Stori ya kusisimua - Kizungumkuti!

Stori ya kusisimua - Kizungumkuti!

Habari za Jumamosi, ni siku nyingine tena tunakutana ndani ya dunia yenye KIZUNGUMKUTI, hapa kuna Carlos na Jacky, kule kuna Kabwe, Liston na Kisu, na huku kuna Yusuf, Jacob na bila kuwasahau ASP Komba na Sajenti Mapambano, halafu kwa mbaali nawaona warembo Diana na Zuhura a.k.a Mama Jasmine...

CC the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, Mine eyes, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY
Mkuu nimechekewa kufika huku nilipata majanga ya ajali, ila tupo pamoja
 
Kizungumkuti! - 53

Na Bishop Hiluka

ILIPOISHIA

“Sawa. Basi twende moja kwa moja kwenye hilo lililokuleteni,” Jacob alimweleza ASP Komba huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.

ASP Komba alimweleza Jacob msaada waliokuwa wakiuhitaji katika ofisi ile, Jacob akaona suala lile halikuhusiana na ofisi yake, hivyo akawachukua hadi kwa Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano wa kampuni ile.

Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano wa kampuni, Zuberi Mwalimu, hakuwa mtu mzima sana, alikuwa na miaka arobaini na mitano hivi, mwenye macho maangavu, uso wa duara na nywele ndogo ndogo alizokuwa amezinyoa mtindo wa low cut.

“Karibuni sana,” Zuberi Mwalimu aliwakaribisha huku akinyoosha mkono wake kwa ASP Komba na baadaye kwa Sajenti Mapambano. Walisalimiana kwa furaha, kisha Jacob akamweleza sababu ya ujio wa wale maofisa wa polisi pale ofisini kwao.

Endelea...

Baada ya maelezo yale yule Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano aliinua simu, akamwita Jonas Maganga, mtaalamu wa masuala ya teknolojia ya habari na mawasiliano ambaye alikuwa tegemea kubwa katika kampuni ile, baada ya kuondoka kwa Jackline Mgaya.

Ndani ya dakika mbili Jonas alikuwa amefika katika ofisi ya bosi wake Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano kuitika ule wito. Alikuwa kijana mrefu wa wastani na hakuwa na umri wa zaidi ya miaka thelathini.

Alikuwa amevaa shati jeupe la mikono mirefu na juu yake alivaa koti jeusi lililokuwa na mistari myeupe, na saa ya mkononi. Chini alivaa suruali ya kadeti ya rangi ya kaki na buti ngumu za ngozi miguuni.

Yule Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano alimweleza yule kijana kilichowaleta pale wale maofisa wa polisi na kumpa zile namba nne ambazo ASP Komba na Sajenti Mapambano walikuwa wamezitilia shaka kutoka katika simu ya Yusuf.

“Jonas, tafadhali fuatilia hizi namba kwenye kompyuta na utupatie taarifa zote muhimu za wateja wenye kumiliki namba hizi, ikiwemo majina yao, namba za vitambulisho vyao walivyotumia kusajili, locations zao, na namba zote ambazo zimekuwa zikiwasiliana na namba hizi kwa tarehe husika na saa… sijui itakuchukua muda gani kuifanya kazi hii, maana taarifa hii inatakiwa haraka sana,” yule Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano alimwambia Jonas huku akimkazia macho.

Jonas aliipokea ile karatasi yenye zile namba akaziangalia zile namba kwa kitambo nkifupi huku akifikiria kidogo, “Wala haitachukua muda, boss. Yote hayo yamo kwenye Kompyuta.”

“Kama nusu saa?” yule Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano aliuliza kwa shauku.

“Haifiki, ni kama dakika kumi hadi kumi na tano tu zinanitosha kuimaliza kazi.”

“Ooh, basi itakuwa vyema!” yule Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano alisema huku akitabasamu.

Jonas aliwatupia jicho ASP Komba na Sajenti Mapambano haraka haraka na kuachia tabasamu kisha alitoka haraka huku macho ya wale maofisa wa polisi yakimfuata hadi alipotoka kabisa na kuufunga mlango wa ile ofisi.

“Huyu kijana ndiye tegemeo letu hapa ofisini kwa sasa, kwa kweli anastahili makubwa zaidi… hamtaamini jinsi atakavyoifanya kazi hii kwa uharaka sana na kuleta majibu chanya,” yule Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano aliwaambia wale maofisa wa polisi baada ya Jonas kuondoka.

“Anaonekana tu kwa jinsi anavyojiamini,” ASP Komba alisema akionekana kuafiki.

“Je, mnadhani hii inaweza kuwa njia sahihi ya kuwakamata hao wezi? Na kama hawakutumia mawasiliano ya simu…” yule Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano alimuuliza ASP Komba huku akimkazia macho lakini ASP Komba alimkatisha kabla hata hajamaliza kuongea.

“Kwetu, hilo si suala la kudhani, tumekwisha fanya kazi nyingi na ngumu za uhalifu hatari zaidi wa mtandaoni na kufanikiwa. Vyovyote iwavyo lazima tuwatie mbaroni tu,” ASP Komba alisema katika namna ya kujigamba huku akimtupia jicho Jacob.

Kisha yule Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano aliamua kubadilisha maongezi, na baada ya takriban dakika kumi na tano Jonas alirejea ofisini kwa Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano akiwa ameshika karatasi kadhaa zilizokuwa zimechapwa kwa maandishi ya kompyuta zikiwa na taarifa zote muhimu zilizohitajika.

Alipoingia alizikkabidhi karatasi zile kwa Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano. Yule Mkurugenzi alizipokea zile karatasi na kuanza kuzipitia papo hapo huku uso wake ukichanua kwa tabasamu dogo la kuridhika na alichokiona. Kisha alimkabishi ASP Komba.

“Naona kijana amefanya kazi nzuri sana, kila ulichohitaji kuhusu hizo namba kimo humo, hebu zipitie kwanza hapa hapa ujiridhishe kabla hujaondoka ili uone kama bado kuna chochote ungependa kutafutiwa.”

ASP Komba na Sajenti Mapambano walizipitia zile karatasi haraka haraka kwa kupokezana kisha ASP Komba alisimama kutoka kwenye kiti alichoketi na kumpa mkono yule Mkurugenzi kumshukuru huku akionesha furaha yake.

“Naona mtaalamu kafanya kazi kubwa na nzuri sana, tunashukuru kwa kweli,” ASP Komba alisema kwa furaha huku akimpa mkono kwa pongezi Jonas.

“Hata hivyo, kuna namba moja kati ya hizo imenisumbua kidogo, ilikuwa imewekewa mfumo maalumu wa kiulinzi,” Jonas alimwambia ASP Komba huku akimtazama kwa makini.

“Una maana gani unaposema mfumo maalumu wa kiulinzi?” ASP Komba alimwuliza Jonas huku akimtulizia macho yake.

“Inaonekana wazi mtumiaji wa namba hiyo ni mtaalamu aliyebobea sana kwenye masuala ya teknolojia ya habari na mawasiliano na ana ufahamu mkubwa sana wa masuala ya kompyuta, aliiwekea namba yake programu maalumu ambayo inamuwezesha mtumiaji wa namba hiyo kutojulikana mahali alipo na ameweza hata kuzuia mawasiliano yake yasiingiliwe na watu wengine, na pia aliifanya namba hiyo kutumika katika simu yake tu.”

“Duh, natumai umefanikiwa kuiondoa hiyo programu ya kiulinzi, siyo?” ASP alimuuliza Jonas kwa shauku huku akimtulizia macho kwa makini.

“Ndiyo, nimeweza kuiondoa programu hiyo japo imenipa shida kidogo, sasa mtaweza kuona jinsi anavyoweza kuwasiliana na watu wengine ingawa mahali alipo wakati anawasiliana na watu bado inaweza kuwa shida,” Jonas alisema huku akishusha pumzi ndefu.

“Hata hivyo, umetusaidia sana… enhe, ni namba ipi kati ya hizi?” ASP Komba alimuuliza Jonas kwa shauku huku akimsogezea zile karatasi.

“Ni hii hapa!” Jonas alisema huku akimwonesha ASP Komba ile namba baada ya kuzitazama zile namba kwa makini.

Itaendelea...

CC the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, Mine eyes, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY IFRS
Shukrani sana boss wangu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom