Stori ya kusisimua - Kizungumkuti!

Stori ya kusisimua - Kizungumkuti!

Kizungumkuti! - 44

Na Bishop Hiluka

ILIPOISHIA

Jacky akaanza kuliondoa gari lake taratibu akielekea mbele nia yake ilikuwa kuchukua uelekeo wa kurudi Mtoni Kijichi baada ya kufika kwenye mzunguko wa barabara mbele kidogo ya viwanja vya Sabasaba, mara akaliona gari aina ya Toyota Lexus RX la rangi nyeusi likija nyuma yake kwa mwendo wa kasi.

Jacky alipunguza mwendo ili kulipisha lile gari lipite lakini lile gari lilipokuwa likimpita ghafla likapunguza kidogo mwendo huku magurudumu yake yakiserereka kwenye barabara ya lami na baadaye gari likaanza kwenda sambasamba na gari la Jacky. Ikabidi Jacky ageuze shingo yake kumtazama dereva wa lile gari kwa jicho la wasiwasi kidogo.

Endelea...

Macho yake yalitia nanga kwenye sura ya kijana mtanashati aliyekuwa akiendesha lile gari ambaye alikuwa akimtazama Jacky kwa umakini sana na kuonesha kubabaishwa kidogo na uzuri wake. Sura ya yule mwanamume ilionesha uchangamfu na macho yake yalikuwa makini kuliko hata simba anayewinda.

Yule mwanamume alionekana kama aliyekuwa akihisi msisimko wa ajabu ukimtambaa mwilini mwake na kuzifanya nywele zake kumsimama baada ya kumuona Jacky. Midomo yake ilionesha kumkauka ghafla na mapigo ya moyo wake yakabadilika na kuanza kukimbia.

Alimtazama Jacky kwa umakini akijihisi kama yupo ndotoni, hata hivyo, milango yake ya fahamu ilikuwa makini zaidi kujaribu kuishirikisha akili yake kikamilifu kuhusu kile alichokuwa amekiona mbele yake.

Jacky aliligundua hilo, hivyo akaachia tabasamu laini ili kumchanganya zaidi yule mwanamume huku akimtazama kwa makini, hata hivyo alijikuta akiwa ameupita ule mzunguko wa barabara ambapo alitarajia kugeuza ili kurudi Mtoni Kijichi, na wakati huo alikuwa karibu kabisa na eneo la Uhasibu, hivyo akaanza kuongeza mwendo ili kuliacha lile gari lakini kabla hajaliacha akahisi sauti ikiliitwa jina lake.

“Jackline!” yule mwanamume alikuwa ameshusha kioo cha gari lake na kuita kwa sauti kubwa iliyopenya hadi kwenye ngoma ya sikio la Jacky, japokuwa alikuwa amepandisha vioo vya gari lake lakini aliweza kuisikia vyema ile sauti. Jacky aligeuza tena shingo yake kumtazama yule mwanamume na ndipo alipogundua kuwa hata yeye alikuwa anamfahamu.

“Jacob!” alijikuta akilitamka jina hilo kwa mshangao huku akikanyaga breki, gari likaserereka kwenye lami na kuyumba kidogo, kisha akaliegesha gari lake kando ya barabara ya Kilwa mbele ya kituo cha daladala cha Uhasibu. Jacob naye alikanyaga breki na kusimama akiliegesha gari lake mbele ya gari la Jacky kisha akateremka kumfuata.

Hallow Jackline, how are you doing? I missed you so much, my love,” (Hallo Jackline, habari gani? Nilikumisi sana, mpenzi wangu) yule mwanamume alimsalimia Jacky mara tu alipomfikia.

What do you want from me?” (Unataka nini kwangu?) Jacky alimuuliza yule mwanamume na mara moja akayakwepesha macho yake baada ya kugundua kuwa alikuwa akimtazama usoni kwa makini.

Yule mwanamume aliendelea kumtazama Jacky kwa kitambo huku akitabasamu kisha akavuta pumzi ndefu na kuzishusha taratibu.

Oh Jackline, don't you just leave your mockeries?” (Oh Jackline, hujaacha tu masihala yako?) yule mwanamume alisema huku akiendelea kutabasamu.

Jacob, say what you want to say and leave immediately, I don’t need you anymore,” ((Jacob, sema unachotaka kusema na uondoke mara moja, sikuhitaji tena) Jacky alisema kwa sauti iliyoonesha kwamba hakuwa akitania.

“Jacky, when will you open again your heart to me? When will you be ready to sit and listen to me?” (Jacky, Hivi ni lini utaufungua tena moyo wako kwangu? Lini utakuwa tayari kukaa na kunisikiliza?) yule mwanamume alimuuliza Jacky kwa sauti tulivu ya kubembeleza lakini Jacky hakumjibu na badala yake aliachia tabasamu la dharau.

Why did you fail even to look for me as we had planned?” (Kwa nini umeshindwa hata kunitafuta kama tulivyokuwa tumepanga?) yule mwanamume aliendelea kumuuliza huku akimkazia macho. Jacky alivuta pumzi ndefu na kuzishusha taratibu.

Mr Jacob, can you please stop this drama? It’s over between us,” (Bwana Jacob, unaweza kuachana na haya maigizo? Mimi na wewe tulikwisha malizana) hatimaye Jacky alimwambia yule mwanamume huku akimkazia macho yake.

“What?” (Nini?) yule mwanamume alimuuliza Jacky huku akimtazama kwa makini.

We can’t go on like this, stop drama and don’t waste your time following me, it’s time to end things now,” (Hatuwezi kwenda hivi, acha maigizo na usipoteze muda wako kunifuatilia, ni muda sasa wa kusitisha mambo haya) Jacky alisema huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.

Why do we need to end it so inappropriately?” (Kwa nini tusitishe mambo kienyeji?) yule mwanamume aliuliza huku akimkazia macho Jacky kisha akaendelea, “Ni hapo tu unaponiudhi…”

“Jacob…” Jacky alitaka kusema neno lakini Jacob akamzuia.

Don’t say anything, Jacky. You know exactly how much I love you and I’ll never stop loving you no matter what,” (Usiongee chochote Jacky. Unajua kabisa ni jinsi gani nakupenda na sitaacha kukupenda hata iweje) yule mwanamume aliongea kwa sauti yenye ukali kidogo.

Liar!” (Muongo!) Jacky naye alisema kwa sauti yenye ukali kidogo.

I’m not a liar, I love you with all my heart,” (Mimi si muongo, ninakupenda kwa moyo wangu wote) yule mwanamume alisema kwa sauti tulivu na ya kubembeleza.

Jacky alishusha pumzi za ndani kwa ndani huku akiinua mabega yake juu na kubetua midomo akiashiria kuwa hana namna ya kufanya.

Jacky, why can’t we skip the past and talk about our future?” (Jacky, kwa nini tusiachane na mambo yaliyopita na kuzungumzia mustakabali wetu?) yule mwanamume alimwambia Jacky huku akimtazama machoni.

It’s not easy, Jacob. You know exactly how much I loved you very much but you broke my heart! I was real disappointed, very disappointed,” (Siyo rahisi. Unajua hasa kiasi gani nilikupenda sana lakini ukautia moyo wangu majeraha! Nilifadhaika kweli kweli, nilifadhaika sana) Jacky alisema huku akishusha pumzi ndefu.

I’m sorry for everything, I’m real very sorry,” (Nasikitika kwa yote, nasikitika sana kwa kweli).

Nothing has changed. You’re still the same deceiver… by the way, can you be honest with me, Jacob, where is Diana?” (Hakuna kilichobadilika. Wewe ni yule yule msaliti… hivi unaweza kuniambia ukweli, Jacob, Diana yuko wapi?) Jacky alimuuliza Jacob huku akimkazia macho.

She is married and living happily with her police officer, ASP Komba…” (Kaolewa na anaishi maisha ya furaha na mumewe ofisa wa polisi, ASP Komba…) Jacob alisema huku akijiegemeza kwenye gari la Jacky.

And… I guess you’re still making love with her, right?” (Na… nihisi bado utakuwa unatembea naye, sawa?) Jacky alimuuliza Jacob huku akiwa amemkazia macho.

Nope, how’d I do that?” (Hapana, kwa nini nifanye hivyo?) Jacob alijitetea huku akitingisha kichwa chake kukataa.

Are you married?” (Umeoa?) Jacky alimuuliza Jacob swali jingine akiwa bado amemkazia macho.

I am still single, all three years I have been looking for you…” (Bado sijaoa, miaka yote mitatu nimekuwa nikikutafuta wewe…) Jacob alimwambia Jacky kwa sauti tulivu ya kusihi.

You’re a liar, by the way, I’m already married,” Jacky alisema huku akimkazia macho Jacob.

“You must be kidding! Well…” (Kwa vyovyote utakuwa unatania! Sawa…) Jacob alisema na kutoa Jacky business card akionekana mwenye haraka kidogo, akanyoosha mkono wake kumpa Jacky ile kadi.

Itaendelea...
 
Kizungumkuti! - 45

Na Bishop Hiluka

Are you married?” (Umeoa?) Jacky alimuuliza Jacob swali jingine akiwa bado amemkazia macho.

I am still single, all three years I have been looking for you…” (Bado sijaoa, miaka yote mitatu nimekuwa nikikutafuta wewe…) Jacob alimwambia Jacky kwa sauti tulivu ya kusihi.

You’re a liar, by the way, I’m already married,” Jacky alisema huku akimkazia macho Jacob.

“You must be kidding! Well…” (Kwa vyovyote utakuwa unatania! Sawa…) Jacob alisema na kutoa Jacky business card akionekana mwenye haraka kidogo, akanyoosha mkono wake kumpa Jacky ile kadi.

Endelea...

“This is my number, please let’s keep in touch, I'm on my way to the police station, my friend has been arrested,” (Hii ni namba yangu, tafadhali tuwasiliane, kwa sasa naelekea kituo cha polisi, rafiki yangu amekamatwa) Jacob alisema na kuanza kuondoka haraka.

Jacky alionekana kushtuka sana baada ya kusikia habari za mtu kukamatwa na hakujua kwa nini alishtuka! Hata hivyo, alijikuta akitokwa na jasho jepesi mwilini na mapigo ya moyo wake yakabadili mwendo wake na kwenda mbio isivyo kawaida!

His friend has been arrested! Who?” (Rafiki yake amekamatwa! Nani?) Jacky aliwaza huku akitamani kumuuliza Jacob ni rafiki yake yupi kati ya aliowahi kuwafahamu, hata hivyo aliamua kubaki kimya, alimshuhudia Jacob akiingia kwenye gari lake kisha akaliondoka kwa mwendo wa kasi kuelekea mjini.

Jacky alilisindikiza kwa macho lile gari hadi lilipopotea kwenye upeo wa macho yake, kisha mawazo mengi yakaanza kupita kichwani kwa Jacky, Mawazo yaliyompeleka mbali miaka mitatu na ushee iliyokuwa imepita, kuhusu uhusiano wake na Jacob Haule, wakati huo walikuwa wakifanya kazi pamoja katika kampuni ya simu jijini Dar es Salaam.

I loved him very much and we spent so many beautiful moments together… but the moment I turned my back, he was cheating me…” (Nilimpenda sana na muda mwingi tulifurahia pamoja… lakini kila nilipompa mgongo tu, alikuwa akinisaliti…) Jacky aliwaza.

Jacky alikumbuka jinsi yeye na Jacob walivyoajiriwa kwa wakati mmoja katika kampuni ile kubwa ya simu nchini, Jacky aliajiriwa kama mtaalamu wa habari na mawasiliano baada ya kuhitimu Shahada ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Information Technology), na Jacob aliajiriwa kama mkurugenzi wa masoko akiwa amehitimu shahada ya pili ya Sanaa katika Uongozi wa Masoko (Master of Arts in Marketing Management).

Kwa wakati huo Jacob alikuwa na wiki chache tu tangu aliporejea Tanzania akitokea nchini Uingereza alikokuwa akifanya kazi, baada ya kuhitimu masomo yake.

Kutokana na kufanya kazi katika ofisi moja, Jacky na Jacob walijikuta wakijenga ukaribu zaidi na haikuwachukua muda mrefu kuzoeana sana, kisha urafiki wao uliposhamiri hatimaye wakajikuta wametumbukia kwenye mapenzi mazito kiasi cha kuonewa wivu na wafanyakazi wengine walioitamani sana bahati hiyo.

Ni lini Jacky alianza kutekwa na penzi la Jacob? Hakukumbuka hasa siku, kwani ilitokea tu kama vile mtu apitiwavyo na usingizi, huwa vigumu kuitambua dakika aliyolala kwani usingizi huja kwa namna ya mwizi anayenyemelea.

Jacky alichoweza kukumbuka ni kuwa alianza kumpenda Jacob tangu siku ya kwanza tu aliyomtia machoni, kwani Jacob alikuwa kijana mtanashati kweli kweli, msomi, mkarimu na mcheshi kwa watu wa rika zote. Sifa kubwa aliyokuwa nayo Jacob ni kwamba hakujua kuringa wala kujivunia usomi wala cheo chake.

Ingawa wanasema mtu hakosi kasoro, kasoro kubwa ya Jacob ilikuwa kupenda sana vidosho. Hakupenda kupitwa na vidosho. Ila ukiachana na tabia hiyo ya kupenda vidosho hata wasiomstahili, Jacob alikuwa mpole na mkarimu sana, hata angemwamshwa saa nane za usiku na mfanyakazi mwenziye mwenye shida angeacha usingizi au jambo lolote lenye faida kwake ili amsaidie.

Tabia ya kusaidia watu haikuishia kazini tu, hata pale mtaani kwao alikokuwa akiishi wakati huo, maeneo ya Kijitonyama, watu walimpenda sana, si watoto si wakubwa.

Jacky alijikuta akimuwaza Jacob tu kila wakati na alijikuta akiwa amepata mshirika mpya katika maisha yake, akimuona kijana huyo kila mahali, tangu katika sahani ya chakula, kwenye bilauri ya maji, hadi kitandani.

Kila mara alipokutana na Jacob alijihisi kugwaya na hofu ya chini chini ilimtambaa na kusababisha maungo yake yazizime kwa msisimko ambao ilikuwa vigumu kuuelezea.

Aliwahi kumfumania Jacob mara kadhaa na wasichana wengine lakini hakuwa na uwezo wa kumwacha au kumkabili, kwani kila alipossimama mbele yake alijikuta maungo yake yakigeuka yakaingiwa ganzi, moyo wake uliunguruma sana kama uliopambana na kazi isiyo ya kiasi chake na ulimi wake uligeuka kipande cha chuma! Hakujiweza kabisa kila aliposimama mbele ya Jacob.

Mapenzi yao yalikolea na mara nyingi walitoka pamoja kwa matembezi ya jioni ama katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo au za kijamii. Ilifikia hatua walipeana ahadi ya kwenda kuwaona wazazi na kuoana huku wakiapa kulilinda pendo lao thabiti ambalo waliamini lingeweza kuvumilia raha na shida zote za ulimwengu kama chuma cha pua.

Walikubaliana kujenga pendo ambalo wangehakikisha halipwayi wala kupauka, na ilibaki siku chache tu wavishane pete ya uchumba ambayo ingekuwa mkataba wa milele usioweza kuvunjwa kwa kupwa na kujaa kwa bahari, ndipo lilipotokea la kutokea na kulifanya penzi lao libaki kuwa historia.

Ilikuwa siku ya Ijumaa jioni, Jacky alikwenda nyumbani kwa Jacob bila taarifa na kumkuta Jacob akijivinjari na Diana, tena wakitumia njia mbadala. Japo Jacky aliwahi kumfuma Jacob mara kadhaa na wasichana, lakini kilichomuumiza zaidi ni kumfumania na rafiki yake kipenzi, Diana waliyesoma darasa moja pale Jangwani Secondary School. Ni Jacky ndiye aliyemtambulisha Diana kwa Jacob.

Jacky aliukuta mpambano mkali sana pale sebuleni kati ya Jacob na Diana, walikuwa wamehama kabisa katika ulimwengu huu na kuhamia katika sayari nyingine kabisa yenye raha zisizoelezeka. Vilio na miguno kuashiria raha waliyoipata vikihanikizwa na sauti kubwa ya muziki ndivyo vilivyokuwa vikisika.

Wakati Diana na Jacob wakijivinjari katika sayari ya mahaba, tena kinyume na maumbile, Jacky alikuwa amefika nyumbani kwa Jacob pasipo taarifa, lakini alipokuwa nje alianza kusikia sauti kubwa ya muziki uliokuwa ukisikika kutokea ndani.

Jacky alishangaa sana kwani haikuwa kawaida ya Jacob kufungulia muziki kwa sauti ya juu isipokuwa wakati walipokuwa katika ulimwengu wa mahaba, hivyo alisimama nje ya nyumba akijiuliza kulikuwa na nini mle ndani bila kupata jibu. Alipokosa majibu alishika kitasa cha mlango na kukinyonga, mlango ukasalimu amri na kufunguka ukimruhusu kuingia ndani.

Aliingia ndani na kupiga hatua kwa madaha akikivuka chumba kidogo na kuingia sebuleni. Alichokiona pale sebuleni kilimfanya ahisi kama dunia yote ilikuwa imemkalia kichwani, alitamani ingekuwa ni ndoto lakini haikuwa ndoto bali kilikuwa kitu cha kweli alichokuwa akikiona mbele yake.

Alikuwa amepatwa na mshtuko mkubwa sana na kuhisi miguu yake ilikuwa inaishiwa na nguvu, akawahi kushika ukuta na kujiegemeza ukutani, kwani mwili wote ulikuwa unamtetemeka.

Katika sofa kubwa Diana alikuwa amepiga magoti na kuinama kwa mbele huku akilia kilio ambacho kilikosa kabisa tafsiri, alikuwa akichezeshwa kwata na Jacob aliyekuwa amesimama nyuma yake, na wote wawili walikuwa katika sayari ya mbali ya mahaba mazito yasiyo na staha.

Kwa nukta kadhaa moyo wa Jacky ulisahahu mapigo yake, na yalipoanza tena alivuta pumzi ndefu, akazishusha. Alijikuta akishindwa kusogea hata hatua moja na kubaki kumkodolea macho yule msichana aliyekuwa amepiga magoti kwenye sofa akichezeshwa dombolo ya solo na Jacob.

Itaendelea...
 
Kizungumkuti! - 46

Na Bishop Hiluka

Katika sofa kubwa Diana alikuwa amepiga magoti na kuinama kwa mbele huku akilia kilio ambacho kilikosa kabisa tafsiri, alikuwa akichezeshwa kwata na Jacob aliyekuwa amesimama nyuma yake, na wote wawili walikuwa katika sayari ya mbali ya mahaba mazito yasiyo na staha.

Kwa nukta kadhaa moyo wa Jacky ulisahahu mapigo yake, na yalipoanza tena alivuta pumzi ndefu, akazishusha. Alijikuta akishindwa kusogea hata hatua moja na kubaki kumkodolea macho yule msichana aliyekuwa amepiga magoti kwenye sofa akichezeshwa dombolo ya solo na Jacob.

Endelea...

Jacky alimwangalia kwa makini akijaribu kukumbuka ni wapi alipopata kumwona msichana huyo, kwani alikuwa na hakika sura yake haikuwa ngeni machoni kwake ila hakukumbuka alimwona wapi!

“Jacob!” Jacky alijikuta akiita kwa hasira huku akiendelea kuwakodolea macho. Jacob na Diana waliokuwa wamemezwa na ulimwengu filauni walishtuka na kugeuka kumtazama Jacky, na hapo wakakutana na sura ya Jacky iliyojaa hasira.

Jacky akamuona vizuri yule msichana aliyekuwa anachezeshwa kwasakwasa na kila aina ya mitindo na kumtambua. Mshtuko wa Jacky uliongezeka mara dufu baada ya kumtambua Diana kuwa ndiye aliyekuwa akijivinjari na Jacob, na hapo mwili wake ulianza kumtetemeka zaidi kwa hasira.

Jacob na Diana walipatwa na mshtuko mkubwa sana kumuona Jacky akiwa amesimama mbele yao akiwatazama kwa hasira, hawakutegemea kabisa kumuona pale muda ule.

Oh my God, Diana!” Jacky aling’aka huku akimkodolea macho Diana akiwa haamini macho yake.

What are you doing here, Jackline?” (Unafanya nini hapa, Jackline?) Jacob alimuuliza Jacky kwa ukali huku jasho jingi likimtiririka. Diana alibaki akimkodolea macho Jacky pasipo kusema neno, aliogopa sana kwani alimjua Jacky kuwa mkorofi sana, na kama angeamua kuanzisha timbwili pale basi hakuna mtu ambaye angeweza kumzuia. Angeweza kuwatandika wote kama watoto wadogo kutoka na mafunzo maalumu ya sanaa ya mapigano aliyokuwa ameyapata.

Jacky hakujibu badala yake alibaki kimya akiwatazama kwa makini huku akionekana kupatwa na fadhaa kubwa, aliminya midomo yake huku akishindwa kuendelea kuwatazama na kuinamisha kichwa chake. Kisha msirimbi wa kipaji cha uso wake ukaumuka, milizamu ikatutusika chini ya masikio yake kama iliyopulizwa, na mara kikamtoka kikohozi kikubwa na michirizi ya machozi ikapasuka machoni mwake.

Sidhani kama kuna haja ya kukueleza (msomaji wangu) jinsi ambavyo Jacky alihisi moyoni mwake muda ule, bali waweza kukisia. Huenda yalikukuta kama hayo kwa mtu mmoja huko mtaani kwenu.

Je, ulihisije? Pole sana! Na kama hayajakukuta, mshukuru Mungu wako na umlaaani shetani yasikukute, maana kijasho kitakutoka na utatamani ardhi ipasuke ikumeze mzima mzima. Mambo haya ni mazuri hivi uyasomapo tu lakini yakikukuta ni mateso makubwa moyoni!

Jacky aliishiwa kabisa nguvu, hakutaka kuendelea kusimama pale akiyashuhudia yale mambo machafu ya kifilauni yakifanyika kati ya mpenzi wake Jacob na rafiki yake Diana, hivyo kwa unyonge aligeuka na kutoka nje taratibu, akaufungua mlango na kusubiri teksi yoyote ambayo ingepita.

Haukupita muda mrefu aliiona teksi moja ikija, akaisimamisha na kuingia, kisha akamwelekeza dereva sehemu ya kumpeleka.

Alichokifanya tu mara alipofika nyumbani kwake ni kuingia chumbani na kujilaza kitandani huku akihisi maumivu makali ya kichwa kutokana na kulia sana kwa uchungu. Pale kitandani alimwaza Diana tu, msichana filauni kabisa, aliyeamua bila haya kujivinjari na shemeji yake, mbaya zaidi alikuwa akimlisha Jacob ‘kisamvu cha kopo’.

I’ve found Jacob several times with some girls and I forgave him because I love him, but to find him and the cursed Diana, I’ll never forgive them…” (Nimewahi kumfumania Jacob mara kadhaa na wasichana na nikamsamehe kwa sababu nampenda, ila kumkuta na yule mlaaniwa Diana, siwezi kuwasamehe abadani…) Jacky alijisemea kimoyomoyo alipokuwa kalala pale kitandani.

Jacky hakuishia kumlaani Diana tu bali alianza kumlaumu Jacob kwa kuanzisha uhusiano na Diana hali akijua fika urafiki wao ulivyokuwa, jinsi Jacky alivyozidi kuwaza ndivyo alivyozidi kupandwa na hasira, akataka kutoka amwendee Diana nyumbani kwake akamchambe, na ikiwezekana amtembezee mkong’oto.

Even if I go to her, what will I do? If I’ve failed to do anything when I found her in Jacob's house, what will I do then?” (Hata nikimwendea, nitamfanya nini? Kama nimeshindwa kumfanya chochote nilipomfumania kwa Jacob huko kwake nitafanya nini?) Jacky alijiuliza na kukosa jibu.

From now on I’ll stop Diana, I don't want to see her again, it’s clear that she’s not a good friend of mine. Even Jacob I don’t want to see him, because he doesn’t love me but he’s just using me,” (Kuanzia leo nitamkomesha Diana, sitaki kumuona tena, kanidhihirishia wazi kuwa si rafiki mwema kwangu. Hata huyo Jacob pia sitaki kumuona, kwani hanipendi bali ananitumia tu) Jacky aliendelea kuwaza.

Hata hivyo, swali moja lilikuwa linamtesa Jacky, alijiuliza angewezaje kuepuka asimuone Jacob ilhali walikuwa wakifanya kazi ofisi moja? Alifikiria sana na mwishowe akaamua kuacha kazi kwani asingeweza kuvumilia kumuona Jacob kila siku baada ya kushuhudia kitendo kile alichomfanyia.

Zilipita siku tatu Jacky akishinda nyumbani tu bila kwenda kazini na hata Jacob alipojaribu kumpigia simu alikuwa hapokei na alipoona kero imezidi aliamua kuzima simu. Pia Jacob alikuwa akituma ujumbe wa kuomba msamaha lakini Jacky aliufuta pasipo hata kuusoma.

Hatimaye siku ya tatu aliamua kuandika barua ya kuacha kazi na kumtafuta mfanyakazi mmoja wa ofisini kwao akampa ile barua ili aipeleke kwa bosi wake na yeye kuamua kuelekea Arusha, alibadilisha kabisa namba yake ya simu.

Huko Arusha hakuchelewa akapata kazi katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC), na taratibu akaanza kumsahau Jacob. Baada ya miezi mitano tu tangu kuanza kazi pale AICC ndipo akakutana na Carlos…

______

Simu kutoka kwa Carlos ndiyo iliyomzindua Jacky kutoka kwenye lindi la mawazo. Jacky aliitazama kwa makini simu yake na kuipokea kisha akaiweka sikioni.

Yes darling…” Jacky aliongea kwa mbwembwe mara tu baada ya kuiweka simu sikioni.

Have you seen that information on WhatsApp?” (Umeona hiyo habari kwenye WhatsApp?) sauti ya Carlos iliongea upande wa pili wa simu.

No, what information?” (Hapana, habari gani?) Jacky aliuliza kwa wasiwasi huku akiikodolea macho simu yake kana kwamba alikuwa ameshika bomu lililokuwa lilipuke muda wowote.

About today's theft in the bank…” (Kuhusu wizi wa leo katika benki…) sauti ya Carlos ilipenya kwenye ngoma ya sikio la Jacky na kumfanya ahisi kizunguzungu.

“What?” Jacky alijikuta aking’aka na kukata simu kisha alifungua katika sehemu ya ujumbe wa WhatsApp kuangalia. Hapo akakutana na taarifa iliyokuwa ikisambaa kwa kasi kwenye makundi mbalimbali ya WhatsApp kuhusu wizi wa mabilioni katika Benki ya Biashara:

Taarifa ile ilieleza kwa kifupi kuhusu wizi wa mabilioni ya fedha katika Benki ya Biashara na wafanyakazi kadhaa walikuwa wanashikiliwa na polisi kwa mahojiano. Taarifa ile ilisema Mzungu akiwa na Waswahili wawili waliingia benki na kusomba mabilioni huku ikiambatana na kipande kifupi cha picha ya video kikiwaonesha wanaume watatu ambao sura zao hazikuonekana sawasawa wakitoka benki na kuingia kwenye gari aina ya Ford Transit lenye nembo ya NeoVision Security.

Itaendelea...
 
Kizungumkuti! - 47

Na Bishop Hiluka

“What?” Jacky alijikuta aking’aka na kukata simu kisha alifungua katika sehemu ya ujumbe wa WhatsApp kuangalia. Hapo akakutana na taarifa iliyokuwa ikisambaa kwa kasi kwenye makundi mbalimbali ya WhatsApp kuhusu wizi wa mabilioni katika Benki ya Biashara:

Taarifa ile ilieleza kwa kifupi kuhusu wizi wa mabilioni ya fedha katika Benki ya Biashara na wafanyakazi kadhaa walikuwa wanashikiliwa na polisi kwa mahojiano. Taarifa ile ilisema Mzungu akiwa na Waswahili wawili waliingia benki na kusomba mabilioni huku ikiambatana na kipande kifupi cha picha ya video kikiwaonesha wanaume watatu ambao sura zao hazikuonekana sawasawa wakitoka benki na kuingia kwenye gari aina ya Ford Transit lenye nembo ya NeoVision Security.

Endelea...

Jacky alitweta, alikikodolea macho kile kipande cha picha ya video akiwa hajui afanye nini, mara akaikumbuka kauli ya Jacob aliposema kuwa alikuwa anaelekea kituo cha polisi kumuona rafiki yake alikuwa amekamatwa.

* * * * *

Kwenye chumba maalumu cha mahojiano katika kituo kikuu cha polisi jijini Dar es Salaam, Yusuf alikuwa ameketi kwenye kiti akihojiwa na mbele yake kulikuwa na meza ndefu yenye umbo mstatili.

Nyuma ya ile meza kulikuwa na wanaume wawili shupavu, maofisa wa polisi ambao kati yao mmoja alikuwa amevaa sare maalumu za jeshi la polisi na juu ya mabega yake kulikuwa na alama ya nyota tatu zilizoonesha cheo chake kuwa alikuwa Mrakibu Msaidizi wa Polisi.

Ofisa huyo wa polisi aliitwa Ibrahim Komba, au kwa kifupi ASP Komba, alikuwa bado kijana na umri wake ulikuwa miaka therathini na mbili, japo alikuwa amevaa sare za jeshi la polisi lakini alionekana mtanashati sana.

Alikuwa na urefu wa takriban futi sita, akiwa na umbo kakamavu la kimichezo lililomfanya aonekane kama wachezaji wa ligi ya mpira wa kikapu wa Marekani.

Ofisa wa pili wa polisi alikuwa amevaa nguo za kiraia na alikuwa pembeni ya ASP Komba. Yeye alikuwa na cheo cha “V” tatu na aliitwa Venance Mapambano, maarufu kama Sajenti Mapambano, alikuwa askari wa upelelezi, maarufu kama askari kanzu.

Sajenti Mapambano alikuwa mrefu na mwembamba ila mwenye mwili ulio imara, akionekana kuwa alikuwa amepitia na kuhitimu vizuri mafunzo maalumu ya kijeshi na sanaa ya mapigano.

Wale maofisa wa polisi walikuwa wameketi kwenye viti vyao na macho yao yote yalikuwa yakimtazama Yusuf kwa makini kama yaliyokuwa yakijaribu kusoma mawazo yake. juu ya ile meza kulikuwa na mashine ndogo ya kurekodia sauti.

Yusuf aliyatembeza macho yake taratibu kuwatazama wale maofisa wa polisi kwa zamu kabla ya kuweka kituo kwa ASP Komba ambaye alikuwa ameketi mbele yake wakitazamana.

Hakuwa na shaka yoyote kuwa alikuwa amefikishwa kwenye chumba kile kwa sababu moja muhimu ya mahojiano kuhusiana na sakata la wizi wa shilingi bilioni moja na milioni mia tatu kutoka katika Benki ya Biashara aliyokuwa akifanya kazi.

Tangu alipofikishwa kwenye kile chumba hakuwa ameulizwa chochote hadi muda ule, kitambo kirefu cha ukimya kilipita akiwa ameketi pale, tumbo lilikuwa likimsokota na mapigo ya moyo wake yalikuwa yanakwenda mbio isivyo kawaida.

ASP Komba alimtazama Yusuf kwa makini kisha aliingiza mkono wake kwenye mfuko wa gwanda lake akionekana kutafuta kitu. Alipotoa mkono ulitoka na pakiti ya sigara kisha akatoa sigara moja na kuibana kwenye pembe ya mdomo wake.

Kisha alianza kuhangaika kutafuta kiberiti chake mfukoni ili ajiwashie ile sigara, hata hivyo Sajenti Mapambano akawahi kutoa kiberiti chake kutoka mfukoni na kumuwashia ile sigara kwenye pembe ya mdomo wake.

Pamoja na tukio lile la kuwashiwa sigara na msaidizi wake Sajenti Mapambano lakini hakukuwa na tashwishwi yoyote katika sura ya ASP Komba, badala yake aliivuta sigara yake kwa utulivu mno kuikoleza moto, kisha alipoitoa mdomoni akapuliza moshi wake pembeni huku akiutazama kwa makini kabla ya macho yake kuweka kituo kwenye uso wa Yusuf.

Baada ya mikupuo kama miwili hivi ya moshi wa sigara Ibrahim Komba aliinua mkono wake wa kulia kumuonesha Yusuf hundi aliyokuwa ameishika mkononi, kisha akabonyeza kitufe fulani kilichokuwa juu ya ile mashine ya kurekodia sauti.

“Tuambie, Yusuf, unakiri kwamba wewe ndiye uliyepokea hundi hii iliyoletwa na hao watu watatu unaosema kuwa hujapata kuwaona hata siku moja?” ASP Komba aliuliza kwa sauti tulivu huku akiwa amemkazia macho Yusuf pasipo kupepesa macho yake.

“Ndiyo, afande,” Yusuf alijibu kwa huzuni.

“Uliwezaje kuidhinisha kiasi kikubwa vile cha fedha kitolewe kwa watu unaokiri kuwa hukuwahi kuwaona?” ASP Komba aliuliza tena huku macho yake yakiwa bado yameweka kituo kwenye uso wa Yusuf yakimtazama kwa uyakinifu.

“Lakini sikuidhinisha mimi, afande,” Yusuf aliongea kwa utulivu akijaribu kujitetea.

“Ni nani mwingine aliyeidhinisha?” ASP Komba alimuuliza Yusuf huku akiiweka tena sigara yake kwenye pembe ya mdomo wake na kupiga mkupuo mmoja wa moshi wa sigara.

“Meneja wa tawi, hata ukiangalia utaiona saini yake iko hapo hapo.”

ASP Komba aliinamisha macho yake akaitazama ile hundi kwa umakini sana, kikapita kitambo kifupi cha ukimya kisha akainua tena uso wake na kumkazia macho Yusuf.

“Wewe na meneja wako wa tawi ni nani aliyeanza kuweka saini katika hundi hii?” ASP Komba akauliza swali jingine kwa sauti tulivu lakini iliyokuwa ikiyatetemesha maini ya Yusuf.

“Ni mimi, afande…” Yusuf alijibu huku akionesha wasiwasi mkubwa.

“Kwa nini asianze meneja wako wa tawi na badala yake ukaanza wewe?”

“Yeye mara nyingi anakuwa na shughuli nyingi huko ndani, hivyo masuala ya wateja huwa anatutegemea zaidi sisi.”

“Ndiyo kusema kama wewe usingeisaini hii hundi, yeye pia asingesaini, kweli si kweli?” ASP Komba alikuwa makini zaidi kumtazama Yusuf wakati alipokuwa akimuuliza Yusuf maswali.

Yusuf alifungua mdomo wake kutaka kujibu lakini sauti yake haikutoka, akabaki kimya akimtumbulia macho yule ofisa wa polisi kwa hofu. Kitambo kifupi cha ukimya kikapita mle ndani huku wote wakitazamana kwa makini bila kusema neno, kisha ASP Komba baada ya kukung’uta majivu ya sigara pembeni aliongea huku hasira ikionekana kuchipua taratibu machoni mwake.

“Unajua, uongo ni suluhisho la muda mfupi sana katika kutatua tatizo la kudumu… sipendi kutumia nguvu ili kukufanya uzungumze, lakini ukinilazimisha ninaweza kutumia nguvu kwani huwa siwavumilii kabisa watu waongo…” ASP Komba alisema kwa sauti tulivu huku tabasamu la kinyama likichanua usoni kwake.

Yusuf alionekana kushikwa na wasiwasi na kuinamisha kichwa chake chini huku donge la fadhaa likimkaba kooni na kumfanya ashindwe kupumua vizuri.

“Nakuuliza tena, kama wewe usingeisaini hii hundi, meneja wako wa tawi pia asingesaini, kweli si kweli?” ASP Komba aliuliza kwa sauti ya juu kidogo iliyoonesha ukali.

“Kweli!” hatimaye Yusuf alijibu na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.

ASP Komba alibetua kichwa chake huku akipiga mkupuo mkubwa wa moshi wa sigara, alitulia kidogo akionekana kutafakari kisha akapuliza moshi mwingi pembeni.

“Una mke?” ASP Komba alimuuliza Yusuf huku akiwa amemtulizia macho yake usoni.

“Ndiyo, na mtoto mmoja,” Yusuf alijibu kwa utulivu na unyonge huku akimtazama yule ofisa wa polisi kwa huzuni.

“Utaipa shida familia yako,” ASP Komba alisema huku akimkazia macho Yusuf kwa umakini zaidi kisha akatingisha kichwa chake kumsikitikia.

Itaendelea...
 
Kizungumkuti! - 48

Na Bishop Hiluka

ASP Komba alibetua kichwa chake huku akipiga mkupuo mkubwa wa moshi wa sigara, alitulia kidogo akionekana kutafakari kisha akapuliza moshi mwingi pembeni.

“Una mke?” ASP Komba alimuuliza Yusuf huku akiwa amemtulizia macho yake usoni.

“Ndiyo, na mtoto mmoja,” Yusuf alijibu kwa utulivu na unyonge huku akimtazama yule ofisa wa polisi kwa huzuni.

“Utaipa shida familia yako,” ASP Komba alisema huku akimkazia macho Yusuf kwa umakini zaidi kisha akatingisha kichwa chake kumsikitikia.

Endelea...

“Lakini mimi sihusiki kabisa, afande, wala sijui lolote,” Yusuf alizidi kujitetea huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani. Wakati huo machozi yalianza kumlengalenga kwenye macho yake.

“Sijasema kuwa wewe unahusika au unajua lolote, lakini nina kila sababu ya kuamini kwamba unaweza kuisaidia polisi katika wizi huu, kwani wewe ndiye uliyewaona vizuri hao wahalifu,” ASP Komba alisema huku akiminya midomo yake.

“Afande, naomba uniamini, mimi siwafahamu kabisa…”

ASP Komba aliizima ile mashine ya kurekodia sauti huku akitingisha kichwa chake kwa huzuni, aliendelea kuminya midomo yake na baada ya sekunde chache aliruhusu tabasamu la kifedhuli kuchanua usoni kwake, kisha aligeuza shingo yake kumtazama Inspekta Mapambano na kuonesha ishara fulani ya kichwa.

Sajenti Mapambano alisimama kwa ukakamavu na kuzunguka ile meza akimsogelea Yusuf, kisha alimshika na kumnyanyua kwa nguvu kama vile alikuwa akinyanyua kipeto cha sufi.

“Kabla hujamweka korokoroni, hakikisha unaorodhesha vitu vyake vyote,” ASP Komba alimwambia Sajenti Mapambano huku akiuma mdomo wake wa chini.

Kusikia hivyo, Yusuf aliishiwa kabisa nguvu akionekana kupatwa na mshtuko mkubwa, muda ule ule aliingiza mkono wake mfukoni na kutoa simu yake aina ya Tekno Spark K9.

“Afande, naomba nimpe jamaa yangu yupo hapo nje hii simu ili aondoke nayo,” Yusuf alisihi kwa sauti ya kubembeleza huku akimtazama ASP Komba kwa wasiwasi.

ASP Komba alimtazama Yusuf huku tabasamu la kifedhuli likizidi kuchanua usoni kwake, kisha aliangua akicheko hafifu. “Kwa hiyo sisi hutuamini, siyo?” ASP Komba alimuuliza Yusuf huku akiendelea kucheka.

“Nawaamini, afande, lakini…”

“Kama unatuamini iache hapa hapa, kwanza hatukuruhusu utoke tena nje,” ASP Komba alisema huku akikunja sura yake iliyotengeneza ndita.

Yusuf alionekana kunywea na kuishiwa kabisa nguvu, baridi nyepesi ya mshtuko wa hofu ikasambaa mwilini mwake na nywele zake zilimsimama kichwani huku koo lake likimkauka.

Sajenti Mapambano alimshika Yusuf kwa nguvu na kumuongoza akimtoa nje ya kile chumba cha mahojiano. Wakatoka wakimwacha ASP Komba akiwa bado ameketi katika kile chumba peke yake huku akitafakari kwa kina.

Kisha ASP Komba na Sajenti Mapambano waliwahoji watu wengine wanne wakiwemo wale askari wawili wa ulinzi waliokuwa zamu siku ile pale benki na wafanyakazi wawili walioshuhudia kwa ukaribu wakati wale watu watatu wakiingia mle Benki ya Biashara na kutoka.

Wakati akiwahoji baadhi ya wafanyakazi na wale askari wa ulinzi, ASP Komba alishindwa kuwahoji akiwa ameketi kitini pake, hivyo akawa anarandaranda mle chumbani.

“Nataka mkumbuke vizuri…” ASP Komba aliwaambia huku akiwakazia macho.

“Ninyi wawili, isipokuwa askari wa ulinzi, mlikuwamo mle benki wakati hawa jamaa watatu wanasimama pale kaunta na kumkabidhi Yusuf hundi kabla hawajatoka na fedha. Pamoja na kuwa kulikuwa na wateja wengi nanyi mlikuwa mkishughulika na wateja wengine, lakini mnaweza kukumbuka vitu viwili vitatu juu ya watu hawa, sura zao, kwa mfano, urefu wao, sauti zao… na vitu kama hivyo,” ASP Komba alinyamaza kidogo, akawatazama mmoja mmoja.

Kisha akaendelea, “Hebu wewe Pauline, umesema ulikuwa karibu zaidi, nieleze unavyoweza kuwakumbuka,” alimuuliza mfanyakazi mmoja wa kike ambaye wakati kina Kisu wanaingia benki alikuwa amesimama kaunta ya jirani na alipokuwepo Yusuf.

Pauline alitoa kikohozi cha chini chini, akaketi vema, “Wote watatu walikuwa wamevaa miwani myeusi iliyoonesha kuficha macho yao, walikuwa wakakamavu na yule mmoja wao aliyekuwa anaburuza begi la magurudumu ndiye alisimama karibu sana na dirisha langu.”

“Kwa hiyo ulimchunguza vizuri?”

“Alikuwa jasiri sana, afande, isitoshe sikujua kama hawakuwa raia wema,” Pauline alisema.

“Nimekuelewa, nimekuelewa,” ASP Komba alimkatiza. “Hebu jaribuni kukumbuka vitu vingine juu ya hawa watatu… kama kumbukumbu zenu ni nzuri.”

Kijana mmoja aliyeitwa Elibariki alijiinamia kwa dakika nzima bila kusema lolote. Alipoinua uso wake alionekana kukumbuka kitu. “Kuna yule mzungu, nahisi kama hakuwa mzungu ila ni mweupe tu, na hata zile nywele zake zilizokuwa zimelalia mgongoni nadhani zilikuwa nywele za bandia…”

ASP Komba alimtazama Elibariki kwa kitambo kirefu bila kukupesa macho. “Una uhakika?” hatimaye alimuuliza ili kujiridhisha.

“Ndiyo afande, nina uhakika hakuwa mzungu na inawezekana alikuwa na upara, ni kama nimewahi kumuona sehemu fulani hivi,” Elibariki alijibu bila hata kufikiria.

Baada ya mahojiano yaliyochukua takriban dakika ishirini ASP aliwaruhusu kuondoka lakini akawataka kufika kituoni kila watakapohitajika. Waliondoka na kumwacha akifikiria sana kuhusu yale maelezo. Kisha aliishika ile simu ya Yusuf na kuitazama kwa makini huku akiigeuza geuza katika namna ya kuichunguza kwa makini.

Kisha aliiwasha na kuanza kuzipitia namba za simu zilizopigwa na majina yaliyokuwa yameorodheshwa kwenye ile simu. Wakati akiyapitia yale majina, baadhi ya majina alionekana kuyatilia shaka na hivyo alikuwa akiyaandika pembeni kwenye notebook yake.

Alichukua muda mrefu akizichunguza zile namba kwenye ile simu, na wakati akiendelea na uchunguzi ule mara mlango wa kile chumba cha mahojiano ukagongwa na kumfanya ageuke kuutazama kule mlangoni.

Muda ule ule mlango ukafunguliwa na hapo akaingia Sajenti Mapambano akiwa ameongozana na Nassos Chatzopoulos. ASP Komba alimtazama Nassos kwa makini na kumuonesha sehemu ya kuketi. Kwa mkono

Nassos aliketi kimya akiwa na wasiwasi kidogo huku akimtazama ASP Komba kwa umakini zaidi. ASP Komba aliendelea kuzipitia zile namba za simu kwenye ile simu ya Yusuf na baadaye alifungua sehemu ya ujumbe mfupi na kuanza kusoma ujumbe uliokuwa umetumwa katika ile simu.

Alisoma ujumbe kwa umakini huku akizinakiri baadhi ya namba za simu zilizokuwa zimetumika kutuma ule ujumbe na kuandika taarifa fulani kwenye kitabu chake kidogo na alipomaliza kuandika aliinua uso wake kumtazama Nassos huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.

You’re welcome,” (Karibu sana) ASP Komba alimkaribisha Nassos kana kwamba ndiyo alikuwa amemuona kwa mara ya kwanza.

Thank you, officer,” (Ahsante, afande) Nassos alijibu huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.

Do you know Swahili?” (Unajua Kiswahili?) ASP Komba alimuuliza huku akimtulizia macho.

Yes, but a little, officer,” (Ndiyo, lakini kidogo, afande) Nassos alijibu kwa kujiamini.

Are you the chief executive director of The Jacarandah Group, right?” (Wewe ndiye mkurugenzi mtendaji wa The Jacarandah Group, sawa?) ASP Komba alimuuliza Nassos huku akiwa amemtulizia macho yake usoni pasipo kupepesa.

Yes, officer,” (Ndiyo, afande) Nassos alisema huku akilamba midomo yake iliyoanza kukauka.

Itaendelea...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom