku ile kama siku iliyokuwa imebeba matukio mabaya yenye kumuumiza roho yake, kwanza rafiki yake Yusuf alikuwa mahabusu baada ya kuhusishwa na tukio la wizi wa mabilioni, alikwenda kituo cha polisi mara mbili, mara ya pli akiwa ameongozana na mke wa Yusuf, Mama Jasmine kujaribu kumshawishi ASP Komba ili waweze kumwekea dhamana Yusuf.

Ushawishi wake uligonga mwamba mara mbili, hasa kwa kuwa ilionekana dhamana ile ingeweza kusababisha mchakato wa upelelezi wa kesi ile uwe mgumu zaidi. ASP Komba alimweleza Jacob kuwa kulikuwa na watu wawili wahusika katika wizi ule wa mabilioni, Joram Mbezi na Belinda Jackson waliopaswa kupatikana kwanza…

Jacob aliyakumbuka yote, na sasa alikuwa sebuleni na Jacky, alijikuta akimtazama Jacky machoni kwa udadisi zaidi na kumsogeza zaidi karibu yake huku akimkumbatia, “Ni nani aliyekuudhi mpenzi wangu?” Jacob alimuuliza Jacky, hata hivyo Jacky hakujibu badala yake alikilaza kichwa chake kwenye kifua cha Jacob.

“Niambie mpenzi wangu, nani aliyekuudhi nimshughulikie, you know I don't want to see you so sad!” (…unajua sipendi kukuona ukiwa una huzuni kiasi hiki!) Jacob alisema na kumfanya Jacky ainue uso wake kumtazama Jacob usoni huku macho yake yakionesha kuzingirwa na malenge lenge ya machozi.

“Hakuna aliyeniudhi, mpenzi,” Jacky alisema kwa sauti laini ya chini lakini iliyokuwa imebeba uchungu mwingi.

Now what makes you so sad?” (Sasa nini kinachokufanya kuhuzunika kiasi hiki?) Jacob aliuliza kwa udadisi.

It’s you,” (Ni wewe) Jacky alijibu na kumshtua sana Jacob, kitendo kilichomfanya Jacob akamkazie macho kumtazama kama ambaye hakuwa amemsikia vizuri.

“Mimi!” Jacob aliuliza kwa mshangao.

“Ndiyo, ni wewe,” Jacky alisisitiza huku akiendelea kumtazama Jacob kwa huzuni.

What have I done to you, my love?” (Kwani nimekufanya nini, mpenzi?) Jacob alimuuliza Jacky huku akimtazama kwa makini.

Jacky alivuta pumzi ndefu kisha akazishusha taratibu na kuminya midomo yake huku akimtulizia macho, “To be honest, I began to forget you, but now you’ve come back into my life and hurt the sore that started to heal,” (Kusema ukweli, nilianza kukusahau, lakini sasa umerudi katika maisha yangu na kutonesha kidonda kilichoanza kupona) Jacky alisema huku akijiegemeza kifuani kwa Jacob.

I’m so sorry for what happened, but the truth is that I still love you very much, I couldn’t stop myself from following you,” (Nasikitika samahani kwa kilichotokea, lakini ukweli ni kwamba bado nakupenda sana, sikuweza kujizuia kukufuatilia) Jacob alimwambia Jacky huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.

Jacky alimtazama Jacob machoni na kutabasamu, “How many of you live here?” (Hivi humu ndani mnaishi wangapi?)

For now I’m all alone… but I live with my two siblings, a young sister Daisy and a young brother Goodluck, they’ve gone for a short vacation in Songea…” (Kwa sasa niko peke yangu… ila naishi na ndugu zangu wawili, wa kike Daisy Haule na wa kiume Goodluck Haule, ambao wapo Songea kwa likizo fupi…) Jacob alisema huku akimtazama Jacky na kutabasamu.

What is it?” (Kwani vipi?) kisha Jacob akamuuliza Jacky kwa shauku.

I’m just curious, you live alone in a big building like this! No wife, no servant to serve you?” (Najiuliza tu, unaishi peke yako kwenye jumba kubwa kama hili! Huna mke, huna hata mtumishi wa kukusaidia kazi?)

Itaendelea...

CC the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, Mine eyes, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY
Shukrani sana Bishop...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kizungumkuti! - 59

Na Bishop Hiluka

ILIPOISHIA

“Eti yule malaya ananiletea pozi! Sasa keshokutwa ndiyo atanitambua mimi ni nani labda nisimuone, nitafanya mambo juu ya kaunta…” Liston alisema.

“Umeona eh! Yule bwana si katuahidi kutukatia hamsini zetu! Keshokutwa ndo watajua sisi ni nani, watu tumefanya kweli bladikenge, keshokutwa ndo keshokutwa, hapakaliki hapa,” Kabwe alipaza sauti yake na kurusha mkono wake hewani kitendo kilichomfanya kumpiga mwanamume mmoja aliyekuwa akipita karibu yake.

Wakati yule mwanamume akitaka kuzozana na kabwe mara yule dada aliyemkimbia Liston akarudi mle ndani ya ule ukumbi akiwa ameongozana na Meneja wa ile klabu na kuonekana akinyoosha kidole chake kuelekeza walipokuwa Kabwe na Liston.

Endelea...

Yule Meneja alikuwa mwanaume mfupi mwenye sura ya umbo duara, miwani iliyokuwa imetuama kwenye macho yake makubwa, pua ya kibantu na mdomo wenye kingo pana uliokuwa umezungukwa na ndevu zilizokuwa zimenyolewa vizuri mtindo wa “O”. Alikuwa na kitambi cha ukwasi huku akiwa amevaa suti ya rangi nyeusi, shati la rangi ya kijivu na tai nyekundu shingoni.

Aliwafuata Kabwe na Liston na kuongea nao kwa kitambo kifupi akiwasihi kunywa pombe kistaarabu na kutowabughudhi wateja wengine au kama hawawezi basi waondoke. Kabwe na Liston hawakufurahishwa kupangiwa jinsi ya kutumia fedha zao, walionekana kuchukia sana na kuondoka kwa hasira, lakini waliahidi kurudi tena siku nyingine.

* * * * *

Saa tatu kasoro robo usiku Jacky alikuwa amesimama sebuleni katika nyumba ya Jacob akiwa tayari amekwisha vaa nguo zake akitaka kuondoka. Hiyo ilikuwa ni baada shughuli pevu ya raundi mbili mfululizo kutoka kwa Jacob iliyomuacha hoi.

You are so wonderful Jacky. I swear in heaven and earth, I'll never find a woman who knows how to make love like you. You are so amazing,” (Wewe ni ajabu sana Jacky. Naapa kwa mbingu na ardhi, sitakuja kumpata mwanamke anayeyajua mapenzi kama wewe. Unashangaza sana) Jacob alimwambia Jacky baada ya mzunguko wa kwanza kumalizika.

Where are you going, come here, darling,” (Unaenda wapi, njoo hapa, mpenzi) Jacob alimwambia Jacky baada ya kumuona akijiinua kutoka pale sakafuni.

I need to call my husband first, I don't want to make him worried,” (Nahitaji kumpigia simu mume wangu kwanza, sitaki kumfanya apate wasiwasi) Jacky alimwambia Jacob huku akichukua simu yake na kuelekea bafuni.

Alijifungia mle bafuni na kumpigia simu Carlos, akamweleza yote aliyoyasikia kutoka kwa Jacob kuhusu Kisu. Alimtaka Carlos afanye kila awezavyo kuwasiliana na Kisu na kumgawo wake ili atoroke nchi kabla polisi hawajamfikia, na alipomaliza kuongea na Carlos alirejea pale sebuleni na kumkuta Jacob akimsubiri kwa hamu.

Hmm! It was not unfortunate, I wanted this to happen. Although I don't like but I needed to do this for a special reason. It has also helped me discover what was hidden inside me, obviously I do love Jacob. I deeply love him and for that I can't argue with my soul…” (Hmm! Haikuwa ni bahati mbaya, nilihitaji kitu kama hiki. Japo sipendi lakini nilihitaji kufanya hivi kwa sababu maalumu. Pia imenisaidia kugundua kilichokuwa kimejificha ndani mwangu, ni wazi bado nampenda Jacob. Nampenda sana na kwa hilo siwezi kubishana na nafsi yangu…) Jacky aliwaza wakati akimfuata Jacob aliyekuwa bado kajilaza pale sakafuni.

Jacob hakusema chochote alimvuta Jacky huku akimtazama kwa macho ya uchu kama fisi aliyeona mfupa na kumkumbatia kwa nguvu huku akimporomoshea mabusu mazito mazito. Jacky alijikuta hajiwezi tena na alihitaji huduma kwa mara nyingine tena.

Jacky alikifahamu alichokihitaji Jacob, hakumkawiza akaanza manjonjo yake na kumpatia huduma, wakaingia katika mzunguko wa pili huku ile sebule ikijazwa na vilio vya mahaba toka kwa Jacky kuashiria raha aliyokuwa akiipata. Walichezeshana gwaride la uhakika na hadi wanamaliza mzunguko wa pili wote walikuwa hoi bin taaban.

Jacky, you are still hot, my love,” (Jacky, hakika bado unadai mno, mpenzi wangu) Jacob alimwambia Jacky huku akitweta baada ya kumaliza ule mzunguko wa pili. Jacob alikuwa amejilaza chali pale sakafuni juu ya zulia nene la manyoya akitiririkwa na jasho jingi. Shughuli aliyoifanya haikuwa ndogo. Jacob alishusha pumzi na kujiinua kutoka pale katika zulia alikokuwa amelala, akajimiminia mvinyo katika bilauri yake na kunywa huku akitweta.

Jacky alichukua nguo zake na kukimbilia bafuni na baada ya muda mfupi alitoka akiwa tayari amekwisha vaa nguo zake zote na kuchukua mkoba wake.

I thought today you would spend the night with me, darling?” (Nilidhani leo ungekesha nami, mpenzi?) Jacob alimuuliza Jacky huku akimtazama kwa makini na kumfanya Jacky anyanyue mkono wake na kuitazama tena saa yake ya mkononi.

It’s quarters to nine, my love, I don't want to upset my husband, see you tomorrow,” (Ni saa tatu kasoro robo, mpenzi, sitaki kumuudhi mume wangu, tutaonana kesho) Jacky aliongea kwa sauti hafifu ya kirafiki na hapo akamuona Jacob akimtazama kwa macho yaliyokuwa yamejaa wivu.

But I thought…” (Lakini nilidhani…) Jacob alisema lakini Jacky akamkatiza.

Another day, darling, please…” (Siku nyingine, mpenzi, tafadhali) Jacky alisema huku akirembua macho yake kisha akaanza kuondoka.

“Jacky…”

“Abee”

I love you so much until I feel confused,” (Nakupenda sana hadi najihisi kuchanganyikiwa) Jacob alisema huku akijiinua pale sakafuni.

Me too,” (Mimi pia) Jacky alisema huku akimtazama Jacob kwa makini.

Please don't let me down, my love, see you tomorrow,” (Tafadhali usiniangushe, mpenzi wangu, kesho tuonane).

Until death separates us,” (Hadi kifo kitakapotutenganisha) Jacky aliongea kwa utulivu huku akiruhusu tabasamu lake kuchanua usoni, kisha alimsogelea Jacob na kumbusu mdomoni.

Taratibu akageuka na kuanza kuondoka akimwacha Jacob anamsindikiza kwa macho huku akiutazama mtikisiko maridhawa wa umbo lake zuri. Jacob alibaki akimkodolea macho jacky huku akihisi nafsi yake ilikuwa imepata utajiri mkubwa wa furaha isiyoelezeka.

Jacky alitoka ndani ya lile jumba la Jacob na kuingia ndani ya gari lake aina ya kisha aliliondoa gari lake aina ya Range Rover Sport L494 la rangi nyeupe taratibu.

Muda ule ile hali ya hewa ya jiji la Dar es Salaam ilikuwa imepoa zaidi, manyunyu hafifu ya mvua yalikuwa yakianguka kutoka angani kulikotanda wingu la mvua kiasi cha kuweza kuizuia nyota. Muda wote alikuwa akiwaza namna ya kujikwamua na lile balaa kutokana na kushiriki katika wizi wa mabilioni pale Benki ya Biashara.

Wakati akiendesha gari macho yake yalikuwa makini kutazama kila mahali katika namna ya kuchunguza kuwa hapakuwa na mtu yeyote aliyekuwa akimfuatilia nyendo zake.

Itaendelea...

CC the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, Mine eyes, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY
 
Kizungumkuti! - 60

Na Bishop Hiluka

Jacky alitoka ndani ya lile jumba la Jacob na kuingia ndani ya gari lake aina ya kisha aliliondoa gari lake aina ya Range Rover Sport L494 la rangi nyeupe taratibu.

Muda ule ile hali ya hewa ya jiji la Dar es Salaam ilikuwa imepoa zaidi, manyunyu hafifu ya mvua yalikuwa yakianguka kutoka angani kulikotanda wingu la mvua kiasi cha kuweza kuizuia nyota. Muda wote alikuwa akiwaza namna ya kujikwamua na lile balaa kutokana na kushiriki katika wizi wa mabilioni pale Benki ya Biashara.

Wakati akiendesha gari macho yake yalikuwa makini kutazama kila mahali katika namna ya kuchunguza kuwa hapakuwa na mtu yeyote aliyekuwa akimfuatilia nyendo zake.

Endelea...

Alipofika nyumbani kwake ilikuwa tayari imekwisha timia saa nne za usiku lakini hakumkuta Carlos, hata alipompigia simu ilikuwa inaita tu pasipo kupokelewa.

* * * * *

Saa tatu usiku kwenye chumba cha ofisi ya Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai ya Kanda Maalumu katika jengo la kituo kikuu cha polisi jijini Dar es Salaam, ukimya ulikuwa umetawala.

ASP Komba alikuwa ameketi nyuma ya ile meza ndefu mwisho wa kile chumba upande wa kushoto akiwa katika uso wa kusawajika huku akiwa ameegemea kiti chake.

Mche wa sigara ulikuwa ukiteketea taratibu kwenye pembe ya mdomo wake na macho yake yalikuwa yakitazama picha kadhaa za mnato zilizochukuliwa wakati gari aina ya Ford Transit lililokuwa na nembo ya NeoVision Security lilikiungua nmoto a kubaki chuma chakavu.

Kwenye kiti kingine kilichokuwa jirani na kile cha ASP Komba alikuwa ameketi kachero wa polisi, Sajenti Mapambano, ambaye alikuwa kimya akizitazama zile picha za gari na kisha akasoma nyaraka fulani za taarifa kutoka Idara ya Intelijensia ya Jinai.

ASP Komba na Sajenti Mapambano walizipitia kwa makini zile taarifa kutoka katika ofisi ya Idara ya Intelijensia ya Jinai ambazo zilikuwa zimebeba taarifa nyingi na nyeti kumhusu Joram Mbezi.

Hii ilikuwa ni baada ya kuzipitia kwa makini picha za video zilizonaswa na kamera za ulinzi za ile benki maarufu kama CCTV zikionesha tukio lote la wizi pale katika Benki ya Biashara tawi la barabara ya Lumumba Mnazi Mmoja.

Kabla hajaziangalia zile picha za CCTV ASP Komba aliamini kuwa kiongozi wa wizi ule alikuwa mzungu kama ilivyosemwa na watu lakini zile picha ya video kutoka katika kamera za ulinzi zilimuonesha kwa uwazi kabisa kuwa mtu waliyedhani ni mzungu alikuwa Joram Mbezi, ambaye yeye ASP Komba alimfahamu fika.

Alimfahamu kwa kuwa mara mbili alishamwekwa ndani lakini akalazimika kumwachia kwa sababu ya kukosekana ushahidi wa kutosha kumfungulia kesi.

ASP Komba alichukua tena remote ya runinga na kucheza tena ile picha ya video iliyonaswa na kamera za ulinzi huku akiliangalia lile tukio la wizi wa benki kwa mara ya kumi na mbili. Alikiangalia kwa umakini zaidi kile kipande cha picha ya CCTV kilichokuwa kikimuonesha Joram Mbezi akitangulia kuingia na kutembea kwa madaha huku akifuatwa na wanaume wengine wawili.

Kisha akakirudia na kile kipande ambacho kilimuonesha wakati anatoka huku mmoja wao akiburuza begi la magurudumu hadi pale walipoingia kwenye gari aina ya Ford Transit lililokuwa na nembo ya NeoVision Security.

Sasa ASP Komba aliafikiana kabisa na maelezo yaliyokuwa yametolewa awali na mfanyakazi wa Benki ya Biashara aliyeshuhudia lile tukio, Elibariki, aliyeonesha wasiwasi wake kuhusu mzungu aliyeingia benki kuiba kuwa hakuwa mzungu ila alikuwa mweupe kama mzungu na alivaa nywele bandia kuwahadaa watu wadhani alikuwa mzungu.

Ile picha ya video iliyonaswa na kamera za ulinzi ilimuonesha Joram Mbezi akiwa na nywele ndefu zilizolalia mgongoni na alikuwa amevaa miwani mikubwa myeusi ili kuficha utambulisho wake lakini hiyo haikumzuia ASP Komba kumtambua katika picha ile.

ASP Komba aliisimamisha tena ile picha ya video na kuirudisha nyuma kisha alizitazama zile sura nyingine kwa umakini ili kujiridhisha. Hata hivyo, bado hakuweza mara moja kuwatambua wale wengine, alidhani kuwa ingemchukua muda kuweza kuwatambua endapo angeituliza akili yake, hivyo aliigandisha ile picha ya CCTV na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.

“Ukimtazama haraka haraka huwezi kabisa kudhania kama huyu mtu ni Joram Mbezi…” ASP Komba alisema kwa sauti yenye utulivu huku akiendelea kuiangalia ile picha, kisha alishusha pumzi ndefu huku akiminya midomo yake na kumtupia jicho Sajenti Mapambano. “Labda nikuulize, ni lini, mara ya mwisho ulikutana na huyu mtu?”

“"Kama wiki tatu hivi zilizopita... nakumbuka ilikuwa Jumamosi pale Masai Club,” Sajenti Mapambano alisema baada ya kutafakari kwa sekunde chache.

“Ilikuwa kama saa ngapi hivi?" ASP Komba alimuuliza Sajenti Mapambano huku akimtulizia macho.

"Ilikuwa saa tano na nusu za usiku, siku hiyo tulikwenda kwa ajili ya kuwakamata madada poa na makaka poa. Tukamkuta yuko na yule mwanamke wake Doris. Sisi tukafanya kazi yetu na kuondoka.”

“Yeye mkamwacha?”

“Tungemfanya nini, afande, wakati alikwenda pale kutumia kama watu wengine?” Sajenti Mapambano alimuuliza ASP Komba huku akimkazia macho.

“Mngewakamata wote, yeye na bibi yake, mkawaweka ndani!” ASP Komba alisema huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.

“Japokuwa ana historia ya uhalifu lakini ni mjanja sana, nakumbuka mara mbili ulishamwekwa ndani, ukamtoa kwa sababu ya kukosekana ushahidi wa kutosha kumfungulia kesi,” Sajenti Mapambano alimwambia ASP Komba.

“Sasa naanza kupata wasiwasi, inawezekana kabisa Doris ndiye Belinda Jackson tunayemtafuta,” ASP Komba alisema huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.

“Inawezekana akawa ni Doris, lakini kinachonichanganya, Doris aliwezaje kuwasiliana kwa siri na Joram wakati watu wote wanajua kuwa ni mzazi mwenziye na wana watoto wawili? Kama waliwahi kuishi pamoja na kupata watoto wawili ni wazi hawakuwa na wasiwasi wa kuficha mawasiliano yao, nadhani hapa kuna jambo ambalo hatulifahamu lililomfanya mtu anayejiita Belinda Jackson kuficha utambulisho wake ili mtu mwingine asifahamu!” Sajenti Mapambano alisema huku akimtazama ASP Komba kwa makini.

Yeah, you’re right… nadhani kwa leo inatosha. Leo imekuwa ni siku ndefu sana kwetu. Tukapumzike na kesho asubuhi tuanze kazi rasmi tukianzia Sinza nyumbani kwa Joram,” ASP Komba alimwambia Sajenti Mapambano na kugeuza uso wake, akaitazama tena ile picha ya video iliyogandishwa kwenye runinga na kushusha pumzi. Safari hii uso wake ulijenga matuta ya hasira.

This time you are no longer smart, Joram, I must put you in prison,” (Safari hii huna tena ujanja, Joram, lazima nikutie mbaroni) ASP Komba alisema kwa sauti tulivu lakini iliyobeba hasira.

* * * * *

Asubuhi ya saa moja na dakika ishirini na tano katika barabara ya Igesa eneo la Sinza Makaburini Carlos alikuwa amesimama karibu na baa ya Mwika. Alifika katika eneo lile muda mrefu, takriban dakika ishirini na ushee zilizokuwa zimetangulia akasimama kando ya makaburi akiangalia kila kilichokuwa kinaendelea katika nyumba moja jirani na yale makaburi.

Tangu alipopigiwa simu na Jacky siku iliyokuwa imetangulia na kuelezwa kuhusu maofisa wa polisi kumtilia shaka Kisu kuwa alikuwa mmoja wa walioshiriki katika ule wizi wa mabilioni pale Benki ya Biashara, Carlos hakuweza kulala.

Usiku ule ule alianza harakati za kumtafuta Kisu na bahati mbaya simu yake ilikuwa haipatikani. Alikwenda katika viwanja alivyodhani angeweza kumuona Kisu lakini hakuwepo, hatimaye aliamua kwenda nyumbani kwa Doris, mwanamke aliyewahi kuishi na Kisu na walikuwa na watoto wawili. Hata hivyo Doris alimwambia Carlos kuwa hakuwa ameonana na Kisu kwa takriban wiki tatu, tangu walipoachana Masai Club Kinondoni baada ya kutofautiana.

Itaendelea...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom