Bishop Hiluka
R I P
- Aug 12, 2011
- 7,150
- 14,725
- Thread starter
- #261
Kizungumkuti! - 42
Na Bishop Hiluka
ILIPOISHIA
Carlos na kampani yake walikuwa kimya pale sebuleni wakinywa na kutafakari, na juu ya meza ndogo zilizokuwa mbele yao kulikuwa na mizinga mitatu mikubwa ya mvinyo na bilauri kadhaa. Hii ilikuwa ni kama sherehe ndogo baada kwa kufanikiwa kufikisha mzigo salama licha ya hekaheka za kupita huku na kule, barabara hizi na zile katika safari ya mzunguko ambao ingekuwa vigumu sana mtu yeyote kuelewa walielekea wapi endapo angejaribu kuwafuatilia.
Kwa kifupi ni kwamba, baada ya kutoka pale Benki ya Biashara tawi la barabara ya Lumumba gari lao aina ya Ford Transit lenye nembo ya NeoVision Security liliifuata barabara ya Bibi Titi Mohammed na kwenda moja kwa moja hadi makutano ya barabra ile na barabara ya mtaa wa Nkrumah.
Hapo Carlos aliongeza kasi ya mwendo wa gari huku akipiga king’ora kuyataka magari mengine yakae kando huku akikatisha katikati ya majengo ya ghorofa ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), yaliyokuwa katika pande zote mbili za barabara ile ya Nkrumah.
Endelea...
Alipoivuka reli katika eneo la Goldstar alikunja na kuingia kushoto akiifuata barabara ya mtaa wa Lugoda, wakapita katikati ya majengo makubwa yalikuwa na ofisi mbalimbali na kwenda kutokea katika barabara ya mtaa wa Gerezani iliyokuwa ikitokea Posta, na hapo akakunja na kuingia upande wa kulia akiifuata barabara ile ya Gerezani.
Aliendelea kupiga king’ora kuyataka magari mengine yakae kando huku akiyapita kwa mwendo wa kasi na kuufika mzunguko wa barabara za Gerezani iliyotokea Kariakoo kwenda Posta na ile ya Bandari iliyoelekea Kurasini. Aliifuata barabara ya Bandari na mwendo wake haukuwa wa kubahatisha hata kidogo.
Akalivuka daraja ambalo chini yake kulikuwa na njia za treni kuelekea bandarini, hakupunguza mwendo hadi alipofika katika mzunguko ulioziunganisha barabara za Bandari, Kilwa na Mandela. Na hapo akazunguka na kuifuata barabara ya Kilwa.
Alizidi kusonga mbele zaidi hadi alipoivuka baa maarufu ya Pentagon mbele kidogo akaachana na barabara ya Kilwa na kuingia katika mtaa mmoja kushoto kwake, kisha akaivuka Meshack Automotive Solutions halafu akakata tena kushoto akiingia ndani zaidi katika eneo la Mivinjeni, kisha alikwenda kuliegesha gari lake chini ya kivuli cha miti mikubwa katika eneo lile la Mivinjeni.
Kwa muda ule eneo lile halikuwa na pilika pilika zozote, hivyo kitendo bila kuchelewa, wote walishuka haraka kutoka kwenye lile gari huku Kabwe akilishusha lile begi lenye fedha kisha wakaingia kwenye gari jingine la kifahari aina ya Toyota Alphard jeupe lililokuwa likiwasubiri pale.
Ndani ya lile gari aina ya Toyota Alphard kulikuwa na mtu mmoja tu, dereva ambaye ni Jacky, aliyekuwa ameketi nyuma ya usukani kwa utulivu.
Muda ule ule Liston alitumia utaalamu wake wa hali ya juu wa uhandishi wa umeme, kukorofisha mfumo wa umeme wa lile gari aina ya Ford Transit, na hapo gari likashika moto.
Kisha aliingia haraka kwenye lile Toyota Alphard lililoanza kuondoka taratibu, alipoingia tu likaondoka kwa mwendo wa kasi kutoka eneo lile kabla hata watu hawajang’amua nini kilichokuwa kikiendelea pale. Kitendo kile kilifanyika ndani ya muda mfupi sana sawa kitendo cha kufumba jicho na kufumbua.
Jacky alikuwa makini sana na kazi yake na alikuwa amevaa soksi maalumu za mikononi (gloves). Wakati wanatokomea mtaani waliliacha lile gari aina ya Ford Transit likiteketea kwa moto na hivyo kuvuta makundi ya watu kushuhudia na wengine wakijaribu kuuzima ule moto, na hivyo hakuna aliyeweza kuwafuatilia.
Kutoka pale walielekea moja kwa moja Mtoni Kijichi na kufika kwenye lile jumba, Carlos akabonyeza remote maalumu ya kufungua geti kubwa jeusi mbele ya lile jumba na mara lile geti likaanza kufunguka, walipoingia ndani lile geti likajifunga.
Jacky alikwenda moja kwa moja kwenye chumba maalumu kilichokuwa kinatumika kama ofisi maalumu na maktaba ya siri kilichofanana na kile kilichojengwa kwenye ile nyumba ya Segerea, alikuwa anaburuza lile begi lenye magurudumu lililojaa fedha.
Chumba hiki kilikuwa na ulinzi wa uhakika na ili kuingia mle ndani ilikuwa ni lazima ubofye namba fulani za siri zilizokuwa kwenye kisanduku kidogo chenye namba pembeni ya mlango.
Jacky alipoufikia mlango wa chumba kile, ambao juu yake kulikuwa na taa nyekundu ikiwaka alibonyeza namba nne za siri kwenye kile kisanduku kilichokuwa pembeni ya mlango kisha akaweka dole gumba la mkono wake wa kulia katika sehemu maalumu iliyokuwa ikiwaka taa ya kijani.
“Thank you, Jackline, you’re welcome…” sauti maalumu kwenye spika ndogo pembeni ya mlango ikasikika ikimkaribisha Jacky huku ikiambatana na maandishi “Welcome Jackline” na mara mlango ule ukafunguka.
Jacky aliliingiza lile begi na kulihifadhi kwenye kabati maalumu na kutoka kwenda kujiunga na watu wengine waliokuwa wameketi sebuleni wakijipongeza kwa mvinyo. Kabwe alinyanyua bilauri yake na kugida pombe yote iliyokuwemo kwa mkupuo mmoja, kisha aliikita ile bilauri mezani huku akisisimkwa mwili, alionekana kuwa mwenye haraka ya jambo fulani.
“Kwa hiyo, kamanda, inakuwaje sasa?” Kabwe alimuuliza Carlos huku akimkazia macho.
“Kuhusu nini?” Carlos alimuuliza Kabwe kwa mshangao huku akimtazama kwa makini.
“Kuhusu pesa, baba’ke… tupe chetu tusepe kwani tunasubiri nini hapa?” Kabwe alijibu huku akifinya macho yake kutokana na ulevi ulioanza kumwingia.
“Naomba tusifanye papara ya kugawana fedha, tusubiri kwanza kwa siku mbili tuone hali itakuwaje,” Carlos aliongea kwa sauti ya utulivu huku akiwatazama watu wote na kuupeleka mche wake wa sigara mdomoni.
Kabwe alikunja sura yake na kutingisha kichwa kwa nguvu akionesha kukataa na wakati huo huo hasira zilikwisha anza kumpanda.
“Aah, hiyo sasa noma, kamanda…” Kabwe alisema na kugeuka kuwatazama Kisu na Liston, “Au siyo wanangu! Eti tusubiri siku mbili, huu si ndiyo mwanzo wa kuingizwa cha kike! Siku mbili tusubiri nini, pingu?”
“Hatusubiri pingu, wala hakuna mtu yeyote mwenye kutaka kuwaingiza cha kike, kwanza siku mbili wala siyo nyingi, na kama mambo yatakuwa shwari tukutane kule kwenye nyumba ya Segerea ili kila mtu achukue chake. Kwani tatizo liko wapi?” Carlos alisema kwa sauti tulivu huku akiwatazama mmoja baada ya mwingine.
Kabwe alizidi kutingisha kichwa chake kukataa, aliwatazama Kisu na Liston kwa kitambo, kisha akamgeukia tena Carlos.
“Unajua mkubwa, hii shughuli haikuwa mchezo, na wewe unajua hilo,” Kabwe aliongea kwa hamaki huku akiwa amekunja sura yake iliyotengeneza ndita usoni.
“Najua sana, ndiyo maana nilihitaji kupata watu wa aina yenu ili kuifanya,” Carlos alisema kwa sauti tulivu akionesha kukubaliana na maneno ya Kabwe.
“Sasa kama unajua hivyo, ni lazima ujue vile vile kwamba tumejitolea roho zetu ili tutengeneze fedha itusaidie kwenye maisha yetu, au siyo, kamanda?”
“Sawa sawa!”
“Sasa fedha yenyewe si ndo hii tuliyoipata? We tukatie chetu tuondoke ili kila mtu ajue ustaarabu wake, kwani kero iko wapi?” Kabwe alizidi kusisitiza apewe mgawo wake huku akionekana kukosa uvumilivu.
Hata hivyo, muda wote wakati Kabwe akiongea, Kisu alikuwa akitabasamu tu bila kusema chochote na Liston alikuwa kimya kabisa akisikiliza kwa makini jinsi ambavyo Carlos na Kabwe walivyokuwa wakilumbana, ingawa wote kila mmoja alikuwa na yake rohoni.
“Tatizo lako Kabwe hunifahamu vizuri, mbona hushangai Kisu na Liston hawana presha? Sina kawaida ya kumdhulumu mtu, nimeshafanya nao kazi kibao za fedha nyingi kuliko hata hii na nikawapa chao bila usumbufu,” Carlos alisema na kushusha pumzi za ndani kwa ndani huku akijaribu kuidhibiti hasira.
“Kabwe, Listoni na Kisu ni watu watatu tofauti na kila mmoja ana changamoto zake, huenda wao wameshiba lakini mimi nina njaa. Ninahitaji fedha ili kutatua matatizo yangu na kama sijakosea tulikubaliana kulipana mara baada ya kazi, na kazi yenyewe ndo hii imeshafanyika kwa ufanisi mkubwa, sijui haya mengine ya kusubiri siku mbili yanatoka wapi, mkubwa!” Kabwe alisema huku akirusha mikono yake juu kwa hasira.
Itaendelea...
Na Bishop Hiluka
ILIPOISHIA
Carlos na kampani yake walikuwa kimya pale sebuleni wakinywa na kutafakari, na juu ya meza ndogo zilizokuwa mbele yao kulikuwa na mizinga mitatu mikubwa ya mvinyo na bilauri kadhaa. Hii ilikuwa ni kama sherehe ndogo baada kwa kufanikiwa kufikisha mzigo salama licha ya hekaheka za kupita huku na kule, barabara hizi na zile katika safari ya mzunguko ambao ingekuwa vigumu sana mtu yeyote kuelewa walielekea wapi endapo angejaribu kuwafuatilia.
Kwa kifupi ni kwamba, baada ya kutoka pale Benki ya Biashara tawi la barabara ya Lumumba gari lao aina ya Ford Transit lenye nembo ya NeoVision Security liliifuata barabara ya Bibi Titi Mohammed na kwenda moja kwa moja hadi makutano ya barabra ile na barabara ya mtaa wa Nkrumah.
Hapo Carlos aliongeza kasi ya mwendo wa gari huku akipiga king’ora kuyataka magari mengine yakae kando huku akikatisha katikati ya majengo ya ghorofa ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), yaliyokuwa katika pande zote mbili za barabara ile ya Nkrumah.
Endelea...
Alipoivuka reli katika eneo la Goldstar alikunja na kuingia kushoto akiifuata barabara ya mtaa wa Lugoda, wakapita katikati ya majengo makubwa yalikuwa na ofisi mbalimbali na kwenda kutokea katika barabara ya mtaa wa Gerezani iliyokuwa ikitokea Posta, na hapo akakunja na kuingia upande wa kulia akiifuata barabara ile ya Gerezani.
Aliendelea kupiga king’ora kuyataka magari mengine yakae kando huku akiyapita kwa mwendo wa kasi na kuufika mzunguko wa barabara za Gerezani iliyotokea Kariakoo kwenda Posta na ile ya Bandari iliyoelekea Kurasini. Aliifuata barabara ya Bandari na mwendo wake haukuwa wa kubahatisha hata kidogo.
Akalivuka daraja ambalo chini yake kulikuwa na njia za treni kuelekea bandarini, hakupunguza mwendo hadi alipofika katika mzunguko ulioziunganisha barabara za Bandari, Kilwa na Mandela. Na hapo akazunguka na kuifuata barabara ya Kilwa.
Alizidi kusonga mbele zaidi hadi alipoivuka baa maarufu ya Pentagon mbele kidogo akaachana na barabara ya Kilwa na kuingia katika mtaa mmoja kushoto kwake, kisha akaivuka Meshack Automotive Solutions halafu akakata tena kushoto akiingia ndani zaidi katika eneo la Mivinjeni, kisha alikwenda kuliegesha gari lake chini ya kivuli cha miti mikubwa katika eneo lile la Mivinjeni.
Kwa muda ule eneo lile halikuwa na pilika pilika zozote, hivyo kitendo bila kuchelewa, wote walishuka haraka kutoka kwenye lile gari huku Kabwe akilishusha lile begi lenye fedha kisha wakaingia kwenye gari jingine la kifahari aina ya Toyota Alphard jeupe lililokuwa likiwasubiri pale.
Ndani ya lile gari aina ya Toyota Alphard kulikuwa na mtu mmoja tu, dereva ambaye ni Jacky, aliyekuwa ameketi nyuma ya usukani kwa utulivu.
Muda ule ule Liston alitumia utaalamu wake wa hali ya juu wa uhandishi wa umeme, kukorofisha mfumo wa umeme wa lile gari aina ya Ford Transit, na hapo gari likashika moto.
Kisha aliingia haraka kwenye lile Toyota Alphard lililoanza kuondoka taratibu, alipoingia tu likaondoka kwa mwendo wa kasi kutoka eneo lile kabla hata watu hawajang’amua nini kilichokuwa kikiendelea pale. Kitendo kile kilifanyika ndani ya muda mfupi sana sawa kitendo cha kufumba jicho na kufumbua.
Jacky alikuwa makini sana na kazi yake na alikuwa amevaa soksi maalumu za mikononi (gloves). Wakati wanatokomea mtaani waliliacha lile gari aina ya Ford Transit likiteketea kwa moto na hivyo kuvuta makundi ya watu kushuhudia na wengine wakijaribu kuuzima ule moto, na hivyo hakuna aliyeweza kuwafuatilia.
Kutoka pale walielekea moja kwa moja Mtoni Kijichi na kufika kwenye lile jumba, Carlos akabonyeza remote maalumu ya kufungua geti kubwa jeusi mbele ya lile jumba na mara lile geti likaanza kufunguka, walipoingia ndani lile geti likajifunga.
Jacky alikwenda moja kwa moja kwenye chumba maalumu kilichokuwa kinatumika kama ofisi maalumu na maktaba ya siri kilichofanana na kile kilichojengwa kwenye ile nyumba ya Segerea, alikuwa anaburuza lile begi lenye magurudumu lililojaa fedha.
Chumba hiki kilikuwa na ulinzi wa uhakika na ili kuingia mle ndani ilikuwa ni lazima ubofye namba fulani za siri zilizokuwa kwenye kisanduku kidogo chenye namba pembeni ya mlango.
Jacky alipoufikia mlango wa chumba kile, ambao juu yake kulikuwa na taa nyekundu ikiwaka alibonyeza namba nne za siri kwenye kile kisanduku kilichokuwa pembeni ya mlango kisha akaweka dole gumba la mkono wake wa kulia katika sehemu maalumu iliyokuwa ikiwaka taa ya kijani.
“Thank you, Jackline, you’re welcome…” sauti maalumu kwenye spika ndogo pembeni ya mlango ikasikika ikimkaribisha Jacky huku ikiambatana na maandishi “Welcome Jackline” na mara mlango ule ukafunguka.
Jacky aliliingiza lile begi na kulihifadhi kwenye kabati maalumu na kutoka kwenda kujiunga na watu wengine waliokuwa wameketi sebuleni wakijipongeza kwa mvinyo. Kabwe alinyanyua bilauri yake na kugida pombe yote iliyokuwemo kwa mkupuo mmoja, kisha aliikita ile bilauri mezani huku akisisimkwa mwili, alionekana kuwa mwenye haraka ya jambo fulani.
“Kwa hiyo, kamanda, inakuwaje sasa?” Kabwe alimuuliza Carlos huku akimkazia macho.
“Kuhusu nini?” Carlos alimuuliza Kabwe kwa mshangao huku akimtazama kwa makini.
“Kuhusu pesa, baba’ke… tupe chetu tusepe kwani tunasubiri nini hapa?” Kabwe alijibu huku akifinya macho yake kutokana na ulevi ulioanza kumwingia.
“Naomba tusifanye papara ya kugawana fedha, tusubiri kwanza kwa siku mbili tuone hali itakuwaje,” Carlos aliongea kwa sauti ya utulivu huku akiwatazama watu wote na kuupeleka mche wake wa sigara mdomoni.
Kabwe alikunja sura yake na kutingisha kichwa kwa nguvu akionesha kukataa na wakati huo huo hasira zilikwisha anza kumpanda.
“Aah, hiyo sasa noma, kamanda…” Kabwe alisema na kugeuka kuwatazama Kisu na Liston, “Au siyo wanangu! Eti tusubiri siku mbili, huu si ndiyo mwanzo wa kuingizwa cha kike! Siku mbili tusubiri nini, pingu?”
“Hatusubiri pingu, wala hakuna mtu yeyote mwenye kutaka kuwaingiza cha kike, kwanza siku mbili wala siyo nyingi, na kama mambo yatakuwa shwari tukutane kule kwenye nyumba ya Segerea ili kila mtu achukue chake. Kwani tatizo liko wapi?” Carlos alisema kwa sauti tulivu huku akiwatazama mmoja baada ya mwingine.
Kabwe alizidi kutingisha kichwa chake kukataa, aliwatazama Kisu na Liston kwa kitambo, kisha akamgeukia tena Carlos.
“Unajua mkubwa, hii shughuli haikuwa mchezo, na wewe unajua hilo,” Kabwe aliongea kwa hamaki huku akiwa amekunja sura yake iliyotengeneza ndita usoni.
“Najua sana, ndiyo maana nilihitaji kupata watu wa aina yenu ili kuifanya,” Carlos alisema kwa sauti tulivu akionesha kukubaliana na maneno ya Kabwe.
“Sasa kama unajua hivyo, ni lazima ujue vile vile kwamba tumejitolea roho zetu ili tutengeneze fedha itusaidie kwenye maisha yetu, au siyo, kamanda?”
“Sawa sawa!”
“Sasa fedha yenyewe si ndo hii tuliyoipata? We tukatie chetu tuondoke ili kila mtu ajue ustaarabu wake, kwani kero iko wapi?” Kabwe alizidi kusisitiza apewe mgawo wake huku akionekana kukosa uvumilivu.
Hata hivyo, muda wote wakati Kabwe akiongea, Kisu alikuwa akitabasamu tu bila kusema chochote na Liston alikuwa kimya kabisa akisikiliza kwa makini jinsi ambavyo Carlos na Kabwe walivyokuwa wakilumbana, ingawa wote kila mmoja alikuwa na yake rohoni.
“Tatizo lako Kabwe hunifahamu vizuri, mbona hushangai Kisu na Liston hawana presha? Sina kawaida ya kumdhulumu mtu, nimeshafanya nao kazi kibao za fedha nyingi kuliko hata hii na nikawapa chao bila usumbufu,” Carlos alisema na kushusha pumzi za ndani kwa ndani huku akijaribu kuidhibiti hasira.
“Kabwe, Listoni na Kisu ni watu watatu tofauti na kila mmoja ana changamoto zake, huenda wao wameshiba lakini mimi nina njaa. Ninahitaji fedha ili kutatua matatizo yangu na kama sijakosea tulikubaliana kulipana mara baada ya kazi, na kazi yenyewe ndo hii imeshafanyika kwa ufanisi mkubwa, sijui haya mengine ya kusubiri siku mbili yanatoka wapi, mkubwa!” Kabwe alisema huku akirusha mikono yake juu kwa hasira.
Itaendelea...