Shupavu
JF-Expert Member
- Apr 23, 2015
- 371
- 526
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]Hahahah Bishop bwana nilikumiss tu mm
Unaanziaga mbali kweli mkuu.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]Hahahah Bishop bwana nilikumiss tu mm
Hahahahaaa[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Unaanziaga mbali kweli mkuu.
Kweli huu mwaka wako Shunie.Hahahaaa... Shunie ni very professional, she knows how to take care, hata kama ulikuwa hutaki utajikuta unavutika tu kama vile mbwa kaona chatu... 😀😀😀
Jacky hajawahi kuacha mwanaume salama...[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Unaanziaga mbali kweli mkuu.
Sem kweli jamani[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Unaanziaga mbali kweli mkuu.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Prisoner ebu acha kunifurahisha
Hahahahha
Nitakuja bwana naona umebadili avatar sasa miguu ya mzungu ya nn we binti tafuta kasura uweke
Wakina Liston mbona wanataka kuharibu sasaKizungumkuti! - 58
Na Bishop Hiluka
“Jacky, in my life I’ve met many women but none of them are like you, I love you very much Jacky,” (Jacky, katika maisha yangu nimekutana na wanawake wengi lakini hakuna kati yao aliye kama wewe, nakupenda sana Jacky) Jacob alisema na kumkumbatia Jacky kwa nguvu.
Jacky aliachia tabasamu kisha akalipandisha juu gauni lake na hapo nguo yake ya ndani ikaonekena, taratibu akaanza kuishusha ile nguo na kuiweka pembeni huku akimtazama Jacob kwa namna iliyozidi kumchanganya mno.
Endelea...
Muda huo huo Jacky alimsogelea Jacob akaanza kuufungua mkanda wa suruali yake na mara suruali hiyo ikaanguka chini huku Jacob akibakiwa na boksa tu. Kisha aliivuta taratibu ile boksa ya Jacob, akaishusha hadi magotini na kuupeleka mkono wake ikulu. Jacob alianza kuhema ovyo utadhani bata, hakujiweza tena.
Jacky alimtazama Jacob kwa makini kisha akamsukuma, Jacob alianguka sakafuni kwenye zulia laini. Kabla hajajua afanye nini, Jacky alikuja juu yake na kumkalia, na muda mfupi uliofuata walikuwa pale sebuleni juu ya zulia, Jacob chini na Jacky juu huku Jacob akiishuhudia mijongeo ya Jacky ya taratibu alipokuwa akipanda juu na kushuka chini…
* * * * *
Saa tatu usiku wa siku ile iliwakuta Kabwe na Liston wakiwa katika ukumbi wa chini wa baa ya Masai Club iliyokuwa katika Barabara ya Mwinjuma, Kinondoni mkabala na benki ya ACB jijini Dar es Salaam.
Masai Club ilikuwa ni klabu ya usiku ya kisasa kabisa yenye kila kionjo cha burudani cha daraja la kimataifa ikiwa na kumbi tatu za baa, ukumbi mmoja ulikuwa katika eneo la chini na kumbi mbili zilikuwa ndani ya klabu.
Kulikuwa na ukumbi kwa ajili ya kujipatia vyakula vya kimataifa wenye meza ndefu za kisasa zilizozungukwa na viti vizuri vya sofa vyenye foronya laini pamoja na ukumbi mwingine mkubwa wenye jukwaa zuri lililokuwa linatazamana na viti vingi vya kisasa kwa ajili ya kufanyia shughuli za muziki na mikutano mbalimbali.
Kila ukumbi ulikuwa umejitenga na hivyo kutengeneza mgawanyo mzuri wa starehe tofauti zenye utulivu zilizoweza kufanyika kwa wakati mmoja.
Kabwe na Liston walikuwa katika ukumbi wa chini wa baa uliokuwa mkubwa na wenye uwezo wa kumeza watu wengi bila bugudha yoyote huku ukiwa na meza nyingi ndogo fupi na pana zilizozungukwa na viti vya mbao na vya plastiki.
Pia kulikuwa na meza nyingi za mchezo wa Pool table na kulikuwa na taa nzuri zenye mwanga hafifu zilikuwa zikiangaza mle ndani.
Kabwe na Liston walikuwa wameketi kwenye stuli ndefu katika kaunta ya ile baa, Kabwe alikuwa kaegemea kaunta na mbele yake kulikuwa na chupa kubwa ya pombe kali aina ya Grant’s Blended Scotch Whisky na bilauri.
Liston alikuwa akiongea na msichana mmoja mfanyakazi wa pale baa, aliyekuwa ameketi upande wa pili wa ile kaunta.
Kwenye ukumbi ule kulikuwa na wateja wengi waliokuwa wameketi kwa utulivu huku wakijipatia vinywaji na vyakula na wengine wakiendelea na maongezi yao.
Mzee mmoja alikuwa ameketi kwenye meza ya pembeni kabisa na msichana mzuri ambaye kimuonekana angeweza hata kuwa mjukuu wake na pengine ilikuwa hivyo, na walikuwa wakinywa soda.
Hapa na pale kulikuwa wasichana warembo kama machangudoa, waliokuwa wanazunguka zunguka wakiwa wamevaa nguo zilizokuwa zinaonesha sehemu kubwa ya miili yao na kuwavutia mno wanaume.
Kutokana na pilika pilika zao wakijipitisha huku na kule walionekana bila shaka yoyote kuwa walikuwa wakingoja kuopolewa.
Kulikuwa na wahudumu wa kike warembo waliokuwa wakihudumia wateja waliokuwa mle ndani ya ukumbi. Muziki laini ulikuwa ukisikika taratibu mle ndani ya ukumbi na hivyo kuzikonga vizuri nyoyo za watu waliokuwa ndani ya ule ukumbi.
Runinga pana zilizokuwa zimetundikwa ukutani mle ukumbini zilikuwa zimejikita katika kurusha burudani mbalimbali.
Kabwe na Liston walikuwa wameanza kulewa na muda ule Kabwe alikuwa akipiga kelele zilizokuwa zikiwakera wateja wengine ndani ya ule ukumbi wa baa. Wateja waliokuwemo ndani ya ule ukumbi walikuwa wakimtazama Kabwe kwa mshangao.
Kabwe aliinuka kutoka kwenye kiti alichokuwa amekalia akiwa ameshika ile chupa kubwa ya pombe kali na kuimimina yote chini huku akipiga kelele na kuyumba.
“Hii ni trela tu, picha kamili keshokutwa! Hakyamungu keshokutwa hakai mtu hapa… mi naapa! Nitakunywa na nitatembea uchi ukumbi mzima. Mademu wakinimaindi poa tu au vipi kichaa wangu?” Kabwe alipiga kelele na kuwafanya watu wote wageuke kumtazama kwa mshangao.
Muda ule Liston alikuwa analazimisha kumshika matiti dada mmoja asiyemjua, aliyepita karibu yake. Yule dada alikuwa amevaa t-shirt laini ya rangi nyeupe, sketi fupi ya rangi ya pinki, viatu virefu vya rangi ya pinki vyenye visigino virefu na wigi lenye nywele ndefu aligeuka kumtazama Liston kwa hasira na kusonya.
Kuona vile Liston alimvuta yule dada kwa nguvu na kumkumbatia kwa kuzungusha mikono yake kwenye kiuno cha yule dada. Yule dada alimsukuma Liston kwa nguvu, akamtazama kwa dharau kuanzia juu hadi chini, kisha akabinua midomo yake kwa dharau na kusonya.
“Wewe kaka vipi! Unadhani kila mwanamke anayeingia hapa ni malaya? Mimi siko hapa kujiuza,” yule dada alisema kwa hasira huku akimkazia macho Liston.
“I don’t care who you are! Kama siyo malaya unatafuta nini hapa? Si ungekaa na mumeo nyumbani!” Liston alisema kwa sauti ya kilevi huku akiyumba.
“Wewe ni nani hadi unipangie maisha?” yule dada alisema kwa hasira na kusonya huku akibinua midomo yake kwa dharau.
“Mijanaume mingine sijui vipi, sijaja kwako kuomba msaada, kwa kipi kwanza ulichokuwa nacho!” alisema na kuanza kupiga hatua kuondoka.
“I don’t give a shit!” Liston alisema huku akimdaka mkono yule dada na kuung’ang’ania huku akimvutia kwake huku akimfinyia macho yake kilevi.
“We mwanamke, unadhani mimi bwege kama hao mabwana zako, eh? Mimi nina hela ya kuulisha ukoo wenu wote kwa mwaka mzima,” Liston alisema huku akitema mate ya ulevi.
Yule dada aliutoa mkono wake kwa nguvu kutoka kwenye mkono wa Liston na kumchapa kibao cha uso huku akionekana kupandwa na hasira. Kisha aliondoka haraka kutoka eneo lile na kukimbilia nje ya ukumbi. Liston alijipangusa uso wake huku akisonya kwa hasira, kisha aligeuka kumtazama Kabwe.
“Eti yule malaya ananiletea pozi! Sasa keshokutwa ndiyo atanitambua mimi ni nani labda nisimuone, nitafanya mambo juu ya kaunta…” Liston alisema.
“Umeona eh! Yule bwana si katuahidi kutukatia hamsini zetu! Keshokutwa ndo watajua sisi ni nani, watu tumefanya kweli bladikenge, keshokutwa ndo keshokutwa, hapakaliki hapa,” Kabwe alipaza sauti yake na kurusha mkono wake hewani kitendo kilichomfanya kumpiga mwanamume mmoja aliyekuwa akipita karibu yake.
Wakati yule mwanamume akitaka kuzozana na kabwe mara yule dada aliyemkimbia Liston akarudi mle ndani ya ule ukumbi akiwa ameongozana na Meneja wa ile klabu na kuonekana akinyoosha kidole chake kuelekeza walipokuwa Kabwe na Liston.
Itaendelea...