Spika Ndugai na Katibu wa Bunge wapelekwe Mahakamani kwa kutoiheshimu Katiba waliyoapa kuitetea

Kutoheshimu katiba ya nchi unayo apa kuifuata na kuilinda ni kosa kubwa la pili baada ya uhaini na mauaji.

Spika wa Bunge Job Ndugai na Katibu wa Bunge wanapaswa kupelekwa mahakamani kama sio leo basi baada ya utawala huu unaowalinda kuondoka madarakani.

Sakata la Wanachama wa CHADEMA waliofukuzwa uanachama na kuendelea kuwa wabunge kinyume na maelekezo ya katiba ni kuidharau hiyo katiba na kwa maana hiyo ni kosa kubwa la jinai linalofanywa kwa makusudi.

Kama Spika wa Bunge hawezi kuheshimu katiba kuna sababu gani raia wengine kuiheshimu?
Wivu utakuumiza sana
Let's say bungeni wangekuwa hawapati pesa yoyote ni kazi ya kujitolea sidhan kama ungekuja kulialia hapa
 
Kutoheshimu katiba ya nchi unayo apa kuifuata na kuilinda ni kosa kubwa la pili baada ya uhaini na mauaji.

Spika wa Bunge Job Ndugai na Katibu wa Bunge wanapaswa kupelekwa mahakamani kama sio leo basi baada ya utawala huu unaowalinda kuondoka madarakani.

Sakata la Wanachama wa CHADEMA waliofukuzwa uanachama na kuendelea kuwa wabunge kinyume na maelekezo ya katiba ni kuidharau hiyo katiba na kwa maana hiyo ni kosa kubwa la jinai linalofanywa kwa makusudi.

Kama Spika wa Bunge hawezi kuheshimu katiba kuna sababu gani raia wengine kuiheshimu?
Mbona ruzuku hamuachi?
 
Uko sawa, ila niambie hata mishipa ya fahamu hawana kuwa katiba inavunjwa?
Anzeni kwanza chadema kukataa ruzuku inayotoka kwenye serikali ambayo imeingia kwa uonevu Then ndio mje na ishu ya ndugai
 
Wivu utakuumiza sana
Let's say bungeni wangekuwa hawapati pesa yoyote ni kazi ya kujitolea sidhan kama ungekuja kulialia hapa
We kweli mwehu! Kwani kalia au kaeleza?
Halafu sidhani kama Chadema wanashida na wanalipwa nini! Walisha weka wazi kuwa Ndugai awatambue tuu wabunge wake lakini wasiseme wabunge wa Chadema bali awaite apendavyo maana hawana agenda ya chama wanayo iwakilisha pale.
Akae nao na kuwalipa apendavyo, ila bado atakuwa kavunja katiba maana mbunge lazima awe na chama.
Umenielewa brother!
 
Anzeni kwanza chadema kukataa ruzuku inayotoka kwenye serikali ambayo imeingia kwa uonevu Then ndio mje na ishu ya ndugai
Nimewaomba ushahidi wa risiti ya kutoa na kupokea hiyo ruzuku mmeshindwa kuonyesha. Basi inaelekea COVID imewapanda kichwani.
CHADEMA wamekataa hiyo inayoiywa ruzuku inayotokana na uchaguzi haramu.
Ujue mnadanganyana nyie maCCM na propaganda zisizo na mashiko.
 
Chadema ilitoa fursa ya waliofukuzwa kukata rufaa na kwa mantiki hiyo hukumu ya kamati kuu haikupelekwa kwa spika mpaka Baraza kuu litakapokaa na kuisikiliza rufaa ya wanachama 19.

Mpaka hapo mpira uko miguuni mwa Chadema,Baraza kuu litabariki maamuzi ya kamati kuu na kumuandikia spika au baraza kuu litawasamehe na kuwarudishia uanachama wao,NI suala la muda.

Mpaka sasa Ndugai yupo huru kufanya lolote na hao wabunge 19!

Ni kwa uelewa wangu!!
Umepotoka Sana, nadhani ni kwasababu ya njaa.
Spika alishapelekewa barua kumfahamisha kuwa Hilo kindi limefukuzwa uanachama. ILITOSHA.
Kuwasimamisha, siyo suala la hukumu.
Mcoment huku mkimwogopa Mungu.

Huku mkijua kuwa baada ya maisha haya kuna maisha nje ya ulimwengu huu kwa mujibu was maandiko matakatifu
 
Wamejiwekea sheria ya kulinda maovu yao. Sheria haramu hakuna atakayeiheshimu. Utawala ukija mwingine, watafungwa tu maisha jela
Kama Chadema walivyojiwekea sheria ndani ya Katiba yao kulinda udhalimu wao eti Mwanachama akienda Mahakamani kukishitaki chama basi moja kwa moja uanachama wake unakuwa umekoma
 
Tuna shida kubwa sana kwamba tuna rais asiyejua kwamba kila mtu ktk nchi anapaswa kufuata sheria bila shuruti.

Tatizo Magufuli amejenga tabia ya kiburi na kuamini kua yeye yuko juu ya sheria na kwamba kwa kauli yake anaweza kutengua sheria yoyote iliyomo kwenye katiba ya nchi.

Ndugai yupo kutii chochote kile anachoagizwa na Magufuli kukifanya, atafanya tu na wala kamwe hawezi kuhoji na ndio maana Magufuli alipanga akawapa kinga bandia ya kutokushitakiwa.
 
Kutoheshimu katiba ya nchi unayo apa kuifuata na kuilinda ni kosa kubwa la pili baada ya uhaini na mauaji.

Spika wa Bunge Job Ndugai na Katibu wa Bunge wanapaswa kupelekwa mahakamani kama sio leo basi baada ya utawala huu unaowalinda kuondoka madarakani.

Sakata la Wanachama wa CHADEMA waliofukuzwa uanachama na kuendelea kuwa wabunge kinyume na maelekezo ya katiba ni kuidharau hiyo katiba na kwa maana hiyo ni kosa kubwa la jinai linalofanywa kwa makusudi.

Kama Spika wa Bunge hawezi kuheshimu katiba kuna sababu gani raia wengine kuiheshimu?
Mahakama ipi ?
 
Job Ndugai alishasema waziwazi kwamba hakuna mahakama Tanzania inauwezo wa kumsimamisha na kumhoji juu ya jambo lolote lile - Yeye ndiye mwenye uwezo wa kumwita Jaji yoyote yule Bungeni na akachukuliwa hatua za kinidhamu lakini si yeye kwenda the other side
 
Ndugai ndie mbunge ambae daima ni mfano bora wa kuepukwa na jamii, Amelifanya bunge kuwa la kudharauliwa kuliko mabunge yote tangu tupate uhuru! Sidhani kama lina hadhi ya kuitwa bunge!
Kama kuna kifyonza damu kinacho nyonya damu ya watanzania kinguvu ni hili dude tunaloliita bunge.
Kodi zote za waTz zinazolipwa kwa hawa watu ikiwa ni mishahara na posho nene ni wizi wa kutumia nguvu.
Hakuna taasisi iliyojidharaulisha na kwa hivyo kukosa uhalali kwa nchi kama hili bunge la Ndugai.
 
Kama Chadema walivyojiwekea sheria ndani ya Katiba yao kulinda udhalimu wao eti Mwanachama akienda Mahakamani kukishitaki chama basi moja kwa moja uanachama wake unakuwa umekoma
Tunajadiri Nchi, Bunge la nchi. Kesho njoo na hoja ya CDM. Hii ni Ndugai na Bunge la JMT!
 
Umepotoka Sana, nadhani ni kwasababu ya njaa.
Spika alishapelekewa barua kumfahamisha kuwa Hilo kindi limefukuzwa uanachama. ILITOSHA.
Kuwasimamisha, siyo suala la hukumu.
Mcoment huku mkimwogopa Mungu.

Huku mkijua kuwa baada ya maisha haya kuna maisha nje ya ulimwengu huu kwa mujibu was maandiko matakatifu
Niliandika nilivyoelewa hilo suala.Nashukuru mno na hii ina maana hata rufaa yao ikikubaliwa watarudi kuwa wanachama lakini ubunge utakuwa NO kwa mtizamo wa ki CDM.
Asante kunielimisha ila Alhamdullila sina njaa kiasi cha kuandika kitu ambacho sicho ninachoamini na nikihisi panaweza na sababu za "kiusalama"mara nyingi naacha kuandika.
 
Back
Top Bottom