Star times na usumbufu/utapeli wao

terabojo

JF-Expert Member
Aug 3, 2010
215
45
Wana jf mtakuwa ama mumeona au hata kununua vingamuzi (decoder) na antena za kampuni ya star times ambayo ni mshiriki wa tbc katika mambo ya tv. Jirani yangu alinunua decoder hiyo kwa shs. 79,000.= na akaelekezwa namna ya kufunga na kuanza kutumia/kupata picha. Kifupi ilimchukua siku 9 (baada ya kutemebelea duka lao mara 4 pale msimbazi road karibu na polisi station) ndipo alipoanza kuona picha. Kifupi wale pale wanakuuzia na nadhani hawapeleki taarifa huko tbc mwenge ambako naambiwa ndo hasa wana "activate" decoder ile. Swali: Kwa nini wanakuwa wazembe kiasi hicho. Kwa nini wanamuibia mteja kwa kutomuwezesha kuona tv kwa siku 9? Kibaya zaidi ukipiga nmaba za customer care hakuna hata moja inayopokelewa na unapojaribu kuongeza airtime pia simu zao hazifanyi kazi. Jamani wachina na tbc ya mheshimiwa sana wa wizara ya habari...
 
hawa jamaa namimi nimesumbuana nao sana, customer care ni zero.
ukiwa na tatizo ni vizuri uende pale kwao makao makuu uwakabe makoo hapohapo ndiyo utafanikiwa, rasivyo kupiga simu unapoteza muda
 
Mwanzoni walianza vibaya, lakini TBC wametambua tatizo hilo, wamefanya mabadiliko. Asilimia 90 ya wale customer care wakorofi wameondolewa. Hali ni shwari sasa. Mimi ni mteja wa StarTimes, ila kuna tatizo moja ambalo nataka kulifuatilia... kwenye hizo channels zao wanaweka lile tangazo lao MARA MBILI, tena kati kati ya kipindi! Wanaboa! Lakini kimsingi, content zao ni nzuri. Jaribuni sana kuangalia Discovery World, mtajifunza mambo mengi mazuri!
 
Kwa ambao wameshatumia hii huduma ya startimes kwa muda sasa,
naomba msaada wenu.
je kuna channels ngapi na ni zipi?
ubora wake ukoje, maana nilisikia kuwa kuna kipindi matangazo yalikuwa yanakatika katika sana.
na hii kampuni mpya ya TING wanapatikana katika mkoa wa Mwanza?
 
Wakuu Star time ni nzuri sana bado sijaona tatizo mpaka sasa zipo channel nzuri eg MGM,E channel,BBC,Aljazeera,Kuna channel za Kenya,kuna channel ya wanyama nadhani ni kifaransa pia kuna channel ya Kiindi na nk.

Wapenzi wa mpira Startime wamefulia hakuna kitu kabisa sijui mbele ya safari wataifanyia kazi !.
 
Habari zenu wana jamvi!!

Unaweza kupata ITV,EATV,EMMANUEL TV NK. kupitia StarTimes ila Channel za TBC1 and TBC2 na other 10Channels zitatoka ila waweza kuzirudishia na zile package zijazo na ITV kuwa overwritten.Nilifurahia sana hilo kupitia StarTimes,yeyote aweza kufanya bila msaada wa StarTimes Technical personel.
 
Habari zenu wana jamvi!!

Unaweza kupata ITV,EATV,EMMANUEL TV NK. kupitia StarTimes ila Channel za TBC1 and TBC2 na other 10Channels zitatoka ila waweza kuzirudishia na zile package zijazo na ITV kuwa overwritten.Nilifurahia sana hilo kupitia StarTimes,yeyote aweza kufanya bila msaada wa StarTimes Technical personel.
Kumbe inawezekana..........lakini huu si utakuwa ni wizi.
 
Mbona kwenye usumbufu haujasema kitu? Anyway,wenyewe wame enable bila kutangazia watu wao ndio wameiba na watu ni watafiti wamgundua na wanatumia matunda ya ugunduzi wao.
 
Mbona kwenye usumbufu haujasema kitu? Anyway,wenyewe wame enable bila kutangazia watu wao ndio wameiba na watu ni watafiti wamgundua na wanatumia matunda ya ugunduzi wao.
Ahahahahahaaaah du eti ugunduzi..........nimekubali.
 
Mkarabishea jamaa huyo TZ......uzembe is our middle name..................................
 
Ni kweli ugunduzi mtu wangu na watu wanaangalia bila shida.Tumwage hapa setup zake ukajatribu home kama unayo Decoder ya StarTimes??
 
asilaumiwe mchina bali customer service mbovu za wabongo

Ndo tulivyo wabongo, kila kitu tunasingizia mchina. Si ajabu hapo baadae ukamsikia mzazi akilalamika kuwa mtoto wake jeuri na hasikii ukimkanya sababu ni wakichina.
Customer cares wa taasisi/kampuni nyingi ni wazembe katika suala zima la utendaji kazi, wameomba kazi lakini hawako makini na kazi zao.

Ni kweli ugunduzi mtu wangu na watu wanaangalia bila shida.Tumwage hapa setup zake ukajatribu home kama unayo Decoder ya StarTimes??

Tuwekee hizo setup procedure nasi tukafaidi
 
Tbc walikuja kwa kasi na hata kutishia amani kw baadh ya vituo vya kurushia matangazo, ila walipo anguka wameanguka mazima hakuna vipindi vizuri tena hususani sisi wapenda soccer, hata atn wameifunika kwa champions league......bila kusahau vijana wao wanaendekeza sana kampeni zisizo namsingi...wanaboa sana
 
Setup ni kuwa
1.Click Menu button kisha down arrow key mpaka kwenye Item ya nne itakupatia Two Options,Manual and Automatic
2.Click right arrow key ili uende kwenye hizo options kisha uwe kwenye Manual options.
3.Click OK kisha bonyeza 530 kisha Click OK.
4.Ita search na kuonyesha 12channels found.
5.Exit mpaka kwenye Menu kisha ITV,EATV zitaonekana
6.Ukiona ITV na EATV havina sauti bonyenya Track button chini ya Power button kwenye Remote yako mpaka utaona sauti inapatikana.
&.Waambie na wengine.

Nakutakia kila la heri
 
bora trace umenipa mwanga , nataka ninunue hiyo decoder very soon , ila wengine wananambia haishiki vzr inasumbua ndio wananikatisha tamaa hao
 
Mwanzoni walianza vibaya, lakini TBC wametambua tatizo hilo, wamefanya mabadiliko. Asilimia 90 ya wale customer care wakorofi wameondolewa. Hali ni shwari sasa. Mimi ni mteja wa StarTimes, ila kuna tatizo moja ambalo nataka kulifuatilia... kwenye hizo channels zao wanaweka lile tangazo lao MARA MBILI, tena kati kati ya kipindi! Wanaboa! Lakini kimsingi, content zao ni nzuri. Jaribuni sana kuangalia Discovery World, mtajifunza mambo mengi mazuri!

Toka niminunua haijanisumbua na wala sijasumbuka na Cust cae... may be waongezee channel za maan na si utumbo wa macelebrity...!!
 
kama wabongo mmeshagundua kuchakachua kupata tb joshua basi nitakwenda kununua na me kwani nilitaka kununua dish kwa ajili hyo
 
Setup ni kuwa
1.Click Menu button kisha down arrow key mpaka kwenye Item ya nne itakupatia Two Options,Manual and Automatic
2.Click right arrow key ili uende kwenye hizo options kisha uwe kwenye Manual options.
3.Click OK kisha bonyeza 530 kisha Click OK.
4.Ita search na kuonyesha 12channels found.
5.Exit mpaka kwenye Menu kisha ITV,EATV zitaonekana
6.Ukiona ITV na EATV havina sauti bonyenya Track button chini ya Power button kwenye Remote yako mpaka utaona sauti inapatikana.
&.Waambie na wengine.

Nakutakia kila la heri


Duh! Uligunduaje? Nimepata ITV na EATV bila matatizo, na zimeongezeka nyingine kama vile DW TV Africa!

Safi sana! Endelea kutuelimisha!

Nadhani sasa wakiongeza channels nyingine kimya kimya zitaingia tu. Kumbe hawakutaka tujue hizi? Safi! ITV inaonekana vizuriiiiii!
 
Back
Top Bottom