Bishop Hiluka
R I P
- Aug 12, 2011
- 7,150
- 14,724
- Thread starter
- #341
Kizungumkuti! - 49
Na Bishop Hiluka
ILIPOISHIA
Alisoma ujumbe kwa umakini huku akizinakiri baadhi ya namba za simu zilizokuwa zimetumika kutuma ule ujumbe na kuandika taarifa fulani kwenye kitabu chake kidogo na alipomaliza kuandika aliinua uso wake kumtazama Nassos huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.
“You’re welcome,” (Karibu sana) ASP Komba alimkaribisha Nassos kana kwamba ndiyo alikuwa amemuona kwa mara ya kwanza.
“Thank you, officer,” (Ahsante, afande) Nassos alijibu huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.
“Do you know Swahili?” (Unajua Kiswahili?) ASP Komba alimuuliza huku akimtulizia macho.
“Yes, but a little, officer,” (Ndiyo, lakini kidogo, afande) Nassos alijibu kwa kujiamini.
“Are you the chief executive director of The Jacarandah Group, right?” (Wewe ndiye mkurugenzi mtendaji wa The Jacarandah Group, sawa?) ASP Komba alimuuliza Nassos huku akiwa amemtulizia macho yake usoni pasipo kupepesa.
“Yes, officer,” (Ndiyo, afande) Nassos alisema huku akilamba midomo yake iliyoanza kukauka.
Endelea...
“I’ve information that you went to the Commercial Bank four days ago to put a large amount of money, and the next day you took a certain amount of money… Do you remember the amount of money you took that day?” (Ninazo taarifa kwamba ulifika pale Benki ya Biashara siku nne zilizopita kuweka kiasi kikubwa cha pesa, kisha kesho yake ukatoa kiasi fulani cha pesa… Je, unakumbuka idadi ya pesa ulizochukua siku hiyo?)
“I took only four hundred million shillings, officer.” (Nilichukua shilingi milioni mia nne tu, afande).
“Since that day you’ve never signed in any check from your office?” (Tangu siku ile hujatia tena saini katika hundi yoyote ya ofisini kwenu?)
“Not yet!” (Bado!)
ASP Komba aliminya midomo yake na kushusha pumzi za ndani kwa ndani akionekana kutafakari kidogo, kisha alinyoosha mkono wake kumpa Nassos ile hundi.
“Can you look well and identify for those signatures?” (Unaweza kuziangalia vizuri na kuzitambua hizo saini hapo?) ASP Komba alisema huku kamkazia macho Nassos. Nassos aliipokea ile hundi na kuitazama kwa makini, alitingisha kichwa chake kwa huzuni huku akishusha pumzi ndefu.
“I’m very shocked, this one is my very signature, but I did not sign in this check!” (Imenishangaza sana, afande, hii moja ni saini yangu kabisa, lakini mimi sikutia saini kwenye hundi hii!) Nassos alisema kwa masikitiko huku akimrudishia ASP Komba ile hundi.
“And who’s this other sign?” (Na hii saini nyingine ni ya nani?) ASP Komba aliuliza.
“It belongs to my accountant, Japhet Lutego, but I'm sure he didn't sign this check,” (Ni ya aliyekuwa mhasibu wangu, Japhet Lutego, lakini nina uhakika pia yeye hakusaini hundi hii) Nassos alisema kwa kujiamini.
“Why are you sure that he was not the one who signed?” (Kwa nini una uhakika kuwa si mhasibu wako aliyesaini?)
“Because he has traveled to Sweden since last week, and if he’d have been involved in this scandal he’d have not left before this robbery. He’d have possibly waited for his portion.” (Kwa sababu amesafiri tangu wiki iliyopita kwenda masomoni Sweden, na angekuwa ameshiriki kwenye kashfa hii asingeondoka kabla wizi huu mkubwa haujafanyika. Kwa vyovyote angesubiri mgawo wake).
“How do you know, maybe he decided to travel before this robbery just to complicate the evidence that he was involved and he might ask them to send his portion there where he went?” (Unajuaje, pengine aliamua kusafiri kabla ya wizi huu ili kupoteza ushahidi kuwa alishiriki na huenda aliomba atumiwe mgawo wake huko huko alikokwenda?) ASP Komba aliuliza tena huku akikunja sura yake.
Nassos alikunja sura yake kutafakari kidogo, kikapita kitambo kifupi cha ukimya kisha alitingisha kichwa chake kukataa.
“I don't think so… anyway, I don't know,” (Sidhani… hata hivyo, siwezi kujua) Nassos alisema huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.
Kilipita tena kitambo kifupi cha ukimya, ASP Komba alimtazama Nassos kwa huku akitafakari, kisha alikohoa kidogo kusafisha koo lake. “Tell me, who exactly is keeping your check book?” (Hebu niambie, ni nani hasa anayetunza kitabu cha hundi ofisini kwenu?)
“It's me!” (Ni mimi!) Nassos alijibu.
“Do you lock it or leave with it?” (Huwa unakifungia kabatini au unaondoka nacho?)
“I don't lock it or leave with it, it's always on my table…” (Sikifungii wala siondoki nacho, mara nyingi huwa kipo juu ya meza yangu…)
“Who enters your office regularly?” (Ni nani anayeingia ofisini kwako mara kwa mara?)
“I don't allow people to go into my office, and if a person needs a loan we have a system that he or she’d meet my accountant and then all procedures are followed…” (Huwa siruhusu watu kuingia ofisini kwangu, na kama mtu anahitaji mkopo tuna utaratibu kwamba aonane na mhasibu wangu na kisha taratibu zote hufuatwa…) Nassos alisema kwa utulivu.
Kikapita tena kitambo kifupi cha ukimya, Nassos alikuwa ameinamisha kichwa chake akitafakari kidogo, mara alionekana kugutuka na kuinua uso wake kumtazama ASP Komba.
ASP Komba ambaye muda wote alikuwa akimtazama Nassos kwa makini aliingiwa na shauku baada ya kumuona Nassos akigutuka na kumkazia macho.
“Is there anything you want to share with me?” (Kuna kitu unataka kunishirikisha?) ASP Komba aliuliza kwa shauku.
“I remember, there is only one person who is free to enter my office at any time, but I don't think if she can be involved with a big deal like this…” (Nimekumbuka, kuna mtu mmoja tu ambaye huwa yuko huru kuingia ofisini kwangu saa yoyote, lakini sidhani kama anaweza kuhusika na njama kubwa kiasi hiki…) Nassos alisema huku akikunja sura yake.
“Who is she?” (Ni nani?) ASP Komba aliuliza tena kwa shauku.
“Her name is Jasmine Kombo. She deals with the cleanliness of my office.” (Anaitwa Jasmine Kombo. Yeye hushughulikia usafi wa ofisi yangu.)
ASP Komba aliinamisha uso wake kwenye notebook yake na kuandika maelezo mafupi huku akilipigia mstari jina la Jasmine, kisha akamkazia macho Nassos.
“How long have you worked with Jasmine?” (Umefanya kazi na Jasmine kwa muda gani sasa?)
“This is the fifth year now,” (Huu mwaka wa tano sasa) Nassos alijibu baada ya kufikiria kidogo.
“Can I have an interrogation with her?” (Naweza kumpata ili nimhoji?)
“I wonder, today is the third day she has not come to work and I’ve no information, I don't know what has happened to her!” (Nashangaa, leo ni siku ya tatu hajafika kazini na sina taarifa zake, sijui amepatwa na nini!) Nassos alisema huku akinyanyua juu mabega yake juu kuonesha kuwa hajui.
Maelezo ya Nassos yakamfanya ASP Komba aweke kituo na kumtazama Nassos kwa macho yaliyoonesha kuhisi jambo lisilo la kawaida. Aligeuza kichwa chake kumtazama Sajenti Mapambano, kisha aliyarudisha tena macho yake kwa Nassos.
“Your employee has not come to work without notice for three days and you’re not worried even to look for her! Don't you see this is not normal?” (Mfanyakazi wako hajatokea kazini pasipo taarifa kwa siku tatu na wala hujahangaika kumtafuta! Huoni kama hili si jambo la kawaida?) ASP Komba aliuliza huku akivuta sigara yake kwa mara mwisho na kuupuliza moshi pembeni.
Itaendelea...
Na Bishop Hiluka
ILIPOISHIA
Alisoma ujumbe kwa umakini huku akizinakiri baadhi ya namba za simu zilizokuwa zimetumika kutuma ule ujumbe na kuandika taarifa fulani kwenye kitabu chake kidogo na alipomaliza kuandika aliinua uso wake kumtazama Nassos huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.
“You’re welcome,” (Karibu sana) ASP Komba alimkaribisha Nassos kana kwamba ndiyo alikuwa amemuona kwa mara ya kwanza.
“Thank you, officer,” (Ahsante, afande) Nassos alijibu huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.
“Do you know Swahili?” (Unajua Kiswahili?) ASP Komba alimuuliza huku akimtulizia macho.
“Yes, but a little, officer,” (Ndiyo, lakini kidogo, afande) Nassos alijibu kwa kujiamini.
“Are you the chief executive director of The Jacarandah Group, right?” (Wewe ndiye mkurugenzi mtendaji wa The Jacarandah Group, sawa?) ASP Komba alimuuliza Nassos huku akiwa amemtulizia macho yake usoni pasipo kupepesa.
“Yes, officer,” (Ndiyo, afande) Nassos alisema huku akilamba midomo yake iliyoanza kukauka.
Endelea...
“I’ve information that you went to the Commercial Bank four days ago to put a large amount of money, and the next day you took a certain amount of money… Do you remember the amount of money you took that day?” (Ninazo taarifa kwamba ulifika pale Benki ya Biashara siku nne zilizopita kuweka kiasi kikubwa cha pesa, kisha kesho yake ukatoa kiasi fulani cha pesa… Je, unakumbuka idadi ya pesa ulizochukua siku hiyo?)
“I took only four hundred million shillings, officer.” (Nilichukua shilingi milioni mia nne tu, afande).
“Since that day you’ve never signed in any check from your office?” (Tangu siku ile hujatia tena saini katika hundi yoyote ya ofisini kwenu?)
“Not yet!” (Bado!)
ASP Komba aliminya midomo yake na kushusha pumzi za ndani kwa ndani akionekana kutafakari kidogo, kisha alinyoosha mkono wake kumpa Nassos ile hundi.
“Can you look well and identify for those signatures?” (Unaweza kuziangalia vizuri na kuzitambua hizo saini hapo?) ASP Komba alisema huku kamkazia macho Nassos. Nassos aliipokea ile hundi na kuitazama kwa makini, alitingisha kichwa chake kwa huzuni huku akishusha pumzi ndefu.
“I’m very shocked, this one is my very signature, but I did not sign in this check!” (Imenishangaza sana, afande, hii moja ni saini yangu kabisa, lakini mimi sikutia saini kwenye hundi hii!) Nassos alisema kwa masikitiko huku akimrudishia ASP Komba ile hundi.
“And who’s this other sign?” (Na hii saini nyingine ni ya nani?) ASP Komba aliuliza.
“It belongs to my accountant, Japhet Lutego, but I'm sure he didn't sign this check,” (Ni ya aliyekuwa mhasibu wangu, Japhet Lutego, lakini nina uhakika pia yeye hakusaini hundi hii) Nassos alisema kwa kujiamini.
“Why are you sure that he was not the one who signed?” (Kwa nini una uhakika kuwa si mhasibu wako aliyesaini?)
“Because he has traveled to Sweden since last week, and if he’d have been involved in this scandal he’d have not left before this robbery. He’d have possibly waited for his portion.” (Kwa sababu amesafiri tangu wiki iliyopita kwenda masomoni Sweden, na angekuwa ameshiriki kwenye kashfa hii asingeondoka kabla wizi huu mkubwa haujafanyika. Kwa vyovyote angesubiri mgawo wake).
“How do you know, maybe he decided to travel before this robbery just to complicate the evidence that he was involved and he might ask them to send his portion there where he went?” (Unajuaje, pengine aliamua kusafiri kabla ya wizi huu ili kupoteza ushahidi kuwa alishiriki na huenda aliomba atumiwe mgawo wake huko huko alikokwenda?) ASP Komba aliuliza tena huku akikunja sura yake.
Nassos alikunja sura yake kutafakari kidogo, kikapita kitambo kifupi cha ukimya kisha alitingisha kichwa chake kukataa.
“I don't think so… anyway, I don't know,” (Sidhani… hata hivyo, siwezi kujua) Nassos alisema huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.
Kilipita tena kitambo kifupi cha ukimya, ASP Komba alimtazama Nassos kwa huku akitafakari, kisha alikohoa kidogo kusafisha koo lake. “Tell me, who exactly is keeping your check book?” (Hebu niambie, ni nani hasa anayetunza kitabu cha hundi ofisini kwenu?)
“It's me!” (Ni mimi!) Nassos alijibu.
“Do you lock it or leave with it?” (Huwa unakifungia kabatini au unaondoka nacho?)
“I don't lock it or leave with it, it's always on my table…” (Sikifungii wala siondoki nacho, mara nyingi huwa kipo juu ya meza yangu…)
“Who enters your office regularly?” (Ni nani anayeingia ofisini kwako mara kwa mara?)
“I don't allow people to go into my office, and if a person needs a loan we have a system that he or she’d meet my accountant and then all procedures are followed…” (Huwa siruhusu watu kuingia ofisini kwangu, na kama mtu anahitaji mkopo tuna utaratibu kwamba aonane na mhasibu wangu na kisha taratibu zote hufuatwa…) Nassos alisema kwa utulivu.
Kikapita tena kitambo kifupi cha ukimya, Nassos alikuwa ameinamisha kichwa chake akitafakari kidogo, mara alionekana kugutuka na kuinua uso wake kumtazama ASP Komba.
ASP Komba ambaye muda wote alikuwa akimtazama Nassos kwa makini aliingiwa na shauku baada ya kumuona Nassos akigutuka na kumkazia macho.
“Is there anything you want to share with me?” (Kuna kitu unataka kunishirikisha?) ASP Komba aliuliza kwa shauku.
“I remember, there is only one person who is free to enter my office at any time, but I don't think if she can be involved with a big deal like this…” (Nimekumbuka, kuna mtu mmoja tu ambaye huwa yuko huru kuingia ofisini kwangu saa yoyote, lakini sidhani kama anaweza kuhusika na njama kubwa kiasi hiki…) Nassos alisema huku akikunja sura yake.
“Who is she?” (Ni nani?) ASP Komba aliuliza tena kwa shauku.
“Her name is Jasmine Kombo. She deals with the cleanliness of my office.” (Anaitwa Jasmine Kombo. Yeye hushughulikia usafi wa ofisi yangu.)
ASP Komba aliinamisha uso wake kwenye notebook yake na kuandika maelezo mafupi huku akilipigia mstari jina la Jasmine, kisha akamkazia macho Nassos.
“How long have you worked with Jasmine?” (Umefanya kazi na Jasmine kwa muda gani sasa?)
“This is the fifth year now,” (Huu mwaka wa tano sasa) Nassos alijibu baada ya kufikiria kidogo.
“Can I have an interrogation with her?” (Naweza kumpata ili nimhoji?)
“I wonder, today is the third day she has not come to work and I’ve no information, I don't know what has happened to her!” (Nashangaa, leo ni siku ya tatu hajafika kazini na sina taarifa zake, sijui amepatwa na nini!) Nassos alisema huku akinyanyua juu mabega yake juu kuonesha kuwa hajui.
Maelezo ya Nassos yakamfanya ASP Komba aweke kituo na kumtazama Nassos kwa macho yaliyoonesha kuhisi jambo lisilo la kawaida. Aligeuza kichwa chake kumtazama Sajenti Mapambano, kisha aliyarudisha tena macho yake kwa Nassos.
“Your employee has not come to work without notice for three days and you’re not worried even to look for her! Don't you see this is not normal?” (Mfanyakazi wako hajatokea kazini pasipo taarifa kwa siku tatu na wala hujahangaika kumtafuta! Huoni kama hili si jambo la kawaida?) ASP Komba aliuliza huku akivuta sigara yake kwa mara mwisho na kuupuliza moshi pembeni.
Itaendelea...