Stori ya kusisimua - Kizungumkuti!

Stori ya kusisimua - Kizungumkuti!

Kizungumkuti! - 56

Na Bishop Hiluka

ILIPOISHIA

“Sijui unatumia kinywaji gani?” Jacob alimwuliza Jacky huku akimtazama kwa makini.

“Mvinyo mwepesi tafadhali,” Jacky alisema, na hapo Jacob akainuka na kuelekea kwenye jokofu kubwa la vinywaji.na kurudi na chupa ya mvinyo, akamimina katika bilauri mbili, moja akampatia Jacky na nyingine akabaki nayo mwenyewe, kisha waligongesha zile bilauri kutakiana afya njema huku Jacob akiachia tabasamu pana.

Endelea...

Alikunywa kidogo na kuiweka bilauri yake juu ya meza huku akimtazama Jacky katika namna ya kuuajabia uzuri wake. Jacky alikuwa amevaa gauni jepesi jeusi la kata mikono lililokuwa limelichora vyema umbo lake na kuishia juu ya magoti yake na hivyo kuifichua hazina nzuri ya miguu yake. Miguuni alikuwa amevaa viatu vyekundu vyenye visigino virefu.

Kope zake zilikuwa zimekolea wanja mwembamba mfano wa mwezi mwandamo na kuyafanya macho yake makubwa, meupe na legevu yaifanye akili ya Jacob isikinai kumtazama muda wote. Kila wakati tabasamu lake lilizisogeza kingo pana za mdomo wake wa juu na wa chini na hivyo kufanya meno yake meupe yaliyopangika vizuri kuonekana bila kificho.

Alikuwa amevaa hereni nzuri za madini ya tanzanite kwenye masikio yake huku mkufu mwembamba wa dhahabu safi ukiizunguka vyema shingo yake nyembamba na kisha kidani chake kupotelea katikati ya matiti yake.

When you called me you really confused me a lot, and so far I don’t know what’s exactly the problem can be that makes you want to see me so quickly!” (Uliponipigia simu kwa kweli ulinichanganya sana, na hadi sasa sijajua una tatizo gani kiasi cha kutaka kuniona haraka kiasi hiki!) Jacob alisema huku akipiga funda jingine la mvinyo na kuketi karibu ya Jacky huku akimtazama kwa makini.

First I must thank you for giving me such great honor to welcome me to your home. A great person like you to invite someone like me is not a small thing,” (Kwanza nakushukuru sana kwa kunipa heshima kubwa kama hii kunikaribisha nyumbani kwako. Mtu mkubwa kama wewe kukubali kunikaribisha mtu kama mimi si jambo dogo) Jacky alisema kwa mzaha huku akilazimisha tabasamu.

Stop flattering me, here is your home and you don't need to ask to come here, you’re welcome anytime, by the way, I’d not want to miss an angel like you. You don’t know the joy I had after receiving your phone call. After many years of escaping me today I am lucky to be with you, just the two of us, alone, my heart is full of joy,” (Acha kunizingua, hapa ni nyumbani kwako na huna haja ya kuomba kuja, muda wowote unakaribishwa, hata hivyo, nisingeweza kukosa kuonana na malaika kama wewe. Huwezi kujua furaha niliyokuwa nayo baada ya kupokea simu yako. Baada ya miaka mingi ya kunikimbia hatimaye leo hii nimepata bahati ya kuwa na wewe, tukiwa wiwili tu, faragha, moyo wangu umejaa furaha sana) Jacob alisema huku akiupitisha mkono wake mmoja nyuma ya Jacky na kuanza kumpapasa nyama za mgongo.

Jacky alijitahidi kutabasamu lakini uso wake haukuonesha furaha na wala haukuwa na tashwishwi yoyote, alionesha kuwa alikuwa jambo zito lililokuwa likimtatiza sana moyoni, alikuwa na huzuni moyoni iliyojionesha wazi wazi kwenye macho yake ingawa alijitahidi sana kuificha hali ile lakini hakufanikiwa.

Jacob alimtazama Jacky kwa makini na kuhisi uwepo wa jambo lisilo la kawaida, moyo wake ukaingiwa na ganzi huku akijaribu kujiuliza nini kilichokuwa kikimtatiza Jacky?

Jacob alijikuta akiiona siku ile kama siku iliyokuwa imebeba matukio mabaya yenye kumuumiza roho yake, kwanza rafiki yake Yusuf alikuwa mahabusu baada ya kuhusishwa na tukio la wizi wa mabilioni, alikwenda kituo cha polisi mara mbili, mara ya pli akiwa ameongozana na mke wa Yusuf, Mama Jasmine kujaribu kumshawishi ASP Komba ili waweze kumwekea dhamana Yusuf.

Ushawishi wake uligonga mwamba mara mbili, hasa kwa kuwa ilionekana dhamana ile ingeweza kusababisha mchakato wa upelelezi wa kesi ile uwe mgumu zaidi. ASP Komba alimweleza Jacob kuwa kulikuwa na watu wawili wahusika katika wizi ule wa mabilioni, Joram Mbezi na Belinda Jackson waliopaswa kupatikana kwanza…

Jacob aliyakumbuka yote, na sasa alikuwa sebuleni na Jacky, alijikuta akimtazama Jacky machoni kwa udadisi zaidi na kumsogeza zaidi karibu yake huku akimkumbatia, “Ni nani aliyekuudhi mpenzi wangu?” Jacob alimuuliza Jacky, hata hivyo Jacky hakujibu badala yake alikilaza kichwa chake kwenye kifua cha Jacob.

“Niambie mpenzi wangu, nani aliyekuudhi nimshughulikie, you know I don't want to see you so sad!” (…unajua sipendi kukuona ukiwa una huzuni kiasi hiki!) Jacob alisema na kumfanya Jacky ainue uso wake kumtazama Jacob usoni huku macho yake yakionesha kuzingirwa na malenge lenge ya machozi.

“Hakuna aliyeniudhi, mpenzi,” Jacky alisema kwa sauti laini ya chini lakini iliyokuwa imebeba uchungu mwingi.

Now what makes you so sad?” (Sasa nini kinachokufanya kuhuzunika kiasi hiki?) Jacob aliuliza kwa udadisi.

It’s you,” (Ni wewe) Jacky alijibu na kumshtua sana Jacob, kitendo kilichomfanya Jacob akamkazie macho kumtazama kama ambaye hakuwa amemsikia vizuri.

“Mimi!” Jacob aliuliza kwa mshangao.

“Ndiyo, ni wewe,” Jacky alisisitiza huku akiendelea kumtazama Jacob kwa huzuni.

What have I done to you, my love?” (Kwani nimekufanya nini, mpenzi?) Jacob alimuuliza Jacky huku akimtazama kwa makini.

Jacky alivuta pumzi ndefu kisha akazishusha taratibu na kuminya midomo yake huku akimtulizia macho, “To be honest, I began to forget you, but now you’ve come back into my life and hurt the sore that started to heal,” (Kusema ukweli, nilianza kukusahau, lakini sasa umerudi katika maisha yangu na kutonesha kidonda kilichoanza kupona) Jacky alisema huku akijiegemeza kifuani kwa Jacob.

I’m so sorry for what happened, but the truth is that I still love you very much, I couldn’t stop myself from following you,” (Nasikitika samahani kwa kilichotokea, lakini ukweli ni kwamba bado nakupenda sana, sikuweza kujizuia kukufuatilia) Jacob alimwambia Jacky huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.

Jacky alimtazama Jacob machoni na kutabasamu, “How many of you live here?” (Hivi humu ndani mnaishi wangapi?)

For now I’m all alone… but I live with my two siblings, a young sister Daisy and a young brother Goodluck, they’ve gone for a short vacation in Songea…” (Kwa sasa niko peke yangu… ila naishi na ndugu zangu wawili, wa kike Daisy Haule na wa kiume Goodluck Haule, ambao wapo Songea kwa likizo fupi…) Jacob alisema huku akimtazama Jacky na kutabasamu.

What is it?” (Kwani vipi?) kisha Jacob akamuuliza Jacky kwa shauku.

I’m just curious, you live alone in a big building like this! No wife, no servant to serve you?” (Najiuliza tu, unaishi peke yako kwenye jumba kubwa kama hili! Huna mke, huna hata mtumishi wa kukusaidia kazi?)

Itaendelea...

CC the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, Mine eyes, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY
 
Kizungumkuti! - 57

Na Bishop Hiluka

What is it?” (Kwani vipi?) kisha Jacob akamuuliza Jacky kwa shauku.

I’m just curious, you live alone in a big building like this! No wife, no servant to serve you?” (Najiuliza tu, unaishi peke yako kwenye jumba kubwa kama hili! Huna mke, huna hata mtumishi wa kukusaidia kazi?)

Endelea...

I told you I've never get married since you ran away from me… but I have a maid who leaves after she has finished her chores.” (Nilikuambia sijawahi kuoa tangu uliponikimbia… lakini nina mfanyakazi ambaye huondoka mara tu akishamaliza kazi zake).

Ooh!

I don't like a crowd of servants, because I’m not the king…” (Sipendi kundi kubwa la wafanyakazi wa kunihudumia, kwa sababu mimi siyo mfalme…) Jacob alisema na kuongeza, “By the way, you called me, right? What were you saying?” (Hata hivyo, ulinipigia, au siyo? Ulikuwa unasemaje?)

I have nothing, I just wanted to be with you,” (Sina, nilitaka tu kuwa na wewe) Jacky alisema huku akiangalia chini kuyakwepa macho ya Jacob. Jacob alimtazama kwa makini na kutingisha kichwa chake.

Come on, darling… just tell me! I know you have something to tell me, I promise you, from now on I’m going to protect you. I’m going to make you the happiest woman on earth. Nobody will never hurt you,” (Niambie mpenzi… niambie! Najua una jambo la kuniambia, nakuahidi, kuanzia sasa nitakulinda. Nitahakikisha unakuwa mwanamke mwenye furaha kuliko wote duniani. Hakuna atakayeweza kukuumiza) Jacob alisema huku akimtazama Jacky kwa uadisi.

I just wanted to see you… I wanted to spend this moment with you, now I feel like I’m in heaven,” (Nilitaka kukuona… nilitaka kuwa na wewe muda huu, sasa najihisi kama nipo mbinguni) Jacky alimwambia Jacob huku akiachia tabasamu pana na kuongeza, “…though I’m married and I’ve tried very hard to get rid of you but I have failed…” (…ingawa nimeolewa na nimejitahidi sana kukutoa moyoni mwangu lakini nimeshindwa…)

I'm glad to hear it, but when I lost you I lost something worth more than the wealth I have, I didn't see how I would live without joy or peace in my heart,” (Nina furaha kusikia hivyo, lakini nilipokupoteza nilipoteza kitu cha thamani kuliko hata utajiri nilio nao, sikuona nitaishi vipi bila furaha wala amani moyoni mwangu,” Jacob alisema kwa hisia huku akimtazama Jacky.

Jacob, you never lost me. I was there and I’ll always be there by your side. But there is one important thing I want to tell you…” (Jacob, hujawahi kunipoteza. Nilikuwepo na siku zote nitakuwa na furaha nikiwa na wewe. Lakini kuna kitu cha muhimu nataka kukueleza…) Jacky alisema na kuonekana kusita.

What is that?”(Kitu gani?) Jacob alimuuliza Jacky baada ya kumuona akisita huku akimtazama kwa makini.

Jacky akamshika Jacob mikono huku akimtazama usoni, “I love you so much. I love you from my heart. The love I have for you cannot be expressed. What I feel for you is more than love. The love I have for you cannot be expressed. I think to run away from my marriage so that I can open a new page of life with you…” (Nakupenda sana. Nakupenda toka ndani ya moyo wangu. Upendo nilio nao kwako siwezi kuueleza. Ninavyojihisi juu yako ni zaidi ya pendo… Ninafikiria kutaka kuikimbia ndoa ndoa yangu ili nifungue ukurasa mpya wa maisha pamoja nawe…)

Darling, you don’t have an idea how many days and night I’ve been waiting to hear those words you’ve just said to me. I believe our encounter was not unfortunate, God had His purposes even though on the one hand today has been my sad day…” (Mpenzi, hujui ni kwa muda gani nimekuwa nimekuwa nikisubiri kusikia maneno hayo uliyoniambia. Naamini kukutana kwetu haikuwa bahati mbaya, Mungu alikuwa na makusudi yake japokuwa kwa upande mmoja siku ya leo imekuwa ya huzuni kwangu…)

I wanted to ask you, how it went to the police station?” (Nilitaka kukuuliza, ilikuwaje kule kituo cha polisi ulikokwenda?) Jacky alimuuliza Jacob kwa sauti tulivu kisha akamvuta na kumbusu huku akimpapasa sehemu mbali mbali za mwili wake.

The police have refused to give him bail for fear that the investigation can be destroyed…” (Polisi wamekataa kumpa dhamana kwa kuhofia kuvurugwa kwa upelelezi…) Jacob alisema kwa huzuni.

So, what have they found so far? You told me they came to your office to monitor the phone numbers that were communicating with your friend Yusuf,” (Kwa hiyo, wamegundua nini hadi sasa? Uliniambia walikuja ofisini kwenu kufuatilia namba za simu zilizokuwa zinawasiliana na huyo rafiki yako anayeitwa Yusuf) Jacky aliuliza kwa shauku.

They have already found about a man named Joram Mbezi, and they are still struggling to find someone who calls herself Belinda Jackson…” (Tayari wamegundua kuhusu mtu mmoja anayeitwa Joram Mbezi, na bado wanahangaika kumtafuta mtu mwingine anayejiita Belinda Jackson…) Jacob alisema na kumfanya Jacky ashtuke.

So they have already catched up Joram?” (Kwa hiyo tayari wameshamkata huyo Joram?) Jacky aliuliza huku akionesha kushtuka sana, alimkazia macho Jacob.

Not yet, tomorrow they’ll start chasing him… but what has that to do with us?” (Bado, kesho wataanza kumfuatilia… lakini haya yanahusianaje na sisi?)

It's just humanity… just to care for one another joy and sorrow.” (Ni ubinadamu tu… ni kujaribu kujali furaha na huzuni za watu wengine).

Good. Now let’s leave this and focus our own issues. Let’s enjoy life my angel,” (Vizuri. Sasa tuachane na hayo na tuangalie masuala yanayotuhusu. Tufurahie maisha malaika wangu) Jacob alisema kisha akamvuta Jacky na kumbusu, akaanza kumpapasa sehemu mbalimbali za mwili wake.

Jacky alijilegeza, akamkumbatia Jacob na kuanza kumchezea maeneo nyeti ambayo ghafla yalifura kwa hasira kali, “I know you have been waiting for this for so long, this’s what you want Jacob…” (Najua umekuwa unasubiri kitu hiki kwa muda mrefu, hiki ndicho unachokitaka Jacob) Jacky alimwambia Jacob na kumporomoshea mabusu mfululizo yaliyomchanganya zaidi.

Jacky, in my life I’ve met many women but none of them are like you, I love you very much Jacky,” (Jacky, katika maisha yangu nimekutana na wanawake wengi lakini hakuna kati yao aliye kama wewe, nakupenda sana Jacky) Jacob alisema na kumkumbatia Jacky kwa nguvu.

Jacky aliachia tabasamu kisha akalipandisha juu gauni lake na hapo nguo yake ya ndani ikaonekena, taratibu akaanza kuishusha ile nguo na kuiweka pembeni huku akimtazama Jacob kwa namna iliyozidi kumchanganya mno.

Itaendelea...
 
Kizungumkuti! - 58

Na Bishop Hiluka

Jacky, in my life I’ve met many women but none of them are like you, I love you very much Jacky,” (Jacky, katika maisha yangu nimekutana na wanawake wengi lakini hakuna kati yao aliye kama wewe, nakupenda sana Jacky) Jacob alisema na kumkumbatia Jacky kwa nguvu.

Jacky aliachia tabasamu kisha akalipandisha juu gauni lake na hapo nguo yake ya ndani ikaonekena, taratibu akaanza kuishusha ile nguo na kuiweka pembeni huku akimtazama Jacob kwa namna iliyozidi kumchanganya mno.

Endelea...

Muda huo huo Jacky alimsogelea Jacob akaanza kuufungua mkanda wa suruali yake na mara suruali hiyo ikaanguka chini huku Jacob akibakiwa na boksa tu. Kisha aliivuta taratibu ile boksa ya Jacob, akaishusha hadi magotini na kuupeleka mkono wake ikulu. Jacob alianza kuhema ovyo utadhani bata, hakujiweza tena.

Jacky alimtazama Jacob kwa makini kisha akamsukuma, Jacob alianguka sakafuni kwenye zulia laini. Kabla hajajua afanye nini, Jacky alikuja juu yake na kumkalia, na muda mfupi uliofuata walikuwa pale sebuleni juu ya zulia, Jacob chini na Jacky juu huku Jacob akiishuhudia mijongeo ya Jacky ya taratibu alipokuwa akipanda juu na kushuka chini…

* * * * *

Saa tatu usiku wa siku ile iliwakuta Kabwe na Liston wakiwa katika ukumbi wa chini wa baa ya Masai Club iliyokuwa katika Barabara ya Mwinjuma, Kinondoni mkabala na benki ya ACB jijini Dar es Salaam.

Masai Club ilikuwa ni klabu ya usiku ya kisasa kabisa yenye kila kionjo cha burudani cha daraja la kimataifa ikiwa na kumbi tatu za baa, ukumbi mmoja ulikuwa katika eneo la chini na kumbi mbili zilikuwa ndani ya klabu.

Kulikuwa na ukumbi kwa ajili ya kujipatia vyakula vya kimataifa wenye meza ndefu za kisasa zilizozungukwa na viti vizuri vya sofa vyenye foronya laini pamoja na ukumbi mwingine mkubwa wenye jukwaa zuri lililokuwa linatazamana na viti vingi vya kisasa kwa ajili ya kufanyia shughuli za muziki na mikutano mbalimbali.

Kila ukumbi ulikuwa umejitenga na hivyo kutengeneza mgawanyo mzuri wa starehe tofauti zenye utulivu zilizoweza kufanyika kwa wakati mmoja.

Kabwe na Liston walikuwa katika ukumbi wa chini wa baa uliokuwa mkubwa na wenye uwezo wa kumeza watu wengi bila bugudha yoyote huku ukiwa na meza nyingi ndogo fupi na pana zilizozungukwa na viti vya mbao na vya plastiki.

Pia kulikuwa na meza nyingi za mchezo wa Pool table na kulikuwa na taa nzuri zenye mwanga hafifu zilikuwa zikiangaza mle ndani.

Kabwe na Liston walikuwa wameketi kwenye stuli ndefu katika kaunta ya ile baa, Kabwe alikuwa kaegemea kaunta na mbele yake kulikuwa na chupa kubwa ya pombe kali aina ya Grant’s Blended Scotch Whisky na bilauri.

Liston alikuwa akiongea na msichana mmoja mfanyakazi wa pale baa, aliyekuwa ameketi upande wa pili wa ile kaunta.

Kwenye ukumbi ule kulikuwa na wateja wengi waliokuwa wameketi kwa utulivu huku wakijipatia vinywaji na vyakula na wengine wakiendelea na maongezi yao.

Mzee mmoja alikuwa ameketi kwenye meza ya pembeni kabisa na msichana mzuri ambaye kimuonekana angeweza hata kuwa mjukuu wake na pengine ilikuwa hivyo, na walikuwa wakinywa soda.

Hapa na pale kulikuwa wasichana warembo kama machangudoa, waliokuwa wanazunguka zunguka wakiwa wamevaa nguo zilizokuwa zinaonesha sehemu kubwa ya miili yao na kuwavutia mno wanaume.

Kutokana na pilika pilika zao wakijipitisha huku na kule walionekana bila shaka yoyote kuwa walikuwa wakingoja kuopolewa.

Kulikuwa na wahudumu wa kike warembo waliokuwa wakihudumia wateja waliokuwa mle ndani ya ukumbi. Muziki laini ulikuwa ukisikika taratibu mle ndani ya ukumbi na hivyo kuzikonga vizuri nyoyo za watu waliokuwa ndani ya ule ukumbi.

Runinga pana zilizokuwa zimetundikwa ukutani mle ukumbini zilikuwa zimejikita katika kurusha burudani mbalimbali.

Kabwe na Liston walikuwa wameanza kulewa na muda ule Kabwe alikuwa akipiga kelele zilizokuwa zikiwakera wateja wengine ndani ya ule ukumbi wa baa. Wateja waliokuwemo ndani ya ule ukumbi walikuwa wakimtazama Kabwe kwa mshangao.

Kabwe aliinuka kutoka kwenye kiti alichokuwa amekalia akiwa ameshika ile chupa kubwa ya pombe kali na kuimimina yote chini huku akipiga kelele na kuyumba.

“Hii ni trela tu, picha kamili keshokutwa! Hakyamungu keshokutwa hakai mtu hapa… mi naapa! Nitakunywa na nitatembea uchi ukumbi mzima. Mademu wakinimaindi poa tu au vipi kichaa wangu?” Kabwe alipiga kelele na kuwafanya watu wote wageuke kumtazama kwa mshangao.

Muda ule Liston alikuwa analazimisha kumshika matiti dada mmoja asiyemjua, aliyepita karibu yake. Yule dada alikuwa amevaa t-shirt laini ya rangi nyeupe, sketi fupi ya rangi ya pinki, viatu virefu vya rangi ya pinki vyenye visigino virefu na wigi lenye nywele ndefu aligeuka kumtazama Liston kwa hasira na kusonya.

Kuona vile Liston alimvuta yule dada kwa nguvu na kumkumbatia kwa kuzungusha mikono yake kwenye kiuno cha yule dada. Yule dada alimsukuma Liston kwa nguvu, akamtazama kwa dharau kuanzia juu hadi chini, kisha akabinua midomo yake kwa dharau na kusonya.

“Wewe kaka vipi! Unadhani kila mwanamke anayeingia hapa ni malaya? Mimi siko hapa kujiuza,” yule dada alisema kwa hasira huku akimkazia macho Liston.

I don’t care who you are! Kama siyo malaya unatafuta nini hapa? Si ungekaa na mumeo nyumbani!” Liston alisema kwa sauti ya kilevi huku akiyumba.

“Wewe ni nani hadi unipangie maisha?” yule dada alisema kwa hasira na kusonya huku akibinua midomo yake kwa dharau.

“Mijanaume mingine sijui vipi, sijaja kwako kuomba msaada, kwa kipi kwanza ulichokuwa nacho!” alisema na kuanza kupiga hatua kuondoka.

I don’t give a shit!” Liston alisema huku akimdaka mkono yule dada na kuung’ang’ania huku akimvutia kwake huku akimfinyia macho yake kilevi.

“We mwanamke, unadhani mimi bwege kama hao mabwana zako, eh? Mimi nina hela ya kuulisha ukoo wenu wote kwa mwaka mzima,” Liston alisema huku akitema mate ya ulevi.

Yule dada aliutoa mkono wake kwa nguvu kutoka kwenye mkono wa Liston na kumchapa kibao cha uso huku akionekana kupandwa na hasira. Kisha aliondoka haraka kutoka eneo lile na kukimbilia nje ya ukumbi. Liston alijipangusa uso wake huku akisonya kwa hasira, kisha aligeuka kumtazama Kabwe.

“Eti yule malaya ananiletea pozi! Sasa keshokutwa ndiyo atanitambua mimi ni nani labda nisimuone, nitafanya mambo juu ya kaunta…” Liston alisema.

“Umeona eh! Yule bwana si katuahidi kutukatia hamsini zetu! Keshokutwa ndo watajua sisi ni nani, watu tumefanya kweli bladikenge, keshokutwa ndo keshokutwa, hapakaliki hapa,” Kabwe alipaza sauti yake na kurusha mkono wake hewani kitendo kilichomfanya kumpiga mwanamume mmoja aliyekuwa akipita karibu yake.

Wakati yule mwanamume akitaka kuzozana na kabwe mara yule dada aliyemkimbia Liston akarudi mle ndani ya ule ukumbi akiwa ameongozana na Meneja wa ile klabu na kuonekana akinyoosha kidole chake kuelekeza walipokuwa Kabwe na Liston.

Itaendelea...
 
Kizungumkuti! - 58

Na Bishop Hiluka

Jacky, in my life I’ve met many women but none of them are like you, I love you very much Jacky,” (Jacky, katika maisha yangu nimekutana na wanawake wengi lakini hakuna kati yao aliye kama wewe, nakupenda sana Jacky) Jacob alisema na kumkumbatia Jacky kwa nguvu.

Jacky aliachia tabasamu kisha akalipandisha juu gauni lake na hapo nguo yake ya ndani ikaonekena, taratibu akaanza kuishusha ile nguo na kuiweka pembeni huku akimtazama Jacob kwa namna iliyozidi kumchanganya mno.

Endelea...

Muda huo huo Jacky alimsogelea Jacob akaanza kuufungua mkanda wa suruali yake na mara suruali hiyo ikaanguka chini huku Jacob akibakiwa na boksa tu. Kisha aliivuta taratibu ile boksa ya Jacob, akaishusha hadi magotini na kuupeleka mkono wake ikulu. Jacob alianza kuhema ovyo utadhani bata, hakujiweza tena.

Jacky alimtazama Jacob kwa makini kisha akamsukuma, Jacob alianguka sakafuni kwenye zulia laini. Kabla hajajua afanye nini, Jacky alikuja juu yake na kumkalia, na muda mfupi uliofuata walikuwa pale sebuleni juu ya zulia, Jacob chini na Jacky juu huku Jacob akiishuhudia mijongeo ya Jacky ya taratibu alipokuwa akipanda juu na kushuka chini…

* * * * *

Saa tatu usiku wa siku ile iliwakuta Kabwe na Liston wakiwa katika ukumbi wa chini wa baa ya Masai Club iliyokuwa katika Barabara ya Mwinjuma, Kinondoni mkabala na benki ya ACB jijini Dar es Salaam.

Masai Club ilikuwa ni klabu ya usiku ya kisasa kabisa yenye kila kionjo cha burudani cha daraja la kimataifa ikiwa na kumbi tatu za baa, ukumbi mmoja ulikuwa katika eneo la chini na kumbi mbili zilikuwa ndani ya klabu.

Kulikuwa na ukumbi kwa ajili ya kujipatia vyakula vya kimataifa wenye meza ndefu za kisasa zilizozungukwa na viti vizuri vya sofa vyenye foronya laini pamoja na ukumbi mwingine mkubwa wenye jukwaa zuri lililokuwa linatazamana na viti vingi vya kisasa kwa ajili ya kufanyia shughuli za muziki na mikutano mbalimbali.

Kila ukumbi ulikuwa umejitenga na hivyo kutengeneza mgawanyo mzuri wa starehe tofauti zenye utulivu zilizoweza kufanyika kwa wakati mmoja.

Kabwe na Liston walikuwa katika ukumbi wa chini wa baa uliokuwa mkubwa na wenye uwezo wa kumeza watu wengi bila bugudha yoyote huku ukiwa na meza nyingi ndogo fupi na pana zilizozungukwa na viti vya mbao na vya plastiki.

Pia kulikuwa na meza nyingi za mchezo wa Pool table na kulikuwa na taa nzuri zenye mwanga hafifu zilikuwa zikiangaza mle ndani.

Kabwe na Liston walikuwa wameketi kwenye stuli ndefu katika kaunta ya ile baa, Kabwe alikuwa kaegemea kaunta na mbele yake kulikuwa na chupa kubwa ya pombe kali aina ya Grant’s Blended Scotch Whisky na bilauri.

Liston alikuwa akiongea na msichana mmoja mfanyakazi wa pale baa, aliyekuwa ameketi upande wa pili wa ile kaunta.

Kwenye ukumbi ule kulikuwa na wateja wengi waliokuwa wameketi kwa utulivu huku wakijipatia vinywaji na vyakula na wengine wakiendelea na maongezi yao.

Mzee mmoja alikuwa ameketi kwenye meza ya pembeni kabisa na msichana mzuri ambaye kimuonekana angeweza hata kuwa mjukuu wake na pengine ilikuwa hivyo, na walikuwa wakinywa soda.

Hapa na pale kulikuwa wasichana warembo kama machangudoa, waliokuwa wanazunguka zunguka wakiwa wamevaa nguo zilizokuwa zinaonesha sehemu kubwa ya miili yao na kuwavutia mno wanaume.

Kutokana na pilika pilika zao wakijipitisha huku na kule walionekana bila shaka yoyote kuwa walikuwa wakingoja kuopolewa.

Kulikuwa na wahudumu wa kike warembo waliokuwa wakihudumia wateja waliokuwa mle ndani ya ukumbi. Muziki laini ulikuwa ukisikika taratibu mle ndani ya ukumbi na hivyo kuzikonga vizuri nyoyo za watu waliokuwa ndani ya ule ukumbi.

Runinga pana zilizokuwa zimetundikwa ukutani mle ukumbini zilikuwa zimejikita katika kurusha burudani mbalimbali.

Kabwe na Liston walikuwa wameanza kulewa na muda ule Kabwe alikuwa akipiga kelele zilizokuwa zikiwakera wateja wengine ndani ya ule ukumbi wa baa. Wateja waliokuwemo ndani ya ule ukumbi walikuwa wakimtazama Kabwe kwa mshangao.

Kabwe aliinuka kutoka kwenye kiti alichokuwa amekalia akiwa ameshika ile chupa kubwa ya pombe kali na kuimimina yote chini huku akipiga kelele na kuyumba.

“Hii ni trela tu, picha kamili keshokutwa! Hakyamungu keshokutwa hakai mtu hapa… mi naapa! Nitakunywa na nitatembea uchi ukumbi mzima. Mademu wakinimaindi poa tu au vipi kichaa wangu?” Kabwe alipiga kelele na kuwafanya watu wote wageuke kumtazama kwa mshangao.

Muda ule Liston alikuwa analazimisha kumshika matiti dada mmoja asiyemjua, aliyepita karibu yake. Yule dada alikuwa amevaa t-shirt laini ya rangi nyeupe, sketi fupi ya rangi ya pinki, viatu virefu vya rangi ya pinki vyenye visigino virefu na wigi lenye nywele ndefu aligeuka kumtazama Liston kwa hasira na kusonya.

Kuona vile Liston alimvuta yule dada kwa nguvu na kumkumbatia kwa kuzungusha mikono yake kwenye kiuno cha yule dada. Yule dada alimsukuma Liston kwa nguvu, akamtazama kwa dharau kuanzia juu hadi chini, kisha akabinua midomo yake kwa dharau na kusonya.

“Wewe kaka vipi! Unadhani kila mwanamke anayeingia hapa ni malaya? Mimi siko hapa kujiuza,” yule dada alisema kwa hasira huku akimkazia macho Liston.

I don’t care who you are! Kama siyo malaya unatafuta nini hapa? Si ungekaa na mumeo nyumbani!” Liston alisema kwa sauti ya kilevi huku akiyumba.

“Wewe ni nani hadi unipangie maisha?” yule dada alisema kwa hasira na kusonya huku akibinua midomo yake kwa dharau.

“Mijanaume mingine sijui vipi, sijaja kwako kuomba msaada, kwa kipi kwanza ulichokuwa nacho!” alisema na kuanza kupiga hatua kuondoka.

I don’t give a shit!” Liston alisema huku akimdaka mkono yule dada na kuung’ang’ania huku akimvutia kwake huku akimfinyia macho yake kilevi.

“We mwanamke, unadhani mimi bwege kama hao mabwana zako, eh? Mimi nina hela ya kuulisha ukoo wenu wote kwa mwaka mzima,” Liston alisema huku akitema mate ya ulevi.

Yule dada aliutoa mkono wake kwa nguvu kutoka kwenye mkono wa Liston na kumchapa kibao cha uso huku akionekana kupandwa na hasira. Kisha aliondoka haraka kutoka eneo lile na kukimbilia nje ya ukumbi. Liston alijipangusa uso wake huku akisonya kwa hasira, kisha aligeuka kumtazama Kabwe.

“Eti yule malaya ananiletea pozi! Sasa keshokutwa ndiyo atanitambua mimi ni nani labda nisimuone, nitafanya mambo juu ya kaunta…” Liston alisema.

“Umeona eh! Yule bwana si katuahidi kutukatia hamsini zetu! Keshokutwa ndo watajua sisi ni nani, watu tumefanya kweli bladikenge, keshokutwa ndo keshokutwa, hapakaliki hapa,” Kabwe alipaza sauti yake na kurusha mkono wake hewani kitendo kilichomfanya kumpiga mwanamume mmoja aliyekuwa akipita karibu yake.

Wakati yule mwanamume akitaka kuzozana na kabwe mara yule dada aliyemkimbia Liston akarudi mle ndani ya ule ukumbi akiwa ameongozana na Meneja wa ile klabu na kuonekana akinyoosha kidole chake kuelekeza walipokuwa Kabwe na Liston.

Itaendelea...
Wakina Liston mbona wanataka kuharibu sasa

Pombe zina wenyewe aisee kuna watu vichwa vyepesi

Bishop wangu santeee ukipata kamda tuongezee episode nyingine nakupenda tu mm
 
Passed, Bishop ni Konk... Fire🔥🔥utabaki kileleni, juu mawinguni. In Pierre's voice.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom